Moduli 5, Mboji, samadi na mbolea maji (revised)

Page 1

Mkulima Mbunifu Moduli namba 5

MBOJI, SAMADI NA MBOLEA MAJI Mboji inahusika moja kwa moja na kilimo hai. Sehemu ya kutengenezea mboji ni muhimu sana kwa kuwa mbolea yote inayozalishwa shambani ndipo hukusanywa, kuozeshwa kwa ajili ya mimea, na kurudishwa kwenye mzunguko wa virutubisho kama mbolea na njia ya kufufua udongo uliochoka. Mboji ni uwekezaji wa muda mrefu kwenye udongo. Inaongeza rutuba kwenye udongo kwa kuongeza viini vya asili, na kuimarisha muundo wa udongo, na kutoa virutubisho kwa mimea ambavyo hutolewa taratibu na kwa muda mrefu.

Kuoza, njia ya asili Viumbe hai vyote, iwe mimea au wanyama, vitaoza vitakapomaliza mzunguko wa uhai/maisha yao. Kazi hiyo ni jukumu kubwa la viumbe hai vidogo sana ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho na vipo katika mazingira yetu, kwenye udongo, kwenye maji, na hata katika hewa. Bila wao, maisha duniani yasingewezekana. Mamilioni ya viumbe hawa wanaweza kupatikana katika kiganja cha udongo wenye rutuba. Kuozesha ni njia tu ya kuhamasisha njia hii ya kutengeneza mbolea na kuwa na tumaini la kuwa na mbolea nzuri. Matokeo ya muozo unatokana na malighafi hai zilizopata unyevu. Mbolea hiyo huupa udongo rangi nyeusi na si rahisi kuoza zaidi.

Mbolea asili huboresha rutuba kwenye udongo Kutumia mboji huongeza rutuba kwenye udongo baada ya muda mrefu. Hii ni sehemu na matokeo ya mbolea za asili: • Zinachukua na kuhifadhi kwa kiasi kikubwa sana cha virutubisho na chembechembe ndogo muhimu kwa ukuaji na ustawi wa mimea. • Zinaweka na kuhifadhi maji, na kuyafanya yapatikane kwa ajili ya mimea kwa kipindi kirefu. • Zinaboresha muundo wa udongo na kuukinga dhidi ya mmomonyoko unaosababishwa na maji na upepo.

Mbolea za asili na zisizo za asili Mbolea za asili kama vile mboji na samadi, aina kuu ya virutubisho vya mimea, nitrojeni (N) fosiforasi (P), na Potashiamu (K) na aina nyingine za virutubisho zimefungamanishwa kwenye mbolea za asili na huachiliwa kwa ajili ya mimea taratibu. Mbolea zisizo za asili kwa kawaida huwa na Nitrojeni, fosiforasi, na potashiamu, kwa kiwango kikubwa sana. Zinayeyuka kirahisi kwenye maji na kunyonywa haraka. Hata hivyo kutumia mbolea za viwandani peke yake hakuimarishi rutuba kwenye udongo na kuna hatari ya kusababisha tindikali (acid) kwenye udongo. Mbolea za asili zinahitajika kwa ajili ya kuhifadhi virutubisho na maji kwenye udongo. Mbolea zisizo za asili zinapotumika mkulima pia anahitajika kuzingatia kiwango cha malighafi na mbolea za asili kwenye udongo. Mbolea za asili ni muhimu sana hasa katika uzalishaji wa mboga. Aina nyingi za mboga hufanya vizuri kwenye udongo ambao una mbolea ya asili ya kutosha, mfano mnafu, kabichi, matango, au magimbi. Kwenye udongo wa aina hii mimea huvumilia minyoo ambayo ingeweza kuwa tatizo. Moduli ya MkM namba 4 (Virutubisho vya mazao ya asili) inakupa taarifa zaidi juu ya mbolea za asili na matumizi yake.

“Mboji” ina maanisha mkusanyiko, mchanganyiko. Karibu malighafi zote za mimea ya asili zinaweza kutumika kutengeneza mboji. Kutoka shambani na bustanini Mabaki ya mazao, magugu, majani yaliyodondoka, kukata matawi (aina yoyote ya mimea)

Kiasi kikubwa cha mimea yenye magonjwa inapendekezwa kuozeshwa kwa kutumia njia ya joto (Njia nzuri, tazama ukurasa unaofuata)

Kutoka kwenye banda la mifugo Samadi na mkojo, matandiko, na mabaki ya malisho. Kutoka nyumbani

Mabaki ya jikoni, maji yanayotumika nyumbani, majivu ya kuni, taka zilizofagiliwa nyumbani, na karatasi zilizochanwa chanwa.

USITUMIE:

Mabaki ya nyama (yanavutia panya na wadudu wengineo, mbwa na wanyama wa mwitu) Malighafi zisizo za asili kama plastiki na vyuma laini.


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.
Moduli 5, Mboji, samadi na mbolea maji (revised) by Mkulima Mbunifu - Issuu