Child Rights Brochure

Page 1

GOOD NEIGHBORS KIMATAIFA Jitahada nyingi zimefanyika kumkomboa mtoto wa kike lakini bado vikwazo ni vingi sana katika kufikia malengo yao. Hivyo, ni vyema kila mtu kushiriki katika kulinda utu wa mtoto wa kike kwa kupaza sauti kukataa ukatili majumbani na kutokomeza viashiria vyote vinavyopelekea ukiukwaji wa haki za mtoto wa kike. Mtoto wa kike anastahili kuwa huru na ana mchango mkubwa katika ustawi wa familia, jamii na taifa kwa ujumla.

KLABU ZA UTETEZI WA HAKI ZA MTOTO MASHULENI Shirika la Good Neighbors kwa kushirikiana na serikali pamoja na walimu lilifanikiwa kuunda klabu za utetezi wa haki za mtoto katika shule 18 zilizopo katika wilaya 3 ambazo ni Bagamoyo (9), Kinondoni (6) pamoja na Kigamboni (3). Lengo la kuundwa kwa klabu hizi ni kumwezesha mtoto kuwa na uelewa wa kutosha juu ya haki zake za msingi kama zilivyoainishwa kwenye sheria ya haki za mtoto ya mwaka 2009 na kuhakikisha kuwa, haki hizo zinalindwa na kuheshimiwa na kila mtu. Kazi kubwa ya klabu hizi ni kuelimisha jamii nzima wakiwemo watoto juu ya haki za mtoto kwa njia ya matamasha, vipeperushi, midahalo na semina mbalimbali. Shirika la Good Neighbors limekuwa likiwajengea uwezo klabu za utetezi kwa kuwapatia semina mahususi, mbinu mbalimbali za kufikisha ujumbe wa haki za mtoto pamoja na kuwawezesha katika kutoa elimu hiyo. Miongoni mwa mafanikio makubwa yaliyopatikana kutokana na kuwepo kwa klabu hizi mashuleni ni pamoja na kuongezeka kwa uelewa wa haki za watoto miongoni mwa wanafunzi mashuleni pamoja na jamii zilizo karibu na shule hizo. Pia, elimu hizo zinazotolewa na klabu kwa jamii zimepelekea kupungua kwa kiasi kikubwa kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto. Shirika la Good Neighbors lina mpango wa kuendelea kuunda klabu hizi za utetezi kwenye shule mbalimbali ili kuhakikisha elimu hii inazifikia jamii nyingi zaidi kadiri iwezekanavyo.

GNI ni shirika la kimataifa lisilo la kiserikali la misaada ya kibinadamu na maendeleo ya jamii lenye kutambulika na baraza la kiuchumi na mambo ya kijamii la umoja wa kimataifa. GNI limepiga hatua kubwa katika malengo yake ya kusaidia watu dunia kote kupata maisha yenye ubora tangu kuanzishwa kwake 28/3/1991. Limeweza kufikia nchi 35 duniani kote GNI lilianzishwa 1991 jamuhuri ya watu wa korea na makao makuu yapo korea kusini. GNTZ lilianzishwa mwaka 2005 na likiwa na makao yake makuu Dar es salaam. Pia shirika toka kuanzishwa kwake Tanzania mwaka 2005 limeweza kutanuka na kufanya kazi katika mikoa ifuatayo Dar es salaam, Dodoma, Shinyanga, Pwani, Mwanza, Mbeya, Morogoro, na Kigoma.

MALENGO YETU GNTZ inajitahidi kubadilisha dunia kuwa yenye amani na usalama kwa kuhakikisha hakuna mtu yeyote atakaye pata shida ya njaa au kuathirika kwa ugonjwa wowote ule unaotibika.

KAZI ZETU □ Kutetea na kulinda haki za watoto □ Kuwajengea uwezo wananchi kiuchumi, kwa kuanzisha miradi mbalimbali kama vile ufugaji wa kuku, kilimo cha kahawa, ufungaji nyuki, kilimo cha mananasi, kilimo cha mihogo nk □ Kutoa misaada mbalimbali ya kielimu ikiwemo ujenzi wa shule, vifaa vya michezo, ugawaji wa daftari, unifomu, vitabu, nk. □ Kusaidia sekta ya afya katika kutoa elimu ya afya kwa kushirikiana na serikali pamoja na jamii, kutoa bima za afya kwa watoto, kujenga na kukarabati vituo vya afya na kutoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya matibabu.

