AHLULBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Page 1

AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI ‫أهل البيت عليهم السالم‬

Kwa mujibu wa Tabari, Tha’labi, Baghawi, Raazi, Zamakhshari, Baydhawi, Qurtubi, Ibn Kathir, Suyuti, Burusawi, Alusi na Qasimi.

Kimeandikwa na: Sheikh Nizar al-Hasan

Kimetarjumiwa na: Ustadh Haj. Hemedi Lubumba

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 1

2/14/2018 12:11:25 PM


AHLUBAYT 14_February_2018.indd 2

2/14/2018 12:11:25 PM


© Haki ya kunakili imehifadhiwa na: AL-ITRAH FOUNDATION ISBN: 978 - 9987 - 17 - 101 - 9 Kimeandikwa na: Sheikh Nizar al - Hasan Kimetarjumiwa na: Ustadh Haj. Hemedi Lubumba Kupangwa katika Kompyuta na: Al-Itrah Foundation Toleo la kwanza: Oktoba, 2018 Nakala: 1000 Kimetolewa na kuchapishwa na: Alitrah Foundation S.L.P. 19701 Dar es Salaam, Tanzania Simu: +255 22 2110640 / 2127555 Barua Pepe: alitrah@yahoo.com Tovuti: www.ibn-tv-com Vitabu mtandaoni: www.alitrah.info/ebooks/ ILI KUSOMA QUR’ANI MUBASHARA KWA NJIA YA MTANDAO, TEMBELEA www.somaquran.com

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 3

2/14/2018 12:11:25 PM


YALIYOMO Utangulizi................................................................................................... 5 SEHEMUYA KWANZA Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Tabari, inayoitwa Jamiul - Bayan Amtaawiil Ayil-Qur’an................................................... 11 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsiri ya At-Thaalabiy, inayoitwa Al-Kashfu Wal-Bayan Fii Tafsiril-Qur’ani............................. 46 SEHEMU YA PILI Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Al-Baghawi, inayoitwa Maalimut-Tanziil................................................................... 104 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Zamakhshari, inayoitwa Al-Kashafu Fii haqaiqit-Taawiil............................................ 124 Ahlul - Bayt (a.s.) ndani ya Tafsir ya Razi, inayoitwa At - tafsirul Alkabir au Mafatihul Ghaybi.............................................. 137 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsiri ya Al-Baydhawi, inayoitwa Anwarut Tanziil Waaasratut-Taawil....................................................... 158 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsiri ya al-Qurtubi, inayoitwa Al-Jamiuliahkamil - Qur’ani.................................................................. 166 SEHEMU YA TATU Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Ibnu Kathir, Inayoitwa Tafsirul-Qur’an Al-Adhim.................................................... 207 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsiri ya Suyuti, Inayoitwa Ad-Durul-Manthur Fit Tafsir al-Maathur.............................. 238 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Burusawi, Inayoitwa Tafsir Ruhul-Bayan Fi Tafsiril-Qur’an................................. 292 Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Alusi, inayoitwa Ruhul - Ma’aniy Fit-Tafsiril Qur’an Al-Adhim Wasab’ul-Mathaniy................................................................................ 319

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 4

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

NENO LA MCHAPISHAJI

K

itabu kilichoko mikononi mwako ni tarjuma ya kitabu cha Kiarabu kiitwacho, Ahlu ‘l-Bayti Fi Tafasiri Ahli ‘s-Sunnah kilichoandikwa na Sheikh Nizar Hasan. Sisi tumekiita, ­Ahlul Bayt Ndani ya Tafsiri za Kisunni. Hii ni tafsiri za wanavyuoni wakubwa wa Kisunni – Tabari, Tha’labi, Baghawi, Raazi, ­Zamakhshari, ­Baydhawi, Qurtubi, Ibn Kathir, Suyuti, Burusawi, Alusi na Qasimi.

Ahlul Bayt, yaani Watu wa Nyumba ya Mtume Muhammad SAW ni viongozi ambao Mtume alituusia tuwafuate. Katika ­hotuba yake ndefu na maarufu aliyoitoa pale Ghadir Khumm katika msafara wake wa kurejea kutoka Hija yake ya mwisho, Mtukufu Mtume SAW alisema haya mbele ya masahaba na mahujaji zaidi ya laki moja: “...Nakuachieni vitu viwili vizito: Qur’ani na Ahlul Bayt wangu. ­Viwili hivyo havitaachana mpaka vinifikie katika [hodhi ya] Kawthar. Nawausia juu ya Ahlul Bayt wangu! ­Angalieni jinsi mtakavyojihusisha nao. Kama mkishikamana na viwili hivi hamtapotea kamwe...” (kwa maelezo zaidi soma kitabu cha ­al-Ghadir) Lakini bahati mbaya sana sio Waislamu wote wanaowafuata Ahlul Bayt AS pamoja na kwamba wanavyuoni wa madhehebu zote wameandika habari zao katika vitabu vyao na kuonesha kwamba hawa ni viongozi wa Umma huu wa Kiislamu. Mwandishi wa kitabu hiki anajaribu kuthibitisha hilo kwa kutoa rejea mbalimbali kutoka katika vitabu maarufu vya wanavyuoni wa ­Kisunni. 1

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 1

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ni muhimu kukubaliana na kuziheshimu tofauti za kila mmoja na kutambua msimamo na mtazamo wa kila mmoja. Matatizo huja pale mtu anapolazimisha tabia, imani na mila zake zitawale wengine au kuzifisha itikadi na misimamo ya wengine. Ni muhimu kufikiria kila aina ya maoni katika kujaribu kuamua ukweli. Uislamu ­kimsingi uko dhidi ya kufuata kibubusa. Wafuasi wa madhehebu nyingine wanaweza kuchambua uthibiti wa kitabu hiki ili kujenga maoni yao wenyewe kuhusu mtazamo mzuri wa mtu mwenyewe. Ni muhimu mtu kuelewa hoja za wale ambao hakubaliani nao. Inaweza ikasemwa kwamba wale ambao hawaelewi kabisa mtazamo wa maoni tofauti, hawaelewi kwa ukamilifu mtazamo wa kwao wenyewe. Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote, ambapo uwongo, ngano za kale na upotoshaji wa historia ni mambo ambayo hayana nafasi tena katika akili za watu. Kutokana na ukweli huo, Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation imeamua kuchapisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili kwa ­madhumuni yake yaleyale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili. Tunamshukuru ndugu yetu, Ustadh Hemedi Lubumba kwa ­kukubali jukumu hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwake. Ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitakuwa ni changamoto kubwa kwa wasomaji wetu. Mchapishaji: Al-Itrah Foundation 2

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 2

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

NENO LA JUMUIYA

H

akika mirathi ya Ahlul-Bait ambayo imehifadhiwa na kambi yao na wafuasi wao dhidi ya upotovu inaonyesha ni kambi ­iliyokusanya aina mbalimbali za taaluma za kiislamu. Kambi hii imeweza kulea nafsi mbalimbali zilizo tayari kunywa kutoka kwenye chemchem hiyo, na kuupa umma wa kiislamu wanavyuoni wakubwa wenye kufuata nyayo za ujumbe wa Ahlul-Bait. Wanavyuoni waliokusanya vidodosa na maswali mbalimbali ya madhehebu na mitazamo tofauti ya kifikira kuanzia ndani ya desturi ya kiisilamu hadi nje ya desturi hiyo, huku wao wakitoa majibu na utatuzi makini juu ya maswali hayo ndani ya karne zote. Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bait imefanya hima kutetea tukufu za ujumbe wa Uislamu na ukweli wake ambao umechafuliwa na makundi, madhehebu na wanaharakati mbalimbali wenye chuki na Uislamu. Jumuiya imefuata nyayo za Ahlul-Bait na za wafuasi wa kambi yao njema ambayo imefanya hima kujibu madai yenye kuendelea na daima ikajaribu kubaki ndani ya msitari wa mapambano kwa kiwango kinachohitajika ndani ya kila zama. Hakika uzoefu ambao umehifadhiwa ndani ya vitabu vya wanavyuoni wa kambi ya Ahlul-Bait katika dhamira hii ni wa aina ya pekee, kwa sababu una akiba ya kielimu inayotegemea akili na hoja, huku ukijiepusha na matamanio na upendeleo uliokatazwa. Unazungumza na wasomi na wanafikra wenye fani maalumu, mazungumzo ambayo yanakubalika kiakili na yanapokewa na maumbile yaliyo salama. 3

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 3

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Jaribio hili la Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bait limekuja kuwapa watafuta ukweli hatua mpya ya uzoefu wa thamani kupitia mada na vitabu vinavyoandikwa na waandishi wa zama hizi ambao ni wafuasi wa madhehebu ya Ahlul-Baiti (a.s.) au miongoni mwa wale ambao Mwenyezi Mungu amewapa neema ya kujiunga na kambi hii tukufu. Achia mbali kwamba jumuia hii pia hujishughulisha na uchapishaji na uhakiki wa yale yenye faida toka katika vitabu vya ulamaa wa zamani wa kishia, ili vitabu hivi viwe maji matamu kwa nafsi zenye kuitafuta haki, ili ziweze kufikia kwenye haki ambayo inatolewa na Kambi ya Ahlul-Bayt ulimwengu mzima, ndani ya zama ambazo akili inaerevuka na nafsi na roho zinaboreka kwa kasi ya pekee. Tunatoa shukurani njema kwa Samahatu Sheikh Nazar Hasan kwa kuandika kwake kitabu hiki, na kwa ndugu zetu wote waliosaidia kukichapisha. Na sote tunategemea na kutaraji kuwa tutakuwa tumetoa kile tulichokiweza katika juhudi za kutekeleza baadhi ya wajibu tulionao mbele ya ujumbe wa Mtukufu Mola wetu Mlezi ambaye alimtuma Mtume Wake na uongofu na dini ya haki ili aipe ushindi dhidi ya dini zote. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi. Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bait Kitengo cha Utamaduni

4

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 4

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

UTANGULIZI

K

ila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote. Rehema na amani zimwendee Mtume Muhammad, yeye na aali zake watoharifu. Na daima laana iwe juu ya wote walio maadui zao na wakanushaji wa fadhila zao. Qur’ani iliteremkia katika nyumba tohara na safi, ­ambazo ­imeidhinishwa zitukuzwe, katika nyumba za aali Muhammad ­watoharifu, ambazo Mwenyezi Mungu Mtukufu amezifanya ­makhsusi kwa ajili ya heshima na utukufu kuliko nyingine, na ­Mwenyezi Mungu akazighani (nyumba hizo) kupitia Aya za Qur’ani tukufu ambazo zitaendelea kubaki muda wa dahari yote zikisomwa usiku na mchana, na si nyumba za viumbe vingine. Kwa ajili hiyo tunawaona (a.s.) wao ndio watambuzi na wajuzi wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu kuliko wengine wote, na kwa ajili hiyo tunamwona Amirul-Muuminina (a.s.) Ali bin Abu Talib (a.s.) akisema: “Lau nikitandikiwa mto kisha nikaketi juu yake nitahukumu baina ya wanataurati kwa Taurati yao na wanainjili kwa Injili yao, na baina ya wanazaburi kwa Zaburi yao na wanafurqan kwa Furqani yao. Wallahi hakuna Aya yoyote iliyoteremshwa bara au baharini, katika tambarare au jabali, mbinguni au ardhini, usiku au mchana, ila mimi namjua ni nani iliteremka kwa ajili yake, na iliteremka kuhusu nini.”1

Abu Naiim ameandika katika kitabu Hilyatul-Awliyai kutoka kwa Imam Ali (a.s.) kwamba alisema: “Wallahi hakuna Aya iliyoteremka ila najua iliteremka kwa ajili ya nani, na wapi iliteremka, na hakika Mola wangu Mlezi amenitunukia moyo wenye akili na ulimi wenye kudadisi.”   Matwalibus-Suul, cha Ibnu Talha as-Shafiiyu Juz. 1, Uk. 125, chapa ya Taasisi ya Ummul-Qura.

1.

5

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 5

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Na pia Abu Naiim ameandika katika kitabu Hilyatul-Awliyai ­kutoka kwa Ibnu Masuud, amesema: “Hakika Qur’ani iliteremshwa kwa herufi saba, hakuna herufi yoyote ila ina dhahiri na batini, na hakika Ali bin Abu Talib ndiye mwenye dhahiri na batini.” Na kuna kauli moja inanasibishwa na Amirul-Muuminina (a.s.): “Lau nikitaka kuwapigisha magoti ngamia arubaini kwa tafsiri ya Qur’ani ninaweza.” Kisha wao ndio wafasiri wa wahyi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, wenza wa Kitabu chake na Kitabu kitamkacho, haya ndio yathibitishwayo na Hadithi ya Vizito viwili: “Mimi ni mwenye kuacha kati yenu vizito viwili: Cha kwanza ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu, humo mna uongofu na nuru…., na Ahlul-Baiti wangu, nawakumbusheni Mwenyezi Mungu kuhusu Ahlul-Baiti wangu, nawakumbusheni Mwenyezi Mungu kuhusu Ahlul-Baiti wangu.”2 Hivyo wao ndio wabainishaji, wafafanuzi na wafasiri wa misamiati ya Qur’ani Adhimu. Kwa sababu Kitabu cha Mwenyezi Mungu kina haja ya kupata mfasiri, mfafanuzi na mfasiri, hivyo ni aula kifani chake na mwenza wake ndiye mbainishaji, mfasiri, alimu na mjuzi wa Kitabu hicho na si mwingine. Kwa ibara nyingine tunaweza kusema: Hakika Ahlul-Baiti (a.s.) ndio waliokusudiwa, kuainishwa na kuashiriwa katika semi zake (s.w.t.). Bali ni katika nyumba zao ndimo kulimoteremka Kitabu, na wenye nyumba ndio wajuzi zaidi wa yale yaliyomo ndani ya ­nyumba yao. Kuanzia hapa tunawakuta Ahlul-Baiti (a.s.) siku zote wakiifasiri Qur’ani na Maneno ya Mwenyezi Mungu vizuri zaidi na kwa ­ukamilifu mno. Na watu wote wakirejea kwao bila kumtenga yoyote, na wala hatujaona tukio lililo kinyume na hali hiyo, hata Ibnu Abbas ambaye ni kinara na kiongozi wa wafasiri miongoni mwa sahaba yeye   Sahih Muslim, Juz. 4, Hadithi ya 1873.

2.

6

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 6

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

naye alikuwa ni mwanafunzi wa Ali (a.s.), yeye mwenyewe anasema: “Tafsiri ya Qur’ani niliyonayo ni kutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.).” Hapo hapo tunawaona ulamaa wa makundi mawili, Shia na Sunni wameifasiri Qur’ani Tukufu kupitia riwaya na nukuu, kama vile Tafsiri ya Ali bin Ibrahim al-Qummiy, Tafsirul-Ayyashiy na Furatil-Kufiy, Kanzud-Daqaiq ya Ibnu al-Mash’hadiy, al-Burhan ya Sayyid Hashim al-Bahraniy, Nurut-Thaqalayn ya Sheikh Abdu Ali al-Hawiziy, na wengineo miongoni mwa Maimamiya ambao wameifasiri Qur’ani kupitia Ahlul-Baiti (a.s.). Na miongoni mwa Masunni ni kama vile al-Haskaniy katika Shawahidut-Tanziil, Isfihaniy katika an-Nuru al-Mushtaalu na al-Wahidiy katika Asbabun-Nuzuul. Pia zipo tafsiri zilizozagaa huku na huko ambazo zinategemewa na Sunni katika utafiti na mchakato wa kielimu. Tafsiri hizi zimefasiri baadhi ya Aya tukufu kwamba walengwa halisi wa Aya hizo ni aali Muhammad (a.s.), hivyo tumejaribu kuzikusanya na kuziweka pamoja Aya hizi toka katika kabati za vitabu vya tafsiri muhimu zenye kutegemewa kwao. Miongoni mwazo ni: Jamiul-Bayan Fii Tafsiril-Qur’ani ya Abu Ja’far Muhammad bin Jarir bin Yazid bin Kathiir bin Ghalib at-Tabari, aliyefariki mwaka 310 A.H. Nasi hapa tumetegemea chapa ya Misri yenye juzuu 30. al-Kashfu wal-Bayan Antafsiril-Qur’ani ya Abu Is’haqa Ahmad ibnu Ibrahim at-Thaalabiy an-Nisaburiy al-Muqriu, aliyefariki mwaka 427 A.H. Maalimut-Tanziil ya Abu Muhammad Husain bin Masuud bin Muhammad, maarufu kwa jina la Farrau al-Baghawi as-Shafiy, aliyefariki mwaka 516 A.H. Nasi hapa tumetegemea chapa ya Beirut ambayo ina Juzuu 4. al-Kashaf Anihaqaiqit-Tanziil Wauyuunil-Aqawiil Fii WujuhitTaawiil ya Abu Qasim Mahmudu bin Umar bin Muhammad bin Umar al-Khawarazimiy al-Hanafiy al-Muutazaliy az-Zamakh7

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 7

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

shariy, mwenye lakabu ya Jarullah, aliyefariki mwaka 538 A.H. Nasi hapa tumetegemea chapa ya Misri ya mwaka 1948 A.D. Mafatihul-Ghaybi ya Abu Abdillah Muhammad bin Umar bin Husain bin Hasan bin Ali at-Tamimiy al-Bakriy at-Tarstaniy ­ar-Razi, mwenye lakabu ya Fakhrud-Din, maarufu kwa jina la Ibnul-Khatib as-Shafiy, aliyefariki mwaka 606 A.H. An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil ya Kadhi Mkuu NasrudDin (Abul-Khayri), Abdullah bin Umar bin Muhammad bin Ali ­al-Baydhawi as-Shafiy, aliyefariki mwaka 691 A.H. iliyo katika ­juzuu mbili, iliyochapishwa Misri mwaka 1968 A.D. al-Jamiu Liahkamil-Qur’ani ya Abu Abdillah Muhammad bin Ahmad bin Abubakri al-Ansariy al-Khazrajiy al-Undlusiy ­al-Qurtubiy, aliyefariki mwaka 761 A.H. iliyo katika juzuu ishirini, ­iliyochapishwa Misri mwaka 1950 A.D. Tafsirul-Qur’ani al-Adhiim ya Hafidh Imadud-Din (Abul-Fidai), Ismail bin Amru bin Kathiir bin Dhaw’u bin Kathiir bin Zar’i ­al-Baswriy ad-Damashqiy, Ibnu Kathiir, aliyefariki mwaka 774 A.H. iliyo katika juzuu tano, iliyochapishwa Beirut. ad-Duru al-Manthur Fii Tafsiri Bil-Maathur ya Hafidh Jalalud-Din (Abul-Fadhli), Abdurahman bin Abubakri bin Muhammad as-Suyuti, aliyefariki mwaka 911 A.H. iliyo katika juzuu nne, iliyochapishwa Misri. Ruhul-Bayan ya Allamah Sheikh Ismail Haqiyyu al-Barsiyyu, aliyefariki mwaka 1137 A.H. iliyo katika juzuu thelathini, nasi hapa tumetegemea chapa ya Uthmaniya ya mwaka 1330 A.H. Ruhul-Maaniy ya Allamah Abul-Fadhli Shihabud-Din, Sayyid Muhammad Al-Alusiy, aliyefariki mwaka 1270 A.H., iliyo katika juzuu thelathini, nasi hapa tumetegemea chapa ya Misri ambayo ilipigwa chapa na Al-Muniriyah mwaka 1345 A.H. 8

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 8

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Tafsirul-Qummiy, maarufu kwa jina la Mahasinut-Taawiili ya Allamah as-Sham Muhammad bin Jamalud-Din al-Qasimiy, aliyefariki mwaka 1322 A.H., iliyo katika juzuu kumi na saba, nasi hapa tumetegemea chapa ya Beirut ya Ihyaut-Turathil-Arabiy ya mwaka 1415 AH. Tafsiri hizi zimepangwa kulingana na kipaumbele na umuhimu. Hivyo kutokana na wajibu wa kiitikadi na jukumu la kisheria, pia kutokana na kuwepo mapungufu ambayo ni lazima tuyazibe kwa kile kinachonasibiana na ukubwa wa mahitaji ya upungufu huo, na ili kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu Ambaye mara kwa mara ametangaza katika Qur’ani wito wa kuwapenda aali Muhammad (a.s.) aliposema: “Sema: Kwa haya siombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa kizazi changu” (Qur’ani Tukufu Sura Ash-Shura 42:23) tumefanya kazi hii iliyobarikiwa ambayo inamimina maji kutoka katika bahari ya aali Muhammad (a.s.) ­iliyojaa na yenye kububujika. Na ni kutokana pia na umuhimu wa kazi hii katika kuthibitisha maarifa na nafasi ya Ahlul-Baiti (a.s.), ili uthibitisho huo uwe hoja yenye nguvu, na hapo utimie msemo “Nafuata kinywa chako.” Pia ni ili kuthibitisha kwamba wao ndio walioainishwa na kukusudiwa na Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kazi hii imeendelea toka siku ya kumi na nane ya mfunguo pili mwaka 1420 A.H. mpaka siku ya ishirini na tatu ya mfunguo tatu mwaka 1426 A.H., lakini kazi hii ilikumbwa na matatizo mengi ikiwa ni pamoja na hali kutotulia, kutopatikana rejea, na nyudhuru nyingine mfano wa hizo. Pamoja na hayo yote tulivumilia kwa kalamu ya mahaba na upendo wetu kwa wateule Ahlul-Baiti (a.s.) nyudhuru zote zilizotukabili, tukazama katika kina cha tafsiri na wafasiri ili tutoe humo johari na vito vya aali Muhammad (a.s.) baada ya kuwa 9

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 9

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

vimefichwa na kufunikwa na vumbi la historia kwa sababu za siasa ya kidunia. Pia katika ziara yetu ya kitafsiri tumezitambua nafsi za wafasiri, hivyo tumegundua kwamba Ibnu Kathir ndiye mwenye maradhi makubwa ya nafsi na ndiye mwenye chuki kubwa dhidi ya AhlulBaiti (a.s.) na wafuasi wao wema. At-Thaalabiy ndiye mwadilifu na mwenye insafu kuliko wengine. Utafiti huu tuliuwakilisha kwenye kongamano la mwaka la Sheikh Tusiy ambalo lilifanyika katika Jamhuri ya Kiislam ya Iran katika Jiji la Qum Takatifu, mwaka 1426 A.H. hatimaye ukapata tuzo katika kongamano hilo adhimu. Haya yote ni sehemu ya fadhila za Mola wangu na neema kutoka Kwake (s.w.t.), na ni sehemu ya msaada toka katika roho toharifu (a.s.), kwa sababu kazi hii ni kwa ajili yao na si kwa ajili ya mwingine. Mwisho tunainua mikono yote kutoa shukurani kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, tunamwomba maghufira dhidi ya utelezo na makosa yaliyotoka kwetu, kwa sababu umaasumu ni wa wenye nao. Pia tunamtaka msamaha msomaji mpendwa kutokana na makosa yasiyo ya kukusudiwa atakayoyakuta humu. Na kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe wote. Nizar Hasan 2 Mfunguo Nne 1427 Hijiria. Qum Takatifu

10

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 10

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA TABARI, INAYOITWA JAMIUL-BAYAN ANITAAWIIL AYIL-QUR’ANI SURA AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na watoto wa Ibrahim na watoto wa Imran juu ya walimwengu wote.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:33).

Al-Muthana amenisimulia, amesema: “Abdullah bin Salih ­ametusimulia, amesema: Muawiya amenisimulia kutoka kwa Ali, kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na watoto wa Ibrahim na watoto wa Imran juu ya walimwengu wote.” (Sura Aali Imran; 3:33), amesema: ‘Hao ni waumini toka aali Ibrahim, aali Imran, aali Yasini na aali Muhammad (s.a.w.w.).”3 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

3.

afsirut-Tabariy Juz. 3, Uk. 234. Inadhihiri toka katika baadhi ya tafsiri kama Tafsiri T ­Al-Khazin, Durul-Manthuur na Shawahidut-Tanziil kwamba Aali Yasin ndio hao hao Aali Muhammad (s.a.w.w.). 11

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 11

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ­ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:42).

Bushru ametusimulia, amesema: Ametusimulia Yazid, amesema: Said ametusimulia kutoka kwa Qatadah kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na Malaika waliposema: Ewe Maryam!” kwamba tumeambiwa kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akisema: “Yakutosha juu ya wanawake wa ulimwenguni: Maryam binti Imran, mke wa Firaun, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.”4 Nimesimuliwa kutoka kwa Ammar, amesema: Ametusimulia Ibnu Abi Ja’far kutoka kwa baba yake kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na Malaika waliposema...”, akasema: “Thabitu al-Bunaniy alikuwa akisimulia kutoka kwa Anas bin Malik kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: ‘Kati ya wanawake wa ulimwenguni wabora ni wanne: Maryam binti Imran, Asia binti Muzahim mke wa Firaun, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.”’ Amesema: Ametusimulia Adam al-Asqalani, amesema: Shaabah ametusimulia, amesema: Ametusimulia Amru bin Murrah, amesema: Nilimsikia Murrah al-Hamdani akisimulia kutoka kwa Abu Musa alAsh’ariy kwamba amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Kati ya wanaume wamekamilika wengi, na kati ya wanawake hawajakamilika ila Maryam, Asia mke wa Firaun, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.” Amesema: Ametusimulia Abul-As’wad al-Misriy, amesema: Ametusimulia Ibnu Twiat kutoka kwa Umarat bin Ghazyat, kutoka kwa Muhammad bin Abdurahman bin Amru bin Uthman, kwamba alisimuliwa na Fatima binti Husein bin Ali kwamba: Fatima binti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Siku moja Mtume   Tafsirut-Tabari, Juz. 3, Uk. 263.

4.

12

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 12

2/14/2018 12:11:26 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliingia kwa Aisha nami nikiwa humo, akaninong’oneza nami nikalia, kisha akaninong’oneza tena nami nikacheka, Aisha akaniuliza kuhusu hali hiyo, nikamwambia: ‘Bila shaka umefanya haraka hivi kweli nikupe siri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu?’ akaniacha. “ Alipofariki Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) Bibi. ­ isha alimuuliza, naye akamjibu: Ndio alininong’oneza akaseA ma: “Jibril alikuwa akiipitia Qur’ani kila mwaka mara moja, na hakika mwaka huu kaipitia Qur’ani mara mbili, na hakika hakuna Nabii yeyote ila alipewa nusu ya umri wa Nabii aliyekuwa kabla yake, na hakika ndugu yangu Isa umri wake ulikuwa miaka mia moja na ishirini, nami hivi sasa nina miaka sitini, nami ni mwenye ­kufariki ndani ya mwaka huu, na hajapata mwanamke yeyote kati ya wanawake wa ulimwenguni kufikwa na msiba mfano wa ule utakaokufika, wala usiwe mwanamke usiye na subira” ndipo nikalia, kisha akasema (s.a.w.w.): “Hakika wewe ni mbora wa wanawake wa peponi.”5 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsirut-Tabari Juz. 3 Uk. 264. Vipi Fatima asiwe mbora wa wanawake wa peponi na hali yeye ndiye kiumbe mtukufu na mkweli kuliko wao. Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alisema kuhusu haki yake kama ilivyo katika kitabu Bukhari Juz. 2 Uk. 185: “Fatima ni sehemu ya nyama yangu…”, na bila shaka ni kwamba Mtume ndiye mbora katika nyumba zote mbili (Dunia na Akhera) na Fatima ni kipande na sehemu ya baba yake, hivyo ni lazima Fatima awe mbora wa wanawake wa ulimwenguni katika nyumba zote mbili (Dunia na Akhera).

5.

13

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 13

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Ametusimulia Ibnu Hamid, amesema: Ametusimulia Jariri kutoka kwa Mughira, kutoka kwa Amir, amesema: “Akaamrishwa, yaani Mtume (s.a.w.w.) kuombeana laana na watu wa Najran kwa kauli yake (s.w.t.): “Na watakaokuhoji…”, hivyo (watu wa Najran) wakaahidiana wamwombee laana na wakamuahidi iwe ni siku ya kesho, ndipo wakaenda kwa Sayyid Askofu, naye alikuwa ndiye mwenye akili kuliko wao hivyo wakamfuata, wakaenda kwa mtu mwenye akili miongoni mwao, wakamweleza yale waliyokubaliana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), akawaambia: “Mmefanya nini?” akawalaumu na kuwaambia: “Ikiwa kweli ni Mtume kisha akiwaombea mabaya katu Mwenyezi Mungu hatomghadhibisha kati yenu. Na ikiwa ni Mfalme akiwashinda katu hatowabakisheni.” Wakasema: Tutafanya nini nasi tayari tumeshamwahidi? Basi walipokwenda Mtume alikwenda na hali amemkumbatia Hasan na amemshika mkono Husein na Fatima akitembea nyuma yake, akawaita, wakasema: Tunajikinga kwa Mwenyezi Mungu. Kisha akawaita tena, wakasema: Mara zote tunajikinga kwa Mwenyezi Mungu. Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Ingieni katika Uislamu mtapata haki waliyo nayo waislamu, na mtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwa waislamu….”6 Ametusimulia Ibnu Hamid: Ametusimulia Isa bin Farqad kutoka kwa Abul-Jarud, kutoka kwa Zayd bin Ali kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu…” amesema: “Walikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, Ali, Fatima, Hasan na Husein.”7   Tafsirut-Tabari, Juz. 3, Uk. 299. al-Haskaniy ameiandika katika Shawahidut-Tanziil Juz. 1 Uk. 120, chapa ya Beirut. 7.   Tafsirut-Tabari Juz. 3 Uk. 300. 6.

14

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 14

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ametusimulia Muhammad bin Husein, amesema: Ametusimulia Ahmad bin al-Mufadhil, amesema: Kutoka kwa as-Sadiy kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii…”, Mtume (s.a.w.w.) aliwashika mkono Hasan, Husein na Fatima, akamwambia Ali tufuate, akatoka pamoja nao, siku hiyo hakuna nasara yeyote aliyejitokeza, Mtume akasema: “Lau wangejitokeza basi wangeteketea.”8 Yunus amenisimulia, amesema: Ibnu Wahbi ametupa habari, amesema: Ametusimulia Ibnu Zayd, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliambiwa: “Lau ungewalaani kaumu ungekuja na nani uliposema: “…watoto wetu na watoto wenu…”? Akasema (s.a.w.w.): “Hasan na Husein.”9 Muhammad bin Sanan amenisimulia, amesema: Ametusimulia Abu Bakr al-Hanafiy, amesema: Ametusimulia al-Mundhir bin Thaalabah, amesema: Ametusimulia Ulbau bin Ahmar al-Yashkriy, amesema: Ilipoteremka Aya hii: “Waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu…” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alituma waitwe Ali, Fatima, na watoto wao wawili Hasan na Husein, kisha akawaita wakristo ili waombeane laana. Kijana miongoni mwa Mayahudi akasema: “Ole wenu! Si waliwausieni jana ndugu zenu ambao waligeuzwa nyani na nguruwe kwamba msishiriki maapizo.” Wakaacha.10 Ametusimulia Hasan bin Yahya, amesema: Abdurazaq ametupa habari, amesema: Maamar ametupa habari kutoka kwa Qatadah kuhusu kauli Yake (s.w.t.): “Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii…”, amesema: Mtume (s.a.w.w.) alipowakusudia watu wa Najran alimshika mkono Hasan na Husain, akamwambia Fatima tufuate, maadui wa Mwenyezi Mungu walipoona mwonekano huo wakarejea.11   Tafsirut-Tabari, Juz. 3, Uk. 300.   Tafsirut-Tabari Juz. 3 Uk. 301. 10.   Tafsirut-Tabari Juz. 3 Uk. 301. 11.   Tafsirut-Tabari Juz. 3, Uk. 301. Tunapata nukta zifuatazo kama faida kutoka katika Aya ya Maapizano: 8. 9.

15

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 15

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na hakika Mwenyezi Mungu aliwatimizia miadi yake….” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:152). Ametusimulia Muhammad, amesema: Ametusimulia As’bat ­kutoka kwa as-Sadiy, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu ­alipotokeza kwa mushrikina huko Uhud aliwaamuru askari wa mishale wakakaa juu ya mlima wakiwa wamezielekea ngamia za mushrikina, akasema: “Msitoke mlipo..” na akamfanya Abdullah bin Jubair kuwa kiongozi wao. Kisha akasimama Talha bin Uthman mshika bendera ya mushrikina akasema: “Enyi kundi la wafuasi wa Muhammad! Bila shaka nyinyi mnadai kwamba Mwenyezi Mungu atatuharakisha motoni kupitia panga zenu na atawa-harakisheni peponi kupitia panga zetu, basi je yupo yeyote miongoni mwenu anayetaka Mwenyezi Mungu amuharakishe peponi kupitia upanga wangu au aniharakishe motoni kupitia upanga wake?” Akasimama Ali bin Abu Talib akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi Mwake, sitokuacha mpaka Mwenyezi Mungu akuharakishe motoni kupitia upanga wangu.” Ali akampiga dharuba lililokata miguu yake na hatimaye akaanguka chini, tupu yake ikafunuka, akasema: “Nakuomba kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na udugu ewe binamu yangu.” Ndipo akamwacha, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa Takbira na sahaba zake wakamwambia Ali: “Kitu gani kilikuzuia usimuuwe moja kwa moja.” Akasema: “Hakika binamu yangu aliniomba pindi utupu wake ulipofunuka, hivyo nikamwonea haya.”12

Tafsirut-Tabari Juz. 4, Uk. 125.

12..

16

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 16

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Amesema: Ametusimulia Abdullah bin Salih, amesema: “Amenisimulia Muawiya bin Salih kutoka kwa Ali bin Talha, kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini…” inamkusudia Ali bin Abu Talib.”13 Ametusimulia Muhammad bin Husein, amesema: Ametusimulia Ahmad bin al-Fadhlu, amesema: Ametusimulia Asbat kutoka kwa as-Sadiy, amesema: “Kisha akawajuza ni nani atakayewatawala, akasema: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Ali bin Abu Talib alipitiwa na ombaomba akiwa amerukui msikitini, ndipo akampa pete yake.” Ametusimulia Hinad bin as-Sariy, amesema: Ametusimulia Ubdat kutoka kwa Abdul-Malik, kutoka kwa Abu Ja’far, amesema: “Nilimuuliza kuhusu Aya hii: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini…” Tukasema: Wale walioamini. Tukasema: Imetufikia kwamba iliteremka kwa ajili ya   Tafsirut-Tabari Juz. 6, Uk. 288. Pia Al-Ayyashiy ameiandika katika tafsiri yake Juz. 1, Uk. 356, chapa ya Beirut.

13.

17

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 17

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ali bin Abu Talib. Akasema: “Ali ni miongoni mwa wale walioamini.” Ametusimulia Ismail bin Israil ar-Ramliy, amesema: Ametusimulia Aywabu bin Suwaydi, amesema: “Ametusimulia Utbah bin Abu Hakim kuhusu Aya hii: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini…” akasema: Ali bin Abu Talib.” Amenisimulia al-Harith, amesema: Ametusimulia AbdulAziz, amesema: Ametusimulia Ghalib bin Ubaydullah, amesema: “Nimemsikia Mujahid akisema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini…”, akasema: Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, ­alitoa sadaka na hali akiwa katika rukuu.”14

SURA AL-A’ARAF Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Na toeni haki yake siku ya ­kuvunwa kwake…” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:141). Ametusimulia Umar bin Ali, amesema: Ametusimulia Kathiir bin Hisham, amesema: Ametusimulia Ja’far bin Barqan kutoka kwa Yazid bin al-Aswam, amesema: “Ilikuwa mtende unapokatwa mtu huja na tawi lake na kuliweka pembezoni mwa msikiti, masikini huja na kulipiga kwa fimbo yake, zikipukutika tende huzila, ndipo siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu akaingia akiwa pamoja na Hasan na Husein (a.s.) mmoja wao akaokota na kula tende, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamtemesha toka kinywani mwake. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na Ahlul-Baiti zake walikuwa hawali sadaka. Hivyo wakateremshiwa: “…Na toeni haki yake siku ya kuvunwa kwake…”15   Tafsirut-Tabari Juz. 6 Uk. 289.   Tafsirut-Tabari Juz. 8, Uk. 57.

14. 15.

18

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 18

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AL-A’ARAF Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na tutaondoa chuki vifuani mwao……” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf 7:43) Ametusimulia Muhammad bin Abdul-Aala, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Thawri kutoka kwa Maamar, kutoka kwa Qatadah, amesema: Ali bin Abu Talib alisema: “Hakika mimi16 nataraji bila shaka kuwa ndiye niliye miongoni mwa wale ambao Mwenyezi Mungu amesema kuwahusu: “Na tutaondoa chuki vifuani mwao……”

SURA AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na walipokupangia njama wale w ­ aliokufuru ili wakufunge au wakuue au wakutoe…” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:30) Ametusimulia Hasan bin Yahya, amesema: Ametupa habari Abdurazaq, amesema: Baba yangu amenipa habari kutoka kwa Akrimah, amesema: “Pindi Mtume (s.a.w.w.) alipotoka kwenda pangoni alimwamuru Ali bin Abu Talib (a.s.) akalala kitandani kwake, wakakesha mushrikina wakimlinda, kila walipomwona amelala walidhani ndiye Mtume (s.a.w.w.) hivyo wakamwacha. Ilipofika asubuhi walimvamia na hali wakidhani ndiye Mtume (s.a.w.w.), ghafla wakajikuta wamemzingira Ali (a.s.).”17   Tafsirut-Tabari Juz. 8, Uk. 183. al-Haskaniy ameandika katika kitabu Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 220, kutoka kwa Abdullah bin Malil, kutoka kwa Ali (a.s.) kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na tutaondoa chuki vifuani mwao……” kwamba alisema (a.s.): “Iliteremka kwa ajili yetu.” 17.   Tafsirut-Tabari, Juz. 9, Uk. 228. al-Hafidh al-Haskaniy amesema katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 96, kwamba: “Ali alipolala juu ya kitanda cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) Mwenyezi Mungu aliteremsha Qur’ani nayo ni kauli yake (s.w.t.): “Na miongoni mwa watu kuna ambaye huiuza nafsi yake kwa ajili ya kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni Mwenye huruma juu ya waja.” (Sura alBaqarah: 207).” 16.

19

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 19

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Amenisimulia al-Muthana, amesema: Ametusimulia Abdurazaq kutoka kwa Maamar, amesema: Uthman al-Jazriy amenipa habari kwamba: Hakika Muqsim huria wa Ibnu Abbas alimpa habari kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na walipokupangia njama wale waliokufuru” kwamba alisema: “Makuraishi walishauriana usiku mmoja huko Makka, baadhi yao wakasema: Akiamka mfungeni kwa kizuizi. Wakimkusudia Mtume (s.a.w.w.). Na wengine wakasema: Muuweni huku wengine wakisema: Mfukuzeni. Ndipo Mwenyezi Mungu akamjuza Nabii wake mkakati huo. Ali bin Abu Talib akalala usiku huo juu ya kitanda cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na Mtume akatoka, walipofika asubuhi walimvamia na walipomuona kuwa ni Ali, Mwenyezi Mungu alizuia njama yao, wakasema: “Yupo wapi swahiba wako?” Akajibu: “Sijui.” Wakafuata nyayo zake na walipoufikia mlima na kupitia pangoni wakaona utando wa buibui mlangoni.” Muhammad bin Husein, amesema: Ametusimulia Ahmad bin Mufdhil kutoka kwa as-Sadiy kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na walipokupangia njama wale waliokufuru ili wakufunge…”, amesema: “Ni pindi wazee wa kikuraishi walipokusanyika kushauriana kuhusu Mtume (s.a.w.w.). Ibilisi akaja kwa sura ya mtu mmoja miongoni mwa watu wa Najdi akaingia pamoja nao katika bunge. Baadhi yao wakasema: “Muhammad atakapolala kitandani kwake mshikeni na kumweka kizuizini katika nyumba, tumzuie kwa muda tuone itakuwaje.” Ibilisi akasema: “Hilo ulilosema ni baya mno, mtamweka kizuizini katika nyumba jamaa zake watakuja na kumtoa.” Wakasema mzee amesema kweli. Abu Jahli ambaye alipata ubora kwao kwa kutiiwa na ­Ibilisi akasema: “Bali tuliweke jukumu hili katika kila tumbo miongoni mwa matumbo ya kikuraishi, tumchague 20

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 20

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mtu mmoja toka kila tumbo na tumpe silaha na wote wamvamie Muhammad kwa pamoja, wampige pigo la mtu mmoja, hapo kizazi cha Abdul-Mutalib hawawezi kuwaua makuraishi hivyo hawatoambulia ila fidia tu.” Ibilisi akasema: “Umesema kweli, kijana huyu ndiye mwenye mawazo mazuri mno kati yenu.” Wakatekeleza hilo. Mwenyezi Mungu akampa habari hiyo Mtume Wake, akaenda pangoni na Ali bin Abu Talib akalala juu ya kitanda chake.”18 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na jueni kwamba chochote ­mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na masikini na msafiri……” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:41). Amenisimulia Ibnu Wakiiu, amesema: Baba yangu amenisimulia kutoka kwa Sharik, kutoka kwa Khaswif, kutoka kwa Mujahid, amesema: “Aali Muhammadi haikuwa halali kwao sadaka ndipo akawawekea khumsi.”19 Amenisimulia Ahmad bin Is’haqa, amesema: Ametusimulia Abu Ahmad, amesema: Katusimulia Sharik kutoka kwa Khaswif kutoka kwa Mujahid, amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu na AhlulBait wake hawakuwa wakila sadaka ndipo wakawekewa khumsi.” Amenisimulia Muhammad bin Ammara, amesema: Ametusimulia Ismail bin Aban, amesema: Ametusimulia Swabahu bin Yahya al-Mazniy kutoka kwa as-Sadiy, kutoka kwa Ibnu Daylamiy, amesema: Ali bin Husein (a.s.) alimwambia mzee mmoja wa Sham: “Hivi umewahi kusoma katika Surat al-Anfal: “Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi   Tafsirut-Tabari Juz. 9, Uk. 229.   Tafsirut-Tabari Juz. 10, Uk. 5. Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 218.

18. 19.

21

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 21

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mungu na Mtume na jamaa…” Mzee akasema: “Ndio, kwani nyinyi ndio hao?” Akasema (a.s.): “Ndio.” Amenisimulia al-Harith, amesema: Ametusimulia Abdul-Aziz, amesema: Ametusimulia Abdul-Ghaffar, amesema: Ametusimulia al-Man’hal bin Amru, amesema: Nilimuuliza Abdullah bin Muhammad bin Ali na Ali bin Husein kuhusu khumsi, wakasema: “Hiyo ni ya kwetu.” Nikamwambia Ali: “Hakika Mwenyezi Mungu anasema: “…na mayatima na masikini…” Akasema: “Mayatima wetu na maskini wetu.”20

SURA AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1).

Ametusimulia Ahmad bin Is’haqa, amesema: Ametusimulia Abu Ahmad, amesema: Ametusimulia Israil kutoka kwa Abu Is’haq, kutoka kwa Zayd bin Yushyau, amesema: “Iliteremka Sura Baraa Mtume wa Mwenyezi Mungu akamtuma nayo Abu Bakr kisha akamtuma Ali, akaichukua toka kwake. Abu Bakr aliporejea kwa Mtume akasema: ‘Je kuna chochote kili-choteremka kunihusu?’ Mtume (s.a.w.w.) akasema: ‘Hapana, lakini bila shaka nimeamrishwa niitangaze mimi mwenyewe au mtu kutoka katika Ahlul-Baiti wangu.”’21 Ametusimulia Ibrahim bin Said al-Jawhariy, amesema: Ametusimulia Husein bin Muhammad, amesema: Ametusimulia SulayTafsirut-Tabari, Juz. 10, Uk. 8.   Tafsirut-Tabari, Juz. 10, Uk. 64.

20.  21.

22

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 22

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

man bin Qarmi kutoka kwa Aamash, kutoka kwa Hakim, kutoka kwa Muqsim, kutoka kwa Ibnu Abbas, kwamba: “Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr na Sura Baraa, kisha akamtumia Ali aichukue toka kwake. Abu Bakr akasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! kuna lolote limetokea kwangu?’ Akasema (s.a.w.w.): ‘Hapana, wala hafikishi kwa niaba yangu ila mimi mwenyewe au Ali.’ Alikuwa amemtuma Ali mambo manne: Haiingii peponi ila mwislamu, baada ya mwaka huu mushriku haruhusiwi kuhiji wala kutufu na hali mtupu. Na yule ambaye kati yake na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuna ahadi basi itaendelea mpaka mwisho wa muda wake. Ametusimulia Ibnu Hamid, amesema: Ametusimulia Salmah, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Is’haq kutoka kwa Hakim bin Ibad bin Hanif, kutoka kwa Abu Ja’far Muhammad bin Ali bin Husein bin Ali, amesema: “Ilipoteremka Sura Baraa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr, akaambiwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! ungemtumia mtu Abu Bakr. Akasema: ‘Hafikishi kwa niaba yangu ila mtu kutoka katika AhlulBaiti wangu.’ Kisha akamwita Ali bin Abu Talib na kumwambia: ‘Ondoka na kisa hiki toka mwanzo wa Baraa, watangazie watu siku ya kuchinja watakapokusanyika.’ Ali bin Abu Talib akatoka akiwa amepanda ngamia wa Mtume wa Mwenyezi Mungu al-Adhbau.”22 Amenisimulia Muhammad bin Husein, amesema: Ametusimulia Ahmad bin al-Mufdhil, amesema: Katusimulia Asbat kutoka kwa as-Sadiy, amesema: “Aya hizi mpaka aya ya arubaini, Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma nazo Abu Bakr na akamwamuru azitangaze kwa mahujaji. Alipotembea hadi kuufikia mti kwa Njia ya Dhilhalifa alimtumia Ali akaichukua toka kwake. Abu Bakr akarejea 22.

Tafsirut-Tabari Juz. 10, Uk. 65. 23

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 23

2/14/2018 12:11:27 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kwa Mtume na kusema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! baba yangu na mama yangu wawe fidia kwako, je kuna chochote kimeteremka kunihusu?’ Akasema (s.a.w.w.): ‘Hapana, lakini hafikishi kwa niaba yangu asiyekuwa mimi au asiyetokana na mimi.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:19).

Amenisimulia Yunus, amesema: Ibnu Wahbi ametupa habari, amesema: Nimepewa habari kutoka kwa Abu Swakhri, amesema: Nilimsikia Muhammad bin Kaab al-Qardhiyu akisema: “Talha bin Shayba toka kizazi cha Abdudar, Abbas bin Abdul-Mutalib na Ali bin Abu Talib kila mmoja alijigamba. Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba, funguo zimo mikononi mwangu na hata nikitaka nalala humo.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mgawa maji na msimamizi wake na hata nikitaka nalala msikitini.’ Ali akasema: ‘Sijui mtasema nini. Bila shaka nimeswali miezi sita kabla ya mtu yeyote na mimi ndiye mwanajihadi.’ 24

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 24

2/14/2018 12:11:28 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu….””23 Muhammad bin Hasan amenisimulia, amesema: Ahmad bin alMufdhil ametusimulia, amesema: Amesema Asbat kutoka kwa asSadiy kuhusu “kuwanywesha mahujaji ….” kwamba: “Ali, Abbas na Shayba bin Uthman kila mmoja alijigaba. Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mbora wenu, mimi huwanywesha mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu.’ Shayba akasema: ‘Mimi naamirisha misikiti ya Mwenyezi Mungu.’Ali akasema: ‘Mimi nilihama pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu na hupigana jihadi pamoja naye katika Njia ya Mwenyezi Mungu.’ ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “….na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu?...”24

SURA HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:17) Ametusimulia Muhammad bin Ammara al-Asadiy, amesema: Ametusimulia Zariq bin Marzuq, amesema: Ametusimulia Swabahu al-Farai kutoka kwa Jabir, kutoka kwa Abdullah bin Yahya, amesema: Ali (a.s.) alisema: “Hakuna mtu yeyote miongoni mwa makuraishi ila Aya moja au mbili zilishuka kwa ajili yake.” Ndipo mtu mmoja akamwambia: “Ni ipi iliyoteremka kwa ajili yako?’’ Ali akasema: “Hivi hausomi Aya iliyoteremka katika Sura Hud: “….. na anaifuata na shahidi atokaye kwake..”25   Tafsirut-Tabari Juz. 10, Uk. 96.   Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 244. al-Manaqib cha Ibnu al-Mughazaliy, Hadithi ya 324. Ghayatul-Marami, Mlango wa 63. 25.   Tafsirut-Tabari Juz. 12, Uk. 15. Rejea Tafsirul-Ayyashiy Juz. 2, Uk. 153. Na al-Burhan Juz. 2, Uk. 213. 23. 24.

25

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 25

2/14/2018 12:11:28 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:7).

Ametusimulia Ahmad bin Yahya as-Swufiy, amesema: Ametusimulia Hasan bin Husein al-Ansariy, amesema: Ametusimulia Maadh bin Muslim, amesema: Ametusimulia al-Harawi kutoka kwa Atau bin as-Saib, kutoka kwa Said bin Jubair kutoka kwa Ibnu Abbas, amesema: “Ilipoteremka: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake na kusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji na kila kaumu ina wa kuwaongoza.’ Akaashiria mkono wake kwenye bega la Ali bin Abu Talib na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji. Kupitia kwako wataongoka wenye kutaka kuongoka baada yangu.” 26

Tafsirut-Tabari, Juz. 13, Uk. 108.

26.

26

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 26

2/14/2018 12:11:28 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AN-NAHL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na hatukutuma kabla yako ila wanaume tuliowapa wahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho ­ikiwa nyinyi hamjui.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nahl; 16:43). Ametusimulia Ibnu Wakiu, amesema: Ametusimulia Ibnu Yaman kutoka kwa Israil kutoka kwa Jabir, kutoka kwa Muhammad bin Ali bin Husein bin Ali, Abu Ja’far, kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” Amesema: “Sisi ndio wenye ukumbusho.”27

SURA BANI-ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” (Qur’ani ­Tukufu Sura Bani Israel; 17:26). Amenisimulia Muhammad bin Ammara al-Asadiy, amesema: Ametusimulia Ismail bin Aban, amesema: Ametusimulia Swabahu bin Yahya al-Muzniy kutoka kwa as-Sadiy, kutoka kwa Abu Daylam, amesema: Ali bin Husein (a.s.) alimwambia mzee mmoja wa Sham: “Hivi umewahi kusoma Qur’ani?” akajibu ndio. Ali akasema: “Hivi hujasoma katika Sura Israi: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake..”?” mzee akasema: “Hivi nyinyi ndio jamaa wa karibu ambao Mwenyezi Mungu, Ambaye zimetukuka sifa Zake, ameamuru wapewe haki yao?!!” Ali akasema: “Ndio sisi.”28

SURA TWAHA Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirut-Tabari Juz. 14, Uk. 109.   Tafsirut-Tabari, Juz. 15, Uk. 72.

27. 28.

27

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 27

2/14/2018 12:11:28 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika mimi ni Mwingi wa maghufira kwa anayetubia na akaamini na akatenda mema tena akaongoka.” (Qur’ani Tukufu Sura Twaha; 20:82).

Wengine wamesema yale aliyotusimulia Ismail bin Musa alFazari, amesema: Umar bin Shakir ametupa habari, amesema: Nilimsikia Thabit al-Bunan akisema kuhusu kauli yake (s.w.t.) “Hakika mimi ni Mwingi wa maghufira kwa anayetubia na akaamini…” “Ni kuamini Uwalii wa Ahlul-Baiti wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)”29

SURA AL-ANBIYA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na hatukutuma kabla yako ila wanaume tuliowapa wahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anbiya; 21:43)

Amenisimulia Ahmad bin Muhammad Tusiy, amesema: Amenisimulia Abdurahman bin Salih, amesema: Amenisimulia Musa bin Uthman kutoka kwa Jabir al-Jaafiy, amesema: “Ilipoteremka: “Na hatukutuma kabla yako ila wanaume tuliowapa wahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” Ali bin Abu Talib alisema: ‘Sisi ndio wenye ukumbusho.’”   Tafsirut-Tabari, Juz. 16, Uk. 195.

29.

28

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 28

2/14/2018 12:11:29 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AL-HAJJ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hawa mahasimu wawili waliohasimiana kwa ajili ya Mola wao...” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hajj; 22:19).

Amenisimulia Yaakub, amesema: Ametusimulia Haytham, amesema: Abu Hashim ametupa habari kutoka kwa Abu Mujliz, kutoka kwa Qaysu bin Ubada, amesema: “Nilimsikia Abudhari akiapa kiapo kwa ajili ya Aya hii: “Hawa mahasimu wawili waliohasimiana kwa ajili ya Mola wao...” kwamba iliteremka kwa ajili ya wale waliojitokeza kupambana Siku ya Badri: Hamza, Ali na Ubayda bin al-Harith. Na kwamba Ali alisema: “Mimi ndiye wa awali au wa kwanza atakayepiga magoti mbele ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama kwa ajili ya uhasama.”30

SURA ASH-SHU’ARAA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na uwonye jamaa zako walio karibu.” (Sura Ash-Shu’araa 26: 214).

Amesema: Ametusimulia Salmah, amesema: Ametusimulia ­ uhammad bin Is’haqa kutoka kwa Abdul-Ghaffar bin al-Qasim, M kutoka kwa al-Manhal bin Amru, kutoka kwa Abdullah bin al-Harith bin Nawfal bin al-Harith bin Abdul-Mutalib, kutoka kwa Abdullah bin Abbas kutoka kwa Ali bin Abu Talib, amesema: “Ilipoteremka Aya hii kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Na uwonye jamaa zako walio karibu,” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) 30.

Tafsirut-Tabari, Juz. 17, Uk. 131. 29

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 29

2/14/2018 12:11:29 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

aliniita na kuniambia: ‘Ewe Ali! Hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru niwaonye jamaa zangu walio karibu. Suala hilo likaniumiza kichwa na nikatambua kwamba nitakapowadhihirishia jambo hili nitakumbana na nisiyoyapenda toka kwao. Nikanyamaza mpaka aliponijia Jibril na kuniambia: Ewe Muhammad! Hakika usipofanya unayoamrishwa Mola wako atakuadhibu. Ewe Ali! Tuandalie pishi la chakula uweke mguu wa mbuzi na utujazie birauli ya maziwa, kisha niku-sanyie watoto wa Abdul-Mutalib ili niwaeleze na kuwafikishia yale niliyoamrishwa.’ Nikatekeleza aliyoniamrisha (s.a.w.w.).’ Kisha nikamwitia na wakati huo walikuwa wanaume arobaini, amezidi mtu mmoja au amepungua mmoja, humo walikuwemo ami zake: Abu Talib, Hamza, Abbas na Abu Lahab. Walipokwishakusanyika kwake alinitaka niwaletee chakula nilichowatengenezea, nami nikawaletea. Nilipokiweka Mtume wa Mwenyezi Mungu alichukua kipande kidogo cha nyama akakikata kwa meno yake kisha akakitupia pembezoni mwa sinia, akasema: “Chukueni kwa Jina la Mwenyezi Mungu. “Kaumu wakala mpaka wakatosheka na wala sikuona ila sehemu ambazo mikono yao ilikuwa ikimega. Naapa kwa Mwenyezi Mungu Ambaye nafsi ya Ali imo mikononi mwake, chakula nilichowapa wote ni cha kuweza kula mtu mmoja. “Kisha akasema wape watu kinywaji, nikaja na ile bilauri wakanywa mpaka wakatosheka wote. Naapa kwa Mwenyezi Mungu kilikuwa ni kinywaji cha kutosheka mtu mmoja. “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipotaka kuwaeleza, Abu Lahab alimtangulia kuongea, akasema: “Jamaa yenu amewaroga kwa karamu.” Ndipo kaumu wakatawanyika na wala Mtume wa 30

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 30

2/14/2018 12:11:29 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) hakufanikiwa kuwaeleza, akasema (s.a.w.w.): “Kesho Ali. Hakika mtu huyu amenitangulia kusema yale uliyoyasikia, kaumu wametawanyika kabla sijawaeleza, hivyo tuandalie chakula mfano wa kile ulichoandaa kisha unikusanyie. “Nikatekeleza kisha nikawakusanya, kisha akanitaka nilete chakula nikawaletea naye akafanya kama alivyofanya jana, wakala mpaka wakatosheka. Mtume akasema wape kinywaji nikawaletea bilauri wakanywa mpaka wote wakatosheka. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akaongea kwa kusema: “Enyi wana wa Abdul-Mutalib! Hakika mimi wallahi simjui kijana wa kiarabu aliyewaletea jamaa zake kitu bora kuliko hiki nilichowaletea. Hakika mimi nimewaletea kheri ya dunia na akhera. Na hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru niwalinganie kwayo, basi ni nani kati yenu atanisaidia katika jambo hili, awe ndugu yangu na kadha wa kadha.” “Watu wote wakakaa kimya, nikasema na hali mimi nikiwa ndiye mdogo kiumri kuliko wote, mwenye tongotongo machoni (mtoto) kuliko wote, mwenye tumbo kubwa kuliko wote na mwenye muundi wenye majeraha madogo kuliko wote: “Mimi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu nakuwa waziri wako.” Akaishika shingo yangu kisha akasema (s.a.w.w.): “Hakika huyu ni ndugu yangu na kadha wa kadha, msikilizeni na mumtii.” Kaumu wakaongea na hali wakicheka na wakimwambia Abu Talib: “Bila shaka amekuamuru umsikilize na kumtii mwanao.’”31

SURA AS-SAJDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsirut-Tabari Juz. 19, Uk. 121.

31.

31

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 31

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.” (Qur’ani Tukufu Sura As-Sajda; 32:18)

Ibnu Hamid ametusimulia, amesema: Ametusimulia Salmah bin al-Fadhli, amesema: Amenisimulia Ibnu Is’haq kutoka kwa baadhi ya maswahiba zake, kutoka kwa Atau bin Yasar, amesema: “Iliteremka Madina ikimhusu Ali bin Abu Talib na Walid bin Uqbah bin Abu Muit. Kulikuwa na maneno baina ya Walid na Ali, Walid bin Uqbah akasema: ‘Mimi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye meno makali kuliko wewe na shujaa kuliko wewe.’ Ali akasema: ‘Nyamaza bila shaka wewe ni fasiki.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.”32

SURA AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Amenisimulia Yunus, amesema: Ibnu Wahab ametupa habari, amesema: Amenisimulia Muhammad bin Al-Muthana, amesema: Ametusimulia Bakru bin Yahya bin Zaban al-Inziy kutoka kwa Abu Said al-Khidriy, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: “Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” imeteremka kwa ajili ya watano: Kwa ajili yangu, Ali, Hasan, Husein na Fatima.”33 32. 33.

Tafsirut-Tabari, Juz. 21, Uk. 107. Tafsirut-Tabari, Juz. 22, Uk. 6. 32

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 32

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ametusimulia Ibnu Wakiu, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Bashir kutoka kwa Zakariya, kutoka kwa Mas’ab bin Shayba, kutoka kwa Swafiya binti Shayba, amesema: Aisha alisema: “Siku moja Mtume alitoka akajifunika shuka lililodariziwa na manyoya meusi. Akaja Hasan akamwingiza na kuwa pamoja naye katika shuka, kisha akasema: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Ametusimulia Ibnu Wakiu, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Bakr kutoka kwa Hamad bin Salmah, kutoka kwa Ali bin Zayd, kutoka kwa Anas, amesema kwamba: “Hakika Mtume alikuwa akipitia nyumbani kwa Ali muda wa miezi sita kila alipotoka kwenda kusali, na alikuwa anasema: ‘Swala enyi Ahlul-Baiti. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”34 Amenisimulia Musa bin Abdurahman al-Masruqiy, amesema: Ametusimulia Yahya bin Ibrahim bin Suwayd an-Nakhaiy kutoka kwa Hilal – yaani Ibnu Maqlaswi-, kutoka kwa Zayd, kutoka kwa Shahru bin Hawshab, kutoka kwa Ummu Salama, amesema: “Mtume, Ali, Fatima, Hasan na Husein walikuwa kwangu, nikawaandalia henzirani wakala na kulala, akawafunika shuka kisha akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! hawa ni Ahlul-Baiti wangu, waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”35 Ametusimulia Wakiu, amesema: Ametusimulia Abu Naiim, amesema: Ametusimulia Yunus bin Abu Is’haqa, amesema: Abu Daud amenipa habari kutoka kwa Abul-Hamrau, amesema: “Niliishi Madina miezi sita bila kutoka zama za Mtume (s.a.w.w.), nilimwona Tafsirut-Tabari Juz. 19, Uk. 121.   Tafsirut-Tabari Juz. 22 Uk. 6.

34.  35.

