Ujenzi na utakaso wa nafsi

Page 1

UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Mwandishi: Dkt. Muhammad Ali Shomali

Kimetarjumiwa na: Salman Shou

Kimehaririwa na: Al-Hajj Ramadhani S. K. Shemahimbo

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 1

7/10/2013 3:33:20 PM


‫ﺗﺮﲨﺔ‬ ‫ﺗﺮﲨﺔ‬

‫ﺗﺮﲨﺔ‬ ‫تقويم النفس و تزكيتھا‬

‫تزكيتھا‬ ‫و‬ ‫النفس‬ ‫تقويم‬ ‫تقويم النفس و تزكيتھا‬ ‫ﺗﺄ ﻟﻴﻒ‬

‫محمد علي شومالي‬

‫ﻟﻴﻒ‬ ‫ﺗﺄﺗﺄ ﻟﻴﻒ‬

‫ﻣﻦ ﺍﻟﻠﻐﺔ ﺍﻹﳒﻠﻴﺰﻳﺔ ﺍﱃ ﺍﻟﻠﻐﺔ ﺍﻟﺴﻮﺍ ﺣﻠﻴﺔ‬

‫شومالي‬ ‫علي شومالي‬ ‫محمد علي‬ ‫محمد‬

‫‪2‬‬

‫ﺍﻟﺴﻮﺍﺣﻠﻴﺔ‬ ‫ﺍﻟﻠﻐﺔﺍﻟﺴﻮﺍ‬ ‫ﺍﱃ ﺍﻟﻠﻐﺔ‬ ‫ﺍﻹﳒﻠﻴﺰﻳﺔ ﺍﱃ‬ ‫ﺍﻟﻠﻐﺔ ﺍﻹﳒﻠﻴﺰﻳﺔ‬ ‫ﺣﻠﻴﺔ‬ ‫ﻣﻦﻣﻦﺍﻟﻠﻐﺔ‬ ‫ﻣﻦ اﻟﻠﻐﺔ اﻟﻌﺮﺑﻴﺔ إﻟﻰ اﻟﻠﻐﺔ اﻟﺴﻮاﺣﻠﻴﺔ‬ ‫‪ ‬‬ ‫‪7/10/2013 3:33:23 PM‬‬

‫‪09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 2‬‬


©Haki ya kunakili imehifadhiwa na: AL-ITRAH FOUNDATION

ISBN: 978 - 9987 - 17 - 037 - 1

Kimeandikwa na: Dkt. Muhammad Ali Shomali

Kimetarjumiwa na: Salman Shou

Kimehaririwa na: Al-Hajj Ramadhani S. K. Shemahimbo

Kimepangwa katika Kompyuta na: Al-Itrah Foundation

Toleo la kwanza: Septemba, 2013 Nakala: 1000

Kimetolewa na kuchapishwa na: Alitrah Foundation S.L.P. - 19701, Dar es Salaam, Tanzania Simu: +255 22 2110640 / 2127555 Barua Pepe: alitrah@yahoo.com Tovuti: www.ibn-tv-com Katika mtandao: w.w.w.alitrah.info

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 3

7/10/2013 3:33:23 PM


09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 4

7/10/2013 3:33:23 PM


Yaliyomo Tahariri................................................................................ 01 Neno la Mchapishaji............................................................ 06 Ujenzi na Utakaso wa Nafsi................................................. 08 Njia tofauti za kimbinu kwenye mambo ya kiroho............ 21 Matendo mbalimbali ya kiroho........................................... 29 Kutupia macho mchakato wa Ujenzi wa Nafsi.................... 39 Maelekezo ya kivitendo juu ya safari ya Kiroho................. 61 Ushauri wa kivitendo wa kushirikisha sifa hizi katika maisha yako.............................................................. 77 Dhana za msingi katika utakatifu wa Kiislamu.................. 80 Upendo, Shukurani na unyenyekevu................................. 80 Matokeo ya Safari ya Kiroho............................................. 103

v

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 5

7/10/2013 3:33:23 PM


09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 6

7/10/2013 3:33:23 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Tahariri

K

itabu hiki ni mkusanyiko wa makala saba juu ya utakaso wa nafsi kutoka kwenye majarida ya Message of Thaqalayn yanayochapishwa na Ahlul-Bayt World Assembly na Kituo cha Kiislam cha Uingereza. Ninaamini kwamba wasomaji watatusaidia kwa kutuletea maoni yao ya thamani kwa kutuandikia kupitia barua pepe alitrah@yahoo.com Taasisi ya Al-Itrah Foundation inajihisi kuwa na wajibu wa kuwasilisha mafundisho ya Uislam kwa jumla na ya Madhehebu ya Ahlul-Bayt kwa umakhsusi hasa yote kwa uaminifu na usahihi hasa na kwa wakati huohuo kutilia mkazo sana katika yale mas’ala ya jumla yanayotuunganisha Waislam wote pamoja. Katika kitabu hiki tunawasilisha makala saba zilizoandikwa na Dr. Mohamed Shomali zenye vichwa vya habari kama ifuatavyo: 1. UMUHIMU WA KUJIDHIBITI NA UTAKASO WA NAFSI Katika makala hii ulazima na umuhimu wa kujidhibiti na utakaso wa nafsi katika hali ya kiroho ndani ya Uislam imesisitizwa sana. Yeye anajadili kwamba hatuwezi kujiendeleza binafsi kwa kufanya yale tunayopenda. Kwa kutumia namna fulani ya udhibiti, tunaweza kubadilisha nafsi zetu kutoka kwenye ile ambayo inapendelea tamaa mbaya na kuwa nafsi yenye hamu na tamaa ya mambo mema na mazuri tu. Kwa kujizoesha na kujitakasa, nafsi zetu zenyewe zinakuwa wasaidizi na waandamizi kwetu sisi katika safari yetu ya kiroho. Kazi kubwa ya mitume na 1

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 1

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

hususan Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ilikuwa ni kuwasaidia watu kujitakasa wenyewe. Njia moja kuu ya kujitakasa ni mtu kujitolea pesa zake mwenyewe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ili kuondokana na kufungamana sana na maisha ya kidunia – uyakinifu. 2. NJIA TOFAUTI ZA KIMBINU KWENYE MAMBO YA KIROHO Katika Makala hii ya pili Hujjatul-Islam Mohammad Ali Shomali anachunguza njia zilizotwaliwa na wanachuoni wa Kiislam katika kuchunguza hali ya kiroho kwa ujumla wake na hususan tabia njema (akhlaq) yaani mtazamo wa kifalsafa, mtazamo wa kisufii na mtazamo wenye misingi ya maandiko. Akilinganisha mitazamo hii mitatu, anajadili kwamba mtazamo wa sawa na unaotosheleza ni lazima uzingatie manufaa ya kila mmoja kati ya mitatu hiyo na uwe kiunganishi cha yote. 3. MATENDO MBALIMBALI YA KIROHO Katika Makala ya tatu, mwandishi anachambua njia tatu tofauti ambazo Qur’ani na Hadith zimechukulia mchakato wa uendelezaji wa nafsi na kuelezea bidii na juhudi ya mwanadamu katika kupata uchamungu na hali ya kiroho. Hali ya kiroho au mchakato wa kuijenga nafsi unaelezewa kama ni namna ya mapambano, dawa na kama safari maalum. 4. KUTUPIA MACHO MCHAKATO WA UJENZI WA NAFSI Katika Makala hii Dr. Mohammad Ali Shomali anatoa mchanganuo mfupi wa safari ya kiroho. Hatua ya kwanza kabisa ni kuwa macho na makini. Ni pale tu mtu an2

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 2

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

apokuwa macho na mwenye tahadhari kiroho na kwamba anaweza akaamua kuingia kwenye safari hiyo na asipoteze fursa yoyote ile ya kuweza kupata kiasi cha masurufu kwa ajili ya safari hii. 5. MAELEKEZO YA KIVITENDO JUU YA SAFARI YA KIROHO Makala hii inarejelea kwenye maelekezo ya kivitendo matano yaliyotolewa na wakufunzi wa kiroho wa Kiislam. Maelekezo haya matano ambayo msingi wake ni kwenye Qur’ani na Sunnah ni kama haya yafuatayo: I.

Kutokula kupita kiasi

II.

Kutokuongea sana

III. Kutokulala sana IV.

Kuwa na muda wa faragha kwa ajili ya tafakari

V. Na kumkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi kiasi iwezekanavyo. Matano haya ambayo ni rahisi kuyaelewa na ambayo hayahitaji mpangilio maalum au zana ni yenye matokeo mazuri sana na kama mtu akianza kuyafuatilia kwa vitendo ataona mabadiliko mara moja na haraka sana. 6. Makala hii ya sita inarejea kwenye sifa kuu tatu ambazo kila mtu anahitaji kuwa nazo kwa ajili ya maendeleo yake ya kiroho. Kuwa na imani au kukosa imani kunahusiana moja kwa moja na kiwango cha mapenzi yake mtu kwa Mwenyezi Mungu. Kwa kuongeza elimu yake mtu juu ya Mwenyezi Mungu na Viumbe Wake, na kutafakari juu ya 3

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 3

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

hilo, mapenzi juu ya Mwenyezi Mungu yanaweza kupatikana na hili litaboresha hali ya kiroho ya mhusika. Kuhusiana na mapenzi ni kuwa mwenye shukurani, kwani yule mwenye shukurani atampenda Mwenyezi Mungu. Mwishowe, unyenyekevu wa hali ya juu unachukuliwa kuwa ni wenye umuhimu wa hali ya juu kabisa, ambao juu yake utumwa na utiifu kwa Mwenyezi Mungu pamoja na sifa nyingine njema na nzuri hutegemea. 7. MATOKEO YA SAFARI YA KIROHO Kwa kuendeleza mjadala wa hali ya kiroho katika makala sita zilizotangulia, katika makala hii ule mtazamo au njia ya kupata ukaribu na Mwenyezi Mungu inadhihirisha manufaa ya kiroho ambayo wanajaaliwa nayo wale wanaoshika njia ya safari hii. Watu wanaofanya jitihada za kuishi kiuchamungu huku wakidumisha moyo safi uliohuru kutokana na machafu wana mwelekeo wa kufikia ukaribu na Mwenyezi Mungu. Dr. Shomali anazipata athari za kuishi maisha kama hayo kutoka kwenye Qur’ani na Sunnah. Wale wanaoichukua safari hii wanao uwezo wa kupata: I.

Msaada kamili kutoka kwa Mwenyezi Mungu

II.

Elimu bora na kamilifu

III. Utiifu kwa Mwenyezi Mungu IV.

Kuingia kwenye uwanja wa nuru

V.

Mapenzi mazito kwa ajili ya Mwenyezi Mungu

VI. Kumshuhudia Mwenyezi Mungu katika kila kitu; na VII. Amani ya ndani ya nafsi. 4

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 4

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Hujjatul-Islam Dr. Mohammad Ali Shomali ni Profesa Mshiriki na Mkuu wa Idara ya Dini katika Taasisi ya Elimu na Utafiti ya Imam Khomein Educational and Research Institute ya Qum – Iran. Yeye pia ni Mkuu wa Masomo ya Shahada ya Juu kwa ajili ya Wanafunzi wa Kimataifa katika Jami’at azZahra, Chuo Kikuu cha Kiislam kwa ajili ya Wanawake kilichoko mjini Qum. Muhammad Ali Shomali

5

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 5

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

NENO LA MCHAPISHAJI

K

itabu ulichonacho mikononi mwako ni mkusanyiko wa makala saba juu ya utakaso wa nafsi kutoka kwenye majarida ya Message of Thaqalayn yanayochapishwa na AhlulBayt World Assembly na Kituo cha Kiislamu, kama ilivyoelezwa hapo juu katika tahariri kwa juhudi kubwa iliyofanywa na mwanachuoni mashuhuri Dkt. Muhammad Ali Shomali. Makala hizi zimeshughulikia namna na njia ambazo mtu anaweza kujipatia utakaso wa nafsi. Mwandishi ameelezea hatua mbalimbali za kufanya ili kufikia kiwango hiki cha utakaso wa nafsi. Sisi kama wachapishaji tunakiwasilisha kitabu hiki kama kilivyo kwa wasomaji wetu na kuwashauri wasome yaliyomo humo, wayafanyie kazi na kuyazingatia ili kufikia kiwango hiki cha utakaso, kitu ambacho ni lengo kubwa kwa muumini. Kitabu hiki kimekusanya mada mbalimbali juu ya utakaso wa nafsi kwa mpangilio mzuri kwa mtu kuweza kufuatilia na kujifunza. Hii ni moja kati ya kazi kubwa zilizofanywa na Taasisi ya Al-Itrah katika kuwahudumia kielimu wasomaji wake wazungumzaji wa Kiswahili. Na kwa maana hiyohiyo imeamua kukichapisha kitabu hiki chenye manufaa makubwa kwa lugha ya Kiswahili kwa lengo lake lilelile la kuwahudumia Waislamu, hususan wanaozungumza Kiswahili. Hivyo, ni matumaini yetu kwamba wasomaji wetu watanufaika vya kutosha kutokana na kitabu hiki, kwani tumekiona ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa 6

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 6

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote ambapo uwongo, ngano za kale na upotoshaji wa historia ni vitu ambavyo havina nafasi tena katika akili za watu. Tunamshukuru mwandishi wa kitabu hiki Dkt. Muhammad Ali Shomali kwa kazi kubwa aliyofanya kwa ajili ya Umma huu wa Waislamu, Allah ‘Azza wa Jallah amlipe kila kheri na amuingize Peponi kwa salama na amani insha’Allah. Halikadhalika tunamshukuru Ndugu yetu Salman Shou kwa kukitarjumi kwa Kiswahili kitabu hiki, insha’Allah na yeye Allah ‘Azza wa Jallah amlipe kila kheri hapa duniani na Akhera pia, bila kuwasahau na wale wote waliochangia kwa namna moja au nyingine mpaka kufanikisha kuchapishwa kwake, Allah awalipe wote malipo mema hapa duniani na huko Akhera pia. Mchapishaji Al-Itrah Foundation.