VIPAO MBELE □ Tunafanya kazi mahali popote penye mahitaji bila kujali rangi, dini, itikadi na tofauti za jiografia. □ Tuna hamasisha kujitegemea na maendeleo bora ya mtu mmojammoja, familia na jumuiya kwa ujumla. □ Kulinda, na kutetea haki za watoto □ Tunaeneza ujumbe Duniani kote juu ya msisitizo wa heshima kwa wote, kuishi kwa umoja na maelewano.

MTOTO NI NANI? Mtoto ni mtu aliye na umri chini ya miaka kumi na nane.

HAKI ZA MTOTO

Plot 2407K, Block 2047B Tegeta Wazo, Dar es Salaam, Tanzania P.O Box 33104 DSM Tanzania Tel: +255 732991530 | Email: tanzania@goodneighbors.org

Haki ya Kutokutengwa Haki ya Jina na Utaifa Haki ya Kuishi na Wazazi au Walezi Haki ya Kupata Huduma Haki ya Kushiriki Michezo na Shughuli za Kiutamaduni Haki ya Huduma ya pekee kwa Mlemavu Haki kwa Mali za Wazazi Haki ya Kutoa Maoni


HAKI ZA MTOTO 1.

Haki ya Kutokutengwa:

Mtoto atakuwa na haki ya kuishi huru bila kuwapo na namna yoyote ya kutengwa; yaani, kuonekana kuwa hastahili kujumuika na wenzake katika kundi.

2. Haki ya Jina na Utaifa: Mtoto ana haki ya kujua jina lake, utaifa, na wazazi wake waliomzaa na ukoo wa familia yake. Mtu yeyote haruhusiwi kumnyima mtoto haki ya kujua jina lake, utaifa, na kujua wazazi wake waliomzaa na wengine katika ukoo wa wazazi wake. 3. Haki ya Kuishi na Wazazi au Walezi: Mtoto ana haki ya kuishi na wazazi au walezi wake. Mtu yoyote haruhusiwi kumnyima mtoto haki ya kuishi na wazazi, walezi au familia yake. Pia, ni haki ya mtoto kukua katika malezi na mazingira ya amani. 4. Wajibu wa kumtunza mtoto: Ni wajibu wa mzazi, mlezi au mtu yeyote mwenye kumlea mtoto kutoa matunzo kwa mtoto. Wajibu huu hasa unampatia mtoto haki ya: (a) Chakula; (b) Malazi; (c) Mavazi; (d) Dawa pamoja na chanjo;(e) Elimu na maelekezo au mafunzo; (f) Uhuru; na (g) Haki ya kucheza na kupumzika. 5. Haki ya Kupata Huduma: Mtu yeyote haruhusiwi kumnyima mtoto haki ya kupata elimu, chanjo, chakula, mavazi, malazi, huduma ya afya na dawa au kitu chochote kinachohitajika kwa ajili ya maendeleo ya mtoto. Mtu yeyote haruhusiwi kumkatalia mtoto huduma ya dawa kwa sababu ya dini au imani yoyote ile.

ya Kushiriki Michezo na Shughuli za Kiutamaduni: Mtu yeyote haruhusiwi kumnyima

kutibiwa, kupewa nyenzo stahili kwa ajili ya kurekebisha ulemavu wake. Kwa mfano, viti na baiskeli za walemavu wa viungo, ďŹ mbo kwa kipofu au hati za alama kwa bubu. Mlemavu ana haki ya kupewa nafasi sawa katika elimu na mafunzo pale inapowezekana, ili kuendeleza vipaji vyake na uwezo wa kujitegemea. 8. Wajibu na Jukumu la Mzazi: Mtoto atakuwa na haki ya kuishi, kwa hadhi, heshima, uhuru, afya, kupumzika, na kupatiwa elimu na malazi kutoka kwa wazazi. Haki ya kupumzika na uhuru kwa mtoto vitategemea maelekezo na uwezo wa wazazi, walezi au ndugu. Kila mzazi ana wajibu na majukumu kwa mtoto. Wajibu na majukumu hayo yatatekelezwa, yawe yamewekwa na sheria au vinginevyo. 9. Haki kwa Mali za Wazazi: Mtu haruhusiwi kumnyima mtoto kumiliki na kutumia mali ya urithi kutoka kwa mzazi. 10.

kumnyima mtoto mwenye uwezo wa kutoa maoni haki ya kueleza maoni, kusikilizwa na kushiriki katika kufanya maamuzi yatakayoathiri ustawi wake. 11.