33

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 33

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mtume kila ichomozapo alfajiri akienda kwenye mlango wa Ali na Fatima na kusema: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu.” Amenisimulia Abdul-Aala bin Waswil, amesema: Ametusimulia al-Fadhlu bin Dukyan, amesema: Ametusimulia Abdusalama bin Harbi kutoka kwa Kulthum al-Muharabiy, kutoka kwa Abu Ammar, amesema: “Mimi nilikuwa nimeketi kwa Wathila bin al-Asqau ndipo walipomtaja Ali na kumkashifu, walipoondoka akasema (Wathila): ‘Keti mpaka nikupe habari za huyu waliyemkashifu, mimi nilikuwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) pindi walipomjia Ali, Fatima, Hasan na Husein, akawafunika shuka lake kisha Mtume akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! hawa ni Ahlul-Baiti wangu. Ewe Mwenyezi Mungu! waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”’ Amenisimulia Abdul-Karim bin Abu Umayri, amesema: Ametusimulia Walid bin Muslim, amesema: Ametusimulia Abu Amru, amesema: Amenisimulia Shaddad, amesema: Nilimsikia Wathilat bin al-Asqau akisimulia kwamba: “Nilimuulizia Ali nyumbani kwake, Fatima akanijibu kwamba ametoka lakini punde tu atakuja akiwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), punde Mtume wa Mwenyezi Mungu akafika na kuingia ndani nami nikaingia. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akaketi juu ya kitanda na kumkalisha Fatima kuliani kwake na Ali kushotoni kwake na Hasan na Husein mbele yake, akawafunika nguo yake na kusema: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio watu wa nyumba yangu, ewe Mwenyezi Mungu watu wa nyumba yangu ndio wenye haki zaidi (kuliko mtu baki).”36 Amenisimulia Abu Karib, amesema: Wakiu ametusimulia ­kutoka kwa Abdul-Hamid bin Bahram, kutoka kwa Shahri bin Hawshab,   Tafsirut-Tabari Juz. 22 Uk. 7.

36.

34

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 34

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

k­ utoka kwa Fudhaylu bin Marzuq, kutoka kwa Atia kutoka kwa Abu Said al-Khudriy, kutoka kwa Ummu Salama, amesema: “Aya hii ilipoteremka: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume…” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husein akawafunika kishamia cha Khaibari, akaseama: ‘Ewe Mwenyezi Mungu hawa ndio Ahlul-Baiti wangu. Ewe Mwenyezi Mungu waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.’ Ummu Salama akasema: ‘Mimi ni miongoni mwao?’ Akasema (s.a.w.w.): ‘We utaelekea katika kheri.” Ametusimulia Abu Karib, amesema: Ametusimulia Masw’ab bin al-Miqdam, amesema: Ametusimulia Said bin Zarbiyu kutoka kwa Muhammad bin Sirini kutoka kwa Abu Huraira, kutoka kwa Ummu Salama, amesema: “Fatima alikwenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akiwa amebeba chungu chake chenye uji akakiweka mbele yake, akasema (s.a.w.w.): ‘Yuko wapo mwana wa ami yangu na wanao?’ akasema: ‘Nyumbani.’ Akasema (s.a.w.w.) waite, Fatima akatoka na kwenda kwa Ali na kumwambia: ‘Itikia wito wa Mtume wewe na wanao.’ Ummu Salama anasimulia kwamba: Alipowaona wakija alinyoosha mkono wake hadi kwenye kishamia kilichokuwa juu ya kitanda akakivuta na kukitandika na akawakalisha juu yake, kisha akazishika pembe za kishamia kwa mkono wake wa kushoto akazikusanyia juu ya vichwa vyao na akanyoosha mkono wake wa kulia kwa Mola wake Mlezi na kusema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu hawa ndio Ahlul-Baiti wangu, waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”37 Ametusimulia Abu Karib, amesema: Ametusimulia Hasan bin Atiyah, amesema: Ametusimulia Fadhilu bin Marzuq kutoka kwa   Tafsirut-Tabari Juz. 22 Uk. 7.

37.

35

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 35

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Atiyah kutoka kwa Abu Said kutoka kwa Ummu Salama mke wa Mtume (s.a.w.w.) kwamba: “Hakika Aya hii iliteremka nyumbani kwake: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu..”. Alisema: “Nami nilikuwa nimeketi mlangoni, nikamwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mimi sio miongoni mwa Ahlul-Baiti? Akanijibu: ‘Hakika wewe utaelekea katika kheri, wewe ni miongoni mwa wakeze Mtume (s.a.w.w.).’” Ummu Salama alisema: “Ndani ya nyumba alikuwemo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), Ali, Fatima, Hasan na Husein radhi za Mwenyezi Mungu ziwaendee.” Ametusimulia Abu Karib, amesema: Ametusimulia Khalid bin Mukhallad, amesema: Ametusimulia Musa bin Yakub, amesema: Amenisimulia Hashim bin Utbah Ibnu Abu Waqqas, kutoka kwa Abdullah bin Wahab bin Zam’at, amesema: “Ummu Salama alinipa habari kwamba: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliwakusanya Ali, Fatima, na Hasan na Husein kisha akawafunika nguo yake, kisha akaelekea kwa Mwenyezi Mungu na kusema: ‘Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu.’ Ummu Salama akasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! (Allah) Amenijumuisha pamoja nao?’ akasema (s.a.w.w.): ‘Hakika wewe ni miongoni mwa wake zangu.”’38 Amenisimulia Ahmad bin Muhammad at-Tusiy, amesema: Ametusimulia Abdurahman bin Salih, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Sulayman al-Isbahani kutoka kwa Yahya bin Ubaydul-Makkiy, kutoka kwa Atau, kutoka kwa Umar bin Abu Samla, amesema: “Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume…” iliteremka kwa Mtume (s.a.w.w.) hali akiwa nyumbani kwa Ummu Salama. Mtume akamwita Hasan, Husein na Fatima na kuwakalisha mbele yake, akamwita Ali akamkalisha nyuma yake, wakajifunika yeye na wao   Tafsirut-Tabari Juz. 22, Uk. 8.

38.

36

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 36

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kishamia kisha akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu hawa ndio AhlulBaiti wangu, waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.’” Amenisimulia Muhammad bin Ammara, amesema: Ametusimulia Ismail bin Aban, amesema: Ametusimulia Swabbah bin Yahya al-Mar’iyyu kutoka kwa as-Sadiy kutoka kwa Abu Daylam, amesema: Ali bin Husein (a.s.) alimwambia mzee wa Sham: “Umewahi kusoma katika Sura Ahzab: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.’” Mzee akasema: “Hivi ni nyinyi hao?” Ali bin Husein akasema: “Ndio ni sisi.” Ametusimulia Ibnu al-Muthana, amesema: Ametusimulia Abu Bakr al-Hanafiy, amesema: Ametusimulia Bakiri bin Mismar, amesema: Nilimsikia Amir bin Said akisema: Saad amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wahyi ulipomteremkia alimchukua Ali, wanae na Fatima akawaingiza chini ya nguo yake kisha akasema: Mola wangu Mlezi hawa ndio ndugu zangu na Ahlul-Baiti wangu.”39 Ametusimulia Ibnu Hamid, amesema: Ametusimulia Abdullah bin Abdul-Quddus kutoka kwa Aamash, kutoka kwa Hakim bin Said, amesema: “Tulimtaja Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee mbele ya Ummu Salama, akasema: Kwa ajili yake iliteremka: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Ummu Salama akasema: Mtume (s.a.w.w.) alikuja nyumbani kwangu, aka-niambia usimpe yeyote idhini ya kuingia. Akaja   Tafsirut-Tabari Juz. 22, Uk. 7.

39.

37

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 37

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

­ atima sikuweza kumzuia na baba yake, kisha akaja Hasan sikuF weza kumzuia asiingie kwa babu yake na mama yake. Akaja Husain sikuweza kumzuia, akaja Ali sikuweza kumzuia, ndipo wakamzunguka Mtume (s.a.w.w.) wakiwa juu ya busati, Mtume wa Mwenyezi (s.a.w.w.) akawafunika kwa kishamia alichokuwa amejitanda, kisha akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu hawa ndio Ahlul-Baiti wangu. Waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.’ Ndipo ikateremka Aya hii walipokusanyika juu ya busati. Nikasema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Na mimi? Ummu Salama anasema: “Wallahi hakukubali bali alisema: Hakika wewe utaelekea katika kheri.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).

Ametusimulia Ibnu Hamid, amesema: Ametusimulia Harun kutoka kwa Anbasat kutoka kwa Uthman bin Mawhib kutoka kwa Musa bin Talha kutoka kwa baba yake, amesema: “Mtu mmoja alikwenda kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: Nimemsikia Mwenyezi Mungu akisema: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii…” ni ipi namna ya kukusalia? Mtume akasema: ‘Sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.’”40   Tafsirut-Tabari, Juz. 22, Uk. 43.

40.

38

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 38

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ametusimulia Abu Karib, amesema: Ametusimulia Malik bin Ismail, amesema: Ametusimulia Abu Israil kutoka kwa Yunus bin Khabab, amesema: Bifaris alituhutubia akasema: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii…” amenipa habari yule aliyemsikia Ibnu Abbas akisema: ‘Hivi ndivyo ilivyoteremka. Tukamwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama sala tutakusaliaje? Akasema: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.’41 Ametusimulia Bushru, amesema: Ametusimulia Yazid, amesema: Ametusimulia Said kutoka kwa Qattadah kuhusu kauli yake (s..w.t.): “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii…” amesema: “Ilipoteremka Aya hii walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama sala tutakusaliaje? Akasema: ‘Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim.”’ Ametusimulia Ibnu Hamid, amesema: Ametusimulia Jarir kutoka kwa Mughira kutoka kwa Ziyad kutoka kwa Ibrahim kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii…” amesema: “Walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama sala tutakusaliaje? Akasema: ‘Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad mja wako na Mtume wako na Ahlul-Baiti wake, kama ulivyomrehemu Ibrahim hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.”’ Amenisimulia Ja’far bin Muhammad al-Kufiy, amesema: ­Ametusimulia Yaala bin al-Ajlahu kutoka kwa al-Hakam bin Utbah,   Tafsirut-Tabari Juz. 22, Uk. 44.

41.

39

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 39

2/14/2018 12:11:30 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kutoka kwa Abdullah bin Abu Layla, kutoka kwa Kaab bin Ajarah, amesema: “Ilipoteremka: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii…” nilimwendea na kumwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama sala tutakusaliaje? Akasema (s.a.w.w.): Sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad, kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad, kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.”

SURA AS-SAFFAT Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amani kwa Ilyasin.” (Qur’ani Tukufu Sura as-Saffat; 37:130) Amesema: Maana yake ni Salamu kwa aali Muhammad (s.a.w.w.).42

SURA ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23).

Ametusimulia Abu Karib, amesema: Abu Usama ametusimulia kutoka kwa Abdul-Malik bin Maysara kutoka kwa Taus kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” amesema: “Ibnu Abbas aliulizwa kuhusu Aya hiyo, Ibnu Jubayri akasema: Hao ni karaba ambao ni aali Muhammad.”43   Tafsirut-Tabari Juz. 23, Uk. 96. Tafsirut-Tabari, Juz. 25, Uk. 23.

42. 43.

40

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 40

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Amenisimulia Muhammad bin Ummara, amesema: Ametusimulia Ismail bin Aban, amesema: Kutoka kwa As-Sadiy kutoka kwa Abu Daylam amesema: Alipoletwa Ali bin Husein na hali ni mateka na kusimamishwa katika barabara kuu ya Damascus alisimama mzee mmoja kati ya watu wa Sham, akasema: ‘Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye amewauwa na kuwang’oeni na kung’oa mzizi wa fitina.’ Ali bin Husein radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu ndio. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’Akajibu nimewahi kusoma Qur’ani na sijawahi kusoma Aali Haa Miim. Akasema (a.s.): ‘Hujawahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...”’ Mzee akasema: ‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’

SURA AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha, hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu “ (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Amenisimulia Muhammad bin Amru, amesema: Ametusimulia Abu Aswim, amesema: Ametusimulia Isa kutoka kwa Ibnu Abu Najihu kutoka kwa Mujahid kuhusu kauli yake (s.w.t.): “… basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha…” amesema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka. 41

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 41

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee, alitoa sadaka ya dinari. Ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.).”44 Ametusimulia Muhammad bin Ubaydu bin Muhammad al-Muhariby, amesema: Ametusimulia al-Mutalib bin Ziyad kutoka kwa Mujahid, amesema: Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee alisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nayo ni: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana…..”” Amenisimulia Musa bin Abdurahman al-Masruqiy, amesema: Ametusimulia Abu Usama kutoka kwa Shablu bin Ubada kutoka kwa Mujahid kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume …..” amesema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume mpaka watoe sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee. Alitoa sadaka ya dinari. Ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.). Abu Karib ametusimulia, amesema: Ametusimulia Ibnu Idirisa, amesema: Nilimsikia Laythu kutoka kwa Mujahid, amesema: Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee alisema: “Kuna Aya katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu. Nilikuwa na dinari moja nikaichenji na kupata dirhamu kumi, nikawa kila niendapo kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) hutoa sadaka dirhamu moja.” 44.

Tafsirut-Tabari, Juz. 28, Uk. 20. 42

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 42

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AT-TAGHABUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni jaribio, na kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Taghabun; 64:15).

Ametusimulia Abu Karib, amesema: Ametusimulia Uthman bin Najiyah kutoka kwa Husein bin Waqid, amesema: Abdullah bin Barida amesema: “Nilimwona Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akitoa hotuba ghafla wakaja Hasan na Husein radhi za Mwenyezi Mungu ziwaendee wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuamka, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akateremka toka mimbarini akawachukua na kuwanyanyua na kuwaweka mapajani mwake kisha akasema: ‘Mwenyezi Mungu na Mtume wake wamesema kweli. Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni jaribio, nilipowaona hawa wawili sikuweza kuvumilia.’”45

SURA AL-HAQQA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Haqqa; 69:12).

Ametusimulia Ali bin Sahli, amesema: Ametusimulia Walid bin Muslim, amesema: Nimemsikia Makhula akisema: “Mtume wa   Tafsirut-Tabari, Juz. 28, Uk. 126.

45.

43

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 43

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisoma: “…na sikio lisikialo lisikie.” Kisha akamgeukia Ali na kusema: ‘Nilimwomba Mwenyezi Mungu sikio lako alifanye hivyo.’ Ali radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee alisema: ‘Basi sikuwahi kusikia kitu chochote toka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kisha nikakisahau.”’46 Amenisimulia Muhammad bin Khalqu, amesema: Amenisimulia Bushru bin Adam, amesema: Ametusimulia Abdullah Ibnu Zubair, amesema: Amenisimulia Abdullah bin Rustam, amesema: Nilimsikia Burayda akisema: “Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema kumwambia Ali (a.s.): ‘Ewe Ali! Hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru nikusogeze karibu, nisikutenge mbali na nikuelimishe nawe usikie vilivyo. Na Mwenyezi Mungu ­amehakikisha unasikia vilivyo.’ Ndipo ikateremka: “…na sikio lisikialo lisikie.”” Amenisimulia Muhammad bin Khalfu, amesema: Ametusimulia Ismail bin Ibrahim Abu Yahya at-Tamimiy kutoka kwa Burayda al-Aslamiy, amesema: “Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema kumwambia Ali (a.s.): ‘Hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru nikuelimishe, nikusogeze karibu, nisikunyanyapae na nisikutenge mbali.”’

SURAT AL-BAYYINA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Bayyina; 98:7).   Tafsirut-Tabari Juz. 29 Uk. 55.

46.

44

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 44

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ametusimulia Ibnu Hamid, amesema: Ametusimulia Isa bin Farqad kutoka kwa Abul-Jarud kutoka kwa Muhammad bin Ali kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.” amesema: Mtume akasema: “Ali ni wewe na wafuasi wako.”47

Tafsirut-Tabari, Juz. 30, Uk. 265.

47.

45

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 45

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA ­AT-THAALABIY, INAYOITWA AL-KASHFU WAL-BAYAN FII TAFSIRIL-QUR’ANI SURA AL-FATIHA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Tuongoze njia iliyonyooka.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Fatiha; 1:6).

Muhammad bin Abdullah al-Qayiniy ametupa habari, amesema: Ametusimulia Abu Hasan bin Uthman an-Naswibiy huko Baghdad, amesema: Ametusimulia Abul-Qasim, amesema: Ametusimulia Abu Hafsa Umar bin Ahmad bin Uthman, amesema: Baba yangu ametusimulia, amesema: Ametusimulia Hamid bin Sahli, amesema: ­Ametusimulia Abdullah bin Muhammad al-Ajliy, amesema: Ametusimulia Ibrahim bin Jabir kutoka kwa Muslim bin Hayyan kutoka kwa Burayda kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Tuongoze njia iliyonyooka.” amesema: “Ni Njia ya Muhammad na aali zake amani iwe juu yao wote.”48

SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Ameipokea Shahru Ashub katika kitabu al-Manaqib Juz. 2, Uk. 271.

48.

46

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 46

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya ­ wenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja.” M (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:207).

At-Thaalabi amesema: Nimeona katika baadhi ya vitabu kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipotaka kuhama alimwacha badala yake Ali bin Abu Talib huko Makka ili alipe madeni yake na akabidhi amana zilizokuwa kwake. Na alimwamuru siku aliyotoka kwenda pangoni – Mushrikina wakiwa wameizingira nyumba yake - alale kitandani kwake na alimwambia: “Jitande joho langu la kijani na ulale juu ya kitanda changu hakika hutopatwa na lolote lichukizalo kutoka kwao inshaallah.” Ali alifanya hivyo. Ndipo Mwenyezi Mungu akawafunulia malaika (Jibril na Mikail): Hivi hamui kama Ali bin Abu Talib! nimeweka undugu kati yake na Muhammad naye amelala juu ya kitanda chake akijitoa fidia kwa niaba yake na kuupa uhai wake (Muhammad) kipaumbele kabla ya uhai wake binafsi. Teremkeni aridhini mkamlinde dhidi ya adui wake. ` Malaika Jibril akateremka na kukaa kichwani kwake na Mikail akakaa miguuni kwake na hali Jibril akinadi: “Pongezi pongezi! Ewe Ali! Mwenyezi Mungu anajionea fahari kwako mbele ya Malaika.” Kwa ajili ya Ali Mwenyezi Mungu akateremsha kwa Mtume wake akiwa njiani kuelekea Madina: “Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya ­Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja.”49

Abu Muhammad Abdullah bin Muhammad Abdullah alQadhiy ametupa habari, amesema: Abu Husein Muhammad bin   Ameipokea al-Haskaniy katika kitabu Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 123, Hadithi ya 133. Ameipokea al-Ghazali katika kitabu Ihyau Uluumid-Din Juz. 3, Uk. 238 katika kubainisha fadhila zake na utoaji kipaumbele wake. Ameipokea Ibnu Shahri Ashub katika kitabu chake Al-Manaqib Juz. 2, Uk. 65.

49.

47

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 47

2/14/2018 12:11:31 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Uthman bin Hasan an-Naswibiy ametusimulia huko Baghdad, amesema: Abu Bakr Muhammad bin Hasan bin Salih as-Subiiy ametusimulia huko Halbi, amesema: Ametusimulia Ahmad bin Muhammad bin Said, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Mansur, amesema: Ametusimulia Ahmad bin Abu Abdurahman, amesema: Ametusimulia Hasan bin Muhammad Farqad, amesema: Ametusimulia al-Hakam bin Dhahir, amesema: Ametusimulia as-Sadiy kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja,” amesema: Ibnu Abbas alisema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.) pindi Mtume (s.a.w.w) alipowatoka Mushrikina na kwenda pangoni akiwa pamoja na Abu Bakr. Ali ndipo alipolala juu ya kitanda cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.).”50 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274)

Amenipa habari Ibnu Fanjawihi, amesema: Ametusimulia Abu Ali bin Habish al-Maqriy, amesema: Ametusimulia Wahib kutoka kwa Ayub kutoka kwa Mujahid, kutoka kwa Ibnu Abbas, amesema: “Ali bin Abu Talib alikuwa na dirhamu nne hakuwa anamiliki nyingine zaidi ya hizo, akatoa sadaka dirhamu moja kwa siri na ny  Rejea kitabu Sharhu Nahjul-Balagha cha Ibu Abil-Hadid Juz. 1, Uk. 789.

50.

48

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 48

2/14/2018 12:11:32 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ingine kwa dhahiri, nyingine usiku na nyingine mchana. Ndipo ­ikateremka Aya hii.”51

SURA AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na watoto wa Ibrahim na watoto wa Imran juu ya walimwengu wote.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:33).

Abu Muhammad Abdullah bin Muhammad al-Qadhiy ametusimulia, amesema: Ametusimulia Abu Hasan Muhammad bin Uthman bin Hasan an-Naswibiy, amesema: Ametusimulia Abu Bakr Muhammad bin Husein bin Salih as-Subiiy, amesema: Ametupa habari Ahmad bin Muhammad bin Said, amesema: Ametusimulia Ahmad bin Maytham bin Abu Naim, amesema: Ametusimulia Abu Junada asSaluliy kutoka kwa Aamash kutoka kwa Abu Wail, amesema: Nimesoma katika Msahafu wa Abdullah bin Mas’ud: “Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na watoto wa Ibrahim na watoto wa Imran juu ya walimwengu wote.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Ameipokea al-Wahidiy katika kitabu Asbabun-Nuzuul Uk. 64. Ibnu Asakir katika kitabu Taarikhud-Damashqi Juz. 2, Uk. 13, Hadithi ya 918. Na Tabari katika kitabu ar-Riyadh an-Nadhrah Juz. 2, Uk. 206.

51.

49

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 49

2/14/2018 12:11:32 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Alipomzaa alisema: Mola wangu! Nimemzaa mwanamke, na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa. Na mwanamume si kama mwanamke na nimemwita Maryam...” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:36).

Abu Zar’at amepokea kutoka kwa Abu Huraira kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha katika wanawake wa ulimwenguni: Maryam binti Imran, Asia mke wa Firaun, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:37).

Kutoka kwa Jabir bin Abdullah amesema kwamba hakika Mtume (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bila kula chakula mpaka hali hiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenye nyumba za wakeze lakini hakukuta chochote kwao ndipo akaenda kwa Fatima na kumwambia: “Ewe mwanangu mpendwa! Je una chochote ninachoweza kula kwani hakika mimi ni mwenye njaa?” Akamjibu: “Wallahi sina ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa haki ya baba yangu na mama yangu.” Mtume alipotoka jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vya mkate na finyango ya nyama. Fatima akawatuma Hasan na Husein waende kumwita Mtume (s.a.w.w.) naye akaenda. Fatima akamweleza na kumfunulia bakuli. Ghafla Fatuma akakuta bakuli limejaa mikate na nyama na akatambua kuwa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu. Mtume (s.a.w.w.) akasema: Umetoa wapi hivi? 50

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 50

2/14/2018 12:11:32 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Akajibu: “Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Mtume akamuhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Ambaye amekufanya kifani wa bibi mtukufu wa wana wa Izrael (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwa aruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Kisha Mtume (s.a.w.w.) akampeleka ujumbe Ali aje. Akala Mtume na Ahlul-Baiti wake wote kwa pamoja mpaka wakashiba. Fatima alisema: “Bakuli lilibaki kama lilivyokuwa likiwa limejaa. Hivyo nikawagawia majirani zangu wote na Mwenyezi Mungu aliweka humo kheri nyingi na baraka.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

At-Thaalabi amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipousomea ujumbe wa Najran Aya hizi na kuwaomba wafanye maombi ya laana walisema: “Mpaka turejee na tutafakari jambo hili kisha kesho tutakuja tena.” Ndipo kesho wakaenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), na Mtume akatoka akiwa amemkum51

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 51

2/14/2018 12:11:32 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

batia Husein na amemshika mkono Hasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima. Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Askofu wa Najran akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia, na hatabaki mkiristo yeyote hapa duniani mpaka siku ya Kiyama.” Wakasema: “Ewe Abul-Qasim! Tumeona tusiapizane na wewe na tukuwache uendelee kuwa katika dini yako nasi tuendelee kubaki katika dini yetu. ” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Mkikataa kufanya maapizano basi msilimu mtapata haki waliyonayo waislamu na mtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwao.” Wakakataa, ndipo Mtume akawaambia: “Basi hakika mimi nitawafukuzeni kupitia waarabu.” Wakasema: “Hatuna nguvu ya kupigana vita na waarabu, lakini sisi tunafanya suluhu na wewe usitushambulie kivita na wala usitufukuze na wala usitutoe katika dini yetu. Kwa sharti tukupe kila mwaka Hilla52 elfu mbili: Elfu moja katika mwezi wa Safar na elfu nyingine katika mwezi wa Rajab.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akafanya nao suluhu kwa sharti hilo na akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake hakika adhabu imeshateremka juu ya watu wa Najran. Na lau wangefanya maapizano wangegeuzwa nyani na nguruwe na bonde lao lingewaka moto. Na Mwenyezi Mungu angeiteketeza Najran na watu wake hata ndege aliyopo juu ya mti. Wala mwaka usingepita wakristo wote wangekuwa wameteketea.”53   Jina la pesa kama vile Dola, Shilingi, Paundi na mfano wa hizo.   Ameipokea Ahmad bin Hanbal katika kitabu al-Fadhail Uk. 27. al-Wahidiy katika kitabu Asbabun-Nuzuul Uk. 74. Na ameipokea pia Tabarani katika kitabu Dalailun-Nubuwa Juz. 1, Uk. 197, Sura ya 21.

52. 53.

52

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 52

2/14/2018 12:11:32 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Kama mmepatwa jeraha, basi kuna kaumu wamekwishapata jeraha kama hilo, na siku za namna hii tutawaletea watu kwa zamu. Na ili apate kuwajua Mwenyezi Mungu ambao wameamini katika nyinyi na afanye miongoni mwenu mashahidi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:140).

Anas bin Malik amesema: Ali bin Abu Talib, Mwenyezi Mungu autukuze uso wake, alikuja siku hiyo kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akiwa na majeraha zaidi ya sabini, yatokanayo na mikuki, pigo la mishale. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawa anayapangusa nayo yanapona kwa idhini ya Mwenyezi ­Mungu kama vile hayakuwa ni majeraha.

SURA AN-NISAA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

53

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 53

2/14/2018 12:11:33 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Enyi mlioamini! Msikaribie Swala na hali mmelewa mpaka myajue mnayoyasema; wala mkiwa na janaba isipokuwa mkiwa safarini mpaka muoge. Na muwapo wagonjwa au mko safarini au akawa mmoja wenu ametoka chooni au mkagusana na wanawake, kisha msipate maji, basi tayamamuni na mchanga ulio twahara; mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe Mwenye kughufiria.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nisaa’; 4:43).

Ismaili bin Umaiyya amesema kutoka kwa Husein kutoka kwa Ummu Salama, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika kuingia ndani ya msikiti wangu ni haramu kwa kila mwanamke mwenye hedhi na kila mwanaume mwenye janaba ila kwa Muhammadi na Ahlul-Baiti wake: Ali, Fatima, Hasan na ­Husein (a.s.).”54

SURA AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Ibnu Abbas amesema: as-Sadiy, Utba bin Hakim na Ghalib bin Abdullah wamesema: Kauli yake (s.w.t.): “Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Alimkusu  Tanbihi: at-Thaalabi katika kuifasiri kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ambao mmestarehe nao katika wao, basi wapeni mahari yao yaliyo lazimu.” (Sura Nisai: 24) amesema: Ali bin Abu Talib alisema: ‘Lau si Umar kukataza kuoa ndoa ya muda (Muta) asingelizini ila mwovu wa kupindukia.”’

54.

54

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 54

2/14/2018 12:11:33 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

dia Ali bin Abu Talib. Ombaomba alipita kwake na hali yeye karukui msikitini akampa pete yake. Kutoka kwa Ibayat bin ar-Rabiiyyu, amesema: Alipokuwa Abdullah Bin Abbas ameketi katika ukingo wa Kisima cha Zamzam ghafla alikuja mtu aliyekuwa kafunga kilemba. Ikawa kila Ibnu Abbas akisema: ‘Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema’ naye husema: ‘Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema’. Ndipo Ibnu Abbas akasema: Nakuomba kwa heshima ya Mwenyezi Mungu uniambie wewe ni nani? Akaondoa kilemba usoni na kusema: ”Enyi watu! Anayenitambua ameshanitambua. Mimi ni Jundub bin Junada niliyepigana vita vya Badri Abudhari al-Ghaffari. Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kwa masikio yangu haya mawili la sivyo yapatwe na ukiziwi, akisema: “Ali ni kiongozi wa watu wema. Muuwaji wa makafiri. Atasaidiwa yule mwenye kumsaidia na atatelekezwa yule mwenye kumtelekeza.” “Hakika mimi siku moja niliswali pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) Swala ya Adhuhuri, ombaomba akaomba msikitini na hakuna yeyote aliyempa, ndipo ombaomba akainua mikono yake mbinguni na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu shuhudia kwamba bila shaka mimi nimeomba ndani ya msikiti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu na sijapewa chochote na yeyote.” Kipindi hicho Ali alikuwa amerukuu ndipo akamwashiria kwenye chanda chake cha kulia kilichokuwa na pete. Ombaomba alikwenda na kuchukua pete toka kwenye chanda chake na hali Mtume akitizama kwa macho yake. “Mtume alipomaliza Swala yake aliinua kichwa chake mbinguni na kusema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! Ndugu 55

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 55

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

yangu Musa alikuomba: Akasema: Ee Mola wangu! Nipanulie kifua changu. Na unifanyie wepesi kazi yangu. Na ufungue fundo katika ulimi wangu. Wapate kufahamu kauli yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Harun. Nitie nguvu kupitia yeye. Na umshirikishe katika kazi yangu.” (Sura Twaha: 25 – 32) ukamteremshia Qur’ani yenye kutamka: “Akasema: Karibuni tutautia nguvu mkono wako kwa ndugu yako na tutakupeni ushindi..” (Sura al-Qasas: 35). “Ewe Mwenyezi Mungu! Na mimi ni Muhammad Nabii wako na chaguo lako. Ewe Mwenyezi Mungu Nipanulie kifua changu. Na unifanyie wepesi kazi yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Ali. Nitie nguvu kupitia yeye.’” Abu Dharri anasema: “Wallahi kabla Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) hajamaliza Jibril akateremka kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kusema: Ewe Muhammad soma. Akasema nisome nini? Akamwambia soma: “Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.”55 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako; na kama hutafanya, basi hukufikisha ujumbe wake. Na Mwenyezi   Ameipokea Humawi katika kitabu Faraidus-Samtwayn Juz. 1, Uk. 191, Chapa ya ­Beirut, Hadithi ya 162, Mlango wa 39.

55.

56

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 56

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:67).

Abu Ja’far Muhammad bin Ali amesema: “Maana yake ni: Fikisha uliy-oteremshiwa kuhusu ubora wa Ali bin Abu Talib. Ilipoteremka Aya hii Mtume alimshika Ali mkono na kusema: Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.” Kutoka kwa Adiy bin Thabit kutoka kwa al-Barrau, amesema: Tuliporudi pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) tulifika sehemu iitwayo Ghadir Khum. Akanadi Swalatu Jamia, na akafagia chini ya miti miwili. Akauinua mkono wa Ali na kusema: “Mimi si nina mamlaka zaidi kwa waumini kuliko nafsi zao?” Wakajibu: “Ndio una mamlaka ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Akasema: “Huyu ni mwenye mamlaka juu ya kila ambaye mimi nina mamlaka juu yake. Ewe Mwenyezi Mungu mpende yule atakayempenda na mfanyie uadui yule atakayemfanyia uadui.” Umari akamwendea na kumwambia: “Hongera ewe mwana wa Abu Talib, umekuwa mwenye mamlaka juu ya kila muumini wa kiume na wa kike.” Kutoka kwa al-Kalbiy, kutoka kwa Abu Salih, kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako..” amesema: Iliteremka kwa ajili ya Ali, Mtume aliamrishwa afikishe kwa ajili yake. Akauinua mkono wa Ali na kusema: “Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali ana mamlaka juu yake. Ewe Mwenyezi Mungu mpende ampendaye na mfanyie uadui amfanyiaye uadui.”56   Ameipokea Ibnu Asakir katika kitabu Taarikh Damashqi Juz. 2, Uk. 85, Chapa ya pili, Hadithi ya 588.

56.

57

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 57

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na ­masikini na msafiri……” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:41).

Az-Zahri amesema: “Fatima na Abbas walikuja kwa Abu Bakr kumwomba mirathi yao toka katika Shamba la Fadak na ghanima za vita vya Khaibar. Abu Bakr akawaambia: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: ‘Sisi Manabii haturithiwi, ­tunayoyaacha ni sadaka.’” Man’hal bin Umar anasema: “Nilimuuliza Abdullah bin ­ uhammad bin Ali na Ali bin Husein kuhusu khumsi. Wakasema: M ‘Ni ya kwetu.’ Nikamwambia Ali: Mwenyezi Mungu anasema: “….. na mayatima na masikini na msafiri……” Akasema: ‘Mayatima wetu, maskini wetu na wasafiri wetu.’”

SURA AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1). 58

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 58

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Muhammad bin Is’haqa na Mujahid wamesema: Ulipoingia mwaka wa tisa Mtume wa Mwenyezi Mungu alikusudia kwenda Hija akasema: Bila shaka mushrikina watahudhuria ili wahiji na hali wakiwa uchi, sipendi kuhiji mpaka watakapokuwa kinyume na hivyo. Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu akamtuma Abu Bakr awe kiongozi awaongoze watu katika msimu wa Hija hiyo. Akampa aende na Aya arobaini toka mwanzo wa Sura Baraa ili akawasomee mahujaji wa msimu huo. Baada ya Abu Bakr kuondoka Mtume wa Mwenyezi Mungu alimwita Ali na kumwambia: “Nenda na kisa hiki kuanzia mwanzo wa Baraa kawatangazie watu watakapokusanyika.” Ali akotoka akiwa juu ya ngamia wa Mtume wa Mwenyezi Mungu mpaka alipomdiriki Abu Bakr huko Dhul-Halifa akaichukua Sura ile toka kwake. Abu Bakr akarejea kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Baba yangu na mama yangu wawe fidia kwako, je kimeteremshwa chochote kunihusu?’ Mtume (s.a.w.w.) akasema: ‘Hapana, lakini hapaswi kufikisha kwa niaba yangu ila mimi mwenyewe.’ Au alisema: ‘Mtu atokanaye na mimi.’57 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Muhajirina na Ansari...” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1).

Baadhi yao wamesema: Mwanamume wa kwanza kumwamini Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni Ali bin Abu Talib. Hiyo   Al-Haskaniy amepokea kisa hiki kwa njia mbalimbali na kwa matamshi tofau-ti katika Hadithi ishirini kuanzia Hadithi ya 308 mpaka Hadithi ya 328 katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil.

57.

59

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 59

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ni kauli ya Ibnu Abbas, Jabir, Zayd bin Arqam, Muhammad bin alMunkadir, Rabiarur-Raayi na Abu Hazim al-Madaniy. Al-Kalbiy amesema: “Ali aliupokea Uislamu angali mtoto wa miaka tisa.” Mujahid na Ibnu Is’haqa wamesema: “Aliupokea ­Uislamu angali mtoto wa miaka kumi. ” Na imepokewa kwamba Abu Talib alimwambia Ali: “Ewe mwanangu, ni imani gani hii uliyo nayo?” Akajibu: “Ewe baba yangu mpendwa, nimemwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na nimesadikisha aliyoyaleta na nimeswali pamoja naye kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. ” Akamwambia: “Hakika Muhammad halinganii ila kwenye kheri shikamana naye. ” Ubaydullah bin Musa amepokea kutoka kwa al-Alau bin Man’hal bin Umar, kutoka kwa Abbas bin Abdullah, amesema: “Nilimsikia Ali akisema: “Mimi ni mja wa Mwenyezi Mungu na ndugu wa mjumbe wake, na mimi ni Swidiqi mkubwa. Hatodai hayo baada yangu ila ni mwongo mzushi. Nimeswali miaka saba kabla ya watu.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:119).

Abdullah bin Muhammad bin Abdullah amenipa habari, ­amesema: Ametusimulia al-Kalbiy, kutoka kwa Abu Salih kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu Aya hii: “Enyi mlioamini! mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.” Amesema: Ni kuwa pamoja na Ali bin Abu Talib na maswahaba wake.” Na Abdullah amenipa habari, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Uthman, amesema: Ametusimulia Mufadhal bin Salih 60

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 60

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

k­ utoka kwa Jabir kutoka kwa Abu Ja’far kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Enyi mlioamini! mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.” Amesema: “Ni kuwa pamoja na aali Muhammad.”58

SURA HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:17).

Abdullah al-Qariu amenipa habari, amesema: Ametupa habari alQadhi Abul-Husain an-Naswibiy, amesema: Ametupa habari Hasan bin Hasan kutoka kwa Habban kutoka kwa al-Kalbiy, kutoka kwa Abu Salih, kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake..” kuwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na “..na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” ni Ali peke yake.59 Abul Jarud ametupa habari kutoka kwa Habib bin Yasar kutoka kwa Zadhan, amesema: “Nilimsikia Ali akisema: “Naapa kwa Yule Ambaye ameotesha punje na kuumba nafsi, lau nikitandikiwa mto nikaketi juu yake nitawahukumu wanataurati kwa Taurati yao, wanainjili kwa Injili yao, wanazaburi kwa Zaburi yao na wanafurqan kwa Furqani yao. Naapa kwa Yule Ambaye ameotesha punje na kuumba nafsi, hakuna mtu yeyote miongoni mwa makuraishi aliyepitiwa na mtihani ila mimi najua matokeo yake kama utampeleka peponi au   Al-Haskaniy ameipokea katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil, Hadithi ya 353. Na Sayyid Hashim al-Bahraniy katika kitabu Ghayatul-Marami Uk. 375, Mlango wa 77. . 59.   Ameipokea Ibnu Asakir katika kitabu Taarikh Damashqi Juz. 2, Uk. 420, Hadithi ya 928, kwenye wasifu wa Amirul-Muuminiina. 58.

61

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 61

2/14/2018 12:11:34 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

utamwingiza motoni.” Akasimama mtu mmoja na kumwambia: “Ni ipi Aya yako ewe Amirul-Muuminina iliyoteremka kuhusu madai yako? ” Akasema: “Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” Mtume wa Mwenyezi Mungu ana dalili ya wazi toka kwa Mola wake na mimi ni shahidi atokaye kwake. ”60

SURA AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani za mizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina na isiyochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale. Na tunaifanya bora baadhi yake kuliko mingine katika kula. Hakika katika hayo kuna ishara kwa watu wanotia akilini.” (Qur’ani Tukufu Sura Ra’d; 13:4).

Kutoka kwa Abdullah bin Muhammad bin Aqiil, kutoka kwa Jabir, amesema: “Nilimsikia Mtume wa Mewenyezi Mungu (s.a.w.w.) akimwambia Ali: “Watu wanatokana na miti tofauti. Na mimi na wewe tunatokana na mti mmoja.”61   Ameiandika Humawi katika kitabu Faraidus-Samtwayn Juz. 1, Uk. 238, Mlango wa 63.   Al-Haskaniy ameipokea katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil, Hadithi ya395. Na ameipokea Ibnu Asakir katika kitabu Taarikh Damashqi Juz. 1, Uk. 142,Hadithi ya 177, Chapa ya Pili.

60. 61.

62

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 62

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d 13:7).

Kutoka kwa Said bin Jubair, kutoka kwa Ibnu Abbas, amesema: “Ilipoteremka Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake na kusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji.’ Akaashiria mkono wake kwenye bega la Ali na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji. Kupitia kwako wataongoka wenye kutaka kuongoka baada yangu.”62 Kutoka kwa Sufyan Ath-Thawriy, kutoka kwa Abu Is’haqa, kutoka kwa Zaid bin Yatbau, kutoka kwa Hudhayfa amesema kwamba: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Mkimwacha Ali awatawale mtamkuta ni Kiongozi mwongozaji.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale ambao wameamini na wakafanya matendo mema, raha ni yaona marejeo mazuri.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:29).

Kutoka kwa Abu Ja’far amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu aliulizwa kuhusu kauli yake (s.w.t.): “…raha ni yao na marejeo mazuri.” akasema: “Tuba ni mti ambao shina lake limo ndani ya nyumba yangu na matawi yake yamewafikia watu wa Peponi.” 62.

Ibu Hajar al-Asqalaniy ameiandika katika kitabu Lisanul-Mizan Juz. 2, Uk. 99. 63

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 63

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kisha akaulizwa tena mara nyingine akasema: “Ni mti wa peponi shina lake limo ndani ya nyumba ya Ali na matawi yake yamewafikia watu wa peponi.” Akaambiwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mwanzo tulikuuliza ukasema: “Tuba ni mti shina lake limo ndani ya nyumba yangu na matawi yake yamewafikia watu wa Peponi.” Tukakuuliza tena ukasema: “Ni mti wa peponi shina lake limo ndani ya nyumba ya Ali na matawi yake yamewafikia watu wa peponi.” Vipi hili? Akajibu: “Hakika nyumba yangu na nyumba ya Ali kesho ni moja sehemu moja.”63 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale ambao wamekufuru wanasema wewe hukutumwa. Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi na yule mwenye elimu ya Kitabu.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:43).

Abdullah bin Atau amesema: “Nilikuwa nimeketi na Abu Ja’far msikitini ndipo nikamwona Ibnu Abdullah bin Salam pembeni. Nikamwambia Abu Ja’far: “Wanadai eti ambaye ana elimu ya Kitabu ni Abdullah bin Salam. Akasema: “Hakika huyo (mwenye elimu ya Kitabu) ni Ali bin Abu Talib.”64 I bnu al-Batriq ameiandika katika kitabu Khasaisul-Wahyi al-Mubin Uk. 209, Chapa ya Pili, Mlango wa Tatu. Na pia kaiandika Tabarasiy katika Tafsiri yake Majmaul-Bayan anapoifasiri Aya hii. Na kaiandika al-Irbaliy katika kitabu Kashful Ghummah Juz. 1, Uk. 323. 64.   Ameiandika Ibnu al-Mghzaliy katika kitabu chake al-Manaqib, Hadithi ya 258 Uk. 313. 63

64

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 64

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa Abu Umar Zadhan, kutoka kwa Hudhayfa kuhusu kauli yake (s.w.t.): “…na yule mwenye elimu ya Kitabu.” Alisema: “Huyo ni Ali bin Abu Talib.”65

SURA MARYAM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” (Qur’ani Tukufu Sura Maryam; 19:96).

Kutoka kwa al-Barau bin Azib amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali bin Abu Talib: “Ewe Ali, sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwako na niwekee mapenzi katika nyoyo za waumini.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.”66

SURA TWAHA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Twaha.” (Sura Twaha: 1). Amesema Ja’far bin Muhammad as-Sadiq (a.s.): “Twaha: Ni utakaso wa Ahlul-Baiti wa Muhammad.” Kisha akasoma: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).   Ameiandika Abu Naiim al-Asfahaniy katika kitabu an-Nuru al-Mushtaalu Fii Maa unzila Minal-Qur’an Fii Ali, Uk. 152, Sura ya kumi na tisa. 66.   Ameiandika Humawi katika Juz. 1, Uk. 8, Mlango wa 14. 65.

65

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 65

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AN-NUR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Katika nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameruhusu ziinuliwe na kutajwa humo jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nur; 24:36).

Akasimama mtu mmoja na kumuuliza: “Ni nyumba zipi hizi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Akasema: “Nyumba za Manabii.” Abu Bakr akasimama na kusema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nyumba hii ni miongoni mwazo, nyumba ya Ali na Fatima?” Akajibu: “Ndio ni miongoni mwazo bali ndio iliyo bora kuliko ­nyingine.”

SURA AL-FURQAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Naye ndiye aliyemuumba mwanadamu kutokana na maji na akamjaalia kuwa na nasaba na ukwe. Na Mola wako ni Mwenye uwezo.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Furqan; 25:54).

Amesema: Iliteremka ikimuhusu Mtume (s.a.w.w.) na Ali bin Abu Talib. Mtume alimuozesha Ali kwa Fatima, naye ni mtoto wa ami yake na mume wa binti yake, hivyo wao wawili wakawa na nasaba na ukwe. 66

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 66

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA ASH-SHU’ARAA

“Na uwonye jamaa zako walio karibu.” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shu’araa; 26:214).

Kutoka kwa Abu Is’haqa amesema: Ilipoteremka Aya hii: “Na uwonye jamaa zako walio karibu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu aliwakusanya watoto wa Abdul-Muttalib kipindi hicho wakiwa ni wanaume arobaini. Mtu mmoja kati yao alikuwa akila mbuzi mzima. Akamwamuru Ali aandae mguu wa mbuzi akautengeneza chakula kisha Mtume akasema: “Karibuni kwa jina la Mwenyezi Mungu. ” Watu wakakaribia na wakala mpaka wakatosheka. Kisha baada ya hapo akaomba maziwa akanywa funda moja kisha akawaambia: “Kunyweni kwa jina la Mwenyezi Mungu.” Wakanywa mpaka wakatosheka. Ndipo Abu Lahabi akawatangulia kwa kusema: “Huu ndio uchawi aliowaroga mtu huyu.” Mtume akanyamaza hakusema chochote siku hiyo. Kisha siku iliyofuata waliwaita na kuwaandalia chakula na kinywaji mfano wa kile. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaonya, akasema: “Enyi wana wa Abdul-Muttalib! Hakika mimi ni mwonyaji kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na ni mbashiri wa yale ambayo hakuna yeyote aliyewaletea. Hakika mimi nimewaletea kheri ya dunia na akhera. Silimuni na mnitii mtaongoka. Na ni nani ataniunga mkono na kunisaidia awe mrithi wangu, wasii wangu na khalifa wangu kwa watu wangu na anilipie deni langu.” Kaumu wakakaa kimya. Akarudia wito huo mara tatu. Mara zote hizo kaumu walikaa kimya na Ali akisema: “Mimi.” Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Wewe.” Kaumu wakanyanyuka na 67

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 67

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

hali wakimwambia Abu Talib: “Bila shaka amekuamuru umsikilize na kumtii mwanao.”

SURA AN-NAML Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Suleiman alimrithi Daud. Na akasema: Enyi watu! Tumefunzwa usemi wa ndege. Na tumepewa kila kitu. Hakika hii ni fadhila iliyo dhahiri.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Naml; 27:16).

Ja’far bin Muhammad as-Saddiq amepokea kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake, kutoka kwa Hasan bin Ali, amesema: “Kipozamataza – aina ya ndege – aliapo huwa anasema: Ewe ­Mungu wangu! Walaani wenye kuwabughudhi aali Muhammad.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Watakaokuja na wema watapata bora kuliko hayo. Nao ­watasalimika na.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Naml; 27:89).

Kutoka kwa Abu Daud as-Sabuiy, kutoka kwa Abdullah banalJadliy, amesema: Niliingia kwa Ali bin Abu Talib akaniambia: “Ewe Abdullah nikueleze wema ambao atakayeuleta Mwenyezi Mungu atamwingiza peponi?” Nikamwambia ndio. Akasema: Wema huo ni kutupenda sisi na uovu ni kutubughudhi sisi.”

68

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 68

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ­ chafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa u kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Amesema: Bakru bin Yahya bin Rayyan al-Askari ­ametusimulia, amesema: Ametusimulia Aamash kutoka kwa Atia, kutoka kwa Abu Said al-Khudri, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka ­kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” imeteremka kwa ajili ya ­watano: Kwa ajili yangu, Ali, Hasan, Husein na Fatima.”67 Ametusimulia aliyemsikia Ummu Salama akisema kwamba: “Mtume (s.a.w.w.) alikuwa nyumbani kwake ndipo ­akaja Fatima akiwa na chungu chenye uji na kuingia nacho kwa Mtume. Mtume akamwambia mwite mumeo na ­wanao. Alikuja Ali, Hasan na Husein wakaingia kwa Mtume na wakaketi wakinywa uji huo na hali Mtume akiwa juu ya kitanda chake cha mbao kilichotandikwa kishamia cha Khaibari. Nikiwa chumba kingine naswali ghafla Mwenyezi ­Mungu aliteremsha Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa ­nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”   Ameipokea al-Haythami katika Majmauz-Zawaid, Mlango wa Fadhila za Ahlul-Baiti, Juz. 9, Uk. 167. Na al-Wahid katika kitabu chake Asbabun-Nuzuul Uk. 267.

67.

69

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 69

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Nikaingiza kichwa chumbani kwa Mtume na kumwambia: Je na mimi ni pamoja nanyi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Hakika wewe upo katika kheri. Bila shaka wewe upo katika kheri.”68 Kutoka kwa Awamu bin Hawshab, amesema: “Amenisimulia mtoto wa ami yangu toka kizazi cha Harith bin ­Taymullah anayeitwa Mujmiu, amesema: Niliingia na mama yangu kwa Aisha, mama yangu akamuuliza kwa kusema: “Umeona ulikuwa sawa kutoka na kwenda ­kupigana Vita vya Jamali?” Akasema: Hakika ilikuwa na makadara kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kisha akamuuliza kuhusu Ali. Aisha akasema: “Umeniuliza kuhusu mtu aliyekuwa akipendwa sana na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuliko watu wote. Mume aliyekuwa akipendwa sana na Mtume wa Mwenyezi Mungu ­kuliko watu wote. Nilimuona Ali, Fatima, Hasan na Husein wamefunikwa nguo na Mtume wa Mwenyezi Mungu ­kisha akasema: ‘Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu na ndugu zangu wa karibu, hivyo waondolee uchafu na uwatakase kabisa.’ Nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je mimi ni miongoni mwa ndugu zako? Akasema: ‘Wewe ni mtu baki hakika wewe utaelekea kwenye kheri.’69 Kutoka kwa Abdullah bin Ja’far at-Twayyar, kutoka kwa baba yake, amesema: “Mtume alipoitazama rehema ikishuka toka mbinguni (mvua) alisema: ‘Ni nani atakayeniitia?’ alisema mara mbili. Zainab akasema: “Mimi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu.”   Ameipokea Ahmad bin Hanbal katika kitabu al-Fadhail Uk. 79, Hadithi ya 11, Chapa ya Kwanza. Na katika kitabu al-Musnad Uk. 292. 69.   Ameiandika Ibn Asakir katika Tarikh Damashqi Juz. 2, Uk. 163, Chapa 2, Hadithi 650. 68.

70

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 70

2/14/2018 12:11:35 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Akasema: Niitie Ali, Fatima, Hasan na Husein. ­Akamweka Hasan kuliani kwake, Husein kushotoni kwake na Ali na Fatima usoni kwake. Kisha akawafunika kishamia cha Khaibar na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu kila Nabii ana ndugu na hawa ndio ndugu zangu.” Ndipo ­Mwenyezi Mungu akateremsha: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa ­nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Zainab akasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi niingie pamoja nanyi?’ Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Baki hapo hapo, bila shaka inshaallah utaelekea katika kheri.”70 Kutoka kwa Awzaiy, kutoka kwa Shaddad Abu Ammar, amesema: “Niliingia kwa Wathila bin al-Asqau nikamkuta ameketi na baadhi ya watu. Ndipo walipomtaja Ali na kumkashifu nami nikamkashifu. Walipoondoka (Wathila) akaniambia: ‘Hivi kweli umemkashifu mtu huyu?!!!’ Nikamwambia nimeona watu wanamkashifu nami nikashirikiana nao kumkashifu. Akaniambia je nikueleze yale niliyosikia kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)? ­Nikasema ndio nieleze. Akasema: “Nilikwenda kwa Fatima nikimuulizia Ali. Fatima akanijibu kwamba ameelekea kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), nikaketi na punde Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akaja na kuingia akiwa pamoja na Ali, Hasan na Husein akiwa amemshika kila mmoja wao (Hasan na Husein) mkono. Akawaita Ali na Fatima na kuwakalisha mbele yake. Na akamkalisha Hasan na Husein kila mmoja pajani kwake. Kisha akawafunika nguo yake na kusoma   Ameipokea Ibnu al-Mughaziliy katika kitabu al-Manaqib Uk. 305. Na al-Haythamiy katika Majmauz-Zawaid Juz. 9, Uk. 167.

70.

71

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 71

2/14/2018 12:11:36 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Kisha akasema: Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio watu wa nyumba yangu. Na watu wa nyumba yangu ndio wenye haki zaidi (kuliko mtu baki).”71 Kutoka kwa Zayd bin Arqam, amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nawaapizeni kwa Mwenyezi Mungu kuhusu Ahlul-Baiti wangu. Nawaapizeni kwa Mwenyezi Mungu kuhusu Ahlul-Baiti wangu.” Kutoka kwa Nafiu Abu Daud, kutoka kwa Abul-Hamrau, amesema: Niliishi Madina miezi tisa kama vile ni siku moja (yaani sikutoka nje ya Madina muda wa miezi tisa). Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa anakuja kila siku asubuhi na kusimama kwenye mlango wa Ali na Fatima na kusema: “Swala. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”72 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).

Ametupa habari Abdurahman bin Abu Layala, amesema: Amenisimulia Kaab bin Ajara, amesema: Ilipoteremka: “Hakika Mwenyezi   Ameiandika Ibnu Hanbal katika kitabu chake al-Musnad Juz. 4, Uk. 107. Na katika kitabu chake al-Fadhail Uk. 66, Hadithi ya 102, Chapa ya Kwanza. 72.   Ameipokea Dhahabi katika kitabu chake Mizanul-Iitidal Juz. 2, Uk. 381. 71.

72

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 72

2/14/2018 12:11:36 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” Nilisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu ni ipi namana ya kukusalia? Mtume akasema: “Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.” Kutoka kwa Ibnu Mas’ud al-Ansariy alisema: “Mtume alikuja na kutukuta tumeketi katika baraza la Saad bin Ubada. Bushru bin Saad akamwambia: Mwenyezi Mungu ametuamuru tukuswalie ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi ni vipi tutakavyokusalia?” Mtume akakaa kimya mpaka tukatamani kwamba asingemuuliza. Kisha akasema (s.a.w.w.):

Semeni: “Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim katika walimwengu, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.” Na salamu ni kama mlivyojifunza. Kauli ya Mwenyezi Mungu:

73

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 73

2/14/2018 12:11:36 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha. Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kumbwa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:57-58).

Muqatil amesema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali. Hiyo ni pale ­baadhi ya wanafiki walipokuwa wakimuudhi na kumtukana.”73

SURA YASIN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ikasemwa: Ingia peponi! Akasema: Laiti watu wangu wangejua, jinsi Mola wangu alivyonighufuria na akanifanya katika waheshimiwa.” (Qur’ani Tukufu Sura Yasin; 37:130).

Kutoka kwa Abdurahman bin Abu Layla, kutoka kwa baba yake, amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Vinara wa umma ni watatu hawa-jamkufuru Mwenyezi Mungu hata kidogo: Ali bin Abu Talib, rafiki wa Yasin na muumini wa aali Firaun. Wao ndio wasadikishaji wakubwa: Habib an-Najar muumini wa aali Yasin, Hazbil muumini wa aali Firaun na Ali bin Abu Talib naye ndiye mbora wao.”74

SURA AS-SAFFAT Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amani kwa Ilyasin.” (Qur’ani Tukufu Sura as-Saffat; 37:130).   Ameipokea al-Wahidiy katika kitabu chake Asbabun-Nuzuul Uk. 273.   Ameipokea Ibnu Asakir katika kitabu Taarikh Damashqi Juz. 2 Uk. 282, Hadithi ya 813.

73. 74.

74

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 74

2/14/2018 12:11:36 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Atakayesoma Aali Yasin kwa kukokoteza basi amekusudia Aali Muhammad.75

SURA AL-MU’MIN (AL-GHAFIR) Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale wanaobeba Arshi, na wanaoizunguka, wanamsabihi kwa kumuhimidi Mola wao, na wanamuamini na wanawaombea msamaha walioamini. Mola wetu! Umekienea kila kitu kwa rehema na ujuzi. Basi wasamehe ambao wametubu na wakaifuata Njia Yako, na waepushe na adhabu ya Jahannamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mu’min (al-Ghafir); 40:7).

Amepokea Said bin Jubair kutoka kwa Abul-Hamrau mtumishi wa Mtume (s.a.w.w.), amesema: “Nilimsikia Mtume (s.a.w.w.) akisema: “Siku nilipopelekwa mbinguni niliona nguzo ya Arshi imenakishiwa kwa: Hapana Mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu mmoja. Na hakika Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Nimempa nguvu kupitia Ali na nimemsaidia.”76   Kuna riwaya nyingi zimepokewa zikisema kwamba Aali Yasin katika Aya hii ndio hao hao Aali Muhammad (a.s.). al-Haskaniy amepokea Hadithi saba zikiwa na maana hii, kuanzia Hadithi ya 791 mpaka ya 797. Na al-Irbaliy naye kazitaja katika kitabu chake Kashful-Ghumma Juz. 1, Uk. 324 katika anwani inayozungumzia Aya zilizoteremka kumuhusu Ali. Unaweza kurejea huko. 76.   Al-Muttaqi al-Hindiy ameipokea ndani ya kitabu chake Kanzul-Ummal Juz. 6, Uk. 158. 75.

75

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 75

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Amepokea Said bin Jubair kutoka kwa Abul-Hamrau mtumishi wa Mtume (s.a.w.w.), amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hasan na Husein ni hereni za Arshi na si zile za kutungikwa (za kuvaa na kuvuliwa bali ni za asili zisizoachana na Arshi).”

SURA ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura 42:23).

Kutoka kwa Said bin Jubair, kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Ilipoteremka: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” walimuuliza: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa ndugu ambao ni imewajibishwa juu yetu kuwapenda. Akasema: “Ali, Fatima na watoto wake wawili.”77 Kutoka kwa Amru bin Musa, kutoka kwa Zayd bin Ali bin Husein kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu yake Ali bin Abu Talib, amesema: “Nilimshitakia Mtume kuhusu husuda za watu dhidi yangu. Akasema: ‘Hivi huridhii kuwa mmoja kati ya wanne. Wa kwanza kuingia Peponi. Ni Mimi, Wewe, Hasan, Husein na wake zetu wakiwa kuliani kwetu na kushotoni kwetu. Na wajukuu zetu wakiwa nyuma ya wake zetu. Na wafuasi wetu wakiwa nyuma yetu.”’   Ameiandika al-Mughzali katika kitabu chake al-Manaqib Juz. 352, Uk. 307. Na al-Fayruz Abad katika kitabu chake Fadhailul-Khamsa Juz. 1, Uk. 250.

77.

76

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 76

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa Shahru Hawshab, kutoka kwa Ummu Salama, kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alimwambia Fatima: “Niitie mume wako na wanao.” Wakaja na ndipo akawafunika kishamia cha kutoka Fadak, akainua mikono yake juu yao na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio aali Muhammad, ziweke rehema zako na baraka zako juu ya Muhammad na aali Muhammad. Hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.” Nikainua kishamia ili niingie, ghafla akakivuta na kusema: “Hakika wewe u katika kheri.” Abu Hazim amepokea kutoka kwa Abu Huraira, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtazama Ali, Fatima, Hasan na Husein, kisha akasema: “Mimi ni mwenye kumpiga vita yule mwenye kuwapigeni vita. Na ni mwenye kuishi naye kwa amani yule mwenye kuishi nanyi kwa amani.” Kutoka kwa as-Sadiy, kutoka kwa Abu Daylam, amesema: “Alipoletwa Ali bin Husein na hali ni mateka na kusimamishwa katika barabara kuu ya Damascus alisimama mzee mmoja kati ya watu wa Sham, akasema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye amewauwa na kuwang’oeni na kung’oa mzizi wa fitina.” Ali bin Husein akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu: “Ndio.” Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’Akajibu: “Nimewahi kusoma Qur’ani na sijawahi kusoma Aali Haa Miim.” Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...”’ Mzee akasema: ‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’” Ametusimulia Ali bin Musa Ridha (a.s.), amesema: “Amenisimulia baba yangu Musa bin Ja’far (a.s.), amesema: Ametusimulia baba yangu Ja’far bin Muhammad 77

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 77

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

as-Sadiq (a.s.), amesema: “Pete ya baba yangu Muhammad bin Ali (a.s.) ilikuwa imenakishiwa kwa nakshi ya: Dhana yangu nzuri ni kwa Mwenyezi Mungu, kwa Nabii mwaminiwa, kwa wasii mwenye ihisani na kwa Husein na Hasan.” Muhammad bin Abdurahman az-Zaafaraniy, amesema: “Aliniapia Ahmad bin Ibrahim al-Jarjaniy, amesema: Mansur al-Faqihu, amesema: “Ikiwa kwa kuwapenda kwangu watano faradhi zangu hutukuka; na kuwachukuia kwangu wenye kuwafanyia uadui ni urafidhi, basi mimi ni rafidhi.” Kutoka kwa Anas bin Malik amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: “Sisi ni kizazi cha ­Abdul-Muttalib mabwana wa watu wa Peponi: Mimi, Hamza, Ja’far, Ali, Hasan, Husein na Mahdi.” Ali bin Musa Ridha (a.s.) amesema: “Amenisimulia Baba yangu Musa bin Ja’far (a.s.), amesema: Amenisimulia Baba yangu Ja’far bin Muhammad (a.s.), amesema: Amenisimulia baba yangu Muhammad bin Ali (a.s.), amesema: Amenisimulia baba yangu Ali bin Husein (a.s.), amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Pepo imeharamisha juu ya yule aliyewadhulumu Ahlul-Baiti wangu na akaniudhi kwa kuwaudhi kizazi changu. Yeyote atakayemtendea wema yeyote miongoni mwa kizazi cha Abdul-Muttalib na ikawa hajalipwa kutokana na wema huo, basi mimi nitamlipa kesho atakapokutana nami Siku ya Kiyama.” Ametusimulia Yaala bin Ubaydu kutoka kwa Ismail bin Abu Khalid, kutoka kwa Qaysu bin Abu Hazim, kutoka kwa Jarir bin Abdullah al-Bajliy, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi 78

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 78

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

amekufa na hali ni shahidi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ameghufuriwa. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ametubia. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ni muumini aliyekamilika kiimani. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali malaika wa mauti ameshambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakir. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atamfungulia milango miwili ya Pepo kaburini. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad atasindikizwa Peponi kama biharusi asindikizwavyo kwenda nyumbani kwa mumewe. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amefia ndani ya Sunna na Jamaa. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad atakuja Siku ya Kiyama na hali imeandikwa baina ya macho yake mawili: Amekata tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad basi amekufa na hali ni kafiri. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu ya Pepo.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na anayefanya wema tutamzidishia wema. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwingi wa shukrani.” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23). 79

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 79

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa as-Sadiy, kutoka kwa Abu Malik, kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na anayefanya wema tutamzidishia wema.” amesema: “(Wema hapo) Ni kuwapenda aali Muhammad.”78

SURA AZ-ZUKHRUF Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na waulize Mitume wetu tuliowatuma kabla yako: Je, tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Mwingi wa rehema.” (Qur’ani Tukufu Sura az-Zukhruf; 43:23).

Kutoka kwa Abdullah bin Mas’ud, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: “Malaika aliniijia na kuniambia: ‘Ewe 316. Na al-Haskaniy katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil, Hadithi ya 846. Muhammad! Waulize tuliowatuma kabla yako miongoni mwa Mitume, tuliwatuma walinganie nini.’ Nikasema uliwatuma walinganie nini? Akasema: ‘Walinganie uwalii wako na uwalii wa Ali bin Abu Talib.”’79

SURA AD-DUKHAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Ameipokea al-Mughazaliy katika kitabu chake al-Manaqib, Hadithi ya 360 Uk.   Ameipokea Ibnu Asakir katika kitabu chake Taarikh Damashqi Juz. 2, Uk. 98, Hadithi ya 602, Chapa ya Pili.

78. 79.

80

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 80

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Mbingu na ardhi hazikuwalilia; wala hawakupewa muda.” (Qur’ani Tukufu ad-Dukhan; 44:29).

As-Sadiy amesema: “Alipouwawa Husein bin Ali (a.s.) mbingu ilimlilia na kilio chake ni wekundu wake.” Ametupa habari Abu Bakr al-Jawzaqiy kutoka kwa Hisham, kutoka kwa Muhammad bin Sirin, amesema: “Tulipewa habari kwamba wekundu uliyopo kwenye mawingu haukuwapo awali mpaka pale Husein (a.s.) alipouwawa.” Ametusimulia Hammad bin Salma, amesema: “Ametupa habari Sulaymu al-Qadhi amesema: “Tulinyeshewa na mvua ya damu pindi Husein alipouwawa.”

SURA AL-AHQAF Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Basi leo mtapewa adhabu ya ­fedheha….” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahqaf; 46;20). Na Kauli ya Mwenyezi Mungu: “….Bali imewapotea, na huo ndio uwongo wao na waliyokuwa wakiyatunga.” (Qur’ani Tukufu Sura ­al-Ahqaf; 46:28). Kutoka kwa Thawbani huria wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa anaposafiri mtu wa mwisho kumuaga ni mtu toka katika ndugu zake. Na wa kwanza atakayeingia kwake kumsalimu baada ya kurejea ni Fatima. Aliporudi toka kwenye moja ya vita alisimama mlangoni kwa Fatima na ghafla akamwona Hasan na Husein wamevaa pingu mbili za fedha. Akarudi na hakuingia kwake. Fatima alivyoona hivyo akadhani kwamba hakuingia kutokana na aliyoyaona. Akatoka ndani na kuwavua watoto pingu. Watoto wakalia, ndipo akaikata na kuigawa vipande viwili kati yao. Wakaenda kwa Mtume 81

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 81

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wa Mwenyezi Mungu na hali wakilia, Mtume wa Mwenyezi Mungu akaichukua pingu ile toka kwao na kusema: “Ewe Thawbani nenda na hii kwa watoto wa fulani (familia moja ya huko Madina) na umnunulie Fatima mkufu na bangili za meno ya ndovu.” Na akasema: “Hakika hawa ni Ahlul-Baiti wangu, sipendi wale vizuri vyao katika maisha ya dunia.”

SURA AL-FATH Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Mwenyezi Mungu amekuahidini ngawira nyingi mtakazozichukua, kisha akakutimizeni haya, na akaizuia mikono ya watu isikufikieni, na ili iwe dalili kwa waumini na kukuongozeni njia iliyonyooka.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Fath 48:20).

Kutoka kwa Ibnu Jarir, amesema: “Ametusimulia Ibnu Bashari, amesema: Ametusimulia Muhammad bin Ja’far, amesema: Wametusimulia baadhi yao, wamesema: Tulitoka pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kwenda Khaibar usiku. Amir bin al-Ukui alikuwa pamoja nasi, ndipo mtu mmoja akamwambia, ewe Amir bin al-Kui mbona hautusikilizishi mashairi yako. Amir alikuwa ni malenga hodari basi akawa anawaghania watu huku akisoma mashairi.” Msimuliaji anasema: “Tukawazingira mpaka tukapatwa na njaa kali kisha Mwenyezi Mungu akatupa ushindi. Hiyo ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimkabidhi bendera Umar na wakaondoka pamoja naye wale waliofanikiwa kwenda naye 82

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 82

2/14/2018 12:11:37 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

hadi wakafika Khaibar, kisha Umar na jamaa zake wakakimbia. Wakarejea kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) huku jamaa zake wakimshutumu kwa uoga naye akiwashutumu wao kwa uoga. Kipindi hicho Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa anasumbuliwa na maumivu ya kichwa hivyo hakuweza kutoka kwenda kuwaeleza chochote watu. Abu Bakr akachukua bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) naye alikwenda akapambana mapamabano makali sana. Kisha akarejea na ndipo akaichukua Umar tena na kupambana mapambano makali kuliko alivyopamabana katika mapambano ya kwanza. Kisha akarejea. Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akapewa habari hizo, akasema: “Hakika kesho nitamkabidhi bendera mtu ambaye anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanampenda. Ataichukua kwa nguvu.” Na hapo hakuwepo Ali. Ilipofika kesho Abu Bakr, Umar na makuraishi kwa ujumla walitamani jambo hilo kila mmoja akitaraji awe ndiye mtu huyo. Mtume wa Mwenyezi Mungu akamtuma Salma bin al-Kui amwite Ali. Akamwita, na Ali alikuja akiwa juu ya ngamia wake mpaka akasogea karibu mno na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) hali akiwa anaumwa macho. Salma anasema: “Nilikuja naye nami nikimwongoza mpaka kwa Mtume (s.a.w.w.). Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Vipi hali yako?” Akajibu: “Nimepatwa na maradhi ya macho.” Akamwambia: “Sogea karibu yangu.” Akasogea na ndipo akamtemea mate machoni basi kuanzia muda huo hakuugua macho mpaka anaingia kaburini. Kisha akamkabidhi bendera, akaondoka na bendera huku akiwa amevaa joho la rangi ya urujuani nyekundu. Akafika mji wa Khaibar 83

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 83

2/14/2018 12:11:38 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

na ndipo Marhab aliyekuwa mlinzi wa ngome akatoka na hali amevaa dirizi (deraya) ya rangi ya njano na juu ya kichwa chake kavaa jiwe alilolitoboa mfano wa yai huku akisema:

“Khaibar imeshajua kwamba hakika mimi ni Marha; mwenye silaha kali na komandoo mzoefu. Pindi moto wa vita unapowashwa, mara hufuma mshale na mara hupiga. Himaya yangu huwa haikaribiwi.” Ali akajitokeza kumkabili naye akisema:

Mimi ndiye ambaye mama yangu alinipa jina la Haidari (Simba) Kama simba pori, shujaa mkali. Nitakuuweni kwa upanga wangu mauwaji ya kuteketeza. Wakapigana mapigo mawili na ndipo Ali akamuwahi na kumpiga pigo moja lililopasua jiwe na dirizi na kukipasua kichwa vipande viwili mpaka upanga ukafika kwenye megego. Na hatimaye aliuteka mji na ushindi ukapatikana mikono mwake. Abu Rafiu huria wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) anasema: “Tulitoka pamoja na Ali pindi Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipomtuma akiwa amemkabidhi bendera yake. ­Alipoikaribia ngome walitoka wanangome na akapambana nao. Ndipo mtu mmoja miongoni mwa mayahudi akampiga na hatimaye 84

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 84

2/14/2018 12:11:38 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ngao yake ikadondoka. Ali akang’oa mlango wa ngome na kuugeuza ngao yake, basi uliendelea kuwa mikononi mwake kama ngao na hali yeye akipigana mpaka Mwenyezi Mungu alipompa ushindi. Baada ya kumaliza aliutupa chini, hakika (lau ungekuwepo) ungeniona nikiwa mmoja katika kundi la watu saba tukijitahidi kuugeuza mlango huo lakini hatuwezi.” Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu na walio pamoja naye ni imara mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao….” (Sura al-Fat’ha: 29). Ahmad bin Yazid ad-Daybajiy amesema: Ametusimulia alMadaniy kutoka kwa Zayd, kutoka kwa Ibnu Umar, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Ewe Ali! Wewe ni mtu wa Peponi na wafuasi wako ni watu wa Peponi.”

SURA AR-RAHMAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Amezikutanisha bahari mbili. Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Rahman; 55:19-20).

Ametusimulia Abu Hudhuyfa kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Sufyan at-Thawri amesema kuhusu “Amezikutanisha bahari mbili. Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.” Kwamba ni Fatima na Ali. Na akasema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Katika hizo mbili hutoka lulu na marijani.” (Sura Rahman: 22): kwamba ni Hasan na Husein. Na “Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.” Ni Muhammad. 85

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 85

2/14/2018 12:11:38 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Karibu tutawakusudieni, enyi vizito viwili.” (Qur’ani Tukufu arRahman; 55:31).

Mtume (s.a.w.w.) alisema: “Bila shaka mimi ni mwenye kuwaachia vizito viwili kati yenu: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu.” Akavijaalia kuwa ni vizito viwili kwa sababa ya utukufu ulivyonao na thamani iliyonavyo.

SURA AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemeza hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Mujahid amesema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee, alitoa sadaka ya dinari. Ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.).” Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee alisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayei86

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 86

2/14/2018 12:11:38 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

fanyia kazi baada yangu, nayo ni: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemeza hayo ni bora kwenu na ni safi sana…..” ilifaradhishwa kisha hukumu yake ikafutwa.” Ibnu Umar alisema: “Ali alikuwa na mambo matatu ambayo kuwa nalo moja kati ya hayo ni jambo nilipendalo mno kuliko kuwa na ngamia mwekundu: Kuozwa Fatima, kukabidhiwa bendera Siku ya Khaibar na Aya ya kuongea siri na Mtume.”

SURA AT-TAGHABUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni jaribio, na kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Taghabun; 64.15).

Kutoka kwa Husein bin Waqid Kadhi wa Muruwu, amesema: Abdullah bin Barida amenisimulia kutoka kwa baba yake, amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akitoa hotuba na ghafla wakaja Hasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuamka, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akateremka toka mimbarini akawafuata na kuwachukua na kuwaweka mapajani mwake juu ya mimbari, kisha akasema: ‘Mwenyezi Mungu amesema kweli. Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni jaribio, nilipowaona hawa wawili sikuweza kuvumilia.”

SURA AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake, na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim 66:4). 87

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 87

2/14/2018 12:11:38 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa Muhammad bin Ja’far bin Muhammad bin Ali bin Husein bin Ali bin Abu Talib (a.s.) amesema: “Amenisimulia mtu mmoja mwaminifu akiivusha toka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.), amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “…na waumini wema…”: ‘Ni Ali bin Abu Talib.’”80 Kutoka kwa Musa bin Ja’far, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu zake (a.s.), kutoka kwa Asmau binti Umaysi amesema: “Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: ‘Na waumini wema ni Ali bin Abu Talib.’”81 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Mariam binti Imran aliyejilinda tupu yake….” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:12).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: “Kati ya wanaume wamekamilika wengi na wala hawajakamilika kati ya wanawake ila wanne: Asia binti Muzahim mke wa Firaun, Mariam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.”

SURA AL-HAQQA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Haqqa; 69:12).   Ameiandika Ibnu Hajar al-Haythamiy katika kitabu as-Swawaiqul-Muhriqah Uk. 144.   Ameipokea al-Humawi katika kitabu chake Faraidus-Samtwayni Juz. 1 Uk. 363, Chapa ya Kwanza, Mlango wa 67, Hadithi ya 290.

80. 81.

88

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 88

2/14/2018 12:11:39 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa Abu Hamza at-Thumali amesema: “Amenisimulia Abdullah bin Hasan, amesema: Ilipoteremka Aya hii: “Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nilimwomba Mwenyezi Mungu sikio lako alifanye hivyo ewe Ali.’’ Ali akasema: “Baada ya hapo sikuwahi kusahau chochote na wala sikupasa kusahau.”82 Kutoka kwa Burayda al-Aslamiy amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ameniamuru nikusogeze karibu nisikutenge mbali, na nikuelimishe nawe usikie vilivyo. Na Mwenyezi Mungu amehakikisha unasikia vilivyo.”

SURA AL-MA’ARIJ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea. Juu ya makafiri, hapana awezaye kuizuia.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ma’arij; 70:1-2).

Sufyan bin Uyayna aliulizwa kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Muulizaji aliuliza” iliteremka kumhusu nani? Akasema: “Umeniuliza suala ambalo hakuna aliyeniuliza kabla yako. Baba yangu alinisimulia kutoka kwa Ja’far bin Muhammad kutoka kwa baba zake, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipofika Ghadir Khum aliwaita watu wakakusanyika. Akaunyanyua mkono wa Ali na kusema: “Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali ni mwenye mamlaka juu yake.”   Al-Haskaniy ameiandika katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil.

82.

89

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 89

2/14/2018 12:11:39 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Habari hizo zikazagaa na kuenea miji mbalimbali, ndipo zikamfikia al-Harith bin Nuuman al-Fihriy. Akaja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akiwa amepanda ngamia wake. Alipofika Abtahu aliteremka na kumfunga ngamia wake kisha akamfuata Mtume katikati ya kundi la masahaba zake. Akasema: “Ewe Muhammad! Umetuamrisha tushahidilie kwamba hapana Mungu wa haki ila Allah na kwamba wewe ni Mtume wa Allah, tumekubali hilo kutoka kwako. Umetuamuru tuswali Swala tano tumekubali hilo kutoka kwako. Umetuamrisha tutoe Zaka tumekubali. Umetuamrisha kuhiji tumekubali. Umetuamrisha tufunge mwezi mzima tumekubali. Kisha haujatosheka kwa haya yote mpaka umenyanyua mikono ya binamu yako na kumfanya bora juu yetu ukasema: ‘Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali ni mwenye mamlaka juu yake.’ Je jambo hili ni kutoka kwako binafsi au ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu?” Mtume akasema: “Naapa kwa yule ambaye hapana Mungu ila Yeye, hakika hili ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Al-Harith akageuka na kuelekea kwenye mnyama wake huku akisema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Ikiwa ayasemayo ni haki basi tuteremshie mvua ya mawe kutoka mbinguni na utuletee adhabu iumizayo.” Kabla hajamfikia mnyama wake Mwenyezi Mungu akamwangushia jiwe utosini na likatokea nyumani kwake akadondoka hapo hapo na kuuwawa. Mwenyezi Mungu akateremsha: “Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea. Juu ya makafiri, hapana awezaye kuizuia.”83   Ameipokea Ibnu Batrik katika sura ya pili ya kitabu chake Khaswaisul-Wahyi al-Mubin Uk. 31, Chapa ya Kwanza.

83.

90

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 90

2/14/2018 12:11:39 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA AL-MUDDATHIR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Kila nafsi itafungika kwa ilizozichuma. Isipokuwa watu wa kheri.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Muddathir; 74:38-39).

Kutoka kwa Abu Hamza at-Thumali kutoka kwa Abu Ja’far alBaqir (a.s.) amesema: “Sisi na wafuasi wetu ndio watu wa kheri.”84

SURA AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Al-Haskaniy ameiandika katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil Juz. 2, Uk. 388, ­Hadithi ya 1038.

84.

91

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 91

2/14/2018 12:11:39 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake itaenea. Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani. Hakika sisi tunaogopa kutoka kwa Mola wetu siku yenye shida na taabu. Basi Mwenyezi Mungu atawalinda katika shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema na furaha. Na atawapa mabustani na hariri kwa sababu walisubiri. Humo wataegemea viti vya enzi humo hawataona jua wala baridi.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:7-13).

Alitusimulia huko Basara Abul-Hasan Muhammad bin Ahmad bin Suhayli bin Ali bin Mahran al-Bahiliy, alisema: Alitusimulia Abu Mas’ud Abdurahman bin Fahri bin Hilal, alisema: Alitusimulia al-Qasim bin Yahya kutoka kwa Abu Ali al-Anbariy, kutoka kwa Muhammad bin as-Saib, kutoka kwa Abu Salih, kutoka kwa Ibnu Abbas. Abul-Hasan bin Mahran amesema: Na alinisimulia Muhammad Zakariya al-Basriyu, alisema: Amenisimulia Said bin Waqid al-Mazniy, alisema: Alitusimulia al-Qasim bin Bahram kutoka kwa Laythu, kutoka kwa Mujahid kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake itaenea.” Alisema: Hasan na Husein walipatwa na maradhi, babu yao Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona akiwa pamoja na Abu Bakr na Umar na waarabu kwa jumla walikwenda kuwaona. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ewe Abal-Hasan ni vizuri lau ukiweka nadhiri kwa ajili ya wanao. Na kila nadhiri isiyotimia haina wajibu wowote.” Ali akasema: “Ikiwa wanangu watapona ugonjwa walionao nitafunga siku tatu kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu.” Vijana wawili hao wakapata afya njema na hali nyumbani kwa aali Muhammad hawana kitu si kichache wala kingi. Ali akaenda 92

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 92

2/14/2018 12:11:39 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kwa Simon bin Jaba mtu wa Khaibari, naye alikuwa ni Myahudi, akakopa toka kwake pishi tatu za ngano. Na katika Hadithi ya al-Mazniy ni kwamba: “Ali alikwenda kuomba kuchambua pamba kwa jirani yake myahudi aliyekuwa akiitwa Simon Jaba. Alimwambia: “Je unaweza kunipa pamba akuchambulie binti Muhammad kwa malipo ya pishi tatu za ngano?” Akasema: Ndio. Akampa naye akaja na pamba na ngano. Akamweleza hayo Fatima naye akakubali na kutii. Wamesema: “Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano, kila mmoja mkate mmoja. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume swala ya Maghrib alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, mara masikini akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni masikini katika watoto wa kiislamu nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Ali akamsikia, akasoma shairi:

“Fatima mwenye ubora na yakini, ewe binti wa mbora kuliko watu wote. 93

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 93

2/14/2018 12:11:40 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Hivi humwoni mkata masikini amesimama mlangoni, akitoa sauti ya uchungu. Akimshitakia Mwenyezi Mungu na akinyenyekea. Analalamika kwetu kwamba ni mwenye njaa na mwenye huzuni. Kila mtu ni rehani wa chumo lake na mwenye kutenda kheri atabainika. Ahadi yake ni Pepo ya juu, aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu kwa bakhili. Na bakhili ana kisimamo dhalili, Mola Mlezi atamtupa gerezani (motoni). Kinywaji chake humo ni maji ya moto na usaha.� Naye Fatima akasoma shairi:

Amri yako kwangu ewe binamu yangu ni yenye kutekelezwa. Sina haja na uduni wala udhalili. Umenyonyeshwa katika kheri maziwa ya ngamia, namlisha wala sisubiri muda. Nataraji nitakapowashibisha wenye njaa, nitaungana na wabora na jamaa. Na nitaingia Peponi na hali nikiwa na uombezi. Wakampa chakula na wakashinda mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya pili Fatima akachukua pishi akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) alikuja 94

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 94

2/14/2018 12:11:40 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nyumbani na kikawekwa chakula mbele yao, mara akafika mlangoni kwao yatima toka katika watoto wa muhajirina ambaye baba yake alikufa kishahidi siku ya Aqabah, akagonga akisema: “Nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Ali akamsikia, akasoma shairi:

Fatima binti wa Sayyid karimu. Binti wa Nabii asiye muovu. Mwenyezi Mungu amemleta yatima. Atakayewahurumia watu naye atahurumiwa. Ahadi yake ni katika Pepo yenye neema. Bila shaka Pepo imeharamishwa juu ya muovu. (Usipompa) Mikono yako itakuwa katika moto wenye kuunguza, kinywaji chake ni usaha na maji ya moto.” Fatima naye akasoma shairi akisema:

Hakika mimi nampa wala sijali, namtanguliza Mwenyezi Mungu kabla ya familia yangu. Wameshinda na njaa na wao 95

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 95

2/14/2018 12:11:40 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ni wanangu, mdogo wao atauwawa katika vita. Huko Karbala atauwawa kwa njama, ole wake na adhabu yule mwenye kumuuwa. Moto utamvuta mpaka chini, na hali mikononi mwake kafungwa pingu na minyororo. Kizuizi juu ya kizuizi. Wakampa chakula na wakashinda siku ya pili mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya tatu Fatima akachukua pishi lililobaki akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yao, mara mfungwa wa kivita akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mnatuteka na kutufunga na wala hamtupi chakula! Nipeni chakula mimi ni mateka wa Muhammad.� Ali akamsikia, akasoma shairi:

Ewe binti wa Mtume Ahmad. Binti wa Mtume bwana mtiiwa. Huyu hapa mfungwa wa Mtume mwongozaji. Amefungwa pingu yake na kizuizi. Anatulalamikia njaa imembana. Atakayelisha chakula leo atakikuta kesho. 96

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 96

2/14/2018 12:11:40 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mbele ya Aliye juu Mmoja mwenye kupwekeshwa. Wanayoyalima wakulima watayavuna. Mlishe bila masimango yachafuayo. Ili ulipwe yale yasiyokwisha. Fatima naye akasoma shairi akisema:

Kati ya kile kilicholetwa hakijabaki ila pishi moja. Bila shaka kitanga changu kimeondoka pamoja na mkono85 wangu. Wallahi wanangu wana njaa, ewe Mola usiuache ­(mkono) upotee. Hutenda wema kwa kuanza, yule ambaye ni mpana karimu mwenye uwezo. Na juu ya kichwa changu sina hijabu, ila hijabu ­iliyofumwa kwa kamba. Wakampa chakula na wakashinda siku ya tatu mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya nne wakiwa tayari wameshatimiza nadhiri yao, Ali alimshika Hasan mkono wa kulia na Husein mkono wa kushoto na kwenda nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na hali wao wawili wakitetemeka kama vifaranga kutokana na ukali wa njaa. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipowatizama ­alisema: “Ewe Abal-Hasan! 85

kono na Kitanga hapa ni kinaya ya Pishi la Kwanza na la Pili. Hivyo anaomba pishi M hizo zisiende na kupotea bure bali ziambatane na malipo mema. –Mtarjumi. 97

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 97

2/14/2018 12:11:40 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Hali niionayo yaniumiza mno twendeni kwa binti yangu Fatima.” Wakaenda kwake wakamkuta akiwa mihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake na macho yake yamebadilika kutokana na ukali wa njaa. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipomtazama na kutambua njaa aliyonayo kupitia uso wake, alisema: “Ee Mwenyezi Mungu nakuomba msaada, Ahlul-Baiti wa Muhammad wanakufa kwa njaa.” Jibril (a.s.) akateremka na kusema: “Ewe Muhammad pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Mtume akasema: “Nichukue nini ewe Jibril?” Jibril (a.s.) akamsomea:

98

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 98

2/14/2018 12:11:40 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika ulimfikia mtu wakati fulani wa zama ambapo hakuwa kitu kinachotajwa. Kwa hakika tulimuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyochanganyika, tunamjaribu, hivyo tukamfanya ni mwenye kusikia mwenye kuona. Hakika sisi tumemuongoza njia awe mwenye kushukuru au awe mwenye kukufuru. Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto uwakao. Hakika watawa watakunywa katika kikombe kilichochanganyika na kafuri. Chemchemu watakayoinywa waja wa Mwenyezi Mungu, wataitiririsha mtiririko. Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake itaenea. Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani. Hakika sisi tunaogopa kutoka kwa Mola wetu siku yenye shida na taabu. Basi Mwenyezi Mungu atawalinda katika shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema na furaha. Na atawapa mabustani na hariri kwa sababu walisubiri. Humo wataegemea viti vya enzi humo hawataona jua wala baridi.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:1-13).– mpaka mwisho wa Sura.86

Qatadah bin Mahran al-Bahiliy amesema katika Hadithi hii kwamba: “Mtume akaharakisha mpaka akaingia kwa Fatima (a.s.). alipoiona hali yao waliyonayo aliwakumbatia na kuanza kulia, kisha akawaambia: “Naona nyinyi mna siku tatu na mimi ni mwenye kughafilika nanyi.” Ndipo Jibril (a.s.) akateremka na Aya hizi: Hakika watawa watakunywa katika kikombe kilichochanganyika na kafuri. Chemchemu watakayoinywa waja wa Mwenyezi Mungu, wataitiririsha mtiririko. Akasema: “Hiyo ni chemchemu iliyopo katika nyumba ya Mtume (s.a.w.w.) inatiririka kwa kusambaa kwenye nyumba za Manabii na waumini. 86.

l-Haskani ameipokea kwa mhtasari kwa matamshi mbalimbali katika Hadithiishirini, A kuanzia Hadithi ya 1042 mpaka Hadithi ya 1061, katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil. Sheikh as-Swaduq amepokea Hadithi 11 katika al-Majlis na Hadithi 44 katika AmalisSwaduq Uk. 212. Ibnu al-Batriq ameipokea kwa njiayake kutoka kwa at-Thaalabi katika sura ya 12 ya kitabu chake Khaswaisul-Wahyi al-Mubin Uk. 100. Na katika kitabu chake kingine Al-Awasit katika sura ya 36Hadithi ya 570 amepokea kutoka kwenye kitabu alUmdat Uk. 180. Na ameipokeaal-Khawarazimiy kwa njia yake kutoka kwa at-Thaalabi katika sura ya 17 yakitabu Manaqibu Amiril-Muuminina Uk. 188, Chapa ya Al-Gharri. 99

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 99

2/14/2018 12:11:41 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Wanatimiza nadhiri: Yaani Ali, Hasan, Husein na mtumishi wao Fidha. Wanaiogopa siku ambayo shari yake itaenea. Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Na hali wana haja nacho lakini wanmpa kipaumbele mwingine. Masikini: Ni miongoni mwa masikini wa kiislamu. Yatima: Ni miongoni mwa mayatima wa kiislamu. Mfungwa wa kivita: Ni miongoni mwa mateka toka kwa Mushrikina. Na wanapowapa chakula husema: Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani. Hakika sisi tunaogopa kutoka kwa Mola wetu siku yenye shida na taabu. Wallahi hawakulisema hili kwa ndimi zao bali kwa dhamira zao ndani ya nyoyo zao. Ndipo Mwenyezi Mungu akafichua dhamira zao kwamba wanasema: “Hatutaki malipo wala shukurani kutoka kwenu msije baadae kutusimbulia. Lakini sisi tumekupeni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kutaka thawabu zake.” Mwenyezi Mungu akasema: Basi Mwenyezi Mungu atawalinda katika shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema:- Katika sura zao. Na furaha:- Katika nyoyo zao. Na atawapa mabustani:- Watakayoishi humo. Na hariri kwa sababu walisubiri:- Watakayovaa na kutandika. Humo wataegemea viti vya enzi humo hawataona jua wala baridi.” Ibnu Abbas amesema: “Pindi watu wa Peponi watakapokuwa peponi ghafla wataona mwanga kama mwanga wa jua na Pepo ­imeangazwa kwa mwanga huo. Watu wa Peponi watasema: Ewe Ridhwan, Mola wetu Mtukufu amesema: “Hawataona jua wala ­baridi.” Ridhwan atawaambia: “Hili si Jua wala si Mwezi, lakini huyu ni Fatima na Ali wamecheka, kicheko ambacho kimeiangazia Pepo kutokana na nuru ya kicheko chao.” Na kwa ajili ya hao wawili 100

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 100

2/14/2018 12:11:41 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu aliteremsha: “Hakika ulimfikia mtu wakati fulani wa zama ambapo hakuwa kitu kinachotajwa.” Mpaka “Na juhudi yenu imethaminiwa.”87 At-Thaalabiy anasema: Nina shairi kuhusu hilo:

Mimi ni mwenye kumtawalisha, kijana ambaye kwa ajili yake, aliteremshiwa Sura Hal Ata.

SURA AL-BALAD Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, anadhani kuwa hapana yeyote anayemuona?” (Qur’ani Tukufu Sura al-Balad; 90:7). Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Mtume wa Mwenyezi ­Mungu alisema: “Nyayo ya mtu haitonyanyuka Siku ya Kiyama mpaka ­aulizwe kuhusu mambo mane: Umri wake aliutumia katika nini. Mali yake aliichumaje na aliitumiaje. Kazi yake, alifanya nini katika kazi yake. Na kuhusu mapenzi yetu watu wa nyumba ya Mtume.”

SURA AD-DHUHA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na Mola wako hivi karibuni atakupa na utaridhika.” (Qur’ani Tukufu Sura ad-Dhuha; 93:5). Ja’far bin Muhammad amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu aliingia kwa Fatima akiwa amejifunika kishamia kilichotokana na pamba (kizito) na hali akitwanga kwa mkono wake na akimnyonye  Kuanzia Aya ya Kwanza mpaka ya Ishirini na Mbili. – Mtarjumi.

87.

101

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 101

2/14/2018 12:11:41 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

sha mwanae. Macho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu yakadondosha machozi baada tu ya kumtazama. Akasema (s.a.w.w.): “Ewe mwanangu mpemdwa! Yaanze machungu ya dunia uje kupata utamu wa Akhera. Bila shaka Mwenyezi Mungu ameniteremshia: “Na Mola wako hivi karibuni atakupa na utaridhika.”88

Nimemaliza kuitafiti Tafsiri hii siku ya ishirini na nne ya Mfungo Tatu, siku ya ­Mubahala, Mwaka 1425 huko katika Jiji la Qum Takatifu.

88.

102

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 102

2/14/2018 12:11:41 PM


SEHEMU YA PILI Kwa Mujibu Wa Baghawi, Raazi, Zamakhshari, Baydhawi Na Qurtubi

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 103

2/14/2018 12:11:41 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA AL-BAGHAWI, INAYOITWA: MAALIMUT-TANZIIL89 SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274).

Imepokewa kutoka kwa Mujahid, kutoka kwa Ibnu Abbas, amesema: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib; alikuwa na dirhamu nne hakuwa anamiliki nyingi zaidi ya hizo, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, nyingine siri na nyingine dhahiri.”90

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Chapa ya Beirut ya Mwaka 2004 A.D.   Tafsirul-Baghawi Juz. 1, Uk. 197, Chapa ya Beirut ya Darul-Kutubi Al-Ilmiyahya Mwaka 2004. Na ameipokea Ibnu Athiir katika wasifu wa Amirul-MuumininaAli katika kitabu Usudul-Ghaba Juz. 4, Uk. 25. Na Tabarani katika kitabu al-Muujam al-Kabir Juz. 3, Uk. 112 katika anwani: Yaliyopatikana kwa njia ya IbnuAbbas. Na al-Wahidiy katika kitabu Asbabun-Nuzuul Uk. 64.

89. 90

104

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 104

2/14/2018 12:11:41 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ­ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:42).

Ametupa habari Abu Bakri Said bin Abdullah Ahmad at-Tahiriy, amesema: “Ametupa habari babu yangu Abdurahman bin AbdusSwamad al-Bazar kutoka kwa Qatadah kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha katika wanawake wa ulimwenguni: Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad na Asia mke wa Firaun.”91 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Amesema: “…watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu..” imesemwa kwam  Tafsirul-Baghawi Juz. 1, Uk. 232.

91.

105

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 105

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ba: Watoto wetu ni Hasan na Husein. Wanawake zetu ni Fatima na Nafsi zetu yaani ni yeye mwenyewe na Ali.92” Amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipousomea ujumbe wa Najran Aya hizi na kuwaomba wafanye maombi ya laana walisema: Mpaka turejee na tutafakari jambo hili kisha kesho tutakuja tena. Wakajadiliana na kumwambia Aqib naye alikuwa ndiye wamfuatae katika rai: ‘Ewe mja wa Masihi unasemaje?’ Akasema: W’allahi enyi wakristo nimeshakujulisheni kwamba hakika Muhammad ni Nabii na Mtume, na wallahi katu hakuna watu walioombeana laana na Mtume kisha mkubwa wao akaendelea kuishi au mdogo wao kuzaliwa. Na kama mtafanya hivyo bila shaka tutaangamia, hivyo hakuna cha kufanya ila ni nyinyi kuendelea kubakia katika imani yenu kuhusu jamaa yenu (Isa), nendeni mkamuage mtu huyu na mrejee nchini kwenu.” Ndipo kesho wakaja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na Mtume akatoka akiwa amemkumbatia Husein na amemshika mkono Hasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima. Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Askofu wa Najran akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia, na hatabaki mkiristo yeyote hapa duniani mpaka siku ya Kiyama.” Wakasema: Ewe Abul-Qasim! Tumeona tusiapizane na wewe na tukuwache uendelee kuwa katika dini yako nasi tuendelee kubaki katika dini yetu.   Hivyo ‘nafsi zetu na nafsi zenu’ inaonyesha kwamba uimamu umethibiti kwa Ali kwani Mwenyezi Mungu amemfanya ndio nafsi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kuungana kwa kuwa kitu kimoja ni muhali hivyo maana yake ni kwamba wanalingana katika mamlaka ila unabii.

92.

106

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 106

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Mkikataa ­kufanya maapizano basi msilimu mtapata haki waliyonayo waislamu na mtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwao.” Wakakataa, ndipo Mtume akawaambia: “Basi hakika ­nitawafukuzeni.” Wakasema: “Hatuna nguvu ya kupigana vita na waarabu, ­lakini sisi tunafanya suluhu na wewe usitushambulie kivita na wala usitufukuze na wala usitutoe katika dini yetu. Kwa sharti tukupe kila mwaka Hilla93 elfu mbili: Elfu moja katika mwezi wa Safar na elfu nyingine katika mwezi wa Rajab.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akafanya nao suluhu kwa sharti hilo na akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake hakika adhabu imeshateremka juu ya watu wa Najran. Na lau wangefanya maapizano wangegeuzwa manyani na nguruwe na bonde lao lingewaka moto. Na Mwenyezi Mungu angeiteketeza Najran na watu wake hata ndege aliyopo juu ya mti. Wala mwaka usingepita wakristo wote wangekuwa wameteketea.”94

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55). Ibnu Abbas na as-Sadiy wamesema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na   Jina la pesa kama vile Dola, Shilingi, Paundi na mfano wa hizo.   Tafsirul-Baghawi Juz. 1, Uk. 240. Na ameipokea Hamwawi katika mlango wa kumi na nne katika kitabu Faraidus-Samtwayn Juz. 2, Uk. 23, Chapa ya Kwanza. Pia ameipokea Ibu al-Mughazaliy katika kitabu Manaqibu Amiril-Muuminina Uk. 263, Hadithi ya 310. Na al-Baghawi katika kitabu Misbahus-Sunnah Juz. 2, Uk. 201. Na pia ameipokea Ibnu Hajar katika kitabu as-Sawaiqul-Muhriqah Uk. 93.

93. 94.

107

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 107

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” kwamba alimkusudia Ali bin Abu Talib, muombaji alipita kwake msikitini na hali akiwa amerukuu ndipo akampa pete yake.”95 Na amesema Abu Ja’far Muhammad bin Ali al-Baqir (a.s): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini…” iliteremka kwa ajili ya wale walioamini. Pakasemwa: Watu wanasema kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib. Akasema: ‘Ali ni miongoni mwa wale walioamini.96”

SURAT AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na walipokupangia njama wale waliokufuru ili wakufunge au wakuue au wakutoe, wakapanga njama na Mwenyezi Mungu akapanga njama na Mwenyezi Mungu ndiye mpangaji bora wa njama.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:30). Ibnu Abbas amesema: “Jibril alimjia Mtume (s.a.w.w.) na kumpa habari na kumwamuru asilale katika kitanda chake alichokuwa akilala siku zote na Mwenyezi Mungu akampa idhini ya kutoka kuelekea Madina. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamwamuru Ali bin Abu Talib alale kitandani kwake na kumwambia: “Jifunike shuka langu hili hakika hautofikwa na jambo likuchukizalo.” Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akachukua fungu la udongo na Mwenyezi Mungu akawafumba macho yao na Mtume akawa anawanyunyuzia udongo juu ya vichwa vyao na hali akiso  Tafsirul-Baghawi Juz. 2, Uk. 38. Ameipokea al-Haythami katika mlango wa fadhila za Ali katika kitabu Majmauz-Zawaid Juz. 9, Uk. 134. Na al-Muttaqiy al-Hindiy katika Kanzul-Ummal Juz. 7, Uk. 305, Chapa ya Kwanza. Na Shablanji katika kitabu NurulAbsar Uk. 69. 96.   Nurul-Absar Uk. 39. Na dhahiri kwamba iwapo kweli riwaya hii ni sahihi basi jibu la Imam hapa ni la mfumo wa Taqiyya ndio maana ametoa jibu la jumla. 95.

108

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 108

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ma: “Hakika sisi tumeiweka minyororo shingoni mwao nayo inafika videvuni, kwa hiyo vichwa vyao vikainuliwa.” Na akaenda zake pangoni huko Thauri akiwa na Abu Bakri na akamwacha Ali badala yake huko Makka akirudisha amana zilizokuwa kwake. Amana zilikuwa zikiwekwa kwake kutokana na ukweli wake na uaminifu wake. Mushrikuna walikesha wakimlinda Ali akiwa amelala katika kitanda cha Mtume wa Mwenyezi Mungu huku wakidhani kuwa ndiye Mtume (s.a.w.w.). Palipopambazuka walimzingira na ghafla wakamkuta ni Ali, wakamuuliza rafiki yako yuko wapi? Akajibu sijui….”97

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1). Amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Hakuna nusra nisipowanusuru.” Mwaka wa nane Hijriya akaandaa msafara kuelekea Makka, ulipoingia mwaka wa tisa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliazimia kuhiji, kisha akasema: “Hakika mushrikina watahudhuria na kutufu uchi.” Ndipo akamtuma Abu Bakr awe kiongozi wa Hijja katika msimu huo, akampa pia Aya arobaini za mwanzo wa Surat Baraa akawasomee mahujaji wa msimu huo. Kisha baada yake akamtuma Ali aende na ngamia wake akawasomee mwanzo wa Sura Baraa na akamwamuru atangaze huko Makka, Mina na A’fara kwamba: Mwenyezi Mungu na Mtume wake (s.a.w.w.) wamejitoa katika dhima dhidi ya kila Mushriku na wala wasitufu na hali wakiwa uchi. Ndipo Abu Bakr akarejea na kusema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Baba yangu na mama yangu   Tafsirul-Baghawi Juz. 2 Uk. 205.

97.

109

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 109

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ni fidia kwako, kuna lolote limeshuka kwa ajili yangu?’ Akasema (s.a.w.w.): ‘Hapana, lakini haipasi yeyote yule afikishe hili kwa niaba yangu ila mtu kutoka katika ndugu zangu.’98 Akaendelea mpaka akasema: “Ilipofika siku ya kuchinja Ali alisimama na kuwatangazia amri aliyotumwa na akawasomea Sura Baraa.” Zaid bin Thabit amesema: Tulimuuliza Ali ulitumwa kitu gani katika Hija hiyo? Akasema: ‘Nilitumwa mambo manne: Mushriku haruhusiwi kuhiji wala kutufu na hali yu tupu. Yule ambaye kati yake na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuna ahadi basi itaendelea mpaka mwisho wa muda wake, na yule ambaye ahadi yake haina muda basi muda wake ni miezi minne tokea sasa. Haingii peponi ila mwislamu. Na baada ya mwaka huu waislamu na mushrikina hawahiji tena pamoja.99 Baghawi amesema: Lau mtu akisema: Vipi Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma Abu Bakr kisha akamuuzulu na kumtuma Ali? Tutajibu: Alimtuma Ali akatangaze Aya hizi, na sababu ni kwamba waarabu walikuwa wamezoea kwamba asiwakilishe katika kuweka mikataba yao na kujitoa katika mikataba hiyo ila yule aliye bwana wao au mtu kutoka katika ukoo wao.100 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” (Sura Tawba: 19).   An-Nasai ameiandika katika kitabu chake al-Khaswais Uk. 144, Chapa ya Beirut. Pia Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake Juz. 3, Uk. 212, Chapa ya Kwanza. Ibnu Asakir katika Tarikh Damashq katika wasifu wa Amirul-Muuminin Ali Juz. 2 Uk. 376, Namba 878. 99.   Tafsirul-Baghawi Juz. 2, Uk. 225. 100.   Tafsirul-Baghawi Juz. 2, Uk. 225. 98.

110

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 110

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Hasan, Shaabiy na Muhammad bin Kaab al-Qardhiy wamesema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, Abbas bin Abdul-Mutalib na Talha bin Shayba, kila mmoja alijigamba.” Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba funguo zimo mikononi mwangu.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mgawa maji na msimamizi wake.’ Ali akasema: ‘Sijui mtasema nini. Bila shaka nimeswali miezi sita kabla ya mtu yeyote na mimi ndiye mwanajihadi.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, mnafanya ­kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu….”101

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake…..” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:17).

Palisemwa: Shahidi hapa ni Ali bin Abu Talib. Na Ali (a.s.) alisema: “Hakuna mtu yeyote miongoni mwa makuraishi ila kuna Aya moja ilishuka kwa ajili yake.” Ndipo mtu mmoja akamwambia: “Ni ipi iliyoteremka kwa ajili yako?’’Ali akasema: “Na anaifuata na shahidi atokaye kwake..”102   Tafsirul-Baghawi Juz. 2, Uk. 232. Na pia ameiandika Ibnu al-Mughazali katika Manaqib Uk. 321, Hadithi ya 367 na 368. Na al-Wahidiy katika Asbabun-Nuzuul Uk. 182. Na Abul-Faraji al-Isfahani katika kitabu chake al-Aghaniy Juz. 4, Uk. 185. 102.   Tafsirul-Baghawi Juz. 2, Uk. 318. Na ameipokea al-Muttaqi al-Hindi katika Juz. 1, Uk. 251, Chapa ya Kwanza. Na Ibnu Asakir katika kitabu chake Tarikh Damashq katika wasifu wa Imam Ali Juz. 2, Uk. 420. Na Ibnu Abil-Hadid katika Sharhun-Nahji Juz. 2, Uk. 236. 101.

111

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 111

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AN-NAHL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na tukampa wema katika dunia, na hakika yeye katika Akhera atakuwa katika watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nahl; 16:122).

Amesema Muqatil bin Hayyan: “Anamaanisha ­anazoombewa katika umma huu, unaposema:

rehema

Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na Aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na Aali Ibrahim.”103

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Siku tutakapowaita kila watu na Imam wao.....” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:71). Imamu wao hapa imesemwa anamaanisha mama zao. Na hilo lina aina tatu za hekima, mojawapo ni sharafu ya Hasan na Husein (a.s.).104

SURAT HAJJ Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hawa mahasimu wawili waliohasimiana kwa ajili ya Mola wao...” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hajj; 22:19). Iliteremka kwa ajili ya wale waliojitokeza kupambana Siku ya Badri: Hamza, Ali, Ubayda bin al-Harith, Utba na Shayba watoto wa ar-Rabia na al-Walid bin Utba.   Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 74.   Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 104.

103. 104.

112

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 112

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa Qays bin Ubada amesema kwamba Ali bin Abu Talib alisema: “Mimi ndiye wa awali ambaye atasimama mbele ya Rahman Siku ya Kiyama kwa ajili ya uhasimu.”105

SURAT ASH-SHU’ARAA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na uwaonye jamaa zako walio karibu.” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shu’araa; 26:214). Kutoka kwa Abdullah bin Abbas kutoka kwa Ali bin Abu Talib, amesema: “Ilipoteremka Aya hii kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Na uwaonye jamaa zako walio karibu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliniita na kuniambia: ‘Ewe Ali! Hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru niwaonye jamaa zangu walio karibu. Suala hilo likaniumiza kichwa na nikatambua kwamba nitakapowadhihirishia jambo hili nitakumbana na nisiyoyapenda toka kwao. Nikanyamaza mpaka aliponijia Jibril na kuniambia: Ewe ­Muhammad! Hakika usipofanya unayoamrishwa, Mola wako atakuadhibu. Ewe Ali! Tuandalie pishi la chakula na mguu wa mbuzi na utujazie birauli ya maziwa, kisha nikusanyie watoto wa Abdul-Mutalib ili niwaeleze na kuwafikishia yale niliyoamrishwa. Nikatekeleza aliyoniamrisha (s.a.w.w.). Kisha nikamwitia na wakati huo walikuwa wanaume arobaini, amezidi mtu mmoja au amepungua mmoja, humo walikuwemo ami zake: Abu Talib, Hamza, Abbas na Abu Lahabi. Walipokwishakusanyika kwake alinitaka ni  Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 235. Na ameipokea Bukhari katika Sahih yake katika tafsiri ya Aya hii chini ya namba 4428 Juz. 17 katika ufafanuzi wa al-Karmani Uk. 216, Chapa ya Beiruti. Na al-Khawarazimiy katika Manaqib Ali Juz. 107, Hadithi ya 12, Sura ya 16.

105.

113

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 113

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

waletee chakula nilichowatengenezea, nami nikawaletea. Nilipokiweka, Mtume wa Mwenyezi Mungu alichukua kipande kidogo cha nyama akakikata kwa meno yake kisha akakitupia pembezoni mwa sinia, akasema: “Chukueni kwa Jina la Mwenyezi Mungu.” Watu wakala mpaka wakatosheka. Naapa kwa Mwenyezi Mungu, chakula nilichowapa wote ni cha kuweza kula mtu mmoja. Kisha akasema wape watu kinywaji, nikaja na ile birauli wakanywa mpaka wakatosheka wote. Naapa kwa Mwenyezi Mungu kilikuwa ni kinywaji cha kutosheka mtu mmoja. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipotaka kuwaeleza, Abu Lahabi alimtangulia kuongea, akasema: “Jamaa yenu amewaroga kwa karamu.” Ndipo kaumu wakatawanyika na wala Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) hakufanikiwa kuwaeleza, akasema (s.a.w.w.): “Kesho Ali. Hakika mtu huyu amenitangulia kusema yale uliyoyasikia, na hatimaye watu wametawanyika kabla sijawaeleza, hivyo tuandalie chakula mfano wa kile ulichoandaa kisha unikusanyie.” Nikatekeleza kisha nikawakusanya, kisha akanitaka nilete chakula nikawaletea naye akafanya kama alivyofanya jana, wakala na kunywa mpaka wakatosheka. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akaongea kwa kusema: “Enyi wana wa AbdulMutalib! Hakika mimi nimewaletea kheri ya dunia na akhera. Na hakika Mwenyezi Mungu ame niamuru niwalinganie kwayo, basi ni nani kati yenu atanisaidia katika jambo hili, awe ndugu yangu, wasii ­wangu na khalifa wangu?” Watu wote wakakaa kimya, nikasema na hali mimi nikiwa ndiye mdogo kiumri kuliko wote: Mimi ewe Mtume wa Mwenyezi ­Mungu, nakuwa waziri wako. Akaishika shingo yangu kisha akasema (s.a.w.w.): “Hakika huyu ni ndugu yangu, wasii wangu na khalifa 114

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 114

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wangu kwenu, hivyo msikilizeni na mumtii.” Kaumu wakanyanyuka na hali wakidhihaki na wakimwambia Abu Talib: “Bila shaka amekuamuru umsikilize Ali na kumtii.”106

SURAT AS-SAJDA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.” (Qur’ani Tukufu Sura as-Sajda; 32:18). Iliteremka ikimuhusu Ali bin Abu Talib na Walid bin Uqbah bin Abu Muit ndugu yake Uthman kwa upande wa mama. Kulikuwa na mzozo na maneno baina yao, Walid bin Uqbah akamwambia Ali: ‘Nyamaza wewe bado mtoto na mimi wallahi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye meno makali kuliko wewe na shujaa kuliko wewe na hodari wa mapambano kuliko wewe.’ Ali akamjibu: ‘Nyamaza bila shaka wewe ni fasiki.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.”107

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika si mengineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura alAhzab; 33:33).   Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 343. Na ameiandika Ibn Asakir katika kitabu chake Tarikh Damashq katika wasifu wa Imam Ali Juz. 1, Uk. 99, Namba 137, Chapa ya Kwanza. Na Ahmad bin Hanbal katika Fadhailus-Sahaba Uk. 161, Hadithi ya 230, Chapa ya Kwanza. 107.   Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 433. Ameipokea Khatibu al-Baghdad katika kitabu chake Tarikhul-Baghdad Juz. 13, Uk. 321, Namba 7291. Muhibu Tabari katika ar-Riyadh anNadhrah Juz. 2, Uk. 206, Chapa ya Pili. Ibn Aatham al-Kufiy aliyefariki miaka ya 314 A.H. ameiandika katika kitabu chake al-Futuhu Juz. 2, Uk. 354, Chapa ya India. Na al-Hafidh al-Mazziy katika kitabu Tahdhibul-Kamal Juz. 8, Uk. 1475. Na al-Mas’ud katika Murujud-Dhahabi Juz. 2, Uk. 357, Chapa ya Misri. 106.

115

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 115

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Abu Said na jamaa wengine miongoni mwa tabiina akiwemo Mujahid, Qatadah na wengineo wamesema kwamba: Walengwa hapa ni Ali, Fatima, Hasan na Husein. Kutoka kwa Aisha Umul-Muuminina alisema kwamba: “Siku moja Mtume alitoka akawa amejifunika shuka lililodariziwa na manyoya meusi. Akaketi na ghafla akaja Fatima na akamfunika, akaja Ali akamfunika, akaja Hasan akamfunika, akaja Husein naye akamfunika, kisha akasema: “Hakika si mengineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.’” Kutoka kwa Ummu Salama mke wa Mtume (s.a.w.w.) amesema kwamba: “Hakika Aya hii iliteremka nyumbani kwangu: “Hakika si mengineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu enyi watu wa nyumba ya Mtume..” Mtume wa Mwenyezi Mungu akatuma ujumbe waje Fatima, Ali, Hasan na Husein, walipokuja akasema: ‘Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu.’” Nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mimi sio miongoni mwa Ahlul-Baiti? Akanijibu: “Ndiyo, wewe sio inshaallah.”108 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia (wanamtakia rehma) Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).   Tafsirul-Baghawi Juz. 3 katika tafsiri ya Aya hii. Na pia ameipokea Baghawi katika kitabu Misbahus-Sunna Juz. 2, Uk. 200. Na pia Is’afur-Raghibina kwenye pambizo la Nurul-Absar Uk. 82.

108.

116

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 116

2/14/2018 12:11:42 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Abdurahman bin Abi Layla amesema: Kaab bin Ajrah alikutana na mimi na kuniambia: Je nikupe zawadi niliyoisikia kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)? Nikasema ndio nizawadie. Akasema: Tulimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu tukasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tutawaombeaje rehema enyi AhlulBaiti? Kwani Mwenyezi Mungu tayari ameshatufundisha namna ya kukusalimu.Akasema (s.a.w.w.):

“Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na kizazi cha Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na kizazi cha Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.”

Kutoka kwa Ibnu Mas’ud amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Mtu bora kwangu Siku ya Kiyama ni yule mwenye kunisalia sana.”109 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini ­wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kumbwa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:58).   Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 467.

109.

117

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 117

2/14/2018 12:11:43 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Muqatil amesema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, walikuwa wakimuudhi na kumkashifu.”110

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu. Na anayefanya wema tutamzidishia wema, kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23).

Abdul-Wahid Ahmad al-Malihiy amesema: “Kutoka kwa Bashari kutoka kwa Muhammad bin Ja’far, kutoka kwa Abdul-Malik bin Maysara, amesema: ‘Nilimsikia Taus akisimulia kutoka kwa Ibn Abbas kwamba aliulizwa kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” Said bin Jubayri akasema: “Hao ni karaba ambao ni aali Muhammad.” Kadhalika wamepokea as-Shaabiy na Taus kutoka kwa Ibn Abbas kwamba alisema: “isipokuwa mapenzi katika ndugu” maana yake muwahifadhi karaba zangu, muwapende na kuuthamini udugu wangu. Na baadhi wamesema: Maana yake ni hakuna jingine ila kuwapenda karaba zangu na kizazi changu na mnithamini kupitia kwao, na hiyo ndio kauli ya Saidi bin Jubayri na Amr bin Shuaybu. Wametofautiana kuhusu karaba zake: Fatima Zahrau, Ali na watoto wao wawili, na wao ndio walioteremshiwa: “Hakika si mengineyo,   Tafsirul-Baghawi Juz. 3, Uk. 469

110.

118

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 118

2/14/2018 12:11:43 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu enyi watu wa nyumba ya Mtume..”111

SURAT AD-DUKHAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Mbingu na ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muda. “ (Qur’ani Tukufu Sura Ad-Dukhan 44:29). Atau amesema: “Kulia kwa mbingu ni ule wekundu wa kwenye ncha zake.” Na As-Sadiy amesema: “Alipouwawa Husein bin Ali (a.s.) mbingu ilimlilia na kilio chake ni wekundu wake.”112 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Mwenyezi Mungu amekuahidini ngawira nyingi mtakazozichukua, kisha akakutimizeni haya, na akaizuia mikono ya watu isikufikieni, na ili iwe dalili kwa waumini na kukuongozeni njia iliyonyooka.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Fath; 48:7).

Kisa cha Khaybar amekipokea Sahlu bin Saad, Anas na Abu Huraira. Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa   Tafsirul-Baghawi Juz. 4, Uk. 111. Ibnu Hanbal ameipokea katika kitabu chakeal-Fadhail Uk. 187, Hadithi ya 263. Ibnu Hajar amepokea shairi katika kitabuSawaiqul-Muhriqah katika mlango wa kumi kutoka kwa Imamu wake, ash-Shafi’ilikionyesha wajibu wa kuwapenda na kuwatii Aali Muhammad (a.s.):

111.

Enyi watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu kuwapendeni ni faradhitoka kwa Mwenyezi Mungu iliyoteremshwa katika Qur’ani. Inatosha kwamba nifahari kubwa kwenu kuwa yule asiyewasalia hana Swala. 112.   Tafsirul-Baghawi Juz. 4 Uk. 136. Hili si jambo gumu, kwani wametaja katika tafsiri ya Aya hii kwamba: Muumini anapofariki mbingu na ardhi humlilia muda wa siku arobaini. Na bila shaka Imam Husein (a.s.) ni bwana wa waumini na kinara wao, na hili ni jamabo ambalo riwaya zote zinazozungumzia kufa kishahidi kwa Husein zimeafikiana juu yake. Kwa undani zaidi rejea kitabu Kamiluz-Ziarati cha Ibnu Qawlayhi. 119

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 119

2/14/2018 12:11:43 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

habari akasema: “Hakika kesho nitamkabidhi bendera mtu ambaye anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanampenda. Mwenyezi Mungu ataleta ushindi mikononi mwake.” Akamwita Ali bin Abu Talib akamkabidhi bendera na kumwambia: ‘Nenda wala usigeuke nyuma.’” Akafika mji wa Khaybar na ndipo Marhabu aliyekuwa mlinzi wa ngome akatoka na hali amevaa deraya na juu ya kichwa chake kavaa jiwe alilolitoboa mfano wa yai. Ali akajitokeza kumkabili akampiga dharuba iliyopasua jiwe na deraya na kupasua kichwa chake mpaka upanga ukafika wenye magego yake. Na katika riwaya nyingine: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Hakika kesho nitamkabidhi bendera mtu ambaye anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanampenda.” Nikamfuata Ali na kumleta huku nikimwongoza kwani alikuwa amepatwa na maradhi ya macho. Mpaka tukafika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamtemea mate na akapona na akamkabidhi bendera. Marhab ­akatoka na kusema:

“Khaibar imeshajua kwamba hakika mimi ni Marhab mwenye silaha kali na komandoo mzoefu. Pindi moto wa vita unapowashwa, mara hufuma mshale na mara hupiga.” Ali akajitokeza kumkabili naye akisema:

120

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 120

2/14/2018 12:11:43 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Mimi ndiye ambaye mama yangu alinipa jina la Haidari (Simba) Kama simba pori mwenye kutisha Nitakuuweni kwa upanga wangu mauwaji ya kuteketeza. (kama kupima pishi)”113 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu na walio pamoja naye ni imara mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao, utawaona wakirukuu na kusujudu wakitafuta fadhila za Mwenyezi Mungu na radhi Yake. Alama zao ni katika nyuso zao kwa athari ya kusujudu, huo ndio mfano wao katika Taurati, na mfano wao katika Injili. Kama mmea uliotoa matawi yake, kisha yakautia nguvu, ukawa mnene ukasimama sawa sawa juu ya shina lake ukawafurahisha walioupanda, ili awakasirishe makafiri kwa ajili yao. Mwenyezi Mungu amewaahidi walioamini na kutenda mema katika wao msamaha na malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Fath; 48:29).

Imepokewa kutoka kwa Mubaraka bin Fadhala kutoka kwa Hasan, amesema: “…Utawaona wakirukuu na kusujudu wakitafuta   Tafsirul-Baghawi Juz. 4, Uk. 177.

113.

121

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 121

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

fadhila za Mwenyezi Mungu na radhi Yake.” Ni Ali bin Abu Talib. “Ukawa mnene ukasimama sawa sawa juu ya shina lake” Ni Ali bin Abu Talib, Uislamu uliimarika kwa upanga wake.114

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu “ (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Mujahid amesema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee, alitoa sadaka ya dinari na akasema naye siri. Ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.). Hivyo Ali alikuwa akisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nayo ni Aya ya kusema siri na Mtume.”115 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Baghawi Juz. 4, Uk. 186. al-Katib al-Baghdadiy amepokea katika kitabu chake Tarikh Baghdad Juz. 13, Uk. 153, Namba 7131. al-Haskaniy amepokea katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil Juz. 2, Uk. 184, Namba 890, Chapa ya Kwanza. 115. Tafsirul-Baghawi Juz. 4 katika tafsiri ya Aya hii. Na ameiandika an-Nasai kati-ka kitabu Khaswaisu Amiril-Muuminina Uk. 176, Chapa ya Beirut. Na Humawi katika kitabu Faraidus-Samtwayn katika mlango wa 66 wa Samtwi ya Kwanza, Juz. 1, Uk. 358, Chapa ya Beirut. 114.

122

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 122

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).

Mujahid na Atau wamepokea kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba: Iliteremka kwa ajili ya Ali. Yeye alifanya kazi kwa Myahudi kwa malipo ya shairi kidogo, akachukua theluthi ya shairi akatwanga na kuoka chakula kidogo, kilipoiva akatokea masikini na kuomba, ndipo wakampa chakula chote. Kisha wakaoka theluthi ya pili, kilipoiva alikuja yatima akaomba wakampa chote. Akaoka theluthi ya tatu iliyobaki na kilipoiva alikuja mfungwa toka kwa mushrikina, akaomba nao wakamlisha na kushinda siku hiyo bila kula.116

Tafsirul-Baghawi Juz. 4, Uk. 397. Na al-Qunduziy katika Yanabiul-Mawaddah Juz. 1, Uk. 93 na Uk. 94.

116.

123

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 123

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA ZAMAKHSHARI, INAYOITWA AL-KASHAFU FII HAQAIQIT-TAAWIIL SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Kila mara Zakariya ­alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: ‘Ewe Maryam, unatoa wapi hivi.’ Akasema: ‘Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika ­Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:37). Zamakhshari ametaja katika tafsiri yake al-Kashafu anapoifasiri Aya hii tukufu kwamba: “Mtume alipatwa na njaa kipindi cha ukame ndipo Fatima akamfanyia kipaumbele baba yake kwa kumzawadia vipande viwili vya mkate na kipande cha nyama, naye (s.a.w.w.) akavirejesha kwa Fatima na kusema: ‘Chukua ewe binti yangu.’ ­Alipofunua bakuli akalikuta limejaa mikate na nyama, akapigwa na butwaa na akagundua kwamba vimeteremka kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Mtume akamuuliza: ‘Umetoa wapi hivi?’ Akasema: ‘Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Mtume akasema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ­Ambaye amekufanya kifani wa seyida wa wana wa Israel (Mariam.)” Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawakusanya Ali bin Abu Talib, Hasan na Husein na watu wote wa nyumbani kwake wakala pamoja mpaka wakashiba na chakula kikabakia kama kilivyokuwa. Hivyo Fatima akawagawia majirani zake.117   Tafsirul-Kashafu Juz. 1, Uk. 321, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D. Chapa ya Mustafa al-Babi al-Halbiy.

117.

124

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 124

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: ­Njooni ­tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na ­wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa ­unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Zamakhshari amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipowaita kwenye maapizano walisema: Mpaka turejee na tutafakari jambo hili. Walipoachana wakamwambia Aqib naye alikuwa ndiye wamfatae katika rai: ‘Ewe mja wa Masihi unasemaje?’ Akasema: ‘Wallahi enyi wakristo nimeshakujulisheni kwamba hakika Muhammad ni Nabii na Mtume, na bila shaka amewajieni na hoja yakinifu kuhusu mtu wenu (Yesu), wallahi katu hakuna watu walioombeana laana na Mtume kisha mkubwa wao akaendelea kuishi au mdogo wao kuzaliwa. Na kama mtafanya hivyo bila shaka tutaangamia, ila ni nyinyi kuendelea kubakia katika imani yenu na dini yenu, nendeni mkamuage mtu huyu na mrejee nchini kwenu.” Ndipo kesho wakaja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na Mtume akatoka akiwa amemkumbatia Husein na amemshika mkono Hasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima. Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.”

125

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 125

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Askofu wa Najran akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia, na hatabaki mkiristo yeyote hapa duniani mpaka siku ya Kiyama.” Wakasema: “Ewe Abul-Qasim! Tumeona tusiapizane na wewe na tukuwache uendelee kuwa katika dini yako nasi tuendelee kubaki katika dini yetu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Mkikataa kufanya maapizano basi msilimu mtapata haki waliyonayo waislamu na mtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwao.” Wakakataa, ndipo Mtume akawaambia: “Basi hakika mimi nitawafukuzeni.” Wakasema: “Hatuna nguvu ya kupigana vita na waarabu, lakini sisi tunafanya suluhu na wewe usitushambulie kivita na wala usitufukuze na wala usitutoe katika dini yetu. Kwa sharti tukupe kila mwaka Hilla118 elfu mbili: Elfu moja katika mwezi wa Safar na elfu nyingine katika mwezi wa Rajab, na diraya thelathini za kawaida za chuma.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akafanya nao suluhu kwa sharti hilo na akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, hakika adhabu imeshateremka juu ya watu wa Najran. Na lau wangefanya maapizano wangegeuzwa nyani na nguruwe na bonde lao lingewaka moto. Na Mwenyezi Mungu angeiteketeza Najran na watu wake hata ndege aliyopo juu ya mti. Wala mwaka usingepita wakristo wote wangekuwa wameteketea.”119 Pia Zamakhshari amepokea kutoka kwa Aisha kwamba: “Siku moja Mtume alitoka akajifunika shuka lililodariziwa na manyoya meusi. Akaja Hasan akamfunika, kisha akaja Husein akamfunika, akaja Fatima na kisha Ali nao akawafunika, kisha akasema: “Hakika si men  Jina la pesa kama vile Dola, Shilingi, Paundi na mfano wa hizo.   Tafsirul-Kashafu Juz. 1, Uk. 326, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

118. 119.

126

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 126

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

gineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume.� Zamakhshari akajiuliza kwa kusema: Ukiniambia: Hakuwaita kwenye maapizano ila ni kwa ajili ya kutaka kubaini ni nani muongo kati yake na hasimu wake, na kikawaida suala hili ni makhsusi kwake na kwa yule anayemkadhibisha, hivyo nini maana ya yeye kwenda na watoto na wanawake? Nitasema: Hiyo ni kuitia uzito hali yake ya kujiamini na kuwa na yakini na ukweli wa dai lake kiasi kwamba amepata ujasiri wa kuwatoa watu ambao ni vipenzi vyake na ni sehemu ya ini lake, hivyo huku akiwa na imani kwamba hasimu wake ni mwongo hakutosheka na kujitoa yeye mwenyewe tu, bali alitoka nao ili hasimu wake ahiliki pamoja na vipenzi vyake iwapo maapizano yatatimia. Amewahusisha watoto na wanawake kwa sababu wenyewe ndio vipenzi vya mtu na ndio mwambata wa moyo wa mtu, baadhi ya nyakati mtu hujitoa fidia kwa ajili yao na kupigana mpaka kuuwawa kwa ajili yao. Pia walikuwa wakienda nao kimoyo vitani ili wawazuiye kukimbia huku wakiwahami barabara kwa roho zao. Kisha ameanza kuwataja kabla ya nafsi ili abainishe umuhimu wa nafasi yao na ukaribu wao kiasi kwamba hupewa kipaumbele kabla ya nafsi na hivyo mtu hujitoa fidia kwa ajili yao. Na humo mna dalili yenye nguvu kuliko nyingine juu ya ubora wa Watu wa Kishamiya (a.s.), na mna hoja ya wazi juu ya kusihi kwa unabii wa Mtume (s.a.w.w.), kwa sababu hakuna yeyote miongoni mwa watu wa madhehebu yetu na walio nje ya madhehebu yetu aliyepokea kwamba walikubali wito huo (wa kufanya maapizano).120   Tafsirul-Kashafu Juz. 1, Uk. 326, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

120.

127

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 127

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na iogopeni adhabu ambayo haitawapata peke yao wale waliodhulumu nafsi zao miongoni mwenu, na jueni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:25).

Zamakhshari amesema: “Imepokewa kwamba Zubair siku moja alikuwa akitembea na Mtume (s.a.w.w.) na ghafla Ali (a.s.) akatokeza na Zubairi akamfurahia. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamwambia Zubair: “Unampendaje Ali?” Akajibu: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Baba yangu na mama yangu ni fidia kwako, hakika mimi nampenda kama nimpendavyo mwanangu au zaidi kuliko mwanangu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamwambia: “Utakuwaje wewe utakapotembea usiku kwenda kupambana naye kivita?”121

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1).   Tafsirul-Kashafu Juz. 2 Uk. 11, Tafsiri ya Surat Anfal, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

121.

128

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 128

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Iliteremka mwaka wa tisa wa hijiriya na ukombozi wa Makka ulikuwa mwaka wa nane. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr awe kiongozi wa Hija ya msimu wa mwaka wa tisa. Alipokuwa njiani Jibril (a.s.) akateremka na kusema: “Ewe Muhammad! Hafikishi ujumbe wako ila mtu atokanaye na wewe.” Akamtuma Ali na Abu Bakr akarejea kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na kusema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! je kimeteremshwa chochote kutoka mbinguni?’’ Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Naam.’’122

SURAT YUSUF Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na akasema: Enyi wanangu, msiingie katika mlango mmoja bali ingieni katika milango mbalimbali.” (Qur’ani Tukufu Sura Yusuf 12:67). Zamakhshari amesema: “Imepokewa kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alikuwa akiwakinga Hasan na Husein (a.s.) akisema:

Nawakinga kupitia maneno timamu ya Mwenyezi Mungu dhidi ya kila jicho baya na dhidi ya kila shetani na jambo litishalo.”123

SURAT MARYAM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” (Qur’ani Tukufu Sura Maryam; 19:96).   Tafsirul-Kashafu Juz. 2, Uk. 26, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.   Tafsirul-Kashafu Juz. 2, Uk. 146,

122. 123.

129

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 129

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Imepokewa kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali bin Abu Talib: “Ewe Ali sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwako na niwekee mapenzi katika nyoyo za waumini.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii.124

SURAT AZ-ZUMAR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na anapotajwa Mwenyezi Mungu peke yake nyoyo za wale wasioamini Akhera huchukia, na wanapotajwa wale walio kinyume naye, mara wanafurahi.” (Qur’ani Tukufu Sura az-Zumar; 39:45).

Zamakhshari amepokea kwamba Rabiu bin Khaytham – Naye hakuwa msemaji - alipewa khabari za kuuawa Husein (a.s.) na akamkasirikia muuwaje wake. Watu wakasema kwamba hivi sasa ataongea, na hakuzidisha zaidi ya kusema: Bila shaka wameshatenda. Kisha akasoma Aya hii. Na imepokewa kwamba baada ya Aya hii alisema: Ameuawa yule ambaye Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akimkalisha juu ya mapaja yake na kuweka ulimi wake ndani ya kinywa chake.125

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” (Qur’ani ­ ­Tukufu Sura ash-Shura; 42:23).   Tafsirul-Kashafu Juz. 2, Uk. 294, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.   Tafsirul-Kashafu Juz. 3 Uk. 34, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

124. 125.

130

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 130

2/14/2018 12:11:44 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Imepokewa kwamba: Ilipoteremka walimuuliza: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa ndugu ambao ni wajibu juu yetu kuwapenda. Akasema: “Ni Ali, Fatima na watoto wake wawili.” Na hilo lathibitishwa na ile riwaya isemayo kwamba Ali bin Abu Talib alisema: “Nilimshitakia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) husuda za watu dhidi yangu. Akasema: ‘Hivi huridhii kuwa mmoja kati ya wane. Wa kwanza kuingia Peponi ni Mimi, Wewe, Hasan, Husein. Wake zetu wakiwa kuliani kwetu na kushotoni kwetu. Na wajukuu zetu wakiwa nyuma ya wake zetu.” Mtume (s.a.w.w.) alisema: “Pepo imeharamishwa juu ya yule ­aliyewadhulumu Ahlul-Baiti wangu na akaniudhi kwa kuwaudhi kizazi changu. Yeyote atakayemtendea wema yeyote miongoni mwa kizazi cha Abdul-Muttalib na ikawa hajalipwa kutokana na wema huo, basi mimi nitamlipa kesho atakapokutana nami Siku ya Kiyama.”126 Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ehe! a­ takayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ni shahidi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ameghufuriwa. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ametubia. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni muumni aliyekamilika kiimani. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali malaika ameshambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakir.   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 81, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

126.

131

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 131

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad atasindikizwa Peponi kama biharusi asindikizwavyo kwenda nyumbani kwa mumewe. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafungulia mlango malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amefia ndani ya Sunna. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni kafiri. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu ya Pepo.”127

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Ali bin Abu Talib (radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee) alisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 82, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

127.

132

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 132

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

h­ akuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu. Nilikuwa na dinari nikaichenji hivyo nikawa natoa dirhamu moja kila nisemapo siri naye.” Ibnu Umar alisema: “Ali alikuwa na mambo matatu, ambayo kuwa nalo moja kati ya hayo ni jambo nilipendalo mno kuliko kuwa na ngamia mwekundu: Kuozwa Fatima, kukabidhiwa bendera Siku ya Khaibar na Aya ya kuongea siri na Mtume.”128

SURAT AT-TAGHABUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, na kwa ­Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura ­at-Taghabun; 64:15).

Imepokewa kwamba: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akitoa hotuba na ghafla wakaja Hasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuinuka, akateremka toka mimbarini akawafuata na kuwachukua na kuwaweka mapajani mwake juu ya mimbari, kisha akasema: ‘Mwenyezi Mungu amesema kweli. “Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani,” nilipowaona hawa wawili sikuweza kuvumilia.’ Kisha akaendelea na Khutba yake.’”129

SURAT AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 211, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 236, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

128. 129.

133

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 133

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na Mariam binti Imran aliyejilinda ubikira wake, na tukampulizia humo roho yetu na akayasadikisha maneno ya Mola wake Mlezi, na vitabu vyake na alikuwa miongoni mwa wanyenyekevu. “ (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:12).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: “Kati ya wanaume wamekamilika wengi na wala hawajakamilika kati ya wanawake ila wanne: Asia binti Muzahim mke wa Firaun, Mariam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.”130

SURAT AL-HAQQA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Sura al-Haqqah: 69:12).

Ilipoteremka Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali (a.s.): “Nilimwomba Mwenyezi Mungu alifanye hivyo sikio lako ewe Ali.’’ Ali alisema: “Baada ya hapo sikuwahi kusahau chochote na wala sikupaswa kusahau.”131

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 250, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 250, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.

130. 131.

134

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 134

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).

Ibnu Abbas alisema: “Hasan na Husein walipatwa na maradhi, babu yao Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona akiwa pamoja na baadhi ya watu. Wakasema: “Ewe Abal-Hasan ni vizuri lau ukiweka nadhiri kwa ajili ya wanao.” Ndipo Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhiri kwamba iwapo watapona watafunga siku tatu. Waliweka nadhiri na hali hawana kitu, ndipo Ali akaenda kwa Simon Myahudi wa Khaybar, akakopa toka kwake pishi tatu za ngano. Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano kulingana na idadi yao, wakaiweka mbele yao ili wafuturu, mara masikini akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni maskini katika watoto wa kiislamu nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakamfanyia kipaumbele na wao wakalala na hali hawajaonja ila maji tu na wakaamka wakiwa na Swaumu. Waliposhinda na Swaumu na kuweka chakula mbele yao mara akafika mlangoni kwao yatima naye wakamfanyia kipaumbele. Na mara mfungwa wa kivita akafika mlangoni kwao siku ya tatu, naye wakamfanyia hivyo hivyo. Asubuhi iliyofuata Ali aliwashika mkono Hasan na Husein na kwenda nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Alipowatizama na hali wao wawili wakitetemeka kama vifaranga alisema: “Hali niionayo kwenu yaniumiza mno.” Akasimama na kwenda nao, ndipo wakamkuta Fatima akiwa mihrabuni 135

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 135

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake na macho yake yamezama. Hali hiyo ikamuuma sana, ndipo Jibril (a.s.) ­akateremka na kusema: “Ewe Muhammad pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Jibril (a.s.) akamsomea Sura hii.132

SURAT AN-NASR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi mtakase Mola Wako kwa sifa njema na umuombe msamaha, hakika yeye ndiye apokeaye sana toba.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nasr; 110:3).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Fatima (a.s.) na kumwambia: “Ewe binti yangu mpendwa! Nafsi ­yangu ­inajiomboleza.” Fatima akalia. Akamwambia: “Usilie, kwani ­hakika wewe ndiye wa kwanza kukutana nami miongoni mwa watu wangu.”133

Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 297, Chapa ya Misri ya Mwaka 1948 A.D.   Tafsirul-Kashafu Juz. 3, Uk. 365. Nimemaliza mchakato juu ya tafsiri hii usiku wa Iddi ya mwaka 1425 A.H. katika Jiji la Qum Takatifu, saa tisa usiku.

132. 133.

136

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 136

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA RAZI, INAYOITWA AT-TAFSIRU AL-KABIR AU MAFATIHUL-GHAYBI SURAT AL-FATIHA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye ­kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Fatiha; 1:1)

Kusoma Bismillahi kwa sauti: Mas’ala ya tisa katika hoja ya tano: Bayhaqiy amepokea katika kitabu Sunanul-Kubra kutoka kwa Abu Huraira kwamba: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akisoma Bismilahi Rahman Rahim kwa sauti katika Sala. Kisha Sheikh Bayhaqiy amepokea kwamba Umar bin Khattab, Ibnu Abbas, Ibnu Umar na Ibnu Zubair walikuwa wakiisoma kwa sauti.” Ama Ali bin Abu Talib yeye imethibiti kwa tawaturi kwamba alikuwa akisoma Bismillahi kwa sauti, na yule mwenye kumfuata Ali katika dini yake bila shaka huyo ndiye aliyeongoka. Na dalili juu ya hilo (kuwa bila shaka ameongoka) ni kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Ewe Mwenyezi Mungu! Iweke haki pamoja na Ali vyovyote awavyo.”134

At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 1 Uk. 205, Chapa ya Maktabatut-Tawfiyqiyyah, Uhakiki wa Imad Zakiyyu al-Barudiy. Yapasa utambue ni hili tu ndilo nililofaidika nalo kutoka katika chapa hii iliyotajwa.

134.

137

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 137

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akamfundisha Adam majina yote, kisha akaonyesha mbele ya Malaika, na akasema: Niambieni majina ya hawa ikiwa mnasema kweli.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:31).

Kutoka kwa as-Shaabiy amesema: “Nilikuwa kwa Hajjaj, mara akaletwa Yahya bin Yaamur mwanafiqhi wa huko Khurasan akiwa amefungwa pingu za chuma. Hajjaj akamwambia: “Wewe umedai kwamba Hasan na Husein ni kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Akasema ndio. Hajjaj akasema: “Niletee dalili ya wazi toka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu la sivyo nitakukatakata kiungo kimoja baada ya kingine.” Akasema: “Ewe Hajjaj, nitakuletea ya wazi iliyo bayana toka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu.” As-Shaabiy anasema: Nikashangazwa na ujasiri wake kwa kusema: Ewe Hajjaj. Ndipo Hajjaj akamwambia: “Usiniletee Aya hii: ‘Tuwaite watoto zetu na watoto zenu.. “ Akamwambia: “Nitakuletea Aya iliyo wazi toka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, nayo ni kauli yake: “Na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:84-85). Nani aliyekuwa baba wa Isa na hali kaunganishwa na kizazi cha Nuh?” 138

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 138

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

As-Shaabiy anasema: “Akainamisha kichwa muda kidogo kisha akainua kichwa na kusema: “Kana kwamba mimi sijawahi kuisoma Aya hii toka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Mfungueni pingu yake na mpeni kiasi kadhaa cha mali.135 Bedui mmoja alimwendea Husein (a.s.) akamsalimu na kumwomba haja yake. Akasema: “Nilimsikia babu yako akisema: “Muombapo haja iombeni toka kwa mmoja kati ya watu hawa wanne: Ima mwarabu sharifu au bwana mkarimu, aliyehifadhi Qur’ani au mwenye uso wenye mvuto.” Ama kuhusu waarabu bila shaka wamepata sharafu kupitia babu yako. Ama ukarimu ninyi ndio chanzo chake na ndio tabia yenu. Ama Qur’ani ni ndani ya nyumba zenu ndimo ilimoshukia. Ama uso wenye mvuto ni kwamba mimi nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: Mkitaka kunitazama mtazameni Hasan na Husein.” Husein (a.s.) akamwambia: “Ni ipi haja yako?” Akaiandika juu ya ardhi. Husein (a.s.) akamwambia: “Nilimsikia baba yangu Ali (a.s.) akisema: ‘Thamani ya kila mtu ni kwa kadiri ya mazuri ayatendayo.’ Na nilimsikia babu yangu akisema: ‘Wema ni kwa kadiri ya maarifa.’ Hivyo nakuuliza maswali matatu ukiweza kujibu vizuri jibu moja utapata theluthi ya haja yako kutoka kwangu, na ukijibu mawili utapata theluthi mbili na ukijibu matatu utapata haja yako yote toka kwangu. Na hapa nimebeba fuko la pesa toka Iraq. Akasema: “Uliza na wala hakuna ujanja na nguvu ila kutoka kwa Mwenyezi Mungu.” Akasema (a.s.): “Ni amali ipi iliyo bora?” Bedui akajibu: “Kumwamini Mwenyezi Mungu.” Akasema (a.s.): “Kipi kitakachomwokoa mja asihiliki?”   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 2, Uk. 194, Chapa ya Darul-Kutubi al-Ilmiyyah.

135.

139

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 139

2/14/2018 12:11:45 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Bedui akajibu: “Kumtumainia Mwenyezi Mungu.” Akasema (a.s.): “Kitu gani humpamba mtu?” Bedui akajibu: “Elimu yenye hekima.” Akasema (a.s.): “Akikosa hilo?” Bedui akajibu: “Awe na ukarimu.” Akasema (a.s.): “Akikosa hilo?” Bedui akajibu: “Awe fukara mvumilivu.” Akasema (a.s.): “Akikosa hilo?” Bedui akajibu: “Basi asubiri kimondo kutoka mbinguni kimuunguze.” Husein akacheka na kumpa fuko la fedha.136 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya ­ wenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja.” M (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:207).

Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.) alilala juu ya kitanda cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) usiku aliotoka kwenda pangoni. Imepokewa kwamba alipolala juu ya kitanda chake Jibril (a.s.) alisimama kichwani kwake na Mikail (a.s.) miguuni kwake na hali Jibril akinadi: “Pongezi pongezi! Nani mfano wako ewe Ali bin Abu Talib, Mwenyezi Mungu anajionea fahari kwako mbele ya Malaika.” Ndipo ikateremka Aya hii.137 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 2, Uk. 198,   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 5, Uk. 204.

136. 137.

140

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 140

2/14/2018 12:11:46 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hao Mitume tumewatukuza baadhi yao zaidi kuliko wengine.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:253).

Al-Bayhaqiy amepokea katika kitabu Fadhailus-Sahaba kwamba alitokeza Ali kwa mbali, ndipo Mtume akasema: “Huyu ni bwana wa Waarabu.” Aisha akasema: “Hivi wewe sio bwana wa Waarabu?” Mtume akasema: “Mimi ni bwana wa viumbe vyote na yeye ni ­bwana wa Waarabu.”138 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2-274).

Ibnu Abbas amesema: “Ali bin Abu Talib alikuwa na dirhamu nne hakuwa anamiliki nyingine zaidi ya hizo, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, nyingine kwa siri na nyingine kwa dhahiri. Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Kitu gani kilichokupelekea kufanya hivyo?” Akasema: Yaliyoniwajibisha kufanya hivyo ni yale aliyoniahidi Mola wangu Mlezi. Mtume akasema: “Umeshapata hilo.” Ndipo ikateremka Aya hii.139

At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 6, Uk. 198.   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 7, Uk. 83.

138. 139.

141

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 141

2/14/2018 12:11:46 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Mariam, hakika Mwenyezi Mungu amekuchagua na amekutakasa, na amekuchagua kuliko wanawake wa ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:42).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha katika wanawake wa ulimwenguni: Maryam, Asia mke wa Firaun, Khadija na Fatima binti Muhammad.”140 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na ­wanawakewenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa ­unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Imepokewa kwamba alipotoa dalili kwa wakristo wa Najran nao wakang’ang’ania ujinga wao aliwaambia: “Hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru kwamba msipokubali hoja niapizane nanyi.”   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 8, Uk. 53.

140.

142

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 142

2/14/2018 12:11:46 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Wakasema: “Ewe Abal-Qasim! mpaka turejee na tutafakari jambo hili kisha kesho tutakuja tena.” Waliporejea wakamwambia Aqib naye alikuwa ndiye wamfuatae katika rai: “Ewe mja wa Masihi unasemaje?” Akasema: “Wallahi enyi wakristo, mmeshajua kwamba hakika Muhammad ni Nabii na Mtume, na wallahi katu hakuna watu walioombeana laana na Mtume kisha mkubwa wao akaendelea kuishi au mdogo wao kuzaliwa. Na kama mtafanya hivyo bila shaka tutaangamia.” Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa katoka akiwa kajitanda kishamiya kilichodariziwa na manyoya meusi huku kamkumbatia Husein na amemshika mkono Hasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima. Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Askofu wa Najran akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia, na hatabaki mkiristo yeyote hapa duniani mpaka Siku ya Kiyama.” Wakasema: “Ewe Abul-Qasim! Tumeona tusiapizane na wewe na tukuwache uendelee kuwa katika dini yako nasi tuendelee kubaki katika dini yetu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Mkikataa kufanya maapizano basi msilimu mtapata haki waliyonayo waislamu na mtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwao.” Wakakataa, ndipo Mtume akawaambia: “Basi hakika mimi nitawafukuzeni kwa kuwauwa.” Wakasema: “Hatuna nguvu ya kupigana vita na waarabu, lakini sisi tunafanya suluhu na wewe usitushambulie kivita na wala usitutoe katika dini yetu. Kwa sharti tukupe kila mwaka Hilla141 elfu mbili: Elfu moja katika mwezi wa Safar na   Jina la pesa kama vile Dola, Shilingi, Paundi na mfano wa hizo.

141.

143

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 143

2/14/2018 12:11:46 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

elfu nyingine katika mwezi wa Rajab, diraya thelathini za chuma za kawaida.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akafanya nao suluhu kwa sharti hilo.142 Fakhru Razi amesema: Aya hii inaonyesha kwamba Hasan na Husein (a.s.) walikuwa watoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Aliwaahidi kwamba atawaita watoto wake, ndipo akaja na Hasan na Husein hivyo ikawajibika kuwa watoto wake. Na linalotia nguvu kauli hii ni kauli ya Mwenyezi Mungu iliyopo katika Surat An’aam: “Na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Sura An’aam:84 – 85). Na yajulikana kwamba Isa amenasibika kwa Ibrahim (a.s.) kupitia mama na si baba. Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote na wala msifarakane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:103).

Imepokewa kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Hakika mimi nawaachieni vizito viwili kati yenu: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka toka mbinguni hadi ardhini. Na kizazi changu Ahlul-Baiti wangu.”143 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 8, Uk. 80. Razi katika riwaya hii ameweka maelezo kwamba: “Tambua kwamba riwaya hii usahihi wake ni sawa na yenye itifaki baina ya wanatafsiri na wanahadithi.” 143.   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 8 Uk. 162. 142.

144

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 144

2/14/2018 12:11:46 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika wale waliokimbia miongoni mwenu siku yalipokutana makundi mawili, ni shetani ndiye aliyewatelezesha kwa sababu ya baadhi ya waliyoyachuma..” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:155).

Razi amesema: “Muradi ni wale watu waliokimbia vitani Siku ya Uhudi. Muhammad bin Is’haqa ametaja kwamba theluthi ya watu walikimbia vitani na miongoni mwa waliokimbia vitani hapo ni Umar bin Khattab na pia Uthman, yeye alikimbia pamoja na watu wawili miongoni mwa Maansari. Walikimbia mpaka wakafika eneo la mbali kabisa kisha wakarejea baada ya siku tatu. Mtume wa ­Mwenyezi Mungu akawaambia:”144

SURAT AN-NISAA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi ambaye amewaumba kutokana na nafsi moja na akaumba kutokana na hiyo wa pili wake.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nisaa’; 4:1).

Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Fatima ni pande la ­nyama yangu. Huniudhi yale yanayomudhi yeye.”145

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 9, Uk. 50.   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 9, Uk. 160.

144. 145.

145

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 145

2/14/2018 12:11:46 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr kwamba alisema: “Hakika siku moja niliswali pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) Swala ya Adhuhuri, muombaji akaomba msikitini na hakuna yeyote aliyempa, ndipo muombaji akainua mikono yake mbinguni na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu shuhudia kwamba bila shaka mimi nimeomba ndani ya msikiti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu na sijapewa chochote na yeyote.” Kipindi hicho Ali alikuwa amerukuu ndipo akamwashiria kwenye chanda chake cha kulia kilichokuwa na pete. Muombaji alikwenda na kuchukua pete toka kwenye chanda chake na hali Mtume akitizama kwa macho yake. Mtume akasema: Ewe Mwenyezi Mungu! Ndugu yangu Musa alikuomba; akasema:

“Ee Mola wangu! Nipanulie kifua changu. Na unifanyie wepesi kazi yangu. Na ufungue fundo katika ulimi wangu. Wapate kufahamu kauli yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Harun. Nitie nguvu kupitia yeye. Na umshirikishe katika kazi yangu.” 146

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 146

2/14/2018 12:11:47 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

(Qur’ani Tukufu Sura Twaha; 20:25-32), ukamteremshia Qur’ani yenye kutamka: Akasema: “Karibuni tutautia nguvu mkono wako kwa ndugu yako na tutakupeni ushindi..” (Qur’ani Tukufu Sura alQasas; 28:35). Ewe Mwenyezi Mungu! Na mimi ni Muhammad Nabii Wako na chaguo Lako. Nipanulie kifua changu. Na unifanyie wepesi kazi yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Ali. Nitie nguvu kupitia yeye.”

Abu Dhari anasema: “Wallahi kabla Mtume wa Mwenyezi ­Mungu (s.a.w.w.) hajamaliza Jibril akateremka na kusema: Ewe Muhammad soma: “Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.”146 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako; na kama hutafanya, basi utakuwa hukufikisha ujumbe Wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:67).

Kutoka kwa Ibnu Abbas na Barau bin Azib wamesema: “Aya hii iliteremka kuonyesha fadhila za Ali bin Abu Talib (a.s.). ilipoteremka Aya hii Mtume alimshika mkono Ali na kusema: “Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu ni mwenye mamlaka juu yake. Ewe Mwenyezi Mungu mpende yule atakayempenda na mfanyie uadui yule atakayemfanyia uadui.” Umar bin Khattab akamwendea na kumwambia: “Hongera ewe mwana wa Abu Talib, umekuwa mwenye mamlaka juu ya kila muumini wa kiume na wa kike.”147   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 12, Uk. 26.   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 12, Uk. 48.

146. 147.

147

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 147

2/14/2018 12:11:47 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-AN’AM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayyub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:84-85). Aya hii inaonyesha kwamba Hasan na Husein (a.s.) ni katika kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), kwa sababu Mwenyezi Mungu amemfanya Isa katika kizazi cha Ibrahim (a.s.) japokuwa hanasibiki kwa Ibrahim ila kupitia mama. Kadhalika Hasan na Husein (a.s.) ni katika kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu. Japokuwa wananasibika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kupitia mama lakini imewajibika wao kuwa miongoni mwa kizazi chake.148

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 13, Uk. 66.

148.

148

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 148

2/14/2018 12:11:47 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ­hawaongozi watu madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:19).

Talha bin Shayba, Abbas na Ali kila mmoja alijigamba. ­Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba funguo zimo mikononi mwangu na hata nikitaka nalala humo.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mgawaji wa maji na msimamizi wake.’ Ali akasema: ‘Mimi ndiye mwanajihadi.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii.149

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake…..”(Qur’ani ­Tukufu Sura Hud; 11:17). Makusudio ya Shahidi hapa ni Ali bin Abu Talib (a.s.).150

SURAT AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:7). Mwonyaji ni Mtume (s.a.w.w.) na Mwongozaji ni Ali. Ibnu Abbas amesema: “Ilipoteremka aya hii, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake na kusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji.’ Kisha akaashiria mkono wake kwenye bega la Ali bin Abu Talib na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji. Kupitia kwako wataongoka wenye kutaka kuongoka baada yangu.”151   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 16, Uk. 11.   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 17, Uk. 201. 151.   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 19, Uk. 14. 149. 150.

149

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 149

2/14/2018 12:11:47 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT TWAHA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Twaha.” (Qur’ani Tukufu Sura Twaha; 20:1). Imesimuliwa kutoka kwa Jafar as-Sadiq (a.s.) kwamba Twa ni utakaso wa Ahlul-Bait. Na Ha ni uongofu wao.152

SURAT AL-HAJJ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hawa mahasimu wawili waliohasimiana kwa ajili ya Mola wao...” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hajj; 22:19).

Amenisimulia Qays bin Ubada kutoka kwa Abu Dharr kwamba alikuwa akiapa kuwa Aya hii iliteremka kwa ajili ya watu sita miongoni mwa Maquraishi waliojitokeza kupambana Siku ya Badri: Hamza, Ali na Ubayda bin al-Harith, Utbatu na Shayabatu watoto wa Rabiu na Walid bin Utbatu. Na kwamba Ali alisema: “Mimi ndiye wa awali ambaye atapiga magoti mbele ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama kwa ajili ya uhasimu.”153

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 22, Uk. 2.   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 23, Uk. 21.

152. 153.

150

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 150

2/14/2018 12:11:47 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia (wanamtakia rehma) Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni (Mtakieni rehma) na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliulizwa ni ipi namna ya kukusalia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Mtume akasema: “Semeni:

“Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim. Na mbariki ­Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.’’

SURAT AL-MU’MIN (AL-GHAFIR) Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akasema mtu muumini aliyekuwa mmoja wa watu wa Firaun anayeficha imani yake; je, mtamuuwa mtu kwa sababu tu anasema Mola wangu Mlezi ni Mwenyezi Mungu?” (Qur’ani Tukufu Sura al Mu’min (al-Ghafir); 40:28).

Imepokewa kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Wakweli ni watatu: Habibu Najjari muumini toka aali Yasin, Muumini toka aali Firaun ambaye alisema: “je, mtamuuwa mtu kwa sababu tu anasema Mola wangu Mlezi ni 151

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 151

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu?” na watatu ni Ali bin Abu Talib naye ndiye mbora wao.”154

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23). Razi amesema: Mwandishi wa kitabu cha tafsiri al-Kashafu amenukuu kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni shahidi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ameghufuriwa. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ametubia. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni muumin aliyekamilika kiimani. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali malaika ameshambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakir. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad atasindikizwa Peponi kama biharusi asindikizwavyo kwenda nyumbani kwa mumewe. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atamfungulia milango miwili ya Pepo kaburini. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake.   At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 27, Uk. 57.

154.

152

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 152

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ehe! atkayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amefia ndani ya Sunna. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni kafiri. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu ya Pepo.” Haya ndiyo aliyoyapokea mwandishi wa al-Kashafu. Na mimi nasema: “Hakuna shaka kwamba Fatima, Ali, Hasan na Husein ­walikuwa na uhusiano wa nguvu mno na Mtume wa Mwenyezi ­Mungu. Na jambo hili ni yakini kwa nukuu mutawatiri hivyo ikawajibika wao wawe ndio aali zake. “Pia watu wametofautiana kuhusu Aali zake, wapo waliosema ni wale karaba zake na wengine wakasema ni umma wake. Tukisema karaba zake ndio Aali basi wao (Ali, Fatima, Hasan na Husein) ndio Aali. Na tukisema Aali ni umma wake uliokubali utume wake bado vilevile wao (Ali, Fatima, Hasan na Husein) ndio Aali zake. Hivyo inathibiti kwamba kwa kipimo chochote kile bado wao ni Aali zake.”155 Lakini je wasiokuwa wao nao wanaingia chini ya tamko Aali? Ni kwamba mwandishi wa Tafsirul-Kashafu amepokea ­kwamba ilipoteremka Aya hii palisemwa: “Ewe Mtume wa ­Mwenyezi ­Mungu! Ni akina nani hawa karaba zako tuliowajibishwa ­kuwapenda?” ­Akajibu: “Ali, Fatima na watoto wao wawili.” Hivyo ­imethibiti kwamba hawa ndio karaba wa Mtume (s.a.w.w.). na hili likithibiti inawajibika taadhima ya ziada iwe makhsusi kwao. Na hilo ­linathibitishwa na mambo mane: Kwanza: Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Mapenzi katika ndugu.” 155.

At-Tafsiru al-Kabir cha Razi Juz. 27, Uk. 66. 153

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 153

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Pili: Hamna shaka kwamba Mtume (s.a.w.w.) alikuwa akimpenda sana Fatima (a.s.), akasema: “Fatima ni pande la nyama yangu, huniudhi yale yanayomuudhi.” Na imethibiti kwa nukuu mutawatiri kutoka kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kwamba alikuwa akiwapenda Ali, Hasan na Husein. Likithibiti hilo inawajibika mfano wa hilo kwa umma wote (yaani umma wote uwapende) kwa mujibu wa kauli yake (s.a.w.w.): “Mfuateni ili mpate kuongoka.”156 Na kauli yake (s.w.t.): “Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni Mwenyezi Mungu atawapenda”157 Na kauli yake (s.w.t.): “Bila shaka mnao mfano mwema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu”.158 Tatu: Hakika dua kwa ajili ya Aali ni hadhi adhimu, na kwa ajili hiyo ameifanya dua hii kuwa ni hitimisho la Tashahudi katika Swala. Nayo ni kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad na Aali Muhammad na mrehemu Muhammad na Aali Muhammad.” Taadhima hii haijapatikana katika haki za mwingine asiyekuwa Aali. Hayo yote yanaonyesha kwamba kuwapenda Aali Muhammad ni wajibu. Imam Shafi amesema:

“Ewe uliye juu ya kipando! simama Mina eneo lenye changarawe. Mtangazie aliyopo maeneo ya bondeni na yale ya miinuko. Usiku watakapofurika mahujaji Mina. Kama yafurikavyo mawimbi ya mto Furati.   (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:158).   (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:31). 158.   (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:21). 156. 157.

154

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 154

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ikiwa kuwapenda Aali Muhammad ni urafidhi Basi vizito viwili vishuhudie kwamba mimi ni rafidhi.”159

SURAT AL-AHQAF Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na kubeba mimba na kumwachisha ziwa ni miezi thelathini” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahqaf; 46:15). Amesema: Aya hii imeonyesha kwamba muda wa chini kabisa wa mimba kukaa tumboni ni miezi sita, kwa sababu jumla ya muda wote wa mimba na kunyonya ni miezi thelathini. Amesema (s.w.t.): “Na wazazi wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili;” hivyo katika miezi thelathini tukitoa miaka miwili kamili ambayo ni sawa na miezi ishirini na nne, inabaki miezi sita ambayo ndio muda wa chini kabisa wa mimba kukaa tumboni. Imepokewa kutoka kwa Umar kwamba kuna mwanamke alipelekwa kwake na alikuwa amejifungua mimba ya miezi sita, ndipo (Umar) akaamuru apigwe mawe. Ali (a.s.) akasema: “Hastahiki kupopolewa mawe.” Na akataja kanuni ya ufumbuzi kama tulivyoeleza.160

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 27, Uk. 66.   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 28, Uk. 15.

159. 160.

155

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 155

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Al-Wahidiy ametaja kutoka kwa jamaa zetu katika kitabu alBasiti kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali. Na mwandishi wa alKashafu toka kwa muutazila amekitaja kisa hiki kwa kupokea toka kwa Ibn Abbas kwamba alisema: Hasan na Husein (a.s.) walipatwa na maradhi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona akiwa pamoja na baadhi ya watu. Wakasema: “Ewe AbalHasan ni vizuri lau ukiweka nadhiri kwa ajili ya wanao.” Ndipo Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhiri kwamba iwapo watapona watafunga siku tatu. Wakapona na hali wao hawana kitu, ndipo Ali akakopa toka kwa Simon Myahudi wa Khaybar, pishi tatu za ngano. Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano kulingana na idadi yao, wakaiweka mbele yao ili wafuturu, mara masikini akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni maskini katika watoto wa kiislamu nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakamfanyia kipaumbele na wao wakalala na hali hawajaonja ila maji tu na wakaamka wakiwa na Swaumu. Waliposhinda na Swaumu na kuweka chakula mbele yao mara akafika mlangoni kwao yatima naye wakamfanyia kipaumbele. Na mara mfungwa wa kivita akafika mlangoni kwao siku ya tatu, naye wakamfanyia hivyo hivyo. Asubuhi iliyofuata Ali aliwashika mkono Hasan na Husein (a.s.) na kwenda nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Alipowatizama na hali wao wawili kutokana na njaa kali wakitetemeka kama vifaranga alisema: “Hali niionayo kwenu yaniumiza mno.” Akasimama na kwenda nao, ndipo wakamkuta Fatima akiwa mihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake na macho yake yamebadilika. Hali hiyo ikamuuma sana, ndipo Jibril (a.s.) akateremka na kusema: “Ewe Muhammad 156

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 156

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Jibril (a.s.) akamsomea Sura hii.161

SURAT AL-KAWTHAR Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika sisi tumekupa kheri ­nyingi.” (Qur’ani Tukufu Sura al Kawthar; 108:1). Amesema: Kheri nyingi (Kawthar) hapa ni watoto wake (s.a.w.w.). Wamesema: Kwa sababu Sura hii iliteremka ikiwa ni jibu kwa wale waliokuwa wakimkashifu Mtume (s.a.w.w.) kwa ­kutokuwa na ­watoto wa kiume. Hivyo maana yake ni kwamba Yeye (s.w.t.) atampa kizazi kitakachodumu muda wote. Hebu tazama ni watu wangapi wameuawa toka katika Ahlul-Baiti lakini bado ­ulimwengu umejaa wao, na hakuna Bani Umaiyya yeyote ambaye anatiliwa umuhimu na kuheshimiwa. Kisha tazama ni jinsi gani wao (AhlulBaiti) walivyotoa ulamaa wakubwa kama vile al-Baqir, ­as-Sadiq, ­al-Kadhim, ar-Radhi (a.s.) na Nafsuz-Zakiyya.162

At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 30, Uk. 244.   At-Tafsir al-Kabir cha Razi Juz. 32, Uk. 124.

161. 162.

157

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 157

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA AL-BAYDHAWI, INAYOITWA AN’WARUT-TANZIIL WAASRARUT-TAAWIIL: SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274). Imesemwa kwamba: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya AmirulMuuminina (a.s.), hakuwa anamiliki zaidi ya dirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, nyingine siri na nyingine dhahiri.”163

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:37). Imepokewa kwamba Fatima alimzawadia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) vipande viwili vya mkate na kipande cha nyama, naye akavirejesha kwa Fatima na kusema: “Chukua ewe binti yangu.” Alipofunua bakuli akalikuta limejaa mikate na nyama. Mtume akamwambia umetoa wapi hivi? Akasema: “Ni kutoka kwa Mwe  Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 1, Uk. 141, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D.

163.

158

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 158

2/14/2018 12:11:48 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Mtume akasema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ­Ambaye amekufanya kifani wa bibi wa wana wa Israel (Mariam).” Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawakusanya Ali bin Abu Talib, Hasan na Husein na watu wote wa nyumbani kwake wakala pamoja mpaka wakashiba na chakula kikabakia kama ­kilivyokuwa. Hivyo Fatima akawagawia majirani zake.164 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipowaomba wafanye maapizano walisema mpaka tutafakari. Walipoachana wakamwambia Aqib naye alikuwa ndiye wamfuatae katika rai: “Unaonaje?” Akasema: “Wallahi enyi wakristo mmeshaujua utume wake na bila shaka amewajieni na hoja yakinifu kuhusu mtu wenu (Yesu), wallahi katu hakuna watu walioombeana laana na Mtume kisha mkubwa wao akaendelea kuishi au mdogo wao kuzaliwa. Na kama mtafanya hivyo bila shaka mtaangamia, hivyo ila ni nyinyi kuendelea kubakia   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 1, Uk. 158, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1969 A.D.

164

159

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 159

2/14/2018 12:11:49 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

katika imani yenu na dini yenu, nendeni mkamuage mtu huyu na mrejee nchini kwenu.” Ndipo kesho yake wakaenda kwa Mtume wa Mwenyezi ­Mungu (s.a.w.w.), na Mtume akatoka akiwa amemkumbatia Husein na amemshika mkono Hasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima. Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Askofu wao akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia.” Wakamsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu na wakampa kodi ya Hilla165 elfu mbili na diraya thelathini za chuma. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, lau wangefanya maapizano wangegeuzwa nyani na nguruwe na bonde lao lingewaka moto. Na Mwenyezi Mungu angeiteketeza Najran na watu wake hata ndege aliyopo juu ya mti. Al-Baydhawi mwandishi wa tafsiri hii anasema katika maelezo yake: Nayo ni dalili ya unabii wake na ya ubora wa wale aliokwenda nao miongoni mwa Ahlul-Baiti wake.166

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Jina la pesa kama vile Dola, Shilingi, Paundi na mfano wa hizo.   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 1, Uk. 164, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D.

165. 166.

160

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 160

2/14/2018 12:11:49 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Yenyewe iliteremka kwa ajili ya Ali (a.s.) pindi muombaji ­alipomwomba na hali amerukuu ndani ya Swala, akamvulia pete yake.167

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.”(Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1).

Imepokewa kwamba ilipoteremka Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma Ali (a.s.) akiwa amepanda al-Adhbau168 ili akawasomee mahujaji wa msimu huo. Kabla ya hapo alikuwa tayari keshamtuma Abu Bakr awe kiongozi wa Hija ya msimu huo. Pakasemwa: Kwa nini usingemtuma Abu Bakr akawasomee? Akasema: “Hafikishi kwa niaba yangu ila mtu atokanaye na mimi.”169

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Siku tutakapowaita kila watu ­pamoja na viongozi wao.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:71).   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 1, Uk. 291, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D. 168.   Jina la ngamia wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). 169.   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 1, Uk. 404, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D. 167.

161

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 161

2/14/2018 12:11:49 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Pakasemwa: Viongozi wao: Yaani tutawaita kwa majina ya mama zao. Na hekima katika hilo ni kumtukuza Isa (a.s.) na kudhihirisha sharafu ya Hasan na Husein (a.s.).170

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Imepokewa kwamba siku moja Mtume (s.a.w.w.) alitoka na hali kajifunika shuka lililodariziwa na manyoya meusi. Akaketi na ghafla akaja Fatima akamfunika, kisha akaja Ali akamfunika, wakaja Hasan na Husein (a.s.) akawafunika, kisha akasema: “Hakika si mengineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume.”171 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini ­wanawake pasi na wao kustahili, hakika wamebeba uzushi na ­dhambi kumbwa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:58).   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 1, Uk. 592, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D. 171.   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 2, Uk. 245, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D. 170.

162

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 162

2/14/2018 12:11:49 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Imesemwa: Iliteremka kwa ajili ya wanafiki pale walipokuwa wakimuudhi Ali (a.s.).172

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa ­mapenzi katika ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23).

Imepokewa kwamba: Ilipoteremka palisemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa karaba zako ­ambao tumewajibishwa kuwapenda? Akasema: “Ali, Fatima na watoto wake wawili.”173

SURAT AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na tukampulizia humo roho yetu na akayasadikisha maneno ya Mola Wake Mlezi, na vitabu vyake na alikuwa miongoni mwa ­wanyenyekevu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:12).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: “Kati ya ­wanaume wamekamilika wengi na wala hawajakamilika kati ya wa  Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 2, Uk. 252, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D. 173.   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 2, Uk. 357, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D. 172.

163

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 163

2/14/2018 12:11:50 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nawake ila wanne: Asia binti Muzahim mke wa Firaun, Mariam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.”174

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Hasan na Husein (a.s.) walipatwa na maradhi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona akiwa pamoja na baadhi ya watu. Wakasema: “Ewe Abal-Hasan ni vizuri lau ukiweka nadhiri kwa ajili ya wanao.” Ndipo Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhiri kwamba iwapo watapona watafunga siku tatu. Wakapona na hali wao hawana kitu, ndipo Ali akakopa toka kwa Simon Myahudi wa Khaybar, pishi tatu za ngano. Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano, wakaiweka mbele yao ili wafuturu, mara masikini akafika mlangoni kwao wakamfanyia kipaumbele na wao wakalala na hali hawajaonja ila maji tu na wakaamka wakiwa na Swaum. Waliposhinda na Swaumu na kuweka chakula mbele yao mara akafika mlangoni kwao yatima naye wakamfanyia kipaumbele. Na mara mfungwa   Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 2, Uk. 488, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D.

174.

164

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 164

2/14/2018 12:11:50 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wa kivita akafika mlangoni kwao siku ya tatu, naye wakamfanyia hivyo hivyo. Ndipo Jibril (a.s.) akateremka na Sura hii na kusema: “Ewe Muhammad ipokee, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa ­kitendo cha watu wa nyumba yako.”175

Tafsirul-Baydhawi iitwayo An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil Juz. 2, Uk. 526, Chapa ya Pili ya Misri ya Mwaka 1968 A.D.

175.

165

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 165

2/14/2018 12:11:50 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA AL-QURTUBI, INAYOITWA AL-JAMIU LIAHKAMIL-QUR’ANI SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya ­ wenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja.” M (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:207).

Imesemwa kwamba Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.) alipoachwa na Mtume (s.a.w.w.) alale kitandani kwake usiku aliotoka kwenda pangoni.176 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274).

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.), alikuwa na dirha  Tafsirul-Qurtubi Juz. 3, Uk. 21. Na pia imepokewa katika kitabu Tadhkiratul-Khuwas Uk. 35 na kitabu Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 97 na kitabu Faraidus-Samtwayni Juz. 1, Uk. 330.

176.

166

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 166

2/14/2018 12:11:50 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, ­nyingine siri na nyingine dhahiri.”177

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ­ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:42).

Imepokewa kwa njia sahihi kama ilivyopokewa kutoka kwa Abu Huraira kwamba (s.a.w.w.) alisema: “Kati ya wanawake wa ulimwenguni wabora ni wanne: Maryam binti Imran, Asia binti Muzahim mke wa Firaun, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad.”178 Na katika Hadithi ya Ibn Abbas ni kwamba Mtume alisema: “Walio bora kati ya wanawake wa Peponi ni: Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad, Maryam binti Imran na Asia binti Muzahim.” Na katika njia nyingine kutoka kwake amesema walio bora kati ya wanawake wa Peponi ni: “Baada ya Mariam ni Fatima na Khadija.” Amepokea Musa bin Aqaba kutoka kwa Kuraybu kutoka kwa Ibn Abbas amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Seyyida wa wanawake wa peponi ni Mariam, Fatima, Khadija na Asia.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Qurtubi Juz. 3, Uk. 347.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 4, Uk. 83.

177. 178.

167

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 167

2/14/2018 12:11:50 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Al-Qurtubi amesema: “Hakika Mtume (s.a.w.w.) alikwenda na Hasan na Husein na Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma yao huku akisema: “Nitakapoomba muitikie.” Na anasema: Ulamaa wengi wamesema: “Hakika kuwaita Hasan na Husein wakati wa maapizano kwamba ni watoto: “tuwaite watoto wetu na watoto wenu” na kusema kuhusu Hasan: “Hakika mwanangu huyu ni bwana.” Uitaji huo ni makhsusi kwa ajili ya Hasan na Husein (a.s.), wao ndio waitwe watoto wa Mtume (s.a.w.w.) na si wengineo, hiyo ni kwa mujibu wa kauli yake: “Kila sababu na nasaba itakatika Siku ya Kiyama ila nasaba yangu na sababu yangu.” Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na bila shaka Mwenyezi Mungu alikusaidieni katika Badri hali nyinyi ni madhalili. Basi mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kushukuru.”(Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:123). Ibnu Is’haqa ametaja kutoka kwa Ammar binYasir kwamba alisema: “Mimi na Ali tulikuwa pamoja katikaVita vya Ashira huko Batnu Yanbui.

168

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 168

2/14/2018 12:11:50 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipofika hapo alikaa mwezi mmoja na hatimaye akafanya suluhu na Bani Mudliju na washirika wao kutoka Bani Dhamra kisha akawaaga. Ali bin Abu Talib (a.s.) aliniambia: “Upo tayari ewe Abul-Yaqdhan tuwaendee hawa jamaa? Kundi la Bani Mudliju linafanya kazi katika mto wao, twende tukachunguze jinsi gani wanavyofanya kazi.” Tukawaendea na tukaona ardhi ifaayo tukalala hapo. Wallahi hakuna aliyetuamsha ila Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa nyayo zake. Tukaketi na hali tumetapakaa udongo na siku hiyo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Una habari gani ewe Abu Turab?” Naye akamweleza jambo letu. Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Je, niwajulisheni watu wawili walio waovu mno kuliko watu wengine?” Tukasema, ndio ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: “Uhaymar wa kabila la Thamudi yule aliyemchinja ngamia. Na yule atakayekupiga dhoruba ewe Ali juu ya hiki.” Mtume wa Mwenyezi Mungu akaweka mkono wake juu ya kichwa cha Ali. “Mpaka hizi zilowane kwa damu yake.” Akaweka mkono wake juu ya ndevu zake.179

SURAT AN-NISAA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsirul-Qurtubi Juz. 4 Uk. 192

179.

169

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 169

2/14/2018 12:11:51 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Enyi mlioamini! Msikaribie Swala na hali mmelewa mpaka myajue mnayoyasema; wala mkiwa na janaba isipokuwa wapita njia mpaka muoge. Na muwapo wagonjwa au mkiwa safarini au akawa mmoja wenu ametoka chooni au mkagusana na wanawake, kisha msipate maji, basi tayamamuni na mchanga ulio twahara; mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe Mwenye kughufiria.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nisaa’; 4:43).

Imepokewa kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba haikuwa ni ruhusa kwa yeyote kupita ndani ya msikiti wala kukaa humo ila Ali bin Abu Talib (a.s.).180 Na ameipokea Atiyyat al-Awafiy kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Haipasi wala haifai kwa mwislamu kupatwa na janaba na akawa msikitini ila mimi na Ali.” Na linaloonyesha kwamba nyumba ya Ali ilikuwa msikitini ni ile riwaya aliyoipokea Shihab kutoka kwa Salim bin Abdullah, amesema: “Mtu mmoja alimuuliza baba yangu kuhusu Ali na Uthman ni yupi kati ya hawa wawili alikuwa bora? Abdullah bin Umar akamwambia: ‘Hii ni nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu.’ Huku akiashiria nyumba ya Ali (a.s.).”181 Umar bin Maymun amepokea kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Zibeni milango ila mlango wa Ali.” Akaacha mlango wake (Ali) tu msikitini.182   Tafsirul-Qurtubi Juz. 5, Uk. 207. Atau amepokea kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Haikuwa Muta ila ni huruma ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake na lau si Umar kukataza kuoa ndoa ya muda (Muta) asingelizini ila mwovu wa kupindukia.” Tazama Tafsirul-Qurtubi Juz. 5, Uk. 130. 181.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 5, Uk. 207. 182.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 5, Uk. 208. 180.

170

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 170

2/14/2018 12:11:51 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Enyi mlioamini! Mtiini ­Mwenyezi Mungu na mtiini Mtume na wenye mamlaka katika nyinyi.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nisaa’; 4:59). Al-Qurtubi amesema: “Hakika muradi wa “Wenye mamlaka” ni Ali na Maimamu maasumina.”183

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Ibnu Abbas amepokea kwamba aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.), ni kwamba muombaji aliomba ndani ya msikiti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na hakuna yeyote aliyempa kitu. Muda huo Ali alikuwa amerukuu akiswali na hali kuliyani amevaa pete, ndipo akamwashiria muombaji mpaka akaichukua.184 Na imepokewa kwamba Ali (a.s.) alimpa muombaji kitu na hali akiwa katika Swala.185

SURAT AL-AN’AM Kauli ya Mwenyezi Mungu: 183.  Tafsirul-Qurtubi Juz. 5, Uk. 261. 184.  Tafsirul-Qurtubi Juz. 6, Uk. 221. 185.  Tafsirul-Qurtubi Juz. 6, Uk. 222. Kadhalika amepokea katika Dhakhairul-Uqba Uk. 102; Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 161. Na Manaqibul-Maghazali Uk. 311. Na Yanabiul-Mawaddah Uk. 218. 171

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 171

2/14/2018 12:11:51 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na tukampa Is’haka na Yaakub, wote tukawaongoza, na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:84-85).

Al-Qurtubi anasema: “Isa amejumuishwa katika kizazi cha Ibrahim na hali ni mtoto wa kupitia binti, hivyo watoto wa Fatima (a.s.) ni kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.).”186 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mpasuaji wa mbegu na kokwa, hutoa mzima katika maiti, na mtoaji wa maiti katika mzima, huyo ndiye Mwenyezi Mungu, basi mnageuzwa wapi?” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:95).

Katika Sahih Muslim imepokewa kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema: “Naapa kwa yule ambaye huchipusha mbegu na ku  Tafsirul-Qurtubi Juz. 7, Uk. 32.

186.

172

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 172

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

umba nafsi, hakika yenyewe ni ahadi aliyoniahidi Mtume kwamba ­hanipendi ila muumini na wala hanichukii ila mnafiki.”187

SURAT AL-A’ARAF Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Ni nani aliyeharamisha mapambo ya Mwenyezi Mungu ambayo amewatolea waja wake na vitu vizuri vya riziki? Sema: Vitu hivyo ni kwa waumini katika maisha ya dunia na khasa Siku ya Kiyama. Hivyo ndivyo tunavyozibainisha Aya kwa watu wanaojua.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:32).

Imepokewa kutoka kwa Ali bin Husein bin Ali bin Abu Talib (a.s.) Sheikh wa Malik, kwamba alikuwa akivaa joho lililotengenezwa kwa hariri lenye thamani ya dinari khamsini, analivaa masika na inapofika kiangazi analitoa sadaka au analiuza na anatoa sadaka pato lake.188 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na juu ya mahala palipoinuka patakuwa na watu watakaowafahamu wote kwa alama zao.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf: 7:46).   Tafsirul-Qurtubi Juz. 7, Uk. 44. Na ameiandika al-Jazriy as-Shafi katika Asnal-­Matwalib Uk. 55, na Ibnu Athir katika Usudul-Ghaba Juz. 6, Uk. 84 na Tahdhibut-Tahdhib Juz. 3, Uk. 479, na al-Iswabah Juz. 2, Uk. 35, na Kanzul-Ummal Juz. 6, Uk. 394, na arRiyadhun-Nadhrah Juz. 2, Uk. 224, na Nurul-Absar Uk. 72 na Hilyatul-Awliyai Juz. 6, Uk. 294. 188.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 7, Uk. 195. 187.

173

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 173

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

At-Thaalabi ametaja kwa njia yake kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “ Na juu ya mahala palipoinuka patakuwa na watu” kwamba ni sehemu ya juu iliyopo kwenye Sirat hapo atakuwepo Hamza, Ali bin Abu Talib na Jafar mwenye mbawa mbili (a.s.), wao watawatambua wale wenye mapenzi na wao kwa mng’aro wa nyuso zao na wale wenye chuki na wao kwa ufifiaji wa nyuso zao.189 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Musa akamwambia ndugu yake Haruni: Shika nafasi yangu katika watu wangu na utengeneze wala usifuate njia ya waharibifu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:142).

Katika Sahih Muslim kutoka kwa Said bin Abi Waqqas amesema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akimwambia Ali pindi alipomwachia nafasi yake alipoenda katika moja ya vita vyake: “Huridhii kwamba wewe una nafasi kwangu sawa na ile ya Harun kwa Musa ila ni kwamba hakuna Nabii baada yangu?”190 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wale wanaomcha Mungu zinapowagusa pepesi za Shetani mara hukumbuka tahamaki wamekwishaona njia.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:201). Iswamu bin al-Mutliq amesema: Niliingia Madina mara nikamwona Hasan bin Ali (a.s.), umbo na hulka yake vikanishangaza na ndipo husuda iliyokuwa imefichwa na kifua changu   Tafsirul-Qurtubi Juz. 7, Uk. 212.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 7 Uk. 277. Ameiandika Sheikh Kamalud-Din Muhammad bin Talha as-Shafi katika kitabu chake Matalibus-Suul Fi Manaqibi Alir-Rasuul Juz. 1 Uk. 85, Chapa ya Muassasatu Ummil-Qura.

189. 190.

174

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 174

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

miongoni mwa chuki dhidi ya baba yake ikanijaa na ghafla ­nikasema: “Wewe ni mtoto wa mwana wa Abu Talib? “ Akasema ndio. Nikapindukia katika kumtusi na kumtusi baba yake. Akanitizama kwa jicho la upole na huruma kisha akasema: “Najikinga kwa Mwenyezi Mungu dhidi ya Shetani. Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu: “Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:199). Kisha akasema: “Jipunguzie uzito, najiombea na ninakuombea maghfira kwa Mwenyezi Mungu, lau ungetuomba msaada wa hali tungekusaidia. Lau ungetuomba msaada wa mali tungekupa. Lau ungetuomba tukuongoze tungekuongoza.” Akatambua majuto niliyokuwa nayo juu ya ukiukwaji uliyotokana na mimi. Akasema: “Hakuna lawama juu yenu leo, Mwenyezi Mungu atakusameheni, naye ni Mbora wa kurehemu. Je wewe ni mtu wa Shamu?” Nikasema ndio. Akasema: “Ni ada niijuayo toka kwa nyoka.191 Mwenyezi Mungu akupe uhai na kuinua heshima yako. Akupe afya njema na akusaidie. Eleza haja yako na matatizo yako kwetu utatukuta ni kinyume na dhana yako juu yetu, inshaallah.” Iswamu anasema: “Japo ardhi ni pana lakini niliona imenibana, nikatamani inimeze kisha nijifiche humo. Nikatoka hapo na hali hakuna mtu nimpendaye katika ardhi hii kuliko yeye na baba yake.”192

Waswahili husema: Mtoto wa nyoka ni nyoka. – Mtarjumi.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 7 Uk. 397.

191. 192.

175

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 175

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na walipokupangia njama wale waliokufuru ili wakufunge au wakuue au wakutoe na wakafanya hila na Mwenyezi Mungu akafanya hila na Mwenyezi Mungu ni Mbora wa wafanyao hila.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:30).

Hii ni kutoa habari za njama na hila walizokubaliana Mushrikina kumfanyia Mtume (s.a.w.w.) huko katika bunge lao, hivyo wakakubaliana wamuuwe na hivyo usiku wakamzingira na kumvizia kwenye mlango wa nyumba yake usiku kucha ili wamuuwe atakapotoka. Mtume (s.a.w.w.) akamwamuru Ali bin Abu Talib alale kitandani kwake na akamwomba Mwenyezi Mungu awafumbe macho wasione azimio lake. Mwenyezi Mungu akawafumba macho yao na walipofika asubuhi Ali alitoka na kuwaambia ndani ya nyumba hamna mtu yeyote.193 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na masikini na msafiri……” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:41). Al-Man’hal bin Amru amesema: Nilimuuliza Abdullah bin Muhammad bin Ali na Ali bin Husein kuhusu Khumsi, akasema: “Hiyo ni ya kwetu.” Nikamwambia Ali: Hakika Mwenyezi Mungu anasema: “…na mayatima na masikini na msafiri…” Akasema: “Mayatima wetu na maskini wetu.”194   Tafsirul-Qurtubi Juz. 7 Uk. 397.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 10.

193

194.

176

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 176

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:19).

Al-Qurtubi anasema: “Dhahiri ya Aya ni kubatilisha kauli ya ­aliyejigamba miongoni mwa Mushrikina kwa kunywesha mahujaji na kuamirisha msikiti kama alivyotaja as-Sadiy, amesema: Abbas alijigamba kwa kunywesha, na as-Shayba kwa kuamirisha na Ali kwa uislamu na jihadi. Mwenyezi Mungu akamuunga mkono Ali na kuwapinga hao wawili.195 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Bila shaka Mwenyezi Mungu amekusaidieni katika mapigano mengi na Siku ya Hunayn.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:25). Waislamu walishindwa na kukimbia vitani na hakuna yeyote ­aliyemjali mwenzake. Mtume akabaki thabiti akiwa pamoja na ndugu zake Ali na Abbas. Siku hiyo ya Hunayni Ali (a.s.) aliuwa watu arobaini kwa mkono wake.196   Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 91. Asbabun-Nuzuul Uk. 164. Rabiul-Abrar cha Zamakhshari Uk. 484. Al-Fusuulul-Muhimmah Uk. 106. Manaqibul-Mughazaliy Uk. 321. Faraidus-Samtwayni Juz. 1, Uk. 203. 196.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 97. 195.

177

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 177

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Yeye ndiye aliyemtuma Mtume Wake kwa mwongozo na kwa dini ya haki ili ishinde dini zote, ingawa Mushrikina watachukia.” (Qur’ani Tukufu Sura atTawba; 9:33). Yaani ni dini ya Uislamu izishinde dini zote. As-Sadiy amesema: “Hiyo ni pale atakapodhihiri Mahdi, hapo hatabaki yeyote ila ataingia katika Uislamu na kulipa kodi. Na zimeenea habari sahihi kwamba Mahdi ni kutoka kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)197 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Muhajiri na Ansari...” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:100). Imepokewa kutoka kwa Zaid bin Arqam, Abu Dharr, ­Miqdad na wengineo kwamba: Wa kwanza kuupokea uislamu ni Ali (a.s.).198 Al-Hakim Abu Abdillah amesema: “Siijui tofauti ya wanahistoria juu ya kwamba Ali ndiye wa kwanza kuupokea uislamu.” Is’haqa bin Ibrahim Rahawayhi al-Handhaliy alikuwa mwandishi wa khabari, hivyo alikuwa akisema: Wa kwanza kusilimu katika wanawake ni Khadija na katika watoto ni Ali.199 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Bila shaka Mwenyezi Mungu amekwishapokea toba ya Mtume na Muhajiri na Ansari waliomfuata yeye katika saa ya dhiki….” (Qur’ani Tukufu Sura atTawba; 9:117). Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alitoka mwezi wa Rajab akakaa Tabuk mwezi wa Shabani na siku kadhaa katika mfungo wa   Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 121.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 236. 199.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 237. 197. 198.

178

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 178

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ramadhan. Akatuma kikosi chake na kufanya suluhu na jamaa kwa sharti la kodi. Katika vita hivi alimwacha Ali Madina. Wanafiki wakasema: Amemwacha kwa sababu amemchukia. Akamfuata Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia. Mtume akasema: “Huridhii kwamba una nafasi kwangu sawa na ile ya Harun kwa Musa.”200

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola Wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:17).

Imepokewa kwamba Ibnu Abbas alisema: Shahidi ni Ali bin Abu Talib (a.s.).201 Imepokewa kutoka kwa Ali kwamba alisema: “Hakuna mtu yeyote miongoni mwa makuraishi ila Aya moja au mbili zilishuka kwa ajili yake.” Ndipo mtu mmoja akamwambia: “Ni ipi iliyoteremka kwa ajili yako?’’Ali akasema: “….. Na anaifuata na shahidi atokaye kwake..”

SURAT AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsirul-Qurtubi Juz. 8, Uk. 280.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 9, Uk. 16.

200. 201.

179

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 179

2/14/2018 12:11:52 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani za mizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina na isiyochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:4).

Imepokewa kutoka kwa Jabir bin Abdullah kwamba alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akimwambia Ali (a.s.): “Watu wanatokana na miti tofauti. Na mimi na wewe tunatokana na mti mmoja.” Kisha Mtume (s.a.w.w.) akasoma: “Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani za mizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina na isiyochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale.”202

SURAT AN-NAHL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Anayemkataa Mwenyezi Mungu baada ya imani yake (ataadhibiwa) isipokuwa yule aliyelazimishwa hali moyo wake unatulia kwa imani.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nahl; 16:106).

Imepokewa kutoka kwa Anas bin Malik kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Pepo ina shauku na watu watatu: Ali, Ammar na Salman.”203

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Qurtubi Juz. 9, Uk. 283.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 10, Uk. 181.

202. 203.

180

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 180

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Kama mkifanya wema mtajifanyia wema nafsi zenu, na kama ­mkifanya ubaya, basi mtajifanyia wenyewe...” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:7).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Mwenyezi Mungu alimfunulia Muhammad (s.a.w.w.) kwamba: “Hakika mimi nilimuua Yahya bin Zakariya mara elfu sabini. Na hakika mimi nitamuua mtoto wa binti yako maradufu ya elfu sabini.”204 Na kutoka kwa Qarrat bin Khalid amesema: Mbingu haikumlilia yeyote ila Yahya bin Zakaria na Husein bin Ali. Na wekundu wake ndio kilio chake. Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Siku tutakapowaita kila watu pamoja na viongozi wao.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:71). Muhammad bin Kaab amesema: Viongozi wao: Yaani mama zao. Ili kud-hihirisha sharafu ya Hasan na Husein (a.s.).205

SURAT AL-KAHF Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na ama yule kijana, basi wazazi wake walikuwa waumini, na tukahofia kwamba asije akawapele kea katika uasi na ukafiri.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Kahf; 18:80).

Abu Umar bin Abdul-Barri katika kitabu at-Tamhid kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba Ali alisema: “Mtume (s.a.w.w.) alipofariki   Tafsirul-Qurtubi Juz. 10, Uk. 217.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 10, Uk. 297.

204. 205.

181

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 181

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

na kufunikwa na nguo kuna sauti ilitoka upande mmoja wa nyumba, wakawa wanasikia sauti lakini hawamwoni msemaji: ‘Assalam Alaykum Warahmatullah Wabarakatuhu. Assalamu Alaykum AhlalBayt.”’206

SURAT MARYAM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” (Qur’ani Tukufu Sura Maryam; 19:96).

Imesemekana kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali (a.s.). Al-Barau bin Azib amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali bin Abu Talib: “Ewe Ali sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwako na niwekee mapenzi katika nyoyo za waumini.”207

SURAT AL-ANBIYA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na hatukutuma kabla yako ila ­ wanaume tuliowapa wahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anbiya; 21:43). Jabir al-Jaafiy, amesema: “Ilipoteremka Aya hii Ali bin Abu Talib alisema: ‘Sisi ndio wenye ukumbusho.’” 208   Tafsirul-Qurtubi Juz. 11, Uk. 44.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 11, Uk. 161. 208.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 11, Uk. 272. 206. 207.

182

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 182

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-FURQAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Naye ndiye aliyemuumba mwanadamu kutokana na maji na akamjaalia kuwa na nasaba na ukwe. Na Mola wako ni Mwenye uwezo.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Furqan; 25:54).

Amepokea Muhammad bin Is’haqa kutoka kwa Yazid bin ­Abdullah bin Qusayti kutoka kwa Muhammad bin Usama bin Zaid kutoka kwa baba yake kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ewe Ali! Wewe ni mkwe wangu na baba wa wanangu. Na wewe ni kutokana na mimi na mimi ni kutokana na wewe.” 209

SURAT AN-NAML Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Suleiman alimrithi Daud. Na akasema: Enyi watu! Tumefunzwa usemi wa ndege. Na tumepewa kila kitu. Hakika hii ni fadhila iliyo dhahiri.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Naml; 27:16).

Hasan bin Ali bin Abu Talib (a.s.) amesema: “Kipozamataza aliapo huwa anasema: Ewe Mungu wangu! Walaani wenye kuwabughudhi Aali Muhammad.”210

SURAT AS-SAJDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Qurtubi Juz. 13, Uk. 60.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 13, Uk. 166.

209. 210.

183

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 183

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.” (Qur’ani Tukufu Sura as-Sajda; 32:18).

Ibnu Abbas na Atau bin Yasar wamesema: “Iliteremka ikimuhusu Ali bin Abu Talib na Walid bin Uqbah bin Abu Muit. Walizozana na ndipo Walid bin Uqbah akasema: ‘Mimi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye meno makali kuliko wewe na shujaa kuliko wewe.’Ali (a.s.) akasema: ‘Nyamaza bila shaka wewe ni fasiki.’ Ndipo ikateremka Aya hii. 211 Az-Zajjaj na an-Nuhhas wametaja kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali na Uqba bin Abi Muit.

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Al-Kalbiy amesema: Nao ni Ali, Fatima, Hasan na Husein tu. Katika kuthibitisha hili kuna Hadithi kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.). ummu Salama amesema: Aya hii iliteremkia nyumbani kwangu. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husein akawafunika kishamia cha Khaybar, akasema: “Hawa ndio Ahlul-Bait wangu.” Akasoma Aya. Kisha akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.’’ Ummu   Tafsirul-Qurtubi Juz. 14, Uk. 105. Shawahidut-Tanziil ya al-Haskaniy Juz. 1, Uk. 445. Manaqibul-Maghazaliy Uk. 324. Asbabun-Nuzuul Uk. 236.

211.

184

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 184

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Salama akasema: ‘Mimi ni pamoja nao ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?’Akasema (s.a.w.w.): ‘Wewe bakia ulipo na wewe upo katika kheri.”’ Hadithi hii ameiandika Tirmidhi na wengineo.212 Al-Qurtubi amesema: “Jambo hili limeenea katika habari kwamba ilipoteremka Aya hii Mtume (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husein, akachukua kishamiya na kuwafunika, kisha akainua mkono wake mbinguni na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu hawa ndio Ahlul-Bait wangu. Ewe Mwenyezi Mungu waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”213 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).

Malik amepokea kutoka kwa Ibnu Mas’ud al-Ansariy alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuja na kutukuta tumeketi katika baraza la Saad bin Ubada. Bushru bin Saad akamwambia: Mwenyezi Mungu ametuamuru tukuswalie ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi ni vipi tutakavyokusalia?” Mtume akakaa kimya mpaka tukatamani kwamba asingemuuliza. Kisha akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): Semeni:   Tafsirul-Qurtubi Juz. 14, Uk. 182.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 14, Uk. 84. Pia imepokewa katika Tafsirul Kabir ya Razi Juz. 22, Uk. 137. Ruhul-Maaniy Juz. 16 Uk. 284. Manaqibul-Khawarazmiy Uk. 23. ManaqibulMaghazaliy Uk. 301. Tafsirul-Qummiy Juz. 2, Uk. 67.

212. 213.

185

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 185

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali ­Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim juu ya walimwengu, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa. Na salamu ni kama mlivyojifunza.’’214 Amesema Abu Umar: “Shuuba na Thawru wamepokea kutoka kwa al-Hakam bin Abdurahman bin Abi Layla, kutoka kwa Kaabiy bin Ajrah, amesema: Ilipoteremka: “Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu;” mtu mmoja alikuja kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ni ipi namna ya kukuswalia? Mtume akasema: Sema:

“Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.” Al-Qurtubi amesema: “Tumepokea katika kitabu as-Shifa cha Kadhi Iyadhi kwa njia ya upokezi ulioungana kutoka kwa Ali bin   Tafsirul-Qurtubi Juz. 14, Uk. 233.

214.

186

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 186

2/14/2018 12:11:53 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Abu Talib (a.s.), alisema: “Alizihesabu mikononi mwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). na akasema (s.a.w.w.): Naye alizihesabu mikononi mwa Jibril na kusema hivyo ndivyo zilivyoshuka kutoka kwa Mola Mwenye nguvu:

Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomsalia Ibrahim na aali Ibrahim. Hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.

Ewe Mwenyezi Mungu! Mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim. Hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.

Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim. Hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.

Ewe Mwenyezi Mungu! Muhurumie Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomuhurumia Ibrahim na aali Ibrahim. Hakika wewe ni Muhimidiwa Msifiwa.”215 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Qurtubi Juz. 14, Uk. 234.

215.

187

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 187

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:58).

Imesemwa kwamba: Iliteremka kwa ajili ya Ali. Hakika wanafiki walikuwa wakimuudhi na kumzushia uongo.216

SURAT AS-SAFFAT Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amani kwa Ilyasin.” (Qur’ani Tukufu Sura as-Saffat; 37:130). As-Suhayliy amesema: “Baadhi ya wanatheiolojia wanapotoa maana za Qur’ani wamesema kwamba Aali Yasin ni Aali Muhammad (a.s.).”217

SURAT SWAD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na tukautia nguvu ufalme wake na tukampa hikima na kukata hukumu.” (Qur’ani Tukufu Sura Swad; 38:20).

Imepokewa kwamba Ali bin Abu Talib alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliponipeleka Yaman kundi moja la   Tafsirul-Qurtubi Juz. 14, Uk. 240.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 15, Uk. 120

216. 217.

188

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 188

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

watu lilichimba shimo ambalo ni mtego wa simba, na hatimaye simba akanasa humo. Watu wakamuonea huruma simba ndipo watu wanne wakaingia humo kwa mtindo wa kubebana (kwa lengo la kumnasua). Simba akawajeruhi na kuwauwa. Watu wakashikiana silaha na kukaribia kuuwana. Ndipo nikawafuata na kuwaambia: Mnataka kuwauwa watu mia mbili kwa ajili ya watu wanne?! Njooni niwatoleeni hukumu, mkiiridhia ndio itakayokuwa hukumu kati yenu, na kama mkiikataa basi shitaka lenu nitalipeleka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwani yeye ndiye mwenye haki zaidi ya kutoa hukumu. Basi wa kwanza toka juu akamtengea robo ya fidia, wa pili theluthi ya fidia, wa tatu nusu ya fidia na wa nne fidia nzima. Na akawajibisha fidia hizo zitolewa na wale waliochimba mtego wa simba, wayape makabila manne. Baadhi wakaridhia na wengine wakakasirika, kisha wakaenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na kumsimulia kisa. Akasema (s.a.w.w.): “Mimi nitatoa hukumu baina yenu.” Ndipo mmoja wao akasema: “Hakika Ali tayari ameshatoa hukumu baina yetu.” Akamsimulia jinsi Ali alivyotoa hukumu. Mtume akasema: “Hukumu ni kama alivyoitoa Ali.”218 Huku ndiko kukata hukumu na elimu ya hukumu ambayo imegusiwa na moja ya tafsiri za Hadithi ya Mtume: “Jaji wenu Mkuu ni Ali.”219 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Warudisheni kwangu, na akaanza kuwapangusa miguu na shingo.” (Qur’ani Tukufu Sura Swad; 38:33).   Tafsirul-Qurtubi Juz. 15, Uk. 163.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 15, Uk. 164.

218. 219.

189

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 189

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

At-Tahawi ameandika katika kitabu Mushkilul-Hadithi kutoka kwa Asmau binti Umays kwamba Mtume (s.a.w.w.) alikuwa akipewa wahyi na hali kichwa chake kikiwa juu ya mapaja ya Ali, akawa hajaswali mpaka jua likazama. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Umeshaswali ewe Ali?” Akasema bado. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hakika yeye alikuwa katika kukutii wewe na kumtii Mtume Wako, naomba ulirudishe jua kwa ajili yake.” Asmau anasema: “Nililiona limezama mara ghafla nikaliona baada ya kuzama limechomoza juu ya mlima na ardhi. Na hiyo ilikuwa huko Khaybari.220

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23). Katika Bukhari kutoka kwa Taus kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba aliulizwa kuhusu kauli yake (s.w.t.): “….. Isipokuwa mapenzi katika ndugu,” Said bin Jubayri akasema: Karaba ni Aali Muhammad. 221 Na katika riwaya ya Said bin Jubair kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Mwenyezi Mungu alipoteremsha: “Sema: Kwa haya   Tafsirul-Qurtubi Juz. 15 Uk. 197. Ameandika al-Hafidh Shafi’i katika kitabu ­Kifayatul-Matalib Uk. 381. Na katika at-Thaqib Fil-Manaqib cha Ibnu Hamza Uk. 253. Na Aamali cha Sheikh Mufid, Baraza la 11, Uk. 65. Na Tarikhu Damashqi cha Ibnu Asakir kwenye wasifu wa Imam Ali Juz. 2, Uk. 284. Na Yanabiul-Mawaddah Uk. 137. Na Tadhkiratul-Khuwas Uk. 49 na al-Bihar Uk. 171. Pia jua lilirudi kwa mara nyingine kwa ajili ya Ali huko Babylon Iraq, pale alipotaka kuuvuka mto wa Bebilon. Hilo limeandikwa na Ibnu Shahri Ashub katika kitabu al-Manaqib Juz. 2, Uk. 318. Sharhun-Nahji Juz. 1, Dalailus-Sidqi Juz. 2, Uk. 300. Tafsiru Nurut-Thaqalayn Juz. 5, Uk. 225. al-Bihar Juz. 41, Uk. 171. 222.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 21. 220.

190

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 190

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu...” walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni akina nani hawa karaba zako ambao tunapaswa kuwapenda? Akasema: “Ni Ali, Fatima na watoto wao wawili.” Na pia lathibitishwa na riwaya ya Ali bin Abu Talib ambayo alisema: “Nilimshitakia Mtume (s.a.w.w.) kuhusu husuda za watu dhidi yangu. Akasema: ‘Hivi huridhii kuwa mmoja kati ya wanne. Wa kwanza kuingia Peponi ni: Mimi, Wewe, Hasan, Husein na kizazi chetu.”’222 Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Pepo imeharamisha juu ya yule aliyewadhulumu Ahlul-Bayt wangu na akaniudhi kwa kuwaudhi kizazi changu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ni shahidi.”223 Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake. Atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad atakuja Siku ya Kiyama na hali imeandikwa baina ya macho yake mawili: Amekata tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu. Atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu ya Pepo. Atakayekufa na hali awachukia aali zangu hana fungu lolote katika shafaa yangu.”224 Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ni shahidi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni muumini aliyekamilika kiimani.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 22.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 23. 224.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 23. 222. 223.

191

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 191

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali malaika ameshambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakir. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atamfungulia milango miwili kaburini ya kuelekea Peponi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amefia ndani ya Sunna. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad atakuja Siku ya Kiyama na hali imeandikwa baina ya macho yake mawili: Amekata tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad basi amekufa na hali ni kafiri. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu ya Pepo.”225 Ibnu Abbas amesema: Ni mapenzi kwa Aali Muhammad (s.a.w.w.).226

SURAT AZ-ZUKHRUF Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na akalifanya neno hili liwe lenye kubaki katika kizazi chake ili warejee.” (Qur’ani Tukufu Sura az-Zukhruf; 43:28). As-Sadiy amesema: “Hao ni Aali Muhammad (s.a.w.w.).227”   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 24.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 24. 227.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 16, Uk. 77. 225. 226.

192

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 192

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AD-DUKHAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Mbingu na ardhi hazikuwalilia; wala hawakupewa muda.” (Qur’ani Tukufu Sura ad-Dukhan; 44:29). As-Sadiy amesema: Alipouawa Husein bin Ali (a.s.) mbingu ­ilimlilia na kilio chake ni wekundu wake.228 Jarir amesimulia kutoka kwa Yazid bin Abi Ziyad kwamba ­alisema: “Alipouawa Husein bin Ali bin Abu Talib (a.s.) mbingu ­ilipatwa na wekundu muda wa miezi minne. Na wekundu wake ndio kulia kwake.” Muhammad bin Sirin amesema: “Tulipewa habari kwamba wekundu uliyopo kwenye mawingu haukuwapo awali mpaka pale Husein bin Ali (a.s.) alipouwawa.” Sulayman al-Qadhi amesema: “Tulinyeshewa na mvua ya damu siku Husein alipouawa.” Kutoka kwa Qurrat bin Khalid amesema: “Mbingu haikumlilia yeyote ila Yahya bin Zakaria na Husein bin Ali. Na wekundu wake ndio kulia kwake.”

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsirul-Qurtubi Juz. 16. Ameipokea al-Bayhaqiy katika Dalailun-Nubuwa Juz. 6, Uk. 472. Ameiandika pia Suyuti katika kitabu al-Khasaisul-Kubra Juz. 2, Uk. 127. Dhahabi katika kitabu Tarikhul-Islami Juz. 2, Uk. 348. Tadhkiratul-Khuwas Uk. 284. TarikhulKhulafai Uk. 80.

228.

193

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 193

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Imepokewa kutoka kwa Mujahid kwamba: “Hakika wa awali aliyetoa sadaka katika amri hiyo ni Ali bin Abu Talib (a.s.) alitoa na akaongea siri na Mtume (s.a.w.w.).” Al-Qashayrii na wengineo wametaja kutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.) kwamba alisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nayo ni: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana…..” nilikuwa nina dinari nikaichenji, hivyo ikawa kila nisemapo siri na Mtukufu Mtume natoa sadaka dirhamu moja mpaka zikaisha.” Ibnu Umar alisema: “Ali alikuwa na mambo matatu, ambayo kuwa nalo moja kati ya hayo ni jambo nilipendalo mno kuliko kuwa na ngamia mwekundu: Kuozwa Fatima, kukabidhiwa bendera Siku ya Khaibar na Aya ya kuongea siri na Mtume.”229

SURAT AL-MUMTAHANA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Msiwafanye adui zangu na adui zenu kuwa marafiki.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mumtahana; 60:1).   Tafsirul-Qurtubi Juz. 17, Uk. 302.

229.

194

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 194

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Al-Qushayri na Thaalabi wametaja kwamba: Hatibu bin Abu Balta’ah alikuwa ni mtu wa Yaman na alikuwa na mshirika na mmoja kati ya watu wa Bani Asad huko Makka. Akaja Madina kutoka Makka Sara kijakazi wa Abi Amru bin Swayfiy bin Hashim bin Abdu Manafi, na hali Mtume wa Mwenyezi Mungu akijiandaa kuikomboa Makka. (Sara) Alipokuwa anatoka kurudi Makka Hatib alimfuata na kumwambia: “Nakupa dinari kumi na kishamia kwa sharti kwamba unifikishie barua hii kwa wakazi wa Makka: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu anawakusudieni hivyo chukueni tahadhari.” Sara akatoka na ndipo Jibril akateremka na kumpa habari hiyo Mtume (s.a.w.w.), naye akamtuma Ali na Ammar bin Yasir, akawaambia: “Nendeni mpaka Rawdhatukhakhi,230 hapo pana mwanamke mwenye barua iliyotoka kwa Hatibu kwenda kwa Mushrikina. Mnyang’anyeni na mumwache aende zake na iwapo hatowapeni basi ikateni shingo yake.” Wakamkuta eneo hilo, wakamwambia: Ipo wapi barua? Akaapa kwamba hana barua. Wakapekua mizigo yake na hawakukuta barua, ndipo walipokusudia kurejea. Ali akasema: “Wallahi hatujasema uongo wala hatujadanganywa.” Akauandaa upanga wake na kumwambia: “Toa barua la sivyo wallahi nitakuvua na kuikata shingo yako.” Alipoona msisitizo ndipo akaitoa barua toka kwenye nywele zake.231

SURAT AT-TAGHABUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

J ina la eneo lililopo baina ya Makka na Madina kwa umbali wa maili kumi na mbili kutokea Madina. 231.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18, Uk. 51. 230.

195

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 195

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, na kwa ­Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura ­at-Taghabun; 64:15).

Tirmidhi na wengineo wamepokea kutoka kwa Abdullah bin Burayda kutoka kwa baba yake, amesema: “Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akitoa hotuba na ghafla wakaja Hasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuamka, akateremka toka mimbarini akawafuata na kuwachukua, kisha akasema: ‘Mwenyezi Mungu amesema kweli. Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni jaribio, nilipowaona hawa wawili wakitembea huku wakidondoka sikuweza kuvumilia mpaka nimekatisha mazungumzo yangu na kuwanyanyua.” 232

SURAT AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake, na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:4). Akrima na Said bin Jubayri wamesema: Waumini wema ni Ali bin Abu Talib. 233 Asmau binti Umays alisema: “Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: “Na waumini wema” ni Ali bin Abu Talib.”234

SURAT AL-HAQQA Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18 Uk. 143.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18 Uk. 189. 234.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18 Uk. 192. 232. 233.

196

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 196

2/14/2018 12:11:54 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Haqqa; 69:12).

Makhul amepokea kwamba: Ilipoteremka Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nilimwomba Mwenyezi Mungu alifanye hivyo sikio la Ali.’’235 Thaalabi ametaja kwa kusema: Ilipoteremka: “na sikio lisikialo lisikie.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nilimwomba Mola wangu Mlezi alifanye hivyo sikio lako ewe Ali.’’ Kutoka kwa Abu Barzatu al-Aslamiy amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ameniamuru nikusogeze karibu nisikutenge mbali, na nikuelimishe nawe usikie vilivyo. Na Mwenyezi Mungu amehakikisha unasikia vilivyo.” 236

SURAT AL-MA’ARIJ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea. Juu ya makafiri, hapana awezaye kuizuia.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ma’arij; 70:1-2).

Ibnu Abbas na Mujahid wamesema: “Muulizaji hapa ni al-Harith bin Nu’man al-Fihri. Hiyo ni pale alipofikiwa na habari za kauli ya Mtume kuhusu Ali (a.s.): “Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.” Alimpanda ngamia wake na kuja   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18 Uk. 264.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18 Uk. 264.

235. 236.

197

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 197

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mpaka alipofika Abtahu aliteremka kisha akasema: “Ewe Muhammad! Umetuamrisha kuhusu Allah tushahidilie kwamba hapana Mungu wa haki ila Allah na kwamba wewe ni Mtume wa Allah, tumekubali hilo kutoka kwako. Tuswali Swala tano tumekubali hilo kutoka kwako. Tutoe Zaka tumekubali hilo kutoka kwako. Kisha haujatosheka kwa haya yote mpaka umemfanya binamu yako bora juu yetu! Je jambo hili ni kutoka kwako binafsi au ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu?” Mtume akasema: “Naapa kwa yule ambaye hapana Mungu ila Yeye, hakika hili ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu.” Al-Harith akageuka na kuelekea kwenye mnyama wake huku akisema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Ikiwa ayasemayo ni haki basi tuteremshie mvua ya mawe kutoka mbinguni au tuletee adhabu iumizayo.” Wallahi kabla hajamfikia ngamia wake Mwenyezi Mungu akamwangushia jiwe utosini na likatokea nyumani kwake likamuuwa papo hapo. Ndipo ikateremka: “Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea.” 237

SURAT AL-MUDDATHIR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Kila nafsi itafungika kwa chumo ililochuma Isipokuwa watu wa kheri.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Muddathir; 74:38-39).

Abu Ja’far al-Baqir (a.s.) amesema: “Sisi na wafuasi wetu ndio watu wa kheri. Na kila mwenye kutuchukia ndiye aliye rehani wa matendo yake.” 238   Tafsirul-Qurtubi Juz. 18 Uk. 278.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 19 Uk. 85.

237. 238.

198

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 198

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).

Kutoka kwa Mujahid kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Hasan na Husein walipatwa na maradhi, babu yao Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona, waarabu kwa jumla na masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu nao pia walikwenda kuwaona. Ali akasema: “Ikiwa wanangu watapona nitafunga siku tatu kumshukuru Mwenyezi Mungu.” Mtumishi wao Nubiyatu akasema: “Ikiwa mabwana zangu wawili watapona nitafunga siku tatu kumshukuru Mwenyezi Mungu.” Fatuma naye akasema mfano wa hayo na pia Hasan na Husen wakasema nasi tutawajibikiwa mfano wa hilo. Vijana wawili wakapata afya njema na hali nyumbani kwa aali Muhammad hawana kitu si kichache wala kingi. Ali akaenda kwa Myahudi, Simon bin Hariya mtu wa Khaybar, akakopa toka kwake pishi tatu za shairi. Akaja nazo mpaka akaziweka ndani, ndipo Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, funga yao ya siku ya kwanza ilipopita mara masikini akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni maskini ka199

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 199

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

tika watoto wa umma wa Muhammad, nami ni mwenye njaa, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.� Ali akamsikia, akasoma shairi:

Fatima mwenye ubora na yakini, ewe binti wa mbora kuliko watu wote. Hivi humwoni mkata masikini amesimama mlangoni akitoa sauti ya uchungu. Akimshitakia Mwenyezi Mungu na akinyenyekea. Analalamika kwetu kwamba ni mwenye njaa na mwenye huzuni. Kila mtu ni rehani wa yale aliyoyachuma na mwenye kutenda kheri atabainika. Ahadi yetu ni Pepo ya juu aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu kwa bakhili.Na bakhili ana kisimamo dhalili, Moto utamvuta gerezani. 239 Fatima naye akasoma shairi:

  Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 129.

239.

200

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 200

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Amri yako kwangu ewe binamu yangu ni yenye kutekelezwa, sina haja na uduni wala udhalili. Naharakisha kumpa mkate, namlisha wala sisubiri muda. Nataraji nitakapowashibisha wenye njaa nitaungana na wabora na jamaa. Na nitaingia Peponi na hali nikiwa na uombezi. Wakampa chakula na wakashinda mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya pili Fatima akachukua pishi akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yao, mara akafika mlangoni kwao yatima akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, yatima toka katika watoto wa muhajirana ambaye baba yangu amekufa kishahidi siku ya Aqabah, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Ali akamsikia, akasoma shairi:

Fatima binti wa Sayyid karimu, binti wa Nabii asiye mwanaharamu. Mwenyezi Mungu amemleta yatima, atakayewahurumia watu leo naye atahurumiwa. Ataingia Peponi na hali amesalimika, bila shaka Pepo imeharamishwa juu ya muovu. Hatovuka Siratu iliyonyooka bali ataangukia motoni mpaka Jahim. Kinywaji chake humo ni usaha na maji ya moto. 240   Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 130.

240.

201

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 201

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Fatima naye akasoma shairi akisema:

Namlisha leo wala sijali, namtanguliza Mwenyezi Mungu kabla ya familia yangu. Wameshinda na njaa na wao ni wanangu, mdogo wao atauawa katika vita. Huko Karbala atauawa kwa njama, ole wake na adhabu yule mwenye kumuuwa. Moto utamvuta mpaka chini na hali mikononi mwake kafungwa pingu na minyororo. 241 Wakampa chakula na wakashinda siku mbili mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya tatu Fatima akachukua pishi lililobaki akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yao, mara mateka wa kivita akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mnatuteka na kutufunga na wala hamtupi chakula! Nipeni chakula mimi ni mateka wa Muhammad.” Ali akamsika, akasoma shairi:

Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 130.

241.

202

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 202

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ewe binti wa Mtume Ahmad, binti wa Mtume bwana mtiiwa. Mwenyezi Mungu amempa jina la Muhammad, bila shaka Mwenyezi Mungu amempamba kwa huruma. Huyu hapa mfungwa wa Mtume mwongozaji, amezuiliwa kwa kufungwa pingu yake na kizuizi. Mbele ya Aliye juu Mmoja mwenye kupwekeshwa, wanayoyalima wakulima watayavuna. Fatima naye akasoma shairi akisema:

Kati ya kile kilicholetwa hakijabaki ila pishi moja, bila shaka kitanga changu kimeondoka pamoja na mkono 242 wangu. Wallahi wanangu wana njaa, ewe Mola usiuache (mkono) upotee. Baba yao ni mwenye kutenda kheri, hutenda wema kwa kuanza. Na juu ya kichwa changu sina hijabu ila hijabu iliyofumwa kwa kamba. Wakampa chakula na wakashinda siku tatu mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya nne wakiwa tayari wameshatimiza nadhiri yao, Ali alimshika Hasan mkono wa kulia na Husein mkono wa kushoto na kwenda nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na hali wao wawili wakitetemeka kama vifaranga kutokana na ukali wa njaa. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipowatizama alise  Mkono na Kitanga hapa ni kinaya ya Pishi la Kwanza na la Pili. Hivyo anaomba pishi hizo zisiende na kupotea bure bali ziambatane na malipo mema. – Mtarjumi.

242.

203

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 203

2/14/2018 12:11:55 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ma: “Ewe Abal-Hasan! Hali niionayo yaniumiza mno, twendeni kwa binti yangu Fatima.” Wakaenda kwake wakamkuta akiwa mihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake na macho yake yamebadilika kutokana na ukali wa njaa. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipomtazama na kutambua njaa aliyonayo kupitia uso wake, alilia na kusema: 243 “Ee Mwenyezi Mungu nakuomba msaada, Ahlul-Baiti wa Muhammad wanakufa kwa njaa.” 244 Jibril (a.s.) akateremka na kusema: “Assalam Alayka. Mola wako Mlezi anakusalimu. Ewe Muhammad pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Mtume akasema: “Nichukue nini ewe Jibril?” Jibril (a.s.) akamsomea:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:13).245

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Humo wataegemea viti vya enzi humo hawataona jua wala baridi.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:13).   Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 132. Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 132. 245.   Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 132. 243.

245.

204

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 204

2/14/2018 12:11:56 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SEHEMU YA TATU Kwa Mujibu Wa Ibn Kathir, Suyuti, Burusawi, Alusi Na Qasimi

205

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 205

2/14/2018 12:11:56 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Abbas amesema: “Pindi watu wa Peponi watakapokuwa peponi ghafla wataona mwanga kama mwanga wa jua na Pepo imeangazwa kwa mwanga huo. Watasema: Mola wetu Mtukufu amesema: “Hawataona jua wala baridi.” hii ni nuru ya nini? Ridhwan atawaambia: “Hili si Jua wala si Mwezi, lakini huyu ni Fatima na Ali wamecheka, na kutokana na nuru ya kicheko chao Pepo imeangaziwa.” Na kwa ajili ya hao wawili Mwenyezi Mungu ­aliteremsha Sura:

“Hakika ulimfikia mtu wakati fulani wa zama ambapo hakuwa kitu kinachotajwa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:1).

Ibnu Abbas akasoma shairi:

Mimi ni mfuasi wa kijana ambaye kwa ajili yake ­iliteremshwa Sura Hal Ataa. Huyo ni Ali Al-Murtadha ambaye ni binamu wa ­al-­Mustafa.” 246

Tafsirul-Qurtubi Juz. 19, Uk. 136.

246.

206

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 206

2/14/2018 12:11:56 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA IBNU KATHIR, INAYOITWA TAFSIRUL-QUR’AN AL-ÁDHIM SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Ametusimulia Abu Said al-Ashji kwamba: ‘Alitupa habari Yahya bin Yaman kutoka kwa Abdul-Wahab bin Mujahid kutoka kwa Ibnu Jubayri kutoka kwa baba yake, amesema: ‘Ali alikuwa na dirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, nyingine siri na nyingine dhahiri, ndipo ikateremka: “Wale watoao mali zao…’”247 Lakini Ibnu Mardawayhi ameipokea kwa njia nyingine kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abutalib.248

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 281, Chapa ya Beirut ya Durul-Qalam.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 281, Chapa ya Beirut ya Durul-Qalam.

247. 248.

207

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 207

2/14/2018 12:11:56 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. ­Akasema: “Ewe Maryam unatoa wapi hivi. “Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:37).

Al-Hafidh Abu Ya’la amesema: “Ametusimulia Sahlu bin Zanjila amesema: “Ametusimulia Abdullah bin Salih amesema: Ametusimulia Abdullah bin Lahi’ah kutoka kwa Muhammad bin alMukandir kutoka kwa Jabir kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bila kula chakula mpaka hali hiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenye nyumba za wakeze lakini hakupata kwa yeyote chochote, ndipo akaenda kwa Fatima na kumwambia: “Ewe mwanangu mpendwa! Je una chochote ninachoweza kula kwani hakika mimi ni mwenye njaa?” Akamjibu: “Wallahi sina ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa haki ya baba yangu na mama yangu.” Mtume alipotoka, jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vya mkate na finyango ya nyama, akavitwaa na kuviweka ndani ya bakuli lake, akasema: “Wallahi katika hiki nitampa kipaumbele Mtume wa Mwenyezi Mungu kabla ya nafsi yangu na kabla ya yule aliyopo kwangu.” Japokuwa wote walikuwa wanahitajia chakula lakini Fatima alimtuma Hasan au Husein aende kumwita Mtume (s.a.w.w.) naye alikuja. Fatima akamwambia: “Kwa haki yako na ya mama yangu, Mwenyezi Mungu ameleta kitu nami nimekihifadhi kwa ajili yako.” Akamwambia: “Kilete ewe binti yangu mpendwa.”

208

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 208

2/14/2018 12:11:56 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Akamletea bakuli na alipolifunua ghafla akakuta limejaa mikate na nyama, akapatwa na mshangao na akatambua kuwa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu. Akamuhimidi Mwenyezi Mungu, akamsalia Mtume na akamkabidhi chakula hicho Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Mtume (s.a.w.w.) alipokiona alimuhimidi Mwenyezi Mungu na akasema: “Umetoa wapi hivi ewe binti yangu mpendwa? “Akajibu: “Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Mtume akamuhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Ambaye amekufanya ewe binti yangu mpendwa kifani wa Seyida wa wana wa Israel (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwa aruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu kisha akiulizwa kakipata wapi husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akampelekea ujumbe Ali aje. Akala Mtume, Ali, Fatima, Hasan, Husein na wakeze wote na Ahlul-Baiti wake wote mpaka wakashiba. Fatima alisema: “Bakuli lilibaki kama lilivyokuwa likiwa limejaa. Hivyo nikawagawia majirani zangu wote na Mwenyezi Mungu aliweka humo kheri nyingi na baraka tele.”249 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ­ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:42).   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 310.

249.

209

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 209

2/14/2018 12:11:56 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Tirmidhi amesema: “Ametusimulia Abu Bakr bin Zanjawihi amesema: Ametusimulia Abdur-Razzaq amesema: ‘Ametusimulia Ma’amar kutoka kwa Qatadah kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha katika wanawake wa ulimwenguni: Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad na Asia mke wa Firaun.” Ameipokea ­Tirmidhi peke yake na amesema ni Hadithi Sahihi.250 Na amesema Abdullah bin Abi Jafar Razi kutoka kwa baba yake amesema: “Thabit al-Banani alikuwa akisimulia kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora ulimwenguni ni wanne: Maryam binti Imran, Asia mke wa Firaun, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Ameipokea Ibnu Mardawayhi.251 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni ­tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali Imran; 3:61).

Abu Bakr bin Mardawayhi amesema: “Ametusimulia Sulayman bin Ahmad amesema: Ametusimulia Ahmad bin Daud al-Makkiy amesema:   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 313.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 313.

250. 251.

210

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 210

2/14/2018 12:11:57 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ametusimulia Bashru bin Mahran amesema: Ametusimulia Muhammad bin Dinar kutoka kwa Daud bin Abi Hindi kutoka kwa asSha’biy kutoka kwa Jabir amesema: “Aqib na Tayib walimwendea Mtume (s.a.w.w.) naye akawaomba wafanye maapizano ya kuombeana laana, ndipo wakamwahidi kwamba maapizano hayo yafanyike kesho yake. Mtume akatoka siku iliyofuata akiwa na Ali, Fatima, Hasan na Husein, kisha akawatumia ujumbe waje kwenye maapizano, wakakataa lakini wakakubali kutoa kodi. Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Lau wangekataa (kulipa kodi ya Jizya) basi bonde lao lingewaka moto toka mbinguni.” Jabir amesema: Na “Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu….” iliteremka kwa ajili yao. Jabir amesema: “…na nafsi zetu na nafsi zenu…” ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Ali. “…watoto wetu…” ni Hasan na Husein. Na “…. wanawake zetu….” ni Fatima. Na hivyo ndivyo alivyoipokea al-Hakim kwa maana hiyo katika kitabu chake al-Mustadrak kutoka kwa Ali bin Isa kutoka kwa Ahmad bin Muhammad al-Azhariy, kutoka kwa Ali bin Hajar kutoka kwa Ali bin Mus’har kutoka kwa Daud bin Abi Hindi. Kisha akasema: “Ni Hadithi sahihi kwa mujibu wa sharti za Muslim ijapokuwa hajaiandika. 252

SURAT AN-NISAA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 319

252.

211

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 211

2/14/2018 12:11:57 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Enyi mlioamini! msikaribie Sala hali ya kuwa mmelewa mpaka myajue mnayoyasema, wala mkiwa na janaba isipokuwa mmo safarini, mpaka muoge.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nisaa’; 4:43).

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba baadhi ya ­ aansari milango yao ilikuwa ikitokea msikitini, hivyo baadhi ya M nyakati walikuwa wakipatwa na janaba na hali hawana maji na hivyo watokapo kutafuta maji huwa hawana njia ila msikitini, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “…wala mkiwa na janaba isipokuwa mmo safarini.” Ama ile aliyoipokea Abu Isa Tirmidhi ambayo ni Hadithi ya Salim bin Abi Hafsa kutoka kwa Atiya kutoka kwa Abu Said al-Khudriy ni kwamba amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ewe Ali! Haruhusiwi yeyote asiyekuwa mimi na wewe kupatwa na janaba ndani ya msikiti huu.” Ibnu Kathir amesema: “Yenyewe ni Hadithi dhaifu.”253

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Enyi mlioamini! Tekelezeni ­wajibu...” (Surat al-Maida: 1). Kutoka kwa Zayd bin Ismail as-Saighu al-Baghdadiy amesema: “Ametusimulia Muawiya, yaani Ibnu Hisham, kutoka kwa Isa bin Rashid kutoka kwa Ali bin Budhayma kutoka kwa Akrima kutoka kwa Ibnu Abbas, amesema: “Katika Qur’ani hakuna Aya yenye ibara ‘Enyi mlioamini!’ isipokuwa Ali ndiye kinara wake na kiongozi wake. Na hakuna Sahaba yeyote wa Mtume wa Mwenyezi Mungu ila alifokewa na Qur’ani ila Ali bin Abu Talib, yeye hakufokewa kwa sehemu yoyote ya Qur’ani.254   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 430 na Uk. 431.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 4, Chapa ya Beirut ya Darul-Ma’rifa ya Mwaka 1412 A.H.

253. 254.

212

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 212

2/14/2018 12:11:57 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:3).

Imesemekana kwamba ilimteremkia Mtume wa Mwenyezi Mungu alipokuwa safarini kurudi toka Hija yake ya mwisho. Kisha imepokewa kwa njia nyingine na Abu Jafar Razi kutoka kwa Rabiu kutoka kwa Anas. Na pia ameipokea Ibnu Mardawayhi kwa njia ya Abu Harun al-Abdiy kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba ilimtremkia Mtume wa Mwenyezi Mungu Siku ya Ghadir Khum pale alipomwambia Ali: “Yule ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.” Kisha ameipokea kutoka kwa Abu Huraira na katika maelezo yake ni kwamba ilikuwa ni siku ya kumi na nane ya Mfunguo tatu, yaani alipokuwa akirejea kutoka Hija yake ya mwisho.255 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui…..” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Ametusimulia Abu Said al-Ashji amesema: “Ametusimulia al-Fadhlu bin Dakin Abu Naim al-Ahwal amesema: ‘Ametusimulia Musa bin   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 15.

255.

213

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 213

2/14/2018 12:11:57 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Qaysi al-Hadhramiy kutoka kwa Salma bin Kahil amesema: Ali alitoa sadaka pete yake na hali akiwa amerukuu ndipo ikateremka: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na…..” Ibnu Jariri amesema: al-Harith amenisimulia amesema: “AbdulAziz ame-tusimulia amesema: Ametusimulia Ghalib bin Ubaydullah amesema: Nilimsikia Mujahid akisema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake..” kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib alipotoa sadaka na hali akiwa amerukuu. Na Abdurazzaq amesema: Alitusimulia Abdul-Wahab bin Mujahid kutoka kwa baba yake kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake..” kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib. Ibnu Mardawayhi amepokea kwa njia ya Sufyan Thawri kutoka kwa Abu Sinan kutoka kwa Dhahak kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Ali alikuwa katika Sala ndipo muombaji akapita na hali akiwa katika rukuu akampa pete yake, ndipo ikateremka: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake…..” Kutoka kwa Abi Salih kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda msikitini akawakuta watu wakisali, baadhi wapo katika rukuu na wengine katika sijda, wangine katika kisimamo na baadhi wameketi, na ghafla akamwona masikini akiomba, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu akamuuliza: “Je kuna yeyote amekupa kitu?” Akasema: “Ndio.” Akamuuliza ni nani? Akasema ni yule aliyesimama. Mtume akamuuliza: “Alikupa akiwa katika hali gani? “ Akasema: “Akiwa amerukuu.” Mtume akasema: “Yule ni Ali bin Abu Talib.” Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa takbira huku akisema: “Na anayemtawali214

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 214

2/14/2018 12:11:57 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

sha Mwenyezi Mungu, Mtume wake na wale walioamini, basi ajue hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lishindalo.” Ibnu Kathir amesema: “Njia hii ya upokezi haikutwi na dosari.” 256

SURAT AL-AN’AM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:84-85).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Ametusimulia ibnu Yahya al-Askari amesema: Ametusimulia Abdur-Rahman bin Salih amesema: Ametusimulia Ali bin Abbas kutoka kwa Abdullah bin Atau al-Makkiy, kutoka kwa Abi Harbi bin Abil-As’wad amesema: Hajjaj alituma ujumbe kwa Yahya bin Ya’mur akasema: “Imenifikia habari kwamba wewe unadai kuwa Hasan na Husein ni kizazi cha Mtume (s.a.w.w.) kwa ushahidi wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu, nami nimekisoma kuanzia mwanzo hadi mwisho na wala sijaupata.” Akasema: Hujasoma Sura al-An’am: “Na Nuh tulimwongoza zamani na katika   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 74.

256.

215

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 215

2/14/2018 12:11:57 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.”? Akasema: “Nimesoma.” Yahya akasema: “Basi Isa si kutoka kizazi cha Ibrahim na hali hana baba.” Akasema: “Umesema kweli.”257 Na wengine wamesema: “Watoto wa binti wanaingia katika kizazi cha mtu kutokana na riwaya iliyopo katika Sahih Bukhari kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu alimwambia Hasan bin Ali (a.s.): “Hakika mwanangu huyu ni Sayyidi…”258

SURAT AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na walipokupangia njama wale waliokufuru ili wakufunge au wakuue au wakutoe…” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:30).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Makuraishi walishauriana usiku mmoja huko Makka, baadhi yao wakasema: Akiamka mfungeni kwa kizuizi. Wakimkusudia Mtume (s.a.w.w.). Na wengine wakasema: Muuweni huku wengine wakisema: Mfukuzeni. Ndipo Mwenyezi Mungu akamjuza Nabii wake mkakati huo. Ali bin Abu Talib akalala usiku huo juu ya kitanda cha Mtukufu Mtume na Mtume akatoka mpaka pangoni, mushrikina wakakesha   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 160.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 160.

257. 258.

216

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 216

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wakimlinda Ali wakidhani ndiye Mtume (s.a.w.w.), walipofika asubuhi walimvamia na walimuona kuwa ni Ali, Mwenyezi Mungu alizuia njama yao.259

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1).

Imam Ahmad amesema: “Ametusimulia Affan amesema: Ametusimulia Hamad kutoka kwa Sammak kutoka kwa Anas bin Malik kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma pamoja na Abu Bakr kuibalighisha Sura Baraa, walipofika Dhulhalifa akasema (s.a.w.w.): “Hapasi kuibalighisha ila mimi au mtu atokanaye na Ahlul-Baiti wangu.” Ndipo akamtuma Ali bin Abu Talibi akaibalighishe. Ameipokea pia Tirmidhi katika tafsiri yake.260 Abdullah bin Ahmad bin Hanbal amesema: “Ametusimulia Muhammad bin Sulayman amesema: Ametusimulia Muhammad bin Jabir kutoka kwa Sammak kutoka kwa Hasan kutoka kwa Ali (a.s.) amesema: Zilipoteremka kwa Mtume Aya kumi za mwanzo wa Sura Baraa Mtume (s.a.w.w.) alimwita Abu Bakr na kumkabidhi ili akawasomee wakazi wa Makka. Kisha akaniita na kusema: “Mdiriki Abu Bakr na popote utakapomkuta chukua Sura kutoka kwake na uende kuwasomea wewe wakazi wa Makka. Nikamkuta Juhfa na nikachukua Sura kutoka kwake. Abu Bakr akarejea kwa Mtume   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 316.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 346.

259. 260.

217

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 217

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

(s.a.w.w.) na kumwambia: “Ewe Mtume wa Mweenyezi Mungu! Kuna chochote kimeteremka kunikhusu?” Akasema: “Hapana lakini Jibril amenijia na kuniambia: Hapasi kufikisha kwa niaba yako ila wewe mwenyewe au mtu kutokana na wewe.” Kutoka kwa Abu Is’haqa kutoka kwa Zayd bin Yathighu amesema: “Baraa ilipoteremka Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma Abu Bakr kisha baadae akamtuma Ali akaichukua. Abu Bakr aliporejea alisema: “Je kuna chochote kimeteremka kunihusu?” Akasema: “Hapana lakini nimeamrishwa niibalighishe mimi mwenyewe au mtu kutoka katika Ahlul-Baiti wangu.” (Ali) Akaenda Makka na kuwatangazia watu wake mambo manne: Baada ya mwaka huu mushriku haruhusiwi kuingia Makka, wala haruhusiwi kutufu akiwa uchi, wala hatoingia peponi ila mwislamu, na yule ambaye baina yake na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuna mkataba basi mkataba huo utaendelea mpaka mwisho wa muda wake.261 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:19).

Abdu Razzaq amesema: “Ibnu Uyayna alitupa habari kutoka kwa Ismail kutoka kwa as-Sha’biy amesema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali na Abbas.”   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 346.

261.

218

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 218

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Jariri amesema: “Talha bin Shayba toka kizazi cha Abdudar, Abbas bin Abdul-Muttalib na Ali bin Abu Talib kila mmoja alijigamba. Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba funguo zimo mikononi mwangu na hata nikitaka nalala humo.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mgawa maji na msimamizi wake na hata nikitaka nalala msikitini.’ Ali akasema: ‘Sijui mtasema nini. Bila shaka nimeswali miezi sita kabla ya mtu yeyote na mimi ndiye mwanajihadi.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu….” Na hivyo ndivyo alivyoipokea as-Saddiy.262

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wakasema: Unastaajabu amri ya Mwenyezi Mungu? Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka zake iko juu yenu enyi watu wa ­nyumba hii. Hakika Yeye ndiye Mhimidiwa Mtukuzwa.” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:73).

Amesema: “Imethibiti ndani ya Sahih mbili kwamba walisema: Tumeshajua namana ya kukusalimia basi ni vipi tutakavyokusalia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema:Semeni: “Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa).”263   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 355.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 468.

262. 263.

219

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 219

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT IBRAHIM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru na wakawafikisha watu wao katika nyumba ya maangamizo.” (Qur’ani Tukufu Sura Ibrahim; 14:28).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Alitusimulia baba yangu alisema: Ametusimulia Ibnu Nufayli alisema: Nilisoma mbele ya Ma’qal kutoka kwa Ibnu Abi Husein kwamba: Ali bin Abu Talib alisimama na kusema: “Oh, yeyote aniulize kuhusu Qur’ani, na wallahi lau ningemjua leo yeyote aijuaye kuliko mimi hata kama yupo ng’ambo ya bahari basi ningemfuata.” Abdullah bin al-Kawau akasimama na kusema: “Ni akina nani wale waliobadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru na wakawafikisha watu wao katika nyumba ya maangamizo?” Akasema: “Ni mushrikina toka kwa makuraishi, walijiwa na neema ya Mwenyezi Mungu ambayo ni Imani wakaibadili neema ya Mwenyezi Mungu kwa ukafiri na ndipo wakawafikisha watu wao katika nyumba ya maangamizo.”264

SURAT AN-NAHL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na hatukutuma kabla yako ila wanaume tuliowapa wahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nahl; 16:43   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 558

264

220

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 220

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Abu Jafar al-Baqir (a.s.) alisema: “Sisi ndio wenye ukumbusho.”265 Ibnu Kathir amesema: “Ulamaa wa nyumba tukufu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndio maulamaa bora kwani wao ndio waliokuwa katika Sunna ipasavyo, kama vile Ali, Ibnu Abbas, watoto wa Ali Hasan na Husein, Muhammad bin al-Hanafiyya, Ali bin Husein Zaynul-Abidin, Ali bin Abdullah bin Abbas, Abu Jafar alBaqir ambaye ni Muhammad bin Ali bin Husein, na Mwanae Ja’far na mfano wao miongoni mwa wale wenye kushikamana vilivyo na kamba imara ya Mwenyezi Mungu na njia Yake nyoofu…..”266

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:26).. Al-Hafidh Abu Bakr al-Bazzar amesema: Ametusimulia Ibad bin Ya’kub amesema: Ametusimulia Abu Yahya at-Tamimiy amesema: Ametusimulia Fudhaylu bin Marzuq kutoka kwa Atiya kutoka kwa Abu Said amesema: Ilipoteremka: “Na mpe jamaa wa karibu haki…..” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Fatima na kumpa Fadak. 267 Ibnu Kathir amesema: Na rai ya karibu zaidi ni kwamba yenyewe ni miongoni mwa uzushi wa marafidhi. Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye.268   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 591 na 592.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 591 na 592. 267.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 34. 268.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 34. – Sielewi mpaka sasa ni kwa nini Ibnu Kathir umajununi wake unapanda pale anapoiona fadhila na heshima ya Ahlul-Baiti, na daima anajaribu kuidhoofisha ile iliyo mashuhuri, bila shaka si chochote bali ni uadui wake kwa Ahlul-Baiti (a.s.). Kisha riwaya hiyo wafasiri wakubwa wameitaja kabla yetu kama vile al-Haskaniy katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil. 265. 266.

221

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 221

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-MU’MINUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi litakapopulizwa parapanda, hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.” (Qur’ani Tukufu Sura ­al-Mu’minun 23:101).

Imam Ahmad amesema: “Ametusimulia Abu Sa’id huria wa Bani Hashim amesema: Ametusimulia Abdullah bin Ja’far amesema: ‘Ametusimulia Ummu Bakri binti ya al-Musawwar bin Makhrimah kutoka kwa Abdullah bin Abi R?fi’u kutoka kwa al-Musawwar amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Fatima ni pande la nyama yangu hunisononesha yale yanay-omsononesha, na hunifurahisha yale yanayomfurahisha. Na hakika kila nasaba itakatika Siku ya Kiyama ila nasaba yangu na sababu yangu na ukwe wangu.” Hadithi hii ina asili katika Sahih mbili (Muslim na Bukhari) kutoka kwa al-Musawwar kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Fatima ni pande la nyama yangu, hunikarahisha lile linalomkarahisha na huniudhi lile linalomuudhi.”269

SURAT ASH-SHU’ARAA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na uwaonye jamaa zako wa ­karibu.” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shu’araa; 26:214). Nikawapelekea sinia la chakula, na ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu akachukua kipande kidogo cha nyama akakikata kwa meno   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 3 Uk. 222.

269.

222

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 222

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

yake kisha akakitupia pembezoni mwa sinia, akasema: ‘Kuleni kwa Jina la Mwenyezi Mungu.’ Kaumu wakala mpaka wakatosheka na wala sikuona ila sehemu ambazo mikono yao ilikuwa ikimega. Wallahi, chakula nilichowapa wote ni cha kuweza kula mtu mmoja. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: ‘Wape watu kinywaji ewe Ali.’ Nikaja na ile bilauri wakanywa mpaka wakatosheka wote. Wallahi, kilikuwa ni kinywaji cha kutosheka mtu mmoja. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipotaka kuwaeleza Abu Lahabi alimtangulia kuongea, akasema: ‘Jamaa yenu amewaroga kwa karamu hii.’ Ndipo kaumu wakatawanyika na wala Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) hakufanikiwa kuwaeleza. Ilipowadia siku iliyofuata Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: ‘Ewe Ali! tuandalie chakula na kiny waji mfano wa kile ulichoandaa jana…..’ Nikatekeleza kisha nikawakusanya, naye Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akafanya kama alivyofanya jana, wakala mpaka wakatosheka, nikawaletea bilauri wakanywa mpaka wote wakatosheka. Wallahi, chakula na kinywaji nilichowapa wote ni cha kuweza kutosheka mtu mmoja. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akaongea kwa kusema: ‘Enyi wana wa Abdul-Muttalib Hakika mimi wallahi simjui kijana wa kiarabu aliyewaletea jamaa zake kitu bora kuliko hiki nilichowaletea. Hakika mimi nimewaletea kheri ya dunia na akhera. Na hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru niwalinganie kwayo, basi ni nani kati yenu atanisaidia katika jambo hili, awe ndugu yangu na kadha wa kadha.’ Watu wote wakakaa kimya, nikasema na hali mimi nikiwa ndiye mdogo kiumri kuliko wote, mwenye tongotongo machoni (mtoto) kuliko wote, mwenye tumbo kubwa kuliko wote na mwenye muundi wenye majeraha madogo kuliko wote: ‘Mimi ewe Mtume wa Mwe223

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 223

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nyezi Mungu nakuwa waziri wako.’ Akaishika shingo yangu kisha akasema (s.a.w.w.): ‘Hakika huyu ni ndugu yangu na kadha wa kadha, msikilizeni na mumtii.’ Kaumu wakaongea na hali wakicheka na wakimwambia Abu Taalib: ‘Bila shaka amekuamuru umsikilize na kumtii mwanao.’”270

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na kama hamuwajui baba zao, basi ni ndugu zenu katika dini.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:5). Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali (a.s.): “Wewe watokana na mimi na mimi natokana na wewe.” 271 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akawarithisheni nchi yao na majumba yao na mali zao, na nchimsiyoikanyaga, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo juu ya kilakitu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:27).   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 302. Ibnu Kathir anaielezea habari hii kwa kusema: “Kaipokea kwa mtiririko huu Abdul-Ghaffar bin al-Qasim bin Abi Mariam pekee, naye ni muongo asiyefuatwa na ni Shia.” Maneno kama haya kutoka kwa Ibnu Kathir ni ya ajabu, na inashangaza kuona anajiita aalimu na hali yeye hajui bali anaharakia kuwahukumu wenzake. Hajui kwamba al-Hafidh al-Kunjiy as-Shafi’iyyu aliyefariki mwaka 658 A.H. ametaja tukio hili kwa njia mbili katika kitabu chake Kifayatut-Talib Uk. 304 mlango wa 51, na katika njia zote mbili hajataja jina la Abdul-Ghaffar bin al-Qasim bin Abi Layla, hii ni mosi. Pili: Tukio hili ni mashuhuri bali ni mutawatiri kwani limetajwa na wasimulizi wakubwa na wanahistoria wakubwa, miongoni mwao ni: Tabari katika kitabu chake cha historia Juz. 2, Uk. 62, al-Muttaqiy al-Hindiy katika kitabu Kanzul-Ummal Juz. 6, Uk. 392 na 397, Ahmad bin Hanbal katika al-Musnad Juz. 1, Uk. 195, al-Haythamiy katika Majmauz-Zawaid Juz. 8, Uk. 302, Tabari katika ar-Riyadhun-Nadhrah Juz. 2, Uk. 167, na wengineo. 271.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 399. 270.

224

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 224

2/14/2018 12:11:58 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwacha Ibnu Ummu Maktum Madina na akamkabidhi bendera Ali bin Abu Talib (a.s.). 272 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Kutoka kwa Anas bin Malik amesema kwamba: “Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akipitia nyumbani kwa Ali muda wa miezi sita kila alipotoka kwenda kusali Sala ya alfajri, na alikuwa akisema: ‘Swala enyi Ahlul-Baiti. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.’” Ameipokea Tirmidhi kutoka kwa Abdu bin Hamid kutoka kwa Affan, amesema: “Ni nzuri Gharib.”273 Ibnu Jarir amesema: “Ametusimulia Waki’u kutoka kwa Abu Is’haqa, amesema: Abu Daud amenipa habari kutoka kwa AbulHamrau, amesema: “Niliishi Madina miezi sita bila kutoka zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), nilimwona Mtume kila ichomozapo alfajiri akienda kwenye mlango wa Ali na Fatima (a.s.) na kusema: ‘Sala Sala, Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”’274 Al-Awza’i amesema: “Ametusimulia Shaddad Abu Ammar amesema: “Niliingia kwa Wathila bin al-Asqau nikamkuta ameketi na baadhi ya watu, ndipo walipomtaja Ali na kumkashifu, nami   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 408.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 413. 274.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 413. 272. 273.

225

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 225

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nikamkashifu pamoja nao, walipoondoka akasema (Wathila): ‘Hivi kweli umethubutu kumkashifu huyu?’ Nikasema wamemkashifu ndipo nami nikamkashifu pamoja nao. Akasema: ‘Nikupe habari za yale niliyoyaona toka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu?’ Nikasema ndio. Akasema: Nilikwenda kwa Fatima (a.s.) kumuulizia Ali (a.s.). Fatima akanijibu kwamba ameelekea kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), nikakaa namngojea mpaka Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipokuja akiwa pamo-ja na Ali, Fatima, Hasan na Husain (a.s.) amemshika kila mmoja wao mkono, akaingia kisha akawasogeza Ali na Fatima na kuwakalisha mbele yake, na akamkalisha Hasan na Husein kila mmoja juu ya paja lake, kisha akawafunika nguo yake na kusoma Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Na akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio watu wa nyumba yangu, na watu wa nyumba yangu ndio wenye haki zaidi (kuliko mtu baki).’”275 Imam Ahmad amesema: Imepokewa kutoka kwa Ummu Salama kwamba alikuwa akitaja kuwa Mtume (s.a.w.w.) alikuwa nyumbani kwake ndipo akaja Fatima akiwa na chungu chenye uji na kuingia nacho kwa Mtume. Mtume akamwambia mwite mumeo na wanao. Alikuja Ali, Hasan na Husein wakaingia kwa Mtume na wakaketi wakinywa uji huo na hali Mtume akiwa juu ya kitanda chake kilichotandikwa kishamia cha Khaibari. Nikiwa chumba kingine nasali ghafla Mwenyezi Mungu aliteremsha Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Mtume (s.a.w.w.) akashika pande za kishamia akawafunika, kisha akatoa mkono wake akauelekeza mbinguni kisha akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu hawa ndio Ahlul-Baiti wangu na watu makhsusi kwangu. Waondo  Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 413.

275.

226

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 226

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

lee uchafu na watakase kabisa kabisa.’ Nikaingiza kichwa chumbani kwa Mtume na kumwambia: Je na mimi ni pamoja nanyi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: ‘Hakika wewe upo katika kheri. Bila shaka wewe upo katika kheri.’” 276 Ibnu Jarir amesema: Imepokewa kutoka kwa A’mash kutoka kwa Hakim bin Sa’d amesema: Tulimtaja Ali bin Abu Talib (a.s.) mbele ya Ummu Salama, akasema: “Ndani ya nyumba yangu ndimo ilimoteremka: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” “Ummu Salama akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuja nyumbani kwangu, akaniambia usimpe yeyote idhini ya kuingia. Akaja Fatima sikuweza kumzuia na baba yake, kisha akaja Hasan sikuweza kumzuia asiingie kwa babu yake na mama yake. Akaja Husein sikuweza kumzuia asiingie kwa babu yake na mama yake. Kisha akaja Ali (a.s.) sikuweza naye kumzuia, walipokusanyika Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawafunika kwa kishamia alichokuwa amejitanda, kisha akasema: ‘Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu. Waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.’ Ndipo ikateremka Aya hii walipokusanyika juu ya busati. Nikasema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Na mimi? Ummu Salama anasema: Wallahi hakukubali bali alisema: Hakika wewe utaelekea katika kheri.”277 Ibnu Jarir amesema: Ametusimulia Abu Karib kutoka kwa Abdullah bin Wahab bin Zam’at, amesema: Ummu Salama alinipa habari kwamba: “Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliwakusanya Ali, Fatima, Hasan na Husein (a.s.) kisha akawafunika nguo yake, kisha akaelekea kwa Mwenyezi Mungu na kusema: ‘Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu.’ Ummu Salama akasema: ‘Ewe Mtume wa   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.

276. 277.

227

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 227

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu! (Allah) Amenijumuisha pamoja nao?’ akasema (s.a.w.w.): ‘Wewe ni miongoni mwa wake zangu.”278 Imepokewa kutoka kwa Ummu Salama amesema: Siku moja Mtume akiwa nyumbani kwangu nilimwambia mfanyakazi: “Hakika Ali na Fatima wako mlangoni.” Mtume wa Mwenyezi Mungu akaniambia: “Simama na wapishe Ahlul-Baiti wangu.” “Nikaketi kando kidogo pembezoni mwa nyumba.” Wakaingia Ali na Fatima wakiwa na Hasan na Husein (a.s.) wakiwa bado watoto wadogo, akawachukua watoto na kuwaweka mapajani mwake na akawabusu, akamshika Ali kwa mkono wake mmoja na Fatima kwa mkono wake mwingine, akambusu Fatima na kisha Ali, akawafunika shuka jeusi na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu tulete Kwako na si motoni, mimi na Ahlul-Baiti wangu.”279 Kutoka kwa Ibnu Abi Hatim kutoka kwa al-Awamu bin Hawshab, kutoka kwa ami yake amesema: Niliingia na baba yangu kwa Aisha, nikamuuliza kuhusu Ali (a.s.). Aisha akasema: “Umeniuliza kuhusu mtu aliyekuwa akipendwa sana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kuliko watu wote, na alikuwa mume wa binti yake aliyekuwa akipendwa sana na Mtume wa Mwenyezi Mungu. Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akiwa amewaita Ali, Fatima, Hasan na Husein, akawafunika nguo na kisha akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! hawa ndio Ahlul-Baiti wangu, hivyo waondolee uchafu na uwatakase kabisa.’ Nikasogea na kusema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je mimi ni miongoni mwa Ahlul-Baiti wako? Akasema: ‘Kaa pembeni, hakika wewe upo katika kheri.’”280 Ibnu Jarir amesema: Imepokewa kutoka kwa Atiyyah kutoka kwa Said amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alise  Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414. 280.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414. 278. 279.

228

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 228

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ma: “Aya hii “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” iliteremka kwa ajili ya watu watano: Mimi, Ali, Fatima, Hasan na Husein.”281 Ametusimulia Bakir bin Mismar amesema: Nilimsikia Amir bin Sa’d akisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema pindi wahyi ulipomshukia, akamchukua Ali na wanae wawili na Fatima, akawafunika nguo yake kisha akasema: “Ewe Mola Mlezi! hawa ndio ndugu zangu na Ahlul-Baiti wangu.”282 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Sura Ahzab: 56). Bukhari katika kutafsiri Aya hii amesema: Imepokewa kutoka kwa Ka’ab bin Ájrah amesema: Palisemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”283   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 415.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 415 283.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 432. 281. 282.

229

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 229

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Imam Ahmad amesema: Imepokewa kutoka kwa al-Hakam amesema: “Nilimsikia Ibnu Abi Layla akisema: Kaab bin Ajrah alikutana na mimi na kuniambia: Je nikupe zawadi? Siku moja alikuja Mtume wa Mwenyezi Mungu, nasi tukamuuliza, tukasema: Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”284

Bukhari amesema: “Ametusimulia Abdullah bin Yunus kutoka kwa Abu Said al-Khudriy amesema: Tulimwambia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu basi ni ipi namana ya kukusalia? Akasema: “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad mja Wako na Mtume Wako kama ulivyowarehemu aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”285

Abdurahman bin Abu Layla, amesema: Kutoka kwa Ka’ab bin Ajrah, ame-sema: Ilipoteremka: “Hakika Mwenyezi Mungu   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 432.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 432.

284. 285.

230

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 230

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” Tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu ni ipi namana ya kukusalia? Mtume akasema: “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’’’ 286

Kutoka kwa Ibnu Mas’ud al-Ansariy alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu alikwenda na kutukuta tumeketi katika baraza la Sa’d bin Ubada. Bushru bin Sa’d akamwambia: Mwenyezi Mungu ametuamuru tukutolee salamu ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi ni vipi tutakavyokusalia? Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akakaa kimya mpaka tukatamani kwamba asingemuuliza. Kisha akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim katika walimwengu, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’’’   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 433.

286.

231

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 231

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Pia ameipokea Abu Daud, Tirmidhi, Nasai na Ibnu Jariri kutoka katika hadithi ya Malik. Tirmidhi amesema: Ni nzuri na sahihi.287

SURAT YASIN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ikasemwa: Ingia peponi! Akasema: Laiti watu wangu wangejua. Jinsi Mola wangu alivyonighufuria na akanifanya katika waheshimiwa.” (Qur’ani Tukufu Sura ­Yasin; 36:26-27). Al-Hafidh Abu Qasim Tabaraniy amepokea kwamba: “Alitusimulia Husein bin Is’haq at-Tusturiy kutoka kwa Ibnu Abi Najihi kutoka kwa Mujahid kutoka kwa Ibnu Abbas (a.s.) kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Vinara ni watatu: Kinara kuelekea kwa Musa (a.s.) ni Yoshua bin Nun. Kinara kuelekea kwa Isa (a.s.) ni yule aliyezungumziwa na Sura Yasin, na kinara kuelekea kwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Ali bin Abu Talib (a.s.).” Hakika yenyewe ni Hadithi isiyokubalika haijulikani ila kwa njia ya Husein al-As’haq naye ni Shia asiyefuatwa.288

SURAT AS-SAFFAT Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amani kwa Ilyasin.” (Qur’ani Tukufu Sura as-Saffat; 37:130). Ibnu Mas’ud amesema: Yaani Aali Muhammad (s.a.w.w.). 289

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23).   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 433.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 486. 289.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 21. 287. 288.

232

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 232

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa as-Sadiy, kutoka kwa Abu Daylam, amesema: “Alipoletwa Ali bin Husein na hali ni mateka na kusimamishwa katika barabara kuu ya Damascus alisimama mzee mmoja kati ya watu wa Sham, akasema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye amewauwa na kuwang’oeni na kung’oa mzizi wa fitina.” Ali bin Husein akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu ndio. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’ Akajibu nimewahi kusoma Qur’ani na sijawahi kusoma Aali Haa Miim. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...”’ Mzee akasema: ‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’290 Ibnu Abi Hatim amesema: Ametusimulia Ali bin Husein amesema: “Ametusimulia mtu aliyemtaja jina: Ametusimulia Husein alAshqar kutoka kwa Qaysi kutoka kwa al-A’mash, kutoka kwa Said bin Jubair, kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Ilipoteremka: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” walimuuliza: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa ndugu ambao Mwenyezi Mungu ameamuru kuwapenda? Akasema: “ Fatima na kizazi chake.”291 Imepokewa kutoka kwa Zayd bin Arqam amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuwaachia kati yenu kile ambacho lau mkishikamana nacho katu hamtapotea baada yangu, kimojawapo ni kitukufu kuliko kingine: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka toka mbinguni hadi aridhini. Na kingine ni kizazi changu watu wa nyumba yangu, na havitoachana mpaka vinikute kwenye hodhi, basi angalieni ni jinsi gani mtakavyobaki navyo.”292   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 101.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 102. 292.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 102. 290. 291.

233

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 233

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa Jabir bin Abdillah amesema: “Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu Siku ya Arafa akiwa juu ya ngamia wake al-Qas’wau akiwahutubia watu, nikamsikia akisema: “Enyi watu! Hakika mimi nimeacha kati yenu kile ambacho lau mkishikamana nacho hamtapotea: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu watu wa nyumba yangu.”293 Kutoka kwa Abu Dhari al-Ghaffariy alisema huku akiwa ameshikilia mlango: Enyi watu! Anayenitambua basi ameshanitambua na asiyenitambua basi mimi ni Abu Dhari, nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: “Hakika mfano wa Ahlul-Baiti wangu kwenu nyinyi ni sawa na safina ya Nuh (a.s.) aliyeipanda aliokoka.”294

SURA AD-DUKHAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Mbingu na ardhi hazikuwalilia; wala hawakupewa muda.” (Qur’ani Tukufu Sura ad-Dukhan; 44:29). Ibnu Abi Hatim amesema: “Ametusimulia Ali bin Husein amesema: Ametusimulia Abdusalami bin Asim, amesema: Ametusimulia Ishaq bin Ismail, amesema: Ametusimulia al-Mustawridu bin Sabiq kutoka kwa Ubaydul-Maktabi kutoka kwa Ibrahim, amesema: “Dunia haijamlilia yeyote tangu kuumbwa kwake ila wawili.” Nikamwambia vipi? Akasema: “Inapatwa na wekundu na kuwa kama ua waridi. Hakika Yahya bin Zakariya alipouawa mbingu ilipatwa na wekundu na ikadondosha mvua ya damu. Na hakika Husein bin Ali (a.s.) alipouwawa mbingu ilipatwa na wekundu.”295   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 102.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4, Uk. 102. Lakushangaza sana ni kwamba Ibnu Kathir anaizingatia Hadithi mashuhuri kama hii kuwa ni dhaifu. Sijui amesahau au amejisahaulisha Hadithi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Ardhi haijapata kumbeba wala mbingu haijapata kumfunika mtu mkweli kuliko Abu Dhari al-Ghaffariy.” 295.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 127. 293. 294.

234

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 234

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ametusimulia Jarir kutoka kwa Yazid bin Abi Ziyad amesema: “Alipouwawa Husein bin Ali (a.s.) pande zote za mbingu zilipatwa na wekundu muda wa miezi minne. Na wekundu wake ndio kulia kwake.”296 Na wametaja katika habari za mauaji ya Husein (a.s.) kwamba siku hiyo hakuna jiwe lililoinuliwa au kugeuzwa ila chini yake kulikutwa damu nzito, na kwamba jua lilipatwa, mbingu ikawa nyekundu na ikanyesha mvua ya mawe.297

SURAT AL-AHQAF Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi watu wetu muitikieni Mwitaji wa Mwenyezi Mungu na muaminini, atakusameheni madhambi yenye kuumiza.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahqaf; 46:31).

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba alisema: “Nilikuwa pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) usiku ndipo ukamfikia msafara wa majini, akavuta pumzi. Nikamwambia una nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Ninajiom  Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 127.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 127. Ibnu Kathir katika habari hii anasema: “Dhahiri ni kwamba habari hii ni miongoni mwa uzushi wa mashia na uongo wao ili wakuze jambo….”. Nashangaa ni wepesi ulioje ulionao katika kuwatuhumu wengine? Na hilo tunakujibu nawe ndio wapasa zaidi kuwa muongo, kwa sababu si sisi pekee tuliopokea hadithi hii, hiyo ni mosi. Pili: Wewe mwenyewe katika tafsiri yako umepokea kwamba: Mbingu humlilia muumini siku arubaini. Je washakia Husein kuwa bwana wa waumini na kinara wao duniani na akhera baada ya babu yake, mama yake, baba yake na kaka yake? Tatu: Kwa nini wazikubali habari hizi zihusishwapo na Yahya bin Zakariya lakini si pale zinapomhusu Husein mtoto wa binti ya bwana wa Manabii na Mawasii?

296. 297.

235

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 235

2/14/2018 12:11:59 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

boleza mwenyewe ewe Ibnu Mas’ud.” Nikamwambia ainisha Khalifa. Akauliza nani? Nikamwambia Abu Bakr. Akakaa kimya, kisha ukapita muda kadhaa akavuta tena pumzi, nikamwambia kwa haki ya baba yangu na mama yangu, una nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Ninajiomboleza mwenyewe ewe Ibnu Mas’ud.” Nikamwambia ainisha Khalifa. Akauliza nani? Nikamwambia Umar. Akakaa kimya muda kadhaa, kisha akavuta tena pumzi, nikamwambia una nini? Akasema: “Ninajiomboleza mwenyewe.” Nikamwambia ainisha Khalifa. Akauliza nani? Nikamwambia Ali bin Abu Talib. Akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi Mwake, lau wakimtii basi wote wataingia Peponi.”298

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Imesemekana kwamba hakuna yeyote aliyeifanyia kazi Aya hii kabla ya hukumu yake kufutwa ila Ali bin Abu Talib (a.s.).299 Ibnu Abi Najihu amesema: Kutoka kwa Mujahidu, amesema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib, alitoa sadaka ya dinari kisha akasema siri na Mtume (s.a.w.w.) na alimuuli  Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 147.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 286.

298. 299.

236

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 236

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

za mambo kumi, ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.).” 300 Kutoka kwa Mujahid amesema: Ali (a.s.) alisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nilikuwa na dinari nikaibadili kwa dirhamu kumi, hivyo ikawa kila ninaposema siri na Mtume wa Mwenyezi Mungu natoa sadaka dirhamu moja, mpaka hukumu yake ikafutwa huku hakuna yeyote kabla yangu aliyeifanyia kazi na wala hakuna baada yangu atakayeifanyia kazi, nayo ni: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana… ..””.301

SURAT AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake, na Jibril na waumini wema na Malaika….” ­ (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:4). Laythu bin Abi Salim amesema kutoka kwa Mujahid kwamba: “Na waumini wema’’ ni Ali bin Abu Talib.302 Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na waumini wema’’ kuwa ni Ali bin Abu Talib.303

Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 286.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 286. 302.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 340. 303.   Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 340. Mchakato toka katika tafsiri hii umetimia siku ya ishirini na tatu ya Mfunguo tatu Mwaka 1426 A.H. katika Jiji la Qum Takatifu. 300. 301.

237

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 237

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA SUYUTI, INAYOITWA AD-DURUL-MANTHUR FIT-TAFSIR-­ IL-MAATHUR SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na ­akamkubalia toba yake, hakika yeye ndiye apokeaye toba, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:37).

Ad-Daylami ameiandika katika Musnadul-Firdawsi kwa riwaya aliyoipokea kutoka kwa Ali, kwamba alisema: “Nilimuuliza Mtume (s.a.w.w.) kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Basi Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na akamkubalia toba yake.” Akasema (s.a.w.w.): ‘Hakika Mwenyezi Mungu alimshusha Adam huko India, Hawa huko Jiddah, Ibilisi huko Baysan, na nyoka huko Isfahani. Nyoka alikuwa na miguu kama ya ngamia, Adam akaishi huko India miaka mia moja huku akilia kwa kujutia kosa lake, mpaka Mwenyezi Mungu akampelekea Jibril na kumwambia: ‘Ewe Adam! Hivi sijakuumba kwa mkono wangu! Hivi sijakupulizia roho yangu! Hivi sikuwaamuru malaika wangu wakusujudie! Na hivi sijakuoza Hawa, kijakazi wangu!’ Akasema: ‘Ndio umenifanyia hayo.’ Akamwambia: ‘Basi ni kwa nini walia kiasi hiki?’ Akajibu: ‘Na ni kipi kitanizuia nisilie na hali nimetoka kwenye ujirani wa 238

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 238

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

­ ahman.’ Akamwambia: ‘Shikamana na maneno haya, hakika MweR nyezi Mungu ataipokea toba yako na kukughufiria dhambi yako.’ Akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! hakika mimi nakuomba kwa haki ya Muhammad na aali Muhammad, Subhanaka hakuna Mungu apasaye kuabudiwa ila Wewe. Nimetenda uovu na nimeidhulumu nafsi yangu hivyo nighufirie hakika Wewe ni Ghafuru Rahimu. Ewe Mwenyezi Mungu! hakika mimi nakuomba kwa haki ya Muhammad na aali Muhammad, Subhanaka hakuna Mungu apasaye kuabudiwa ila Wewe. Nimetenda uovu na nimeidhulumu nafsi yangu hivyo nisamehe hakika Wewe ni Mwenye kupokea toba na ni Rahimu.’ Haya ndio maneno aliyoyapokea Adam (a.s.).”’304 Ibnu an-Najjar ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Nilimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kuhusu maneno ambayo aliyapokea Adam toka kwa Mola wake Mlezi na hatimaye akamkubalia toba yake. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Aliomba: Kwa haki ya Muhammad, Ali, Fatima, Hasan na Husein nikubalie toba yangu. Akamkubalia toba yake.”305 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274).   Kwa maelezo zaidi rejea Tafsirul-Burhan Juz. 1 Uk. 86, Chapa ya Ismailiyyan.   Kwa uwazi kabisa inadhihiri kwamba Ahlul-Baiti ni Ali, Fatima, Hasan na Husein (a.s.) nao ndio Aali Muhammad na ndio waliokusudiwa katika Kisa cha Kishamia na katika Aya ya Utakaso.

304. 305.

239

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 239

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Abdurazzaq, Abdu bin Hamid, Ibnu Jarir, Ibnu al-Mundhir, Ibnu Abi Hatim, Tabarani na Ibnu Asakir wameandika kwa njia itokayo kwa Abdul-Wahab bin Mujahid kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibnu Abbas, amesema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri..”: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib alikuwa na dirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, nyingine siri na nyingine dhahiri.”306

SURA AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na kizazi cha Ibrahim na kizazi cha Imran juu ya walimwengu wote.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:33).

Ibnu Jarir, Ibnu al-Mundhir na Ibnu Abi Hatim wameandika kupitia njia ya Ali kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “na kizazi cha Ibrahim na kizazi cha Imran” amesema: “Hao ni waumini kutoka katika aali Imran, aali Ibrahim, aali Yasin na aali Muhammadi (s.a.w.w.).”307   Rejea Shawahidut-Tanziil cha al-Haskaniy Juz. 1, Uk. 109, Chapa ya Beirut ya Kimataifa ya Mwaka 1974. Humo ameandika kutoka kwa al-Kalbiy kutoka kwa Abu Salih kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri..” kwamba aliteremka kwa ajili ya Ali pekee, katika kisa cha dirhamu zake nne alizozitoa sadaka, moja mchana nyingine usiku, nyingine kwa siri na nyingine kwa dhahiri. 307.   Nasema: Aali Yasin ndio aali Muhammad (s.a.w.w.) kwa sababu Yasin ni moja ya majina ya Mtume (s.a.w.w.) kama alivyotamka wazi hilo Suyuti katika tafsiri hii Juz. 5, Uk. 258. Na al-Khazin ametaja hilo katika Juz. 4, Uk. 2 na Juz. 5, Uk. 286. Na limetajwa katika Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 118, Chapa ya Beirut. Kwa ziada rejea Tafsirul’Ayyash Juz. 1, Uk. 191, Chapa ya Beirut ya mwaka 1991. 306.

240

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 240

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:37). Ameandika Abu Ya’la ameandika kutoka kwa Jabir kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bila kula chakula mpaka hali hiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenye nyumba za wakeze lakini hakupa kwa yeyote chochote, ndipo akaenda kwa Fatima na kumwambia: “Ewe mwanangu mpendwa! Je una chochote ninachoweza kula kwani hakika mimi ni mwenye njaa?” Akamjibu: “Wallahi sina.” Mtume alipotoka jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vya mkate na finyango ya nyama, akavitwaa na kuviweka ndani ya bakuli lake, akasema: “Wallahi katika hiki nitampa kipaumbele Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kabla ya nafsi yangu na kabla ya yule aliyopo kwangu.” Japokuwa wote walikuwa wanahitajia chakula lakini Fatima alimtuma Hasan au Husein aende kumwita Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) naye alikwenda. Fatima akamwambia: “Kwa haki yako na ya mama yangu, Mwenyezi Mungu ameleta kitu nami nimekihifadhi kwa ajili yako.” Akamwambia: “Kilete ewe binti yangu mpendwa.” Akamletea bakuli na alipolifunua ghafla akakuta limejaa mikate na nyama, alipokitazama akapatwa na mshangao na akatambua kuwa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu. Akamhimidi Mwenyezi Mungu na akamkabidhi chakula hicho Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Mtume (s.a.w.w.) alipokiona alimhimidi Mwenyezi Mungu na akasema: “Umetoa wapi hivi ewe binti yangu mpendwa?” Akajibu: “Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu ewe baba yangu mpendwa. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” 241

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 241

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mtume akamhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Ambaye amekufanya ewe binti yangu mpendwa kifani wa Seyida wa wana wa Israel (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwa aruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu kisha akiulizwa kakipata wapi husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.”308 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:42).

Al-Hakima ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora ulimwenguni ni: Khadija, Fatima, Maryam na Asia mke wa Firaun.” Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika Mwenyezi Mungu aliwateua wanne kwa ubora kuliko wanawake wote wa ulimwenguni: Asia binti Muzahim, Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad (s.a.w.w.).” Ahmad, Tirmidhi, Ibnu al-Mundhir, Ibnu Habban na al-Hakim wameandika kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha toka katika wanawake wa ulimwenguni: Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad (s.a.w.w.) na Asia mke wa Firaun.”   Nasema: Hilo si zito kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, ikiwa Mariam ni mkweli wa Kizazi cha Israil na Fatima ni mkweli wa umma huu naye ni mbora wa wanawake wote wa ulimwengu.

308.

242

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 242

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Abi Shayba na Ibnu Jarir wameandika kutoka kwa Fatima (a.s.) kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliniambia: Wewe ndiye mbora kuliko wanawake wote wa peponi na si Mariam al-Batul.” Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora wa peponi ni Maryam binti Imran, Fatima binti Muhammad (s.a.w.w.), Khadija binti Khuwaylid na Asia mke wa Firaun.” Ibnu Asakir ameandika kupitia njia ya Muqatil, kutoka kwa Dhahak kutoka kwa Ibnu Abbas kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Wanawake wanne ni wabora kuliko wanawake wote wa zama zao: Maryam binti Imran, Asia binti Muzahim, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad (s.a.w.w.) na yeye ndiye mbora wao kiulimwengu.”309 Ibnu Shayba ameandika kutoka kwa Abdurahman bin Abi Layla kwamba amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Fatima ndiye mbora wa wanawake wa ulimwenguni baada ya Maryam binti Imran, Asia mke wa Firaun na Khadija binti Khuwaylid.”310 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Allama al-Muttaqiy al-Hindiy amepokea katika kitabu Kanzul-Ummal hadithi hii kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Ewe Fatima! Hivi hauridhii wewe kuwa ndiye mwanamke bora kuliko wanawake wote wa ulimwenguni na mbora kuliko wake wote wote wa waumini na mbora kuliko wanawake wote wa umma huu.” Tazama Kanzul-Ummal Juz. 12 Uk. 12, Namba 34232. 310.   Allama al-Bahraniy amepokea katika al-Burhani Juz. 1 Uk. 281, Chapa ya Qum, kutoka kwa al-Mufadhal bin Umar kwamba amesema: Nilimwambia Abu Abdillah (a.s.): Nieleze kuhusu kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu kwamba Fatima ni mbora wa wanawake wa ulimwenguni. Je ni ulimwengu wa zama zake? Akasema (s.a.w.w.): “Hali hiyo ni kwa Mariam yeye ndiye aliyekuwa mbora kwa wanawake wa ulimwengu wa zama zake. Ama Fatima yeye ni mbora wa wanawake wa ulimwengu mzima kuanzia wale wa mwanzo mpaka wa mwisho.” 309.

243

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 243

2/14/2018 12:12:00 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:61).

Al-Hakim, Ibnu Mardawayhi na Abu Naiim katika ad-Dalail wameandika kutoka kwa Jabir kwamba alisema: al-Aqib na Seyyid walikwenda kwa Mtume (s.a.w.w.) naye akawalingania waingie katika Uislamu, wakasema: “Tumesilimu ewe Muhammad.” Akawaambia: “Mmesema uongo, na mkitaka nitawaambieni ni kipi kinachowazuia kuingia katika Uislamu.” Wakamwambia: “Tueleze.” Akawaambia: “Kuupenda msalaba, kunywa pombe na kula nyama ya nguruwe.” Jabir anasema: Ndipo akawaomba wafanye maapizano, nao wakamwahidi iwe siku itakayofuata. Mtume wa Mwenyezi Mungu akatoka siku iliyofuata akiwa amemshika mkono Ali, Fatima, Hasan na Husein, kisha akawatumia ujumbe waje lakini wakakataa kuitikia wito na baadaye wakamkubalia (kufanya suluhu). Mtume akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye alituma kwa haki! Lau wangethubutu kufanya (maapizano) basi bonde lingeteketea kwa moto.” Jabir anasema: Na kwa ajili yao iliteremka Aya: “Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu.” Nafsi zetu na nafsi zenu ni Mtume 244

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 244

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wa Mwenyezi Mungu na Ali. Watoto zetu ni Hasan na Husein. Na wanawake zetu ni Fatima (a.s.). Al-Hakim ameandika kutoka kwa Jabir kwamba: Ujumbe wa Najran ulifika kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: “Unasemaje kuhusu Isa?” Akawaambia: “Yeye ni Roho wa Mwenyezi Mungu, Neno Lake, Mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake.” Wakasema: “Upo tayari kuapizana nasi kwani ukweli si hivyo?” Akasema: “Je hilo mwaliridhia?” Wakasema ndio. Akasema: “Kama mnataka basi hakuna kizuizi.” Ndipo akaenda kuwakusanya watoto wake Hasan na Husein. Kiongozi wao akasema: “Msifanye maapizano na mtu huyu, Wallahi kama mtaapizana naye basi litaangamizwa moja kati ya makundi mawili.” Wakaja na kumwambia: “Ewe Abul-Qasim Hakika waliotaka kufanya maapizano na wewe ni wale masafihi miongoni mwetu, nasi tunapenda utusamehe.” Akaesema: “Nimeshawasamehe.” Kisha akasema: “Hakika adhabu imeshatanda Najran.” Muslim, Tirmidhi, Ibnu al-Mundhir, al-Hakim na al-Bayhaqiy katika Sunan yake wameandika kutoka kwa Sa’d ibnu Abi Waqqas kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii: “Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husein, akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio ndugu zangu.” Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Aliyai bin Ahmar al-Yashkariy kwamba amesema: Ilipoteremka Aya hii: “Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima na watoto wao Hasan na Husein. Akawaita mayahudi waje kwenye maapizano na ndipo kijana toka kwa mayahudi akasema: “Ole wenu! Hivi jana ndugu zenu waliogeuzwa manyani na nguruwe hawakuwakatazeni kwamba msifanye maapizano.” Ndipo wakaacha. 245

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 245

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Al-Bayhaqiy katika ad-Dalail ameandika kupitia njia ya Salmah bin Abdu Yushu’ kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliwaandikia barua watu wa Najran kabla ya kushushiwa Bismillahi ya Sulayman: “Kwa jina la Mungu wa Ibrahim, Is’haqa na Ya’qub. Kutoka kwa Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenda kwa Askofu wa Najran na wakazi wa Najran. Ikiwa mtasilimu basi hakika mimi nitamhimidi Mwenyezi Mungu kwenu Mungu wa Ibrahim, Is’haqa na Ya’qub. Ama baad, hakika mimi nawaita kwenye ibada ya Mwenyezi Mungu na mtoke kwenye ibada ya waja, na nawaita kwenye mamlaka ya Mwenyezi Mungu na mtoke kwenye mamlaka ya waja. Hivyo mkikataa basi ni juu yenu kodi, na kama mkikataa nitaidhinisha vita dhidi yenu, wasalamu.” Askofu aliposoma barua hii aliisadiki na akaingiwa na hofu kubwa, ndipo akatuma ujumbe aitwe mtu mmoja mkazi wa Najrani aliyejulikana kwa jina la Sharhab?l bin Wid?’h, akampa barua ya Mtume (s.a.w.w.) naye akaisoma. Askofu akamuuliza ni ipi rai yako? Sharhab?l akasema: “Nimeyajua yale ambayo Mwenyezi Mungu alimwahidi Ibrahim ambayo ni unabii kutoka katika kizazi cha Ismail, hakuna kizuizi kinachozuia mtu huyu kuwa ndiye, hivyo sina rai katika unabii. Lau ingekuwa ni kuhusu mambo ya kidunia basi ningekupa rai na ningetoa juhudi zote kwako.” Askofu akamwita mmoja baada ya mwingine katika wakazi wa Najran, na wote walisema mfano wa yale aliyosema Sharhab?l, ndipo wakaamua kwa pamoja wamtume Sharhab?l bin Wid?’h, Abdullah bin Sharhab?l na Jabbari bin Faydh waende kumdadisi Mtume wa Mwenyezi Mungu na hatimaye wawaletee habari zake. Ujumbe ukasafiri hadi kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) wakamuhoji naye akawahoji, basi mahojiano yaliende246

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 246

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

lea mpaka wakamwambia: “Unasemaje kuhusu Isa bin Mariam?” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawaambia: “Leo hii sina kitu cha kuwaambieni kuhusu Isa, subirini mpaka kesho asubuhi ndipo nitawaelezeni yale nitakayoteremshiwa kuhusu Isa bin Mariam.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hizi: “Hakika mfano wa Isa mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam, alimuumba kutokana na udongo, kisha akamwambia kuwa, basi akawa. Ndiyo haki itokayo kwa Mola wako Mlezi, basi usiwe miongoni mwa wenye kutia shaka. Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:59-61). Lakini wakakataa kuamini hilo. Siku iliyofuata baada ya kuwa tayari ame-shawapa habari, Mtume wa Mwenyezi Mungu alitoka kwa ajili ya maapizano akiwa na Hasan na Husain ndani ya joho lake na Fatima akiwa nyuma ya mgongo wake, licha ya kwamba kipindi hicho tayari alikuwa ameshakuwa na wanawake wengi. Sharhab?l akawaambia marafiki zake: “Hakika kuna jambo ninaloliona mbele, ikiwa kweli huyu ni Nabii Mtume basi kitendo cha kuapizana naye hakitambakisha yeyote miongoni mwetu juu ya ardhi, hata unywele na ukucha bali ni lazima ataangamia.” Wakamwambia: Ni ipi rai yako? Akasema: “Rai yangu ni kwamba tumuombe abadili maamuzi kwani hakika mimi namwona ni mtu asiyehamia kwenye maamuzi ya kiupuuzi katu.” Wakamwambia hilo ni juu yako. Ndipo Sharhab?l akamwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na kumwambia: “Hakika mimi nimeona kheri nyingine kuliko kuapizana na wewe.” Akamuuliza ni ipi hiyo? Akasema: 247

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 247

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Ubadili hatua yako ya leo mpaka kwenye ile ya usiku (wa jana), na toka kwenye ile ya usiku wako mpaka kwenye ile ya (jana) asubuhi, basi hatua yoyote utakayoichukua hapo kwa ajili yetu tutaipokea.” Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akabadili maamuzi akarejea bila kuapizana nao na akafanya nao suluhu kwa sharti walipe kodi.311 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote kwa pamoja wala msifarakane..” (Sura Aali Imran: 103). Ahmad ameandika kutoka kwa Zayd bin Thabit kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuacha kati yenu mirathi mbili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka baina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu watu wa kwenye hodhi.”312 Tabarani ameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Mimi nawatangulia nanyi mtanikuta katika hodhi, basi angalieni ni jinsi gani mtakavyoishi na vizito viwili nyuma yangu.” Pakasemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni vipi hivyo vizito viwili? Akasema: “Kikubwa ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba ambayo ncha moja imo mikononi mwa Mwenyezi Mungu na ncha nyingine mikononi mwenu, hivyo shikamaneni nacho hamtate  Ameiandika al-Haskani katika kitabu Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 120, chapa ya ­Beiruti. Na al-Manaqib cha Ibnu al-Mughazaliy, Hadithi ya 313. Na Ahmad bin Hanbal katika kitabu Fadhailus-Sahaba, Hadithi ya 27, mlango wa fadhila za Hasan na Husain (a.s.). 312.   Nasema: Baadhi ya wale ambao wana maradhi nyoyoni mwao miongoni mwa wale wenye chuki na uadui na Ahlul-Baiti (a.s.) wameondoa maneno ‘Kizazi changu’ na kuweka badala yake neno ‘sunna yangu’, na hii ni batili ya wazi, kwa sababu hata hiyo Sunna nayo inahitaji mfasiri na mfafanuzi, na hakuna ajuaye hayo ila Ahlul-Bait (a.s.) kwa sababu wao ndio wajuzi zaidi wa yale yaliyomo ndani ya nyumba. 311.

248

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 248

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

leza wala kupotea. Na kidogo ni kizazi changu, na hakika hivyo viwili havitaachana mpaka vinifikie kwenye hodhi. Na hilo nilimuomba Mola wangu Mlezi hivyo msivitangulie mtaangamia na wala msivifundishe kwani hakika hivyo vina ujuzi kulikoni nyinyi.” Ibnu Sa’d, Ahmad na Tabarani wameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudri kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Enyi watu! Hakika mimi ni mwenye kuacha kati yenu mambo mawili ambayo lau mkishikamana nayo hamtapotea baada yangu, kimoja ni kikubwa kuliko kingine: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka baina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu watu wa nyumba yangu, na hakika hayo mawili hayataachana mpaka yanikute kwenye hodhi.”313

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:3).

Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kwa sanad ­dhaifu kutoka kwa Abu Said al-Khudri kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipomsimika Ali Siku ya Ghadiri ya Mfun  Al-Haskani katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 130 anapotafsiri Aya hii, ameandika kutoka kwa Ali bin Musa Ridha (a.s.) kutoka kwa baba zake kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Anayetaka kupanda safina ya uokovu na kushikamana na shikio imara na kushikamana na kamba ngumu ya Mwenyezi Mungu basi amtawalishe Ali na awafuate viongozi toka katika kizazi chake.”

313.

249

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 249

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

guo tatu alisema (s.a.w.w.): “Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali ni mwenye mamlaka juu yake.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: Leo nimekukamilishieni dini yenu.314 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Al-Khatib ameandika katika al-Muttafaq kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Ali alitoa sadaka pete yake ndipo Mtume akamuuliza muombaji - ni nani aliyekupa pete hii? Akasema ni yule aliyomo kwenye rukuu, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Abdurazzaq, Abdu bin Hamid, Ibnu Jarir, Abu Shaykh na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui,” iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib. Tabarani katika al-Awsat na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ammar bin Yasir kwamba alisema: “Muombaji alisimama   Hadithi hii imepokewa na sahaba wakubwa mia moja na kumi, na tabiina thamanini na nne. Pia zaidi ya watu mia nne miongoni mwa wasomi, wanahadithi, wafasiri, wanahistoria na wataalamu wa fani ya wapokezi, wameiandika hadithi hii muhimu. Hivyo anayetaka maarifa zaidi ni juu yake kurejea Enklopedia ya Ghadiri ya Allama al-Amin Juz. 1. Humo ameipokea toka kwa wanazuoni mia tatu na sitini na toka katika vitabu ishirini na sita wote wakiwa ni wanazuoni wa kisunni na ni vitabu vya kisunni.

314.

250

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 250

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kwa Ali na hali akiwa katika rukuu ya Swala ya sunna, ndipo akavua pete yake na kumpa muombaji, naye akaenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumjulisha hilo, ndipo Aya hii ikateremka kwa Mtume (s.a.w.w.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawasomea sahaba zake kisha akasema: “Yule mbaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali ni mwenye mamlaka juu yake. Ewe Mwenyezi Mungu! Mpende ampendaye na mfanyie uadui amfanyiaye uadui.” Abu Shaikh na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.) kwamba alisema: “Aya hii ilimteremkia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) nyumbani kwake: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui”, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoka na kuingia msikitini akawakuta watu wakisali, wengine wamo katika rukuu, wengine katika sijda na wengine katika kisimamo, ghafla akamwona muombaji, akamuuliza: Ewe muombaji, je kuna yeyote aliyekupa kitu? Akajibu: ‘Hapana ila yule aliyemo katika rukuu naye ni Ali bin Abu Talib amenipa pete yake.”’ Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Mujahid kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, alitoa sadaka na hali akiwa katika rukuu. Ibnu Mardawayhi ameandika kupitia njia ya al-Kalbiy kutoka kwa Abu Salih kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Abdullah bin Salam alikuja na kundi lake kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu 251

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 251

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

(s.a.w.w.) wakati wa Adhuhuri, wakasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Hakika nyumba zetu ziko mbali na hatupati wa kuketi nasi na kujumuika nasi kinyume na msikiti huu, na hakika jamaa zetu walipoona tumemsadiki Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na tumeiacha dini yao wametudhihirishia uadui na wameapa kwamba hawatajumuika nasi na wala hawatakula pamoja nasi, jambo hilo limekuwa zito juu yetu.’ Wakiwa bado wanaendelea kumlalamikia hali hiyo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ghafla ilimshukia Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Sala ya Dhuhri ikanadiwa na akatoka Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). akasema (kumuuliza muombaji): ‘Kuna yeyote aliyekupa kitu?’ Akajibu ndio. Akamuuliza: ‘Nani?’ Akajibu: Yule aliyesimama. Akamuuliza: ‘Alikupa akiwa katika hali gani?’ Akajibu: Akiwa katika rukuu. Akasema: ‘Yule ni Ali bin Abu Talib.’ Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa takbira huku akisema: ‘Na mwenye kumtawalisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini, basi kwa hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kushinda.’ Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Ali bin Abu Talib alikuwa amesimama akisali ndipo muombaji akapita, naye akiwa katika rukuu, akampa pete yake, ndipo ikateremka Aya hii: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Iliteremka kwa ajili ya wale walioamini na Ali ndio kinara wao. Abdu bin Hamid, Ibnu Jarir na Ibnu al-Mundhir wameandika kutoka kwa Abu Ja’far kwamba aliulizwa kuhusu Aya hii kwamba ni akina nani walioamini? Akasema: “Ni wale walioamini. 252

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 252

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Akaambiwa imetufikia habari kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib. Akasema: Ali ni miongoni mwa wale walioamini.” Abu Naim ameandika katika al-Hilyah kutoka kwa Abdul-Malik bin Abu Sulayman kwamba alisema: Nilimuuliza Abu Ja’far Muhammad bin Ali kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Nikasema hakika masahaba wa Muhammad (s.a.w.w.) wanasema kwamba ni Ali. Akasema: “Ali ni miongoni mwao.”315 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola Wako; na kama hutafanya, basi hukufikisha ujumbe Wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalim.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:67).

Ibnu Abi Hatim, Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Said al-Khudriy kwamba alisema: Aya hii: “Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola Wako; na kama hutafanya, basi hukufikisha ujumbe Wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalim.” Iliteremka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) Siku ya Ghadir Khum kwa ajili ya Ali bin Abu Talib. Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba alisema: Zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu tulikuwa tukisoma: “Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola Wako;   Rejea pia Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 161, Chapa ya Beirut.

315.

253

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 253

2/14/2018 12:12:01 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kwamba hakika Ali ni mwenye mamlaka juu ya waumini, na kama hutafanya, basi hukufikisha ujumbe Wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu.”316

SURAT AL-AN’AM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na tukampa Is’haka na Yakub, wote tukawaongoza, na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:84-85).

Ibnu Abi Hatim ameandika kutoka kwa Abu Harbi bin al-As’wad kwamba amesema: Hajjaj alituma ujumbe kwa Yahya bin Ya’mar kwamba: ‘Imenifikia habari kuwa wewe unadai kwamba Hasan na Husein ni katika kizazi cha Mtume (s.a.w.w.) kwa ushahidi wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu, nami nimekisoma kuanzia mwanzo wake mpaka mwisho wake lakini sijauona.’ Akamjibu: Hivi unasoma Sura An’am: “Na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafan  Ad-Durul-Manthur Juz. 3, Uk. 28. Pia ameiandika Ibnu Asakir katika kitabu chake Tarikhud-Damashq katika wasifu wa Amirul-Muuminina (a.s.), Hadithi ya 452.

316.

254

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 254

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa?” Akasema ndio nimesoma. Akamuuliza: ‘Huoni Isa ni kizazi cha Ibrahim na hali hana baba?’ Akasema: Umesema kweli. Abu Shaikh, al-Hakim na al-Bayhaqiy wameandika kutoka kwa Abdul-Malik bin Umayri kwamba alisema: Yahya bin Ya’mar aliingia kwa Hajjaj na akamtaja Husein. Hajjaj akasema: “Hakuwa katika kizazi cha Mtume (s.a.w.w.).” Yahya akasema: “Umenena uongo.” Hajjaj akasema: “Niletee dalili juu ya hilo ulisemalo. “ Ndipo akamsomea: “…..na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa” hivyo Mwenyezi Mungu akatoa habari kwamba Isa ni katika kizazi cha Ibrahim. Hajjaj akasema: “Umesema kweli.”317

SURA AL-A’ARAF Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na semeni: Tufutie dhambi zetu, na ingieni mlangoni kwa ­unyenyekevu, tutakusameheni makosa yenu tutawazidishia watendao mema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:161).

Ibnu Shayba ameandika kutoka kwa Ali bin Abu Talib kwamba alisema: Hakika mfano wetu katika umma huu ni kama mfano wa Safina ya Nuhu na mlango wa kufutiwa madhambi wa Kizazi cha Israil.   Rejea Tafsirul-Burhan ya Sayyid Hashim al-Bahraniy Juz. 1, Uk. 538, Chapa ya Qum.

317.

255

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 255

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na masikini na msafiri……” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:41). Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba alisema: Aali Muhammad waliopewa khumsi ni wale Aali Ali, Aali Abbas, Aali Ja’far na Aali Aqil. Ibnu Abi Shayba ameandika kutoka kwa Mujahid kwamba alisema: Aali Muhammad si halali kwao sadaka hivyo akawawekea Khumsi.318 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na kama wakitaka kukuhadaa, basi Mwenyezi Mungu ­atakutosheleza. Yeye ndiye aliyekusaidia kwa ushindi wake na kwa waumini.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:62).

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema: “Arshi imenakishiwa kwa “Hapana Mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mimi pekee sina mshirika, Muhammad ni mja wangu na Mtume wangu, nimempa nguvu kupitia Ali.” Na hiyo ndio kauli ya Mwenyezi Mungu: “Yeye ndiye aliyekusaidia kwa ushindi wake na kwa waumini.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Ad-Durul-Manthur Juz. 3, Uk. 185.

318.

256

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 256

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika wale walioamini na wakahama, na wakapigania dini ya Mwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao, na wale waliowapa mahala pa kukaa na wakainusuru, hao ndio marafiki wao kwa wao.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:72).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alifunga udugu baina ya Ansari na Muhajirina, hivyo akaweka udugu baina ya Hamza bin Abdul-Muttalib na Zayd bin Harith, baina ya Umar bin al-Khattab na Maadh bin Áfrau, baina ya Zubair bin al-Áwwam na Abdullah bin Mas’?d, baina ya Abu Bakr na ?alha bin Abdullah, baina ya Abdurahman bin Awfi na Sa’d bin Rabi’u. na akawaambia masahaba zake wengine fungeni udugu, nami ndugu yangu ni huyu, yaani Ali bin Abu Talib. Waislamu wakaendelea katika hali hiyo mpaka ikateremka Aya hii.319

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1).

Abdullah bin Ahmad bin Hanbal katika Zawaidul-Musnad, na Abu Shaikh Ibnu Mardawayhi, wameandika kutoka kwa Ali (a.s.)   Ad-Durul-Manthur Juz. 3 Uk. 205.

319.

257

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 257

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kwamba alisema: Zilipoteremka kwa Mtume Aya kumi za mwanzo wa Sura Baraa alimwita Abu Bakr ili akawasomee wakazi wa Makka. Kisha akaniita na kusema: “Mdiriki Abu Bakr na popote utakapomkuta chukua Sura kutoka kwake. Abu Bakr akarejea kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kuna chochote kimeteremka kunikhusu?” Akasema: “Hapana lakini Jibril amenijia na kuniambia: Hapasi kufikisha kwa niaba yako ila wewe mwenyewe au mtu kutokana na wewe.” Ibnu Abu Shayba, Ahmad, Tirmidhi, Abu Shaikh na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Anas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma Abu Bakr akiwa na Sura Baraa, kisha akamrejesha na kumwambia: “Haipasi yeyote yule kuibalighisha hii ila mtu kutoka katika ndugu zangu.” Ndipo akamwita Ali na kumkabidhi Sura hiyo. Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Sa’d bin Abi Waqqas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr aende na Sura Baraa kuwasomea wakazi wa Makka, kisha akamtuma Ali nyuma yake akaichukue toka kwake, basi Abu Bakr akahisi hali fulani moyoni mwake. Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Hafikishi kwa niaba yangu ila mimi mwenyewe au mtu kutoka katika ndugu zangu.” Ibnu Habban na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Said al-Khudri kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma Abu Bakr akaifikishe Sura Baraa kwa niaba yake, baada ya kumtuma alimpeleka Ali bin Abu Talib (a.s.) akamwambia: “Ewe Ali! Hakika hafikishi kwa niaba yangu ila mimi mwenyewe au wewe.” Kisha akamwambia amfuate akiwa juu ya ngamia wake al-Adhbu, akaenda mpaka akamkuta Abu Bakr na akaichukua Sura Baraa toka kwake. Abu Bakr akaja kwa Mtume (s.a.w.w.) na hali kaingiwa na khofu kutokana na hilo kwamba huenda kuna chochote kimeterem258

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 258

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

shwa kumhusu yeye. Alipofika kwa Mtume akasema: “Nimefanya nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Akasema: “Hafikishi kwa niaba yangu asiyekuwa mimi au mtu kutokana na mimi.”320 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:19).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kususu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu” kwamba alisema: Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.). Ibnu Jariri ameandika kutoka kwa Muhammad Ka’b al-Qardhiy kwamba alisema: Talha bin Shayba, Abbas na Ali bin Abu Talib kila mmoja alijigamba. Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba funguo zimo mikononi mwangu.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mgawa maji na msimamizi wake.’ Ali akasema: ‘Sijui mtasema nini. Bila shaka nimeswali kabla ya mtu yeyote na mimi ndiye   Hii yenyewe ni dalili tosha kwamba Abu Bakr hastahiki kuwa mwakilishi wa Mtume (s.a.w.w.) katika jambo kama hili, lakini cha kushangaza yeye mwenyewe alijitangaza kuwa ni Khalifa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu bila dalili wala tamko la Mtume au la Qur’ani. Na hali katika Umma yupo aliye mbora kushinda yeye naye si mwingine ni Ali bin Abu Talib.

320.

259

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 259

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mwanajihadi.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wameridhia kuwa pamoja na wanaobakia nyuma, na nyoyo zao zimepigwa muhuri, kwa hiyo hawafahamu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:87).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Sa’d bin Abi Waqqas kwamba Ali bin Abu Talib alitoka na Mtume (s.a.w.w.) mpaka wakafika ThaniyatulWida’u akikusudia kwenda Tabuk na hali Ali akilia na akisema: “Unaniacha pamoja na wanaobaki nyuma.” Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Hivi huridhii kuwa wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa ila ni kwamba hakuna unabii baada yangu.”321 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Muhajiri na ­Ansari...” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:100).

Ibnu al-Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Muhajiri ni: Ali, Salman na Ammar bin Yasir.”   Ad-Durul-Manthur Juz. 3 Uk. 266.

321.

260

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 260

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:119).

Ibnu al-Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.” Kwamba alisema: “Yaani kuweni pamoja na Ali bin Abu Talib.” Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Abu Ja’far kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Na kuweni pamoja na wakweli.” Kwamba alisema: “Yaani kuweni pamoja na Ali bin Abu Talib (a.s.).” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hayo ni kwa sababu haiwafikii kiu wala taabu wala njaa katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawakanyagi njia iwachukizayo makafiri.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:120).

Al-Hakim na Ibnu al-Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alitoka kwenda kwenye moja ya vita na akamwacha Ali kama makamu wake kwa ndugu zake. Ali akasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Unaniacha Maquraishi watasema nini, watasema amemtelekeza binamu yake mapema mno na amemwengua. Nami naona ni bora nitafute fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu nimemsikia Mwenyezi Mungu akisema: “wala hawakanyagi njia iwachukizayo 261

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 261

2/14/2018 12:12:02 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

makafiri.” Mtume akasema: “Ama kauli yako: Maquraishi watasema nini, watasema amemtelekeza binamu yake mapema mno na amemwengua. Bila shaka walishasema: Hakika mimi mchawi na kuhani. Wakasema: Hakika mimi mwongo. Hivyo una kigezo chema kwangu, huridhii kuwa wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa ila ni kwamba hakuna Nabii baada yangu.”

SURAT YUNUS Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kwa fadhili za Mwenyezi Mungu na kwa rehema zake basi wafurahi, hiyo ni bora kuliko wanavyovikusanya.” (Qur’ani Tukufu Sura Yunus; 10:58).

Al-Khatib na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Sema: Kwa fadhili za Mwenyezi Mungu” fadhila ni Nabii (s.a.w.w.). “na kwa rehema zake” rehema zake ni Ali bin Abu Talib.

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:17).

Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndiye al262

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 262

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

iye na dalili itokayo kwa Mola Wake, na mimi ndiye shahidi ­atokaye kwake.” Ibnu Abi Hatim, Ibnu Mardawayhi na Abu Naim katika alMa’rifa wameandika kutoka kwa Ali bin Abu Talibi kwamba: Alisema Ali (a.s.): “Hakuna mtu yeyote miongoni mwa makuraishi ila kuna sehemu ya Qur’ani ilishuka kwa ajili yake.” Ndipo mtu mmoja akamwambia: “Ni ipi iliyoteremka kwa ajili yako?’’Ali akasema: “Hivi hausomi Sura Hud: “Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola Wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndiye aliye na dalili itokayo kwa Mola Wake, na mimi ndiye shahidi atokaye kwake.” Ibnu Mardawayhi ameiandika kwa njia nyingine kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Aliye na dalili itokayo kwa Mola Wake ni mimi, na shahidi atokaye kwake ni Ali (a.s.).”

SURAT AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani za mizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina na isiyochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:4). 263

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 263

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Al-Hakim ameiandika na Ibnu Mardawayhi amesema ni hadithi sahihi, kutoka kwa Jabir kwamba alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: “Ewe Ali! Watu wanatokana na miti tofauti. Na mimi na wewe tunatokana na mti mmoja.” Kisha Mtume (s.a.w.w.) akasoma: “Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani za mizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina na isiyochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale.”322 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” (Qur’ani Tukufu Sura ­ar-Ra’d; 13:7). Ibnu Jariri, Ibnu Mardawayhi, Abu Naim katika al-Ma’rifa, Daylamiy, Ibnu Asakir na Ibnu Najjar wameandika kwamba: Ilipoteremka: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake na kusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji.’ Kisha akaashiria mkono wake kwenye bega la Ali bin Abu Talib na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji. Kupitia kwako wataongoka wenye kutaka kuongoka baada yangu.” Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Abi Barzati al-Aslamiy kwamba alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema: “Hakika wewe ni mwonyaji tu.” Akaweka mkono wake juu ya kifua chake. Kisha akauweka juu ya kifua cha Ali huku akisema: “Kila kaumu ina wa kuwaongoza.” Ibnu Mardawayhi na al-Dhiyau katika al-Mukhtar wameandika kutoka kwa ibnu Abbas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Mwonyaji ni mimi na Mwongozaji ni Ali bin Abu Talib (a.s.).”   Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 44.

322.

264

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 264

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Abdullah bin Ahmad katika Zawaidul-Musnad, Ibnu Abi Hatim, Tabaraniy katika al-Awsat, al-Hakim na wamesema ni hadithi sahihi. Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakiri, hao wote wameiandika kutoka kwa Ali bin Abu Talib kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndiye Mwonyaji, na mimi ndiye Mwongozaji.”323

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Utukufu ni wa yule ambaye alimpeleka mja wake usiku kutoka Msikiti Mtukufu mpaka msikiti wa mbali ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumwonyeshe baadhi ya dalili zetu. Hakika yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:1).

Tabarani ameandika kutoka kwa Aisha kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nilipopelekwa mbinguni niliingizwa peponi, nikaona mti mmoja miongoni mwa miti ya peponi ambao sijaona peponi mzuri kushinda wenyewe, wala wenye majani yang’aayo kushinda wenyewe, na wala wenye matunda matamu kushinda wenyewe, nikachuma moja ya matunda yake na nikala, ndipo mbegu za uzazi zikapatikana katika uti wa mgongo wangu kutokana na tunda hilo, nilipoteremka ardhini nilimwingilia   Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 45

323.

265

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 265

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Khadija na ndipo akashika mimba ya Fatima (a.s.), hivyo niwapo na hamu ya kunusa harufu ya pepo hunusa harufu ya Fatima.”324 Al-Hakim ameandika kutoka kwa Sa’d bin Waqqas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Jibril (a.s.) aliniletea pera nikalila usiku ambao nilipelekwa miraji, na ndipo Khadija akashika mimba ya Fatima, hivyo niwapo na hamu ya harufu ya peponi huinusa shingo ya Fatima.”325 Ibnu Adiy na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Anas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Nilipopelekwa Miiraji niliona nguzo ya Arshi imeandikwa: Hapana Mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah na Muhammad ni Mtume wa Allah nimempa nguvu kupitia Ali.”326 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:26).

Al-Bazzar, Abu Ya’la, Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Fatima na kumkabidhi Fadak.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 153. Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Binti yangu Fatima ni Hurulaini wa kibinadamu, hajawahi kupata hedhi wala nifasi. Na hakika Mwenyezi Mungu alimpa jina la Fatima (Mwachanishi) kwa sababu Mwenyezi Mungu amemwepusha dhidi ya moto yeye na vipenzi vyake.” Tazama kitabu Kanzul-Ummal Juz. 12, Namba 3422. 325.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 153. 326.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 153. 324.

266

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 266

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Ilipoteremka: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu alimpa Fatima Fadak.327

SURAT MARYAM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na amani iko juu yake siku aliyozaliwa na siku atakayofariki, na siku atakayofufuliwa hai.” (Qur’ani Tukufu Sura Maryam; 19:15). Ahmad, Abu Ya’la, Ibnu Habban, Tabarani, al-Hakim na Dhayau wameandika kutoka kwa Abu Said kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hasan na Husain ni mabwana wawili wa vijana wa peponi, ila kwa wana wawili wa khalati: Isa bin Mariam na Yahya bin Zakariya.”328 Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Qurrat kwamba alisema: Mbingu haikuwahi kumlilia yeyote ila Yahya bin Zakariya na Husain bin Ali, na wekundu wake ndio kulia kwake.329 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” (Qur’ani Tukufu Sura Maryam; 19:96).

Ibnu Mardawayhi na Daylamiy wameandika kutoka kwa alBarau kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali bin Abu Talib: “Ewe Ali sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwako na niwekee mapenzi Kwako, na ni  Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 177.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 262. 329.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 264. 327. 328.

267

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 267

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wekee mapenzi katika nyoyo za waumini.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” iliteremka kwa ajili ya Ali (a.s.).330 Tabarani na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.): “Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” yaani mahaba katika nyoyo za waumini.”

SURAT TWAHA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Akasema: Ee Mola wangu! Nipanulie kifua changu. Na unifanyie wepesi kazi yangu. Na ufungue fundo katika ulimi wangu. Wapate kufahamu kauli yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Harun. “ (Qur’ani Tukufu Sura Twaha; 20:25-30).

Salfiy ameandika katika Tuyuriyat kutoka kwa Abu Jafar Muhammad bin Ali kwamba alisema: “Ilipoteremka: “Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Harun. Nitie nguvu kupitia yeye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa juu ya kilele cha mlima, kisha akamwomba Mola wake kwa kusema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nitie nguvu kupitia ndugu yangu Ali. Mwenyezi Mungu akamkubalia ombi hilo.”331   Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 287.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 295. Kauli hiyo inaungwa mkono na kauli ya Mtume:

330. 331.

268

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 268

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-HAJJ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka Mwenyezi Mungu atawaingiza wale walioamini na kufanya vitendo vizuri katika Bustani zipitazo mito chini yake, kwa hakika Mwenyezi Mungu hufanya atakavyo.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hajj; 22:14).

Abdu bin Hamid ameandika kutoka kwa Lahiq bin Hamid kwamba alisema: Iliteremka: “Bila shaka Mwenyezi Mungu atawaingiza wale walioamini na kufanya vitendo vizuri……na kuongozwa kwenye njia ya Mwenye kuhimidiwa.” (Sura Twaha: 14 - 24) kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, Hamza, na Ubaydah bin al-Harith.332 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Mwenyezi Mungu huchagua Wajumbe miongoni mwa Malaika na miongoni mwa watu, kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hajj; 22:75).