7

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 7

7/10/2013 3:33:24 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

N

i fikira ya kawaida miongoni mwa desturi zote za kidini na kiroho kwamba binadamu wanapaswa kuwa na aina fulani ya kujidhibiti wenyewe. Pamoja na kwamba tunafurahia hiari, tunahitajika kutumia hiari zetu kwa njia ya uwajibikaji. Katika njia ile ile ambayo tunatarajia watu wengine waheshimu hadhi zetu na mambo yanayotupendeza, na sisi tunapaswa kuheshimu hadhi za watu wengine na mambo wanayoyapenda. Pia tunapaswa kulinda utu wetu na maslahi ya muda mrefu. Kwa hiyo, hatuwezi kufuata tu haja zetu na matamanio yetu na kufanya kila tutakalo. Tunahitaji kuwa na udhibiti binafsi na kujinadhimu; hali ambayo itatuelekeza kwenye kujitakasa wenyewe. Endapo tutaweza kutakasa nyoyo zetu hatutahitaji tena kuzuia vishawishi vyetu na kujidhibiti dhidi ya tamaa na ashiki za duni, kwani mtu aliyetakasika hatamani chochote isipokuwa kile kilicho kizuri na wema kwa ajili yake yeye na wengine. Kinachofuata sasa, tutachunguza umuhimu wa mtu kujidhibiti na kujitakasa mwenyewe. Kujidhibiti: Kuhusu umuhimu wa mtu kujidhibiti mwenyewe, Qur`ani Tukufu inasema:

‫س َع ِن ْال َھ َو ٰى َفإِنَّ ْال َج َّن َة‬ َ ‫اف َم َقا َم َر ِّب ِه َو َن َھى ال َّن ْف‬ َ ‫َوأَمَّا َمنْ َخ‬ ‫ِي ْال َمأْ َو ٰى‬ َ ‫ھ‬ 8

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 8

7/10/2013 3:33:25 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

“Na kwa yule aliyeogopa kusimama mbele ya Mola wake, na akaikataza nafsi matamanio (maovu). Basi kwa hakika Pepo ndiyo makazi yake.” [79:40&41]

‫اس ِب ْال َح ِّق َو َال‬ َ ‫َيا دَاوُ و ُد إِ َّنا َج َع ْل َن‬ ِ ْ‫اك َخلِي َف ًة فِي ْاألَر‬ ِ ‫ض َفاحْ ُك ْم َبي َْن ال َّن‬ ‫ﷲ‬ ِ َّ ‫يل‬ ِ َّ ‫يل‬ َ ُّ‫ِين يَضِ ل‬ َ ‫ﷲ ۚ إِنَّ الَّذ‬ ِ ‫ون َعنْ َس ِب‬ ِ ‫َت َّت ِب ِع ْال َھ َو ٰى َفيُضِ لَّ َك َعنْ َس ِب‬ ‫ب‬ ِ ‫َل ُھ ْم َع َذابٌ َشدِي ٌد ِب َما َنسُوا َي ْو َم ْالح َِسا‬ “Ewe Daudi!َّ Hakika tumekujaalia kuwaْ khalifa ardhini, ‫اسَ ٰ ِب ْال َ ْ َح ُ ِّق و َال‬ ‫ َف ُاحْ ُك ْم َبي‬kwa ‫ فِي ْاألَرْ ض‬wala ‫اك َخلِي َف ًة‬ ‫َيا َدَاوُ و ُد إ َّنا‬ َ ‫ِين آَجم َع ُنل َنوا‬ ِ َ ‫� َْن َو َلال ْنو‬ basi‫ ُك َ ْم‬uwahukumu ‫ ِب ْالقِسِْ طِ ش َھدَ ا َء‬haki ‫ِين‬ ‫َيا أ ُّي َھا ا‬ ِ‫على أنفس‬ ِ َّ ِ watu َ ‫ ُكو ُنوا َقوَّ ام‬usifuate َ َ ِ ‫لَّذ‬matamanio َّ Mwenyezi ُّ ِ‫َض‬ َّ‫إِ َنَّ ال‬yaًۚ ‫ﷲ‬ َّ‫ُضِ ل‬ yakakupoteza katika njia َ ‫ﷲ‬ ‫يل‬ ‫ك‬Mungu. ‫ َھل َِدَوي ٰى‬Wao ‫تأَ َّت ِبو ِع ْال ْال‬wataِ َّ ‫يل‬ ِ َ ‫ون ٰى َعبنْھ َما َس ۖ ِب َف‬ َ‫ْن َ​َفوي ْاأل‬ َّ ‫ِين َفي‬ ْ‫ين َع ۚنْ إِنْ َس َ ِبي ُك ِن‬ ‫ا�ُلأَ ْو َ​َل‬ ‫قِذيرً َا‬sababu ‫ َغ ِ ِن ّيا أ ْو َف‬walisahau َ ‫ْق َر َِب‬siku َ ِ ِ ِ kali ِ ya‫وا‬Hesabu.” pata ‫ال‬ adhabu kwa

‫ب‬ ‫ُوا َذ ْالابٌَھ َو َٰشىدِيأَ ٌدنْ ِب َت َمعْا ِدلَُنس‬ ‫َل َت ُھ َّت ْبمع َع‬ ِ ‫وا ُۚوا َو َإي ْنْو َم َت ْل ْوُالحوا َِسا‬ ‫ان ِب َما‬ َ ‫ﷲ َك‬ َ َّ َّ‫[أَ ْو ُتعْ ِرضُوا َفإِن‬38:26] ِ ِ ‫ون َخ ِبيرً ا‬ َ ُ‫َتعْ َمل‬ ُ ِ‫ِين ِب ْالقِسْ ط‬ ‫� َو َل ْو َع َل ٰى أَ ْنفُسِ ُك ْم‬ ِ َّ ِ ‫ش َھدَ ا َء‬ َ ‫ِين آ َم ُنوا ُكو ُنوا َقوَّ ام‬ َ ‫َيا أَ ُّي َھا الَّذ‬ َّ ‫ين ۚ إِنْ َي ُكنْ َغ ِن ًّيا أَ ْو َفقِيرً ا َف‬ ‫ا�ُ أَ ْو َل ٰى ِب ِھ َما ۖ َف َال‬ َ ‫ْن َو ْاألَ ْق َر ِب‬ ِ ‫أَ ِو ْال َوالِدَ ي‬ ‫ان ِب َما‬ َ ‫ﷲ َك‬ َ َّ َّ‫َت َّت ِبعُوا ْال َھ َو ٰى أَنْ َتعْ ِدلُوا ۚ َوإِنْ َت ْلوُ وا أَ ْو ُتعْ ِرضُوا َفإِن‬ ‫ون َخ ِبيرً ا‬ َ ُ‫َتعْ َمل‬

“Enyi mlioamini kuweni wenye kusimamia uadilifu, mtoe ushahidi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ijapokuwa ni juu ya nafsi zenu au (juu ya) wazazi (wenu) na jamaa wa karibu. Iwe tajiri au masikini, Mwenyezi Mungu anawastahikia zaidi wote wawili. Basi msifuate matamanio mkaacha kufanya uadilifu. Na kama mkipotoa (ukweli) au mkijitenga, basi hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa yale mnayoyatenda.” [4:135]

Hapa tunaona sehemu mbili za ushauri. Kwanza, kuzingatia Ridhaa ya Mwenyezi Mungu, kumuogopa Yeye na kujaribu 9

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 9

7/10/2013 3:33:25 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kumtii Yeye. Na pili, kuzizuia nafsi zisifanye matendo mabaya na yenye madhara juu yetu. Hali hii inawezekana ya Mwenyezi Mungu, na kumuogopa Yeye nayakujaribu kumtii Yeye. tu pale tunapokuwa aina fulani kujidhibiti. Kwenye Na pili, kuzizuia nafsi zisifanye matendo mabaya na yenye Nahjul-Balaghah, yamo maelezo mazuri sana yenye utambuzi madhara juu yetu. Hali hii inawezekana tu pale tunapokuwa na aina kuhusu asiyetajwa jina. Imam Ali (a.s.) amenukuliwa fulanindugu ya kujidhibiti. Kwenye Nahjul-Balaghah, yamo maelezo akisema: mazuri sana yenye utambuzi kuhusu ndugu asiyetajwa jina. Imam Ali (a.s.) amenukuliwa akisema:

ٌ ‫ضى‬ ‫صغر‬ َ ‫كانَ لي فِي َما َم‬ ِ ‫ﷲ َو َكانَ يُ ْعظ ُمهُ فِي َع ْينِي‬ ِ ‫أخ ِفي‬ َ َ‫ َو َكانَ إذا بَ َد َھهُ أ ْم َران يَ ْنظُ ُر]ن‬.... ‫ال ﱡد ْنيَا فِي َع ْينِ ِه‬ [ ‫ظر‬ َ ]‫ب إلى ا ْل َھ َوى‬ ُ‫فخالَفَهُ[ فَيُ َخالِفُه‬ ُ ‫أ ﱡي ُھ َما اَ ْق َر‬ “Zamani"Zamani nilikuwa na ndugu katika nakwa kwamaoni maoni nilikuwa na ndugu katikaimani, imani, na yangu alikuwa mashuhuri kwa kwa sababu dunia yangu alikuwa mashuhuri sababu duniailikuwa ilikuwa sisi chochote machoni Endapo vitu viwili chochotemwake machoni………… mwake ………… Endapo vitu vingemkviwili basina angeangalia na kipi kuonakiliendana ni kipi kiliendana abili, basivingemkabili, angeangalia kuona ni sana na sana na matakwa yake na angefanya kile kingine badala matakwa yake na angefanya kile kingine badala yake.” [Semi yake.” [SemizazaHekima Hekima - Imam - Imam AliAli no.no. 286286] ] Tunaona kwamba mojawapo ya sifa za ndugu katika imani ilikuwa Tunaona kwamba mojawapo ya sifa za ndugu katika imani kwamba alipokabiliwa na mambo mawili [mathalani ama aende ilikuwa kwamba mambo mahali fulani au alipokabiliwa aende kwingine, na aende kwenyemawili mkutano[mathalani huu au au ashughulike na biashara hii au aende nyingine], ni amamkutano aendemwingine mahali fulani au aende kwingine, kwenye kwamba, alipokuwa kwenye "njia-panda" na alipotakiwa kuchagua mkutano huu au mkutano mwingine au ashughulike na aelekee wapi, kwanza aliangalia nafsi yake, akijaribu kugundua ni biashara hii au nyingine], ni kwamba, alipokuwa kwenye kitendo gani kilikuwa anakipendelea zaidi, halafu huchagua “njia-panda” na ambacho alipotakiwa kuchaguazaidi. aelekee wapi, mtu kwanza kufanya kile hakukipendelea Mathalani, anaweza nafsi kuwa na hiari akijaribu ya ama kutazama TV au kumsaidia mtu gani aliangalia yake, kugundua ni kitendo kufanya kazi yake. Nafsi ambayo haijazoeshwa inaweza kilikuwa anakipendelea zaidi, halafu huchagua kufanya kile kutuhimiza kwenda kutazama TV, na kujisemea kwamba ni ambacho Mathalani, kupotezahakukipendelea muda bure kumsaidiazaidi. mtu mwingine. Lakini mtu badala anaweza yake kuwa na hiari ya ama kutazama TV au kumsaidia mtu ni bora zaidi kutumia muda katika kumsaidia mtu mwingine. kufanya kazi yake. Nafsi ambayo haijazoeshwa inaweza kutuhimiza kwenda kutazama 13 TV, na kujisemea kwamba ni kupoteza muda bure kumsaidia mtu mwingine. Lakini 10

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 10

7/10/2013 3:33:26 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

badala yake ni bora zaidi kutumia muda katika kumsaidia mtu mwingine. Kama mambo yalivyo, si lazima kila wakati tuweze kugundua ni njia gani inayofaa kiutendaji kwa kufuata maelekezo haya. Lakini ni muhimu angalau kujaribu kutafuta na kuona tamaa zetu za kichoyo zinataka tufanye nini. Mwenyezi Mungu ametupatia sisi uwezo wa kutofautisha baina ya ni nini umimi wetu au ulafi unatutaka nini sisi na yale mambo ambayo yamo kwenye manufaa yetu ya “kweli” hasa. Tunapofanya kazi kutokana na manufaa yetu “ya kweli” pia tunaweza kuwa tunalinda maslahi ya watu wengine. Mwenyezi Mungu ametuumba kwa namna ambayo kwamba tunapojihudumia sisi kwa kweli, basi huwa tunawahudumia binadamu wote. Lakini tukijaribu kuwa “wajanja” na kujihudumia sisi wenyewe tu, basi si tu kwamba tunajiharibu sisi wenyewe bali pia tunawaharibu watu wengine. Kuna njia nyingi ambazo zinaweza kutuharibu sisi wenyewe na wengine. Lakini haiwezekani kujihudumia sisi wenyewe kwa ukweli na tusiwahudumie wengine. Ipo mbinu nyingine pia ambayo tunaweza kuitumia pale tunapotaka kufanya uamuzi na tukawa na fursa mbili au tatu za uchaguzi za kufikiria na tukawa hatujui la kufanya. Katika hali kama hizo, inafaa kujaribu kudhani kwamba mtu ambaye ni mcha Mungu sana na ambaye matendo yake unayaamini na kuyakubali, yuko katika nafasi yako. Halafu jaribu kuamua mtu yule angefanya nini kama angekuwa kwenye nafasi yako. Kwa kuwa unazo taarifa kuhusu jinsi mtu huyu anavyofanya maamuzi yake na kuhusu azma zake na nia njema, kwa kumuweka mtu huyo katika akili yako unaweza kuelewa nini la kufanya. Mathalani, unaweza kumfikiria mwanachuoni mcha Mungu au ndugu mcha 11

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 11

7/10/2013 3:33:26 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Mungu, sio lazima awe maasum au mtakatifu. Kwa hiyo, unaweza kufikiria wangeweza kufanya nini na hii inaweza kukupa aina fulani ya utambuzi. Hivyo ni jambo lenye ukweli kimsingi kwamba ni lazima tujizuie. Kama tunaamini kwamba inatupasa tukafanya mambo tutakavyo kwa lengo la kujiridhisha na kujifurahisha tu sisi wenyewe, basi hakuna haja ya kuzungumzia kuhusu mwelekeo wa kiroho. Bila shaka, Uislamu unatuambia kwamba kujizuia ni mwanzo tu, ni kwa ajili ya wale wanaoanza safari. Tunachohitaji kufanya ni kuibadilisha nafsi yetu kutoka kwenye ile inayoendekeza tamaa mbaya na kuifanya iwe nafsi yenye kutamani mambo mazuri. Kisha nafsi yetu inakuwa msaidizi wetu. Lakini hili ni jambo la kuipa mazoezi na kuitakasa nafsi. Ipo simulizi moja nzuri sana kwenye ‘Mathnawi’ iliyoandikwa na Rumi ambayo inaonyesha jinsi ya kuibadilisha nafsi ama kwa njia iliyo nzuri au mbaya. Rumi anasema kwamba hapo zamani palikuwepo na soko la manukato ambapo kila mtu ambaye alitaka kuuza manukato alikuwa na duka. Matokeo yake ni kwamba, kila aliyeingia kwenye soko hili alihisi harufu nzuri ya manukato tu. Kila mtu aliifurahia hali hiyo, hususan wauzaji wa manukato ambao bila shaka, walikuwa ni watu bora katika kuielea harufu ya manukato kutokana na hisi zao za harufu zilizosafika, ambapo sisi huwa tunachanganyikiwa tunapokuwa tumenusa aina nyingi za manukato. Lakini siku moja mtu moja alikwenda sokoni hapo akiwa na farasi na farasi huyo akachafua njia ya soko hilo. Watu walikasirika sana kwa sababu hawakuweza kuvumilia harufu mbaya lakini hakuna mtu aliyekuwa na 12

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 12

7/10/2013 3:33:26 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ujasiri wa kutoa uchafu huo nje. Ilikuwa kama ni mateso kwao. Kwa hiyo mtu moja alitoa ushauri kwamba ni vema wangemleta mtu ambaye kazi yake ilikuwa kusafisha zizi la farasi. Walikwenda kuomba msaada kutoka kwa kijana mmoja ili awasaidie kazi hiyo. Kijana huyo alisema bila shaka angeweza kufanya hivyo kwani hiyo ilikuwa ndiyo kazi yake. Lakini kijana huyo alipoingia kwenye soko hilo, kabla hata hajafika mahali penye uchafu, aliponusa tu ile harufu ya manukato alipoteza fahamu kwa sababu yeye alizoea harufu mbaya kwa hiyo hakuweza kuvumilia harufu nzuri. Kwa njia kama hiyo, kwa upande mmoja, tunawaona watu ambao hufurahia kuswali, ambao hufurahia kuwa na muda wa faragha na Mwenyezi Mungu. Na, kwa upande mwingine, tunawaona watu ambao hukasirika wanapokuona unaswali na huwasababishia uchungu. Na wanapokuona unakwenda msikitini au kanisani, wanajihisi kuudhiwa na hilo. Ipo hadithi isemayo kwamba muumini anapokuwa msikitini ni sawa na samaki aliyeko kwenye maji lakini mnafiki anapokuwa msikitini anahisi kama vile yuko jela na wakati wote anataka kutoroka. Kwa hiyo, hizi ni hali tofauti za nafsi ambazo tunaweza kuzifikia kupitia kujipa mazoezi na kujitakasa.

Kujitakasa: Kwenye Qur`ani Tukufu, Mwenyezi Mungu anasisitiza kuitakasa nafsi ya binadamu na utakaso wake kama ifuatavyo: 13

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 13

7/10/2013 3:33:26 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

‫ار إِ َذا َج َّال َھا‬ ِ ‫َوال َّش‬ ِ ‫مْس َوض َُحا َھا َو ْال َق َم ِر إِ َذا َت َال َھا َوال َّن َھ‬ ‫َواللَّي ِْل إِ َذا َي ْغ َشا َھا‬ ‫س َو َما َسوَّ ا َھا‬ ِ ْ‫َوال َّس َما ِء َو َما َب َنا َھا َو ْاألَر‬ ٍ ‫ض َو َما َط َحا َھا َو َن ْف‬ ْ‫اب َمن‬ َ ‫ُور َھا َو َت ْق َوا َھا َق ْد أَ ْف َل َح َمنْ َز َّكا َھا َو َق ْد َخ‬ َ ‫َفأ َ ْل َھ َم َھا فُج‬ ‫دَ سَّا َھا‬ “Naapa kwa jua na mwanga wake. Na kwa mwezi unapoliandama. Na kwa mchana unapolidhihirisha. Na kwa usiku unapolifunika. Na kwa mbingu na kwa Yule aliyeijenga. Na kwa ardhi na kwa Yule aliyeitandaza. Na kwa nafsi na kwa Yule aliyeitengeneza. Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake. Bila shaka amefaulu aliyeitakasa. Na bila shaka amepata khasara mwenye kuitweza…..” [91:1-10]

Hivyo, baada ya kuapa mara kumi na moja, baada ya msisitizo mkubwa, Mwenyezi Mungu Anatangaza kwamba mtu anayeitakasa nafsi yake atafaulu na atakayeichafua na kuifisidi nafsi yake atapata khasara. Mnamo Siku ya Hukumu, patakuwepo na makundi mawili ya watu: kundi la watu waliofaulu na kufurahi kwa sababu walizitakasa nafsi zao na wale walioko kwenye sehemu mbaya kwa sababu walikuwa wazembe na hawakujali nafsi zao. Utakaso wa nafsi ni sharti la kumkaribia Mwenyezi Mungu. Kwa kweli, sababu yote ya maadili na mambo ya kiroho ni mtu kutakasa nafsi yake. Ni hapo tu ndipo nafsi huanza kung`ara, ikipokea na kuakisi mng`ao na nuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kama tunataka kukutana na Mwenyezi Mungu, Ambaye ni Mtakatifu sana, basi tunahitaji kupata 14

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 14

7/10/2013 3:33:26 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

utakaso. Haiwezekani mtu kuichafua nafsi yake ajaribu kuelekea kwa Mwenyezi Mungu. Endapo tunataka kwenda mahali ambapo watu wapo nadhifu, waliovaa vizuri na wanaonekana kupendeza, na sisi tunahitaji kuwa nadhifu na safi, lazima tuvae nguo nzuri ili na sisi kwa kiwango fulani tuonekane kama wao. Vinginevyo watasema kwamba tutaharibu hafla yao na kuvunja hadhi yao. Mojawapo ya kazi kubwa ya Mitume (a.s.) na lengo kuu katika jitihada zao katika kufundisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu ilikuwa kuwasaidia watu kutakasa nafsi zao. Ikirejelea kazi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Qur`ani Tukufu inasema:

ً ‫ِّين َرس‬ َ ‫ھ َُو الَّذِي َب َع‬ ‫ُوال ِم ْن ُھ ْم َي ْتلُو َع َلي ِْھ ْم آ َيا ِت ِه‬ َ ‫ث فِي ْاأل ُ ِّمي‬ ‫اب َو ْالح ِْك َم َة‬ َ ‫يھ ْم َوي َُعلِّ ُم ُھ ُم ْال ِك َت‬ ِ ‫َوي َُز ِّك‬ ً ‫رس‬katika ْ ‫ث فِي‬ َ ‫َُو الَّذِي َب َع‬kusoma, “Yeye ndiye wasiojua ‫ ِْھ ْم آ َيا ِت ِه‬aliyeleta ‫ ُھ ْم َي ْتلُو َع َلي‬Mtume ‫ُوال ِم ْن‬ ‫ھ‬ َ ‫ِّين‬ َ ‫األ ُ ِّمي‬watu ْ َ َّ ً ْ َ َ َ َ ْ anayetokana nao, Aya Zake na kuwatakasa na ْ ‫ُوال ِمنْ أ ْنفُسِ ِھ ْم‬ ‫ َرس‬anawasomea ‫ِيھ ْم‬ ‫ف‬ ‫ث‬ ‫ع‬ ‫ب‬ ‫ذ‬ ‫ﷲ‬ ‫م‬ ‫د‬ ‫ق‬ ‫ل‬ ‫إ‬ ‫ِين‬ ‫ن‬ ‫م‬ ‫ُؤ‬ ‫م‬ ‫ال‬ ‫ى‬ ‫ل‬ ‫ع‬ َّ‫ن‬ ِ َ َ َ َ َ ِ ‫اب َو ِْال ِح ْك َم َة‬ ‫يھ ْم‬ ‫َوي َُز ِّك‬ َ ‫[ َو ُي ُ َعلِّ ُم ُھ ُم ْال ِك َت‬62:2] ِ kuwafunza Kitabu na hekima…..” ْ ْ ِّ ُ ْ‫اب َوال ِح ْك َم َة َوإِن‬ َ ‫يھ ْم َو ُي َعل ُم ُھ ُم ال ِك َت‬ ِ ‫َي ْتلو َع َلي ِْھ ْم آ َيا ِت ِه َوي َُز ِّك‬ ‫ين‬ ‫ض َال‬ َ ‫َ َ ْ َكا ُنوا ِم َّنْ َق ْب َ ُل َلف ِْي‬ ٍ ‫ِين ٍلإ ْذم َ ُِبب َع‬ ً ‫ِيھ ْم َرس‬ َ ‫ُوال ِمنْ أَ ْنفُسِ ِھ ْم‬ ‫ف‬ ‫ث‬ ‫ن‬ ‫لقد َمنَّ ﷲُ َعلى الم ُْؤ ِم‬ َ ِ ِ ْ‫اب َو ْالح ِْك َم َة َوإِن‬ ‫َي ْتلُو َع َلي ِْھ ْم آ َيا ِت ِه َوي َُز ِّك‬ َ ‫يھ ْم َو ُي َعلِّ ُم ُھ ُم ْال ِك َت‬ ِ ً ُ ‫َ َ ُك َما أَرْ َس ْل َ َنا فِيَ ُك ْم َرس َُوال ِم ْن ُك ْم َي ْتلو َع َل ْي ُك ْم آ َيا ِت َنا َو ُي َز ِّكي ُك ْم‬ ‫ين‬ َ ‫كانوا ِمنْ ق ْب ُل لفِي‬ ٍ ‫ضالْ ٍل َم ُِب‬ ِّ ُ ُ ُ َ َ َ َ ْ‫ع‬ ُ ‫ُون‬ ‫م‬ ‫ل‬ ‫ت‬ ‫وا‬ ‫ن‬ ‫و‬ ‫ك‬ ‫ت‬ ‫م‬ ‫ل‬ ‫ا‬ ‫م‬ ‫م‬ ‫ك‬ ‫م‬ ‫ل‬ ‫ُع‬ ‫ي‬ ‫و‬ ‫ة‬ ‫م‬ ‫ك‬ ‫ح‬ ِ َ َ ‫َو ُي َعلِّ ُم ُك ُم ْال ِك َت‬ ْ َ ْ َ َ َ ‫اب َو ْال‬

“Bila shaka, Mwenyezi Mungu amewaneemesha waumini alً ‫ َرس‬akiwasomea ْ ‫ُوال ِم‬ ‫و ُي َز ِّكي ُك ْم‬Mtume ‫ن ُك ْم َي ْتلُو َع َل ْي‬mwao, ‫َما أَرْ َس ْل َنا فِي ُك ْم‬aya ‫ َك‬Zake َ ‫ ُك ْم آ َيا ِت َنا‬miongoni iowapelekea na akiwatakasa ‫ُون‬ ‫ َت ُكو‬kuwafunza ‫َوي َُعلِّ ُم ُك ْم َما َل ْم‬Kitabu ‫و ْال ِح ْك َم َة‬na ‫لِّ ُم ُك ُم ْال ِك َت‬na ‫ َو ُي َع‬ingawa َ ‫ ُنوا َتعْ َلم‬na َ ‫اب‬ َ hekima zamani walikuwa katika upotovu ulio wazi.” [3:164] 15

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 15

7/10/2013 3:33:27 PM


َّ َّ‫َل َق ْد َمن‬ ً ‫ِيھ ْم َرس‬ َ ‫ِين إِ ْذ َب َع‬ ‫ُوال ِمنْ أَ ْنفُسِ ِھ ْم‬ َ ‫ﷲُ َع َلى ْالم ُْؤ ِمن‬ ِ ‫ثف‬ ْ‫اب َو ْال ِح ْك َم َة َوإِن‬ َ ‫يھ ْم َو ُي َعلِّ ُم ُھ ُم ْال ِك َت‬ ِ ‫َي ْتلُو َع َلي ِْھ ْم آ َيا ِت ِه َوي َُز ِّك‬ UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI ‫ين‬ َ ‫َكا ُنوا ِمنْ َق ْب ُل َلفِي‬ ٍ ‫ض َال ٍل م ُِب‬ ً ‫َك َما أَرْ َس ْل َنا فِي ُك ْم َرس‬ ‫ُوال ِم ْن ُك ْم َي ْتلُو َع َل ْي ُك ْم آ َيا ِت َنا َو ُي َز ِّكي ُك ْم‬ ‫ُون‬ َ ‫اب َو ْالح ِْك َم َة َو ُي َعلِّ ُم ُك ْم َما َل ْم َت ُكو ُنوا َتعْ َلم‬ َ ‫َو ُي َعلِّ ُم ُك ُم ْال ِك َت‬ “Kama tulivyompeleka kwenu Mtume kutoka miongoni mwenu, anakusomeeni aya Zetu, na kukutakaseni na kukufundisheni mliyokuwa hamyajui.” [2:151]

Hivyo tunaona kwamba mojawapo ya kazi za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), zaidi ya kusoma Qur`ani na kufundisha Kitabu na hekima, ilikuwa ni kutusaidia sisi kutakasa nafsi zetu. Kwa kweli, kuteuliwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kwa kazi kama hiyo, lilikuwa ni majibu ya maombi ya Nabii Ibrahim (a.s.) na Ishmael (a.s.), baada ya kunyanyua misingi ya Nyumba [ka`bah]:

‫ت َوإِسْ مَاعِ ي ُل َر َّب َنا َت َق َّب ْل‬ ِ ‫َوإِ ْذ َيرْ َف ُع إِب َْراھِي ُم ْال َق َواعِ َد م َِن ْال َب ْي‬ َ ‫ك أَ ْن‬ ْ‫ْن َل َك َو ِمن‬ َ ‫ِم َّنا ۖ إِ َّن‬ ِ ‫ت ال َّسمِي ُع ْال َعلِي ُم َر َّب َنا َواجْ َع ْل َنا مُسْ لِ َمي‬ َ ‫ك أَ ْن‬ ‫ت‬ َ ‫ك َوأَ ِر َنا َم َناسِ َك َنا َو ُتبْ َع َل ْي َنا ۖ إِ َّن‬ َ ‫ُذرِّ َّي ِت َنا أُم ًَّة مُسْ لِ َم ًة َل‬ ً ‫ِيھ ْم َرس‬ ْ ‫ال َّت َّوابُ الرَّ حِي ُم َر َّب َنا َواب َْع‬ ‫ُوال ِم ْن ُھ ْم َي ْتلُو َع َلي ِْھ ْم‬ ِ ‫ثف‬ َ ‫ك أَ ْن‬ ‫ت ْال َع ِزي ُز‬ َ ‫يھ ْم ۚ إِ َّن‬ َ ‫ِك َوي َُعلِّ ُم ُھ ُم ْال ِك َت‬ َ ‫آ َيات‬ ِ ‫اب َو ْالح ِْك َم َة َوي َُز ِّك‬ ‫ْال َحكِي ُم‬ “Na kumbukeni Ibrahim na Ishmael walipoiinua misingi ya nyumba [wakaomba]; Ee Mola Wetu! Utukubalie, hakika Wewe ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua. Ee Mola Wetu! Utufanye tuwe wenye kunyenyekea Kwako, na katika kizazi chetu [uwafanye] uwe ummah wenye kunyenyekea Kwako 16

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 16

7/10/2013 3:33:28 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

na utuonyeshe ibada zetu, na utupokelee. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kupokea (toba) Mwenye kurehemu. Ee Mola Wetu! Wapelekee Mtume katika wao awasomee Aya Zako na kuwafunza Kitabu na hekima na kuwatakasa. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima.� [2:127-129]

Fikiria ni jinsi gani Ibrahim alikuwa na hekima! Jinsi gani dua yake ilikuwa nzuri! Kwenye sehemu tatu ndani Qur`ani, Mwenyezi Mungu anasema kwamba alimpeleka Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kufanya kazi ileile ambayo Ibrahim (a.s.) na Ismael waliomba: kuwasomea watu Aya Zake na kuwafundisha Kitabu na hekima na kutakasa nafsi zao. Bila shaka, ni lazima itakuwa ni Mwenyezi Mungu Mwenyewe ndiye aliyeshusha wahayi ili waombe namna hiyo. Mwenyezi Mungu ni Mwenye huruma sana hivyo kwamba kwanza anatuambia tumwombe Yeye halafu analeta wahayi wa kutuelekeza tuombe nini halafu anajibu maombi yetu. Hivyo basi utakaso wa watu ilikuwa ni kazi muhimu ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na, kwa kweli, ya Mitume wote (a.s.). Aya hizi zinaonyesha wazi umuhimu mkubwa wa kazi ya utakaso wa nafsi. Inafaa kuangalia kwamba kwenye du’a ya Ibrahim na Ismael ombi la kufundisha Kitabu na hekima limetajwa kabla ya ombi la utakaso, lakini kwenye sehemu zote tatu Mwenyezi Mungu anaelezea kazi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), kazi ya utakaso imetajwa kabla ya kufundisha Kitabu na hekima. Hii inaashiria kipaumbele na umuhimu mkubwa wa utakaso. Hii pia inaonyesha kwamba sharti la kujifunza Kitabu na hekima inapaswa kuwa safi na halisi. 17

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 17

7/10/2013 3:33:28 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Vipo vyanzo kadhaa vya uchafu wa nafsi. Chanzo kikubwa ni kujiambatanisha sana na maisha ya kimada na mambo ya kidunia hivyo kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amenukuliwa akisema:

‫أح ﱠ‬ ُ‫ضه‬ َ ‫ب َما أ ْبغ‬ َ َ‫أال تَ َرى َكيْف‬ ‫َھذا‬

‫أس ُك ﱢل َخ ِطيَئ ِة‬ ُ ‫ُح ﱡب ا ْل ﱡد ْنيَا َر‬ ْ‫ش ﱡد ُج ْرما ِمن‬ َ ‫أي َخطَإ أ‬ ‫ﷲُ َو ﱡ‬

“Kuambatana na dunia hii ni chanzo cha kila kosa. Angalia “Kuambatana na dunia hii ni chanzo cha kila kosa. jinsi mtu Angalia ambaye ameambatana na dunia na hiidunia anavyopenda jinsi mtu ambaye ameambatana hii yale ambayo Mwenyezi Mungu hayapendi. Ni kosa anavyopenda yale ambayo Mwenyezi Mungugani linhayapendi. Nizaidi kosa kuzidi gani linaloweza aloweza kuwa kubwa hili?”1 kuwa kubwa zaidi kuzidi hili?”3

Dunia ya kimaada haina umuhimu na thamani yoyote mbele ya ya Mwenyezi Mungu. Kuambatana na mbele kuifanya Dunia kimaada haina umuhimu na thamaninayo yoyote ya ndiyo lengo kuu katika maishanayo ya na mtu ni kosa kubwa Mwenyezi Mungu. Kuambatana kuifanya ndiyo lengo sana kuu katika maisha mtu nimojawapo kosa kubwaya sana na uchafu. Kwahili hiyo, na uchafu. Kwayahiyo, tiba ya tatizo na mojawapo ya tiba ya tatizo hili na njia muhimu sana katika utakaso njia muhimu sana katika utakaso wa nafsi ni kuwata watu wa nafsi ni kuwata watu kutoa zaka [al-zakat]. Katika aya takribani kutoa zaka [al-zakat]. Katika aya takribani ishirini za Qur’ani ishirini za Qur’ani Tukufu, kutoa zakat kumetajwa mara baada ya Tukufu, kutoa zakat kumetajwa baadaAllah ya kusimamisha kusimamisha sala [iqamat a-salat].mara Mathalani, swt. anasema salandani [iqamat a-salat]. Mathalani, Allah swt anasema ndani ya ya Qur`ani: Qur`ani: ُ ‫ين ُح َن َفا َء َو‬ ‫ يقِيمُوا‬ ‫ﷲ م ُْخل‬ ‫َو َما أ ُ ِم‬ َ ‫ين َل ُه ال ِّد‬ َ ِ‫ ِص‬ َ َّ ‫ رُوا إِ َّال لِ َيعْ ُب ُدوا‬ ْ َّ ‫الص َ​َّال َة َوي ُْؤ ُتوا‬ ‫ َك‬ ‫الز‬ ‫ ا َة ۚ َو ٰ َذل َِك دِينُ ال َق ِّي َم ِة‬ “Wala hawakuamrishwa ila kumwabudu Mwenyezi Mungu

1

kwa kumtakasia yeye dini, hali wameshikamana na haki, “Wala hawakuamrishwa kumwabudu Mwenyezi na wanasimamisha sala na kutoaila zaka, na hiyo ndiyo dini Mungu kwa kumtakasia yeye dini, hali wameshikamana madhubuti.” [98:5] na haki, na wanasimamisha sala na kutoa zaka, na hiyo ndiyo dini madhubuti.” [98:5]

Biharul-Anwar, Juz. ya 67, uk. 309. 3

18

Biharul-Anwar, Juz. ya 67, uk. 309. 21

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 18

7/10/2013 3:33:28 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Zakat inatokana na mzizi uleule kama tazkiyah (utakaso) yaani; za-ka-wa ambayo maana yake ni ukuaji na utakaso. Imeshauriwa [Lisan al-Arab, Juz. 14, uk. 358] kwamba sababu ya kuita sadaka “zakat” imo kwenye ukweli kwamba kulipa zakat hutakasa fedha ya mtu na rasilimali zingine. Pia ni kweli kwamba kulipa zakat husababisha ukuzi [namaa] na baraka [barakah] kwenye fedha na riziki ya mhusika. Inaonyesha kuwa na maana zaidi kushauri kwamba sababu ya kuuitwa “zaka” ni kwamba inasaidia katika kutakasa nafsi kwa kuondoa mapenzi kwa dunia hii. Ndiyo maana Mwenyezi Mungu anamwambia Mtume Muhammad (s.a.w.w.):

ۖ ‫ص ِّل َع َلي ِْھ ْم‬ َ ‫يھ ْم ِب َھا َو‬ َ ‫ُخ ْذ ِمنْ أَمْ َوال ِ​ِھ ْم‬ ِ ‫صدَ َق ًة ُت َط ِّھ ُر ُھ ْم َو ُت َز ِّك‬ َّ ‫ص َال َت َك َس َكنٌ َل ُھ ْم ۗ َو‬ ‫ﷲُ َسمِي ٌع َعلِي ٌم‬ َ َّ‫إِن‬ “Chukua ‫ ٰى إِ َّال‬sadaka ‫عْ َم ٍة ُتجْ َز‬katika ‫ ْندَ هُ ِمنْ ِن‬mali ‫ِي َما َل ُه َي َت َز َّك ٰى‬na‫ ُْؤت‬uwatakase, ‫الَّذِي ي‬ ِ‫ألَ َح ٍد ع‬zao, ِ ‫ َو َما‬uwasafishe kwa hizo (sadaka zao) na uwaombee. Hakika kuomba kwaْ‫ف َير‬ ْ‫ا ْبت َِغا َء َوج‬ndiye ‫ض‬ ‫ ِه َر ِّب ِه ْاألَعْ َل‬Mungu َ Mwenyezi َ ‫ ٰى َو َل َس ْو‬Mwenyezi ko ni utulivu kwao,‫ ٰى‬na Asikiaye, Ajuaye.” [9:103]

Kwenye aya hii, badala ya neno zakat, limetumika neno “sadaka” [sadaqah]. Hata hivyo, maana ni ile ile: Kutoa fedha kwa ajili ya Mwenyezi Mungu husaidia utakaso wa yule anayetoa.2 Mahali pengine Qur`ani inasema: 2

ii ni ziada ya msisitizo mkubwa unaowekwa na Qur`ani kuhusu utoaji wa zakat H inaonyesha kwamba hili si jambo la kilugha au ajali, na kwamba kulipa zakat ni sharti la kidini na tazkiyah [utakaso wa watu] kama kazi kuu ya Mtume zinaungana kwa karibu sana. 19

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 19

7/10/2013 3:33:28 PM


ۖ ‫ص ِّل َع َلي ِْھ ْم‬ َ ‫يھ ْم ِب َھا َو‬ َ ‫ُخ ْذ ِمنْ أَمْ َوال ِ​ِھ ْم‬ ِ ‫ص َد َق ًة ُت َط ِّھ ُر ُھ ْم َو ُت َز ِّك‬ UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI َّ ‫ص َال َت َك َس َكنٌ َل ُھ ْم ۗ َو‬ ‫ﷲُ َسمِي ٌع َعلِي ٌم‬ َ َّ‫إِن‬ ‫الَّذِي ي ُْؤتِي َما َل ُه َي َت َز َّك ٰى َو َما ِألَ َح ٍد عِ ْندَ هُ ِمنْ ِنعْ َم ٍة ُتجْ َز ٰى إِ َّال‬ ‫ض ٰى‬ َ ْ‫ف َير‬ َ ‫ا ْبت َِغا َء َوجْ ِه َر ِّب ِه ْاألَعْ َل ٰى َو َل َس ْو‬ “Ambaye hutoa mali yake kujitakasa. Na hapana yeyote aliyemfanyia hisani ili apate kulipwa. Ila ni kutaka radhi ya Mola wake aliye Mtukufu mno. Na hakika atakuwa radhi.” [92:18:21]

Hivyo, mtu anapotumia fedha yake kwa ajili ya Mwenyezi Mwenyezi Mungu kwenye vitu kama kuwasaidia wenye haja au kujenga sehemu za matumizi mema ya jumla kama vile Misikiti, seminari za Kislamu, mashule na hospitali; mtoaji na mpokeaji wote hunufaika. Hata hivyo, anayenufaika zaidi ni mtoaji ambaye anatoa fedha kitu ambacho mbele ya Mwenyezi Mungu ni chenye thamani ndogo kabisa na badala yake hupata utakaso na radhi ya Mwenyezi Mungu.

ْ‫ب َوأَ َقامُوا الص َ​َّال َة ۚ َو َمن‬ ِ ‫ِين َي ْخ َش ْو َن َر َّب ُھ ْم ِب ْال َغ ْي‬ َ ‫إِ َّن َما ُت ْن ِذ ُر الَّذ‬ ‫ﷲ ْالمَصِ ي ُر‬ ِ َّ ‫َت َز َّك ٰى َفإِ َّن َما َي َت َز َّك ٰى لِ َن ْفسِ ِه ۚ َوإِ َلى‬ “….Hakika unawaonya wale tu wanaomuogopa Mola wao kwa siri na wanasimamisha swala. Na anayejitakasa basi anajitakasa kwa ajili ya nafsi yake, na marejeo ni kwa Mwenyezi Mungu.” [35:18]

20

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 20

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Hitimisho: Ni jambo la muhimu kwamba lazima tujizuie. Mambo ya kiroho hayawezi kuwapo bila kuwepo na nidhamu. Hatuwezi kujiendeleza kwa kufanya mambo kufuatana na utashi wetu kwa lengo la kuridhisha na kufurahisha nafsi zetu. Bila shaka, Uislamu unatuambia kwamba kujidhibiti ama kujizuia ni mwanzo tu. Tuanachotakiwa kufanya ni kuzibadilisha nafsi zetu kutoka kwenye zile zinazopenda matamanio maovu na kuzifanya zitamani mambo mazuri. Kwa kuzielekeza na kuzitakasa nafsi zetu, zenyewe zinakuwa wasaidizi wetu. Kazi kubwa ya Mitume na hususan Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ilikuwa kuwasaidia watu kujitakasa. Sababu ya msisitizo mkubwa kuhusu kujitakasa ni ukweli kwamba Mwenyezi Mungu ni Mtakatifu sana na Muadilifu sana na ni kwa njia ya utakaso wa nafsi ndiyo tunaweza kutimiza nia zetu za kumkaribia Yeye. Njia moja kuu ya utakaso ni kutoambatana na maisha ya anasa za dunia kwa mtu kutoa fedha zake mwenyewe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

21

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 21

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

NJIA TOFAUTI ZA KIMBINU KWENYE MAMBO YA KIROHO

K

wenye makala iliyopita tulizungumzia umuhimu wa mtu kujidhibiti na kujitakasa mwenyewe. Kwenye makala hii tutatafakari na kuzungumzia kwa ufupi mbinu mbalimbali ambazo miongoni mwa wanachuoni wa Kislamu huzitumia katika kuchunguza mambo ya kiroho kwa ujumla na hasa maadili [akhlaq]. Kwa ujumla, tunaweza kuainisha misimamo ya wanachuoni katika njia kuu tatu: 1. Njia ya Kifalsafa 2. Njia ya Nguvu ya Roho [Usufii] 3. Njia Inayotegemea Masomo ya Dini/Maandishi. Njia ya Kifalsafa:

Wanachuoni wengi wa Kiislamu wameiona mitazamo ya baadhi ya wanafalsafa wa Kigiriki, hususan Aristotle, kwa kiwango kikubwa inayovutia kama njia ambamo tunaweza kuzungumza kuhusu nafsi ya mwanadamu. Kwa mtazamo huu, nafsi ya binadamu inazo nguvu [quwwah] za aina tatu zenye kuwajibika kwa vitendo; nazo ni: 1. Nguvu ya akili [al-quwwah al-`aqliyyah] ni nguvu inayowajibika na maarifa. Haya hutusaidia sisi kuelewa mambo na hutuwezesha kujishughulisha na mijadala. Kama nguvu hii ikifanya kazi kikamilifu, mtu anaweza kupata hekima [hikmah] ya kweli. Hii haimaanishi kwamba mtu ajitahidi kupata nguvu za kiakili za kuzidi kiasi, kwa 22

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 22

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kuwa hii ni mojawapo ya visababishi vya nadharia ya kushuku; bali inamaanisha kwamba lazima tushughulike na kudumisha uwiano. Kama mtu hana nguvu hii ya kiakili ya kutosha, anaweza kuwa mtu wa kukubali sana na kuamini kila atakachosikia.Mtu wa aina hii anaweza kudanganyika kwa urahisi sana. Ibn Sinna, katika kauli yake nzito anasema: “Yeyote mwenye kawaida ya kukubali hoja yoyote bila ya fikra yoyote anakuwa sio binadamu tena.” Hii ni kwa sababu sehemu muhimu ya msingi wa ubinadamu ni ufanisi na binadamu mara zote anaelezewa na wanafalsafa kama “mnyama mwenye ufanisi.” Kwa hiyo mtu anatakiwa kuwa mwenye kukubaliana, na si kuwa mwenye busara nyingi sana na mdadisi mno au kuwa msikilizaji sana na kuitikia tu. 2. Nguvu ya ghadhabu [al-quwwah al-ghadabiyyah] ni inayodhibiti ghadhabu zetu. Bila ya nguvu hii hatungekuwa na utashi wa kujihami sisi wenyewe kutokana na hatari. Hata hivyo, kama mtu ataruhusu nguvu hii kuzidi kiasi, atakuwa mshari na wakati wote atakuwa tayari kushambulia. Kwa upande mwingine, kama mtu atakosa nguvu ya ghadhabu matokeo yake atakuwa muoga. Wanafalsafa katika madhehebu hii ya kifikira wanatuhimiza kuwa na uwiano baina ya mawili haya; ili tuweze kupata sifa ya ujasiri.Kwa hiyo, mtu mwema, ni yule anayejua wakati gani wa kukasirika na kwa kiasi kilicho sahihi. 3. Nguvu ya Kuamsha Hamu [al-quwwah al-shahwiyyah] ni nguvu ambayo zaidi inakuwa na hamu ya kufanya mapenzi, lakini pia hujumuisha hamu zetu za chakula na vitu vingne. Endapo nguvu ya kupenda kujamiiana 23

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 23

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

isingekuwepo kwa binadamu, muendelezo wa spishi hii ya binadamu ungekuwa hatarini. Nguvu hii pia lazima iwekwe kwenye uwiano ambapo mtu anakuwa safi na mwenye wastani. Kwa hiyo, kama mtu angekuwa aafikiane na aina zote za nguvu zilizotajwa katika kiwango cha uwiano unaofaa, angepata kuwa na busara, ujasiri na utawa; haya yote ndio ambayo mtu anayahitajia ili kupata uadilifu. Hii ina maana kwamba mtu ambaye ni muadilifu ni yule ambaye amepata ukamilifu wa kila kipengele cha nafsi yake. Kuwa muadilifu si tu kuhusu kujizuia kutenda dhambi, lakini pia ni kuhusu ukamilifu wa kila aina ya hisi. Shule hii ya mambo ya kiroho inaweka majibu ya kimantiki kabisa kuhusu suala la ujenzi wa nafsi. Pamoja na kwamba ni la kimantiki, watu wengine wanaona kuwa ni wa kinadharia mno na linakosa sifa za msukumo na msisimko, sifa ambazo zinaweza kuwaamsha watu hasa na kuwaacha wamehamasika kubadilika. Tunafundishwa kuwa na maafikiano na hisi zetu lakini inawezekana kuwa vigumu kugundua mahali ulipo uwiano huo kwenye hali tofauti. Uendeaji huu unafaa, lakini haukidhi haja; lazima tuongeze elementi za kivitendo na msukumo kwa lengo la kuhamasisha fikira zetu. Njia ya Kumkaribia Mwenyezi Mungu Kwa Tafakuri [Usufii]: Masufii wanafikiri kwamba mlolongo wote wa ujenzi wa nafsi ni safari ya kuelekea kwa Mwenyezi Mungu au ukamilifu na kama suala la ukuaji wa polepole. Tofauti ya njia iliyopita hapo juu na njia hii ni kama ifuatayo: 24

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 24

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Kufuatana na njia ya kwanza, uhusiano wa moyo na ujenzi wa nafsi unaweza kufikiriwa kwa njia ifuatayo: Fikiria kwamba una nyumba ambayo unataka kuiremba; kuna mambo kadhaa ambayo ungeweza kufanya. Ungesafisha na kuondoa taka, halafu ungeanza kuipamba nyumba, na kuweka samani ndani ya nyumba kwa njia ya busara. Kama mtu akiweza kuondoa takataka na vitu vyote visivyopendeza ndani ya nyumba, kabla ya kuipamba na kisha akaweka samani zinazopendeza, ndipo nyumba inakuja kuvutia. Kwa njia hiyo hiyo, tunaweza kufikiria nyumba tunayotaka kuipendezesha ni sawa na vile tunavyotaka kuisafisha na kuipamba nafsi kwa tabia njema. Lazima tuondoe sifa mbaya kutoka kwenye nyoyo zetu ili Allah swt aweze kuingiza nuru ndani humo na kuweka tabia njema ndani ya nyoyo zetu. Mathalani, tunasoma ndani ya hadithi, “malaika hawaingii nyumba ambayo mbwa wanafugwa.”33 Ni lazima tufikirie hali ya nyoyo zetu kwa namna ile ile, na kama nyoyo zetu zitakuwa zenye shari kama mbwa, hasira na maradhi hatuwezi kuwa na matumaini ya malaika kuingia. Kwa hiyo, mchakato huu unahusisha hatua tatu kuu: • Takhliyah – kusafisha • Tabliyah – mapambo • Tajliyah – huanza kung`ara (hali hii hutokea yenyewe mara baada ya kutekeleza hatua mbili za mwanzo) Ingawaje njia hii inahamasisha kwa kiwango fulani, na inaweza kutupatia muundo ambao kupitia humo tuweze kujenga nafsi, lakini njia hii haina uwezo mpana kielimu, 3 3

Tazama Bihar al-Anwar, Juz. uk. 56, uk. 177. 25

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 25

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kwa sababu haielezi kwa ufasaha mtu aanzie wapi na aishie wapi katika safari ya kiroho. Njia hii haisemi tusafishe nini kwanza na mapambo gani tujipambe nayo. Halafu tena, njia hii inafaa lakini haitoshi kwa yenyewe tu kama mpango kamili wa ujenzi wa nafsi. Kufuatana na njia ya pili; uhusiano wa moyo na ujenzi wa nafsi unaweza kufikiriwa kwa njia ifuatayo. Mtu yu kama ua. Na ua haliwezi kukua bila matunzo. Ua linaweza kukua kama ua lingine ambalo lilikua siku za nyuma; jambo hili si la kipekee. Ua hukua polepole kama kila kitu kinafanywa kwa uangalifu. Hali hii inafanana na jinsi mtoto akuavyo hadi anakuwa mtu mzima. Mtu hawezi kuwa kijana kabla ya kuwa mtoto mchanga. Kwa njia kama hii, mtu hawezi kumlisha mtoto mchanga chakula cha kijana na kinyume chake. Kwa hiyo, njia ya pili yaani njia ya kisufi inaangalia ukuaji wa kiroho katika njia yenye uwezo kama utaratibu uliopangiliwa kwa uangalifu. Mtu anahitaji muongozo kutoka kwa watu ambao wamekwisha pita kwenye mchakato huu, ambao wanaweza kutoa ushauri wa kitu gani kifanyike katika kila hatua. Kwa njia hii, kila hatua lazima ishughulikiwe kwa namna ya peke yake. Maana yake ni kwamba, matarajio katika kila hatua yatakuwa tofauti. Kile ambacho kinaweza kuwa kizuri kwa mtu mwingine kwenye hatua moja si lazima kiwe kizuri kwa mtu mwingine katika hatua ya juu zaidi. Mathalani, kama mtoto mdogo ataikariri Surah Al-Fatiah [Ufunguo], na akaisoma, watu watamsifu mtoto na watakuwa wamevutiwa, lakini kama Imam wa swala angesoma kwa kukariri Sura ile ile kwa namna ile ile, watu wangemkosoa na hawangeswali nyuma yake. Kwa hiyo, kila kitu ni suala la kulinganisha juu ya nini tutarajie kutoka kwetu wenyewe 26

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 26

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

katika mazingira tofauti. Ni safari yenye kuendelea kutoka hatua moja kwenda hatua inayofuatia. Njia Inayotegemea Masomo ya Dini / Maandishi. Kufuatana na fikira hii, njia iliyo bora zaidi ni kurejelea Qur`ani na Sunnahh za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na watu wa Nyumba yake (a.s.). Kwa hiyo, wale wanaotetea njia hii waliona hapakuwepo na haja ya muundo wa kifalsafa, na badala yake waliorodhesha sifa za mtu zinazofaa na zisizofaa kufuatana na isemavyo Qur`ani. Mathalani, kuhusu uovu wa tamaa wangechukua aya kutoka kwenye Qur`ani zinazoonyesha kwamba tamaa ni sifa mbaya na kutoa ushahidi na ufumbuzi kutoka kwenye hadithi. Msimamo wetu unapaswa uwe Upi? Wanachuoni wote hawa wametoa mchango mkubwa kwa fikira za kimaadili za Kislamu. Hata hivyo, kila moja ya njia hizi inazo nguvu na udhaifu wake na kama tunataka kunufaika sana lazima tutengeneze njia ambatanishi ambamo manufaa ya kila madhehebu yataingizwa. Masharti kwa ajili ya Njia inayotosheleza: 1. Mtazamo wetu wa kimaadili lazima uendane na Qur`ani na Sunnah, kwani hakuna mwingine aliye bora zaidi ya Allah swt na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika kuongoza, juu ya ni lipi jema au ovu. Kweli yote inatoka kwa Allah swt, bila kujali kama imefika kwetu kupitia kwa masufii au wanafalsafa. 27

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 27

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

2. Mfumo wa kimaadili lazima uwe mpana. hakuna kipengele cha binadamu kinachoweza kupuuzwa. Hatutaki kuwa na mtu ambaye ameendelea kwenye kipengele kimoja tu. Binadamu lazima akue katika vipengele vyote tofauti. 3. Mfumo wa kimaadili lazima uwe wa kimantiki na kuungwa mkono na hoja za kimantiki, lakini pia lazima iwe ya kivitendo na kuvutia. 4. Muundo lazima mikanganyiko.

uwe

thabiti

na

pasijetokea

5. Mfumo wa kimaadili lazima utuambie la kufanya tunapokuwa katika nafasi na vituo mbalimbali kwani ujenzi wa nafsi ni mchakato hai na hautulii. Katika fani yoyote ile ya utafiti au mazoezi mtu hawezi akasema kwamba hahitaji mashauriano ama ushauri. 6. Uislamu ni dini inayochukulia akili kuwa kitu cha muhimu sana. Hakuna jambo lisilotumiliwa akili katika Uislamu. Yapo mambo mengi ambayo yanafundishwa kwa njia ya wahayi, lakini hili si kwa sababu yapo kinyume na akili; ni kwa sababu mambo hayo yapo nje ya uelewa wa akili. Kuonyesha tofauti baina ya kitu kilichopo kinyume cha akili na kile kilichopo nje ya uelewa wa akili na tuangalie mfano huu. Endapo mtu angeulizwa watu wangapi wamo kwenye chumba cha pili, hangeweza kutoa jibu kwa kutumia akili peke yake. Jibu la swali hili halipatikani kwa kutumia akili. Hata hivyo kama ingetokea mtu akajibu kwa kusema kwamba wamo watu milioni moja ndani ya chumba 28

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 28

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kile, akijua ukubwa wa chumba hicho, tungeweza kusema kwamba jibu hili ni kinyume cha akili. Hitimisho: Tunahitaji mfumo wa kimaadili wenye msingi wa Qur`ani na Sunnah,na wakati huohuo uwe na msimamo wa kimantiki na kifalsafa. Pia mfumo lazima uwe na vipaumbele vilivyo wazi, na endapo mambo mawili yanagongana, mfumo lazima uonyeshe ni jambo gani kati ya hayo mawili ni muhimu zaidi. Mwisho, lazima tuweze kujua ni kitu gani tunachoweza kutarajia katika kila hatua, hususan kwa wale ambao wamekwishapita ile hatua ambayo sisi tupo, kwani ushauri na msaada wao ni muhimu sana. Miongoni mwa wanachuoni wetu wa kileo, wametokeza walimu wazuri sana wa mambo ya kiroho ambao wameunganisha madhehebu haya ya fikira, na ambao tunaweza kujifunza kutoka kwao kama vile Imam Khomeini, Allamah Tabatabai Ayatollah Mutahhari na Ayatollah Javadi Amuli.

29

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 29

7/10/2013 3:33:29 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

MATENDO MBALIMBALI YA KIROHO

K

wenye toleo lililopita tulichunguza mielekeo mbalimbali ya kimbinu miongoni mwa wanachuoni wa Kislamu kuhusu mambo ya kiroho. Kwenye toleo hili tutachunguza njia ambazo Qur`ani na hadithi vimeuchukulia huu mchakato wa kuendeleza nafsi na kuelezea juhudi za mwanadamu na mapambano katika kupata ucha-Mungu na mambo ya kiroho. 4 kubwa?" "Kupambana na nafsi yako mwenyewe" 1. Mambo yaAkajibu: kiroho kama mapambano na nafsi: Kufuatana na njia hii, ujenzi wa nafsi ni vita ya ndani kwa ndani dhiMasahaba walikuwa wamewashinda maadui zao kwenye vita kali di ya watayari ndani. Kwenye hadithi mashuhuri na ya kuna adui walikuwa kujitolea kiti wamachokipenda sana, yaani uhai wao, kwa lengo la kutetea Uislamu. Walishtuka na kushangaa ni tia moyo sana, tunasoma kwamba huko Medina, Mtume kitu gani hicho ambacho kingekuwa kikubwa kuliko hicho. Muhammad (s.a.w.w.) aliliona kundi la sahaba wake amMtukufu Mtume alijibu: “Jihadi ya nafsi.” Maana yake ni kupigana na nafsi yako mwenyewe, mapambano dhidi ya nafsi yako. bao walikuwa wanarudi kutoka kwenye vita ambayo walishinda. Mtume Katika Mtukufu hadithi mashuhuri sana akasema: Abu Dharr alimuuliza Mtukufu

Mtume Muhammad (s.a.w.w.): “Ni jihadi gani iliyo bora zaidi?”

“Mmefanya vema! Karibuni nyinyi watu ambao mmeka"‫"ان يجاھد الرجل نفسه وھواه‬ milisha jihadi ndogo na ambao bado mnangojewa na jihadi kubwa“Kupambana zaidi” na nafsi yako na tamaa zako.”5 Mtume wa wa Mwenyezi Mungu aliulizwa:ya“Ni jihadi Mfanano ujenzi wa nafsi kwenye mapambano ndani kwa gani hiyo 44 hakika una mizizi“Kupambana ndani ya Qur`ani. na Kwanafsi mfano, yako Qur`animwenyewe” inasema: kubwa?” Akajibu: �������maadui ����� zao kwenye Masahaba��������� walikuwa��������� wamewashinda ���� �������� ���� ���� � ������������ vita kali na walikuwa tayari kujitolea kitu wanachokipenda Al-kafi,4 Juz. 5.Juz. uk.5.12, Al-Amali na al-Saduq, kikao cha Al-kafi, uk. namba 12, namba33na na Al-Amali na al-Saduq, kikao cha 71, uk. 377,71, uk. 377, na. 8. Ipo kwenye yahapo hapo inayoweza kupatikana kwenye na. nyongeza 8. Ipo nyongeza kwenyehadithi hadithi ya juujuu inayoweza kupatikana kwenye Bihar al-Anwar, na inasomeka ifuatavyo: Bihar al-Anwar, Juz. Juz. 67, 67, uk.uk.6262na inasomeka ifuatavyo:

4 4

5

‫سهُ الَتِي بَيْنَ َج ْن ِب ْيه‬ َ ‫الج َھاد َمن َجا َھ َد نَ ْف‬ َ ‫ثُ َم قال ص أ ْف‬ ِ ‫ضل‬

Nahjul-Fasaha, uk.230, 397(mkusanyiko wa maneno mafupi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa mfano – Jihadi iliyo bora ni mtu kupambana na nafsi yake 30 na matamanio yake.

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 30

32

7/10/2013 3:33:30 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kubwa?" Akajibu: "Kupambana na nafsi yako mwenyewe"4

sana, yaani uhai wao, kwa lengo la kutetea Uislamu. Walishtuka na kushangaa ni maadui kitu gani hicho Masahaba walikuwa wamewashinda zao kwenye vita ambacho kali na walikuwakikubwa tayari kujitolea kiti wamachokipenda sana,Mtume yaani uhai kingekuwa kuliko hicho. Mtukufu alijibu: wao, kwa lengo la kutetea Uislamu. Walishtuka na kushangaa ni “Jihadi ya nafsi.” Maana yake ni kupigana na nafsi yako kitu gani hicho ambacho kingekuwa kikubwa kuliko hicho. mwenyewe, mapambano dhidi ya nafsi yako. Mtukufu Mtume alijibu: “Jihadi ya nafsi.” Maana yake ni kupigana na nafsi yako mwenyewe, mapambano dhidi Abu ya nafsiDharr yako. alimuuliza Katika hadithi mashuhuri sana Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.): “Ni jihadi gani iliyo Katika hadithi mashuhuri sana Abu Dharr alimuuliza Mtukufu bora zaidi?” Mtume Muhammad (s.a.w.w.): “Ni jihadi gani iliyo bora zaidi?”

"‫"ان يجاھد الرجل نفسه وھواه‬ “Kupambana nafsi na tamaa “Kupambana nana nafsi yakoyako na tamaa zako.”5 zako.”5 Mfanano ujenzi wa kwenye nafsi kwenye mapambano Mfanano wawa ujenzi wa nafsi mapambano ya ndani kwa ya ndani kwa hakika una mizizi ndani yaKwa Qur`ani. mfano, Qur`ani hakika una mizizi ndani ya Qur`ani. mfano,Kwa Qur`ani inasema: inasema: ��������� ��������� ������� ����� ���� �������� ���� ���� � ������������

4

‫ِين‬ َ ‫ﷲ َل َغنِيٌّ َع ِن ْال َعا َلم‬ َ َّ َّ‫َو َمنْ َجا َھ َد َفإِ َّن َما ي َُجا ِھ ُد لِ َن ْفسِ ِه ۚ إِن‬

Al-kafi, Juz. 5. uk. 12, namba 3 na Al-Amali na al-Saduq, kikao cha 71, uk. 377, na. 8. Ipo nyongeza kwenye hadithi ya hapo juu inayoweza kupatikana kwenye Biharanayejitahidi, al-Anwar, Juz. 67, uk.basi 62 nabila inasomeka ifuatavyo: “Na shaka anajitahidi kwa ajili

ya nafsi yake, kwa hakika Mwenyezi Mungu si muhitaji kwa ‫هُ الَتِي بَيْنَ َج ْن ِب ْيه‬walimwengu.” ‫س‬ ‫ضل‬ َ ‫الج َھاد َمن َجا َھ َد نَ ْف‬ َ ‫ثُ َم قال ص أ ْف‬ ِ [29:6] 5 Nahjul-Fasaha, uk.230, 397(mkusanyiko wa maneno mafupi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa mfano – Jihadi iliyo bora ni mtu kupambana na nafsi yake Kufuatana na wafasili wengi wa Qur`ani, jitihada hizi na matamanio yake.

au mapambano haya (jihad) ambayo yametajwa hapa ni jihadi ya kiroho. Vipo vipande viwili vikuu vya ushahidi ambavyo wanavitumia katika kulithibitisha hili. Kwanza, matumizi ya 32 neno “yeye mwenyewe” [himself]: hili ni wazi kabisa kwani 5

ahjul-Fasaha, uk.230, 397 (mkusanyiko wa maneno mafupi ya Mtukufu N Mtume (s.a.w.w.) kwa mfano – Jihadi iliyo bora ni mtu kupambana na nafsi yake na matamanio yake. 31

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 31

7/10/2013 3:33:30 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

vitani askari hupigana kwa sababu; inaweza kuwa kwa ajili ya wanaokandamizwa, kwa ajili ya heshima ya Uislamu au kwa ajili ya nchi yake. Hata hivyo aya hii inataja sababu kuwa ni “yeye mwenyewe.” Pili, kabla ya hii Allah swt anasema:

ٍ ‫ﷲ َآل‬ ‫ت ۚ َوھ َُو ال َّسمِي ُع ْال َعلِي ُم‬ ِ َّ ‫ﷲ َفإِنَّ أَ َج َل‬ ِ َّ ‫ان َيرْ جُو لِ َقا َء‬ َ ‫َمنْ َك‬ “Mwenye kutumaini kukutana na Mwenyezi basi َّ ‫ِي‬Mungu, ‫ َھا ِد ِه‬itafika ‫ﷲ َح َّق ِج‬ ‫ف‬shaka, ‫و َجا ِھ ُدوا‬naye ِ bila َ hakika miadi ya Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.” [29:5]

‫ْال َعلِي ُم‬

Dhana hii ya kukutana na Allah swt pia ni sifa ya kiroho ْ‫ﷲ َل َم َع ْالمُح‬ ‫ِين‬ ‫ ُس ُب َل َنا‬ifuatayo ‫ا َل َن ْھ ِد َي َّن ُھ ْم‬yaani: ‫ا َھ ُدوا فِي َن‬aya ‫ِين َج‬ ‫[ َوالَّذ‬29:6] na kwa hiyo َ ‫ سِ ن‬inaendana َ ya َ َّ َّ‫ن‬na ِ‫ۚ َوإ‬aya inayozungumzia jihadi ya nafsi, kwani hii nayo pia ni sifa ya kiroho, Kama mambo yalivyo, haimaanishi kwamba aya hii haijumuishi jihadi ya mapambano ya kijeshi, lakini ni kwamba inajumuisha jihadi ya kiroho pia. Aya zifuatazo pia zinarejelea jihadi ya kiroho, ingawaje zinaweza pia kujumuisha jihadi kijeshi, jihadi ya kijeshi nayo pia َّ ‫ أَ َج َل‬ya َّ ‫ُو لِ َقا َء‬kwani ٍ ‫ﷲ َآل‬ ‫ت ۚ َوھ َُو ال َّسمِي ُع‬ ‫ان َيرْ ج‬ ‫َمنْ َك‬ َّ‫ﷲ َفإِن‬ ِ ِ َ inahitaji utakaso wa nia na nafsi.َ

ٍ ‫ﷲ َآل‬ ‫ت ۚ َوھ َُو ال َّسمِي ُع ْال َعلِي ُم‬ ِ َّ ‫ﷲ َفإِنَّ أ َج َل‬ ِ َّ ‫ان َيرْ جُو لِ َقا َء‬ َ ‫َمنْ َك‬ ‫ﷲ َح َّق ِج َھا ِد ِه‬ ِ َّ ‫َو َجا ِھ ُدوا فِي‬ ‫َھا ِد ِه‬Mungu ‫ﷲ َح َّق ِج‬ ‫وا فِي‬inavyosta‫َو َجا ِھ ُد‬ ِ َّ kama “Na ipiganieni dini ya Mwenyezi hiki…..”

[22:78]

‫ِين‬ َ ‫ﷲ َل َم َع ْالمُحْ سِ ن‬ َ ‫َوالَّذ‬ َ َّ َّ‫ِين َجا َھ ُدوا فِي َنا َل َن ْھ ِد َي َّن ُھ ْم ُس ُب َل َنا ۚ َوإِن‬ ‫ِين‬ َ ‫ﷲ َل َم َع ْالمُحْ سِ ن‬ َ ‫َوالَّذ‬ َ َّ َّ‫ِين َجا َھ ُدوا فِي َنا َل َن ْھ ِد َي َّن ُھ ْم ُس ُب َل َنا ۚ َوإِن‬ “Na wale wanaojitahidi kwa ajili Yetu, lazima tutawaongoza kwenye njia Zetu. Na bila shaka Mwenyezi Mungu yu pamoja na wafanyao mema.” [29:69] 32

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 32

7/10/2013 3:33:31 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Kupigana na adui wa ndani mwako ni mapambano makubwa zaidi kwa sababu ni magumu zaidi. Pale adui anapopatikana ndani ni hatari zaidi na ni vigumu zaidi kumshinda. Ni vigumu zaidi kukabiliana na vita ya wenyewe kwa wenyewe kuliko ile ya adui anayetoka nje na kupigana naye kwenye mipaka ya nchi. Ni vigumu zaidi kumfukuza mtu ambaye yumo ndani ya nyumba kuliko yule ambaye yuko nje. Kama adui yetu yumo ndani mwetu basi anajua siri zetu zote.Anajua udhaifu wetu na nguvu zetu zilipo kwa hiyo anajua kwa usahihi kabisa jinsi ya ‘kutuchezea’ sisi. Adui aliyeko ndani mwetu wakati wote yu na sisi na haturuhusu kupumzika. Tunaweza tukafanya mazungumzo ya kusitisha mapigano na adui wa nje lakini kuhusu adui alioko ndani mwetu vita huendelea wakati wote usiku na mchana bila kukatika. Na kwa bahati mbaya adui huyu aliyeko ndani mwetu tunampenda na kumfurahikia kwa sababu adui huyu ni nafsi yetu wenyewe. Nafsi imetufanyia mambo mengi sana mabaya na bado tunaipenda. Kwa hiyo hivi ni vita vigumu sana na vipana. Tunapaswa kudhamiria kweli kweli na kuwa na hadhari kikamilifu. Kwa kweli Mwenyezi Mungu anapaswa kuwa na huruma nasi kama kweli tunataka kushinda vita hii. Inatubidi kutambua kwamba, pamoja na changamoto zote za kukabiliana nazo kwenye mapambano haya, mwishoni haitakuwa vigumu sana. Mwenyezi Mungu ataongoza na kufanya iwe rahisi kwa wale ambao wanataka ushindi kweli. Ni muhimu sana kwamba tunapokijua kitu tunatakiwa tukifanye kwa vitendo, halafu Mwenyezi Mungu atatupatia ujuzi wa vitu ambavyo hatuvijui. Kama tukivifanyia mazoezi vitu vidogo tunavyovijua vitatia nuru kwenye njia iliyoko mbele yetu. 33

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 33

7/10/2013 3:33:31 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

2. Mambo ya Kiroho kama dawa. Njia nyingine ni kuyachukulia mambo ya kiroho kama aina fulani ya dawa kwa ajili ya nafsi au roho zetu. Matatizo ya kiroho yanaelezewa kama maradhi na kwa hiyo tunahitaji kujitibu kwa kutumia dawa maalum. Sisi ni wagonjwa tunaohitaji tiba, tunahitaji dawa.Kama vile ilivyo kwa miili yetu, nafsi zetu zinaweza pia kuugua maradhi. Kwa bahati mbaya aina ya ugonjwa mgumu zaidi ni pale tunapougua kwa ndani kabisa ya nafsi zetu. Kwenye aya kumi na mbili Qur`ani inazungumzia kuhusu kundi la watu wanaougua “maradhi ndani ya nyoyo zao.” Ugonjwa huu unaweza kuongezwa na Mwenyezi Mungu kwa sababu wahusika hawataki kutibiwa na wanasisitiza kuendelea kuugua. Kwa mfano tunasoma:

َّ ‫وب ِھ ْم َم َرضٌ َف َزادَ ُھ ُم‬ ‫ﷲُ َم َرضًا‬ ِ ُ‫فِي قُل‬ “Katika nyoyo zao, mna maradhi, na Mwenyezi Mungu

ْ‫ون إِ َّال َمن‬ ‫ون َي ْو َم َال َي ْن َف ُع‬ ‫[و َال ُت ْخ ِزنِي َي ْو َم ُيب‬2:10] َ ‫َما ٌل َو َال َب ُن‬amewazidishia َ ‫ َْع ُث‬maradhi…….” َ ٍ ‫ﷲ ِب َق ْل‬ ‫ب َسل ٍِيم‬ َ َّ ‫أَ َتى‬ َّ ‫وب ِھ ْم َم َرضٌ َف َزادَ ُھ ُم‬ ُ‫فِي قُل‬na safi: ‫م َرضًا‬kuhusu َ ُ‫ﷲ‬ Pia Qur`ani inazungumzia nyoyo zilizo ِ imara ْ‫ون إِ َّال َمن‬ َ ‫ون َي ْو َم َال َي ْن َف ُع َما ٌل َو َال َب ُن‬ َ ‫َو َال ُت ْخ ِزنِي َي ْو َم ُيب َْع ُث‬ ٍ ‫ﷲ ِب َق ْل‬ ‫ب َسل ٍِيم‬ َ َّ ‫أَ َتى‬ “Wala usinifedheheshe siku watakapofufuliwa watu. Siku ambayo haitafaa mali wala mtoto. Isipokuwa mwenye kuja kwa Mwenyezi Mungu na moyo safi.” [26:87-89] 34

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 34

7/10/2013 3:33:31 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Hili ni ombi la Mtume Ibrahim (a.s.). Katika aya ya [37:83-84], Mwenyezi Mungu anatutaarifu kwamba ombi hili lilikubaliwa: “Na hakika Ibrahimu alikuwa katika kundi la (Nuh). Alipomjia Mola Wake kwa Moyo safi.” Hivyo, tunaweza kuelewa kwamba kule kuwa na moyo safi na imara ni muhumu sana hivyo kwamba mtu kama Mtume Ibrahimu, baba wa dini zote zinazomuabudu Mwenyezi Mungu Mmoja alimuomba Mwenyezi Mungu amsaidie. Hakika, hiki ndicho tu kitu pekee ambacho kitakuwa chenye manufaa Siku ya Hukumu siku ambapo sio watoto wala fedha zitatufaa. Kwenye Nahjul Balaghah, hotuba Na. 388, Imam Ali (a.s.) anasema: “Mojawapo ya majanga linaloweza kumtokea mtu ni umasikini, lakini gumu zaidi kuliko umasikini ni maradhi. Na gumu zaidi kuliko maradhi ya mwili ni maradhi ya moyo.” Kwa hiyo umasikini mbaya zaidi ni kuugua maradhi ya kukosa ucha-Mungu. Dhana ya tiba pia ni mada husika muhimu sana. Imam Ali (a.s.) anasema katika hotuba ya Wacha Mungu: “[Wacha Mungu ni]ni]wale wanaosimama na kusoma “[Wacha Mungu wale wanaosimama na kusoma sehemu seheya Qur`aniusiku, usiku, na na hujaribu hujaribu kujihuzunisha. Hujaribu mu ya Qur`ani kujihuzunisha. Hujaribu kuchukua tiba kutoka kwenye Qur`ani kama dawa ya marakuchukua tiba kutoka kwenye Qur`ani kama dawa ya 6 maradhi yao..” dhi yao..” 6 Imam Baqir (a.s.)(a.s.) alimwambia Jabir b. Yazid al-Ju‘fi: Imam Baqir alimwambia Jabir b. Yazid al-Ju‘fi:

‫سالَ َم ِة‬ ‫ب ا ْل ﱠ‬ َ ‫سالَ َمةَ َك‬ َ ‫سالَم ِة َو ال‬ ِ َ‫َو اَ ْعلَ ْم أنَهُ ال ِع ْل َم َكطَل‬ ‫ب‬ ِ ‫ا ْلقَ ْل‬ “Na tambua ya kwamba hakuna elimu kama ya kutafuta tambua ya kwamba hakuna elimu kama ya kutafuta 7 afya, na“Na hakuna afya kama afya ya nafsi.” 7 afya, na hakuna afya kama afya ya nafsi.”

Nahj al-Balaghah, Hotuba 193. 7 Tuaf al-Uqul, uk.284. Kuhusu dawa ya kiroho, jambo muhimu ni kwamba ni lazima 6

tujaribu kuyakinga maradhi yasipenye hadi kwenye nafsi zetu, kama vile ambavyo tungejaribu kuwa mbali na wagonjwa, ili 35 maradhi yao yasijetuathiri; kwani, kwa kuwa karibu na wagonjwa tutakuwa tunahatarisha afya zetu wenyewe. Hata hivyo, zipo tiba kwa ajili ya maradhi yetu, kwani Allah swt. ni Mwingi wa Msamaha. Zaidi ya hayo, tunahitaji kiongozi ambaye ataweza 09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 35

7/10/2013 3:33:31 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Kuhusu dawa ya kiroho, jambo muhimu ni kwamba ni lazima tujaribu kuyakinga maradhi yasipenye hadi kwenye nafsi zetu, kama vile ambavyo tungejaribu kuwa mbali na wagonjwa, ili maradhi yao yasijetuathiri; kwani, kwa kuwa karibu na wagonjwa tutakuwa tunahatarisha afya zetu wenyewe. Hata hivyo, zipo tiba kwa ajili ya maradhi yetu, kwani Allah swt ni Mwingi wa Msamaha. Zaidi ya hayo, tunahitaji kiongozi ambaye ataweza kutuonyesha nini cha kufanya na jinsi ya kuzuia au kutibu maradhi yetu. Jambo moja zuri sana ambalo Imam Ali (a.s.) amesema kuhusu Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ni kwamba Mtume (s.a.w.w.) alikuwa daktari, lakini hakuwangoja wagonjwa; badala yake alikuwa akiwaendea yeye mwenyewe, akiwa amebeba vitendea kazi vyake. “Mtume alikuwa kama tabibu anayekwenda huku na huko akiwa ametayarisha dawa zake na kuchemsha vitendea kazi vyake. Yeye (s.a.w.w.) alikuwa akizitumia (tiba zake) popote pale huduma ilipohitajika ya kutibu nyoyo povu, masikio yasiyosikia, na ndimi zilizokuwa bubu. Alifuatilia sehemu zilizoghafilika na sehemu zilizochanganyikiwa.� Walikuwepo watu ambao walikuwa viziwi, vipofu, au wale ambao hawakuweza kuongea ukweli, na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alitumia dawa inayofaa kuwatibu watu hao. Imam Mahdi (a.s.) ambaye ni Imam wa zama zetu pia anao mchango mkubwa; na kama Allah swt akipenda tutapata muongozo na tiba kutoka kwake (a.s.). 3. Mambo ya Kiroho kama Safari. Kwenye fasihi ya Kislamu, mambo ya kiroho pia yameelezewa kama safari.Tunatakiwa kujihisi kama wasafiri. 36

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 36

7/10/2013 3:33:31 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Tumeanza safari kuelekea mbali na Mwenyezi Mwenyezi Mungu na sasa tunarudi Kwake. Sote sisi tumeumbwa na Mwenyezi Mungu na uumbaji Wake ni namna ya kututenganisha na asili yetu. Kabla hatujaumbwa hatukutenganishwa na Mwenyezi Mungu lakini sasa tumetenganishwa. Hata hivyo Mwenyezi Mungu ametupatia fursa ya kurudi Kwake. Qur`ani inasema:

‫ُون‬ َ ‫� َوإِ َّنا إِ َل ْي ِه َرا ِجع‬ ِ َّ ِ ‫إِ َّنا‬ “….. Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na sisi tu wenye kurejea kwake.” [2:156]

Tunapoondoka hapa duniani, mwisho wa safari yetu unaeleweka wazi. Lakini, ili tuweze kufika kituoni kwetu, lazima tuwe waangalifu sana kuhusu upande tunakoelekea. Kama tupo kwenye njia iliyonyooka, hakika tutafika kwenye kituo chetu. Hata hivyo, kama tunafuata njia iliyopotoka hatutafika kwenye kituo chetu na inawezekana hata tukaenda mbali na mbali zaidi ya kituo chetu. Hapa tulipo hatupo kwenye sehemu iliyotulia ama iliyotengwa. Kila siku na kila saa tupo katika mwendo na ama tunakwenda mbali zaidi au tunasogelea kituoni kwetu. Qur`ani inasema:

َ ‫ك َك ْدحً ا َفم َُالقِي ِه‬ َ ‫ك َكا ِد ٌح إِ َل ٰى َر ِّب‬ َ ‫اإل ْن َسانُ إِ َّن‬ ِ ْ ‫َيا أ ُّي َھا‬ “Ewe mtu hakika wewe ni mwenye kufanya juhudi kwa Mola wako, juhudi ambayo utaikuta” [84:6]

Baada ya kusoma aya hii, watu wengine wanaweza kufikiri kwamba hakuna lolote la kuhofia kwa sababu sote 37

