3 minute read

Sura 33. Kinacholala Ng’ambo ya Pili ya Kaburi

Shetani aliyechochea uasi huko mbinguni, alitaka kushawishi wakaaji wa dunia kuungana katika vita yake ya kumpinga Mungu. Adamu na Hawa walikuwa na furaha kamili katika utii kwa sheria ya Mungu ushuhuda wa daima wa kupinga madai ya Shetani ulioweka mbele katika mbingu ya kuwa sheria ya Mungu ilikuwa ya taabu. Shetani akakusudia kuanzisha maanguko yao, ili aweze kumiliki dunia na hapa kuimarisha ufalme wake kwa kupingana na Aliye Juu.

Adamu na Hawa walikuwa wakionywa juu ya adui wa hatari huyu, lakini alikuwa akitumika katika giza, kuficha kusudi lake. Kutumia nyoka kama chombo chake, ndipo kiumbe cha mfano wa kupendeza, akamwambia Hawa: “Ndiyo, Mungu amesema: Msile ya miti yote ya shamba?” Hawa akajihatarisha (akasubutu) kusemana naye na akaanguka mateka kwa uongo wake: “Mwanamuke akamwambia nyoka: Matunda ya miti ya shamba tunaweza kula; lakini matunda ya mti ulio katikati ya shamba Mungu amesema: Musile matunda yake wala musiyaguse, musife. Na nyoka akamwambia mwanamuke; Hakika hamutakufa, kwani Mungu anajua ya kama siku mutakapokula matunda yake, macho yenu yatafunguliwa, na mutakuwa kama miungu, mukijua uzuri na ubaya.” Mwanzo 3:1-5.

Hawa akakubali, na kwa mvuto wake (mwanamuke) Adamu akaongozwa katika zambi. Wakakubali maneno ya nyoka; wakaonyesha kutotumaini Muumba wao na kuwaza ya kama alikuwa akizuia uhuru wao.

Lakini ni kitu gani Adamu alichopata kujua kuwa maana ya maneno, “Kwa maana siku utakapokula, hakika utakufa”? Je, alipaswa kuongozwa katika maisha ya kujiinua zaidi? Adamu hakuona jambo hili kuwa maana ya hukumu ya Mungu. Mungu alitangaza ile kama azabu kwa ajili ya zambi yake, mtu alipashwa kurudi kwa mavumbi: “Kwa sababu mavumbi wewe, na utarudi kwa mavumbi.” Mwanzo 3:19. Maneno ya Shetani, “Macho yenu yatafunguliwa,” yalionekana kuwa ya kweli katika maana hii tu: macho yao yakafunguliwa kutambua ujinga wao. Wakajua ubaya na kuonja tunda la uchungu wa uasi.

Mti wa uzima ulikuwa na uwezo wa kudumisha uzima. Adamu angeendelea kufurahia ruhusa ya uhuru wa kukaribia mti huu na kuishi milele, lakini wakati alipofanya zambi akazuiwa kwa mti wa uzima na akastahili kifo. Kufa ikaondoa kutokufa. Pale hapangalikuwa na tumaini kwa uzao ulioanguka kama Mungu, kwa kafara ya Mwana wake, hangeleta kutokufa karibu nao. Na hivi ‘’kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi,” Kristo “ameleta uzima na maisha yasiyokoma nuru ni kwa njia ya Habari Njema.” Katika Kristo tu kutokufa kunaweza kupatikana. “Anayeamini Mwana ana uzima wa milele; na asiyemwamini Mwana hataona uzima.” Waroma 5:12; 2 Timoteo 1:10; Yoane 3:36.

Uwongo Mkubwa

Yule aliyeahidi uzima katika uasi alikuwa mdanganyi mkubwa. Na tangazo la nyoka katika Edeni “Hakika hamutakufa” lilikuwa hubiri la kwanza lililohubiriwa daima juu ya kutokufa kwa roho (nafsi). Lakini tangazo hili, la kubaki tu kwa mamlaka ya Shetani, linakaririwa kwa mimbara na kukubaliwa kwa watu wengi kwa upesi kama mbele kwa wazazi wetu wa kwanza. Hukumu ya Mungu, “Nafsi inayofanya zambi itakufa” (Ezekieli 18:20) inafanywa kwa kutaka kuonyesha, Nafsi inayofanya zambi, haitakufa, lakini itaishi milele na milele. Kama mtu angalipewa ruhusa ya uhuru ya kukaribia mti wa uzima, baada ya kuanguka kwake, zambi zingalifanywa kukaa milele. Lakini hakuna hata mtu mmoja wa jamaa ya Adamu aliyeruhusiwa kuonja (kutwaa) tunda linalotoa uzima. Kwa hiyo hapo hakuna mwenye zambi wa kuishi milele.

Baada ya Kuanguka, Shetani akaalika malaika zake kufundisha imani katika kutokufa ya milele kwa asili ya mtu. Akiisha kuingiza watu kukubali kosa hili, ilikuwa ni kuwaongoza kuzania kama mwenye zambi angeishi katika mateso ya milele. Sasa mfalme wa giza anamuonyesha Mungu kuwa sultani mkali mwenye kutaka kisasi, kutangaza ya kama anatumbukiza katika jehanum wote wasiompendeza, ya kama wakati wanapojinyonga katika ndimi za moto wa milele, Muumba wao anawatazama chini na kurizika. Kwa hivi ibilisi mukubwa anavika Mtenda mema kwa mwanadamu tabia zake. Ukali ni tabia ya Shetani. Mungu ni mapendo. Shetani ni adui anayejaribu mtu afanye zambi na baadaye akamwangamiza kama awezavyo. Ni mambo ya kuchukiza upendo, rehema, na haki, mafundisho kwamba wafu waovu wanateseka katika jehanum inayowaka ya milele, kwamba kwa zambi za maisha mafupi ya kidunia wanateseka malipizi makali katika maisha yote ya Mungu!

Ni mahali gani katika Neno la Mungu mafundisho ya namna ile inapatikana? Je, mawazo ya wema wa watu wote yageuzwe kwa ukali waushenzi? Hapana, yale si mafundisho ya Kitabu cha Mungu. “Ninavyoishi, Bwana Mungu anasema, sina furaha kwa kufa kwa mwovu; lakini mwovu aache njia yake apate kuishi; geukeni, geukeni mukaache njia yenu mbaya; kwani kwa sababu gani munataka kufa?” Ezekieli 33:11.

Je, Mungu anapendezwa katika kushuhudia mateso yasiyomalizika? Je, Yeye anapendezwa na maumivu wala mazomeo na kilio cha nguvu cha viumbe vinavyoteseka anavyoshikilia katika ndimi za moto? Je, sauti hizi za kuchukiza ziwe sauti za nyimbo katika sikio la yule ambaye ana Upendo Pasipo Mwisho (Mungu)? Loo, matukano gani ya kutiisha! Utukufu wa Mungu hauongezwe kwa kudumisha zambi kupitiamilele na milele.

Ujushi wa Maumivu Mabaya ya Milele

Uovu ulifanyika kwa sababu ya ujushi wa maumivu mabaya ya milele. Dini ya Biblia, inajaa na upendo na wema, inatiwa giza kwa imani ya mambo ya uchawi na inavikwa na hofu kubwa. Shetani amepakaa rangi tabia ya Mungu kwa rangi za uwongo. Muumba wetu wa rehema anaogopwa, na kuhofiwa, hata kuchukiwa. Maoni ya kutisha ya Mungu ambayo

This article is from: