Moduli 2, Kilimo Mseto Na Mzunguko (revised)

Page 1

Mkulima Mbunifu Moduli namba 2

KILIMO MSETO NA MZUNGUKO Kilimo huanza kwa kupanda mazao kwa mzunguko

Mbinu za asili za kilimo zinaweza kusaidia kuboresha kilimo na kuleta ufanisi kwa wakulima wadogo wadogo. Kulima kwa mzunguko ni mbinu namba moja, na situ katika kilimo hai. Ni muhimu sana katika kulinda mazao, na kuwezesha kuwa na rutuba endelevu katika udongo, na chakula cha uhakika - na mtindo huu unapatikana bila gharama yoyote kwa kila mmoja.

Kulima kwa mzunguko: Muhumu kwa mazao yenye afya Kilimo cha mzunguko siku zote kimekuwa kama moyo kwa matokeo mazuri ya kilimo. Kama aina moja ya zao likipandwa katika eneo moja kwa misimu tofauti mfululizo, unaweza kuona kuwa linafanya vibaya kila wakati. Hii inafahamika na wakulima wote ulimwenguni kote kwa karne nyingi, wakulima wamekuwa wakitumia mfumo huu wa kulima kwa mzunguko ili kuepuka madhara hayo. Ni kwa siku za hivi karibuni tu mtindo huu umetelekezwa na baadhi ya wakulima katika sehemu chache duniani. Mbolea na madawa ya viwandani yanaweza lakini ni kwa kitambo tu, huleta madhara mabaya yanayozuia kuendeleza mazao. Baada ya muda mrefu kiasi zaidi cha mbolea na madawa huhitajika kwa lazima, ambapo husababisha kuongezeka gharama, athari za kemikali, na kufanya wadudu na magonjwa kujenga usugu wa madawa.

Faida zaidi: Udongo bora na uhakika wa chakula • Mzunguko wa mazao huboresha muundo wa udongo kutokana na mizizi tofauti, na mazao tofauti. Mizizi inayoenda chini sana husaidia kulainisha udongo, kuwezesha ardhi kunyonya maji na kuongeza unyevu kwenye udongo. Rutuba ya udongo hubaki ilivyo au kuongezeka kutokana na aina ya mazao yanayopandwa kwa mzunguko, na mengine kuwa na uwezo wa kuongeza nitrojeni kwenye udongo mfano jamii ya mikunde ambayo pia ipo kwenye mzunguko. • Katika mzunguko mzuri, zao moja hufuata lingine katika hali ambayo udongo hufunikwa ili kuzuia mmomonyoko wa udongo. • Kilimo cha mzunguko huongeza uhakika wa chakula: Endapo aina nyingi za mazao zitapandwa na zao moja likaanguka, kutakuwa na madhara kidogo sana kuliko vile ambavyo aina chache za mazao zingepandwa.

Kwa nini misimu yote kilimo cha mzunguko kinahitajika Kuna sababu mbili kubwa ni kwa nini mzunguko wa mazao ni muhimu:

Mzunguko wa mazao unaopendekezwa (fuata mtiririko). Anza na zao tofauti katika sehemu tofauti shambani mwako.

Jumuisha majani ya malisho

Kanuni tofauti kwa mazao tofauti! Ni muda gani unatakiwa kusubiri kabla ya kupanda aina flani ya zao katika eneo moja? Hii inategemeana na aina ya wadudu na magonjwa yanayofungamana na zao hilo. Baadhi ya magonjwa na wadudu wanaweza kuishi kwenye udongo kwa miaka mingi. Wengine hawawezi kuishi kwa muda mrefu. Kwenye jedwali la 1 “Jamii ya mimea na mimea inayopandwa mara kwa mara kwa misimu tofauti” katika ukurasa unaofuata, unaweza kuona ni kwa namna gani unavyoweza kupanda mazao yanayopandwa mara kwa mara katika eneo moja, na ni matatizo gani unaweza kukumbana nayo endapo utapanda mara kwa mara. Mboga mboga zinaathiriwa zaidi na magonjwa kuliko nafaka, hivyo zinatakiwa mzunguko kwa umakini sana. Kuwa mzoefu wa aina ya mimea

1. Aina nyingi za magonjwa na wadudu, na hata magugu, hutokana na aina flani ya mimea na yanaweza kuongezeka pale tu kunapokuwa na aina ya zao ambalo hutegeana. Huweza kuishi wakati wa kiangazi na hata baridi kwa kuishi kwenye masalia shambani. Wanafurahia sana endapo msimu ujao utapanda tena aina ya zao ambalo ni chakula chao. Wataanza mara moja kuzaliana zaidi.

Aina ya mimiea inayotokana na jamii ya mimea inayofanana, kwa kawaida huathiriwa na aina inayofanana ya wadudu na magonjwa. Hii ni kwa sababu viazi mviringo, nyanya, pilipili hoho, na bamia, vyote vinatoka katika familia moja ya jamii ya mimea, hivyo unaweza kupanda moja wapo katika sehemu yako ya shamba unayofanya mzunguko wa mazao katika mwaka.

2. Wakati wa ukuaji, kila zao linahitaji aina flani ya virutubisho kutoka kwenye udongo. Kama ukipanda aina moja ya zao katika sehemu moja msimu kwa msimu, hii itasababisha kudhoofisha udongo, ukuwaji hafifu, na kupata mimea dhaifu ambayo pia ni rahisi kushambuliwa na wadudu na magonjwa.

Ni vizuri kufanya mzunguko wa mazao ya majani, matunda, mazao ya mizizi, jamii ya mikunde, na nafaka kama vile ambavyo jamii nyingi za kiafrika tayari wanafanya. Wazo hili huzingatia utofauti wa virutubisho vinavyohitajika. Lakini kwa afya ya mimea hii haitoshi, kama unavyoweza kuona kwenye mfano wa nyanya (zao linaloliwa tunda) na viazi (zao la mizizi) yote ni matunguja (nightshade) na hayatakiwi kufuatana.


Mzunguko wa mazao katika shamba dogo Kulima kwa mzunguko haihusiani na ukubwa wa shamba. Kama una shamba dogo, ina faida zaidi kwa kuwa utakuwa na mazao yenye afya. Mazao yenye afya hutoa mavuno mengi zaidi, chakula kingi, na pesa zaidi. Kama ukipanda mazao kutoka katika jamii tofauti ya mimea, unaweza kufanya mzunguko wake katika shamba lako kila msimu. Mazao yanaweza kulimwa kwa mzunguko katika shamba kubwa na hata katika shamba dogo, na kwa matokeo sawa hata kama ni katika vijungu. Hii ni kwa sababu mahindi na

Jamii Majani ya malisho

Nafaka

Zao

aina nyingine za nafaka hazishambuliwi sana na wadudu na magonjwa kama ilivyo kwa mazao ya mbogamboga na matunda, hivyo hayahitaji kuhamisha sana kama mbogamboga, yanaweza kuchukua nafasi kubwa ya ardhi iliyotengwa kwa ajili ya mazao ya msimu. Mahindi yanaweza kuchukua mbili ya tatu ya eneo, na mpunga pamoja na mazao mengine nusu. Pamba inaweza kuchukua moja ya tatu ya sehemu iliyobaki ya ardhi yako inaweza kutumika kwa mbogamboga na majani ya malisho. Mbogamboga zinaweza kufanyiwa mzunguko na mazao mengine kama vile mahindi na aina nyingine za nafaka.

Mimiea katika shamba moja

Sababu

Matete, Boma, Shonanguo, sudan, Kwa miaka 3 majani ya tembo

Ni mazao ya kudumu

Mahindi, Mahindi matamu, mahindi ya Miaka 2 mpaka 3 watoto, mtama, ulezi.

Ugonjwa wa ukungu

Mpunga

Unaweza kupanda mfululizo, Ugonjwa wa ukungu, na minyoo lakini mzunguko ni muhimu

Ngano, wimbi

Mara moja kwa miaka 2

Ukungu

Shayiri

Mara moja kwa mika 4

Minyoo

Maharage makavu, soya, karanga, cowpeas, pigeon peas, maharage Mara moja kwa miaka 4 machanga.

Madoa madoa, kuoza mizizi, virusi, ukungu, minyoo

Garden peas, snow peas, sugar snaps, Mara moja kwa miaka 6 chickpeas

Minyoo na kuoza kwa mizizi

Mtunguja (Nightshade)

Viazi mviringo, Nyanya, Hoho, pilipili, Mara moja kwa miaka 4 Biringanya

Yanaathiriwa sana na mabaka, magonjwa yanayosababishwa na bakteria, na minyoo

Jamii ya kabichi

Kale, kabichi, broccoli, cauliflower, Mara moja kwa miaka 4 radish, rape, turnips, collards

Inaathiriwa sana na magonjwa unaotokana na bakteria, ukungu wa mizizi na minyoo

Karoti, Figiri, Shamari

Ukungu na kuoza mizizi, na minyoo

Mikunde

Apiaceae

Mizizi (Jamii tofauti) Viazi vitamu, mihogo, magimbi Jamii ya spinachi Jamii ya vitunguu Asteraceae Jamii ya matango (Cucumber) Jamii ya pamba

Mara moja kwa miaka 4 Mara moja kwa miaka 4 Mara moja kwa miaka 2

Spinachi, tembele

Mara moja kwa miaka 4

Vitunguu maji, Saumu,

Mara moja kwa miaka 5

leeks

Mara moja kwa miaka 4

Alizeti,

Mara moja kwa miaka 5

Saladi

Mara moja kwa miaka 4

Boga, kibuyu

Mara moja kwa miaka 4

tango, zucchini

Mara moja kwa miaka 5

tikiti maji

Mara moja kwa miaka 6

Okra, pamba

Mara moja kwa miaka 3

Fukusi, mizizi kuoza, minyoo, bakteria Ukungu na bakteria wanao ozesha mizizi, minyoo Ukungu, mizizi kuoza, minyoo Ukungu, mizizi kuoza, minyoo Kukauka, mengineyo

madoadoa

na

Minyoo na ukungu

Hii ni aina na jamii ya mimea ambayo huathiriwa na aina sawa ya wadudu na magonjwa: Hiki ni kiasi kinachopendekezwa kwa mzunguko wa kiwango cha chini kabisa. Itasaidia kulinda mazao yako dhidi ya magonjwa na wadudu wanaoweza kuishi kwa muda mrefu kwenye udongo. Endapo tatizo ni kubwa, inaweza kuwa lazima kuongeza muda wa mzunguko. Mfano mmojawapo ni wa Fusarium kwenyemaharage: Kipindi cha miaka 6 au zaidi katika sehemu moja ni muhimu kwa ajili ya kuondoa tatizo hili.


Jedwali 1: Jamii ya mimea na mimea inayopandwa mfululizo kila msimu Mzunguko wa mbogamboga Mboga zinachukua muda mfupi kuanzia kupandwa hadi kuvunwa hivyo mzunguko wake ni tofauti na mazao ya muda mrefu, jambo la msingi ni kwamba mboga zipandwe mara moja tu katika shamba ambalo limegawanywa kwa kufuata mzunguko. Kwa kulima misimu miwili kila mwaka, kila sehemu uliyonayo ya kilimo itakuwa na misimu minane (8) kabla ya aina moja ya mboga kupandwa tena. Njia rahisi ya kuwa na mzunguko mzuri wa mbogamboga ni kugawanya shamba lako katika vipande 8 vilivyo sawa au ukubwa tofauti. Eneo hili ni lazima liwe la kudumu kwa miaka inayofuata. Rudisha mpaka kufikia vipande 5 kwa ajili ya mahindi, au vipande 4 kwa ajili ya aina nyingine za nafaka, na sehemu nyingine ukapanda mbogamboga na majani kwa ajili ya mifugo kama unafuga. Unaweza pia kugawa eneo hilo zaidi. Kisha panda kila kisehemu kwa nafasi kulingana na aina ya mimea na jamii yake.

Usiamini kumbukumbu za kichwani Kwa watu walio wengi ni vigumu kukumbuka kila zao walilopanda kwa kila kisehemu kwa miaka iliyopita. Kwa hiyo, unahitaji angalau kuwa na kijitabu kidogo ambacho utaweka kumbukumbu ya mazao yote uliyopanda kila msimu wa mvua. Gawanya shamba lako na lioneshe kila sehemu kisha uzipe majina au namba. Kisha orodhesha aina ya mazao utakayopanda kwa kila kipande, hata kama utapanda mseto. Tunza kitabu hicho katika sehemu nzuri ambayo itakuwa rahisi kwako kukipata kabla ya kuazna kwa msimu mwingine wa kupanda.

Utaratibu mzuri Kuna mfuatano wa baadhi ya mazao ambao unafaa zaidi kuliko mengine, na baadhi ya mfuatano haufai. Katika jedwali la 2 unaweza kuona mfuatano wa mazao tofauti ambao umehakikiwa kuwa na faida kwa afya ya mazao.

Jedwali la 2: Mfuatano mzuri wa mazao ambayo yanazoeleka kupandwa Mfuatano mzuri katika msimu Mazao yote ni mazuri Mazao yote isipkuwa ngano, mtama na shayiri mzunguko wa mpunga:mahindi na aina nyingine za nafaka, Mikunde, pamba, viazi vitamu Mahindi, nafaka, spinachi, karoti, vitunguu Mahindi, nafaka, nyasi, kunde, spinachi, vitunguu, alizeti Mikunde (na aina zote za jamii hiyo isipokuwa mitunguja na tangopepea) Mahindi, nafaka, nyasi, mikunde, nyanya, viazi mviringo na vitunguu Tangopepea, jamii ya vitunguu, jamii ya spinachi, nafaka na nyasi Tanigopepea, spinachi, mchicha na alizet Jamii ya vitunguu, viazi mviringo, karoti, njegere, nafaka na nyasi Nafaka, maharage mabichi, viazi mviringo, spinachi Viazi mviringo, jamii ya vitunguu, spinachi, mikunde, mahindi, nafaka, nyasi Spinachi, mahindi, nafaka, majani ya malisho Mahindi, nafaka, mpunga, viazi mviringo na vitamu, alizeti, spinachi Mahindi, nafaka, spinachi

Zao Mahindi, mtama, ulezi Ngano, shayiri na wimbi mpunga

Ni vizuri kupanda baadae Mazao yote isipokuwa karoti Mazao yote isipokuwa ngano, shayiri, wimbi njegere

Maharagwe

Viazi mviringo, nyanya, kabichi, vitunguu, mahindi, nafaka

Viazi mviringo

Kabichi, spinachi, vitunguu, boga, na alizeti, soya, mahindi, nafaka na mchicha

Nyanya Jamii ya kabichi karoti

Kabichi, mahindi, nafaka na nyasi Mahindi pekee na nafaka nyinginezo, nyasi na kale Mahindi, nafaka, nyasi na maharagwe

Viazi vitamu

Mikunde, mahindi, mpunga, nafaka na nyasi

spinachi

Karanga, soya, mazao yote isipokuwa jamii ya spinachi na mchicha

vitunguu

Mazao yote isipokuwa jamii ya vitunguu

Boga, matunda yanayopondeka karanga mikunde alizeti

Mazao ya mizizi (Isipokuwa viazi mviringo) karoti, viazi vitamu, magimbi, mihogo Nyasi, pamba Viazi mviringo, nyanya, kabichi, boga, mahindi, nafaka, pamba Viazi mviringo, mahindi, nafaka, mikunde


Mseto Kupanda mseto ni njia ya kiasili ya kilimo katika eneo kubwa la ukanda wa tropiki duniani, hasa katika nchi za Afrika. Hii imekuwa inakichukuliwa kama mbinu isiyofaa katika kilimo, na wakulima wamekuwa wakikatishwa tamaa na maafisa kilimo katika kupanda mazao kwa mseto. Miaka ya karibuni pekee faida zake zimeonekana na kukubalika.

