Hii ni nyenzo ya kivitendo maalumu kwa viongozi, wawezeshaji na wataalamu wanaohitaji kurekebisha na kuboresha michakato yao ya kujifunza . Imeandaliwa kwa ajili ya mtu mmoja mmoja , mashirika pamoja na shughuli za mabadiliko katika jamii. Hiki sio tu kitabu kingine kuhusu taratibu za kujifunza katika mashirika na katika mabadiliko ya kijamii. Ni kitabu cha kipekee kwa kuwa hakikuandikwa na mtu mmoja . Na wala sio mkusanyiko wa insha zilizoandikwa na watu tofauti tofauti. Kitabu hiki ni matokea ya jitihada za pamoja za kundi la wataalamu wa maendeleo kutoka duniani kote. Kilibuniwa na kuandikwa kwa kupitia warsha tatu shirikishi na makini za kuandika, maarufu kama warsha za uandishi . Kwa kupitia mchakato huu tumebuni kitu cha kutusaidia sisi wenyewe pamoja na watu wengine katika kuanza na kuendeleza safari yenye mafanikio katika kujifunza na katika kuleta mabadiliko ya kijamii. Sisi (waandishi) sote tuna shauku ya kujifunza na tumekusanya na kutoa uzoefu na utaalamu wetu tofauti tofau