Al-Baghawi ameandika katika Mu’jam, al-Barudiy, Ibnu Qaniu, Tabarani na Ibnu Asakir, wote wameandika kutoka kwa Zayd bin Abi Awfa kwamba alisema: “Niliingia kwa Mtume wa Mwenyezi Mun“Wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa ila ni kwamba hakuna Nabii baada yangu.” Ambayo inatamka wazi kwamba Ali ndiye Khalifa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu na ndiye Wasii, Waziri na Mwenye mamlaka baada yake. Hivyo kila aliyemwondoa katika nafasi yake ni mnyang’anyi. Kwa rejea zaidi rejea kitabu al-Aqdu At-Thamin cha Imam Shawkaniy. 332.   Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 349. 269

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 269

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

gu katika Msikiti wa Madina, akaanza kusema yuko wapi bin fulani? Aliendelea kuwaita mpaka wakakusanyika kwake, kisha akasema: “Mimi nataka kuwasimulieni hadithi hivyo ihifadhini na muizingatie na mje kuwasimulia wale watakaokuja baada yenu: Hakika Mwenyezi Mungu aliteua kutoka miongoni mwa viumbe Wake, viumbe maalumu: “Mwenyezi Mungu huchagua Wajumbe miongoni mwa Malaika na miongoni mwa watu,” viumbe atakaowaingiza peponi. Na mimi nachagua toka miongoni mwenu ambaye nimependa kumchagua, na ninaweka udugu baina yenu kama Mwenyezi Mungu alivyoweka udugu baina ya Malaika.” Kisha akamwita Sa’d bin Abi Waqqas na Ammar bin Yasir, akasema: “Ewe Ammar! Kundi ovu litakuuwa.” Kisha akaweka udugu baina yao. Ndipo akamwita Abu Dardau na Salman al-Farsiy na kusema: “Ewe Salman! Wewe ni katika watu wa nyumba.” Kisha akaweka udugu baina yao. kisha akatizama nyuso za masahaba zake akasema: “Furahini na tulieni.” Ali akasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Roho yangu imenitoka na mgongo wangu umevunjika pale nilipokuona umewafanyia hayo sahaba zako na kuniacha, basi ikiwa ni kutokana na ghadhabu yako juu yangu basi onyo na heshima ni miliki yako. Mtume akasema: “Naapa kwa yule Ambaye amenituma kwa haki, sikukuacha ila ili uwe kwa ajili yangu mwenyewe, kwani wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa, na ni mrithi wangu.” Ali akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nitarithi nini toka kwako? Akasema: “Kile walichorithi warithi wa Manabii kabla yako: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Nabii wao, nawe pamoja na Fatima mtakuwa nami katika kasri la peponi, nawe ni ndugu yangu na rafiki333 yangu.” Kisha Mtume akasoma Aya hii: “Ndugu wakikaa juu ya viti kwa kuelekeana.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hijr; 15:47).   Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 371.

333.

270

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 270

2/14/2018 12:12:03 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AN-NUR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Katika nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameruhusu ziinuliwe na kutajwa humo jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nur; 24:36).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Anas bin Malik na Burayda kwamba walisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisoma Aya hii: “Katika nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameruhusu ziinuliwe na kutajwa humo jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni.” Akasimama mtu mmoja na kumuuliza: “Ni nyumba zipi hizi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Akasema: “Nyumba za Manabii.” Abu Bakr akasimama na kusema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nyumba hii ni miongoni mwazo, nyumba ya Ali na Fatima? “ Akajibu: “Ndio ni miongoni mwazo bali ndio iliyo bora kuliko nyingine.”

SURAT AS-SAJDA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa!” (Qur’ani Tukufu Sura as-Sajda; 32:18). Abu al-Faraj al-Asbahani ameandika katika kitabu al-Aghaniy, al-Wahidiy, Ibnu Adiy, Ibnu Mardawayhi, al-Khatib na Ibnu Asakir, wamepokea kwa njia tofauti kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Walid bin Uqbah bin Abu Muit alimwambia Ali: ‘Mimi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye meno makali kuliko wewe na shujaa kuliko wewe 271

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 271

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

na hodari wa mapambano kuliko wewe.’ Ali akamjibu: ‘Nyamaza, bila shaka wewe ni fasiki.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.” Yaani Muumini ni Ali na Fasiki ni Walid bin Uqbah bin Abu Muit.334 Ibnu Is’haq na Ibnu Jariri wameandika kutoka kwa Atau bin Yasar kwamba alisema: Iliteremka Madina ikimuhusu Ali bin Abu Talib na Walid bin Uqbah. Kulikuwa na mzozo baina ya Walid na Ali, Walid bin Uqbah akamwambia Ali: ‘Mimi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye meno makali kuliko wewe na shujaa kuliko wewe na hodari wa mapambano kuliko wewe.’ Ali akamjibu: ‘Nyamaza, bila shaka wewe ni fasiki.’ Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa!”335 Ibnu Abi Hatim ameandika kutoka kwa Abdurahman bin Abi Layla kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa,” kwamba alisema: Iliteremka ikimhusu Ali bin Abu Talib – yaani ndio Muumini, na Walid bin Uqbah – yaani Fasiki.336 Ibnu Mardawayhi, al-Khatib na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa,” kwamba alisema: Muumini ni Ali bin Abu Talib. Na Fasiki ni Walid bin Uqbah bin Abu Muit. Hiyo inatokana na sababu iliyokuwa baina yao, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha aya hiyo.337

SURAT AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Nabii ana mamlaka zaidi kwa waumini kuliko nafsi zao…” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:6).   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178.   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178. 336.   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178. 337.   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178. 334. 335.

272

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 272

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Abi Shayba, Ahmad na Nasai wameandika kutoka kwa Burayda kwamba alisema: “Nilishiriki vita pamoja na Ali huko Yaman, nikaona kwake ambalo sikupendezwa nalo, nilipofika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) nilimtaja Ali na nikaanza kumshusha hadhi, ghafla nikaona uso wa Mtume wa Mwenyezi Mungu umebadilika, akaniambia: “Ewe Buraydah! Mimi si mwenye mamlaka kwa waumini kuliko nafsi zao?” nikasema ndio ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: “Basi yule ambaye mimi ni mwenye mamlaka juu yake Ali ni mwenye mamlaka juu yake.”338 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na Mwenyezi Mungu amewatosheleza Waumini katika vita…” (Qur’ani Tukufu Sura alAhzab; 33:25). Ibnu Abi Hatim, Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ibnu Masu’d kwamba alikuwa akisoma hivi: “Na Mwenyezi Mungu amewatosheleza Waumini katika vita kupitia Ali bin Abu Talib.”339 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Ibnu Jariri, Ibnu Mundhir, Ibnu Abi Hatim, Tabaraniy na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ummu Salama mke wa Mtume (s.a.w.w.) kwamba: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa nyumbani kwake ameketi juu ya kitanda na hali kajifunika kishamia cha Khaibari, ndipo akaja Fatima akiwa na chungu che  Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 182.   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 192.

338. 339.

273

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 273

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nye uji na kuingia nacho kwa Mtume. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamwambia mwite mumeo na wanao Hasan na Husain. Akawaita na ghafla walipokuwa wakila iliteremka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Mtume akachukua sehemu iliyozidi ya kishamia chake na kuwafunika. Kisha akatoa mkono wake ndani ya kishamia akaunyoosha mbinguni na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu na watu makhsusi kwangu, hivyo waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.” Alisema hivyo mara tatu. Nikaingiza kichwa chumbani kwa Mtume na kumwambia: Je na mimi ni pamoja nanyi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Hakika wewe utaelekea katika kheri.” Alisema mara mbili.340 Tabarani ameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema: Fatima alikuja kwa baba yake akiwa amemletea uji uliokuwa ndani ya bakuli lake, akauweka mbele yake. Mtume akasema: “Yupo wapi mwana wa ami yako?” akasema yupo nyumbani. Akamwambia nenda ukamwite yeye na wanao. Akaja na wanae akiwa amemshika kila mmoja mkono na huku Ali akitembea nyuma yao, mpaka walipoingia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), akamkalisha kila mmoja kati yao (Hasan na Husein) katika paja lake, Ali akakaa kuliani kwake na Fatima kushotoni kwake. Kisha kikachukuliwa kishamia kilichokuwa kimetandikwa juu ya kitanda chumbani kwangu. Tabarani ameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema kumwambia Fatima (a.s.): Niitie mumeo na wanao. Akawaita na ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawafunika kishamia cha Fadaki, kisha akaweka mkono wake juu yao na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 198.

340.

274

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 274

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ndio Aali Muhammadi, hivyo weka Sala zako na baraka zako juu ya Aali Muhammadi kama ulivyoziweka juu ya Aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.” Ummu Salama anasema: Nikainua kishamia ili niingie pamoja nao, lakini akakivuta toka mikononi mwangu na kuniambia: Hakika wewe uko kwenye kheri. 341 Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema: Aya hii iliteremka nyumbani kwangu: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” na nyumbani kulikuwa na watu saba: Jibril, Mikail, Ali, Fatima, Hasan na Husein, nami nikiwa nimesimama mlangoni. Nikamwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu je mimi sio katika AhlulBait? Akasema: “Hakika wewe upo katika kheri, wewe ni miongoni mwa wakeze Mtume.” Ibnu Mardawayhi na Khatib wameandika kutoka kwa Said alKhudriy kwamba alisema: Ilikuwa ni siku ya Ummu Salama mama wa waumini, ndipo Jibril akateremka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu akiwa na Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.,” Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaita Hasan, Husein, Fatima na Ali, akawakumbatia na kuwafunika nguo ilihali kukiwa na pazia kati yao na Ummu Salama, kisha akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu, hivyo waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.” Ummu Salama akasema: Na mimi ni pamoja nao ewe Nabii wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Wewe una nafasi yako na bila shaka wewe upo katika kheri.” Tirmidhiy ameandika na kusema kwamba ni sahihi, Ibnu Jariri, Ibnu Mundhir, al-Hakim, Mardawayhi na Bayhaqi katika Sunnani   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 198.

341.

275

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 275

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Yake, wote wameandika kwa njia tafauti kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema: “Nyumbani kwangu ndimo iliteremkia: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa,” na hali ndani ya nyumba alikuwemo Fatima, Ali, Hasan na Husein, Mtume wa Mwenyezi Mungu akawafunika kishamia alichokuwa amejitanda, kisha akasema: “Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu, hivyo waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”342 Ibnu Jarir, Ibnu Abi Hatim na Tabarani wameiandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa” imeteremka kwa ajili ya watano: Kwa ajili yangu, Ali, Fatima, Hasan na Husein.” Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Muslim, Ibnu Jarir, Ibnu Abi Hatim, na Hakim wameandika kutoka kwa Aisha kwamba alisema: “Siku moja Mtume alitoka akajifunika shuka lililodariziwa na manyoya meusi. Wakaja Hasan na Husain akawafunika, kisha akaja Ali naye akamfunika, kisha akasema: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.’” Ibnu Jarir, Hakim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Sa’d kwamba alisema: Wahyi uliteremka na ndipo akawafunika Ali na Fatima shuka lake, kisha akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio ndugu zangu na Ahlul-Baiti wangu.” Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Ibnu Jarir, Ibnu Mundhir na Tabaraniy wameandika kutoka kwa Wathila bin Asqaf kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuja kwa Fatima akiwa pamoja   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 198.

342.

276

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 276

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

na Hasan na Husain na Ali, akaingia kisha akamsogeza Ali na ­Fatim na kuwakalisha mbele yake, na akawakalisha Hasan na Husein kila mmoja wao juu ya paja lake, kisha akawafunika shuka yake na hali mimi nikiwa nimewapa mgongo, kisha akasoma Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Tirmidhi na amesema ni hadithi hasan, Ibnu Jarir, Ibnu Mundhir, Tabaraniy, Hakim na amesema ni hadithi sahihi, na Ibnu Mardawayhi, wote wameandika kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akipita mlangoni kwa Fatima atokapo kwenda kuswali Sala ya Alfajri na husema: “Sala enyi Ahlul-Baiti, Sala enyi Ahlul-Baiti Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”343 Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: “Ali alipomuoa Fatima, Mtume alikwenda mlangoni kwake siku arobaini kila asubuhi, na alikuwa akisema: “Asalamu Alaykum Ahlul-Baiti Warahmatullah Wabarakatuhu. Mwenyezi Mungu akurehemuni. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa. Mimi ni mwenye kufanya vita na yule mwenye kuwapigeni vita nyinyi na ni mwenye amani na yule mwenye kufanya amani nanyi.” Tabarani ameandika kutoka kwa Abu Hamrau kwamba alisema: “Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu muda wa miezi sita akija kwenye mlango wa Ali na Fatima na kusema: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”   Ad-Durul-Manthur Juz. 5, Uk. 199.

343.

277

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 277

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Tulimshuhudia Mtume muda wa miezi tisa akija kila siku mlangoni kwa Ali bin Abu Talib wakati wa kila Sala na kusema: “Asalamu Alaykum Ahlul-Baiti Warahmatullah Wabarakatuhu. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa. Mwenyezi Mungu akurehemuni.” Kila siku mara tano. Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na ulipomwambia yule ambaye Mwenyezi Mungu amemneemesha na wewe umemneemesha.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:37).

Bazzar, Ibnu Hatim, Hakim, na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Usama bin Zayd kwamba alisema: Abbas na Ali bin Abu Talib walikwenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumwambia: Tumekuja ili utueleze ni yupi umpendaye sana kati ya ndugu zako? Akasema: “Nimpendaye sana kati ya ndugu zangu ni Fatima.” Wakamwambia hatuulizi kuhusu Fatima. Akasema: “Ni Usama bin Zayd ambaye Mwenyezi Mungu amemneemesha nami nimemneemesha.” Ali bin Abu Talib akasema kisha nani ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Kisha wewe kisha Abbas.” Abbas akasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Hivi umemuweka ami yako mwisho!” Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Hakika Ali alikutangulia kwa kuhama.”344 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Ad-Durul-Manthur Juz. 5, Uk. 201

344.

278

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 278

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).

Said bin Mansur, Abdu bin Hamid, Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ka’b bin Ajrah kwamba alisema: Ilipoteremka: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu,” tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”345 Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Ka’b bin Ajrah kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii nilisimama na kumwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:   Ad-Durul-Manthur Juz. 5, Uk. 216.

345.

279

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 279

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim.’” Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Yunus bin Khabab kwamba alisema: “Faris alitutolea khutba akasema: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” Hakika amenipa habari yule aliyemsikia Ibnu Abbas akisema: Hivyo ndivyo ilivyoteremka, nao (masahaba) walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomsalia Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’” Abu Daud, Ibnu Mardawayhi na al-Bayhaqiy katika Sunnan yake, wameandika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema: Mtume wa 280

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 280

2/14/2018 12:12:04 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Anayependa alingane sawasawa na kipimo kamili basi anapotusalia sisi Ahlul-Baiti aseme: Ewe Mwenyezi Mungu msalie Muhammad Nabii, yeye na dhuria wake na Ahlul-Baiti wake kama ulivyowasali Aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.” Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Abdu bin Hamid, Bukhari, Nasai, Ibnu Majah, na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Said al-Khudriy kwamba alisema: Tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad mja Wako na Mtume Wako kama ulivyowasalia aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim.’”346 Abdu bin Hamid, Nasai na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema: Walimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni jinsi gani tutakavyokusalia? Akasema: “Semeni:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad na aali Muhammad, na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomsalia na kumbariki Ibrahim na aali Ibrahim juu ya walimwengu, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’” Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema: “Tulisema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua   Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 218

346.

281

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 281

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

namna ya kukutolea salamu, basi ni vipi tutakavyokusalia? Akasema: “Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Weka rehema na amani, na baraka Zako juu ya Aali Muhammad kama ulivyoziweka juu ya Aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.” Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: Nilisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni namna gani tutakusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu msalie Muhammadi na Aali Muhammad kama ulivyomsalia Ibrahim na Aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.”

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23). Abu Naim na Daylamiy wameandika kwa njia ya Mujahid kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu, mnilindie heshima yangu kwa ndugu zangu na muwapende kwa ajili yangu.”347 Ibnu Mundhir, Ibnu Abi Hatim na Tabaraniy wameandika kwa njia ya Said bin Jubair kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni nani karaba zako hawa ambao tumewajibishwa kuwapenda? Akasema (s.a.w.w.): “Ali, Fatima na watoto wao.” Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Abu Daylam kwamba alisema: Alipoletwa Ali bin Husein bin Ali bin Abu Talib (a.s.) na hali ni mateka na kusimamishwa katika barabara kuu ya Damascus ali  Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 7

347.

282

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 282

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

simama mzee mmoja kati ya watu wa Sham, akasema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye amewauwa na kuwang’oeni na kung’oa mzizi wa fitina.” Ali bin Husein akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu ndio. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’ Akajibu hapana. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...”’ Mzee akasema: ‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’ Muslim, Tirmidhiy na Nasai wameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nawakumbusheni Mwenyezi Mungu kuhusu Ahlul-Baiti wangu, yaani Ali, Fatima, Hasan na Husein.” Ibnu Adiy ameandika kutoka kwa Abu Said kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Atakayetuchukia sisi Ahlul-Baiti basi ni mnafiki.” Tirmidhiy ameandika na kusema ni hadithi sahihi, na Ibnu alAnbariy katika al-Masahifu wameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuwaachia kati yenu vile ambavyo lau mkishikamana navyo katu hamtapotea baada yangu, kimojawapo ni kitukufu kuliko kingine: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka toka mbinguni hadi ardhini. Na kingine ni kizazi changu watu wa nyumba yangu, na havitoachana mpaka vinikute kwenye hodhi, basi angalieni ni jinsi gani mtakavyobaki navyo.” Tabarani ameandika kutoka kwa Hasan bin Ali kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hatatuchukia yeyote wala kutuhusudu ila ataadhibiwa Siku ya Kiyama kwa mjeledi wa moto. 283

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 283

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ahmad bin Habban na al-Hakim wameandika kutoka kwa Abu Said kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake kwamba hakuna mtu yeyote atakayetuchukia sisi Ahlul-Baiti ila ni lazima Mwenyezi Mungu atamwingiza motoni.

SURAT MUHAMMAD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na kama tungependa tungekuonyesha hao na ungewatambua kwa alama zao, na hasa utawafahamu kwa namna ya usemi wao, na Mwenyezi Mungu anavijua vitendo vyenu.” (Qur’ani Tukufu Sura Muhammad; 47:30).

Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “….na hasa utawafahamu kwa namna ya usemi wao, na Mwenyezi Mungu anavijua vitendo vyao”: ni kwa kule kumchukia kwao Ali bin Abu Talib (a.s.).348 Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba alisema: Hatukuwa tunawafahamu wanafiki zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu ila kwa kule kumchukia kwao Ali bin Abu Talib (a.s.).349

SURAT AR-RAHMAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 66.   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 66.

348. 349.

284

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 284

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Amezikutanisha bahari mbili. Baina yao kuna kizuizi haziingiliani. Basi nyinyi wawili mnakataa neema gani ya Mola wenu Mlezi? ­Katika hizo mbili hutoka lulu na marijani.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Rahman; 55:19-22).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili.” Ali na Fatima kati yao kuna kizuizi hawaingiliani, kwani Mtume alisema: “Hutoka kwao hao wawili lulu na marijani, Hasan na Husein.”350 Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Anas bin Malik kwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili”: “Ni Ali na Fatima, hutoka kwao hao wawili lulu na marijani, ambao ni Hasan na Husein.”

SURAT AL-WAQIA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na nyinyi mtakuwa namna tatu. Basi watu wenye kheri, watakuwa namna gani wenye kheri. Na watu wenye shari, watakuwa namna gani wenye shari. Waliotangulia ndio waliotangulia.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Waqia’; 56:7-10).   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 142.

350.

285

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 285

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Waliotangulia ndio waliotangulia” kuwa iliteremka kumuhusu Ali bin Abu Talib, na kila mtu miongoni mwao ni mtangulizi wa umma wake, na Ali ndiye mbora wao katika kutangulia.351 Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Waliotangulia ndio waliotangulia”: Yoshua bin Nun ndiye aliyetangulia kumwamini Musa, Muumini wa Aali Yasin ndiye aliyetangulia kumwamini Isa, na Ali bin Abu Talib ndiye aliyetangulia Muhammad (s.a.w.w.).

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Abdu bin Hamid, Ibnu Mundhir na Ibnu Abi Hatim wameandika kutoka kwa Mujahid kwamba alisema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib, yeye alitoa sadaka ya dinari kisha akasema siri na Mtume (s.a.w.w.) na alimuuliza mambo kumi, ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.).”352   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 154.   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 185.

351. 352.

286

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 286

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Said bin Mansur ameandika kutoka kwa Mujahid kwamba alisema: “Ilikuwa anayesema siri na Mtume ni lazima atoe sadaka ya dinari, na wa awali aliyetekeleza hilo ni Ali bin Abu Talib, kisha ndipo ikateremka ruhusa: “…..na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” Abdu bin Hamid ameandika kutoka kwa Salmah bin Kuhayli kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu”: kuwa wa kwanza aliyeifanyia kazi ni Ali bin Abu Talib, kisha ikafutwa.

SURAT AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni m ­ linzi wake, na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:4). Ibnu Abi Hatim ameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema kuhusu “Na waumini wema’’ kwamba ni Ali bin Abu Talib.353 Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Asmau binti Umaysi kwamba alisema: “Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: “Na waumini wema’’ ni Ali bin Abu Talib.’” Said bin Mansur, Abdu Hamid na Ibnu Mundhir wameandika kutoka kwa Alau bin Ziyad kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na waumini wema’’ ni Ali bin Abu Talib (a.s.).

SURAT AL-HAQQA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Haqqa; 69:12).   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 244.

353.

287

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 287

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Said bin Mansur, Ibnu Jarir, Ibnu Mundhir, Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Makhul kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii: “…..na sikio lisikialo lisikie,” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nilimwomba Mwenyezi Mungu alifanye hivyo sikio la Ali.’’ Makhul anasema: Ali alikuwa akisema: “Sikusikia kitu chochote toka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kisha nikakisahau.”354 Ibnu Jarir, Ibnu Abi Hatim, al-Wahidiy, Ibnu Mardawayhi, Ibnu Asakir na Ibnu Najari wameandika kutoka kwa Burayda kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ameniamuru nikusogeze karibu nisikutenge mbali, na nikuelimishe nawe usikie vilivyo. Na Mwenyezi Mungu amehakikisha unasikia vilivyo.” Ndipo ikateremka Aya hii. Abu Naim ameandika ndani ya al-Hilyah kutoka kwa Ali kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ewe Ali! Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ameniamuru nikusogeze karibu na nikuelimishe nawe usikie vilivyo, ndipo ikateremka Aya hii: “…..na sikio lisikialo lisikie.” hivyo wewe ndio sikio lisikialo vilivyo elimu yangu.”

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9). Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na huwalisha chakula masikini na ya  Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 360.

354.

288

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 288

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

tima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” Kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu ­Talib na Fatima binti ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.).355

SURAT AL-BAYYINA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Bayyina; 98:7).

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Jabir bin Abdillah kwamba alisema: Tulikuwa kwa Mtume na ndipo ghafla akaja Ali bin Abu Talib, Mtume akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, hakika huyu na Shia wake ndio wenye kufuzu Siku ya Kiyama.” Ndipo ikateremka: “Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.” Basi masahaba wa Mtume wakawa atokeapo Ali husema: Amekuja kiumbe bora kushinda wote.356 Ibnu Adi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Ilipoteremka: “Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.” Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema kumwambia Ali: “Ni wewe na Mashia wako, Siku ya Kiyama mtakuja na hali mmeridhia nanyi mmeridhiwa.” Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu aliniambia: “Hivi hujasikia kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.” Ni wewe na Mashia wako, ahadi yangu mimi na nyinyi ni kukutana kwenye Hodhi.   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 299.   Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 379.

355. 356.

289

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 289

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AN-NASR Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Utakapofika msaada wa­ Mwenyezi Mungu na ushindi.” (Qur’ani Tukufu Sura anNasr; 110:1). Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alipofika kutoka Vita vya Hunayni ilimteremkia Aya hii, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ewe Ali bin Abu Talib! Na ewe Fatima binti Muhammad! Msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi vimefika, na nimeona watu wakiingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi.”357 Tabarani ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alipofika kutoka Vita vya Hunayni ilimteremkia Aya hii: “Utakapofika msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi.” ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ewe Ali bin Abu Talib! Na ewe Fatima binti Muhammad! Msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi vimefika na nimeona watu wakiingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi. Ametakasika Mola wangu Mlezi na kila sifa njema ni Yake na ninamuomba sana maghufira, hakika Yeye ni Mwenye kupokea toba. Ewe Ali! Lau ningekuwa namweka yeyote awe khalifa baada yangu basi yeyote asingekuwa na haki (ya ukhalifa huo) kuliko wewe,358 hiyo ni kutokana na ukaribu wako na Uis  Ad-Durul-Manthur Juz. 6, Uk. 407. 1   Nasema: Ni wazi kwamba ziada hii ni nyongeza kutoka kwa wale wenye chuki na Ahlul-Baiti (a.s.), wale ambao kwa juhudi zao zote wamejitahidi kujaribu kuuondoa ukhalifa na uwasii toka kwa Imam Ali na hivyo wakadai kwamba eti Mtume hakuacha Wasii, alifariki bila kuusia. Lakini ukweli ni kama ulivyokwishatambua hapo mwanzo kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliusia ukhalifa kwa Ali na Siku ya Ghadir alimsimika rasmi mbele ya macho ya waumini, na kwa kinywa cha kheri, ulimi wa ukweli na matamshi ya Wahyi akasema: “Yule ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali ni mwenye mamlaka juu yake.”.

357. 358.

290

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 290

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

lamu, ukaribu wako na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), ukwe wako, na kwako ndiko aliko mwanamke bora kushinda wote wa ulimwenguni.”359

Nimemaliza mchakato wa tafsiri hii siku ya tano ya Mfunguo nne wa Mwaka 1421 A.H. katika Jiji la Qum Takatifu.

359.

291

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 291

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA AL-BARUSAWI, INAYOITWA TAFSIR RUHUL-BAYAN FI TAFSIRIL-QUR’AN BISMILAHI RAHMAN RAHIM Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye kurehemu Ukisema: Kuna hekima gani Mwenyezi Mungu kufungua Kitabu chake kwa herufi Bau na si kwa herufi nyingine yeyote? Jibu: Hakika kuna hikma kumi katika hilo la Mwenyezi Mungu ­kufungua Kitabu chake kwa herufi Bau.360 Ya Tisa: Hakika Bau ni herufi iliyokamilika kimaana yenyewe, kwani ni herufi inayoonyesha, mwambatano, msaada na usaidizi. Inakamilisha maana ya tamko lingine pale inapolifanya jina la mbele liwe na Jari na lichukue sifa yake (Bau). Nayo ina hadhi na ­heshima ya juu kutokana na kule kulikamilisha tamko lingine kwa kutoa maana ya Tauhidi na mwongozo, kama alivyoashiria Sayiduna Ali kwa ­kusema: “Mimi ni nukta chini ya herufi Bau.” Hivyo Bau ina cheo cha kuongoza na kuelekeza katika Tauhidi.361

SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tumeichagua ya kumi kwa kuwa ndio inayohusu mazungumzo yetu.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 1 Uk. 7.

360. 361.

292

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 292

2/14/2018 12:12:05 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na ambao huamini uliyoteremshiwa wewe, na yaliyoteremshwa kabla yako, na Akhera wakiisadiki.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:4).

Hakika mwenye kuvuka udhalili wa kizuizi cha dunia hupata utukufu wa kusadikisha mambo ya Akhera na huwa anayaamini bila hata kuyashuhudia kwa macho, hivyo huwa ni mwenye yakini baada ya kuondoa kizuizi, kama alivyosema Amirul-Muuminina Ali (a.s.): “Lau kizuizi kikiondolewa sintazidisha ila yakini.”362 Amesema: Tambua hakika sifa zinazomfanya mtu astahili kulaaniwa ni tatu. Baadhi yao wamesema kwamba Yazid amelaaniwa kutokana na ukafiri wake kuwa mashuhuri na kuenea kwa fedheha ya uovu wake pale alipokufuru pale alipoamuru Husein auwawe. Na pale aliposema huku akinywa pombe: “Ikiwa siku moja itaharamishwa na dini ya Muhammad basi ichukue kupitia dini ya Masihi mwana wa Mariam.” Wameafikiana kwamba inaruhusiwa kuwalaani wale waliomuuwa Husein, au aliyeamuru, au kuruhusu au kuridhia, kama alivyosema Taftazaniy: “Ukweli ni kwamba ridhaa ya Yazid juu ya kumuuwa Husein, furaha yake na kuwadhalilisha kwake Ahlul-Bait (a.s.) ni jambo mashuhuri kimaana ijapokuwa undani wake umetufikia kwa njia ya riwaya zisizokuwa mutawatiri. Sisi hatuna shaka na mambo yake bali na imani yake, laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake na juu ya wasaidizi wake na wafuasi wake. Na Sahib bin Ubbad alipokuwa akinywa maji baridi husema: ‘Kiini cha ubaridi ni katika maji matamu, ambayo hutoa shukurani toka katika kina cha moyo.’ Kisha husema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! Anza upya kumlaani Yazidi.”363 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 1 Uk. 42.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 1 Uk. 179.

362. 363.

293

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 293

2/14/2018 12:12:06 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu, kisha hawafuatishii waliyoyatoa masimbulizi wala udhia, hao wana malipo yao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:262).

Imepokewa kwamba Hasan bin Ali (a.s.) alitamani chakula hivyo akauza kanzu ya Fatima kwa dirhamu sita, muombaji akamwomba naye akampa. Kisha akakutana na mtu anauza ngamia akamnunua kwa mali kauli, kisha akamuuza kwa mtu mwingine, na Hasan alipotaka kumpelekea thamani yake yule aliyemuuzia kwa mali kauli hakumkuta. Ndipo akasimulia kisa kwa Mtume (s.a.w.w.), Mtume akasema: “Ama muombaji alikuwa ni Ridh’wan, Muuzaji alikuwa ni Mikail, ama Mnunuzi alikuwa ni Jibril.” Ndipo ikateremka kauli ya Mwenyezi Mungu: “Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu, kisha hawafuatishii waliyoyatoa masimbulizi wala udhia, hao wana malipo yao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.”364

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsiru Ruhul-Bayan Juz.3 Uk. 419

364.

294

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 294

2/14/2018 12:12:06 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:37).

Mwandishi wa tafsiri hii anasema: “Katika Aya hii kuna dalili juu ya ruhusa ya kuwakirimu mawalii, …….imepokewa kutoka kwa Mtume kwamba Mtume alizidiwa na njaa zama za ukame na ndipo Fatima akamzawadia vipande viwili vya mkate na finyango ya nyama ambapo alimpa kipaumbele kabla ya nafsi yake mwenyewe, lakini Mtume alimrudishia Fatima na kusema: “Chukua ewe mwanangu mpendwa.” Alipofunua bakuli alilikuta limejaa mikate na nyama, ndipo Fatima akapigwa na butwaa na akatambua kuwa kimeteremka toka kwa Mwenyezi Mungu. Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Umetoa wapi hivi?” Akajibu: “Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Mtume akamhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Ambaye amekufanya kifani wa seyida wa wana wa Israel (Mariam).” Kisha Mtume (s.a.w.w.) akawakusanya Ali, Hasan na Husain. Akala Mtume na Ahlul-Baiti wake wote kwa pamoja mpaka wakashiba na chakula kikabaki kama kilivyokuwa kikiwa kimejaa. Ndipo Fatima akawagawia majirani zake wote.365 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

Tafsiru Ruhul-Bayan Juz.3 Uk. 29.

365.

295

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 295

2/14/2018 12:12:06 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:42).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora ulimwenguni ni Maryam, Fatima, Khadija na Asia.” Ni Hadithi Hasan inaoana na Aya. Na kutoka kwa Anas amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha kati ya wanawake wa ulimwenguni: Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad na Asia mke wa Firaun.”366 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:61).

Imepokewa kwamba wakristo wa Najran walipoitwa kwenye maapizano walisema mpaka tutafakari. Walipoachana wakamwambia Aqib: “Unaonaje?” Akasema: Wallahi enyi wakristo mmeshaujua kwamba Muhammad ni Nabii aliyetumwa na bila shaka amewajieni na hoja yakinifu kuhusu mtu wenu (Yesu), wallahi katu hakuna watu walioombeana laana na Nabii kisha mkubwa wao akaendelea kui  Tafsiru Ruhul-Bayan Juz.3 Uk. 33

366.

296

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 296

2/14/2018 12:12:06 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

shi au mdogo wao kuzaliwa. Na kama mtafanya hivyo bila shaka mtaangamia, hivyo hakuna cha kufanya ila ni nyinyi kuendelea kubakia katika imani yenu na dini yenu, nendeni mkamuage mtu huyu na mrejee nchini kwenu. Ndipo kesho yake wakaja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na Mtume akatoka akiwa amemkumbatia Husein na amemshika mkono Hasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima. Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Askofu wao akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zita-muomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia, na wala juu ya uso wa ardhi hatobaki mkristo yeyote mpaka Siku ya Kiyama.” Wakasema: Ewe Abul-Qasim! Tumeona tusiapizane na wewe na tukuwache uendelee kuwa katika dini yako nasi tuendelee kubaki katika dini yetu. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: Mkikataa kufanya maapizano basi msilimu mtapata haki waliyonayo waislamu na mtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwa waislamu. Wakakataa, ndipo Mtume akawaambia: “Basi hakika mimi nitawapiga.” Wakasema: “Hatuna nguvu ya kupigana vita na waarabu, lakini sisi tunafanya suluhu na wewe usitushambulie kivita na wala usitufukuze na wala usitutoe katika dini yetu…...” Kauli ya Mwenyezi Mungu:

297

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 297

2/14/2018 12:12:06 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Ambao hutoa katika raha na katika shida na wenye kujizuia na ghadhabu na wenye kuwasamehe watu, na Mwenyezi Mungu ­hupenda wafanyao wema.”(Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:134).

Imesimuliwa kwamba mtumishi alikuwa amesimama juu ya kichwa cha Husain bin Ali (a.s.) naye (a.s.) akiwa pamoja na wageni wake katika meza ya chakula, ndipo bakuli lililokuwa mikononi mwa mtumishi likamdondokea Hasan (a.s.). mtumishi akasema: “na wenye kuwasamehe watu,” Hasan (a.s.) akasema: “Nimeshakusamehe.” Mtumishi akasema: “Mwenyezi Mungu hupenda wafanyao wema.” Hasan (a.s.) akasema: “Uko huru kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na ninakuoza fulani.”367

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale waliokufuru na kuzikadhibisha Aya zetu, hao ndio watu wa Motoni.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:10).

Amesema: “Itakapofika Siku ya Kiyama bendera ya Mashuhadaa atakabidhiwa Ali, na kila Shahidi atakuwa chini ya bendera yake, na kila aliyeuawa pasi na haki atakuwa chini ya bendera ya Husain bin Ali, na hiyo ndio kauli ya Mwenyezi Mungu: “Siku tutakayowaita kila watu na Imam wao.”368

SURAT AL-AN’AM Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 4 Uk. 95.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 6 Uk. 360.

367. 368.

298

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 298

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na tukampa Is’haka na Yakub, wote tukawaongoza, na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Qur’ani Tukufu Sura al-An’am; 6:84-85).

Na katika kumtaja Isa ni dalili ya kwamba kizazi kinapitia watoto wa binti, hivyo Hasan na Husain ni miongoni mwa kizazi cha Bwana wa Mitume Muhammad (s.a.w.w.) japokuwa ni kwa nasaba ya mama. Na atakayewaudhi hao wawili bila shaka amekiudhi kizazi chake (s.a.w.w.). Fakiri369 anasema: “Ikiwa nasaba ya upande wa mama ni sahihi na inakubalika basi yule ambaye usharifu wake ni kupitia umamani naye anakubalika, kama ilivyo kwa yule mwenye kupitia upande wa baba. Hivyo kigezo (katika usharifu) ni nasaba yake kukomea kwa ima Hasan au Husain, kwa upande wowote ule (sawa uwe mama au wa baba).”370

SURAT AL-A’ARAF Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Mwandishi wa Tafsiru Ruhul-Bayan.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 7 Uk. 61.

369. 370.

299

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 299

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na wakamuuwa yule ngamia na wakaasi amri ya Mola wao Mlezi na wakasema: Ewe Saleh! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa Mitume.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:77).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Ewe Ali hivi wajua ni nani muovu kuliko wote waliotangulia?” Akasema: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiye ajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ni yule aliyemchinja ngamia.” Kisha akasema: “Hivi wajua ni nani muovu kuliko wote watakaokuja?” Akasema: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiye ajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ni yule atakayekuuwa wewe.”371

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1). Kama ilivyopokewa ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimpa uongozi wa Hija ya mwaka wa ukombozi wa Makka Itab bin Usaydi, na katika msimu huo walihiji waislamu na mushrikina pamoja, hivyo ulipowadia mwaka wa tisa Mtume alimpeleka Abu Bakr awe kiongozi wa msimu wa Hija. Alipotoka Abu Bakr kuelekea Makka Mtume alimtumia Ali akiwa amepanda Adhbau372 ili aende kuwasomea Sura Baraa mahujaji. Akaambiwa (s.a.w.w.): “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! ungemtumia Sura   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 8 Uk. 195.   Jina la ngamia wa Mtume.

371. 372.

300

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 300

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

hiyo Abu Bakr.” Akasema: “Hafikishi kwa niaba yangu ila mtu atokanaye na mimi.” Hiyo ni kwa sababu ada ya waarabu ni kwamba hawakilishi kabila katika uandishi au uvunjaji wa mkataba ila yule aliye chifu wa kabila hilo au mtu atokanaye na chifu wao au aliye ndugu wa chifu wao. Hivyo akamtuma Ali ili kuondoa dhana hiyo….373

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“…na zitakuwako umma tutakazo zistarehesha, kisha zitawashika kutoka kwetu adhabu zenye kuumiza.” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:48).

Amesema katika kitabu Uqad-Durar: “Ole wake muuwaji wa Husain vipi itakuwa hali yake pamoja na wazazi wake na babu yake.” Kisha akasoma shairi akisema: Lazima Fatima atafika Siku ya Kiyama na hali gauni lake likiwa limetapakaa damu ya Husain. Ole wake yule ambaye waombezi wake ndio mahasimu wake, na baragumu litapulizwa Siku ya Kiyama. Na katika Hadithi imesemwa: “Muuwaji wa Husain atakuwa katika sanduku la Moto na atapata nusu ya adhabu ya watu wa duniani.”374 Imepokewa kutoka kwa Sha’abiy kwamba: Ali (a.s.) alipita huko Karbala alipokuwa akielekea kwenye Vita vya Siffin, akasimama na akauliza jina la eneo hilo, wakamwambia linaitwa Karbala. Akalia sana mpaka ardhi ikalowana kwa machozi yake, kisha akasema: “Niliingia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) nikamkuta   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 10 Uk. 383.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 143.

373. 374.

301

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 301

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

akilia. Akaniambia: ‘Punde tu Jibril alikuwa nami hapa na akanipa habari kwamba mwanangu Husain atauawa pembezoni mwa Mto Furati katika eneo linaloitwa Karbala. Kisha Jibril akatoa ukufi wa udongo na kuninusisha, ndipo sikuweza kuyazuia macho yangu mpaka yalipotoa machozi.’” Na imepokewa kwamba udongo huo Mtume wa Mwenyezi Mungu aliuweka katika chupa na akamwambia Ummu Salama: “Hakika huu ni udongo wa eneo la ardhi ambayo hapo atauawa Husain, hivyo pindi utakapouona umegeuka damu tambua kuwa ameuawa.” Ummu Salama alisema: “Ulipofika usiku ambao aliuawa Husain nilimsikia msemaji akinadi: ‘Enyi mliomuuwa Husain kwa ujahili, jibashirieni adhabu na udhalili. Mmelaaniwa kwa ulimi wa mwana wa Daud, Musa na aliyekuja na Injili.’375 Nikalia na nikatizama chupa nikakuta udongo umegeuka damu.” Imeelezwa pia kwamba mbingu ilipatwa na wekundu kutokana na kuuawa kwake. Ibnu Sirin amesema: “Wekundu ambao huwa kwenye mawingu haukuwepo hapo kabla mpaka pale alipouawa Husain, na hekima yake ni kama alivyosema Ibnu al-Jawziy kwamba: Hakika ghadhabu zetu husababisha wekundu usoni, na Haki (Mwenyezi Mungu) hana mwili, hivyo kupitia wekundu wa mawingu akadhihirisha ghadhabu yake juu ya yule aliyemuuwa Husain. Amefanya hivyo ili kudhihirisha ukubwa wa jinai. Na Siku hiyo aliyouawa hakuna jiwe lililoinuliwa duniani ila chini yake kulikutwa damu nzito.”376 Abu Shaykhi ameandika kwamba: Hakika kuna kundi la watu lilikumbushana kwamba hakuna yeyote aliyesaidia kuuawa Husain ila alisibiwa na balaa kabla ya kufariki kwake. Mzee mmoja akase  Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 144.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 144.

375. 376.

302

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 302

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ma: ‘Mimi nilisaidia na sijapatwa na chochote.’ Ndipo aliposimama kwenda kutengeneza taa na ghafla akaanza kuwaka moto huku akipiga kelele ‘moto moto moto’, akajidumbukiza katika Mto Furati, lakini pamoja na hilo aliendelea kuwaka mpaka akafariki. Wengine walipatwa na kiu kali, ikawa wanakunywa wawezavyo lakini kiu haitulii. Wengine waliadhibiwa kuuawa au upofu au kusawijika uso au kunyang’nywa utawala baada ya muda mchache tu, na mengineyo kama hayo. Hivyo baada ya kuyajua hayo jiepushe na wale wanaowafanyia uadui Ahlul-Baiti, na wala usiwe rafiki yao, kwani kufanya nao urafiki ni kuwafanyia uadui Ahlul-Baiti na ni kuwachukia.377

SURAT AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Ra’d; 13:7). Mwonyaji ni Muhammad, na kiongozi wa kuwaongoza ni Ali. Hoja juu ya hilo ni kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Wallahi Mwenyezi Mungu kumuongoza mtu mmoja kupitia wewe ni bora kwako kuliko kuwa na ngamia mwekundu.”378 Na Tabarani ameandika kwamba Ali alimwambia Fatima (a.s.): “Nabii wetu ndio Nabii bora kushinda Manabii wote naye ni baba yako. Shahidi wetu ndiye shahidi bora kushinda mashahidi wote naye ni ami ya baba yako Hamza. Na kutoka kwetu amepatikana aliye na mbawa mbili anazorukia peponi atakavyo, naye ni mwana wa ami ya baba yako Ja’far. Na kutoka kwetu wamepatikana watoto wa umma huu Hasan na Husain, nao ni watoto wako. Na kutoka kwetu atapatikana al-Mahdi.”379   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 144.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 13 Uk. 346. 379.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 13 Uk. 346. 377. 378.

303

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 303

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kama mngezimiliki hazina za rehema ya Mola wangu Mlezi, hapo lazima nyinyi mngelizizuia kwa kuogopa kuzitumia, na mwanadamu ni mchoyo sana.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani-Israil; 17:100).

Imepokewa kwamba Zainul-Abidin (a.s.) alikutana na mtu, ndipo mtu yule akaanza kumtukana. Watumwa wake wakakasirika na kutaka kumwadabisha, Zainul-Abidina akawaambia: “Mwacheni mtu huyu.” Kisha akamgeukia na kumwambia: “Yaliyositiriwa miongoni mwa mambo yetu ni mengi, je una haja yoyote tukusaidie?” mtu yule akaona aibu, basi Zainul-Abidina akamvulia kishamia chake na kumpa, na akaamrisha apewe dirhamu elfu moja. Basi tangu siku ile mtu yule akawa akisema: “Nashahidilia kwamba hakika wewe ni miongoni mwa watoto wa mitume, wala aliyepotezwa hadhani kwamba wao walikuwa ni watu wa dunia wenye kuzalisha humo mali, bali ni kwamba walikuwa wakarimu na wenye muruwa, dunia ilikuwa ikiwafuata nao wanaitoa kwa ajili ya kesho, na kwao wao ndipo inaposadikika kauli ya msemaji: ‘Na wao hutoa mali mwanzo wa utajiri na wanatanguliza subira mwisho wa ufakiri. Mgeni afikapo mtaani humkirimu, hivyo hutamjua ni yupi mkata kati yao na ni yupi tajiri.”’380

Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 15 Uk. 207.

380.

304

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 304

2/14/2018 12:12:07 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-KAHF

“Basi wakamkuta mja katika waja wetu, tuliyempa rehema kutoka Kwetu, na tuliyemuelimisha elimu kutoka Kwetu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Kahf; 18:65).

Elimu ya siri ni sawa na mlango kwenye nyumba, na anayetaka kuingia ndani ya nyumba ni wajibu juu yake kupita mlangoni, na Jumba la elimu na Jiji lake ni Mtukufu Nabii (s.a.w.w.), na lango la Jumba hili na la Jiji hili ni Ali (a.s.) kama alivyosema Mtume (s.a.w.w.): “Mimi ni Jiji la elimu na Ali ni lango lake.”381

SURAT AT-TWAHA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Twaha.” (Qur’ani Tukufu Sura Twaha; 20:1). Imam Ja’far as-Sadiq (a.s.) amesema: “Twaha ni kuapa kupitia utakaso wa Ahlul-Baiti na uongofu wao, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: “Na kuwatakaseni kabisa.” (33:33)”382

SURAT AL-HAJJ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Anayedhani ya kwamba Mwenyezi Mungu hatamnusuru (Mtume) katika dunia na akhera, basi afunge kitanzi juu kisha ajinyonge, na   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 15 Uk. 272.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 16 Uk. 361.

381. 382.

305

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 305

2/14/2018 12:12:08 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

aone je, hila yake yaweza kuyaondoa yale yaliyomghadhibisha?” (Qur’ani Tukufu Sura al-Hajj; 22:15).

Imepokewa kutoka kwa Anas bin Malik kwamba alisema: “Kuna myahudi alikuja baada ya kufariki Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na akaingia msikitini na kusema: “Yuko wapi Wasii wa Muhammad?” hadhirina wakamwashiria kwa Abu Bakr, akasema: “Nakuuliza kuhusu mambo ambayo hayajui ila Nabii au Wasii wa Nabii.” Abu Bakr akasema uliza utakalo. Yahudi akasema: “Nieleze ni lipi asilolijua Mwenyezi Mungu, na lisilokuwa la Mwenyezi Mungu, na lisilokuwepo kwa Mwenyezi Mungu?” Abu Bakr akasema: “Akasema haya ni maneno ya wapagani.” Yeye na waislamu waliyokuwepo hapo wakamjia juu. Ibnu Abbas akasema: “Hamjamtendea haki mtu huyu ikiwa mnalo jibu lake, na kama hamna la kumjibu basi nendeni kwa yule atakayemjibu, kwani hakika mimi nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema kumwambia Ali (a.s.): ‘Ewe Mwenyezi Mungu upe nguvu moyo wake na uimarishe ulimi wake.’” Ndipo Abu Bakr na waliokuwa wamehudhuria hapo wakasimama na kumwendea Ali na wakamweleza hayo. Ali akasema: “Ama asilolijua Mwenyezi Mungu ni ile kauli yenu enyi Mayahudi ‘Hakika Uzayru ni mtoto wa Mwenyezi Mungu.’ Mwenyezi Mungu hajui kwamba ana mtoto. Ama lisilokuwa la Mwenyezi Mungu ni kwamba Yeye hana mshirika. Na ama lisilokuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni kwamba kwa Mwenyezi Mungu hakuna uonevu wala ajizi.” Yahudi akasema: “Nashahidilia kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, na hakika wewe ni Wasii wa Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Waislamu wakafurahi kwa hilo.383   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 17 Uk. 14.

383.

306

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 306

2/14/2018 12:12:08 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33). Siku moja Mtume alitoka akiwa amejifunika shuka lililodariziwa kwa manyoya meusi, kisha akaketi. Akaja Fatima akamwingiza katika shuka hilo, kisha akaja Ali akamwingiza katika shuka hilo, kisha wakaja Hasan na Husain nao akawaingiza katika shuka hilo, kisha akasema: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume. Watu wa kishamia ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na binti yake na al-Murtadha (Ali), kisha ni watoto zake wawili pindi walipokusanyika.”384 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56).

Ka’bi bin Ajrah, amesema: Ilipoteremka: “Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” tulisimama na kumwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ni ipi namna ya kukusalia? Mtume akasema: “Semeni:   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 171.

384.

307

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 307

2/14/2018 12:12:08 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Ewe Mwenyezi Mungu! Mpe rehma na amani Muhammad na aali Muhammad kama ulivyompa rehma na amani Ibrahim na aali Ibrahim. Hakika wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.”385 Na katika Hadithi Mtume alisema: “Hakuna dua yoyote ila kati yake na Mwenyezi Mungu kuna kizuizi, mpaka pale atakapomsalia Muhammadi na Aali Muhammad. Likitekelezwa hilo ndipo kizuizi huondoka na dua kupita, na lisipotekelezwa hilo dua hurejea.”386 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Muogopeni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya sawa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:70).

Imeelezwa kwamba: “Hakika Yakub mtoto wa Is’haq aliyejulikana kwa jina la Ibnu Sikit ambaye ni miongoni mwa ulamaa wakubwa wa lugha ya Kiarabu, siku moja alikuwa ameketi na alMutawakil, ghafla akaja al-Muutazu na al-Muayad watoto wa alMutawakil, akasema al-Mutawakil: “Ni yupi umpendaye sana, ni wanangu wawili au Hasan na Husain?” Ibnu Sikit akasema: “Wallahi hakika Qanbar mtumishi wa Ali (a.s.) ni bora kushinda wewe na kushinda watoto wako.” al-Mutawakil akasema: “Ng’oeni ulimi wake toka kinywani mwake.” Wakafanya hivyo na akawa amefariki usiku huohuo.387   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 225.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 230. 387.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 248. 385. 386.

308

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 308

2/14/2018 12:12:09 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AZ-ZUMAR Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Mwenyezi Mungu amekupigieni mfano wa mtu mwenye washirika wanaogombana, na wa mtu mwingine aliyehusika na mtu mmoja, je wako sawa katika hali? Alhamdulillahi! Lakini wengine wao ­hawajui.” (Qur’ani Tukufu Sura az-Zumar; 39:29).

Hasan na Husain (a.s.) walikuwa wakicheza mikononi mwa Mtume (s.a.w.w.), naye akavutiwa nao. Jibril akamjia akiwa na chupa na karatasi, na ndani ya chupa mlikuwa na damu na ndani ya karatasi mkiwa na sumu. Akasema: “Ewe Muhammad je wawapenda hawa, basi tambua kuwa mmoja wao atauwawa kwa upanga na hii ndio damu yake, na mwingine atanyweshwa sumu na hii ndio sumu yake, ghafla akaondoa moyo wake kwa watoto na kuuelekeza moja kwa moja kwa Mwenyezi Mungu….”388 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Ewe Mola Mlezi! Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa yasiyoonekana na yanayoonekana, wewe utahukumu baina ya waja wako katika yale waliyokuwa wakikhitilafiana.” (Qur’ani Tukufu Sura az-Zumar; 39:46).   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 23 Uk. 104.

388.

309

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 309

2/14/2018 12:12:09 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Rabi’u alikuwa miongoni mwa wanahadithi, alikuwa hazungumzi ila lile linalomhusu yeye, basi alipouawa Husain wakasema sasa atazungumza, ndipo akasoma: “Sema: Ewe Mola Mlezi! Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa yasiyoonekana na yanayoonekana, wewe utahukumu baina ya waja wako katika yale waliyokuwa wakikhitilafiana.” Na imepokewa kwamba alisema: “Ameuawa yule ambaye Mtume alikuwa akimkalisha mapajani mwake na akiweka ulimi wake ndani ya kinywa chake.”389

SURAT AL-MU’MIN (AL-GHAFIR) Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akasema mtu muumini aliyekuwa mmoja wa watu wa Firaun anayeficha imani yake; je, mtamuuwa mtu kwa sababu tu anasema Mola wangu Mlezi ni Mwenyezi Mungu?” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mu’min (al-Ghafir); 40:28).

“Watatu hawajamkufuru Mwenyezi Mungu katu hata kidogo: Ezekiel Muumini toka aali Firaun, Habibu Najjari muumini toka aali Yasin, na Ali bin Abu Talib naye ndiye mbora wao.”390

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23).   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 24 Uk. 120.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 24 Uk. 176.

389. 390.

310

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 310

2/14/2018 12:12:09 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Imepokewa kwamba: Ilipoteremka palisemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa ndugu ambao ni imewajibishwa juu yetu kuwapenda. Akasema: “Ali, Fatima na wanangu Hasan na Husain.” Na hilo linathibitishwa na ile riwaya iliyopokewa kutoka kwa Ali kwamba: “Nilimshitakia Mtume wa Mwenyezi Mungu kuhusu husuda za watu dhidi yangu. Akasema: ‘Hivi huridhii kuwa wa kwanza kuingia Peponi. Mimi, Wewe, Hasan, Husein.”391 Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ni shahidi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni shahidi. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ameghufuriwa. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ametubia. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi ­amekufa na hali ni muumni aliyekamilika kiimani. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na hali malaika ameshambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakir. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad atasindikizwa Peponi kama biharusi asindikizwavyo kwenda nyumbani kwa   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 25 Uk. 312.

391.

311

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 311

2/14/2018 12:12:09 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mumewe. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atamfungulia milango miwili ya Pepo kaburini. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Mungu atawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amefia ndani ya Sunna. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad atakuja Siku ya Kiyama na hali imeandikwa baina ya macho yake mawili: Amekata tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad basi amekufa na hali ni kafiri. Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu ya Pepo.”392

SURAT AZ-ZUKHRUF Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akalifanya neno hili liwe lenye kubaki katika kizazi chake ili warejee.” (Qur’ani Tukufu Sura az-Zukhruf; 43:28).

Baadhi wamesema kuhusu sababu ya kusema ‘Karamallahu Wajhahu’ pindi atajwapo Ali bin Abu Talib (a.s.), ni kwamba imepatikana nukuu kutoka kwa mama yake mzazi Fatima binti Asad bin Hashim kwamba kila alipokuwa akitaka kulisujudia sanamu wakati akiwa na mimba yake, Ali alikuwa akimzuia kufanya hivyo (akiwa angali tumboni).393   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 25 Uk. 312.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 25 Uk. 364.

392. 393.

312

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 312

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-FATH Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Alama zao ni katika nyuso zao kwa athari ya kusujudu…..” (Qur’ani Tukufu Sura al-Fath; 48:29). Imam Zaynul-Abidina ambaye ni Ali bin Husain bin Ali (a.s.) alikuwa akiitwa: Mwenye sugu (sagamba). Na alikuwa na miti mia tano ya mizaituni, alikuwa akisali chini ya kila mti mmoja rakaa mbili kila siku. Mshairi akasema: “Nyumba za Ali, Husain, Ja’far, Hamza na Sajadi mwenye sugu”394

SURAT AR-RAHMAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili. ­Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Rahman; 55:19-20). Imesemwa kwamba bahari mbili ni Ali na Fatima, na kizuizi ni Mtume (s.a.w.w.), na hutoka kwao hao wawili Hasan na ­Husein.395

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 26 Uk. 58. Ubeti huu ni wa Da’bal al-Khaza’i (Mwenyezi Mungu amrehemu). 395.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 27 Uk. 296. 394.

313

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 313

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Imepokewa kutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.) kwamba alisema: “Hakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nilikuwa nina dinari nikaichenji kwa dirhamu kumi, hivyo ikawa kila nisemapo siri na Mtukufu Mtume natoa sadaka dirhamu moja. Yaani nilikuwa kila siku nasema siri na Mtume kwa dirhamu moja mpaka siku kumi, na nilikuwa namuuliza kuhusu sifa moja miongoni mwa sifa njema.”396 Ibnu Umar alisema: “Ali alikuwa na mambo matatu, kuwa nalo moja kati ya hayo ni jambo nilipendalo mno kuliko kuwa na ngamia mwekundu: Kuozwa Fatima, kukabidhiwa bendera Siku ya Khaibar na Aya ya kuongea siri na Mtume.”397

SURAT AT-TAGHABUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, na kwa ­Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura ­at-Taghabun; 64:15).

Katika kitabu Mishkatul-Maswabihi imeandikwa kwamba: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akitoa hotuba na ghafla wakaja Hasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuamka, akateremka toka mim  Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 405.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 40.

396. 397.

314

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 314

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

barini akawafuata na kuwachukua na kuwaweka mbele yake, kisha akasema: ‘Mwenyezi Mungu amesema kweli. Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, nilipowaona hawa wawili wakitembea huku wakidondoka sikuweza kuvumilia mpaka nimekatisha mazungumzo yangu na kuwanyanyua.’ Kisha akaendelea na hotuba yake….”398

SURAT AT-TAHRIM Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake, na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tahrim; 66:4). Imepokewa kutoka kwa Mujahid kwamba amesema: Waumini wema ni Ali bin Abu Talib. Fakiri399 anasema: Hiyo inaungwa mkono na kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Ewe Ali! Wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa.” Hivyo ikiwa Ali ni sawa na Harun basi yeye ndio mwema mfano wake.400

SURAT NUH Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.” (Qur’ani Tukufu Sura Nuh; 71:20). Amirul-Muuminina Ali (a.s.) alikuwa akisema: “Niulizeni ­kuhusu njia za mbinguni kwani hakika mimi nazijua zaidi kushinda njia za ardhini.”401   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 18.   Mwandishi wa tafsiri hii Tafsiru Ruhul-Bayan. 400.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 53. 401.   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 29 Uk. 180. 398. 399.

315

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 315

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Hasan na Husein walipatwa na maradhi, babu yao Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona akiwa pamoja na baadhi ya watu. Wakamwambia Ali: “Ni vizuri lau ukiweka nadhiri kwa ajili ya wanao.” Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhiri kwamba ikiwa watapona watafunga siku tatu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kutafuta radhi zake na kumshukuru. Wakapona, na wao wakafunga na hali hawana chochote cha kufuturu. Ali akaenda kwa Simon Myahudi wa Khaibari, akakopa toka kwake pishi tatu za ngano. Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano kulingana na idadi yao. Chakula kikawekwa mbele yao wakati wa kufuturu ili wafuturu, mara masikini akafika mlangoni kwao akasema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni maskini miongoni mwa maskini wa kiislamu, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa chakula na wakashinda mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Asubuhi wakaamka wakiwa wamefunga, waliposhinda mchana kutwa na kukiweka chakula mbele yao ili waftari, mara akafika 316

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 316

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

mlangoni kwao yatima, akasema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, yatima toka katika watoto wa muhajirana, baba yangu amekufa kishahidi Siku ya Aqabah, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa chakula. Asubuhi wakaamka wakiwa wamefunga, waliposhinda mchana kutwa na kukiweka chakula mbele yao ili waftari, mara mfungwa wa kivita akafika mlangoni kwao, akasema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya unabii, mimi ni mfungwa miongoni mwa wafungwa, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa chakula. Ilipofika siku ya nne wakiwa tayari wameshatimiza nadhiri yao Ali alimshika Hasan mkono wa kulia na Husein mkono wa kushoto na kwenda nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na hali wao wawili wakitetemeka kama vifaranga kutokana na ukali wa njaa. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipowatizama alisema: “Hali niionayo yaniumiza mno.” Akasimama na kwenda nao, wakamkuta Fatima akiwa mihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake na macho yake yamebadilika, hilo likamuumiza sana. Ndipo Jibril (a.s.) akateremka na kusema: “Ewe Muhammad pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Na akamsomea Sura hii.402 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Humo wataegemea viti vya enzi, humo hawataona jua wala baridi.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:13). Ibnu Abbas amesema: “Pindi watu wa Peponi watakapokuwa peponi ghafla wataona mwanga kama mwanga wa jua na Pepo imeangazwa kwa mwanga huo. Watasema: Ewe Ridhwan! Mola wetu Mtukufu amesema: “Hawataona jua wala baridi.” hii ni nuru ya   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 29 Uk. 268.

402.

317

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 317

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nini? Ridhwan atawaambia: “Hili si Jua wala si Mwezi, lakini huyu ni Fatima na Ali wamecheka, na kutokana na nuru ya kicheko chao Pepo imeangaziwa.”403

SURAT ASH-SHAMS Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia: Ni ngamia wa Mwenyezi Mungu na kinywaji chake. Lakini walimkadhibisha na wakamchinja. Kwa hiyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao, na akifanya sawa.” (Qur’ani Tukufu Sura ­ash-Shams; 91:13-14)

Katika Hadithi ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Ewe Ali hivi wajua ni nani muovu kuliko wote waliotangulia?” Akasema: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiye ajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ni yule aliyemchinja ngamia.” Kisha akasema: “Hivi wajua ni nani muovu kuliko wote watakaokuja?” Akasema: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiye ajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ni yule atakayekuuwa wewe.”404

Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 29 Uk. 270.   Imeshatangulia riwaya kama hii katika Sura Aaraf Aya ya 77.

403. 404.

318

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 318

2/14/2018 12:12:10 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA ALUSIY, INAYOITWA RUHUL-MA’ANIY FITTAFSIRIL-QUR’AN ­AL-‘ADHIM WASAB’UL-MATHANIY. SURAT AL-BAQARA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na katika watu yuko auzaye ­nafsi yake kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:207) Imamia na baadhi ya maulama wetu wamesema kwamba: Iliteremka kwa ajili ya Ali (a.s.) pindi Mtume alipomwachia jukumu la kulala juu ya kitanda chake huko Makka pale alipoondoka kwenda Pangoni.405 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Baqara; 2:274)

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali (a.s.) alikuwa na dirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana, nyingine siri na nyingine dhahiri.”406   Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 2 Uk. 83.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 41.

