Mwanamke Mkenya Toleo 20

Page 1

1

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Mwaka mmoja baadaye Kutazama utekelezaji wa sheria kwa darubini ya jinsia

…Na Odhiambo Orlale

W

anawake wana kila sababu ya kusherehekea maadhimisho ya mwaka wa kwanza tangu kuzinduliwa rasmi kwa katiba. Milango ambayo hapo awali ilikuwa imeshika kutu nzito isiweze kufunguka imeanza kutiwa mafuta ya kuilegeza na kufunguka, yote hayo sababu yake ikiwa ni mafuta yanayojulikana kama sheria hii mpya. Mnamo siku ya kuanzishwa rasmi kwa katiba, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mwai Kibaki, aliitia saini katiba hiyo na akawaahidi Wakenya kwamba aitailinda na kuitetea sheria hiyo mpya. Kunako siku hii kadhalika Wakenya waliwashuhudia Waziri Mkuu Raila Odinga na Makamu wa Rais Kalonzo Musyoka wakiahidi kuwatumikia Wakenya chini ya katiba hii mpya na kadhalika kuilinda. Watunga sheria ambao ni Wabunge pia walikula viapo vya kuitetea katiba huku mawaziri na majaji pia wakiapa kuitetea katiba hiyo mpya. Hiyo ikiwa na maana ya kuheshimu kila neno lililomo ndani ya katiba hiyo yakiwemo mafanikio ambayo yanapendelea haki za wanawake na kupewa uwezo miongoni mwao, kupewa nafasi zaidi katika ulingo wa siasa na katika ngazi za utoaji maamuzi. Hata hivyo, uamzi wa hivi majuzi wa Baraza la Mawaziri la kutangaza kanuni ya thuluthi moja katika katiba kuwa isiyoweza kutekelezwa ni uzandiki wazi wa ubaguzi wa kijinsia na kutumiwa vibaya kwa manufaa ya wanawake katika sheria hiyo mpya. Hata ingawa baraza hilo la mawaziri lilipendekeza kuundwa kwa jopo kazi la kuchunguza kanuni hiyo ambayo imezusha mgogoro, na kuwasilisha matokeo ya uchunguzi wake kwao, wanawake wana hofu kwamba kama katika hatua hizo za awali za utekelezaji wa katiba unazusha mgogoro, haitachukua muda mrefu tena kabla ya mafanikio ya wanawake kuondolewa kabisa.

Matarajio mema Hata hivyo, Wakenya na wanawake kwa ujumla wanasubiri roho mkononi huku wanawake wakitazamia kwamba mzozo huo utasuluhishwa haraka iwezekanavyo na kwa manufaa yao. Tangu kuanza kutumiwa kwa katiba mpya, wanawake wamefanikiwa kupata kazi za mamlaka makubwa kwenye utekelezaji wa katiba mpya. Kwa mfano Nancy Baraza alipitia moja ya taratibu ngumu za mahojiano ya hadhara ya uteuzi wa Naibu wa Jaji Mkuu, kabla ya kuteuliwa kwenye mamlaka hayo ili kufanyia matengenezo idara hiyo ya mahakama. Ama kwa kweli manufaa ambayo wanawake wamepata kuanzia wakati wa Tume ya Marekebisho ya Katiba ambayo ilijulikana kwa jina maarufu la Bomas miaka mitano iliyopita na kushirikishwa kwenye katiba mpya, yanatekelezwa kikamilifu kwa dhati ya moyo wa katiba hiyo. Uteuzi wa aliyekuwa Mbunge Maalumu Njoki Ndung’u kama mmoja wa majaji saba wa mahakama kuu ni moja ya mafanikio ya wanawake ingawa bado kuna kesi inayopinga urari wa kijinsia katika idadi ya majaji wa mahakama hiyo kuu. Kulingana na wengi wa viongozi wanawake, tatizo kubwa hapa ni kwamba hawako tayari

Picha ya juu aliyekuwa Mkuu wa Sheria, Bw Amos Wako (mwenye wigi kichwani) akishuhudia Rais Mwai Kibaki akitia sahihi stakabadhi kuidhinisha rasmi katiba mpya mnamo Agosti 27, mwaka jana. Kulia, Rais Kibaki akionyesha kwa hadhara stakabadhi hiyo ya kuidhinishwa katiba mpya. Sherehe hii ilifanywa katika bustani ya Uhuru Park, Nairobi. kuwaruhusu viongozi wa kisiasa kuitekeleza katiba kuanza na utekelezaji usiofaa huku kukiwa na udhaifu mkubwa katika kushughulikia maswala ya kijinsia. Jaji Mkuu, Dkt Willy Mutunga alianzisha utangulizi bora wakati alipowaambia wanasiasa kwamba wanahitajika kusikiliza kwa makini na kuelewa kwamba Kenya ina wanawake ambao wana elimu na wenye uwezo wa kufikisha idadi ya thuluthi moja ambayo katiba inapendekeza

izingatiwe, wakati alipowateua wanawake kumi na watatu kati ya watu ishirini na wanane kuchukua nyadhifa za mahakimu wa mahakama kuu ambao wameteuliwa hivi punde. Lydia Achode ambaye ni msajili mkuu wa mahakama anayeondoka ni miongoni mwa majaji walioteuliwa pamoja na Pauline Nyamweya. Wengine ni Mumbi Ngugi, Beatrice Angalia Uk.2


2

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Serikali lazima idhihirishe nia njema ya kisiasa

P

endekezo la Baraza la Mawaziri juu ya haja ya kutafuta njia ya kushughulikia kifungu cha 81(b) cha katiba ambacho kinasema kwamba uteuzi wa maafisa wa kuhudumu katika nyadhifa za umma usizidi thuluthi mbili ya jinsia moja, limezusha wasiwasi mkubwa sio tu kwa wanawake wa Kenya bali pia kwa wananchi ambao walipiga kura kuiunga mkono katiba hiyo mpya. Kulingana na wengi wa Wakenya, hatua hiyo inaenda kinyume na misingi iliyowafanya Wakenya kupigania katiba mpya kwa miongo miwili. Kama alivyosema mkurugenzi mkuu wa baraza la kitaifa la kupigania mageuzi, NCEC, Cyprian Nyamwamu, kwenye mkutano ulioandaliwa na wanawake kutafuta njia ya kupata kutekelezwa kwa ahadi ya kifungu hicho alifafanua kwa ustadi mkubwa.

Ushirikishaji Alisema kwamba harakati za kupigania katiba mpya zilihusu mambo matatu. “Harakati hizo zilinuiwa kupambana na urundikaji wa mamlaka katika sehemu moja na utumiaji mbaya wa mamlaka, hivyo basi kukapatikana ugavi wa mamlaka na kugawanywa kwa kazi na kuleta uwajibikaji, kukabiliana na utovu wa haki za kijinsia na kutoshirikishwa kwa makundi ya watu wanaogandamizwa na makundi ya watu wachache ambapo wanawake ni baadhi yao na kadhalika na kuratibiwa kwa haki na mipango ya utawala katika misingi ya Mswada wa Haki,” akasema Nyamwamu, huku akiongeza kwamba “hili si swala la wanawake, bali ni swala linalowahusu Wakenya wote kwa jumla.” Dkt Linda Musumba naye anathibitisha kwamba suluhisho la swala la thuluthi mbili linapaswa kutafutwa kwa ushirikiano wa serikali na vyama vya siasa kwa kuwa vitakuwa muhimu katika kuhakikisha kwamba wanawake wanafanya idadi ya thuluthi moja ya wale watakaochaguliwa. Mkurugenzi wa kongamano la wanawake viongozi wa kisiasa, Dkt Deborah Okumu alisisitiza kwamba suluhisho la kupatikana kwa kiwango cha thuluthi mbili halihitaji marekebisho ya kikatiba, bali linaweza kupatikana kupitia mswada wa uchaguzi na vyama vya siasa am-

Na Rosemary Okello

bayo miswada hiyo iko mbele ya Bunge “Tangu kongamano za Tume ya Uchunguzi wa Marekebisho ya Katiba ya Kenya (KCRC) hadi kwenye mkutano wa katiba wa Bomas, mkutano wa Naivasha, utaratibu wa kikatiba wa Kilifi na mwishowe Kamati ya Wataalamu, kila mtu na hasa mawakili walikuwepo na tukaambiwa kwamba katiba ni utaratibu wa kisheria ambao haushirikishi mambo kwa urefu na kwamba mambo hayo yenye kueleza kwa urefu yamefanyiwa ukusuru ndani ya sheria hiyo. Kuanzia hapo wanawake wa Kenya wamesonga mbele kuweka mikakati katika miswada hiyo miwili, lakini imekataliwa,” aeleza Okumu. Kulingana na Okumu, ni jambo la kusikitisha kwamba wanaume wanafafanua swala hilo kumaanisha kwamba wanawake wanataka viti vya bure. “Tunahitaji kujifunza kutokana na historia kwamba kufikia kiwango cha asilimia 30 ya wanawake kwenye viti vya kiuchaguzi nchini Kenya limekuwa jambo gumu na tangu uhuru kupatikana hakujakuwa na nia njema kwa upande wa vyama vya siasa kuhusiana na uwakilishi wa wanawake,” akasisitiza. Okumu anaongeza kwamba harakati za upiganaji maslahi ya wanawake ni za kiubaguzi kwa jinsia nyingine ili iweze kuleta ubaguzi ambao utasababisha usawa wa kijinsia kwenye nyadhifa za kiuchaguzi. Huku Wakenya wakijadiliana kuhusu miun-

do mbinu ambayo itatumiwa kufanikisha hitaji la thuluthi mbili ambalo halishirikishi ufafanuzi zaidi wa kina, huko kusini mwa Afrika, viongozi wote wa nchi walitia saini maazimio ya jinsia na maendeleo ambayo yanatilia mkazo hitaji la uwakilishi wa asilimia hamsini wa wanawake katika ngazi zote za serikali kufikia mwaka 2015 na zaidi ya hayo, maazimio hayo yanayataka mataifa wanachama kutunga sheria ambazo zinatoa hakikisho kwamba miundo ya kisiasa na ya kimaongozi inazingatia usawa wa kijinsia. Maazimio hayo yanatayarisha mipango ya utekelezaji ambayo inaweka shabaha maalumu na wakati wa kutekelezea mipango hiyo ya kufanikisha usawa wa kijinsia katika nchi zote wanachama wa Jumuiya ya SADC pamoja na mipango stadi ya uchunguzi na ukaguzi wa mipango hiyo.

Beijing Katiba hiyo mpya ilichukuliwa na makundi ya wachache miongoni mwa Wakenya kuwa chombo cha dhati cha kuimarisha ushiriki wa wanawake katika ngazi za uongozi kuanzia katika kaunti hadi katika ngazi za kitaifa. Hayo yanaambatana na uamuzi wa kuimarisha maslahi ya wanawake katika ngazi za utoaji maamuzi kote ulimwenguni harakati ambazo zilianza kushika kasi mnamo miaka ya 1980 na mapema miaka ya 1990 kupitia msururu wa mikutano ya

“Tunapaswa kujifunza kutokana historia kwamba kupata asilimia 30 kwa vyoo vya kuchaguliwa ni ngumu sana” — Deborah Okumu

kimataifa. Harakati hizo ziliongezewa nguvu na mkutano wa nne wa kimataifa uliofanywa mjini Beijing huko China mnamo mwaka 1995 ambao ulitoa mwito wa kuzingatiwa kwa aslimia 30 ya uwakilishi wa wanawake katika ngazi za kitaifa katika serikali za ulimwengu. Mnamo mwezi Septemba mwaka 2000 kwenye mkutano wa milenia wa Umoja wa Mataifa mjini New York, viongozi wa ulimwengu waliahidi “kuimarisha usawa wa kijinsia na wanawake kupewa uwezo kama njia mwafaka za kupambana na umaskini, njaa na magonjwa na kusisimua maendeleo yanayoweza kudumishwa.” Hivyo basi, ili Kenya ichukue nafasi ya kwanza miongoni mwa nchi za Afrika, wanasiasa wanapaswa kuwajibika katika swala la kanuni ya thuluthi mbili na kama ilivyosemwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dkt Kofi Annan.” Chunguzi baada ya chunguzi zilizofanywa zinaonyesha kwamba hakuna mbinu yoyote ya maendeleo ambayo wanawake hawatekelezi majukumu makubwa na wakati ambapo wanawake hushirikishwa kikamilifu katika utekelezaji wake manufaa huonekana kwa haraka. Jamii huwa na afya bora zaidi na kulishwa vyema na mapato yao na akiba zao na uwekaji raslimali huimarika. Dkt Annan aliongeza kwamba; “Na kilicho ni cha ukweli kwa familia ni cha ukweli kwa jamii nzima na hatimaye kwa nchi nzima.” Rwanda ni mfano ambao unatumiwa katika kuonyesha athari njema za wanawake katika uongozi kwenye hatua katika masuala ya hali ya mwanamke na maendeleo kwa jumla. Akinukuliwa katika taarifa kuhusu wanawake, Oda Gasinzigwa ambaye ni Waziri wa Jinsia wa Rwanda anasema; “Ni vyema kututambua kwamba kuna mafanikio mengi ambayo tumeyapata na utendaji stadi wa kazi unatokana na nia njema ya kisiasa.Uongozi umetuamini kushiriki katika kila ngazi ya sekta zote za kimaendeleo.” Ni kutokana na sababu hizo ndipo majadiliano kuhusu kanuni ya thuluthi mbili inahitaji nia njema ya kisiasa ambayo ni serikalio pekee ndiyo inayoweza kuhakikisha.

Kutazama utekelezaji wa sheria kwa darubini ya jinsia

Kutoka Uk1

Thuranira, Grace Nzioka, Christine Meoli, Hedwig Ongudi, Stella Mutuku, Rose Ougo, Roseline Korir, Abigail Mshila na Stella Muketi. Katiba mpya ilianzisha wadhifa mpya wa msajili mkuu kusimamia shughuli zote za mahakama na wadhifa huo umechukuliwa na Gladys Shollei ambaye ni msajili wa idara ya mahakama, kuchukua mahali pa Lydia Achode. Jaji Mkuu anasema Bi Shollei aliteuliwa baada ya utaratibu thabiti wa mahojiano ya kazi ambao ulikuNjoki Ndung’u Mumbi Ngugi Pauline Nyamweya Lydia Achode wa wa haki na uwazi. Kabla ya kuteuliwa katika wadhifa huo, Gladys Dkt Mutunga alikariri kwamba utaratibu ndani ya muda iliyowekewa wa kukamilisha mswada waUraia wa Kenya na Uhamiaji, mswada alihudumu kama naibu wa afisa mkuu wa usi- wa uteuzi ulitilia maanani pia hali ya mseto wa uchunguzi wa sheria 23 ndani ya mwaka wa wa Uraia wa Kenya na Usimamizi wa Huduma mamizi wa uchaguzi katika tume huru ya muda watu unaodhihiri katika Idara ya Mahakama kwanza tangu kuzinduliwa kwa katiba mpya. za Raia wa Kigeni na mswada wa Miji na Vijiji, ya usimamizi wa uchaguzi (IIECC). kwa lengo la kushughulikia mapengo yaliyomo. Kati ya miswada ishirini na minne ambayo mswada wa Mazingira na Mahakama yaArdhi na Umuhimu wa uteuzi huo wa mahakimu Moja ya mapengo hayo ni ukosefu wa usawa wa inasubiri kukamilishwa ndani ya mwaka wa mswada wa Usimamizi wa Pesa za Umma. kinyume na uteuzi wa majaji wa mahakama kijinsia. Pamoja na hayo yote shughuli ya utekelezaji kwanza wa katiba ya Kenya ya mwaka 2010, ni kuu ni kwamba ulitimiza kanuni na kupitisha Hadi kufikia sasa, Tume ya CIC imehakiki- mswada wa Usimamizi wa Fedha za Umma ndio wa katiba kwa jumla imekuwa shwari kwa wastani kiwango cha thuluthi moja ya jinsia moja kama sha kwamba mengi ya manufaa waliyopata wan- ambao umecheleweshwa na tofauti za kimaon- sio kama ilivyotarajiwa na baadhi ya watu. inavyosisitiza katiba. Kanuni ya kutokuwa na awake kutoka kongamano la kihistoria la Bomas, gozi kati ya pande zinazohusika bado unasubiri Thuluthi mbili zaidi ya thuluthi moja ni swala ambalo bado yamefungamanishwa na kushirikishwa kwenye kukamilishwa na tume hiyo siku kumi kabla ya linazozaniwa mahakamani kuhusiana na uteuzi sheria ishirini na saba zilizopelekwa bungeni na muda wa mwisho kufika. Jitihada zinafanywa Kuna matumaini makubwa miongoni mwa Idara ya Utawala kufanywa sheria. wa majaji wa mahakama kuu. kuhakikisha kwamba mswada huo unakamil- wanawake wakati huu ambao shughuli hiyo Kuhusiana na uteuzi wa majaji, Dkt Muishwa kabla ya muda huo kumalizika. inaingia katika awamu yake ya pili ya utekelezaji Utekelezaji katiba tunga alisema: “Tumewatafuta wagombezi wa Huku muda ukizidi kuyoyoma kuelekea wa katiba hukiu tunaposubiri uchaguzi mkuu nyadhifa hizo kutoka sehemu mbali mbali kama Sheria tano za kwanza za kikatiba ambazo dakika za mwisho, Baraza la Mawaziri limefanya chini ya katiba hiyo mpya. ilivyoagiza katiba na sheria ikiwa ni pamoja na zilijadiliwa na kupitishwa na Bunge la kumi ni kazi ya ziada ili kuhakikisha kwamba inakamilKwa wanawake hakuna kizuizi safari hii katika maswala ya kijinsia, asili, kaunti, vizazi watu wa sheria ya uteuzi huru wa maafisa, sheria ya tume isha shughuli zake kuhusiana na miswada hiyo. jitihada zao za kuhakikisha kwamba wanakamilmakabila madogo na aina nyingine za ugan- huru ya mipaka na uchaguzi, sheria ya huduma Miswada mitatu iliyoidhinishwa na kupelekwa isha kanuni ya thuluthi moja katika nyadhaifa za damizaji. Huku tunapoadhimisha mwaka wa ya Idara ya Mahakama, sheria ya huduma ya bungeni katikati ya mwezi Agosti ni mswada wa uteuzi na za kiuchaguzi kwani elimu wanayo na kwanza tangu kuzinduliwa rasmi kwa katiba Mahakama Kuu, na sheria ya ukaguzi wa majaji Kanuni na ile ya Tume ya Kupambana na ufisa- uwezo wanao. Kenya ina wanawake wenye elimu di, mswada wa Uwezo wa Imani na mswada wa na hamasa kubwa ya kisiasa kufikia shabaha yao mpya, utekelezaji wa katiba kama unavyoon- na mahakimu ya mwaka 2011. Tume ya utekelezaji wa katiba (CIC), im- Mashujaa wa Kenya. ya kanuni ya thuluthi mbili. Wanachohitaji ni kugozwa na Tume ya Usimamizi wa Utekelezaji wa Miswada ambayo inasubiri kushughulikiwa ni pewa nafasi katika uwanja uliojaa wanaume na Katiba umepiga hatua kubwa za manufaa, lakini etekeleza jukumu lake kama ilivyotarajiwa kwa kuhakikisha kwamba inatekeleza kazi zake pamoja na mswada wa Uidhinishaji wa Mikataba, bila shaka watathibitisha kwamba wanaweza. bado kuna changamoto tele.


3

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Mfumo huu wa wanaume Enyi wanawake wa Kenya simameni kulinda haki zenu!

…Na Faith Kasiva

P

endekezo la Baraza la Mawaziri la kutayarisha mswada wa marekebisho ya katiba kufanyia marekebisho kifungu cha usawa wa kijinsia katika katiba ya Kenya (CoK) ya mwaka 2010 ni mwito wa kusisimua kwa dhati harakati za utetezi wa maslahi ya wanawake hapa nchini. Arafa iliyotolewa na Idara ya Habari ya Rais iliyopelekwa kwenye vyombo vya habari siku ya Alhamisi Agosti 18, mwaka huu ilisema: Kuhusiana na hitaji la uwakilishi bungeni la thuluthi moja ya moja ya jinsia, Baraza la Mawaziri limeamua kuunda jopo kazi kutayarisha mswada wa marekebisho ya kikatiba kushughulikia hitaji hili muhimu ambalo lina ugumu mkubwa katika kulitekeleza chini ya kanuni zilizopo. Hizo ni habari za kushtusha sana kwa wengi kwani hata mwaka haujamalizika tangu utekelezaji wa katiba hiyo kuanza kufanywa. Nilipochunguza kwa undani habari hizi nilifahamu kwamba mfumo wa wanaume kutawala mambo unajaribu kujipigania.

Historia Historia ya ukombozi wa wanawake nchini Kenya inatupeleka miaka mingi nyuma kuanzia mapambano ya wanawake kuwa na haki ya kuchaguliwa na harakati za kuratibu mipango ya kisheria na ya kitaasisi inayowahusu wanawake. Mnamo mwaka 1996, Charity Ngilu ambaye kwa sasa anahudumu katika wadhifa wa waziri aliwasilisha hoja bungeni kuhusiana na utekelezaji wa maazimio ya Beijing bila mafanikio. Kadhalika Phoebe Asiyo na Beth Mugo walijaribu bila mafanikio kuwasilisha mswada wa harakati za utetezi wa wanawake katika mwaka wa 1996 na mwaka wa 2000. Mnamo mwaka 2007, Serikali ya Kenya kupitia aliyekuwa wakati huo Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba, Bi Martha Karua, waliwasilisha bungeni mswada wa marekebisho ya katiba ya mwaka 2007 ikipendekeza kuanzishwa viti vingine hamsini katika Bunge la kumi. Mswada huo haukupitishwa kwa sababu Wabunge wanaume walitoka nje ya Bunge na

kuunyima mswada huo Wabunge wa kutosha wa kuujadili na kuuidhinisha. Lakini katiba ya Kenya ya mwaka 2010, ilileta manufaa makubwa kwa wanawake kwa vile inatoa muundo wa kisheria wa usawa wa kijinsia na wanawake kupewa uwezo. Hivyo basi utetezi wa maslahi na haki za wanawake katika katiba zinathibitishwa na kulindwa na vifungu vya sheria ikiwa ni pamoja na kifungu nambari 27(8) ambacho kinasema kwamba Serikali itachukua hatua za kisheria na hatua nyinginezo kutekeleza kanuni kwamba idadi isiyozidi thuluthi mbili ya maafisa katika nyadhifa za uchaguzi au za uteuzi ndio watakaokuwa waakilishi wa jinsi moja. Kifungu nambari 81(b) kinasema kwamba idadi isiyozidi thuluthi mbili ya maafisa wa mashirika ya umma ambao watachaguliwa watakuwa wa jinsi moja.

Naomi Shaaban Hilo ndilo tatizo linalolikanganya akili Baraza la Mawaziri hadi kufikia kusema kwamba kanuni hiyo haitekelezeki, labda kwa sababu ya kesi inayoendelea mahakamani ambako shirika la wanawake nchini likiongozwa na shirika la mawakili wanawake, FIDA, limepinga muundo wa majaji wa mahakama kuu na kuzuia utekelezaji wake hadi leo. Pendekezo hilo la baraza la mawaziri limepokelewa kwa maoni tofauti. Huku mashirika ya wanawake na Wabunge wengine wanawake wakipinga kwa dhati pendekezo hilo, Waziri wa Jinsia, Dkt Naomi Shaaban kwenye mazungumzo na waandishi habari alionekana kuunga mkono pendekezo hilo la Baraza la Mawaziri akisema ni sehemu ya majukumu ya pamoja. Lililoshangaza hata hivyo, ni matamshi ya Dkt Shaaban kwamba wanawake wanapaswa kupigania viti vya Bunge wakishindana na wanaume. Matamshi hayo yanadhihirisha kukosa fahamu kwa upande wa waziri huyo na hayuko sambamba na kanuni za haki na maslahi ya wanawake na usawa wa kijinsia ulimwenguni kote. Harakati za wanawake nchini zinapaswa kuhoji kutoka kwa waziri huyo kama ndiye hakika anayefaa kuongoza wizara hiyo kwa

Wabunge wawili, Bi Joyce Laboso (kushoto) akiwa na mwenzake Mbunge Maalum Bi Rachel Shebesh wakihutubia wandishi habari kulaumu jaribio la Baraza la Mawaziri la kutaka kubadilisha kile kifungu cha theluthi mbili kutoka kwa katiba mpya. kuwa alikuwa mmoja wa kundi la wanasiasa waliopinga kuidhinishwa kwa katiba hii. Bi Atsango Chesoni aliyekuwa naibu mwenyekiti wa Tume ya Wataalamu waliotayarisha katiba ya mwaka 2010, amepinga hatua ya kufanyia marekebisho katiba hiyo kuhusiana na kanuni hiyo ya thuluthi moja. Anapendekeza kwamba kama Baraza la Mawaziri linataka namna na jinsi ya kukabiliana na hitaji hilo, basi linapaswa kurejea kwenye kifungo cha 121 cha katiba ambacho kilipendekeza mseto wa uwakilishi wa maafisa ambao uliwasilishwa kwa kamati ya Bunge mnamo Januari 8, mwaka 2010.

Ubabe wa wanaume Atsango ametaka mashauriano ya dhati kabla ya marekebisho yoyote kufanyiwa katiba ili kuepuka kuzusha mtafaruku. Anasema: “Swala kuu ni iwapo kuna nia njema ya kisiasa kuhusiana na kanuni za usawa na kama tunakabiliwa na wale ambao wanataka kuanzisha mzozo wa kikatiba kwa makusudio ya kuleta uchafuzi.” Kunako maadhimisho ya mwaka wa kwanza wa katiba mpya, manufaa waliyopata wanawake yanakabiliwa na tishio la kuangamizwa

na kubadilishwa. Ubwana wa wanaume wa kutaka kutawala mambo yote unajitokeza upya kupigana kukomesha mafanikio ya wanawake. Maoni ya Baraza la Mawaziri kwamba kanuni ya thuluthi mbili kwa moja haiwezi kutekelezeka hayakubaliki. Nchi nyingine ikiwa ni pamoja na Rwanda, Uganda, Afrika Kusini na nchi za Scandinavia zimetekeleza kanuni hiyo. Licha ya hakikisho la Waziri Mkuu na Makamu wa Rais kwamba uamuzi huo wa Baraza la Mawaziri ulieleweka kimakosa, bado ni mwito wa kuwataka wanawake wawe macho. Wanawake wa Kenya wamesubiri kwa muda mrefu kupata haki zao kwenye nyadhifa za kiuchaguzi na kiuteuzi. Majaribio yoyote ya viongozi wachache kuwanyima wanawake haki zao kama ilivyoidhinishwa na wengi wa Wakenya wakati wa kura ya maoni, wanapaswa kupuuzwa na kutupiliwa mbali kwa njia yoyote ile. Huu ndio wakati ambapo wanawake wa Kenya wanapaswa kuungana pamoja bila kujali kabila, asili, tofauti za kisiasa ili kulinda kwa ushupavu mafanikio ya wanawake waliyopata kupitia katiba mpya ya mwaka 2010 kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Rekebisho dogo katika katiba au kufutwa kwa manufaa yote? ba iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mheshimiwa Abdikadir Mohammed na naibu wake Mheshimiwa Ababu Namwamba mjini Naivasha kupanga idadi ya viti katika Bunge kuwa viti 290. Kwa kuwa idadi iliyokubaliwa ya kaunti ilikuwa ni 47, idadi ya viti vinavyopaswa kushikiliwa na wanawake pia ni 47.

Na Atsango Chesoni

Kipengee hicho Katika makala haya Atsango Chesoni ajibu uamuzi wa Baraza la Mawaziri wa kuifanyia katiba marekebisho dhidi ya manufaa kwa wanawake.

K

amati ya Wataalamu (CoE) kwa hakika iliweka mpango wa mseto wa waakilishi kwenye mapendekezo kadirio ya katiba yaliyowasilishwa kwa Kamati Teule ya Bunge (PSC) mnamo tarehe nane mwezi Januari

mwaka 2010. Kifungu cha 121 cha mapendekezo ya katiba kinalitaka Bunge liwe na:(a) Wabunge wachaguliwe kila eneo mbunge mmoja kama itakavyoagiza sheria. (b) Wanawake wateuliwe mmoja kwa kila kaunti, kila kaunti iwe na mwakilishi wa jinsia hiyo. Kanuni hii ya kisheria ilifanyiwa marekebisho na kamati maalum ya Bunge kuhusu uchunguzi wa kati-

Kisha waliondoa vipengee vyote vinavyohusiana na uwakilishi wa mseto wa Wabunge na kuweka kipengee cha Wabunge 12 wa teule ambao wanawakilisha “maslahi maalum”, aina ya Wabunge ambao watu wa Kenya walielezea kwamba wanafaa kuwepo. Ijapokuwa kamati ya wataalamu ilielezea wasiwasi kuhusu marekebisho hayo, tulifahamishwa ya kwamba hicho ni kipengee ambacho hatupaswi kukigusa na kwamba ndicho kilichosababisha maafikiano ya Naivasha. Kwa kuwa utayarishaji wa katiba ni shughuli ya kisiasa, tulikuwa na

wasiwasi kwamba vipengee kuhusiana na wanawake vingekuwa rahisi kuleta umoja kwa Bunge kufungua mapendekezo ya katiba na kuondoa mafanikio yoyote ambayo yamo ndani ya katiba hiyo. Ni muhimu pia kwamba kumbukumbu ya majadiliano haya zitolewe kwa vile yanaashiria ukosefu wa nia njema ya kisiasa sio tu kwa usawa wa kijinsia bali pia imani kwamba kwa utaratibu wa kisiasa unaotambua usawa wa kibinadamu, kwa hivyo la Profesa Ghai sio kwamba Kamati ya Wataalamu “haikujua ilichukuwa ikikifanya, tulikabiliwa na hali ngumu mno ya kisiasa kwa vile kulitolewa vitisho kwamba wakati Wabunge watakaposoma mapendekezo hayo manufaa ambayo wanawake walikuwa wameyapata yangefutiliwa mbali. Kwa vile katiba katika hali yake ya sasa haitoi utaratibu mwafaka kwa Bunge, kama kuna marekebisho ambayo yanafanywa kwa nia njema itakuwa rahisi kurekebisha kifungu kilichopo sasa nambari 97(1)(c) kurejea katika kifungu cha asili nambari

121 kuliko kuondoa vipengee vinavyolinda kanuni ya thuluthi moja. Swala kuu ni iwapo kuna dhamiri ya kisiasa juu ya kanuni za usawa na kama kwa mara nyingine tena tunataka kuanzisha majadiliano kuhusu katiba kwa malengo mengine. La kushangaza ni kwamba swala la kutotekelezeka kwa kanuni hiyo huzuka tu kuhusiana na usawa wa kijinsia linapowasilishwa bungeni. Swala hili liliwasilishwa mwaka 1997 wakati huo tuliambiwa tulishughulikie swala hilo kwa kushirikisha vipengee vyote kwa pamoja, kisha kwenye kongamano la kitaifa swala hilo likatupiliwa mbali. Ni muhimu kwamba tulitafakari swala hili katika mtazamo wa hali yake ya kihistoria. Inashangaza kwamba hiyo ndiyo sababu inayotumika hasa inapokuwa ni katika shughuli za kiuteuzi.

Mwandishi huyu, Astango Chesoni alikuwa Naibu Mwenyekiti wa Tume ya Wataalamu wa Utayarishaji Katiba. Yeye pia ni wakili wa Mahakama Kuu ya Kenya


4

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Kucheleweshwa utekelezaji kungezusha sheria gushi Wanasema kwamba katiba inaeleza wazi wazi kazi za ngazi mbali mbali za kiserikali. “Hata hivyo, ubidhi wa baadhi ya watu kwamba idara ya utawala wa mikoa inapaswa kudumishwa ni tukio la kusikitisha la kukataa mabadiliko kwa wale wanaodhamiria kudumisha ofisi hiyo na katika hali hiyo kutaka kuvuruga utaratibu wa mabadiliko. Mwito wa aina hiyo hauambatani na matakwa ya mabadiliko na unapaswa kupuuzilowa mbali,” ikaongeza taarifa hiyo.

…Na Faith Muiruri

M

uda wa mwisho wa utekelezaji katiba mpya unafikia kikomo kwa kasi sana. Ni sheria tano pekee ambazo zimepitishwa hadi kufikia sasa kati ya sheria 26 zinazohitajika kufikia wakati uliokubaliwa kwa utengenezaji wa miswada yenye umuhimu wa kwanza kwa kipindi kinachomalizikia tarehe 30 Agosti, mwaka 2011. Habari zilizopokelewa kutoka mtandao wa Tume ya Utekelezaji wa Katiba (CIC) zinaonyesha kwamba ni sheria ya kuunda Tume ya Mipaka na Uchaguzi ya mwaka 2011, Sheria ya Tume Huru ya Uteuzi wa Maafisa ya mwaka 2011, Sheria ya Mahakama Kuu ya mwaka 2011, Sheria ya Tume ya Huduma Huduma za Mahakama ya mwaka 2011 na Sheria ya Tume ya Ukaguzi wa Majaji na Mahakimu ya mwaka 2011. Sheria ambazo utekelezaji wake umechelewa ni pamoja na Mswada wa Uchaguzi, Mswada wa Vyama vya Kisiasa na mswada wa kupambana na ufisadi. Mswada wa Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu, na uraia, sheria kuhusu Tume ya Kanuni na Kupambana na Ufisadi, kuondoka ofisini kwa Wabunge, sheria zote kuhusu ugavi wa mamlaka, na sheria kuhusu hazina maalum ya kukabiliana na mambo yasiyotarajiwa, na udhamini wa mikopo wa serikali kuu.

Ubora Mambo yanazidi kufanywa magumu kutokana na kushindwa kwa watayarishaji wa sheria kuharakisha utaratibu huo. Kukawia huko zaidi sana kunatokana na ulimativu wa maofisa wahusika katiuka utayarishaji wa sheria hizo ambao unatishia kudhgoofisha ubora wa majadiliano kuhusu miswada hiyo, na uwezo wa kamati za Bunge kuichunguza kwa makini miswada hiyo. Jambo hilo matokeo yake ni kupitisha kwa haraka sheria hizo ambapo zinaweza kupitishwa zikiwa na udhaifu mkubwa wa kisheria.

Kuanzishwa

Mwenyekiti wa Tume ya Utekelezaji wa Katiba, Bw Charles Nyachae (kushoto) akiwa pamoja na naibu wake Bi Elizabeth Muli akihutubia mkutano wa waandishi wa habari kuhusu utaratibu ulioko. “Huenda tukaishia na sheria zilizo dhaifu ambazo haziambatani na katiba,”akasema Hassan Omar ambaye ni Kamishna wa Tume ya Kenya ya Haki za Binadamu (KNCHR). Hassan anasema kucheleweshwa huko kwa sheria huenda kukasababisha kuundwa kwa taasisi dhaifu kutokana na kutoeleweka vizuri kwa maswala muhimu, na kadhalika mashindano ya kisiasa kati ya vyama vya ODM na PNU na jitihada za wapinga mabadiliko katika Bunge. “Wapinzani wa mabadiliko wamo katika harakati za kuwaelimiswha habari za upotofu Wakenya kuhusu kile ambacho katiba inazungumzia, Dhana ya ugavi wa mamlaka kwamba ni majimbo huenda ikawafanya wananchi kutumiwa viubaya na viongozi wa kisiasa na kuzua ghasia za kikabila,” aeleza Omar. Anasema kwamba nyingi ya wizara sasa zinajigeuza kuwa tume za kukabiliana na vipengee vya katiba vya kutokuwepo na zaidi ya wizara ishirini na mbili. “Mfano ni kugawanywa katika

sehemu tatu kwa tume ambazo ziko chini ya Tume ya Kenya ya Haki za Binadamu na Tume ya Usawa, (KNHEREC) kuanzisha ofisi ya mpokezi malalamiko ya wananchi kuhusu Serikali mswada wa mwaka 2011, mswada wa tume ya haki za binadamu ya mwaka 2011 na mswada wa tume ya kitaifa kuhusu jinsia,” akaeleza Omar. Omar anadai kwamba kazi ya Tume ya Haki za Binadamu (KNHCR) na tume zilizoundwa hivi majuzi chini ya kifungu cha sheria nambari 59, huenda ikasababisha vurugu miongoni mwa tume hizo. Zaidi ya hayo, mswada wa mahakama ya kazi aya mwaka 2011 kadhalika unajaribu kuwasukuma majaji wa sasa kwenye nyadhifa mpya bila ya hata kuchunguzwa na vyombo vya umma na kuhakikisha kwamba wanatimiza kanuni zinazohitajika kama ilivyoratibiwa kwenye katiba mpya. Omar anawatahadharisha Wakenya wawe macho kuhakikisha kwamba wapiinzani wa mabadiliko hawafanikiwi kuvuruga utekelezaji wa katiba.

Wahusika wengine wasio wa kiserikali kwa upande wao wanaonelea kwamba jitihada zinazoendelea zisizokuwa na mshikamano wa moja kwa moja huenda zikazalisha sheria ambazo hazina uwiano. Wanawataka Wakenya wasimame imara na kupinga majaribio yoyote ya kudhoofisha utekelezaji thabiti wa katiba. “Wakenya wote wana jukumu la kuhakikisha kwamba katiba inatekelezwa kuambatana na vifungu vya sheria vilivyomo ndani ya katiba hiyo,” wakaongeza wahusika hao kwenye taarifa kwa waandishi habari. Wahusika hao ni pamoja na Taasisi ya Uwajibikaji wa Umma (Tisa), Kituo cha Kuimarisha Demokrasia na Utawala Bora (CEDGG), Kituo cha Haki za Binadamu na Elimu kwa Umma (CHRCE),Tume ya Kimataifa ya Waamuzi (ICJ-Kenya) na shirika la kimataifa la uwajibikaji, ambayo yanasema watu wasiotaka mabadiliko wana dhamira kubwa ya kuhakikisha kwamba wanajihami dhidi ya mabadiliko hayo.

“Wakenya wote wana wajibu wa kuhakikisha kwamba Katiba imetekelwzwa kulingana na vifungu vilivyoidhinishwa ndani yake .”

Huku uchaguzi mkuu wa mwaka 2012 ukiwadia, sheria tatu muhimu ni lazima zipitishwe. Sheria hizo ni mswada wa Uchaguzi, mswada wa Vyama vya Kisiasa, na mswada wa Kanuni na Harakati za Kupambana na Ufisadi. Bila ya miswada hiyo kujadiliwa na kuidhinishwa Tume ya Uchaguzi itakuwa haina uwezo wa kuchukua hatua zozote na itakuwa tepetevu. Masuala mengine muhimu ni pamoja na mapendekezo ambayo huenda yakashuhudia kuanzishwa kwa taasisi nyingi ambazo huenda zikahitaji vigezo vingine vya kuhakikisha uwajibikaji na kutoa msingi wa uendelezaji wa uchumi thabiti. Huku harakati za utekelezaji wa katiba zikiendelea, swala jengine muhimu ambalo linaendelea kutatiza ni ugavi wa mamlaka licha ya muda wa mwisho wa Agosti kuwadia. Jambo lingine ambalo limejitokeza lenye kuleta wasiwasi ni mashindano yasiyofaa kati ya taasisi za Serikali hatua ambayo huenda ikaleta sheria zisizoambatana zenye kuenda kinyume na makusudio. Pia kuna swala la kuzuka mgogoro katika sekta ya umma wakati huu ambapo watumishi wa Serikali wanahama kutoka kwenye taasisi zao za awali hadi kwenye taasisi mpya chini ya katiba mpya. Utaratibu huu unapasa kuendeshwa kwa uwazi kwa njia ya haki na kwa ustadi kuhakikisha kwamba serikali za kaunti hazirithi wafanyi kazi wazembe wasioweza kufanya kazi vyema.

Tume yajiandaa kwa uchaguzi wa majaribio

…Na Florence Sipalla

H

uku Kenya ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2012, Tume huru ya muda ya uchaguzi (IIEC) inatayarisha mipango ya kufanya uchaguzi wa majaribio katika maeneo mawili ya Bunge kama njia ya kukadiria jinsi uchaguzi utakavyokuwa chini ya katiba mpya iliyozinduliwa rasmi mwaka 2010. Ni tendo bora linalokubalika kimataifa kwa mashirika ya usimamizi wa uchaguzi kufanya uchaguzi wa majaribio kabla ya uchaguzi mkuu . Kabla ya kura ya hivi majuzi ya maoni nchini Sudan ambayo ilishuhudiwa kuundwa kwa taifa jipya la hamsini na nne, kuliandaliwa uchaguzi wa majaribio kukadiria jinsi upigaji kura utakavyokuwa. Uchaguzi huo wa majaribio utagharibu shilingi milioni sitini. Kwa ajili ya shughuli hiyomuhimu tume ya uchaguzi imechagua maeneo bunge ya Kajiado na Malindi Kaskazini kama vituo vya kupigia kura. “Hii ni kwa sababu maeneo mawili hayo ya Bunge yanawakilisha hali halisi ya kijamii ya nchi nzima kwa jumla. Ni maeneo ambayo yana watu wenye mapato ya juu na ya chini zaidi, kuwa na miji na sehemu zenye watu wengi pamoja na maeneo yenye watu wachache,” alisema Gladys Shollei afisa mkuu wa tume hiyo ya uchaguzi anayeondoka. Uchaguzi huo wa majaribio utaipa nafasi tume ya uchaguzi kukadiria muda utakaochukuliwa kupiga kura kwa kutumia makaratasi

sita ya kupigia kura kwa uchaguzi wa Rais na Maseneta, uchaguzi wa Wabunge, Magavana wawakilishi wa kaunti na wa wanawake, kinyume cha makaratasi matatu ambayo yamekuwa yakitumiwa kupigia kura kwa uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani. “Ni kama mtihani wa majaribio ambao unakupa zoezi na hali ambayo mtihani wenyewe utakavyokuwa,” alieleza Shollei. Uchaguzi huo utaipa tume ya uchaguzi nafasi ya kuwaelimisha wapiga kura na wakati huo kufahamu changamoto ambazo itakabiliana navyo na kujiandaa kukabiliana nazo kwa wepesi.

Majadiliano Tume hiyo itawatumia wapiga kura ambao wamesajiliwa katika maeneo Bunge hayo mawili kama wapiga kura kwenye uchaguzi huo wa majaribio. Hakutasajiliwa wapiga kura wapya kwa ajili ya uchaguzi huo. Tume hiyo huru ya muda ya uchaguzi, inafanya majadiliano ya ni akina nani watakaowatumia kama wagombea uchaguzi. Katika jitihada za kuepuka kuwatumia wanasiasa, tume hiyo inatafakari mipango ya kuwatumia watu wasiounga mkono upande wowote . “Hawa ni Wakenya ambao hawatagombea uchaguzi katika viti hivyo viwili,”aliongeza kusema Shollei. Tume hiyo itaendesha uchaguzi huo kama uchaguzi halisi na itawapa wagombezi vifaa vya kufanyia kampeini. Hiyo itakuwa sehemu ya elimu kwa wapiga kura. Kama ambavyo watafanya kwenye uchaguzi halisi, tume ya uchaguzi itawaajiri wafanyikazi kusaidia kwenye uch-

aguzi huo wa majaribio. Wafanyikazi hao watahudumu chini ya maafisa wa usimamizi wa uchaguzi wa maeneo Bunge . Tume hii ya uchaguzi ina hakika kwamba iko tayari kwa uchaguzi wa mwaka 2012. Uchaguzi mkuu uliopita ulikumbwa na visa vya usajili mara mbili wa wapiga kura. Ili kuondoa tatizo hilo kwenye orodha ya sajili ya wapiga kura tume hiyo ilitoa msamaha kwa wale waliokuwa wamesajiliwa mara mbili na kurejesha kadi zao. “Tume hiyo ya uchaguzi kadhalika inafanya kazi pamoja na machifu na wasajili wa vizazi na vifo kuhakikisha kwamba wapiga kura waliokufa wanaondolewa kwenye orodha ya wapiga kura,” akasema Shollei. “Katika muda wa chini ya sekunde, unaweza kuthibitisha iwapo mtu amesajiliwa hapo awali,” akizungumzia ustadi wa utendakazi wa sajili ya wapiga kura inayotumia vifaa vya kisasa. “Tunatarajia kusambaza sajili hiyo katika kila eneo la Bunge, lakini hilo litategemea udhamini wa pesa,” akaeleza Shollei huku akiongeza kwamba hili ni jambo ambalo linaweza kufanikishwa pole pole. Ingawa wanawake ndio wengi wanaopiga kura, hawawakilishwi ipasavyo kwenye nyadhifa za uongozi. Utekelezaji wa katiba mpya unadhamiriwa kubadilisha hali hiyo kwa vile hakutakuwa na zaidi ya thuluthi mbili ya jinsia moja itakayoruhusiwa kuongoza katika taasisi yoyote. Ili kuhakikisha kwamba kanuni hiyo inafanikishwa, Shollei alivihimiza vyama vya siasa kuwasimamisha wanawake zaidi wa kugombea viti. Katiba kadhalika inahakikisha haki za watu

“Hii ni kama mtihani wa majaribio, inakupatia zoezi na wazo kuhusu jinsi mtihani utakavyokuwa.” — Gladys Shollei, Naibu Kinara wa IIEC aliyeondoka wenye ulemavu. Hayo ni kuhusiana na haki zao za kupiga kura. Katika kuhakikisha kwamba kundi hilo la watu wachache halifungiwi mlango kwenye utaratibu wa kuwaelimisha wapiga kura, tume ya uchaguzi inashirikiana na chama cha walemavu wa akili cha Kenya, (KSMC,) kuhakikisha kwamba vifaa vyote vya upigaji kura vinaweza kutumiwa na watu wwenye ulemavu ikiwa ni pamoja na walemavu wasioweza kufikiria mambo na waliolemaa kiakili.


5

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Sheria yawapa wanawake nafasi ya usimamizi wa vyama

…Na Duncan Mboyah na Jane Godia

W

abunge wamejadili na kupitisha sheria ya vyama vya siasa na kuidhinisha uwekaji wa vyama hivyo katika mfumo wa kitaasisi na kitaalamu katika usimamizi wa vyama hivyo vya siasa. Sheria ya usimamizi wa vyama vya siasa ya mwaka 2011 ilitungwa kuambatana na kanuni za kikatiba kwa mujibu wa vifungu nambari 91 na 92. Sheria hiyo itakomesha mtindo wa wanasiasa kuhama kutoka chama kimoja hadi chama kingine . Kulingana na sheria hiyo, mtu hawezi kuwa mgombeaji wa chama chochote cha siasa kama hajakuwa mwanachama kwa muda wa miezi mitatu. Hata hivyo, kulikuwa na pendekezo la hapo awali kwamba muda wa uanachama uwe miezi sita lakini wanasiasa wakapendekeza miezi mitatu ya uanachama. Inatarajiwa kwamba sheria hiyo italeta heshima katika usimamizi wa vyama hivyo hapa nchini. Kwa miongo mingi vyama vya siasa vimesimamiwa kama kampuni za kibinafsi na wanasiasa huku baadhi yao wakivitumia kama vyombo vya kupigania mamlaka ya uongozi.

Kudumisha Ili chama kiendelee kuwapo ni lazima kisimamishe wagombeaji wa nyadhifa za kitaifa na za kaunti. Chama ni lazima kiwe na wanachama kutoka sehemu zote za nchi. Katika kifungu nambari 91 (1) katiba inasema: “Kila chama cha siasa kitaimarisha na kudumisha umoja wa kitaifa.” Sheria hiyo inapendekeza kufutiliwa mbali kwa chama ambacho hakitafanya uchaguzi wake kwa njia ya haki na hiari na inahimiza hatua kali kuchukuliwa dhidi ya watu wanaohama na kaujiunga na vyama vingine. Sheria itahakikisha kwamba vyama vya siasa vina mtazamo wa ki-kanda na mseto wa kikabila usawa wa kijinsia na uwakilishi wa makundi madogo ya watu na wanaogandamizwa. Kwa mara ya kwanza wanawake watashirikishwa kwenye ngazi za juu za uongozi wa vyama baada ya kutojishirikisha kwa sababu ya kiburi cha wanaume na utumiwaji wa mbinu za kutisha na wanaume hao wakati wa kampeini za uchaguzi. Katika kifungu cha 91 (1) (f), katiba inasema “Kila chama cha siasa kitaheshimu na kuthibiti haki za binadamu na uhuru muhimu na usawa wa kijinsia kutendewa sawa”. Kulingana Joy Othieno, wakili mwenye makao yake mjini Nairobi, alisema;“Wanawake wamejiepusha na kugombea mamlaka makuu ya vyama kwa sababu ya kuhangaishwa na wagombeaji wanaume, lakini hali hiyo sasa itabadilika wakati mswada huo utakapoanza kutumika.” Othieno hata hivyo anafahamisha kwamba ukosefu wa pesa ndicho kikwazo kikubwa kinachowazuia wanawake kushiriki kikamilifu kwenye siasa za vyama. “Imani za kitamaduni za jamii mbali mbali zinapasa kulaumiwa kwa vile jamii nyingi haziamini katika uongozi wa wanawake,” akaeleza. Kulingana na Waziri wa Mambo ya Katiba na Fungamano la Kitaifa, Bw Mutula Kilonzo, sheria ya vyama vya siasa imeshirikisha takwa la kijinsia na ushirikishi wa kanda ambayo

yanapaswa kutimizwa kabla ya usajili wa chama chochote ili kutekeleza matakwa ya katiba mpya. Sheria hiyo inataka muundo wa maafisa wa kitaifa wa chama uwe na mtazamo wa kitaifa, hatua ambayo inataka kupiga marufuku mtazamo wa kikabila na kuleta mtazamo wa kitaifa kwa vyama.. “Sheria hiyo kadhalika inaruhusu miungano ya vyama na makubaliano ya miungano hiyo kuwasilishwa kwa msajili wa vyama katika muda wa siku ishirini na moja za muungano,” alieleza Kilonzo. Alisema kwamba; “Sheria hiyo inawazuia watu binafsi ambao ni wanachama wa vyama vya siasa kutangaza mitazamo, maslahi na maongozi ya chama kingine au kukifanyia kampeini chama kingine au mgombeaji uchaguzi wa chama kingine.” Sheria hiyo inataka kuundwe hazina ambayo itagawanyiwa vyama kuambatana na jumla ya idadi ya kura vilivyopata kwenye uchaguzi mkuu. Ili chama kifuzu kupata pesa hizo, kiasi cha asilimia 15 kwa kutumia kanuni sahihi, asilimia tano kwa usimamizi, asilimia themanini kwa uwakilishi wa usawa, na asilimia arobaini kuwa chini ya misingi ya idadi ya wanawake na vijana wanaojiunga na chama husika. Sheria hiyo hata hivyo, inazuia vyama kupokea pesa kutoka kwa watu wasiokuwa raia na inavihitaji vyama kuchapisha orodha ya wadhamini wa kifedha wa chama. Waziri Msaidizi wa Elimu, Dkt Kilemi Mwiria anasema kuwa miungano ya vyama humu nchini inaundwa kwa sababu ya uzandiki kujitafutia mamlaka na utovu wa uaminifu. Dkt Mwiria analaani mipangilio

Wanawake wakiimba wakiunga mkono chama cha PNU wakati wa uchaguzi mkuu wa 2007. Akina mama wanakosekana kwenye nyadhifa za juu katika vyama vikuu vya kisiasa nchini. ya kikabila katika uundaji wa miungano kama sumu kwa fungamano la kitaifa kwa sababu ni dhihirisho la ukabila. “Vikwazo vinapasa kuwekewa vyama ambavyo vinasisitiza kwamba jamii zao zinapaswa kuelekea njia moja au nyingine au kuwekewa vyama vinavyounda miungano ya kikabila,” akashauri.

James Orengo “Twapaswa kujifunza kutokubaliana ndani ya vyama v ya siasa na kusuluhisha matatizo ndani ya vyama hivyo,” alisema waziri mwingine msaidizi, Mwangi Kiunjuri ambaye ni Mbunge wa Laikipia Mashariki. Alitoa mwito kwa vyama kuunda kamati za kusaidia kusuluhisha mizozo ya ndani badala ya wanaozozana kutoa tofauti zao hadharani, mwenendo ambao husaidia kuleta chuki miongoni mwa jamii tofauti. Waziri wa Ardhi, James Orengo ambaye aliunga mkono mswada huo, aliilaumu Serikali kwa kuchochea kuanguka kwa vyama vya siasa tangu nchi hii ijinyakulie uhuru. Orengo anasema pia kwamba

mtindo wa vyombo vya habari wa kuwashutumu wanasiasa umesaidia kusambaza ghasia ambapo makundi ya watu wa chama kingine hufanyia kampeini wazi wazi chama kingine pinzani. “Hizi ni imani potofu zsa kusadiki kwamba hakuna chochote chenye thamani au dhana mbovu ya kuwa na shaka kwa kila jambo katika siasa. Hali ambayo haina mashiko katika jamii ya kidemokrasia,” akasema. Mwenyekiti wa kituo cha vyama cingi vya kisiasa nchini, (CMD), Justin Muturi anasema kwamba nchi hii inahitaji vyama vyenye nguvu kama taasisi za usimamizi wa umma. Vyama vinastahili kuwa na mtazamo wa kitaifa na kusimamiwa kitaalamu. Hatutaki vyama kuundwa bila misimamo ambavyo shabaha yao ni kushinda nyadhifa za mamlaka, akaeleza Muturi. “Sheria hiyo ina adhabu kali dhidi ya wale wanaoruka kutoka chama kimoja hadi kingine kama panzi,” akakariri. Ingawa kamati ya Bunge ya uangalizi wa mambo ya katiba, (CIOC), iliamini kwamba marekebisho

yatakubaliwa na Bunge, kundi la Wabunge chini ya muungano wa G7 ulishinda mapendekezo ya kamati hiyo hasa kifungu nambari 10. Walipendekeza kwamba vyama viwili au zaidi vinaweza kuunda muungano kabla au baada ya uchaguzi na kuwasilisha makubaliano ya muungano kwa msajili wa vyama vya siasa miezi mitatu kabla ya uchaguzi mkuu kufanywa. Kadhalika walikubalina kwamba miungano hiyo ifanywe baada ya uchaguzi mkuu kinyume na hitaji lililowekwa na katiba. Usimamizi wa vyama vya siasa utafanywa na ofisi ya msajili wa vyama, ambayo itakuwa ofisi ya Serikali. Ofisi hiyo haitakuwa chini ya usimamizi wa Tume Huru ya Mipaka na Uchaguzi (IEBC) iliyoundwa chini ya kifungu 8 nambari 250 ya Katiba. Kila chama ni lazima kiwe na jina tofauti na alama yake. Haitakuwa kama mwaka 2007 wakati chama cha Orange Democratic Party (ODM) na chama cha Orange Democratic Party of Kenya (ODM-K)vilipongángánia alama moja ya chungwa.

Je, vyama vya siasa vitaweza kuwaweka wanawake katika nyadhifa za kutoa maamuzi?

…Na Rosemary Okello

K

ama kuna wakati katika historia ya Kenya ambapo vyama vya siasa vitakabiliwa na uchunguzi mkali hasa kuhusiana na swala la uwakilishi wa wanawake katika ngazi za kitaifa na za serikali za kanda basi ni katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2012. Kinyume na ilivyokuwa hapo awali, vyama vya siasa vilikuwa havichukuliwi hatua zozote kuhusiana na uwakilishaji wa wanawake chini ya sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 2007. Kulingana na Dinah Liech, wa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, sheria mpya ya usimamizi wa vyama vya siasa imeleta mapinduzi makubwa kwenye sheria za vyama vya kisiasa. Anaeleza kwamba sheria ya awali ya vyama vya kisiasa (sehemu ya 108), ilihusu usajili wa kila aina ya vyama. Vyama vya siasa vilisajiliwa kama vyama vingine vyovyote vya kawaida vikiwa na wa kisheria kama vyama vingine kama vile vilabu, vyama vya kitaalamu, vyama vya kijamii, na makundi ya akina mama, miongoni mwa vyama vinginevyo. Hata ingawa sheria hiyo ya vyama sehemu ya 30 (4) inasema kwamba “Hakuna chama chochote cha siasa ambacho kitanufaika na hazina kama maafisa wake waliosajiliwa hawana mtazamo wa thuluthi moja ya kanuni ya kijinsia.” Kulinganana Liech, “Hilo halijakuwa na athari yoyote kwa ngazi ya utoaji maamuzi ya vyama. Uwakilishi wa wanawake katika ngazi za kitaifa,kanda na

“Wanawake huja kama wamechelewa kwenye utaratibu wa kisiasa hivi basi huachwa nyuma maamuzi muhimu yanapotolewa.” — Winnie Guchu maeneo ya ubunge haupo. Kwa sasa idadi rasmi ya uanachama katika vyama vya siasa ni wanaume 82,237 ambayo inawakilisha asilimia 63 na wanawake 48,353 ambao wanawakilisha asilimia 37. Idadi kamili ya wanaume na wanawake katika baraza kuu la vyama ni wanaume 673 wanaowakilisha asilimia 63 na wanawake 402 wanaowakilisha asilimia 37. Idadi kamili ya wanachama wa kamati ya ushirikishi wa kitaifa wa vyama vya siasa ni kama ifuatavyo: Wanaume 35 wanaowakilisha asilimiua 75 na wanawake kumi na wawili wanaowakilisha

asilimia 25. Kamati ya kanda ya ushirikishi wa vyama vya siasa kwa sasa ni kama ifuatavyo wanaume 491 wanaowakiliswha asilimia 82, na wanawake 108 ambao inawakilisha asilimia 18. Kamati ya usimamizi wa ushirikishaji wa vyama ina jumla ya wanachama 166 ambapo 142 ni wanaume wanaowakilisha asilimia 75, ilhali wanawake ni ni arobaini na wawili wanaowakilisha asilimia ishirini na tano. Alisisitiza kwamba chini ya haki za kisiasa na za kiuchaguzi za wanawake katika sura ya pili ya katiba sehemu ya 4 (2), miongoni ma mambo mengine inatilia nguvu hakika kwamba vyama vya siasa vinapasa kuongozwa na kanuni kama vile umoja wa kitaifa, usimamizi wa kisheria, demokrasia, kushiriki kwa raia, usawa, kutobaguana, utawala mwema na uwajibikaji. Hata ingawa wanawake wako huru sawa na wanaume wa kujiamulia katika masuala ya kisiasa ikiwa ni pamoja na haki ya kuunda au kushiriki katika uundaji wa vyama vya kisiasa, Liech anasikitika kwamba kushiriki kwao kwenye masuala ya vyama vya siasa ni dhaifu sana. Kwa mfano wanawake hawashiriki kwenye shughuli za vyama na wamewaachia wanaume kupanga mikakati katika usajili wa wanachama au katika kampeini za vyama vya kisiasa. Hata hivyo, sehemu ya 91(1) iko wazi kuhusu jinsi vyama vya siasa vinavyopaswa kuendesha shughuli zao. Kinavitaka vyama hivyo kuzingatia kanuni za kidemokrasia na utawala bora, kuimarisha na kutekeleza demokrasia kwa vi-

tendo kwa kufanya uchaguzi za mara kwa mara za haki na uwazi, kuheshimu haki za watu wote za kushiriki katika harakati zote za kisiasa, ikiwa ni pamoja na wanawake, makundi ya walio wachache na wanaogandamizwa. Kwa hivyo, huku wanawake wakitafuta mbinu za kuhakikisha kwamba kipengee cha uwakilishi wa kutozidi thuluthi mbili kwa jinsia moja inafanikishwa, katiba chini ya sehemu ya 81, inatambua harakati za kupigania haki za wanawake kama kanuni ya utaratibu wa uchaguzi na kanuni hiyo ni ya kurekebisha upungufu wa uwakilishi wa makundi maalum kama vile wanawake, vijana makundi ya walio wachache na wanaogandamizwa.

Nyadhifa Kama ilivyo kwa sasa, katiba inawataka wanawake na wanaume kuchaguliwa kwenye nyadhifa zifuatazo, urais, wabunge, maseneta, waakilishi wanawake katika kaunti na madiwani. Vyama vya siasa kwa hivyo vitahitajika kutayarisha orodha ya wagombezi yenye mseto wa kijinsia kwenye ugombezi wa viti vya kiuchaguzi na vya uteuzi kabla ya uchaguzi mkuu. Kulingana na Kamishna Winnie Guchu kuna haja ya kutayarisha uchambuzi hakika kuonyesha jinsi wanawake watakavyoshiriki kupitia vyama hivyo vya siasa. “Hii ni kwa sababu wanawake hujitokeza wakiwa wamechelewa hasa kwenye harakati za kisasa na siku zote huachwa nyuma wakati maamuzi makuu yanapofikiwa kwenye vyama,” akaeleza.


6

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Wanawake watwaa viti vya manufaa vya mabaraza

…Na Adow Ina Kalil

U

chaguzi wa mwanamke kwenye mamlaka dhaifu ya mwenyekiti wa kamati katika Baraza la Wilaya lisilofanya vyema huenda lisiwe jambo la kusherehekea. Hata hivyo, likitendeka katika eneo ambalo kidesturi wanawake huzuiwa kupanda ngazi za uongozi tukio hilo linaonekana kama hatua kubwa ya kubadilisha hali kwa wanawake kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2012. Historia ilitendeka katika kanda ya Kaskazini Mashariki wakati wa uchaguzi unaoendelea wa udiwani baada ya wanawake watatu madiwani kuchaguliwa kuwa wenyekiti wa kamati za mabaraza kwenye mabaraza yanayomilikiwa na wanaume ya Wajir na Mandera. Mwanamke wa kwanza kabisa kuchaguliwa diwani wa Baraza la Wilaya ya Wajir, Rukia Abdille Abdullah wa wadi ya Laghbokol Kaskazini, alichaguliwa mwenyekiti wa kamati ya uhasibu naye mwenzake, Fatuma Sheikh akachaguliwa kwa urahisi kuwa mwenyekiti wa kamati ya mazingira, usafi na afya ya jamii.

Mbunge wa Gichugu, Bi Martha Karua (wa pili kushoto) akiwa na akina mama wa mkoa wa Kaskazini Mashariki alipopeleka kampeni yake ya kujipigia debe ya uraisi katika sehemu hiyo. Kwa mara ya kwanza Katiba mpya imewawezesha akina mama katika eneo hilo kupata nyadhifa kwenye mabaraza ya kounti. Picha na: Adow Ina Kalil.

Uteuzi Katika mpaka wa kaunti ya Mandera, diwani maalumu wa chama cha Safina, Maryam Dahir Hussein mwenye umri wa miaka 44, alikuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuongoza kamati ya mazingira na afya ya jamii, baada ya kuchaguliwa bila kupingwa kwenye uchaguzi huo unaoamuliwa katika misingi ya mbari. Hata hivyo, kuchaguliwa kwake kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ya baraza lenye ukubwa wa kilomita 25,920 mraba hakukuwa rahisi. Ilihitaji jitihada za madiwani wanne wanawake kupambana kufa na kupona kupata haki yao kwenye baraza hilo lenye kamati tisa zilizokuwa zikigombaniwa, wakingángána kupata sehemu yao kwenye utekelezaji wa kanuni ya thuluthi mbili za kijinsia kama inavyokokotezwa na katiba. Uchaguzi huo wa kihistoria ulitoa matumaini makubwa kwa wanawake na wapiganiaji usawa wa kijinsia, katika eneo lililofahamika hapo awali kuwa lisilowaruhusu wanawake kumiliki nyadhifa za uongozi. Kinyume na sehemu nyingine za nchi ambako uchaguzi wa mabaraza hushindaniwa vikali huku madiwani wakipelekwa safari na madiwani wanaopinzana kwenye ungángánizi wa viti vya uenyekiti wa kamati tofauti. Katika kanda ya kaskazini wagombeaji hutafuta ridhaa ya wazee wa kijamii kufanya hesabu za kimbari ili kugawana nyadhifa zinazogombaniwa. Kwa mfano katika kaunti ya Mandera, ilimlazimu kijana mmoja kujiondoa ili kumpisha aliyekuwa mwenyekiti hapo awali kinyume cha matakwa ya wengi wa madiwani wa mbari hiyo. Wakati walipoachwa kungángánia nyadhifa za wenyeviti wa kamati, kwenye mkutano uliofanywa usiku uliofuatia, wazee hao wa mbari waliwalazimisha madiwani kumchagua aliyekuwa mwenyekiti hapo awali wa wadi ya Kutulo Kaskazini kuliongoza baraza hilo kama mwenyekiti wa kipindi cha pili. Madiwani hao wanawake wakati wa asubuhi walifanya mapinduzi baridi na kususia uchaguzi huo kwa muda mnamo siku ya uchaguzi hadi wasiwasi wao wa uwakilishi wao wa kijinsia ulipotiliwa maanani. Baada ya zaidi ya saa moja ya mashauriano, madiwani hao wanawake walifanikiwa kupata viti katika kamati muhimu ya mazingira na afya ya umma, baada ya diwani mwa-

“Mara nyingi imekuwa vigumu kwa mwanamke kutegewa sikio kwenye baraza la wazee kumwezesha kuuza ajenda yake kwa wanaanchi.” — Rukia Abdile Abdullahi

naume kujiondoa kwa manufaa ya wanawake hao. “Changamoto zinazowakabili wanawake kwenye nyadhifa za chini zaidi za kiuchaguzi kwenye mabaraza ya kaunti zilionekana kama kifungua macho kwa matatizo yanayowakabili katika kufanikisha kile ambacho katiba mpya imewatengea wanawake katika kanda hiyo,” akasema Habiba Issaq ambaye ni mtaalamu wa mambo ya kijinsia. Issak ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habiba International Women and Youth Affairs, shirika lisilo la serikali lenye makao yake mjini Mandera, anasema kukabiliana na sheria za kienyeji ambazo hazijaandikwa, ambazo zinalifanya kuwa hatia kubwa tendo la kuwashirikisha wanawake kwenye mamlaka ndiyo kazi kubwa inayowakodolea macho wale wanaotaka kuona idadi ya wanawake ikiongezeka kwenye nyadhifa za kiuchaguzi. Zainab Ithifle ambaye zamani alikuwa diwani maalumu na ambaye aligombea kiti cha Bunge cha Lagdera, alisema changamoto kubwa zaidi inayowakabili wanawake kwenye harakati za kuongeza idadi yao kwenye nyadhifa za kiuchaguzi iko kwenye vyama vya siasa ambavyo alivilaumu kwa kuwanyima wanawake nafasi ya kuwa wapeperusha bendera wa vyama hivyo katika maeneo hayo ya wafugaji.

Ithifle anaeleza: “Kwa kuimarisha elimu ya umma kuhusu maswala ya kijinsia katika kanda hiyo,mengi yanaweza kufanikishwa katika kuimarisha uwakilishi wa wanawake katika nyadhifa za kiuchaguzi na za kiuteuzi.” “Katiba mpya inatoa kima fulani cha nyadhifa za uteuzi kwenye mamlaka makuu kwa wanawake kwa kutoa thuluthi moja na hilo litawezekana wakati wanaume waliojaa uongozi wa kisiasa watabadilisha nia zao.” Kwenye uchaguzi mkuu wa 2007, kati ya wanawake 300 walioeleza nia ya kugombea viti vya udiwani, ni wawili tu, Rukia Abdille Abdullahi wa wadi ya Laghbokol Kaskazini katika Kaunti ya Wajir na Hani Hassan Hussein wa wadi ya Fino katika Kaunti ya Mandera, ndio waliochaguliwa. Wengi wa wanawake waliondolewa kwenye mchujo wa viongozi wa mbari wakipendelewa wagombezi wanaume licha ya kuwa maarufu miongoni mwa wapiga kura.

Kaunti ya Ijara Huko Wajir kati ya madiwani 64 katika kaunti ya sehemu hiyo, kuna wanawake sita tu madiwani ambapo kati ya hao watano walichaguliwa kupitia vyama vyao. Katika kaunti ya Mandera, kati ya madiwani 54 kuna wanawake wanne pekee, watatu wakiwa ni wateule na mmoja aliyechaguliwa. Mji wa Mandera una diwani mmoja mteule kati ya madiwani kumi. Katika kaunti ya Garissa ambayo ndiyo makao makuu ya kanda ya Kaskazini Mashariki na ambayo inachukuliwa kuwa iliyoendelea zaidi, kati ya madiwani 43 ni diwani mmoja pekee mwanamke, na katika baraza la mji wa Garissa hakuna mwanamke hata mmoja kati ya madiwani wanane wa baraza hilo. Katika kaunti ya Ijara, kuna diwani mmoja mwanamke kati ya madiwani kumi. Abdullahi ambaye hali yake ni ya kipekee alipata kuchaguliwa kupitia kwa mbari yake na kuchaguliwa diwani kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2007. Anasema matumaini ya wanawake katika kanda hiyo ya wafugaji kufurahia mafanikio yanayotokana na katiba mpya ni haba kwa sababu ya uwezo mkubwa wa baraza la wazee ambalo huwaidhinisha wagombea uchaguzi. “Ni vigumu siku zote kwa mwanamke kupata mtu wa kumsikiza kwenye baraza la wazee linalotoa maamuzi kuwashawishi na kuwaelezea ajenda yako na maono ya watu,” akasema Abdullahi. Akaongeza; “Wakati utakapopata mtu wa ku-

kusikiza kwenye baraza la wazee la mbari yako, huwa ni kibarua kigumu kwao kupendekeza jina lako kwa mbari nyingine ili kukuunga mkono, kwa sababu kupendekeza jina la mwanamke ni sawa na kuwa na utovu wa nidhamu. Kwa hivyo, hilo linamfanya mpinzani wako wa kiume kupewa kipaumbele kwenye makabiliano ya kiuchaguzi. Hata hivyo, Abdillahi ana matumaini kwamba dhamira ya mabaraza hayo ya wazee kumpendekeza yeye na na mwenzake kutoka Wajir kwa nyadhifa hizo za wenyekiti wa kamatini dalili ya kuondoka kwenye msimamo mkali wa kuwabagua wanawake. Anasema: Ingawa bado tuko nyuma ya sehemu kama vile Mumias, Muranga na Bomet ambako wanawake waliweka historia katika mabaraza yao, mwanasiasa huyo anaamini kwamba enzi zile ambapo wanawake walikuwa wakichukuliwa kuwa wapiga kura zimekwisha, wao pia sasa wanakuwa wagombea viti. Huko Mumias, Lillian Osundwa wa wadi ya Township, aliwabwaga wagombezi wanaume na kuchaguliwa meya na huko Murangá, Mary Wanjiku Kimwe wa wadi ya Njoguini kadhalika alichaguliwa meya bila kupingwa. Huko Bomet eneo ambo wanaume wametamalaki mambo, diwani wa Songorwet Joyce Korir alishangaza kwa kuchaguliwa meya baada ya kuwabwaga wapinzani wanaume kwenye uchaguzi wa manispaa uliokuwa na ukinzani mkubwa. “Hatua hiyo ni dalili wazi kwamba viongozio hao wa mbari sasa wanaimini kwamba wanawake hufanya vyema katika “mamlaka ya uongozi kuliko wanaume,” akakariri Abdillahi.

Kuhama “Walipata kwamba huku wanasiasa wengi wanaume huhamia mijini na jamaa zao baada ya kuchaguliwa, viongozi wanawake hubaki miongoni mwao katika hali ngumu na hali nzuri,” alisema Korir kwenye mahojiano. Abdullahi Ahmed mwenye umri wa miaka 67 ambaye ni mzee kutoka Wajir ambaye ni miongoni mwa wale waliopigania kuidhinishwa kwa wanawake kupewa nyadhifa kwenye mkutano wa mbari kabla ya uchaguzi wa baraza la Wajir, waliwachagua viongozi wanawake kuongoza kamati za uhasibu wa ndani pamoja na mazingira na afya ya jamii. “Baraza letu (Wajir) lina matatizo ya usimamizi wa pesa. Kumekuwa na malalamiko ya pesa za baraza kutumiwa vibaya na madiwani wanaume

yaelekea hawana ustadi wa kazi au wameshirikiana na maafisa wakuu kupora pesa,” akasema Ahmed. Alieleza kwamba; “Tuliamua kumjaribu mwanamke kulinda mapato ya baraza letu pamoja na mazingira, usafi na afya ya jamii. Tulipata ya kwamba wanaweza kufanya vyema zaidi kuliko madiwani wanaume. Sisi kama wazee sasa tunashauriana kuona iwapo tunaweza kuwapa wanawake wetu nafasi katika nyadhifa za ugavana na ubunge.” Kubadilisha fikra za kitamaduni za wanawake wenyewe, ambao ndio wengi kati ya wapiga kura ndilo tatizo kubwa kwa mtu yeyote anayetaka kugombea viti vya kiuchaguzi. Kulingana na Halima Osman mwenye umri wa miaka 54 wanawake hawapaswi kupigania uongozi isipokuwa awe ni mjane, aliyepewa talaka au ambaye hataki kuwa na familia.

Usawa Uongozi na kiuchunga familia ni kazi zinazohitaji kujitolea kwa dhati na haiwezikani kwa mtu kufanya usawa katika kuhudumu kama kiongozi na wakati huo huo kutunza mume na watoto. Ni lazima ujitolee katika jambo moja na jukumu la kuangalia mume na watoto halipasi kuwekwa kando kwa sababu ya kazi,”asema Osman. Kwa dhana hiyo, wanawake ambao ndio wengi kati ya wapiga kura na wenye kuaminika katika sehemu ambayo viwango vya watu wasiojua kusoma na kuandika ni asilimia 80, hiyo ni changamoto kubwa inayowakabili wanawake wanaodhamiria kugombea nyadhifa za uongozi katika kanda ya Kaskazini. Abdillahi anasema wanawake hasa katika kanda ya Kaskazini Mashariki ni lazima wawe na ujasiri wa kutosha kukabiliana na vizingiti vya kitamaduni ambavyo vinapunguza uwezo wao wa kuchaguliwa kwenye nyadhifa za uongozi kwa kuthibitisha talanta zao za uongozi. Anasema kwamba inawalazimu kuonyesdha umahiri wao wa uongozi kwa vyama vyao kabla ya kutafuta kura kutoka kwa vyama hivyo. Diwani huyo maalum anasema mara nyingi hafahamishwi mazungumzo ya shughuli za baraza na katika jitihada za makusudi za kumfungia nje ya majadiliano hayo, madiwani wanaume huendesha mikutano yao wakati wa usiku na kufikia maamuzi muhimu ya baraza, ambapo yeye kama mwananchi mwingine wa kawaida hupata habari zake wakati watu wanapoyajadili.


7

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Katika Siaya akina mama wabaguliwa kunyakua vyeo

…Na Omwa Ombara

W

akati Diwani Elizabeth Owino mwenye umri wa miaka 50 alipojibwaga katika uwanja wa kisiasa mnamo mwaka wa 2006, alikuwa na ndoto pana kwa niaba ya akina mama wanaoishi kijijini mwake. Kilichokuwa kikimhuzunisha ni kile alichokitaja kama kutojua miongoni mwa akina mama wanaoishi katika kaunti ya Siaya kwa jumla. Alijiahidi na kuapa kwamba pindi tu atakapoingia ulingoni mwa siasa, atabadilisha hali ya maisha yao kutoka kwenye umasikini unaothiri hadi ule wa matumaini katika maisha yao ya baadaye. Jinsi alivyoshuhudia wanawake wakibaguliwa hali kadhalika watoto, hali hiyo ilimpa motisha ya kujibidiisha zaidi kufikia malengo hayo yake. “Niliona kwamba kulikuwa na mengi ambayo akina mama pale kijijini hawakuwa na habari kwa yale yaliyokuwa yakiendelea ama yale ambayo hayakuwa yakiwafikia kwa njia za habari. Nilianza kujiuliza, je, nitawahamasisha kwa njia gani? Hii hasa ni kwa sababu hawakujua haki zao. Si ajabu pale kijijini mwangu wanawake wengi walikuwa wakipigwa na waume wao, kasha asubuhi kulazimishwa kuwatayarishia waume hao hao kifungua kinywa. Yaani ukiukaji wa haki za kibinadamu kwa wanawake miongoni mwa waume katika kaunti ya Siaya, ni kama mtindo unaokubalika,” akalalamika Owino.

Juu: Hapa mmoja wa wagombezi wa kiti cha mwenyekiti wa Kaunti ya Siaya akisindikizwa na wafuasi wake wakati wa kwenda kujiandikisha kwenye uchaguzi wa hivi majuzi katika sehemu hiyo. Chini: Huyu ndiye Diwani Elizabeth Owino wa wadi ya Jera ambaye naye alikuwa akikemezea mate kiti hicho wakati huo.

Kurithiwa mume Elizabeth analalamika kwamba hali huwa ni mbaya zaidi kwa mwanamke ambaye mumewe ameaga dunia, yaani mjane. Ni jambo la kawaida kwamba mama huyo kimila ni sharti kurithiwa . “utamaduni huo kwangu mimi ni kama ulipitwa na wakati kwa sababu wanawake wengi waliofiwa na waume wao, hawapendi kabisa tendo hilo eti kwa vile wao huambiwa kwamba ili wajiepushe na chira waona watoto waoni sharti kurithiwa ama sivyo eti jamaa yao nzima itapata laana. Mimi kamam Elizabeth Owino, siamini hayo,” alisema. Mambo hayo yalimfikia peupe hivi majuzi wakati kundi fulani la vijana walimshambulia ndani ya jumba la kuhesabia kura la Baraza la Wilaya ya Siayawakisema kwamba kwa vile yeye alikataa kurithiwa, ndiyo sababu ya yeye kutoweza kupigania uongozi wa kiti cha juu cha kisiasa. “Jamaa mmoja alinijia na kisu huku akipiga makelele akisema eti kwa vile nilikataa kurithiwa wakati mume wangu alipofariki, basi ningali nimebeba ch hivyo ni sdhati eti nisafishwe kabla sijakuwa kiongozi. Wewe utawezaje kutuongoza na hali bado umebeba chola? Niliweza tu kujinusuru wakati nilipokimbia na kwenda kujifungia ndani ya choo kilichokuwa hapo karibu. Hata hivyo, walinifuata na hata kujaribu kuninyonga. Mwishowe walifanikiwa hata kunipiga.” Huu ndio uhuhuda kamili ya Diwani Elizabeth Owino wa Baraza la Wilaya ya Siaya baada ya uchaguzi wa majuzi wa uaniaji wa kiti cha mwenyekiti wa baraza hilo. Ghasia za uchaguzi ulioshuhudiwa dhidi yake ulidhihirisha wazi kwamba wanaume wengi hawako tayari kuona akina mama nao wakipigania nyadhifa za uongozi kama ilivyoratibiwa katika katiba mpya. Yale ambayo Elizabeth aliyashuhudia kwa kweli yanaenda kinyume cha haki za kisiasa katika Katiba mpya chini ya Kifungu 38 (30 (c) kinachosema na kueleza: “ Kila mwananchi mzima ana haki, na bila kizuizi chochote kile kuzuiwa kuwa mgombezi kupigania afisi ya umma, ama hata afisi katika chama cha kisiasa ambacho mwananchi kama huyo ni mwanachama na angeweza kuchaguliwa.” Katiba hiyo hiyo inaendelea kueleza katika Kifungu 28. “Kila mtu ana haki za kimsingi kuheshimiwa dhidi ya yale anayotaka kufanya bila kuingiliwa kwa njia yoyote ile pasipo na sababu maalumu ya yeye kunyimwa haki hizo zake ambazo pia zinapaswa

Nilipata kura asilimia 90 ambapo wapinzani wangu wanane wanaume wakapata kura asilimia 10 kwa pamoja. Wakati huo hapakuwepo na fujo ambapo wanaume wengi pia waliniunga mkono — Elizabeth Owino, Diwani wa Jera kaunti ya Siaya kulindwa wakati wote.” Na Katiba inakairi nguvu zake zaidi kwa kueleza chini ya Kifungu 2 (4) kwamba: “Sheria yoyote ile ikiwa ni pamoja na za kiutamaduni na ambayo huenda inahitilafiana nah ii katiba, haitatambuliwa kwa hivyo mbele ya sheria iliyopitishwa, ni sharti kuambatana na y ale yaliyopitishwa na wengi kisheria inayopaswa kufuatwa wakati wote.” Ukiukaji ule wa haki za kimsingi ulioshuhudiwa wilayani iaya dhidi ya Diwani Elizabeth Owino ni dhihirisho tosha kwamba akina mama wengi bado hawaheshimiwi kama ipasavyo kwa vile wananyanyaswa ili wasipiganie viti vya kisiasa ambavyo kwa kweli ni haki yao kikatiba na hasa ikitiliwa maanani kile kifungu cha theluthi tatu ya viti vya uongozi kama vile katiba mpya inavyosisitiza. Kisa hicho cha Elizabeth Owino ni mfano mzuri wa kile wajane wengi watakabiliana nao kutoka kwa wapinzani wa kiume na hasa wakati huu tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa 1212 ambapo porojo nyingi pia zitatukuzwa dhidi ya wanawake na hasa wale ambao kwa bahati mbaya aidha ni wajane ama pengine wametalakiwa. Haitakuwa ajabu kupata kwamba wapinzani wao wa kiume watafanya kila wawezalo, juu chini, kuhakikisha kwamba wanawafungia

milangona njia za kuwaelekeza kwenye viti vya uongozi. Akihojiwa na jarida hili, Elizabeth yeye hatababaishwa kamwe wala kudhulumiwa na wapinzani licha ya kwamba alipoteza kesi dhidi ya wapinzani wake baada ya kuwashtaki kwente Mahakama Kuu ya Kisumu mnamo Agosti 9. “Mimi ninaona mwangaza ambao ni wakwa akina mama wa Siaya ambapo nia yangu ni kuwatumuikia wanawake wa Siaya ili kwamba wakati nitakapoondoka, nitakuwa nimewafanyia mengi kuliko nilivyopata awali,” akaahidi Elizabeth. Yeye amekuwa diwani wa wadi ya Jera tangu mwaka 2008 aliposimama kwa kiti hicho dhidi ya waume wanane na hatimaye kuwabwaga wote. “Nilipata kura asilimia 90 ambao waume hao wanane, kura zaom zikiwekwa pamoja, ndiyo hiyio asilimia kumi waliyopata,” akaeleza Elizabeth kwa furaha akisema wakati huo hapakuwepo na ghasia wala fujo kwani nyingi ya kura pia nilizopata zilitoka kwa wanaume ijapokuwa wale wapinzani wangu wa kiume walikuwa wakiniuliza ni dawa gani niliyotymia kuwavutia wapiga kura wengi wa kike.

Zilipounganishwa Ushawashi wa kisiasa ulianza kwa Elizabeth kutoka kwa kanisa moja nyumbani Siaya. Hakutaka kuwa sembuje anayekaa bura asijue la kufanya baada ya mumewe kuaga dunia. Ijapokuwa hali ya umasikini ilikuwa imethiri sana mle kijijini ambapo hata kanisani waumini waliwajibika kuja na stul za kukalia wakati wa ibada, Elizabeth alichukulia jambo hilo kama funzo kwani baadhi ya waumini ambao hawakuweza kuja na stul kanisani aidha walisimama wakati wa kipindi kizima cha ibada ama sivyo kukaa sakafuni ya udongo wakati huo wote. Wakati kaunti zilipounganishwa kutoka tarafa za Gem, Alego na Ugenya kuunda Kaunti ya Siaya, Elizabeth alijipata katika hali ya kaha li ya kuwashawihi madiwani 29 wa mabaraza hayo ya awali wamchague kama mwenyekiti. Baadhi ya mabnadiliko ambayo Elizabeth angependa kuona yakitendeka katika baraza jipya la Kaunti ya Siaya ni utumizi wa uwazi wa pesa zinazotokana na Local Authority Transferr Fund (LATF) akieleza kwamba kaunti hupokea Sh700,000 mara tatu kwa mwaka kuhudumia miradi katika miezi ya Oktoba, Februari na Mei, mbali na kiasi kingine cha Sh2.1 milioni kila mwaka. Anawashukuru akina mama wengi ambao wamempa misaada kadha wa kadha hapo akitaja baadhi yao kama vile Kamishna Rozah Buyu,Prof Jacquiline Oduol, Mheashimiwa Millie Odhiambon na Bi Ruth Odinga.

Wanawake wa kanda ya Kaskazini Mashariki wahimiza mabadiliko ya kifikra …Na Issa Haroun

W

anawake katika kanda ya Kaskazini Mashariki wanataka kuwe na mabadiliko ya kifikra miongoni iwa jamii ya wafugaji wa sehemu hiyo ili kuwaunga mkono wanawake katika jitihada zao za kupigania mamlaka ya uongozi. Viongozi wa wanawake wanasema licha ya katiba mpya kuhimiza wanawake kutwaa nyadhifa za uongozi, kwenye mikutano kadha ya kisiasa iliyoandaliwa na wazee wa kijamii hususwan kuwaidhinisha wagombezi wanaotaka kuwania viti vya ugavana, useneta na ubunge, wanawake hawashirikishwi kwenye majadiliano. Rukia Abdille mwanamke wa pekee kuchaguliwa diwani kwenye uchaguzi wa madiwani wa Wajir katika wadi ya Laghbogol, aliwashauri wanawake wa Kaskazini Mashariki wajitokeze kutoka kwenye usingizi mkubwa na kupambana na wanaume kutafuta mamlaka ya uongozi. Abdille aliweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuwa diwani kutoka Wajir. Ndiye mwanamke wa kwanza kuchaguliwa diwani katika sehemu hiyo tangu nchi hii ilipojinyakulia uhuru. “Ni kama kwamba nilikuwa nimeenda kinyume cha desturi na utamaduni. Tatizo kubwa lilikuwa ni kuwashawishi jamaa zangu kwamba nataka kuwania kiti cha udiwani,” akasema Rukia ambaye anajulikana kwa jina maarufu la Rainbow. “Ili mtu atafute hatamu za uongozi katika jamii ya Wasomali, jamii ni lazima itoe pendekezo kwa mbari ambao kisha watajitwika jukumu la usimamizi na kuwasilisha pendekezo lao kwa mbari nzima ili kuidhinishwa,” akaeleza Rukia. Kwa muundo huo wa kijamii Abdille akapambana na kiunzi cha kwanza. Jamaa yake haikupendelea, wakiona kuaibika kutoa jina la mwanamke kwenda kugombea mamlaka ya uongozi. “Ilinichukua miezi miwili kuwashawishi jamii yangu na kuwasilisha pendekezo langu. Niliwatumia wanawake kadha kuzungumza na waume zao ili waniidhinishe na nikafanikiwa licha ya kukaribia kukata tamaa,” akasema. Matajiri kadha kutoka ukoo wake walikasirishwa na hatua hiyo na wakatumia mamilioni ya pesa kufanya kampeni ya kuzuia watu kumpigia kura na badala yake kuwapigia wapinzani wake wanne, hata hivyo, yeye ndiye aliyekuwa mshindi. Diwani huyo alianzisha kampeini ya kumsomesha mtoto wa kike na kupigania haki za wanawake huku akiwa amekaa peke yake miongoni mwa madiwani wengi wanaume. Ni kupitia uchaguzi mdogo wa hivi majuzi ndipo alipopata mke mwenzake katika baraza hilo.

Kura za huruma Mwanamke mwengine alichaguliwa baada ya katiba mpya kwenye uchaguzi mdogo baada ya mumewe kufariki dunia. Mumewe alikuwa diwani wa wadi ya Tarbaj. Kaltuma Sheikh alichaguliwa na anajiunga na wanawake walioweka historia katika kanda ya Kaskazini Mashariki. Katika kaunti za Garissa na Mandera, kwa sasa hakuna viongozi wanawake kwenye mabaraza. Wote waliteuliwa na vyama vikuu vya kisiasa. Kanda ya Kaskazini Mashariki imeweka drekodi ya kuwa eneo la pekee ambalo halijawahi kumchagua mbunge mwanamke tangu nchi hii ilipojinyakulia uhuru. Mbunge wa kwanza mwanamke kutoka Kaskazini Mashariki ni Sophia Abdi ambaye aliteuliwa na chama cha ODM. Doris Wangeci ni miongoni mwa wanawake kadha waliogombea viti vya udiwani mjini Garissa bila mafanikio. Hivi majuzi alijiunga na kundi la harakati za wanawake linalopigania utekelezaji wa haraka wa katiba mpya. Kundia la wanawake la harakati za kupigania maslahi ya wanawake mjini Garissa limeelezea wasiwasi wake kuhusu utekelezwaji pole pole wa katiba mpya. Wakizungumza chini ya udhamini wa kundi la upiganaji haki za wanawake la kaunti ya Garissa, wanawake hao walisema utekelezwaji pole pole wa katiba unatia wasiwasi, huku tayari ukiwa umecheleweshwa mnio. Walitoa mwito kwa Rais na Waziri Mkuu kuingilia kati kwa dharura. Tulipiga kura kwa kauli moja kuiunga mkono katiba hii kama wanawake kutoka Kaskazini Mashariki kwa matumaini kwamba tutashuhudia mwanamke wa kwanza kiongozi kuchaguliwa kutoka sehemu hiyo, kwa vile katika siku zilizopita wanawake walifungiwanje ya nyadhifa za uongozi na kauwaacha wanaume wakitamalaki mamlaka ya uongozi,” likasema kundi hilo la Yustur Farah. Kundi hilo liliwahimiza wanawake kote nchini kuungana na kupigania utekelezaji wa haraka wa katiba, likieleza wasiwasi kwamba nchi hii huenda ikatumbukia kwenye ghasia kama tutashindwa kuharakisha utekelezaji wa katiba.


8

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Mijikenda walilia haki za ardhi

…Na Fibi David

J

amii ya marehemu Mzee Nyanje Chula babu ambaye alikuwa ameoa wake wawili aliyekufa zaidi ya miaka kumi na mitano iliyopita, bado haijatambua uhalisi wa katiba mpya. Kavumbi Nyanje mwenye umri wa miaka 40 ambaye ni mwana wa pili wa mke wa pili wa Mzee Chula, daima amekuwa akilalamika kwamba anabaguliwa na ndugu zake wa kiume wa mke wa kwanza kuhusiana na mali ya baba yao na hasa ardhi. Kavumbi aliozwa mume wakati baba yake alipokuwa yungali hai na baadaye kutalikiwa lakini ilimlazimu kungángána yeye peke yake, kurejesha mahari ili apatwe sehemu ya ardhi ya baba yake. Tangu hapo amekuwa akiishi katika ardhi hiyo ya baba yake na amekuwa akipambana kumlisha mama yake mjane ambaye pia ndiye mke aliyebaki wa baba yake kwani mke wa kwanza aliaga dunia hapo awali. Kavumbi ndiye mtoto aliyesalia kwa upande wa mama yake baada ya kaka yake Kadhaa Chula kuuawa na mamba katika mto miaka mitano iliyopita.

Ridhaa Nimepewa shilingi sabuini pekee na kaka zangu kumsaidia mama yangu ambaye anahangaika, tangu niliporejea nyumbani kwa baba, alalamika Kavumbi. Anaongeza; “Nilipokea pesa hizo baada ya kulalamika vikali kwa miaka kumi kwamba bado ni mmoja wa jamii hii kwa vile nililipa mahari yaliyolipwa ili niolewe.” Akaeleza Kavumbi; “Kaka zangu wanachoma makaa ya thamani ya maelfu ya pesa ambazo wanajigawia wao kwa wao wakinisahau mimi na mama yangu.” Wazo la kurithi kipande cha ardhi kutoka shamba la wazazi wake ni ndoto isiyoweza kutimia, “sababu ni kwamba mimi ni mwanamke na mwanamke hana haki katika jamii, ya kudai mgawo wa mali ya jamii. “Urithi! Hilo ni jambo lisilowezekana. Nina hakika nitafukuzwa nyumbani na kaka zangu wakati nitakapoonyesha nia ya kutaka kipande cha ardhi. Ardhi ya jamii siku zote ni ardhi ya wanaume na siwezi kuzungumza juu ya swala hilo. “Hii katiba inawadanganya wanawake wawe vyombo vya kuhangaishwa na kuteswa na jamaa zao majumbani mwao,” Kavumbi asema. Ni dhahiri kwamba katiba haijapenya mashinani katika taifa hili. Watu bado wamekita katika sharuti za kitamaduni.

Serikali ni lazima itekeleze jukumu kubwa katika kuandaa elimu ya kijamii ili kuwaelimisha jamii juu ya hali zao za kikatiba. Kavumbi hayuko peke yake katika swala hili. Wanawake miongoni mwa makabila ya Mijikenda, wanaliona jambo la kurithi ardhi katika jamii hiyo kama ndoto za mchana. Wanawake hawa wanadai kwamba hawajaona manufaa yoyote katika haki ya kumiliki ardhi na usawa wa kijinsia kama inavyoeleza katiba mpya kwa vile utamaduni na desturi za kijamii bado zinawabagua.

Umiliki ardhi “Wanawake chipukizi ambao bado wako chini ya umri wa miaka thelathini huenda wakabadilisha mitindo yao ya maisha na kunufaika na katiba mpya kwa vile wanawake ambao wamekuwa watu wazima tayari wamepitwa na wakati.”alisema Naomi Cidi Kumbatha, kiongozi mwanamke kutoka jamii ya Mijikenda. “Wanawake wenye umri mkubwa wamekita fikra zao katika utamaduni wa kuwaachia wanaume kufanya kila jambo,” aeleza Kumbatha huku akiongeza kwamba wanawake hao wanaamini kwamba haki nyingi ni za wanaume. “Wanawake watu wazima hawana uwezo kitamaduni kurejea kwa wazazi wao na kudai haki zao za umiliki wa ardhi,” akaeleza kiongozi huyo wa kutetea maslahi na matakwa za akina mama mkoani Pwani. Kwenye mswada wa haki kifungu cha 27 juu ya usawa na kutobaguliwa (sehemu ya tatu) ya katiba inasema: “Wanawake na wanaume wana haki ya kutendewa kwa usawa, ikiwa ni pamoja na haki ya nafasi sawa katika mambo ya kisiasa, uchumi, utamaduni na sekta za kijamii.” Kifungu cha 27 (4) kinasema: “Serikali haitambagua kwa njia moja au nyingine mtu yeyote katika misingi yoyote ikiwa ni pamoja na asili ya mtu, kijinsia, uja uzito, kuoa au kuolewa, hali ya afya, asili ya kijamii , rangi, umri, ulemavu, dini, imani, utamaduni, mavazi, lugha au uzazi.” Licha ya kanuni hizo, inatia hofu kwamba watu wa umr ihuu ambayo imefungamana na tamaduni zao huenda wasinufaike na haki za kumiliki ardhi kama inavyohakikishwsa na katiba. “Tunaitarajia katiba mpya kutoa mamlaka kikamilifu mwaka ujao baada ya uchaguzi mkuu wakati viongozi wa nchi hii watakapokuwa wakishughulika na utekelezaji thabiti wa katiba,” alitumai Kumbatha. Utamaduni wa Kimijikenda siku zote umewazuia sana wanawake kuchukua nyadhifa za

Hiki ni kipande cha ardhi katika eneo la uwakilishi bungeni la Magarini mkoani Pwani na ambacho kama sehemu nyingine yoyote ile nchini Kenya, hata wasichana na wanawake wana haki a kupewa ardhi na wazazi wao. Picha: Fibi David

utoaji maamuzi miongoni mwa jamii hiyo. Mzee mmoja wa Kayafungo katika eneo la Kaloleni kaunti ya Kilifi na mshauri wa jamii ya Mijikenda, Babu Katana Kalulu, mwenye umri wa miaka 80 anaipinga katiba mpya akisema inavunja haki za kitamaduni za jamii hiyo. Mzee Kalulu anadai kwamba katiba imeenda kinyume na utamaduni wa Kimijikenda. “Mabinti zangu hawana wawe wameolewa au la, hawawezi kuwa na haki ya kurithi ardhi yangu. Hafai kugawanyiwa ardhi hiyo hata kidogo. Kama kiongozi katika jamii hii, huenda nikaishia kulaaniwa na miungu yetu wakati nitakapotoa ardhi kwa mtoto wa kike,” akalalamika Kalulu.. Akiwa mzee maarufu wa Kigiriama na kiongozi wa kiimani, Mzee Kalulu ana wajibu wa kuongoza ibada katika sherehe zozote za kitamaduni wanazoandaa wana Mijikenda. Mzee Kalulu ni mwanachama wa chama cha

“Kama mzee wa jamii ya Mijikenda, huenda nikalaaniwa na miungu yetu iwapo nitatoa ardhi kwa msichana.” — Mzee Katana Kalulu kitamaduni kinachojulikana kama Malindi District Cultural Association (MADICA). Chama cha MADICA kimekuwa kikiongoza katika kupigania utamaduni wa Kimijikenda na kudumisha kitambulishi cha kitamaduni cha jamii hiyo hapa nchini na katika nchi za nje kupitia Tume ya Kitaifa ya Haki za Kibinadamu (KNCHR). Katiba imeweka wazi usawa wa kijinsia na umilikaji kuwe na utamaduni au usiwepo.

Wanaume sasa waweka vizingiti kwa ugawaji ardhi kwa wanawake

…Na Omwa Ombara

R

amadhan Ibrahim Onguto mwenye umri wa miaka 69 ni mwenye hasira. Ingawa alipiga kura kuiunga mkono katiba, anaapa kwamba hakuipigia kura katiba hiyo ili wanawake wapewe ardhi. Jambo linalozidi kuudhi kulingana na Onguto ni kwamba Serikali inathubutu “kunichukulia mimi kuwa sawa na wanawake hasa kuhusiana na masuala ya ardhi”.

Kulishughulikia “Tangu ulimwengu ulipoanza, jambo hili halijatokea na nakuhakikishia ya kwamba halitatokea. Kwa kusema kweli sintawapa watoto wangu wa kike haki sawa ya ardhi na wale wa kiume. Serikali haiwezi kunilazimisha kufanya jambo kama hilo, isipokuwa iwe inataka vita. Hili ni swala hatari ambalo linaweza kusababisha maafa na hata vifo. Serikai inafaa kulishughulikia jambo hili kwa makini,” alisema Onguto. Onguto ni msemaji wa kijiji na mzee wa kijiji anayeheshimika katika kijii cha Nyakoko huko Kano Kaskazini katika kaunti ya Kisumu.

Ana hasira ka sababu Serikali haiheshimu desturi za kitamaduni ambazo tulizipokea kutoka kwa wazee wetu wa zamani. Anasema katiba mpya inawapa wanawake haki kwa mkono wa kulia na kuwanyang’anya wanaume haki zao kwa mkono wa pili. Onguto tayari ameigawanya ardhi yake ya ukubwa wa ekari moja kwa watoto wake wa kiume na anasubiri hati yake ya kumiliki ardhi iwasili kutoka makao makuu ya Wizara ya Ardhi. Akihojiwa na jarida hili kuhusu watoto alio nao, Onguto aliwataja watoto wake watatu wa kiume na hataji chochote kuhusu watoto wa kike. “Ni jambo la kusikitisha kwamba mabinti zetu ambao tayari wameolewa wanataka keki yao waile. Tayari wana ardhi ya kujenga , kulima na kuvuna . Kwa nini wapate ardhi nyingine kutoka kwa baba zao? Kwa nini warejee kutoka kule waliokoolewa na kuja kung’ang’ania ardhi na ndugu zao wa kiume ambao pia wana wake zao na watoto?” akauliza Onguto. Aliongeza; “Hakuna mtu yeyote katika kijiji hicho ambaye ataruhusu jambo hilo lifanyike. Tutawapeleka mahakamani.”

“Bila shaka sitampa binti yangu yeyote kipande cha ardhi yangu. Serikali haiwezi kunilazimisha kufanya hivyo, ila kama wako tayari kwa vita.” — Ramadhan Ibrahim Onguto

Onguto hata hivyo, anakubali kwamba hatika hali ya matatizo ambapo mabinti zake watafukuzwa na waume zao, hatawaacha wahangaike. “NItawapa mabinti zangu wanaopata taabu kipande kidogo cha ardhi wajenge hapo kwa sababu ya uhusiano wetu wa damu. Ninawapenda sana lakini kuwapa ardhi ni jambo tofauti. Siwezi kuwapa watoto wa kike ardhi yoyote. “ Kulingana na Onguto wanawake katika mpangilio wa kitamaduni huchukuliwa kama paka mwitu kwa sababu ya tabia zao zisizobashirika za kupata mimba wakiwa shule na kuvunjilia mbali matumaini ya wazazi wao baada ya kuweka raslimali katika elimu yao. Jamii inaweza kuuza kipande cha ardhi ilicho nacho ili kupata karo za shule kuwasomesha kisha baadaye wanagundua kwamba binti yao si mja mzito pekee bali ametoroka na mwanaume ambaye hana msingi wowote wa kimaisha. Kwa kawaida mwanamume kama huyo hata kulipa mahari hawezi na wazazi huona ni kama kwamba wamedanganywa. Visa hivyo vimevuruga sana jamii nyingi na kupunguza thamani na heshima aliyokuwa akipewa mtoto wa kike.

“Wasiwasi wangu mkubwa ni kwamba binti aliyeolewa ambaye atarithi ardhi huenda akarithiwa au akaolewa upya na mtu asiyejulikana na mtu huyo akaishia kurithi aridhi yangu. Urithi wa wake bado unaendelea na umekita mizizi katika jamii yetu na hii ndiyo sababu haikubaliki kwa wanaume wengi kuacha ardhi yao kurithiwa na wageni,” akasema Onguto. Kwa katiba mpya aina ya vizuizi na hasira zinazotoka kwa Ongoto na wanaume wengine wenye ardhi vitakuwa visa vitakavyosahauliwa. Katiba itakuwa juu ya sheria zote za kitamaduni na imewapa wanawake uwezo na chombo cha kupigania haki zao za kumiliki ardhi. Si wanawake ambao wanalindwa na kuwa salama bali watoto pia. Sehemu ya 27 na ya 60 ya katiba mpya iko wazi kwani inasema sasa ni kinyume cha sheria kumnyima ardhi mwanamke katika misingi ya kijinsia. Hakika haijalishi kama mwanamke ameolewa au la. Sheria inayosimamia masuala ya kijamii inatilia nguvu msimamo huo wa kisheria ambapo inasema watoto wote watarithi ardhi kwa usawa bila ya kubagua iwapo mtoto ni wa kike au wa kiume.


9

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Harakati za ukombozi wa wanawake wa Gusii kwenye kifungo cha kisiasa

…Na Ben Oroko

W

akati Mary Orwenyo alipostaafu kama mwalimu wa shule za msingi mnamo mwaka 2008, ili kujiingiza katika ndoto yake ya kuongoza na kuwapa uwezo wanawake wa kundi la akina mama la Ritii katika kata ya Kiabonyoru ya kaunti ya Nyamira, haikumthubutukia kwamba alikuwa anajitupa katika ulingo mpana wa mambo makubwa katika majukumu ya uongozi wa wanawake na jamii. Tangu kuchaguliwa kwake katika wadhifa wa mwandishi wa tawi la wilaya la Chama cha Maendeleo ya Wanawake (MWYO) mnamo mwaka 1991, matumaini yake ya uongozi yameimarika, na kwa sasa ni mwenyekiti wa chama hicho tawi la kaunti ya Nyamira. Kuimarika kwake katika sekta ya uongozi kunampa nafasi ya kuwa mmoja wa wanawake viongozi ambao wamo katika nafasi nzuri ya kutwaa nyadhifa zilizotolewa na katiba mpya. Akihimizwa na maarifa yake ya uongozi, Orwenyo ametangaza nia yake ya kugombea kiti cha mwakilishi wa wanawake katika kiti katika kaunti ya Nyamira kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2012. Mary alizaliwa mwaka 1953 katika kijiji cha Monga , Bomagacho katika eneo Bunge la Mugirango Magharibi katika kaunti ya Nyamira, akiwa ni mtoto wa saba wa Mzee Michael Kimwei na Mama Susan Kwamboka. Alisomea shule ya msingi ya Gekomoni huko Mugirango Magharibi kuanzia

mwaka 1962 hadi 1966 kabla ya kujiunga na shule ya msingi ya Rigena klatika sehemu iliyokuwa ikijulikana kama Wanjare Mugirango Kusini katika kaunti ya Kisii kuanzia mwaka 1967 hadi mwaka 1969 ambako alifanya mtihani wa CPE. Alijiunga na shule ya sekondari ya Nyanchwa Mixed High School mjini Kisii ambako alifanya mtihani wa kidato cha nne na kuibuka na hati ya daraja ya tatu yaani Div .III kabla ya kujiunga na chuo cha mafunzo ya ualimu cha Shanzu kwa mafunzo ya ualimu ya P1 kuanzia mwaka 1977 hadi 1979. Baada ya masomo yake ya P1, Orwenyo alipelekwa katika shule ya msingi ya Nyangoge katika sehemu ya Mugirango-Borabu Kaskazini ambako alisomesha katika shule kadha katika sehemu hiyo hadi alipostaafu mwaka 2008.

Harakati Kufuatia kushughulika kwake kwenye harakati nyingi za wanawake nyanjani, aliongoza makundi ya akina mama ya jkijamii na makundi ya kujisaidia wenyewe ambako alipanda mamlaka na kuhudumu katika Chama cha Maendeleo ya Wanawake katika nyadhifa mbali mbali kabla ya kupanda na hatimaye kuwa mwenyekiti wa tawi la kaunti ya Nyamira wa shirika hilo. Mary anawataka wanawake wajinasue kutoka kwenye tamaduni za Kikisii ambazo kwa miaka mingi zimewanyima nafasi ya kuchukua nyadhifa za uongozi. “Nimejiandaa kupigania wadhifa

Omanyo aazimia kuiamsha Nambale …Na Frank Ouma

R

uwaza yake ni kuwatia motisha akina mama, vijana na hata wanaume kiuchumi, kijamii na kisiasa ili kuwawezesha kujiamulia hali yao kwa siku za usoni. Tunataka hali ambapo wakazi wa Nambale wataweza kuamka kutoka kwenye usingizi pono na waweze kumchagua kiongozi kutokana na manifesto yake na ajenda ya kuleta mabadiliko kwenye nyanja za kimaendeleo na wala si kwa sababu mtu kama huyo anachaguliwa kwa sababu alihongana na ndipo akafanikiwa kunyakua kiti cha uongozi, akaeleza Catherine Nakhaabi Omanyo.

Chris Okemo Hapo mwakani 1212, Catherine mwenye umri wa miaka 33, atajibwaga tena uwanjani kwa mara ya pili kugombea kiti cha ubunge cha nambale. Mnamo Mwaka wa 2007 kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Catherine ambaye alikuwa mojawapo wa wale waliokigombea kiti hicho, alinyakua nafasi ya tatu nyuma ya mbunge wa sasa, Chris Okemo wa chama cha Orange Democratic Party aliyefuatwa na John Bunyasi wa chama cha Narc. Omanyo ambaye alisimama na tikiti ya chama cha Kenya African Democratic Development Union, hajatangaza ni chama kipi ambacho Mwaka ujao ataomba tikiti yake. Wakati huu, akasema, nimejitokeza kimatso matso kukinyakua kiti cho kwa upale na ulimbe kwani naamini wakazi wengi wa Nambale wamejipata wameachwa nyuma kimaendeleo kulinganishwa na sehemu nyinginezo za wilaya ya Busia. Tunataka uongozi ambao unatilia maanani mahitaji ya wananchi ili nao waweze kupiga hatua kubwa za kimaendeleo.

Catherine alikubaliana na dhana kwamba si rahisi kwa mwanamke kupambana vilivyo uwanjani na kundi la wapinzani wa kiume. Hata hivyo, anaamini kwmba kilicho muhimu kwa mwanasiasa ye yote Yule jinsi atakavyouza sera zake kwa wapiga kura kabla ya uchaguzi, jambo ambalo anaamini limempa motisha ya kutosha. Ametoa wito kwa wagombezi wa kike kwa viti mbalimbali mwaka ujao, wasilegeza kamba wala kufa moyo kutokana na propaganda chungu nzima ambazo hupenda kupeperushwa na wanasiasa wengi pamoja na wafuasi wao dhidi ya wagombezi wa kike. Alisema kilicho muhimu ni kuanza kujipanga mapema ili wakati filimbi itakapopigwa ya kuingia uwanjani, akina mama wanasiasa wasipatikane kama wameduwaa. Omanyo alisikitika kuona kwamba si wanawake wengi hutangamana na wanasiasa wenzao wa kiume kama itakikanavyo. Alieleza kwamba kufanya hivyo hakumaanishi kwamba ushirikiano kama huo una dhana ama nia ya mambo ya mapenzi, la, kwani hayo yote ni mapenzi ya mtu binafsi na zaidi ya yot hayo, si kila mwanamke huwa yuko tayari kujihusisha na mambo kama hayo eti ndipo aweze kufanikiwa kisiasa. Alilaani mila Fulani za kiutamaduni ambazo zinapinga kuona msichana akigombea kiti cha udiwani ama hata ubunge katika eneo alikozaliwa akisema kwamba mawazo kama hayo yalipitwa na wakati hwa sababu msichana kuolewa kwingineko, huwa ni hiari ya mtu binafsi. Catherine alieleza kwamba kwa sababu tarafa zote za Busia sasa zitakuwa chii ya kaunti moja, nia yake iatakuwa ni kuhakikisha kwamba akichaguliwa, atasukuma gurudumu la maendeleo vilivyo kwa manufaa ya wakazi wote wa Busia kwa jumla.

“Ili taifa hili liweze kufikia malengo ya ruwaza ya 2030 na lengo la ustawi wa milinia, akina mama sharti wapewe motisha kwa yote wafanyayo .” — Mary Orwenyo

wa mwakilishi wa wanawake katika kaunti ya Nyamira kwenye uchaguzi wa mwaka 2012 kwa vie ninaamini kwamba wanawake wana imani na uongozi wangu kwa vile imekuwa nikiwahudumia kuanzia mashinani hadi kwenye chama cha Maendeleo ya Wanawake,” akasema kinara huyo. Nikichaguliwa kwenye mamlaka hayo, Orwenyo anasema, ataendelea kufuatilia kutimiza ndoto yake ya kuhakikisha kwamba wanawake wanakaa mahali wanapostahili katika jamii. Kwenye mahijiano ya pekee na Mwanamke Mkenya, Orwenyo anasema ana imani na wanawake wa sehemu hiyo akisema wana vipaji vya uongozi na kama watapewa nafasi wanaweza kuleta mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi miongoni mwa jamiii na nchi nzima kwa jumla. “Nilizaliwa na kulelewa katika vijiji, nikifahamu kwamba mahali pa mwanamke ni jikoni na kuwatunza watoto nyumbani,” akumbuka Bi Orwenyo. Anaeleza; “Tangu wakati huo mengi yamepeperushwa na upepo na ulimwengu umepitia mabadiliko makubwa na kubadiisha jinsi mambo yalivyokuwa yakifanyika wakati wa uhai wa nyanya yangu.” Anasema wakati umefika ambapo kila mwanamke anapasa kutumia nafasi inayotolewa katika katiba mpya kuwapa amii zao uongozi wa kisiasa na uchumi wa kijamii na kuwapa uwezo wanawake na vijana ambao ndio walio aslimali kubwa zaidi ya kibinadamu nchini. Orwenyo aliamua kujitupa katika uongozi wa wanawake baada

ya kustaafu kazi ya ualimu baada ya kutambua kwamba akiwa darasani hawezi kupata nafasi ya kutangamana na kubadiishana maoni na marika yake ambao walihitaji uongozi wake katika ngazi za kijamii na majumbani. Anasikitika kwamba wanasiasa wamekuwa wakitumia umaskini wa wanawake kwa miongo mingi na kutumiwa vibaya kwenye kampeini za kisiasa na kwenye uchaguzi.

Wanasiasa “Huwa naungulika moyo wakati ninapowaona wanawake katika jamii wakiwa wamebeba watoto wadogo migongoni wakicheza mbele ya wanasiasa siku nzima wakati wa kampeini za uchaguzi, kasha baadaye wanasiasa hao huwapa akina mama hao shilingi hamsini tu,” Orwenyo akalalamika. Akauliza; “Je, shilingi hamsini ni kitu gani kwa mwanamke mwenye watoto wa kuwalisha kuwanunulia nguo na kuwapeleka shule?” Aliwahimiza wanaume kutoka sehemu hiyo waonyeshe mwelekezo wa uongozi na kuwakataza wake zao kutumiwa vibaya na wanasiasa wakati wa kampeini za uchaguzi na badala yake, watafute mbinu za kuwapa uwezo wanawake na wao wenyewe kiuchumi majumbani mwao ili kuziba mapengo ambayo yatawafanya washawishike kwenda kutumiwa vibaya na wanasiasa. “Ili nchi hii ifanikishe ruwaza ya mwaka 2030 na kufanikisha shabaha za millennia, wanawake wanapaswa kupewa uwezokatika sekta zote, “ akaeleza Bi Mary Orwenyo.

Shujaa mwenye azma ya kuingia katika Bunge wa chama cha ODM Kenya. Wakati wa uchaguzi mkuu, Masis alipata kura elfu tisa na kushikilia nafasi ya pili. “Haikuwa rahisi hasa ukifikiria kwamba mpinzani wangu mkuu alikuwa Dkt Noah Wekesa mtu ambaye ana raslimali na kisha ni waziri.” Baada ya uchaguzi, mgombezi huyo ambaye alipata masomo katika shule ya Kibuk Girls kwenye miteremko ya Mlima Elgon, alirejea kwenye kazi yake ya huduma za jamii.

…Na George Omonso

H

ebu fikira haya: Wewe ni mwanamke chipukizi na mwanasiasa, hujatimiza miaka 35, una jamii changa. Uligombea uteuzi wa chama fulani cha kisiasa na kushinda lakini ukatolewa kwa hila kwa sababu wewe ni mwanamke. Matokeo ya uchaguzi yanafutiliwa mbali na hati ya chama cha uakilishi anapewa mwanaume ambaye ulimshinda kwenye uteuzi. Unapeleka malalamiko mahakamani. Rais mwenyewe anaingilia kati na anakwambia ujiondoe akisema; “Wewe bado mtoto mdogo.” kisha akwambie atakupa kazi.

Anang’ang’ania Je, ungetetemeka na kutupilia mbali jitihada zako za kutafuta haki? Je, ungekubali kupewa kazi nzuri , ukifikiria kwamba ulikuwa mfanyi biashara ambaye awali ulikuwa umejiuzulu kazi? Hayo ndiyo masaibu yaliyompata Jeniffer Chekwemoi Masis miaka kumi iliyopita. Leo bado anang’ang’ania kutimiza ndoto yake ya kuwa Mbunge na sasa ameonyesha hamu ya kupigania kiti cha Endebess kilichoanzishwa hivi majuzi. Masis alikuwa ameshinda uteuzi wa chama cha Kanu na alikuwa anajiandaa kupambana na wagombezi wengine katika kiti cha Bunge cha Kwanza. Alikuwa amewabwaga wanaume 14, wawili wakiwa ni wanasiasa shupavu, Michael Kitiyo na Mbunge Maalumu wa zamani, Samwel Moiben. Hati ya chama ilikabiliwa Moiben kwa njia ya udanganyifu baada

Kuwakilisha “Iliniuma roho sana niliponyimwa fursa ya kuwa mgombezi wa chama changu kwenye uchaguzi mkuu uliopita wa 2007.” — Jennifer Chekwemoi Masis ya madai na propaganda kwamba jamii hiyo bado haijakuwa tayari kuwa na kiongozi mwanamke hasa katika mamlaka ya Ubunge. “Liliniuma moyo jambo hili la kunizuia kuwa mpeperusha bendera, katika misingi hiyo,” akasema Masis huku akibubujikwa na machozi. Anakumbuka: “Nilipiga hatua kubwa mwaka 2007 wakati nilipogombea uchaguzi wa kiti cha bunge cha Kwanza ambacho sasa kimegawanywa mara mbii huku sehemu moja ikiwa ni eneo bunge la Endebess.” Masis alikuwa amechapishwa katika gazeti kuwa mgombezi wa ubunge

Kwa kuwa ajenda yake kubwa ni kuwapa wanawake uwezo., Masis ambaye ni mwanaharakati wa kupigania haki za wanawake amesafiri na wanawake kupitia shirika la kibinafsi la Tears of Women, yaani Machozi ya Wanawake. Si mshirikishi tu wa kongamano la wanawake katika uongozi katika kaunti ya Nzoia, bali pia naibu mwenyekiti wa Agenda ya Kitaifa ya Wanawake. Masis anasema kundi la wazee wa Kisabaot kutoka eneo la Kwanza waliiendea jamii yake kuiomba imruhusu kuwawakilisha. Kwanza alisita lakini wazee hao wakasisitiza, wakisema kwamba wamemjua kwa muda mrefu na wameona utenda kazi wake. Waliamini wazee hao kwamba Masis angekuwa kiongozi bora kwa jamii hiyo. “Nilishangaa na nikaomba nipewe wakati wa kufikiria jambo hilo na kutoa uamuzi na kisha kushauriana na jamii yangu na jamaa zetu kwa jumla,” akasema. Maoni ya jamaa zake hayakuwa na msimamo mmoja isipokuwa kwa dada zake wawili, mumewe, baba yake na ndugu zake ambao walimuunga mkono kwa dhati.


10

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Ardhi: Wanubi sasa wana matumaini makubwa

…Na Odhiambo Orlale

S

wala la ardhi katika mtaa wa Kibera mjini Nairobi ni swala zito ambalo ni sawa na bomu iliyotegwa ambayo inaweza kulipuka wakati wowote , hasa kwa wanawake wa Kinubi wenye ardhi. Jamii ya Wanubi inadai kwamba ardhi hiyo ni yao na ambayo wanaiita Kibra, na wametumia kila nafasi kupitia kwa baraza la wazee wao kuwakumbusha wakuu wa Serikali kuhusu maovu ya kihistoria kuhusiana na haki yao ya kisheria na umilikaji wa mali. Wanashikilia kwamba eneo hilo la ardhi lilinyakuliwa na Serikali na watu kutoka nje kujenga majumba ya kifahari bila ya kuwajali. Maafa ya wanawake wenye ardhi katika mtaa huo mkubwa wa mabanda yameongezewa ubaya na kuingizwa kwa siasa kwenye swala la kodi ya nyumba katika siku zilizopita na kukataa kwa baadhi ya wapangaji wanaume kuheshimu makubaliano ya upangaji nyumba za mtaa huo.

Mizizi Wanubi ambao wazee wao wa kale walitoka Sudan Kusini wanasema na kushikilia kwamba walipewa ardhi hiyo na serikali ya mkoloni kwa kutambua jukumu walilotekeleza kwenye vita vya kwanza na vya pili vya dunia. Ardhi hiyo inaanzia sehemu inayojulikana kama Dagoretti Corner karibu na njia panda kwenye duka la Nakumatt katika barabara ya Ngong, hadi kwenye makaburi ya Langata na hadi uwanja wa ndege wa Wilson kwenye barabara hiyo hiyo ya Langata. Kulingana na kumbukumbu za Serikali, eneo hilo la hekta 225 ni mali ya Serikali na asilimia 95 ya wakazi wa sehemu hiyo ni wapangaji. Hivi leo wengi wa Wanubi wanaishi katika maeneo mawili ya vijiji kumi ambapo viwili hivyo ni Maki-

na na Lindi ambako wana moja wa misikiti mikubwa. Kwa upande wao wanawake wa Kinubi hawajaachwa nyuma na siku zote wamekuwa wakipigania haki zao hasa kwa wale ambao wana ardhi. Swala hilo ni gumu mno hivi kwamba wanawake wote waliohojiwa kwa ajili ya taarifa hii wameomba wasitajwe wakihofia kufanyiwa dhuluma . Pia walisema kwamba wamo katika mwezi wa saumu wa Ramadhan ambayo iliangukia katika mwezi wa Agosti katika kalenda ya kimataifa. Mama Amina (silo jina lake halisi) anasema kwamba yeye ni mama wa watoto saba na ni mwenye mabanda kumi katika mitaa ya Makina na Lindi katika mtaa huo wa Kibera ulio katika eneo Bunge la Langata. Alirithi majengo hayo kutoka kwa mumewe ambaye alifariki miaka kumi iliyopita. Wapangaji wake wanamlipa kiasi cha shilingi elfu moja kila mwezi , ambazo si pamoja na malipo mengine kama vile umeme na maji. Wapangaji hao wanatumia choo kimoja pamoja na wapangaji wa nyumba nyingine katika sehemu hizo. Mama Rukia (sio jina lake halisi) ni mama wa watoto watano na anaishi katika mtaa wa Olympic. Ana mabanda ishirini ya kukodisha katika mitaa ya Gatwikira na Kianda ambako analipwa kiasi cha shilingi elfu moja na mia tano kwa mwezi kwa nyumba zake zilizoezekwa kwa mabati ingawa ni za udongo. Rukia ambaye pia ni mjane ilimlazimu kujitetea vikali yeye na wanawe, baada ya mumewe kufariki dunia miaka mitano iliyopita ili kulinda mali yao. Tatizo lingine lilikuwa wapangaji ambao walikuwa ‘kichwa ngumu’ dhidi yake, lakini aliwatumia maajenti na idara ya utawala kumsaidia kukusanya kodi yake kama kawaida. Kwa upande wao, Amina na Rukia ni mifano wazi ya matatizo

Jamii ya Wanubi kutoka mtaa wa Kibera (ama Kibra) wakiandamana nje ya Mahakama Kuu mjini Nairobi wakilalamikia unyakuzi wa ardhi yao. Akina mama wa Kinubi wenye mabanda ya kuishi katika Kibera sasa wana matumaini kwamba katiba mpya itawawawezesha kurejeshewa ardhi yao iliyokuwa imenyakuliwa. Picha: Odhiambo Orlale makubwa ambayo yanawakabili wanawake Wanubi wenye nyumba. Niwahasiriwa wa tamaduni za Kiafrika katika upande mmoja na siasa za Kibera katika upande mwingine na eneo Bunge la Langata kwa upande mwingine.

Kupigania haki Katika siku ziizopita, wamekuwa wakibaguliwa kwa sababu ya jinsia yao. Ndugu zao wa kiume huingilia wakati kuna swala la mirathi wakitoa mifano ya haki za Kiafrika na Kiislamu kuhusu ardhi. Kulingana na Amina ilikuwa vigumu hapo mwanzo. Ilimlazimu kusimama kidete kupigania haki yake kutoka kwa wapangaji wake ambao wengi wao waliwadharau wanawake na kuitumia sababu hiyo kuchelewesha malipo ya kodi ya nyumba. Amina anasema: “Tulilazimika

Mng’ang’anio wa ardhi mpakani watishia kulipuka

…Na Hussein Dido

H

uku Tume Huru ya Mipaka na Uchaguzi, (IEBC), ikianza shughuli zake chini ya katiba mpya, hakika inakabiliwa na kibaru kigumu miongoni mwa maswala mengine kama vile dhuluma za ardhi zilizofanywa na tawala zilizopita na kunako mwanzo wa kupatikana kwa uhuru. Mji wa Isiolo ni moja ya miji ambayo imekalia bomu kubwa linalosubiri kulipuka ambalo linaingojea tume hiyo ya mipaka na uchaguzi kuanza kazi yake.

Uzito wa kikatiba Mji wa Isiolo unakabiliwa na matatizo makubwa baada ya majirani Nyambene kujiamulia kujiwekea mipaka pasi na kufanya mashauriano na wahusika wengine huku kukiwa na mapendekezo ya miradi mipya ambayo ni pamoja na mji wa kisasa wenye barabara za kimataifa na barabara za reli zikikingama mjini humo. Jamii za wafugaji kutoka sehemu iliyojulikana kama wilaya ya mpaka wa kaskazini yaani Northern Frontier District (NFD)walikabiliwa na mizozo ya kisiasa ya uzito wa kikatiba katika siku zilizopita kukiweko na kikundi kilichokuwa kikutaka kujitenga, na kutokana na hayo serikali

ikaanzisha harakati za kupambana na kikundi hicho cha mashifta. Wakati wa kipindi cha machafuko hayo baadhi ya watu waliokuwa na uwezo mkubwa serikalini walichukua nafasi hiyo na kubadilisha mipaka na kuiingiza Isiolo katika wilaya kubwa ya Meru. Chama cha wakfu wa ardhi ya Waso ambacho kinatetea maswala ya ardhi katika sehemu hiyo kilimlaumu Jackson Angaine sasa marehemu, ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Ardhi kwa kufanya mageuzi kadha wa kadha ya mipaka na taratibu za ugavi wa ardhi ambazo zilibadilisha mipaka ya Isiolo huku akipanua wilaya ya Meru. Barua nyingi ziliandikwa kati ya lililokuwa Baraza la Wilaya ya Isiolo, Idara ya Utawala wilayani, Baraza la Wilaya ya Meru na Wizara ya Ardhi mapema miaka ya 1970 ambazo zinaashiria msururu wa harakati zilizofanywa kutokana na umaarufu wa waziri huyo katika kubadilisha mipaka hiyo na kuipendelea wilaya ya Meru. Mshirikishi wa wakfu huo wa ardhi, Hassan Shano anasema kuzinduliwa kwa katiba mpya ni afueni kwa sehemu hiyo na kesi za mipaka na dhuluma za awali zitashughulikiwa chini ya sheria hii mpya. Akiwasilisha taarifa ya kumbukumnbu kwa maafisa wa tume ya TJRC katika kituo cha Mafunzo cha Rural

kutumia idara ya utawala katika visa mbali mbali hasa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 kulipozuka ghasia za baada ya uchaguzi , ili idara hiyo iingilie kati kuwataka wapangaji walipe kodi ya nyumba.” Kwa hakika wengi wa wenye nyumba katika mtaa huo wa Kibera wamekuwa na historia ya chuki kati yao na wapangaji juu ya swala la kodi ya nyumba, ambalo wakati mmoja lililipuka na kusababisha ghasia kubwa na kuwalazimisha polisi kuingilia kati. Visa vibaya zaidi vilitokea baada ya uchaguzi mkuu wa miaka ya 1997 na 2007 wakati nyumba nyingi zilipochomwa na wenye nyumba kulazimika kukimbilia usalama baada ya swala la kodi za nyumba kuingizwa siasa. Anasema Amina; “Katiba hii mpya inawapa wanawake wenye nyumba kaka mimi, matumaini kwamba haki zetu na haki ya kumiliki mali zita-

heshimiwa na kulindwa. Hofu yetu ni kwamba imehukuwa muda mrefu kutekeleza sura muhimu zinazoathiri maisha yetu ya kila siku, lakini bado tuna matumaini.” Hata hivyo, baadhi ya Wanubi ambao wana uhusiano mzuri na wakuu, wamehamia kwenye mitaa ya kisasa iliyojengwa na shirika la taifa la nyumba, yaani National Housing Corporation, shirika la Serikali linalomilikiwa na Wizara ya Nyumba. Mitaa hiyo ni pamoja na mradi wa pamoja kati ya Serikali ya Kenya na shirika la Habitat la Umoja wa Mataifa wa kustawisha mitaa ya mabanda. Baraza lenye uwezo mkubwa la wazee wa Kinubi, limeasilisha taarifa kwa njia ya barua na kwa kusema kwa tume , majopo kazi na tume ya uchunguzi wa marekebisho ya katiba ambako waliwasilisha malalamiko thabiti kwa madai yao.

Training Centre, Shano alisema kwamba Serikali ya Kenya iliyokuwa ndio mwanzo imepata uhuru, ilibadilisha mipaka ya wilaya ya Isiolo bila ya kujali kwa manufaa ya wilaya ya Meru kwa kuchukua maeneo yaliyokuwa ya Isiolo ya malisho, na sehemu nyingine ya rehani na nyingine zenye rasliSehemu ya mji wa Isiolo. Kwa sasa kuna ung’ang’aniaji wa ardhi kwenye mali za kimazingira zinazofaa Kaunti ya Isiolo sawa na tangu Kenya haijajitawala. Wakazi wa sehemu hii kwa malisho zinazopakana na wana matumaini kwamba katiba mpya itasuluhisha mizozo hiyo yote. Picha: wilaya kubwa ya Meru. Hussein Dido Kulinganana taarifa yake, sehemu ambazo zimetwaliwa inayopinga baadhi ya madai na licha kuhifadhi maji kama vile tarafa ya na kuingizwa katika wilaya ya Meru ya rufaa kadha zilizowasilishwa na Kina (Bisan Adi) iliyochukuliwa na na ambazo zinazozaniwa ni pamoja baraza lililokuwa la wilaya ya Isiolo, wilaya kubwa ya Meru. na Boqe, Magaado, Daka Borr, Roqa Serikali haishughuliki katika kusuKwa upande mwingine jamii za (hadi kuvuka mpaka wa mbuga un- luhisha tatizo hili ambalo limekuwa Kisomali ziliingia katika maeneo aopakana na Tharaka), Kambi Roqa, likizusha migogoro katika miaka ya ya Isiolo na sehemu zilizonyakuQubi Chafesa, Kubi Sera, Hamares, hivi karibuni. liwa ni pamoja na Hadado, Arb Ja(Kachuru) Baricha Boru , Jaro, Yaqa Hali hiyo bado inaendelea huku han, Banane, Irres Wachile, Guchi Bute na kuvuka sehemu za Maili Nyambene na majirani wengine Chachafa, Dusot, Basir, Gofo, katika Nane. wakijiongezea maeneo ya kaunti zao wilaya jirani ya Wajir. Sehemu nyingine zilizoathiriwa kutoka kaunti ya Isiolo. Tunatumai Kubadilishwa kwa mipaka na vibaya na mabadiliko ya mipaka hiyo kwamba katiba mpya itatuokoa kuto- dhuluma nyingine za ardhi yasemeni sehemu ambazo ni pamoja na kana na unyanyasaji huo wa kikoloni, kana zilitokea baada ya mwaka 1963 eneo la shamba la ufugaji la Livestock äsema Shano. wakati Serikali ya Kenya ilipotangaza Marketing Holding Group Complex Mshirikishi huyo anasema ka- hali ya hatari katika sehemu za Kaskaambalo liko chini ya vyama kadha tika siku za hivi karibuni, sehemu za zini na kuzitumia sehemu za mkoa ambapo hapo awali maeneo hayo ya- Kaskazini na Mashariki mwa Isiolo wa Kaskazini Mashariki na wilaya likuwa yanakaliwa na mbari za Kiso- zimekuwa zikimenywa na Nyambene jirani zilizowekwa chini ya usimammali za Harti na Issak na wafugaji wa kwa usaidizi wa watu wenye uwezo izi mmoja ili kutekeleza mpango wa mkubwa serikalini. Isiolo imepoteza kiusalama uliosababisha mauaji ya Waso Borana. Ingawa kuna kesi mahakamani sehemu nyingi za malisho na sehemu halaiki na kupotea kwa mali za raia.


11

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Kushinikiza haki za wanawake za kumili kimali Changamoto ni utekelezaji kwa katiba kwa ukamilifu

…Na Ruth Omukhango

W

akati ambapo wanawake wanapigia tarumbetamsfanikio ambayo wamepata kwenye katiba kuhusiana na haki ya umilikaji wa ardhi na mali huku kukitiliwa mkazo mali ya pamoja ya mke na mume waliooana, na urithi wa ardhi, changamoto kubwa itakuwa ni kupatikana kwa haki hizo pale ambapo sheria za tamaduni na sheria za nchi zinagongana. Kidesturi katika jamii nyingi nchini wanawake hawakuruhusiwa kurithi ardhi na mali kwa kuwa baadhi yao walichukuliwa kuwa mali ya waume zao. Wakati inapotokea kwamba ndoa hizo zivunjike kufuatia kifo cha mume, wanawake hao hupoteza mali yake na ardhi ya mumewe kwa sababu mali hiyo hurejea kwa jamaa wa kiume wa mumewe ambao huenda wakawa ndugu za mumewe au watoto wao wa kiume.

Ubaguzi Kwa wengi, wale ambao tamaduni za aina hiyo zimedumisha ubaguzi kwa wanawake kwa kuwazuia kurithi ardhi na mali, sheria mpya imeibuka kama tukio la ajabu na la kushangaza. Imezua maoni tofauti. Ni dhahiri kwamba kwa usaidizi wa sheria hiyo mpya iliyoko ndani ya katiba na maongozi ya kitaifa ya ardhi, kumekuwa na mwelekeo mpya katika kanuni ambazo zimebadilishwa ili kumnufaisha mwanamke ambaye ndiye anayegandamizwa katika jamii. Mfumo huu mpya wa kisheria

inahitaji kuwe na mbinu mpya za utekelezaji kati ya wapiganaji wa haki za wanawake na jamii zinazohusika ili kupatikane mabadiliko ya kinadharia na kifikra. “Kuna haja ya kuchunguza kwa undani na kuelewa tamaduni za jamii hizo ambako tunahudumu kama wapiganaji wa haki za wanawake, kwa lengo la kutekeleza kanuni za katiba mpya na sheria nyingine ambazo zinalinda haki za wanawake za kumiliki mali ili kushughulika kwa njia ya hakika itakayoleta mabadiliko yanayokusudiwa,” asema Priscilla Nyokabi ambaye ni mkurugenzi mkuu wa Kituo cha Sheria .

Wamilikaji ardhi Hadi kuzinduliwa rasmi kwa katiba mpya mnamo mwezi Agosti 2010, haki za wanawake za kumiliki ardhi na mali nyinginezo nchini zilisimamiwa na sheria za kijamii na sheria ya Uingereza ya umiliki wa mali kwa wanawake walioolewa ya mwaka 1882 ambayo ilishirikisha tofauti kadha kuhusu maswala ya mirathi, ubadilishaji wa wamilikaji wa ardhi haukuwashirikisha wanawake katika utoaji maamuzi kuhusu ardhi. Ingawa sheria ya mirathi ilipitishwa mwaka 1991, kulikuwa na migongano kati ya vifungu vya katiba na usawa wa kijinsia na desturi za kitamaduni ambazo ziliwabagua wanawake katika utekelezaji wake. Baadhi ya hitilafu hizo ni kwamba sheria hiyo haishughulikii maswala ya wajane kwenye ndoa za mume mmoja wake wengi na mume mmoja mke mmoja. Kadhalika sheria hiyo inawapa nguvu

“Kuna umuhimu wa kuchunguza na kuelewa tamaduni ili kuwezaesha maongozi yaliyomo katika katiba mpya yanayolinda haki za wanawake kimali yaweze kuwa ya manufaa kwao .” — Priscilla Nyokabi, Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Sheria

zaidi waume kuliko wake zao katika urithi. Zaidi ya hayo ni kwamba sheria hiyo haikutoa ulinzi wa kutosha kwa watoto wanaozaliwa nje ya ndoa. Sehemu ya arobaini ya katiba inasema kwamba kila mtu ana haki ya kumiliki ardhi awe mtu binafsi au kwa kushirikiana na wengine. Haki za wanawake zinatambuliwa zaidi katika kifungu cha 60 (1) (f) ambacho kinaondoa ubaguzi wa kijinsia kwenye umiliki wa ardhi na mali nyingine hapa Kenya. Katiba ambayo ndiyo sheria kuu, inawalinda wanawake na makundi ya watu wanaogandamizwa katika jamii kama inavyosema Sura ya kwanza kifungu 2(4) “Sheria yoyote ikiwa ni pamoja na sheria ya kitamaduni ambayo inaenda kinyume na katiba haifai na kutofaa kwake katika ulinganifu, na sheria yoyote kinyume cha katiba si halali. Kifungu hicho kinawalinda wanawake ambao ndio kundi linalofanya kazi nyingi kwenye ardhi kuliko kundi lolote la watu katika jamii kuanzia asilimia 80 hadi asilimia 90 ya wafanyi kazi katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na zaidi ya asilimia 70 ya uzalishaji wa mazao ya kibiashara, lakini wanabaguliwa katika masuala yote yanayohusu umilikaji wa ardhi. Haki za wanawake za kumiliki ardhi na mali nyingine ndizo ufunguo wa uendelezaji wa ustawi na usalama wa chakula nchini. Ni muhimu hivyo basi kwamba, kila jitihada zifanywe katika kuhakikisha kwamba haki ya wanawake ya kumiliki ardhi na mali mengine zinalindwa kwa njia ya halali, kiuchumi, kijamii na kitamaduni. Kulingana na Nyokabi, wapiganaji wa haki za wanawake bado wana nafasi ya kutoa michango yao na kushiriki katika utungaji wa sheria mpya kuhakikisha kuwa sheria hizo zinafungamanisha mambo yote

na kuwahami wanawake dhidi ya vipengee vilivyo na mianya ambayo inaweza kutumiwa kuwabagua katika masuala ya haki za umilikaji wa ardhi na mali nyinginezo. Hayo kulingana na kifungu cha 68 cha Sura ya tano (iii) ya katiba, inalipa bunge jukumu la kuchunguza, kuzifanya thabiti na kuziimarisha sheria zilizopo na kutunga sheria kusimamia kutambuliwa na kulindwa kwa mali ya watu waliooana hasa nyumba ya wahusika hao wakati na baada ya ndoa kuvunjika.

Mbinu zinazofaa Kulingana na Rebecca Wangui, mshirikishi wa mambo ya haki za ardhi katika shirika la Kenya Land Alliance, wapiganiaji haki za wanawake wanapaswa kujitokeza na mbinu zinazofaa ili kufanikisha malengo yao ya kupata haki kamili za kumiliki ardhi na mali nyinginezo, kupitia mbinu mbali mbali. “Wanawake ni lazima wapate changamoto za kuwahimiza kupata haki za umilikaji wa ardhi na mali nyingine iwe ni katika njia za kibinafsi au kwa ushirikiano na kupata hati ya pamoja ya umilikaji ardhi na waume zao ili kuhami na kulinda maslahi yao katika maswala ya ardhi na mali nyinginezo,” akasema Wangui. Mbali na kutoa ufahamu kuhusu desturi za kitamaduni zenye madhara, kubadilisha dhana na misimamo, kuna haja ya kuwaleta wanaume kwenye harakati za kuwaelimisha kuhusu haja ya kuimarisha usawa wa kijinsia kuanzia kwa kijamii. Kulingana na Wangui ili kuimarisha manufaa yaliyopatikana, wanawake ni lazima wawe walinzi wa sheria za usimamizi wa mambo ya kijinsia katika taasisi za usimamizi kuhakikisha urari wa kijinsia na maongozi na sheria.

Shaibu wa zaidi ya umri wa miaka 85 apigania ardhi yake iliyonyakuliwa …Na Emeldah Rutendo

F

atuma wa Mzee Bonaya ana miaka themanini na mitano. Katika umri huo wakati ambapo anapaswa kupumzika kusubiri siku zake za kuiahiri dunia, kikongwe huyo kila mara anahangaishwa na ukosefu wa usalama na mahali atakapolala usiku utakaofuata k wa sababu wastawishaji miradi wanachukua ardhi yake. Macho yake yaliyochujuka yamezama ndani ya kikombe cha macho na kuonekana kama matundu, lakini ukimtazama kwa makini, utaona ameyaelekeza kwenye ukuta wa matofali hata kupesa ni vigumu. Ukuta huo umezungukwa na huzuni nyingi. “Ükuta ule ambao umenizuia kufikia ardhi yangu ya ekari nne umekuwa jinamizi katika maisha yangu. Mnamo mwisho wa mwaka jana ardhi yangu ilitwaliwa kinyume cha sheria na msitawishaji miradi wa kibinafsi ambaye alivamia ardhi bila ya idhini yangu,” akaeleza Fatuma.

Kujenga nyumba “Nilitupwa nje ya nyumba yangu wakati walipokuwa wakiweka sengenge kuzunguka ardhi hiyo ambayo sasa wanadai wanaimiliki. Sikupewa nafasi yoyote ya kutoa kitu chochote kutoka kwenye nyumba yangu,”akaongeza. Kulingana na Fatuma ardhi inayohusika ilikuwa ya baba yake miaka mingi kabla Kenya kupata uhuru. Baada ya wazazi wake kufariki dunia, aliendelea kuishi katika shamba hilo akilinda raslimali iliyoko ndani ya shamba hilo ambalo limejaa minazi na miembe katika sehemu ya Bichanga tarafa ya Kisauni, Mombasa. “Mzozo huo wa ardhi ulisababisha kufukuliwa kwa maiti ya baba na wastawishaji miradi hao,”akalalama Fatuma huku akiongeza kwamba mstawishaji miradi huyo alifanya hivyo ili apate

kujenga nyumba kwenye sehemu hiyo ya kaburi. “Mnyakuzi huyo wa ardhi alitaka kunipa shilingi elfu hamsini kwa sehemu hiyo ya ardhi ya ekari nne akiniambia niende kununua ardhi mahali pengine, lakini nikakataa,” akasema Fatuma, huku akichungulia ndani ya shamba hilo kwenye tundu la ukuta wa matofali. Kama baba yangu na ndugu yangu wangalikuwa wako hai leo, nisingepitia masaibu haya . Nilikuwa nikilima mazao kama vile mihogo, mahindi, viazi tamu, na mboga , lakini sasa sina chakula wala nguo za kuvaa . Katika umri wangu siwezi kupigana kupata ardhi yangu,”akalalamika.

Dhuluma za ardhi Kisa cha Fatuma ni mfano mzuri wa dhuluma wanazopitia wanawake mikononi mwa wanaume ambao hudai ndio wamiliki halali wa ardhi. Wanawake wengi katika Mkoa wa Pwani wamejipata wakihamishwa kutoka makazi yao ya asili ya ardhi zao za jadi kwa madai kwamba hawana haki ya kumiliki ardhi na mali. Wakati mwingine hata hawafahamu kwamba wana haki ya kumiliki ardhi na kuwa na mali. Wakili mmoja wa Pwani, Samuel Ouma anasema katiba mpya haijafanikisha mengi kwa

“Nilitupwa nje nyumba yangu wakati walipokuja kuweka ua kwenye ardhi yangu na ambayo kwa sasa wanadai ni mali yao.” — Fatuma wa Mzee Bonaya

Ajuza Fatuma wa Mzee Bonaya akichungulia ukutani sehemu ya ardhi iliyokuwa awali mali yake lakini kwa sasa imenyakuliwa na mstawishaji fulani. Kulia, ajuza huyo amejishika tama asijue lakufanya. Picha: Emelda Rutendo

sababu bado inategemea utekelezaji wa maongozi ya kitaifa ya ardhi. “Sheria inayosimamia maongozi mapya ya ardhi haijatayarishwa vilivyo, lakini nina hakika kwamba wakati itakapotekelezwa tutapiga hatua kubwa katika kulinda haki za umilikaji wa ardhi,” akasema wakili huyo. Ouma anasema ni jambo jema kwamba wanawake wana haki sawa na wanaume na sasa wanaweza kumiliki ardhi kinyume cha katiba ya zamani. “Wanawake hawapaswi kunyimwa nafasi ya

kumiliki ardhi, kama watadhulumiwa na msitawishaji miradi yeyote, wana haki ya kushtaki hasa wakiwa na stakabadhi zifaazo kama ushahidi ya umilikaji wa ardhi,” akaeleza Wakili Ouma. Kimsingi ni kwamba hali halisi ya mambo ni tofauti kabisa kwani wanawake wengi wana uwezo haba katika kutoa maamuzi juu ya maswala ya ardhi na umilikaji wa mali nyinginezo. Fatuma sasa anatoa mwito kwa Serikali kuingilia kati na kumsaidia kupata ardhi ambayo ilikuwa mali yake.


12

Toleo Namba 20 • Agosti 2011

Vijana watafuta kuleta mapinduzi katika utaratibu wa uongozi

…Na Ruth Omukhango

K

wa miaka mingi vijana wamegandamizwa kwenye sekta za kisiasa na utoaji wa maamuzi licha ya kuwa sehemu muhimu katika sekta ya kiuchaguzi. Licha ya kuchukuliwa kuwa mhimili wa jamii na tumaini na kiendelezi cha tamaduni na thamani za kijamii hadi kwenye vizazi vijavyo, wamekuwa wakiishi katika dhana potofu ya kuwa viongozi wa kesho. Hata hivyo, kupitia katiba mpya vijana hawatafunikwa tena na msemo huo wa kale na badala yake watakuwa sehemu ya sekta ya kisiasa na ya utoaji maamuzi kama inavyohakikishwa kwenye vifungu tofauti vya katiba.

Sehemu ya tisini Kwa vifungu hivyo vya katiba huenda kukatokea mapinduzi makubwa kuhusiana na jinsi vijana wanavyochukuliwa. Viongozi hawataweza tena kuwatumia vijana hao kama magenge ya kuwashambulia wapinzani wa kisiasa na badala yake watawachukulia kuwa washirika katika jukwaa moja. Kwa mfano katika kifungu cha 97 (1) (b) katiba inasema hivi: “Bunge litakuwa na Wabunge kumi na wawili maalumu ambao watachaguliwa na vyama vya siasa bungeni kulingana na idadi ya Wabunge kila chama kilionao, kuambatana na sehemu ya 90 kuwakilisha makundi ya maslahi maalumu ikiwa ni pamoja na vijana, watu wenye ulemavu na wafanya kazi. Katika kifungu cha 98 (1) ( c) katiba inaeleza: “Baraza la Senate litakuwa na Wabunge wawili ambao watakuwa mwanamume mmoja na mwanamke moja, ambao watawawakilisha vijana.” Vijana ambao ni kundi la watu wa kuanzia umri wa miaka kumi na minane hadi miaka thelathini na mitano lenye kuwakilisha asilimia 75 ya idadi ya watu nchini ambao wanajipanga vilivyo kupitia miungano ya kimbinu ili kuunda mshikamano thabiti na kuleta athari kubwa zaidi kupitia uwakilishi wao katika uwanja wa kisiasa na kijamii. Moja ya makundi hayo ni kundi linalojulikana kama Langata Youth Network, kundi la kijamii la vijana wa kujitolea ambalo linawaleta pamoja vijana thelathini na watano viongozi wa makundi kumi ya kijamii kutoka eneo zima la kaunti ya Langata ambayo inachanganya maeneo ya Bunge ya Langata na Dagoretti. Likijulikana kwa jina maarufu la “Kisima cha akili na vipawa” wanachama cha kundi hilo, walikusanyika pamoja tangu kuzinduliwa rasmi kwa katiba mpya kutumia kwa ustadi manufaa ambayo yanapatikana ndani ya katiba mpya kuleta muungano miongoni mwa vijana kuwahimiza juu ya haki zao za kuanzia, kutekeleza, kuimarisha na kuendeleza maendeleo yao huko Kibera. Moja ya shabaha za kikundi hicho ni kuvunjilia mbali mpango wa

Hawa ni baadhi ya wanachama wa kundi la Lang’ata Youth Network wakitafakari juu ya jambo fulani linalowahusu. Vijana kwa sasa wanawahamasisha wenzao kuhusu manufaa ya katiba mpya. Picha: George Ngesa kutegemea michango ya usaidizi kutoka nje katika mtaa huo wa vibanda kwa kuhimiza na kuimarisha moyo wa kufanya kazi kwa bidii, uaminifu, uthabiti ambao utahakikisha hali bora ya uchumi wa kijamii kwao binafsi na kwa taifa zima na hali ya kisiasa kwa jumla. Wanadhamiria kupeperusha bendera ya uongozi kwa kuonyesha kwamba wanaweza kama vijana kupitia kuwahimiza vijana kujiunga na vyama vya kisiasa na kugombea viti vya kiuchaguzi katika ngazi zote. Vijana hao wanazidi kuungwa mkono kwa wanachama ambao wana maono ya kiuongozi na maarifa ili kugombea nyadhifa muhimu kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2012 . Wanachama wa kundi hilo kadhalika ni wawakilishi wa makundi mbali mbali ya vijana na ambao wamehitimu katika vyuo tofauti ikiwa ni pamoja na vyuo vikuu. Wana hamu na ustadi ambao umekitwa katika dhamira ya kuona jamii ambayo iko huru yenye kutoa nafasi sawa kwa wote na maendeleo kwa vijana wote. “Tunayo katiba sasa na kazi yetu ni kujitendea kazi, na kupitia hali hii tungependa kuona jamii ambayo haitegemei Serikali kutoa kila kitu kuwakimu na kuilaumu wakati mambo yanaposhindikana,” alisema Daniel Orogo, mwenyekiti wa kundi hilo. Alisema kwamba ingawa wingi wa uanachama wa chama hicho uko wazi kwa vijana wenye elimu ya taasisi na vyuo, kundi hilo linaendesha miradi ya ushauri kwa vijana walio katika shule za sekondari pamoja na warsha za kielimu katika baadhi ya shule.

Kwa sababu ya shughuli nyingi za wanachama, mikutano ya viongozi hao wa makundi ya vijana ya Langata (LYN) hufanywa siku za Jumamosi mchana kuanzia saa nane kwenye ofisi zao zilizoko katika shule ya St Cecilia Academy katika kijiji cha Kianda mtaa wa Kibera. Ada ya uanachama hi shilingi 250 ambazo hulipwa mara moja na ada ya shilingi 100 ambayo hulipwa kila mwezi. Faini ya shilingi 50 hutozwa wale ambao hukosa kufika mikutanoni au kwenda mikutanoni wakiwa wamechelewa.

Mwanzilishi Pesa hizo husaidia kugharamia shughuli za chama kama vile kulipa madeni kama vile kodi ya ofisi ambayo huilipa shule. Shughuli za kundi hilo zimekitwa katika vifungu vya katiba ikiwa ni pamoja na mswada wa haki na uongozi na uthabiti. Kulinganana kundi hilo katiba inawapa haki ya kudai kile kilicho chao kama raia, lakini pia wanatambua ya kwamba wanahitajika kuchukua jukumu wenyewe jambo ambalo linaanza na wao wenyewe. Kulinganana Winnie Obure, ambaye ni mwanachama mwanzilishi wa kundi hilo, na mwanzilishi wa kundi la Sebuleni katika mtaa wa Kibera, uongozi na uthabiti huanza na wanachama. Kundi hilo linadhamiria kuweka viwango ambavyo vitazalisha matunda, kwa kujenga na kuwafungulia milango vijana wa vizazi vipya ambavyo vitawajibika kwa vitendo vyao. Kundi hilo limechukua mfano wa kanuni za uongozi na uthabiti

kama inavyokokotezwa na katiba na kushirikisha misingi ya uteuzi wa uthabiti wa kibinafsi, uwezo na kufaa au uchaguzi wa haki na huru. Kwa kutambua manufaa kwa wanawake ndani ya katiba hasa kuhusu harakati za maslahi ya wanawake, kundi hilo linaandaa mikutano maalumu kwa wanawake kuwapa changamoto ya kutilia umuhimu kipengee cha thuluthi moja, lakini wangángánie viti vya mamlaka zaidi ili kuimarisha uwakilishi wao. “Tunapinga propaganda kwamba wanawake watosheke na thuluthi moja kwa sababu tunataka kuona wanawake zaidi wakiwakilisha sekta zote za utoaji maamuzi ili wawe na nguvu za kutosha,”akasema Winnie. “Kulingana na kifungo cha 55 cha Mswada wa Haki, Serikali itachukua hatua, ikiwa ni harakati za maslahi ya wanawake kuhakikisha kwamba vijana wanapata elimu inayofaa na mafunzo, kuwa na nafasi ya tangamano, wawakilishwe na kushiriki katika sekta za siasa,uchumi wa kijamii na sekta nyinginezo za kimaisha, kupata nafasi za kazi, na kulindwa dhidi ya vitendo vya kitamaduni vyenye kuleta madhara na kunyanyaswa.” Shughuli za kundi hilo ni pamoja na kauandaa mikutano kwa vijana kuwaelimisha kuhusu haki zao za kikatiba, kupewa uwezo kiuchumi kupata mikopo kupitia ushirikiano katika Benki ya Equity. Tangu kuanzishwa kwake wanachama wanaweza kushuhudia kwamba baada ya mwaka mmoja jitihada zao zimezaa matunda na kuwapa matumaini ya maisha ya siku za usoni.

“Huwa tunaendesha vipindi vitatu kila wiki katika kituo chetu cha Pamoja FM ili kuhamasisha vijana kuhusu mambo kadha wa kadha na hasa lengo pia likiwa ni kuwataka kuchukua uongozi siku za usoni.” — Daniel Orogo

Chama cha LYN kimeshirikiana na mashirika maarufu nje na ndani ya eneo bunge la Langata kama vile Kituo cha Sheria, Youth Platform for Change, Youth for Kenya, Project Amani, CREAW na Inuka Trust. Kundi hilo limeandaa mikutano ya kuwaelimisha jamii kuhusu haki zao za uchumi wa kijamii kama inavyosema katiba. Baadhi ya haki hizo ni kupata huduma za kijamii ambazo ni pamoja na huduma za afya, elimu, haki ya wanawake ya kumiliki mali na kurithi pamoja na usalama wa kijamii kwa watu wazima katika jamii. Kutokana na kushirikiana na mashirika mengine kama vile Inuka Trust, kundi hilo limefanikiwa kushirikiana na Kliniki ya Bomu katika mtaa wa Changamwe mjini Mombasa kuanzisha kituo cha matibabu katika mtaa wa Soweto, ambao ni moja ya vijiji vya Kibera ambacho wanatumai kitaanza kazi mwakani.

Vyombo vya habari Kwa chama cha LYN ushirikiano na vyombo vya hanbari ni muhimu. Kundi hilo limetumia vituo vya matangazo vya hapa nchini ambavyo ni pamoja na Pamoja FM kutangaza vipindi vyake ambavyo vinawahamasisha vijana kuhusu majukumu na haki zao katika jamii. “Tunaendesha vipindi hivi kila wiki katika radio ya Pamoja FM kuwahamasisha vijana kuhusu maswala mbali mbali ya leo huku uzito ukitiliwa katika swala la uthabiti na kutwaa nyadhifa za uongozi katika ngazi zote,” akakariri. Chama hicho kadhalika kimehusika kwenye harakati za kuleta amani huku wakitilia mkazo vijana kudumisha amani kwa sababu pasi na utulivu hakuwezi kuwa na uongozi. Wanatumia kila nafasi inayopatikana kama vile kufanya usafi na shughuli za michezo.

Mkurugenzi Mkuu: Rosemary Okello-Orlale Mhariri Mkurugenzi: Arthur Okwemba Mhariri Msimamizi: Jane Godia Wahariri Wasaidizi: Bob Okoth, Gunga Chea Waandishi: Mwanamke Mkenya ni toleo la African Woman and Child Feature Service Wapambe: Email: info@awcfs.org www.awcfs.org

Joyce Chimbi, Faith Muiruri, Duncan Mboyah, Omwa Ombara, Florence Sipalla, Ben Oroko, Ruth Omukhango, Adow Ina Kalil, Issa Haroun, Odhiambo Orlale, Fibi David, George Omonso, Emeldah Rutendo Bernadette Muliru na Noel Lumbama, (Noel Creative Media Ltd)

Jarida hili limechapishwa kutokana na usaidizi wa Hazina la Kidemokrasia la Umoja wa Mataifa (UNDEF)


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.