Inafaa sana katika kilimo hai Hapana shaka kuwa kulima mseto ni njia ya kiasili zaidi kuliko kupanda aina moja ya zao. Wakulima wa Afrika wamekuwa wakipata faida kutokana na kupanda mazao kwa kuchanganya (mseto). Endapo tukitaja zote, orodha itakuwa ndefu sana! Hapa kuna mifano michache: • Matete yakichanganywa na mahindi hupunguza uwezekano wa mahindi kushambuliwa na ugonjwa wa kuoza shina • Nyanya-kabichi hupunguza hupunguza kushambuliwa na diamond-back moth • Njegere na mikunde zinaweza kuendelea kupandwa ili kulinda udongo baada ya zao kuu kuvunwa • Kuvuna maharage yanayotambaa au njegere wiki chache kabla ya kuvuna nyanya husaidia kufunika udongo. • Kupanda mistari ya miwa katika sehemu iliyoachwa na nyanya upande mwingine ni matumizi mazuri ya rasili mali. • Kwa ujumla mazao marefu huchanganywa na mazao mafupi yanayohtaji kivuli, na mimea yenye mizizi mirefu huchanganywa na mimea yenye mizizi inayotambaa..

Faida muhimu zaidi • Mseto unaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa uzalishaji katika kipande kidogo cha ardhi, hii ni kwa sababu rasilimali ndogo inatumiwa vizuri ambayo isingewezekana kwa zao moja. • Kupanda mazao tofauti tofauti huongeza rutuba na uhakika wa chakula • Hupunguza uwezekano wa kuwepo wadudu, magonjwa na magugu • Ongezeko la wadudu wa asili kama vile buibui, nyigu, husaidia kupunguza uwezekano wa wadudu waharibifu na mlipuko wa magonjwa • Kuchanganya jamii ya mikunde, njia ambayo imezoeleka sana Afrika, inaongeza mavuno bila kutumia mbolea za viwandani kwa kuwa mimea jamii ya mikunde ina uwezo wa kuongeza nitrojeni kwenye udongo • Udongo ukifunikwa vizuri husaidia kupunguza mmomonyoko wa ardhi na kupunguza uotaji wa magugu • Uchanganyaji mzuri wa zao la msimu kama yakichanganywa vizuri huachwa yakiendelea kukua baada ya zao kuu kuvunwa • Mazao yanayorefuka sana au ya kupanda husaidiwa na mazao ya jamii yake • Mimea laini hupatiwa kivuli au ulinzi

Mseto na mzunguko wa mazao Ni vigumu sana kupanda mazao kwa mseto wakati ukifanya kilimo cha mzunguko, hii ni kwa sababu mazao mengi yanajumuishwa wakati wa kupangilia mzunguko na hata kwa msimu unaofuata. Itakuwa vigumu sana kuacha nafasi kati ya zao na zao kwa mazao ya jamii tofauti. Utatuzi ni mmoja tu: Panda aina nyingi za mazao kadri utakavyoweza kutumia na kuuza, isiwe katika sehemu moja, lakini katika shamba lote na katika misimu tofauti.

Mikunde Umuhimu wa aina hii ya mazao katika kilimo hai hauwezi kuacha kusisitizwa, hii ni kwa sababu ni muhimu sana kwa kuwa ni chanzo kizuri cha nitrojeni katika shamba lako. Lakini endapo mimea jamii ya mikunde itachanganywa na mazao mengine mara kwa mara itakuwa ni vigumu kuepuka uwezekano wa kuwepo na ugonjwa uliopo kwenye udongo unaoathiri jamii ya mikunde. Hivyo basi inashauriwa kujumuisha kwa kiasi kikubwa aina tofauti ya jamii ya mikunde katika mzunguko. Jaribu kuzingatia mzunguko unaopendekezwa angalau kwa umuhimu wa jamii ya mikunde inayolimwa kibiashara kama vile maharagwe machanga (French beans) au njegere. Zitakuwa na ufanisi zaidi!

Mseto wa mahindi-maharagwe. Mseto ni mzuri kwa mazao, udongo, na kwa lishe ya binadamu.

Moduli hii imechapishwa na Mkulima Mbunifu kwa ushirikiano na The Organic Farmer (info@organickenya.org, P.O. Box 14352-00800 Nairobi, Kenya, +254 20 440398), Biovision Africa Trust, www.biovision.ch

Imeandaliwa na Theres SZekely na kutafsiriwa na Ayubu Nnko Mkulima Mbunifu: S.L.P. 14402 Makongoro Street Arusha Rununu: 0717 266 007, 0785 133 005 www.mkulimambunifu.org Barua pepe: info@mkulimambunifu.org


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.