405. 406.

319

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 319

2/14/2018 12:12:11 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na kizazi cha Ibrahim na kizazi cha Imran juu ya walimwengu wote.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:33)

Imepokewa kutoka kwa Ahlul-Baiti (a.s.) kwamba wao husoma: “Na Aali Muhammad juu ya walimwengu wote.”407 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Kila mara Zakariya ­alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika ­Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hesabu.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:37) Abu Ya’la ameandika kutoka kwa Jabir bin Abdullah amesema kwamba hakika Mtume (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bila kula chakula mpaka hali hiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenye nyumba za wakeze lakini hakukuta chochote kwao ndipo akaenda kwa Fatima na kumwambia: “Ewe mwanangu mpendwa! Je una chochote ninachoweza kula kwani hakika mimi ni mwenye njaa?” Akamjibu: “Wallahi sina.” Mtume alipotoka, jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vya mkate na finyango ya nyama. Fatima akapokea na kuweka ndani ya bakuli lake, akasema: “Wallahi katika hiki nitampa kipaumbele Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kabla ya nafsi yangu na kabla ya yule aliyopo kwangu.” Japokuwa wote walikuwa wanahitajia chakula lakini Fatima alimtuma Hasna au Husein aende   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 116.

407.

320

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 320

2/14/2018 12:12:11 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

kumwita Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) naye alikuja. Fatima akamwambia: “Kwa haki yako na ya mama yangu, Mwenyezi Mungu ameleta kitu nami nimekihifadhi kwa ajili yako.” Akamwambia: “Kilete ewe binti yangu mpendwa.” Nikamletea bakuli na nilipolifunua ghafla nikakuta limejaa mikate na nyama, nilipolitazama nikapatwa na mshangao na nikatambua kuwa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu. Nikamhimidi Mwenyezi Mungu na nikamkabidhi chakula hicho Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Alipokiona alimhimidi Mwenyezi Mungu na akasema: Umetoa wapi hivi ewe binti yangu mpendwa? Akajibu: “Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu ewe baba yangu mpendwa. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu. “ Mtume akamhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Ambaye amekufanya ewe binti yangu mpendwa kifani wa seyida wa wana wa Israel (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwa aruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu kisha akiulizwa kakipata wapi husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bila hesabu.” Kisha akawakusanya Ali, Hasan na Husein na Ahlul-Baiti wake wote wakala mpaka wakatosheka na chakula kikabaki kama kilivyokuwa, Fatima akawagawia jirani zake.408 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ­ulimwenguni.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:42)   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 124.

408.

321

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 321

2/14/2018 12:12:11 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Asakir ameandika kupitia moja ya njia zake kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Wanawake bora wa peponi ni Maryam binti Imran, Fatima, Khadija na Asia mke wa Firaun.” Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Fatima (a.s.) kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wewe ni Seyida wa wanawake wa peponi ila Bikira Maryam.” Makusudio ni kwamba Mariam ni mbora kwa wanawake wa zama zake, na hiyo haipelekei yeye kuwa mbora kuliko Fatima (a.s.). Hilo linaungwa mkono na ile riwaya aliyoiandika Ibnu Asakir kwa njia ya Muqatil kutoka kwa Dhahak kutoka kwa Ibnu Abbas (a.s.) kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Wanawake wane ni wabora kushinda wanawake wa zama zao: Mariam binti Imran, Asia binti Muzahim, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad, na mbora wao kiulimwengu ni Fatima.” Na ile aliyoipokea al-Harthi bin Usama katika Musnad yake kwa sanadi sahihi ijapokuwa ni Hadithi ya Mursal: “Mariam ni mbora kwa wanawake wa zama zake.” Na hii ndio rai ya Abu Ja’far (Imam al-Baqir) na ndio rai mashuhuri kutoka kwa Ahlul-Bait (a.s.). Rai ambayo naipa kipaumbele mimi ni kwamba Fatima ni bora kushinda wanawake wote waliotangulia na watakaokuja, kwani yeye ni sehemu ya nyama ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), pili ni kutokana na wasifu mwingine ambao hauchafuliwi na Hadithi hizo zilizotangulia hata tuseme kwamba mwingine asiyekuwa yeye ni bora kumshinda…… Na kuanzia hapa ndipo unapojulikana ubora wake juu ya Aisha. Ama wengi wanaokhalifu rai hiyo, hoja yao ni kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Chukueni theluthi ya dini yenu toka kwa Hamayrau (Aisha).” Na kauli yake (s.a.w.w.): “Ubora wa Aisha juu ya wanawake wengine ni sawa na ubora wa mkate juu ya chakula.” 322

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 322

2/14/2018 12:12:11 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Lakini wewe wajua kilichopo katika dalili hizi na ni kwamba hazielezi ubora wowote wa Aisha juu ya Fatima. Kwanza: Cha maana sana kilichomo katika Hadithi hii iwapo tukisema imethibiti ni kwamba yathibitisha kuwa yeye (Aisha) ni msomi hivyo theluthi ya dini inachukuliwa toka kwake, na hii haikanushi uwepo wa elimu mfano wa hiyo kwa kipande cha nyama ya Mtume (s.a.w.w.) (Fatima). Na kutokana na kujua kwake (s.a.w.w.) kwamba Fatima hatobaki muda mrefu ambao watu wataweza kuchukua elimu toka kwake huenda ndio maana hakusema, na laiti angejua (anao muda wa kutosha) angesema: “Chukueni dini yenu yote kutoka kwa Zahra.” Na kutokutamka kauli hii kumhusu mtu ambaye akili na nukuu vyote vimethibitisha elimu yake haimaanishi kwamba yupo aliye bora zaidi yake, la sivyo Aisha angekuwa bora hata kushinda baba yake (Abu Bakr) kwani hakijapokewa chochote kutoka kwake kinachohusu dini ila kitu kichache. Zaidi ya hapo ni kwamba ile kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Hakika mimi ni mwenye kuwaachia vizito viwili kati yenu: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu, havitoachana mpaka vinikute kwenye hodhi,” inachukua nafasi ya ile riwaya ya ubora wa Aisha ambayo kama ilivyo wazi ni nyongeza (riwaya ya uwongo), kwani itawezekanaje iwe hivyo na hali Fatima ndiye Seyida wa kizazi cha Mtume. Pili: Kwa sababu Hadithi ya pili inapingana na zile zinazoonyesha kwamba wengine wasiyokuwa yeye (Aisha) ni bora kushinda yeye (Aisha). Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Ammar bin Sa’d kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Khadija amefanywa bora kushinda wanawake wa umma wangu kama Mariam alivyofanywa bora kushinda wanawake wa ulimwenguni.” Bali Hadithi hii ni dhahiri katika ubora, na inawasifu kamili kwa yule mwenye kutizama kwa akili yake na akajiepusha na ububusa na ulazimishaji. 323

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 323

2/14/2018 12:12:11 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ama kauli ya mwenye kusema kwamba hakika mabinti wengine wa Nabii ni bora kushinda Aisha, sioni kama ina tatizo. Na kwangu mimi mjadala wa ni nani aliye mbora kushinda wanawake wote wa ulimwenguni ni kati ya Mariam na Fatima tu. Na kutokana na wasifu uliotangulia tayari umeshajua rai yangu ninayoegemea. Imam asSabki aliulizwa kuhusu suala hili akasema: “Tunalolichagua na kulifuata ni kwamba Fatima binti Muhammadi ndiye bora kisha mama yake…”409 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni ­tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura AaliImran; 3:61)

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Ujumbe wa Wakristo wa Najran ulikuja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, nao walikuwa ni watu kumi na wane wakiongozwa na Sayid ambaye alikuwa ndio mkubwa wao, kisha Aqib aliyekuwa akimfuatia kwa ukubwa na ndiye aliyekuwa mwenye uamuzi wa mwisho kwao, Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia: “Silimuni.” Wakasema tumeshasilimu. Mtume akawaambia: “Bado hamjasilimu.” Wakasema tumeshasilimu kabla ya kufika kwako. Mtume akawaambia: “Mnasema uongo, kuna mambo matatu yanawazuia kusilimu: Kuabudu kwenu msal  Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 137 na Uk. 138.

409.

324

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 324

2/14/2018 12:12:11 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

aba, kula kwenu nguruwe, na kudai kwenu kuwa Mwenyezi Mungu ana mtoto.” Mwenyezi Mungu akateremsha:

“Hakika mfano wa Isa mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam, alimuumba kutokana na udongo, kisha akamwambia kuwa, basi akawa. Ndiyo haki itokayo kwa Mola wako Mlezi, basi usiwe miongoni mwa wenye kutia shaka.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:59-60)

Alipowasomea Aya hiyo wakasema hatujui uyasemayo, ndipo ikateremka:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:61)

Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia: “Hakika Mwenyezi Mungu ameniamuru ikiwa hamtakubali hili nifanye maapizano nanyi.” Wakasema: “Ewe Abul-Qasim! mpaka turejee na tutafakari jambo hili kisha tutakuja.” Walipoachana na wakasadikishana wao kwa 325

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 325

2/14/2018 12:12:12 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

wao, Sayid alimwambia Aqib: “Wallahi mmeshajua kwamba hakika mtu huyu ni Nabii na Mtume, na lau mkifanya naye maapizano basi atawateketeza, wallahi katu hakuna watu walioombeana laana na Mtume kisha mkubwa wao akaendelea kuishi au mdogo wao kuzaliwa. Kama hamtomfuata na mkikataa basi nyinyi endeleeni kubakia katika dini yenu, na nendeni mkamuage mtu huyu na mrejee nchini kwenu. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa ametoka akiwa pamoja na Ali, Hasan, Husein na Fatima, akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Ndipo wakakataa kufanya naye maapizano na wakafanya suluhu kwa sharti la kutoa kodi.410 Jabir amesema: Mtume alisema: “Naapa kwa Yule Ambaye aliyenituma kwa haki! Lau wangefanya maapizano bonde lao lingeteketea kwa moto.”411 Na imepokewa kwamba Askofu wa Najran alipomuona Mtume wa Mwenyezi Mungu akija akiwa na Ali, Fatima, Hasan na Husein alisema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane naye mtaangamia.”412 Na katika kadhia hii kuna dalili ya wazi juu ya unabii wake (s.a.w.w.), la sivyo wasingekataa kufanya naye maapizano, na kuna dalili juu ya ubora wa mawalii wa Mwenyezi Mungu na Aali wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, jambo ambalo hana shaka nalo yeyote aliye muumini.413   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167. 412.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167. 413.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167. 410. 411.

326

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 326

2/14/2018 12:12:12 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Muslim, Tirmidhi na weningineo wameandika kutoka kwa Sa’d bin Waqqas kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii: “Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:61), Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husain, akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio watu wa nyumba yangu.”414 Ibnu Abi ‘Allani ambaye ni Muutazila ametoa dalili kupitia kisa hiki kwamba Hasan na Husain (a.s.) walikuwa Mukalafu katika hali hiyo, kwa sababu hairuhusiwi maapizano ila kwa waliobalehe. Kupatikana hali hiyo hakutegemei balehe, kwani ukamilifu unaweza kupatikana kabla yake, bali huenda ukashinda hata ule wa wale waliobalehe, hivyo hakuna kizuizi kinachozuia Hasan na Husain kutokuwa balehe kipindi hicho, isipokuwa tu iwapo ni katika miaka ambayo haiwezekani kwa wao kuwa tayari ni wakamilifu wa akili. Zaidi ya hapo ni kwamba inaewezekana Mwenyezi Mungu akavunja ada kwa hao mabwana hivyo akawapa lile ambalo hakuna mwingine yeyote atakayeshirikiana nao (yaani akawapa akili za utu uzima wangali watoto wadogo – kama ilivyokuwa kwa Nabii Isa alivyoongea akiwa kwenye kitenga cha utotoni), hivyo lau ikisihi kwamba ukamilifu wa akili huwa hauwi katika miaka hiyo, basi inajuzu kuwepo ukamilifu huo kwao kwa ajili ya kuwatofautisha wao na watu wengine, na kwa ajili ya kuwa dalili juu ya nafasi yao kwa Mwenyezi Mungu na umakhususi wao kwake, nao ni kaumu ambayo sifa zilizo makhususi kwao hazihesabiki.415   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 168.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 168.

414. 415.

327

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 327

2/14/2018 12:12:12 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarakane..” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:103). Ahmad ameandika kutoka kwa Zayd bin Thabit kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuacha kati yenu mirathi mbili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka baina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu watu wa nyumba yangu, na hakika hivyo viwili havitaachana mpaka vinikute kwenye hodhi.”416

SURAT AN-NISAA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume, basi hao watakuwapamoja na wale aliowaneemesha Mwenyezi Mungu, miongoni mwaManabii, na Masidiki, na Mashahidi na Watu wema, na hao ndio marafiki wema.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Nisaa’; 4:69).

Amesema: “Pili: Nafasi ya Masidiki nao ni wale ambao wanaowafuata Manabii (a.s.) katika maarifa, na mfano wao ni sawa na yule anayetazama kwa mbali kitu kilivyo, na hiyo ndiyo aliyomaanisha Ali (a.s.) pale alipoambiwa: “Je umemuona Mwenyezi Mungu?” Akajibu: “Siwezi kumwabudu Mola Mlezi nisiyemuona, macho hayamuoni kwa uono wa macho lakini nyoyo zinamuona kwa imani ya kweli.”417   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 4 Uk. 17.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 5 Uk. 68.

416. 417.

328

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 328

2/14/2018 12:12:12 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:3).

Imethibiti kwetu kwamba alisema huko418 kuhusu haki ya Ali (a.s.): “Yule ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.” Na akaongeza zaidi ya hapo kama ilivyo katika baadhi ya riwaya.419 Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Wanahadithi wengi wamesema kwamba yenyewe iliteremka kwa ajili ya Ali. al-Hakim, Ibnu Mardawayhi na wengineo wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwa sanad yenye kuungana kwamba alisema: Abdullah bin Salam na kundi lake waliokuwa wamemwamini Mtume (s.a.w.w.) walikuja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), wakasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Hakika   Yaani katika bonde la Ghadir Khum. Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 6 Uk. 55.

418.

420.

329

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 329

2/14/2018 12:12:12 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

nyumba zetu ziko mbali na hatupati wa kuketi nasi wala kuzungumza nasi kinyume na kikao hiki, na hakika jamaa zetu walipoona tumemsadiki Mwenyezi Mungu na Mtume wake wametutenga na wameapa ndani ya nafsi zao kwamba hawataketi nasi, hawatatuozesha na wala hawatasema nasi, na jambo hilo limekuwa zito juu yetu.’ Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawaambia: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake.” Kisha (s.a.w.w.) akatoka na kuelekea msikitini na akawakuta watu wakiwa wamesimama na wengine wakiwa katika rukuu, ndipo akamuona muombaji, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamuuliza: ‘Kuna yeyote aliyekupa kitu?’ Akajibu ndio, amenipa pete ya fedha. Akamuuliza: ‘Nani?’ Akajibu: Yule aliyesimama. Na akaashiria kwa Ali (a.s.). Mtume akamuuliza: ‘Alikupa akiwa katika hali gani?’ Akajibu: Akiwa katika rukuu. Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa takbira kisha akasoma Aya hii. Has?n akasimama na kusoma shairi: “ Abul Hasan nafsi yangu ni fidia kwako, roho yangu na kila kizito na chepesi chenye kuelekea katika uongofu. ivi kweli sifa zako njema zitakwenda bure bila faida, H hapana; sifa njema zitokazo kwa Mungu hazipotei bure. Kwani wewe ndiye uliyetoa sadaka ulipokuwa katika rukuu, nafsi yangu ni fidia kwako ewe mwenye rukuu bora kushinda zote. Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha kwako uwalii bora, na akauthibitisha ndani ya Kitabu cha sheria.”420

SURAT AL-A’ARAF Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 6 Uk. 149.

420.

330

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 330

2/14/2018 12:12:12 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Na wakamuua yule ngamia na wakaasi amri ya Mola wao Mlezi na wakasema: Ewe Saleh! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa Mitume.” (Qur’ani Tukufu Sura al-A’araf; 7:77).

Imekuja katika Hadithi kwamba muovu kuliko wote waliotangulia ni yule aliyemchinja ngamia. Na muovu kuliko wote watakaokuja ni yule aliyemuua Ali (a.s.). Hilo ndilo Mtume alilomweleza Ali (a.s.). na kwa rai yangu mimi ni kwamba muovu kushinda wote watakaokuja ni muovu zaidi kushinda yule muovu mwenye kuwashinda wote waliotangulia. Na tofauti kati yao ni kama tofauti kati ya Ali na ngamia. Habari zimegusia bali zimetamka kwamba muuwaji wa AmirilMuuminina alikuwa amehalalisha mauwaji hayo, bali alikuwa akiamini kuwa kufanya hivyo ni thawabu kwake, na masahiba zake wamemsifu kwa tukio hilo, ndipo Amran bin Hatwan (Ghadhabu za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake), akatoa shairi: “ Pigo bora lilioje! Kutoka kwa mcha mungu, hakukusudia kwalo ila kupata ridhaa kutoka kwa Mkuu wa Arshi (Mwenyezi Mungu). Hakika mimi namtaja leo na ninamzingatia kwamba ni kiumbe chenye fungu kamili mbele ya Mwenyezi Mungu.” a Mwenyezi Mungu ana neema kwa yule aliyemjibu: N “Pigo ovu lilioje! Kutoka kwa muovu aliyejirithisha Moto, atakutana na Rahman akiwa Amemghadhibikia. Kana kwamba kwa pigo lake hajapata kitu ila kuingia motoni kesho Siku ya mkusanyiko. Hakika mimi namtaja leo na ninamlaani, na pia namlaani Imran bin Hatwan. 331

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 331

2/14/2018 12:12:13 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Na kudai kwamba kitendo chake hicho ni shubha itakayomwokoa, ni kauli ambayo bila shaka ni sehemu ya kuweweseka. Kwani lau ikiwa mfano wa kitendo hicho ni chenye kumwokoa na adhabu ya dhambi hii, basi mtu afanye atakavyo! Umetakasika Mwenyezi Mungu na uzushi huu mkubwa.421

SURAT AL-ANFAL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na walipokupangia njama wale waliokufuru ili wakufunge au wakuue au wakutoe…” (Qur’ani Tukufu Sura al-Anfal; 8:30). Jibril (a.s.) alimjia Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumwambia: “Usiku huu usilale kitandani kwako ambapo huwa unalala.” Ulipowadia usiku walijikusanya mlangoni kwake wakimvizia ni muda upi atalala ili wamvamie. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipoona nafasi yao alimwambia Ali (a.s.): “Lala kitandani kwangu na jifunike shuka hili la kijani la kihadhramiy, hakika hakitakupata chochote chenye kukuudhi toka kwao.” Na ilikuwa ni kawaida ya Mtume wa Mwenyezi Mungu kujifunika shuka hiyo alalapo. Ali (a.s.) akasoma shairi kuashiria neema aliyoneemeshwa na Mwenyezi Mungu, akasema: imemkinga kupitia nafsi yangu yule mbora kushinda wote N waliowahi kukanyaga changarawe, na kuliko wote waliowahi kutufu Nyumba ya kale na kugusa Jiwe. Mtume wa Mwenyezi Mungu amekhofia wasimfanyie hila, ndipo Mungu Mwenye uwezo amemwokoa dhidi ya hila. tume wa Mwenyezi Mungu amelala kwa amani huko pangoni, M akiwa chini ya ulinzi wa Mungu na sitara Yake.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 8 Uk. 147.

421.

332

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 332

2/14/2018 12:12:14 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

imelala nikiwafuatilia wao na yale wanayonituhumu, na hali N nimeituliza nafsi yangu katika kuuawa na kufungwa.”422

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:1). Alusiy amesema: “Riwaya zimetofautiana kuhusu je Abu Bakr alikuwa kaamrishwa kuisoma au la? Nyingi zinaona alikuwa ameamriwa kuisoma, na kwamba Ali alipomfuata na kuichukua toka kwake aliamriwa kuisoma. Na imekuja katika riwaya kutoka kwa Ibnu Habban na Ibnu Mardawayhi kutoka kwa Abu Said al-Khudri kwamba Abu Bakr aliponyang’anywa sura hiyo alikuja kwa Mtume na hali akiwa ameingiwa na khofu kwamba huenda kuna kitu kimeteremka kuhusu yeye. Alipofika kwa Mtume alisema: “Nina nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Mtume akasema: “Ni kheri tupu, wewe ni ndugu yangu na swahiba wangu pangoni, na wewe utakuwa pamoja nami katika hodhi, isipokuwa ni kwamba hafikishi kwa niaba yangu asiyekuwa mimi au mtu atokanaye na mimi.”423 Imekuja katika riwaya ya Ahmad na Tirmidhi, ambayo yeye Tirmidhi, Abu Shaikh na wengineo wameizingatia kuwa ni Hasana, kwamba Anas amesema: “Mtume (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr na Sura Baraa, kisha akamwita na kumwambia: “Haipasi yeyote kuifikisha hii ila mtu katika watu wa nyumba yangu.” Ndipo akamwita Ali na kumkabidhi.424 Kauli ya Mwenyezi Mungu:   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 9 Uk. 176.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 40. 424.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 40. 422. 423.

333

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 333

2/14/2018 12:12:14 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:19).

Imepokewa kwa njia mbalimbali kwamba Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali na Abbas, hiyo ni pale Amirul-Muuminina alimwambia Abbas: “Ewe Ami yangu, ungehamia Madina.” Akamjibu: “Hivi mimi siko katika kazi bora kushinda kuhama, hivi mimi si ninatoa huduma ya maji kwa mahujaji na ninalinda Nyumba.”425 Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Bila shaka Mwenyezi Mungu amekusaidieni katika mapigano mengi na Siku ya Hunayni.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:25). Imepokewa kwamba al-Mutawakkil aliugua sana akaweka nadhiri iwapo Mwenyezi Mungu atamponyesha basi atatoa sadaka mali nyingi. Alipopona aliwauliza ulamaa kipimo cha wingi, ndipo kauli zao zikatofautiana, wakamshauri amuulize Abu Hasan Ali bin Muhammad bin Ali bin Musa al-Kadhim (a.s.), na alikuwa amemuweka kuzuizini huko nyumbani kwake, ndipo akaamuru aandikiwe barua. Akamrudishia jibu kwamba atoe sadaka dirhamu themanini. Walipomuuliza sababu alisoma Aya hii na kusema: Tumehesabu maeneo hayo yakafikia themanini.426   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 60.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 65.

425. 426.

334

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 334

2/14/2018 12:12:14 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT HUD Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” (Qur’ani Tukufu Sura Hud; 11:17).

Ibnu Mardawayhi ameandika kwa njia nyingine kutoka kwa Ali kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake ni mimi. Na na anaifuata na shahidi atokaye kwake ni Ali.”427

SURAT AR-RA’D Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” (Qur’ani Tukufu Sura ­ar-Ra’d; 13:7). Ibnu Jarir, Ibnu Mardawayhi, Daylamiy na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Ilipoteremka Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake na kusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji.’Akaashiria mkono wake kwenye bega la Ali na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji. Kupitia kwako wataongoka wenye kutaka kuongoka baada yangu.”428 Abdullah bin Ahmad ameandika katika Zawaidul-Musnad, Ibnu Abi Hatim, Tabarani katika al-Awsat, al-Hakim katika Sahih yake, na Ibnu Asakir pia, wote wameandika kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema: “Katika aya hii, Mtume wa Mwenyezi Mungu ndio Muonyaji, nami ndiye Mwongozaji.” Na katika kauli ny  Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 12 Uk. 26.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 13 Uk. 97.

427. 428.

335

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 335

2/14/2018 12:12:14 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ingine Mwongozaji ni mtu kutoka kizazi cha Hashim, yaani yeye mwenyewe.429

SURAT IBRAHIM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na mfano wa neno baya ni kama mti mbaya ambao umeng’olewa ardhini hauna uimara.” (Qur’ani Tukufu Sura Ibrahim; 14:25-26).

Imepokewa kutoka kwa Abu Ja’far katika tafsiri ya mti mbaya kwamba ni Bani Umaiya, na mti mzuri ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, Ali, Fatima na watoto wao.430

SURAT AN-NAML Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” (Qur’ani Tukufu Sura an-Naml; 27:43). Jabir amepokea na Muhammad bin Muslim kutoka kwa Abu Ja’far (a.s.) kwamba alisema: “Sisi ndio wenye ukumbusho.”431

SURAT BANI ISRAIL Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” (Qur’ani Tukufu Sura Bani Israil; 17:26).   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 13 Uk. 97.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 13 Uk. 193. 431.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 14 Uk. 134. 429. 430.

336

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 336

2/14/2018 12:12:14 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kutoka kwa as-Asadiy, na ameandika Ibnu Jarir kutoka kwa Ali bin Husain kwamba (a.s.) alimwambia mzee mmoja wa Sham: “Hivi umewahi kusoma Qur’ani?” akajibu ndio. Ali akasema: “Hivi hujasoma katika Surat Israi: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake..”? Mzee akasema: “Hivi nyinyi ndio jamaa wa karibu ambao Mwenyezi Mungu ameamuru wapewe haki yao?!!” Ali akasema: “Ndio sisi.”432

SURAT MARYAM Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.” (Qur’ani Tukufu Sura Maryam; 19:96).

Ibnu Mardawayhi na Daylamiy wameandika kutoka kwa al-Barau kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali bin Abu Talib: “Ewe Ali sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwako na niwekee mapenzi katika nyoyo za waumini.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii. Na Muhammad bin al-Hanafiya alikuwa akisema: Hutampata muumini ila ni yule anayempenda Ali na watu wa nyumba yake.433

SURAT TWAHA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe unatuona.” (Qur’ani Tukufu Sura Twaha; 20:35).   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 15 Uk. 58.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 16 Uk. 130.

432. 433.

337

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 337

2/14/2018 12:12:14 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Mardawayhi, al-Khatib na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Asmau binti Umaysi kwamba alisema: Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu mbele ya Mlima wa Thabir akisema: “Thabir amechomoza, Thabir amechomoza. Ewe Mwenyezi Mungu! Ninakuomba lile alilokuomba ndugu yangu Musa kwamba unipanulie kifua changu. Unifanyie wepesi kazi yangu. Uniondolee fundo katika ulimi wangu. Ifahamike kauli yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Ali. Nitie nguvu kupitia kwake. na umshirikishe katika kazi yangu. Ili tukutukuze sana. Hakika wewe unatuona.”434 Mfano wa hiyo ni ile kauli iliyosihi kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alisema pindi alipompa umakamu juu ya watu wa nyumba yake siku alipokwenda katika Vita vya Tabuk: “Hivi huridhii kwamba wewe nafasi yako kwangu ni ile ya Harun kwa Musa ila ni kwamba hakuna Nabii baada yangu.”435

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ­ chafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa u kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Tirmidhi na Hakim wameandika na kuizingatia kuwa ni riwaya sahihi, na Ibnu Jarir, Ibnu Mundhir, Ibnu Mardawayhi na al-Bayhaqiy katika Sunan yake, wote wameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema: Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 16 Uk. 169.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 16 Uk. 169.

434. 435.

338

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 338

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Sura Ahzab: 33) iliteremkia nyumbani kwangu, na humo alikuwemo Fatima, Ali, Hasan na Husain, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu akawafunika kishamia alichokuwa amejifunika, kisha akasema: “Hawa ndio AhlulBaiti wangu, waondolee uchafu na watakase kabisa.”436 Imekuja katika baadhi ya riwaya kwamba Mtume (s.a.w.w.) a­ litoa mkono wake toka katika kishamiya na kuunyoonsha mbinguni, akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio Ahlul-Baiti na wasiri wangu hivyo waondolee uchafu na watakase kabisa.” Alisema hivyo mara tatu.437 Na katika riwaya nyingine ni kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliwafunika kishamiya cha Khaibar, kisha akaweka mkono wake juu yao kisha akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu.”438 Na katika lafudhi nyingine: “Ewe Mola wangu, shusha rehma zako na baraka zako juu ya aali Muhammad, kama ulivyoziweka juu ya aali Ibrahim, hakika wewe ni Mhimidiwa msifika.”439 “Na katika riwaya aliyoandika Tabarani kutoka kwa Ummu Salama ni kwamba alisema: Nilifunua kishamiya ili niingie pamoja nao lakini Mtume (s.a.w.w) akakivuta toka mikononi mwangu, na akasema: “Hakika wewe upo katika kheri.”440 Na katika riwaya nyingine iliyopokewa na Ibnu Mardawayhi kutoka kwa Ummu Salama ni kwamba alisema: “Je mimi sio katika Ahlul-Baiti wako? Mtume akajibu: “Hakika wewe waelekea katika kheri, hakika wewe ni miongoni mwa wakeze Mtume.”441   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.   438.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14. 439.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14. 440.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14. 441.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14. 436. 437.

339

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 339

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:56). Abdu Razaq, Ibnu Abi Shayba, Imam Ahmad, Abdu bin Hamid, Bukhari, Muslim, Abu Daud, Tirmidhiy, Nasaiy, Ibnu Majah na Ibnu Mardawayhi, wameandika kutoka kwa Ka’bi bin Ajrah, kwamba amesema: “Mtu mmoja alisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ni ipi namna ya kukusalia? Mtume akasema: “Sema:

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim, hakika wewe ni Mhimidiwa Msifika. Ewe Mwenyezi Mungu! mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakika wewe ni Mhimidiwa Msifika.’”442 Imam Ahmad, Bukhari, Nasaiy, Ibnu Majah na wengineo, wameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: Tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama sala tutakusaliaje? Akasema: ‘Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad mja wako na Mtume wako kama ulivyomrehemu Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim.”’443   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 72.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 72

442. 443.

340

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 340

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Imam Ahmad, Abdu bin Hamid na Ibnu Mardawayhi, wameandika kutoka kwa Ibnu Burayda kwamba alisema: “Tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama sala tutakusaliaje? Akasema: ‘Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Shusha rehema zako na baraka zako juu ya Muhammad na juu ya aali Muhammad, kama ulivyoziweka juu ya Ibrahim, hakika wewe ni Mhimidiwa Msifika.”’444

SURAT AZ-ZUMAR Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na aliyeleta ukweli na aliyeusadikisha, hao ndio wamchao (Mwenyezi Mungu)” (Sura 33). Ibnu Jarir, al-Barudiy na Ibnu Asakir kwa njia ya Usayd bin Swaf’wan, wameandika kutoka kwa Ali (a.s.). Na Abu As’wad, ­Mujahid na jamaa miongoni mwa Ahlul-Baiti wamesema kwamba: Aliyeusadikisha ni Ali (a.s.).445

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23). Makusudio ya ndugu zake (s.a.w.w.) hapa ni Ali, Fatima na watoto wake (a.s.), na zimepokewa riwaya za kuvushwa kuhusu hilo. Ibnu al-Mundhir, Ibnu Abi Hatim, Tabarani na Ibnu Mardawayhi wameandika kupitia njia ya Ibnu Jubair kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Ilipoteremka: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” walisema: Ewe   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 72.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 24 Uk. 3.

444. 445.

341

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 341

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni akina nani hawa karaba zako ambao tunapasa kuwapenda? Akasema: “Ni Ali, Fatima na watoto wao wawili.”446 Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Abu Daylam kwamba alisema: Alipoletwa Ali bin Husein (a.s.) na hali ni mateka na kusimamishwa katika barabara kuu ya Damascus alisimama mzee mmoja kati ya watu wa Sham, akasema: ‘Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye amewauwa na kuwang’oeni.’ Ali bin Husein radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu ndio. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’ Akajibu ndio nimewahi kusoma. Akasema (a.s.): ‘Hujawahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...”’ Mzee akasema: ‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’”447 Dhadhan alipokea kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema: “Katika Aali Hamim (Sura Shura) kuna Aya inayotuhusu, hatupendi sisi ila muumini.” Kisha akasoma Aya hii: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” Na hili ndilo aliloashiria Kumayti katika shairi lake aliposema: “Tumewakuta mmo ndani ya Aya ya Aali Hamim, ameifasiri hivyo aliye mchamungu na mwarabu kati yetu.”448 Ibnu Habban na Hakim wameandika kutoka kwa Abu Said kwamba alisema: “Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, hakuna mtu atakayetuchukia sisi Ahlul-Baiti ila ni lazima Mwenyezi Mungu atamwingiza motoni.”449   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 28.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 28. 448.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 29. 449.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 29. 446. 447.

342

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 342

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURA MUHAMMAD Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na ndio Mwenyezi Mungu amewalaani na amewatia uziwi na ame-wapofusha macho yao.” (Qur’ani Tukufu Sura Muhammad; 47:23). Hakuna kizuizi katika kumlaani Yazid kutokana na wingi wa sifa zake

chafu na kutenda kwake madhambi makubwa muda wote wa utu uzima wake. Inakutosha lile alilowafanyia watu wa Madina na Makka, amepokea Tabarani kwa njia hasan kwamba Mtume alisema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Atakayewadhulumu wakazi wa Madina na kuwasababishia khofu, laana za Mwenyezi Mungu, Malaika na watu wote zitakuwa juu yake, haitakubaliwa fidia wala badala kutoka kwake.” Na msiba mkubwa ni kile kitendo alichowafanyia Ahlul-Baiti (a.s.) na kuridhia kuuawa Husain (a.s.) na kufurahia kitendo hicho, na kumdhalilisha yeye na watu wa nyumba yake, kama maana hiyo ilivyo mutawatiri. Jamaa miongoni mwa ulamaa wameamini na kutamka wazi kwamba inasihi kumlaani, miongoni mwao ni Hafidh Nasrus-Sunnah Ibnu al-Jawziy, na kabla yake ni al-Qadhiy Abu Ya’la. Allama Taftazaniy amesema: “Hatusiti kuhusu jambo lake, bali ni kuhusu imani yake, laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake na juu ya watetezi wake na wasaidizi wake.”450   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 26 Uk. 66. Anayetaka kwa undani suala la Yazid bin Muawiya kulaaniwa arejee kitabu Ar-Raddu ‘Alal-Muta’aswib al-‘Anid cha Hafidh Abul Faraj aliye mashuhuri kwa jina la Ibnu al-Jawziy, aliyefariki mwaka 597 A.H.

450.

343

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 343

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AR-RAHMAN Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili. Baina yao kuna kizuizi haziingiliani. Basi nyinyi wawili mnakataa neema gani ya Mola wenu Mlezi? Katika hizo mbili hutoka lulu na marijani.” (Qur’ani Tukufu Sura ar-Rahman; 55:19-22).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Asakir kwamba alisema kuhusu: “Amezikutanisha bahari mbili.” ni Ali na Fatima. “Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.” ni Mtume (s.a.w.w.) “Katika hizo mbili hutoka lulu na marijani.” Ni Hasan na Husein.” Nionalo mimi451 ni kwamba kauli hiyo ikisihi basi si miongoni mwa tafsiri bali ni taawili kama taawili nyingi za masufi katika Aya mbalimbali. Kwangu mimi wote Ali na Fatima ni watu adhimu mno kushinda bahari kuu kielimu na kifadhila, na pia wote wawili Hasan na Husain ni wazuri na wenye kung’ara kushinda lulu na marijani kwa kiwango ambacho kimevuka kipimo cha hesabu.452

SURAT AL-WAQIA’ Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Waliotangulia ndio waliotangulia.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Waqia’; 56:10).   Yaani mwandishi wa tafsiri hii.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 93.

451. 452.

344

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 344

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba: “Iliteremka kwa ajili ya Ezekiel muumini wa aali Firaun, Habib Najar ambaye katajwa katika Sura Yasin, na Ali bin Abu Talib (a.s.)”453

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Al-Hakim ameiandika na kuizingatia kuwa ni sahihi, Ibnu ­al-Mundhir, Abdu bin Hamid na wengineo, wote wameandika ­kutoka kwa Amirul-Muuminina (a.s.) kwamba alisema: “Hakika ­katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna ­yeyote ­aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nayo ni Aya ya kusema siri na Mtume: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana…..” nilikuwa nina dinari nikazibadili kwa dirhamu, hivyo nikawa kila nisemapo siri na Mtume natoa dirhamu moja kabla ya kusema naye siri, kisha ikafutwa na hakuna yeyote aliyeifanyia kazi.”454   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 114.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 28.

453. 454.

345

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 345

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AT-TAGHABUN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, na kwa ­Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura ­at-Taghabun; 64:15).

Imam Ahmad, Abu Daud, Tirmidhiy, Nasaiy, Ibnu Majah na Hakim ambaye ameizingatia kuwa ni sahihi, wote wameandika kutoka kwa Buraida kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akitoa hotuba na ghafla wakaja Hasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuamka, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akateremka toka mimbarini akawafuata na kuwabeba kila mmoja katika bega lake, kisha akapanda juu ya mimbari na kusema: ‘Mwenyezi Mungu amesema kweli. Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, hakika mimi nilipowaona hawa wawili wakitembea na wakidondoka sikuweza kuvumilia mpaka nikakatisha mazungumzo yangu na nikashuka kwenda kuwachukua.”455 Na katika riwaya ya Ibnu Mardawayhi kutoka kwa Abdullah bin Umar ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipokuwa akiwahutubia watu juu ya mimbari, Husain bin Ali alitokeza na kuanza kwenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) ndipo akakanyaga nguo yake aliyokuwa amevaa na akawa amedondoka na kuanza kulia, basi Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akateremka toka juu ya mimbari, watu walipomuona amefanya hivyo walimkimbilia Husain na kuanza kumbembeleza mpaka akafika mikononi mwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na kusema:   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 111.

455.

346

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 346

2/14/2018 12:12:15 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

“Mwenyezi Mungu amuuwe shetani, hakika mtoto ni mtihani, naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake sikuweza kujizuia456 hakika nimeteremka kutoka mimbarini kwangu.”457

SURAT AL-HAQQA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Haqqa; 69:12).

Katika habari ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali (a.s.): “Hakika mimi nilimwomba Mwenyezi Mungu alifanye hivyo sikio lako ewe Ali.’’ Amirul-Mu’minin Ali (a.s.) alisema: “Baada ya hapo sikuwahi kusahau chochote na wala sikupasa kusahau.”

SURAT AL-INSAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu   Katika maelezo ya Juz. 27 Uk. 112 Alusiy amesema: “Sijui ingekuwaje lauMtume wa Mwenyezi Mungu angeiona hali ya Husain (a.s.) katika tukio laKarbala, sijui angefanya nini? Kwa kweli laana ya Mwenyezi Mungu, Malaikazake, Mitume wake na watu wote iwe juu ya yule aliyeamuru yale yaliyotokea,aliyerusha vimondo, kuwasha moto na akaridhia au kuongeza jeshi. 457.   Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 111. 456.

347

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 347

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Insan; 76:8-9).

Riwaya ya Atau kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Hakika Hasan na Husein walipatwa na maradhi, babu yao Muhammad (s.a.w.w.) alikwenda kuwaona, na masahaba nao pia walikwenda kuwaona. Wakasema kumwambia Ali: “Ewe Abu Hasan! Ni bora kama ungeweka nadhiri juu ya watoto wako.” Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhiri kwamba ikiwa watapona watafunga siku tatu kumshukuru Mwenyezi Mungu. Vijana wawili wakapata afya njema na hali nyumbani kwa aali Muhammad hawana kitu si kichache wala kingi. Ndipo Ali akaenda kwa Simon Myahudi wa Khaibari, akakopa toka kwake pishi tatu za ngano. Akaja nazo na Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano kulingana na idadi yao. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume Sala ya Magharibi alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, mara masikini akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni maskini katika watoto wa umma wa kiislamu, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa na wao wakalala bila kuonja kitu ila maji, na siku ya pili wakaamka wakiwa na funga. Ilipofika siku ya pili Fatima akachukua pishi jingine akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) Sala ya Magharibi alikwenda nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, mara akafika mlangoni kwao yatima akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, yatima toka katika watoto wa muhajirana, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa chakula na wakashinda siku mbili mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji, na siku ya tatu wakaamka wakiwa na funga. 348

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 348

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Ilipofika siku ya tatu Fatima akachukua pishi la tatu akatwanga na kuoka mikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) Sala ya Magharibi alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, mara mfungwa wa kivita akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni mateka wa Muhammad, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula.” Wakampa chakula na wakashinda siku tatu mchana kutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji. Ilipofika siku ya nne Ali alimshika mkono Hasan na Husein na kwenda nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), alipowaona (s.a.w.w.) wakitetemeka kama vifaranga kutokana na ukali wa njaa, alisema: “Ewe Abal-Hasan! Hali niionayo kwenu yaniumiza mno.” Akasimama na kwenda nao kwa Fatima (a.s.), wakamkuta akiwa mihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake na macho yake yamebadilika kutokana na ukali wa njaa. Huruma ikamuingi Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na ikamuumiza hali hiyo, ndipo Jibril (a.s.) akateremka na kusema: “Ewe Muhammad pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Mtume akasema: “Nichukue nini ewe Jibril?” Jibril (a.s.) akamsomea Surat Insan.458

Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 29 Uk. 157.

458.

349

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 349

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA AL-QASIMIY, INAYOITWA MAHASINUT-TAAWIL SURAT AALI IMRAN Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Qur’ani Tukufu Sura Aali-Imran; 3:61).

Hafidh Abu Bakr bin Mardawayhi amepokea kutoka kwa Sha’abiy kutoka kwa Jabir kwamba amesema: Aqib na Tayib walikwenda kwa Mtume (s.a.w.w.), naye akawaomba wafanye maapizano, wakamwahidi wafanye maapizano naye kesho yake, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoka na hali amewashika mkono Ali, Fatima, Hasan na Husain, kisha akawatumia ujumbe waje lakini wakakataa na hatimaye wakakubali kutoa kodi. Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Naapa kwa yule aliyenituma kwa haki! Lau wangesema la, basi bonde lao lingeteketea kwa moto.”

350

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 350

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

Jabir anasema: Na kwa ajili ya hao iliteremka Aya hii: “Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Sura Aali Imran: 61). “….. nafsi zetu na nafsi zenu” ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Ali. “….. watoto wetu” ni Hasan na Husein. “…..wanawake zetu” ni Fatima. Hakim ameipokea kwa kuvushwa katika Mustadrak kutoka kwa Sha’bah kutoka kwa Mughira. Na hii ni sahihi zaidi.459

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:3).

Ibnu Mardawayhi amepokea kwa njia ya Abu Harun al-‘Abdiy kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba ilimteremkia Mtume wa Mwenyezi Mungu Siku ya Ghadir Khum pale aliposema kuhusu Ali: “Yule ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.” Kisha ameipokea kutoka kwa Abu Huraira na katika maelezo yake ni kwamba ilikuwa ni siku ya kumi na nane ya Mfunguo tatu.460   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 2 Uk. 71.   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 7 Uk. 34.

459. 460.

351

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 351

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT AL-MAIDA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Maida; 5:55).

Mpaka baadhi yao katika tendo hili wametaja athari inayomhusu Ali bin Abu Talib kwamba: Hakika Aya hii iliteremka kwa ajili yake, muombaji alipita kwake na hali akiwa katika rukuu yake ndipo akampa pete yake.461

SURAT AT-TAWBA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na ni tangazo litokalo kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kwa watu Siku ya Hija kubwa.” (Qur’ani Tukufu Sura at-Tawba; 9:3).

Ibnu Is’haqa amepokea kwa sanadi yake kutoka kwa Abu Ja’far Muhammad bin Ali (a.s.) kwamba ilipoteremka Sura Baraa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na alikuwa tayari ameshamtuma Abu Bakr akaongoze Hija, ndipo akaambiwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu ni vizuri lau ungemtuma nayo Abu Bakr. Akasema: “Hatekelezi kwa niaba yangu ila mtu toka katika Ahlul-Baiti wangu.” Kisha akamwita Ali bin Abu Talib na kumwambia: “Nenda na kisa hiki kuanzia mwan  Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 7 Uk. 156.

461.

352

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 352

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

zo wa Sura Baraa, na nenda kawatangazie watu siku ya kuchinja pindi watakapokusanyika huko Mina, kwamba kafiri haingii peponi, baada ya mwaka huu haruhusiwi Mushriku kuhiji, haruhusiwi kutufu akiwa uchi, na yule ambaye ana mkataba na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) utaendelea mpaka mwisho wa muda wake.”462 Imenukuliwa kwamba Bani Umaiyya walikuwa wakimtukana Ali katika hotuba zao, na ukhalifa ulipoangukia mikononi mwa Umar bin Abdul-Aziz aliondoa kipengele hicho (cha kumlaani Ali) na kuweka badala yake Aya hii. Nasir amesema: “Huenda Aya hii kuwekwa badala ya kashfa hizo ilikuwa ni kutokana na kuoana kati ya maana yake ambayo ni kukataza uovu na ile hadithi inayosema kwamba kumfanyia uadui Ali ni uovu, kwani Mtume (s.a.w.w.) alimwambia Ammar aliyekuwa katika jeshi la Ali: “Litakuuwa kundi ovu.” Naye akauawa akiwa pamoja na Ali (a.s.) Siku hiyo ya Siffin.463

SURAT AL-AHZAB Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ­ chafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa u kabisa.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Ahzab; 33:33).

Mtume (s.a.w.w.) aliwakusanya Fatima, Ali, Hasan na Husain, kisha akawafunika kishamiya alichokuwa amejifunika, kisha akasema: “Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu, waondolee uchafu.”464   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 8 Uk. 85.   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 10 Uk. 543. 464.   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 13 Uk. 506. 462. 463.

353

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 353

2/14/2018 12:12:16 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

SURAT ASH-SHURA Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Qur’ani Tukufu Sura ash-Shura; 42:23). Katika Sahih Bukhari imepokewa kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba aliulizwa kuhusu “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” Said bin Jubair akasema: Ndugu ni aali Muhammad.465 Na aliyoipokea Ibnu Abi Hatim ni kwamba ilipoteremka Aya hii walisema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni akina nani hawa ambao Mwenyezi Mungu ameamuru tuwapende? Akasema: “Ni ­Fatima na kizazi chake.”466

SURAT AL-MUJADILA Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (Qur’ani Tukufu Sura al-Mujadila; 58:12).

Imepokewa kutoka kwa Mujahidu kwamba alisema: “Ali bin Abu Talib (radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee) alisema: ­“Hakika ka  Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 14 Uk. 172.   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 14 Uk. 172.

465. 466.

354

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 354

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

tika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu.”467 Na imepokewa pia kutoka kwake (Mujahid) kwamba ­alisema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe ­sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib (radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee), alitoa sadaka ya dinari. Ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka).”468 Na mwisho wa maombi yetu ni kumshukuru Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe wote.

Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 16 Uk. 55.   Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 16 Uk. 55.

467. 468.

355

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 355

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

ORODHA YA VITABU VILIVYO ­ ­CHAPISHWA NA AL-ITRAH FOUNDATION: 1. 2. 3. 4. 5. 6. 7. 8. 9. 10. 11. 12. 13. 14. 15. 16. 17. 18. 19. 20. 21. 22. 23. 24. 25. 26.

i) Qur’ani Tukufu – Pamoja na Tarjuma ya Kiswahili ii) Qur’an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka Thelathini Uharamisho wa Riba Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Kwanza Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Pili Hekaya za Bahlul Muhanga wa Imamu Husein (A.S.) Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (a.s.) Hijab vazi Bora Ukweli wa Shia Ithnaashari Madhambi Makuu Mbingu imenikirimu Abdallah Ibn Saba Khadijatul Kubra Utumwa Umakini katika Swala Misingi ya Maarifa Kanuni za Ndoa na maadili ya Familia Bilal wa Afrika Abudhar Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu Salman Farsi Ammar Yasir Qur’an na Hadithi Elimu ya Nafsi Yajue Madhehebu ya Shia Ukusanyaji na Uhifadhi wa Qur’an Tukufu 356

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 356

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

27. 28. 29. 30. 31. 32. 33. 34. 35. 36. 37. 38. 39. 40. 41. 42. 43. 44. 45. 46. 47. 48. 49. 50. 51. 52. 53. 54. 55. 56. 57.

Al-Wahda Ponyo kutoka katika Qur’an Uislamu mfumo kamili wa maisha ya kijamii Mashukio ya Akhera Al Amali Dua kwa Mujibu wa Ahlulbayt (a.s) Udhuu kwa Mtazamo wa Qur’ani na Sunna Haki za wanawake katika Uislamu Mwenyezi Mungu na sifa zake Kumswalia Mtume (s) Nafasi za Ahlul Bayt (a.s) Adhana Upendo katika Ukristo na Uislamu Qur’ani na Kuhifadhiwa Kwake Maana ya laana na kutukana katika Qur’ani Tukufu Kupaka juu ya khofu Kukusanya Sala Mbili Bismillah ni sehemu ya Qur’ani na husomwa kwa Jahara Kuwaongoza vijana wa kizazi kipya Kusujudu juu ya udongo Kusheherekea Maulidi Ya Mtume (s) Tarawehe Malumbano baina ya Sunni na Shia Kupunguza Swala safarini Kufungua safarini Umaasumu wa Manabii Qur’an Yatoa Changamoto as-Salaatu Khayrun Mina -’n Nawm Uadilifu wa Masahaba Dua e Kumayl Sauti Ya Uadilifu wa Binadamu 357

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 357

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

58. Umaasumu wa Mitume - Faida Zake Na Lengo Lake 59. Umaasumu wa Mitume - Majibu Ya Aya Zenye Utata 60. Umaasumu wa Mitume - Umaasumu wa Mtume Muhammad (s) 61. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Kwanza 62. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Pili 63. Kuzuru Makaburi 64. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Kwanza 65. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Pili 66. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tatu 67. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Nne 68. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tano 69. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Sita 70. Tujifunze Misingi Ya Dini 71. Sala ni Nguzo ya Dini 72. Mikesha Ya Peshawar 73. Malezi Ya Mtoto Katika Uislamu 74. Ubora wa Imam ‘Ali na Ushia ndio njia iliyonyooka 75. Hukumu za Kifikihi zinazowahusu Wanawake 76. Liqaa-u-llaah 77. Muhammad (s) Mtume wa Allah 78. Amani na Jihadi Katika Uislamu 79. Uislamu Ulienea Vipi? 80. Uadilifu, Amani na Mtume Muhammad (s) 81. Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtume Muhammad (s) 82. Urejeo (al-Raj’ah) 83. Mazingira 84. Utokezo (al - Badau) 85. Hukumu ya kujenga juu ya makaburi 86. Swala ya maiti na kumlilia maiti 87. Uislamu na Uwingi wa Dini 358

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 358

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

88. 89. 90. 91. 92. 93. 94. 95. 96. 97. 98. 99. 100. 101. 102. 103. 104. 105. 106. 107. 108. 109. 110. 111. 112. 113. 114. 115. 116. 117. 118.

Mtoto mwema Adabu za Sokoni Na Njiani Johari za hekima kwa vijana Maalimul Madrasatain Sehemu ya Kwanza Maalimul Madrasatain Sehemu ya Pili Maalimul Madrasatain Sehemu ya Tatu Tawasali (AT- TAWASSUL) Imam Mahdi katika Usunni na Ushia Hukumu za Mgonjwa Sadaka yenye kuendelea Msahafu wa Imam Ali Maimamu wa Ahlul Bait – Ujumbe na Jihadi Idi Al-Ghadir Kusoma sura zenye Sijda ya wajibu Hukumu zinazomuhusu mkuu wa kazi na Mfanyakazi Huduma ya Afya katika Uislamu Sunna za Nabii Muhammad (saww) Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Kwanza) Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Pili) Shahiid Mfiadini Mwanamke Na Sharia Ujumbe -Sehemu ya Kwanza Ujumbe - Sehemu ya Pili Ujumbe - Sehemu ya Tatu Ujumbe - Sehemu ya Nne Mariamu, Yesu na Ukristo kwa mtazamo wa Kiislamu Hadithi ya Thaqalain Ndoa ya Mutaa Ukweli uliopotea sehemu ya Kwanza Ukweli uliopotea sehemu ya Pili Ukweli uliopotea sehemu ya Tatu 359

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 359

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

119. Ukweli uliopotea sehemu ya Nne 120. Ukweli uliopotea sehemu ya Tano 121. Mkutano wa Maulamaa wa Baghdad 122. Safari ya kuifuata Nuru 123. Fatima al-Zahra 124. Myahudi wa Kimataifa 125. Kuanzia ndoa hadi kuwa Wazazi 126. Visa vya kweli sehemu ya Kwanza 127. Visa vya kweli sehemu ya Pili 128. Elimu ya Ghaibu ya Maimamu 129. Mwanadamu na Mustakabali wake 130. Imam Ali (‘a) Ndugu wa Mtume Muhammad (s) (Sehemu ya Kwanza) 131. mam Ali (‘a) Ndugu wa Mtume Muhammad (s) (Sehemu ya Pili) 132. Khairul l’Bariyyah 133. Uislamu na mafunzo ya kimalezi 134. Vijana ni Hazina ya Uislamu 135. Adhana ni Ndoto au ni Wahyi? 136. Tabaruku 137. Saada Kamili – Kitabu cha Kiada cha Maadili 138. Vikao vya furaha 139. Shia asema haya Sunni asema haya Wewe wasemaje? 140. Visa vya wachamungu 141. Falsafa ya Dini 142. Kuhuzunika na Kuomboleza 143. Sunna katika Kitabu Fiqhi al-Sunnah 144. Mjadala wa Kiitikadi 145. Kuonekana kwa Allah 146. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Kwanza) 147. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Pili) 360

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 360

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

148. 149. 150. 151. 152. 153. 154. 155. 156. 157. 158. 159. 160. 161. 162. 163. 164. 165. 166. 167. 168. 169. 170. 171. 172. 173. 174. 175. 176. 177. 178.

Ndugu na Jirani Ushia ndani ya Usunni Maswali na Majibu Mafunzo ya hukmu za ibada Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 1 Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 2 Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 3 Abu Huraira Vipengee kadhaa katika Swala ya Jamaa na Msikiti. Mazingatio kutoka katika Qur’an - Sehemu ya Kwanza Mazingatio kutoka kaitka Qur’an - Sehemu ya Pili Mazingatio kutoka katika Uislamu - Sehemu ya kwanza Mazingatio kutoka katika Uislamu - Sehemu ya Pili Shia na Qur’ani – Majibu na Maelezo Falsafa ya Mageuzi ya Imam Husein (a.s) Amali za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Elimu ya Tiba za Kiislamu - Matibabu ya Maimamu Uislamu Safi Majlisi za Imam Husein Majumbani Je, Kufunga Mikono Uislam wa Shia Amali za Makka Amali za Madina Asili ya Madhehebu katika Uislamu Sira ya Imam Ali kuhusu Waasi Ukweli uliofichika katika neno la Allah Uislamu na Mifumo ya Uchumi Umoja wa Kiislamu na Furaha Mas’ala ya Kifiqhi Jifunze kusoma Qur’ani as-Sahifatul Kamilah as-Sajjadiyyah 361

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 361

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

179. Hayya ‘Alaa Khayri’l-’Amal Katika Adhana 180. Ukweli kuhusu Funga ya Siku ya Ashura 181. Dua za Miezi Mitatu Mitukufu (Rajabu, Shaabani na Ramadhani) 182. Uadilifu katika Uislamu 183. Mahdi katika Sunna 184. Maswali Ya Uchunguzi Kuhusu Uislam 185. Kazi na Bidii ni njia ya maendeleo 186. Abu Talib – Jabali Imara la Imani 187. Ujenzi na Utakaso wa Nafsi 188. Vijana na Matarajio ya Baadaye 189. Historia maana na lengo la Usalafi 190. Ushia – Hoja na Majibu 191. Mateso ya Dhuria wa Mtume (saww) 192. Maombolezo – Msiba wa Bwana wa Mashahidi (a.s.) 193. Shahidi kwa Ajili ya Ubinadamu 194. Takwa 195. Upotoshaji Dhahiri katika (Turathi) Hazina ya Kiislamu 196. Amirul Muuminina (as) na Makhalifa 197. Tawheed Na Shirki 198. Kuvunja hoja iliyotumika kutetea Uimamu wa AbuBakr 199. Adabu za vikao na mazungumzo 200. Hija ya Kuaga 201. Uwazi baina ya Maslahi na Vikwazo 202. Fadhila za watukufu watano katika Sahih Sita 203. Mdahalo baina ya Mwanachuoni waKisunni na Kishia (Al- Muraja’aat) 204. Utawala na Uendeshaji katika Sera ya Imam Ali (as) 205. Imam Husain ni Mfumo wa Marekebisho na Mageuzi 206. Mtazamo kuhusu msuguano wa Kimadhehebu 207. Nchi na Uraia – Haki na wajibu kwa Taifa

362

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 362

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

208. Mtazamo wa Ibn Taymiyyah juu ya Imam Ali (as) 209. Uongozi wa Kidini – Maelekezo na Utekelezaji wa Kijamii 210. Maadili ya Ashura 211. Mshumaa – Shahidi na Kifo cha Kishahidi 212. Mizani ya Hekima – Hadithi za Ahlul Bait (as) – Sehemu ya Kwanza 213. Imam Ali na Mambo ya Umma 214. Imam Ali na Mfumo wa Usawa 215. Uimamu na Tamko la Kutawazwa 216. Mfumo wa Wilaya 217. Vipi Tutaishinda Hofu? 218. Kumswalia Mtume ni Ufunguo wa Utatuzi wa Matatizo 219. Maeneo ya Umma na Mali Zake 220. Nahju ‘L-Balagha– Majmua ya Khutba, Amri, Barua, R­isala, Mawaidha na Semi za Amirul-Muuminin Ali bin Abu Talib (a.s.) 221. Mukhtar – Shujaa aliyelipiza kisasi dhidi ya wauaji wa Imam Husein (as) hapo Karbala 222. Mazingatio Katika Swala 223. Imam Hasan na Mfumo wa Kujenga Jamii 224. Vyakula Na Vinywaji 225. Kuelewa Rehema ya Mwenyezi Mungu 226. Imam Mahdi na Bishara ya Matumaini 227. Mtazamo Mpya - Wanawake katika Uislamu 228. Shia Na Sahaba - Majibu na Maelezo 229. Majanga Na Jukumu la Jamii 230. Shia Na Hadith - Majibu na Maelezo 231. Upotofu Ndani ya Kitabu cha Mitaala kwa Shule za Sekondari 232. Ugaidi Wa Kifikra Katika Medani Ya Kidini 233. Yafaayo kijamii 234. Uswalihina Dhahiri Na Batini Yake 235. Mkakati wa Kupambana na Ufakiri 363

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 363

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

236. Mwanamke Katika Harakati Za Mageuzi 237. Jihadi 238. Hija Katika Maneno Na Ujumbe Wa Imam Khomeini (R.A) 239. Tiba Ya Maradhi Ya Kimaadili 240. Yusuf Mkweli 241. Taqiyya Kwa Mujibu Wa Sheria Ya KIISLAMU 242. Imam Mahdi (A.S) Imam Wa Zama Hizi Na Kiongozi Wa Dunia 243. Talaka Tatu 244. Safari Ya Kuelekea Kwa Mwenyezi Mungu 245. Hotuba Za Kiislamu Juu Ya Haki Za Binadamu 246. Mashairi Ya Kijamii 247. Ngano Ya Kwamba Qur’ani Imebadilishwa 248. Wito Kwa Waumini: “Enyi Mlioamini” 249. Imam Husain (a.s) ni Utu na Kadhia 250. Imam Husain ni Kielelezo cha Kujitoa Muhanga na Fidia 251. Imam Mahdi ni Tumaini la Mataifa 252. Kuchagua Mchumba 253. Mazungumzo ya Umoja – Ukosoaji na Usahihishaji 254. Utamaduni wa Mwamko wa Kijamii 255. Hekima za kina za Swala 256. Kanuni za Sharia za Kiislamu 257. Utamaduni kufuatana na Qur’ani na Utekelezaji wa Kivitendo (Sehemu ya Kwanza) 258. Kauli sahihi zaidi katika kufafanua Hadithi

364

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 364

2/14/2018 12:12:17 PM


AHLUBAYT NDANI YA TAFSIRI ZA KISUNNI

KOPI ZIFUATAZO ZIMETAFSIRIWA KWA LUGHA KINYARWANDA 1. Amateka Na Aba’ Khalifa 2. Nyuma yaho naje kuyoboka 3. Amavu n;amavuko by;ubushiya 4. Shiya na Hadithi 5. Kor’ani Nziranenge 6. Kwigisha Mu Buryo Bw’incamake Uka Salat Ikotwa 7. Iduwa ya Kumayili

ORODHA YA VITABU VILIVYO CHAPISHWA NA AL-ITRAH FOUNDATION KWA LUGHA YA KIFARANSA 1. Livre Islamique

365

AHLUBAYT 14_February_2018.indd 365

2/14/2018 12:12:17 PM


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.