6. Haki

mtoto haki ya kushiriki katika michezo, au shughuli njema za kiutamaduni na kisanii au za starehe. Hata hivyo, ikiwa kwa maoni ya mzazi, mlezi au ndugu, kwamba kushiriki huko kutakuwa na madhara, au shughuli hizo haziendelezi ustawi wa mtoto, haki hiyo inaweza isitolewe. Mtu yeyote haruhusiwi kumtendea mtoto mwenye ulemavu tendo lolote kwa namna isiyo ya heshima. Watoto wenye ulemavu wa aina yoyote ile wanastahili msaada na upendo. 7. Haki ya Huduma ya pekee kwa Mlemavu: Mtoto mwenye ulemavu anastahili kupewa huduma ya pekee. Huduma hizi ni pamoja na:

Haki ya Kutoa Maoni Mtoto atakuwa na haki ya kutoa maoni: Hakuna mtu anayeruhusiwa

12.

akili yake. Hakuna adhabu inayokubalika kwa ajili ya umri mdogo wa mtoto au vinginevyo kwa sababu mtoto hawezi kuelewa nia ya adhabu hiyo. Tendo lenye kudhalilisha, kama maneno hayo yalivyotumika katika fungu hili una maana ya tendo lililofanywa kwa mtoto kwa nia ya kudhalilisha au kumshushia hadhi yake. Kwa mfano, kuchapa mtoto mbele ya wenzake au mbele ya umma wa watu ni tendo lenye nia ya kumdhalilisha mtoto.

WAJIBU WA JUMLA WA MTOTO Mtoto ana haki, lakini pia ana wajibu. Je, wajibu wa mtoto ni upi? Pamoja na haki za kulinda ustawi wa mtoto, mtoto atakuwa na wajibu na jukumu la: (a) Kufanya kazi kwa ajili ya mshikamano wa familia. (b) Kuwaheshimu wazazi, walezi, wakubwa wake na watu wazima muda wote na atawasaidia pale inapohitajika. (c) Kuhudumia jamii yake na taifa lake kwa uwezo wake wote kimwili na kiakili kadiri ya umri na uwezo wake.

Ajira yenye Madhara: Mtu yeyote haruhusiwi kumuajiri mtoto katika shughuli yoyote inayoweza kuwa na madhara katika maendeleo ya afya, elimu, akili, mwili na maadili yake. Kwa mfano, kazi katika viwanda vya kemikali inaleta athari kwa afya ya mtoto. Kazi ya mashambani au machimboni inayozuia mtoto kwenda shule inaathiri elimu, akili na mwili wake. Kazi ya ukahaba inaathiri maadili ya mtoto.

(d) Kutunza na kuimarisha mshikamano wa jamii na Taifa; na

Kulinda Mtoto Asiteswe na Kudhalilishwa: Mtu yeyote hataruhusiwa kumfanya mtoto apate mateso, au adhabu ya kikatili, ya kinyama au afanyiwe matendo yenye kumshushia hadhi. Hii ni pamoja na desturi zozote za mila zenye kudhalilisha utu wa mtoto au zinazosababisha athari za maumivu ya mwili au akili ya mtoto. Kwa mfano, kukeketa wasichana ni kudhuru vibaya mwili, akili na hisia za mtoto wa kike. Pia, ni kitendo kinachomdhalilisha. Hakuna adhabu kwa mtoto inayokubalika ambayo imekithiri kimatendo au kwa kiwango kulingana na umri, hali ya mwili na

Watoto wa kike wanakabiliwa na vikwazo vingi katika kufikia malengo yao. Vikwazo hivyo ni pamoja na ndoa za utotoni, manyanyaso ya kingono, uwiano usio sawa wa kimajukumu majumbani kati ya mtoto wa kike na wa kiume, ukeketaji na mengine mengi. Changamoto nyingi zimejificha kwenye mila ana desturi ambazo zinamkandamiza mtoto wa kike. Haya yote yamkwamisha mtoto wa kike na kumkosesha haki zake za msingi kama kuishi kwa furaha, kupata elimu na huduma muhimu.

(e) Kutunza na kuimarisha mambo mema katika utamaduni wa jamii na Taifa kwa ujumla katika uhusiano na wanajamii au taifa.

MTOTO WA KIKE


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.