Swahili translation

Page 1

Mwongozo wa Siku ya Maombi kwa ajili ya watoto wa ulimwenguni 2010 Mtoto katikati yetu Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki. Marko 10: 16 Mungu Baba, tunakuja kwako leo tukikuomba kwa pamoja kwamba uguse maisha ya watoto ambao hawajapokea mikono ya upendo wala mahali pa kuishi salama. Tunasikitika, kwa sababu hata sisi tumekosa mara nyingi moyo na mikono ya kuwapokea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ili tuwahudumie na kuwaonesha mapenzi yako kwa ulimwengu huu. Tunakuomba kwamba, vilio vya watoto hawa wanaoteseka kwa sababu ya mazingira hatarishi visikike na wale wanaoliamini Jina la Yesu Kristo. Tunakuomba uwatume wavunaji zaidi katika shamba lako la mamilioni ya watoto hawa. Tunakuomba uwalete watetezi wengi zaidi, Baba na Mama wanaoshuhudia upendo wako katika ulimwengu huu wenye tabu. Tunakuomba kwamba jamii zibadilike na watoto waweze kuona upendo wako, na ulimwengu utajua habari njema ya ufalme wako ikiwa watu wanafanya kazi kwa pamoja katika upendo na umoja. Amina. Mwongozo huu wa siku ya maombi kwa ajili ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi umeandaliwa juu ya msingi wa wazo la kumweka mtoto katikati yetu. Kila sehemu ya mwongozo unamtambulisha mtoto mmoja aliyeteseka kwa njia moja ama nyingine na inatutia moyo tumwombee pamoja na hali hii yote. Kwa watoto wengi dunia yetu inaweza kuonekana kuwa imeharibika na kukosa matumaini – lakini sisi tunaamini na kujua kwamba tumaini lipo! Kwa hiyo tunapenda kuongezeka idadi ya wakristo wanaoshiriki na kuomba kwa ajili ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ulimwenguni kote. ’Waacheni watoto waje kwangu’ Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono na kuwagusa, lakini wanafunzi wakawafukuza. Yesu alipoona hayo, alikasirika na kuwakemea wasifanye hivyo. Aliwaambia: ”Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa. Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia humo.“ Marko 10: 13-15


Wakati Yesu alipoishi hapa duniani, watu hawakuelewa kikamilifu maana ya ujumbe wa ”habari njema“ uliohubiriwa naye. Wanafunzi wake walijaribu kuwafukuza watoto wasijewa kwa Yesu, Yesu alifanya jambo la ajabu sana na bila shaka watu wa eneo hilo walishangaa mno: Alichukua mtoto mmoja na kumsimamisha kati yao akisisitiza kwamba, ikiwa wangetaka kuingia kwa kweli katika ufalme wa mbinguni walihitaji kuchagua njia hiyo ya kumfuata ya kugeuka na kuwa kama mtoto huyu. Yesu aliunda na kuweka kanuni muhimu; maana katika habari hiyo tunasoma kwamba, ’akawawekea mikono na akawabariki.’ Sisi tumeitwa kuendeleza huduma ya Yesu hapa duniani. Imetupasa tumwombe Mungu, aguse mioyo yetu kupitia maombi yetu ili tuwasaidie mamilioni ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ya ulimwengu wetu wa leo kwa vitendo na maneno yetu. Tuungane katika maombi na kugundua na kuona kwamba tunageuka! 1. Mtoto katikati yetu anayehitaji familia Fikiria – mtoto anayesimama hapa mbele ana umri wa miaka 2, nywele zake hazin’ga na anajikuna kuna kote mwilini kwa sababu ya upele na shida nyingine ya ngozi yake. Anan’goa nywele zake ili apate kutambuliwa na mlezi wake anayehitaji kuwaangalia watoto 7 wengine. Tuoneshe mwitikio gani? Zaburi 68: 5-6 Mungu akaaye mahali pake patakatifu, ni Baba wa yatima na mlinzi wa wajane. Mungu huwapa fukura makao ya kudumu, huwafungua wafungwa na kuwapa fanaka. Tuombe kwa ajili ya: - Watoto wanaoishi katika nyumba za yatima katika nchi yako. - Watu wote wanaojitoa na moyo wenye huruma na kuwasaidia watoto kufuatana na mahitaji yao kupitia nyumba na huduma kwa ajili ya yatima duniani pote. (maana mara nyingine familia za kufanya hivyo zinakosekana) - Mashirika, huduma na kanisa zinazosaidia kutafuta familia zinazotunza na kuwalea watoto yatima. - Jamii iwajibike kugundua mahitaji ya watoto hawa wanaohitaji walezi watakaowatunza na kuwapenda, na kuweka kipaumbele katika kuwasaidia watoto yatima wapate makazi na familia katika mazingira yao. Vitendo: Wafikirie mpango wa kumkaribisha mtu katika familia yako ambaye hajawahi kuishi katika familia ya watu wanaopendana. Wajadili katika makundi madogo: Jambo gani linamsaidia kujisikia nyumbani? Utajisikiaje kama mtu anayemkaribisha? Shida gani zinaweza kutokea? Ungependa kumwonesha kitu gani? 2. Mtoto katikati yetu anayeteseka kwa kukandamizwa


Fikiria – mtoto huyu anayesimama hapa mbele alipigwa sana na baba yake ambaye amelewa sana. Hisia zake usoni zinamfanya aonekana kuwa mkubwa zaidi kuliko miaka 12. Anatuangalia kwa macho yaliyovimba kwa sababu ya mapigo. Tuoneshe mwitikio gani? Yeremia 29: 11 Maana , mimi Mwenyezi Mungu ninajua mambo niliyowapangia. Nimewapangieni mema na si mabaya, ili mpate kuwa na tumaini la baadaye. Tuombe kwa ajili ya: - watoto wanaoteseka kimwili au kisaikolojia (kwa mfano kupitia maneno matusi au maneno ya kudharauliwa) kutoka kwa wazazi au watu wengine wazima. Tuwaombee watu wa aina hii wabadilike tabia yao. - Mafundisho na semina nzuri zinazowawezesha wazazi na walezi kuwalea watoto bila kuwakandamiza na kuwaumiza. - Serikali itambue/igundue hali ya upekee na thamani ya kikundi cha familia, kuheshimu na kuhamasisha ndoa, kulinda na kusaidia familia na ndoa zishikamane. Vitendo: Chora mkono mmoja mkubwa ubaoni au katika karatasi kubwa. Kusanya vitendo ambavyo mikono yetu inaweza kuvitenda: Vitendo vyema na Vitendo vibaya. (Itakuwa vizuri ukiwa umewaongoza watoto mapema waandike vitendo mbalimbali katika karatasi ndogo wakiwa wanatumia rangi nyeusi kwa vitendo vibaya, na rangi nyekunde kwa ajili ya vitendo vyema. Wakati wa ibada watakuletea vitendo hivi mbalimbali na utavibandika vyote katika mkono huu mmoja) Malizia na maombi na kuomba kwamba Mungu atuoneshe wiki hii nafasi ya kumbariki mtoto mmoja kupitia kwa vitendo vyetu vya mikono. Omba pia, watoto katika mazingira hatarishi wapate kuona mikono inayopenda, kutunza, kuwalinda, mikono inayobariki na sio kuumiza. 3. Mtoto katikati yetu anayekosa nafasi ya kupata elimu Fikiria - mtoto anayesimama hapa mbele ni msichana mdogo mwenye umri wa miaka 9 ama 10. Hawezi kuyasoma maneno yaliyoandikwa katika kipande cha karatasi ambacho anashika mkononi. Ikiwa angeweza kusoma atashangaa, kwa sababu angesoma habari kwamba wazazi walimpeleka aishi mjini wakitumaini apate maisha mazuri. Tuoneshe mwitikio gani? Isaya 54: 13 Watu wako watafunzwa nami Mwenyezi Mungu, wanao watapata ustawi mwingi. Vitendo: Uwaandae watoto wawili waje wakiwa wamevaasale ya shule pamoja na mifuko na daftari zao na eleza kwamba bado watoto wengi hawana nafasi kwenda shuleni kwa sababu mbalimbali. Watoto wenyewe wataje mambo ya kuombea: Tuombe kwa ajili ya: - watoto wanaokosa nafasi kwenda shuleni kwa sababu ya shida ya ulemavu au ugonjwa wa ki-akili.


-

watoto wanaoishi katika familia maskini na kukosa uwezo wa kununuliwa sale ya shule na vitabu, na hivyo hawawezi kwenda shuleni. Watoto wanaohitaji kufanya kazi ili wapate riziki kwao na familia zao, na hivyo hawawezi kwenda shuleni. Mashirika ambayo yanawasaidia watoto wa aina hii kupata elimu, na hasa mashirika ya kikristo. Serikali za nchi zisisitize malengo yaliyokubaliwa na UN Millennium Summit (Millennium Development Goals) ya kuandaa na kutoa elimu kwa watoto wote wa shule ya msingi. Tuwaombee watoto wetu wanaokwenda shuleni wapate kuelewa na kufaulu katika mitihani.

4. Mtoto katikati yetu mwenye mateso kwa sababu ya njaa na umaskini Fikiria – Mtoto anayesimama hapa mbele angefanana kama sanamu tunazoweka katika shamba la mpunga, nguo zake zimechakaa na kupeperushwa na upepo, na anahangaika kuinua kichwa chake. Mwonekano wake unafanana kama mtoto wa umri wa miaka 4, lakini kwa kweli yeye ameshafikisha umri wa miaka 7. Ngozi yake ilikauka na hata rangi yake inaonesha kwamba anakosa afya njema. Alikosa siku zote mlo kamili na hajui hisia za kujisikia kuwa ameshiba vizuri. Tuoneshe mwitikio gani? Mathayo 25: 44-45 Hapo nao watajibu; Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukukuhudumia? Naye atawajibu, ’Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi. Tuombe kwa ajili ya: - Wema na upendo uongezeke kwa ajili ya watoto wanaoishi katika hali ya umaskini. - Serikali za nchi zigawe misaada na vyakula kwa njia ya haki ili walengwa wenyewe wasaidiwe kufuatana na mahitaji yao. - Jamii itambue umuhimu wa kusaidia zaidi kwa upande wa mahitaji ya wenye njaa na umaskini, ili idadi ya vifo na magonjwa yapungue, maana matibabu yatapatikana. - Njia mpya za kuisaidia jamii maskini. - Kuunda sheria mpya zinazowathamini watoto na kuwawezesha kuachana na umaskini na kuwaonesha njia za kuishi maisha ya tumaini. - Jamii ya kikristo ikue katika imani na kupata mazoea ya kumwona Mungu na njia zake za ajabu za kusaidia. Vitendo: Uandae paketi ya biskuti na uwaite watoto kama nane (8) na kuwaketisha chini. Uzigawe biskuti kwa njia isiyo sawa, wengine wanapata bikuti moja tu, wengine mbili, na wengine nyingi kidogo. Uwaulize watu wanavyojisikia kuona baadhi ya watoto wanapata biskuti nyingi na wengine wanakosa, badala yake watasikia njaa. Uwafanye wafikirie hali ya ulimwengu wetu: watoto wengi wanaishi kwa chakula kidogo sana siku kwa siku wakati watu wengine wanakula zaidi kuliko wanavyohitaji. Unajisikiaje ukiwaona watu katika jamii yetu wanaishi hali ya chini sana?


5. Mtoto katikati yetu – aliathiriwa kwa kufiwa Fikiria – Mtoto ambaye anakaa hapa mbele yetu akiwa pamoja na dada na kaka zake anajaribu kusimama akiwa amesimama magotini. Miguuni mwake kuna mtoto mdogo anayetambaa na yeye anamsaidia kusimama akimwinua kwa mkono wake. Ukimtazama kijana huyu mwenye umri wa miaka 13 utasoma uchovu katika sura yake. Alifiwa na watu wazima wote wa familia yake mwaka uliopita. Wote walikufa kwa sababu ya UKIMWI. Tuoneshe mwitikio gani? Mhubiri 3 Kwa kila kitu kuna majira, na wakati kwa kila jambo duniani: Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa..... Tuombe kwa ajili ya: - Kupata familia za kikristo zaidi ambazo zitakuwa tayari kuwapokea watoto waliofiwa na wazazi wao (yatima wa UKIMWI) na kuwalea. - Watoto waliobaki kama kiongozi wa familia, wapate msaada, elimu na kutiwa moyo. - Huduma na mashirika yanayotoa elimu na hamasa kuhusu mambo yote ya UKIMWI. - Nchi zingine zifuate mfano wa Uganda. Serikali yao inasaidia na kuhamasisha kwamba wajawazito wote wapewe dawa ya ARV (dawa ya kupunguza ukali wa virusi) ili watoto wenyewe wasiambukizwe na UKIMWI pia. - Kujenga na kuimarisha mahusiano katika ya ndoa na familia ili wawe na uaminifu kati yao na hivyo kuzuia maambukizo ya UKIMWI. - Watoto katika mazingira hatarishi mengine kama vita, magonjwa na maafa ya asili. Vitendo: Andaa mawe madogo madogo (kama 12- 15) na vipande vidogo vidogo vya nguo. Omba na uwakaribishe watu na watoto wanaokumbuka kitu walichokipoteza/ mtu waliyempoteza wakati ulipopita. Wakati wanapoeleza kwa kifupi wachukue jiwe moja ambalo kiongozi wa kipindi alifunike na kipande cha nguo kuonesha tumekumbuka shida yake. Weka jiwe chini. Baada ya kuwasikiliza watu / watoto mbalimbali upangilie mawe haya yote kama msalaba na umkabidhi Yesu hisia zote zenye huzuni kwa sababu ya kupoteza kitu au mtu. Uwaombee hasa watoto waliowapoteza wazazi au walezi wao kwa moyo wenye huruma. www.viva.org


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.