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 37

7/10/2013 3:33:32 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

tumetoka mahali pazuri na kuna mwisho mzuri mbele yetu. Lakini hali zetu wakati tunapokutana na Mwenyezi Mungu ni muhimu sana. Zipo namna mbili za kumfikia Mwenyezi Mungu: kukutana Naye ambapo anafurahishwa nasi au kukutana Naye ambapo ametukasirikia. Binadamu ni miongoni mwa viumbe wachache sana ambao kiwango chao cha ukamilifu hakipangwi, yaani, wamepewa uwezo wa kujitahidi kujinyanyua au kujishusha wenyewe. Hivyo kwamba, safari ya kiroho ni pamoja na kujaribu kuongeza ukaribu na ujirani wetu kwa Mwenyezi Mungu. Lazima izingatiwe kwamba wakati wote Mwenyezi Mungu yu karibu na sisi, lakini sisi inakuwa hatujilazimishi kuwa karibu Naye. Tunaweza tukafikia mahali tukawa karibu zaidi na Mwenyezi Mungu kupitia utakaso wa nafsi, na kama ambavyo imependekezwa na Qur`ani Tukufu “kukutana� Naye. Kwa kawaida, masufi husema kwamba upo uwezekano wa sisi kupoteza utu wetu, ukomo na mipaka yetu, halafu ndipo tunakuja kuhusishwa na Mwenyezi Mungu. Mimi sishereheshi fikira hii hapa, lakini kwa namna yoyote ile inaelekea wazi kwamba tunaweza kufika karibu zaidi na zaidi kwa Mwenyezi Mungu hadi kufika kiwango ambapo panakuwa hakuna kitu kilichobakia baina yetu sisi na Yeye na hii ndiyo maana ya kurejea kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo maisha haya ni safari na hatuwezi kusema kwamba hatutaki kwenda katika safari hii. Sote tupo katika safari hii na ni juu yetu sisi wenyewe kukusanya masurufu yetu ya kututosha. Mojawapo ya malengo makuu ya ujenzi wa nafsi ni kujaribu kupunguza umbali huu kwa kusafiri kuelekea kwa Allah swt. Njia ya kuelekea Kwake haina mwisho na imejaa changamoto. Hata hivyo, kwa wale watu 38

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 38

7/10/2013 3:33:32 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

wanaoanza safari hii, msaada wote na muongozo vinatolewa. Kuhusu hili, Imam Sajjad (a.s.) anasema: “Na utukuzwe! Ni nyembamba kiasi gani njia ya wale ambao hutawaongoza, na ni njia wazi kiasi gani hiyo kwa wale ambao umewaongoza!�8 Hitimisho: Kwenye sehemu hii tumezungumzia mambo ya kiroho au mchakato wa ujenzi wa nafsi kama aina fulani ya vita, dawa na kama safari. Allah swt anatutia moyo na anatuongoza kwa kutuonyesha mifano mingi. Anatuonyesha kwamba wakati wote matumaini ya kumfikia Yeye yapo na anatusihi kwa kutumia njia nyingi mbalimbali katika kutuhimiza sisi kujikurubisha Kwake. Yeye ni Mwingi wa Rehema.

8

Mafatih al-Jinan, Munajat al-Muridin. 39

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 39

7/10/2013 3:33:32 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

KUTUPIA MACHO MCHAKATO WA UJENZI WA NAFSI

M

chakato wa ujenzi wa nafsi una hatua tofauti mbalimbali. Nitajaribu kuchunguza kwa ufupi mchakato mzima na kurejelea kwenye hatua zake kuu. Kuzindukana au kuwa makini na nafsi: Hatua ya kwanza kabisa ni kuzindukana [yaqzah], yaani kuzindukana kutoka kwenye kujishughulisha sana na mambo ya kidunia kufuta uzembe. Kuzinduka 1. na Kuzindukana au kuwa makini na nafsi:ni kukumbuka mtu kuangalia ucha-Mungu wake, maisha na mambo ya kiroho. HatuaKhomeini; ya kwanzakama kabisa ilivyo ni kuzindukana [yaqzah], yaani Imam kwa wanachuoni wengine, kuzindukana kutoka kwenye kujishughulisha sana na mambo ya ameandika kitabu kiitwacho; “Jihadi Kubwa” [Jihad-e Akhkidunia na kufuta uzembe. Kuzinduka ni kukumbuka mtu bar],kuangalia ambacho ni mkusanyiko wanamihadhara aliyoitoa ucha-Mungu wake, maisha mambo ya kiroho. Imam yeye kama ilivyo wanachuoni wengine, ameandika kwaKhomeini; wanafunzi wake wakwa Hawzah, anasema kwamba hatua ya kitabu ya kiitwacho; “Jihadi Kubwa” [Jihad-e Akhbar], ambacho ni Kwa kwanza mtu kujitakasa mwenyewe ni kuzindukana. mkusanyiko wa mihadhara aliyoitoa yeye kwa wanafunzi wake wa hakika, baadhi ya kwamba wafuasihatua wa Usufi wanaamini kwamba hii Hawzah, anasema ya kwanza ya mtu kujitakasa ni hatua tangulizi tu na kwamba hatuabaadhi ya kwanza huja mwenyewe ni kuzindukana. Kwa hakika, ya wafuasi wabaada Usufi wanaamini kwamba hii ni hatua tangulizi tu na kwamba ya mtu kuzindukana. Hata hivyo, hapana shaka kwamba kwanza huja baada pa ya mtu kuzindukana. hivyo, huuhatua ni ya mwanzo. Mahali kuondokea ni Hata kuzindukana. hapana shaka kwamba huu ni mwanzo. Mahali pa kuondokea ni Tungeweza kusema kwamba sotekwamba ‘tumezinduka,’ lakini huku ni kuzindukana. Tungeweza kusema sote ‘tumezinduka,’ kuzindukana namnakwa iliyotofauti. Kufutana na hadithi, lakini huku nikwa kuzindakana namna iliyotofauti. Kufutana na hadithi, Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amesema: Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amesema: ‫س نِيَا ُم فَإ َذا َماتُوا انُتَبَ ُھوا‬ ُ ‫ا ْلنَ ْف‬ 9 kufa.”9 “Watu wamelala huzindukana tu baada “Watu wamelala na na huzindukana tu baada ya kufa.”ya

9

Bihar al-Anwar, Juz. 50. huzindukana uk. 134. Watu wanapokufa, na kamwe hawalali tena. Lakini

sasa huwa ni kuchelewa sana. Kisha wanakuwa kama msafiri ambaye anazindukana wakati 40 gari moshi limekwishaondoka, wakati ndege imekwisharuka. Wakati huo, hakuna sababu au faida ya kwenda uwanja wa ndege kwa sababu pamoja na kwamba sasa umeamka, tayari umekosa ndege. Unachoweza kufanya ni kujilaumu na kujisikitikia. Unaweza kusema kwamba utakamata 09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 40

7/10/2013 3:33:32 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Watu wanapokufa, huzindukana na kamwe hawalali tena. Lakini sasa huwa ni kuchelewa sana. Kisha wanakuwa kama msafiri ambaye anazindukana wakati gari moshi limekwishaondoka, wakati ndege imekwisharuka. Wakati huo, hakuna sababu au faida ya kwenda uwanja wa ndege kwa sababu pamoja na kwamba sasa umeamka, tayari umekosa ndege. Unachoweza kufanya ni kujilaumu na kujisikitikia. Unaweza kusema kwamba utakamata ndege inayofuata lakini kwa bahati mbaya hakuna safari za ndege tena. Ni mwisho wa dunia, hiyo ilikuwa ndege ya mwisho na tukaikosa kwa sababu tulikuwa tumelala. Kwa hiyo, na tuzinduke, kama tukipata fahamu pale tu tunapokufa, hatuwezi kufanya lolote, kwani bahati haiji mara mbili. Allah swt anasema kuhusu watu ambao huomba kurudishwa, ili waweze kuja kutenda mema. Yeye anajibu: “….Hapana, hakika hili ni neno tu analolisema…..” [23:100]. Kama akipewa nafasi, wala hatabadilika, na hata hivyo, hakuna fursa hiyo; wanangojea tu Siku ya kufufuliwa. Kwa bahati mbaya, kifo kimezoeleka sana au kufanywa jambo la kawaida hivyo kwamba hatufikirii kwamba ipo siku tutakufa, na kila wakati kitatokea kwa mtu mwinginewe. Kwa mujibu wa mshairi wa Kiajemi anasema hivi kwenye shairi lake: “sisi ni kama kundi la kondoo, ambao huchukuliwa mmoja mmoja na kwenda kuchinjwa. kila mmoja anafurahia, bila kufikiria kwamba watafuatia.” Kufuatana na hadithi, Tawrat ya Musa inasema:

41

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 41

7/10/2013 3:33:32 PM


“sisi ni kama kundi la kondoo, ambao huchukuliwa m mmoja mmoja na kwenda kuchinjwa. kila mmojaUJENZI anafurahia, bila kufikiria NA UTAKASO WA kwamba NAFSI watafuatia.” Kufuatana na hadithi, Tawrat ya Musa inasema:

‫ت َكيْفَ يَ ْف َرح‬ ِ ‫ع َِجبْتُ لِ َمنْ أَ ْيقَنَ بِا ْل َم ْو‬ staajabu kwamba ambayeana ana hakika hakika kwamba “Nina “Nina staajabu kwamba mtumtu ambaye 10 kwamba atakufa, anaweza kufurahia kamwe.” atakufa, anaweza kufurahia kamwe.”10 Kwa hiyo, hiyo, tunahitaji tunahitaji kuwa nana kuzinduka kabla Kwa kuwananatahadhari tahadhari kuzinduka kabla hatujafa. Wakati mwingine hili hutokea kupitia tukio muhimu sana hatujafa. Wakati mwingine hili hutokea kupitia tukio muhimu kama vile kuondokewa na ndugu, ugonjwa mbaya, au kukutana na sana kama vile kuondokewa na ndugu, ugonjwa mbaya, au mtu mchamungu. Hata hivyo, tusingoje jambo litokee kabla kukutana na mtu mchamungu. Hata hivyo, tusingoje jambo 10 litokee kabla hatujabadilika; tunaweza kubadilika tu, kwani Irshaad al-Qulub, Juz. 1, uk. 74 hatuna uhakika kwamba jambo lolote linaweza hatujabadilika; tunaweza kubadilika tu, kwani hatunakutokea. uhakika 42 kwamba jambo lolote linaweza kutokea.

Ni rahisi sana kuzinduka; kinachotakiwa ni dhamira na sisi wenyewe kuhusukinachotakiwa umuhimu na maana na ya sisi maisha Ni rahisitufikirie sana kuzinduka; ni dhamira wenyewe tufikirie umuhimukaribu na maana ya maisha haya, hii haya, hii safari yakuhusu kutufikisha zaidi na Allah swt ni safari ya kutufikisha karibu zaidi na Allah swt. ni yetu sisi. Ni yetu sisi. Ni nafasi hii tu tuliyonayo ya kukusanya masurufu nafasi hii tu tuliyonayo ya kukusanya masurufu yetu kwa ajili ya yetusafari kwayetu ajili safari ya wa Akhera. Kwa Ali mujibu ya ya Akhera. Kwayetu mujibu hadithi,Imam (a.s.) wa hadithi,Imam Ali (a.s.) anasema: anasema:

‫ان ا ْللَيل و الن َھار يَع َمالَن فيك؛ فَاعمل فيھما‬ “Nyakati za mchana nanausiku wakati wote zinakuathiri “Nyakati za mchana usiku wakati wote zinakuathiri wewe kwa wewe piapia unapaswa kujaribu kuziathiri wewehiyo kwa hiyo wewe unapaswa kujaribu kuziathiri nyakati hizi.”11 nyakati hizi.”11 Maana yake maisha yako yanapita haraka. Kila wakati Maana yakeni kwamba ni kwamba maisha yako yanapita haraka. wa mchana na wa usiku unakunya wewe kuwa mzee zaidi .Kwa Kilamaneno wakatimengine, wa mchana na wa usiku unakufanya wewe kuwa kila mchana na usiku unakupeleka wewe karibu mzee zaidi .Kwa maneno kila kwa mchana na usiku na mwisho wa maisha yako mengine, ya hapa duniani, hiyo, jaribu kufanya kitu. wewe karibu na mwisho wa maisha yako ya unakupeleka hapa duniani, kwa hiyo, jaribu kufanya kitu.

Upo mfano mzuri sana kuhusu hali zetu. Maisha ya hapa duniani yanafananishwa na kamba kwa ajili ya mtu aliyeingia ndani ya 10 Irshaad al-Qulub, uk. 74 na jinsi ya kuokoka kwake ni kushikilia kisima chenyeJuz. kina1,kirefu 11 Ghurar al-Hikam, Na.120. kamba tu. Kama akiikosa kamba hii amekwisha. Halafu pia, huko juu ya kisima, wapo panya wawili moja mweupe mwingine mweusi 42 unakuja ambapo kamba hiyo ambao wanatafuna kamba. Wakati itakatika. Panya hao wamedhamiria kweli hawako tayari kuondoka. Hii ndiyo hali tuliyonayo. Kamba inawakilisha maisha yetu. Panya 11

Ghurar al-Hikam, Na.120. 09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 42

7/10/2013 3:33:32 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Upo mfano mzuri sana kuhusu hali zetu. Maisha ya hapa duniani yanafananishwa na kamba kwa ajili ya mtu aliyeingia ndani ya kisima chenye kina kirefu na jinsi ya kuokoka kwake ni kushikilia kamba tu. Kama akiikosa kamba hii amekwisha. Halafu pia, huko juu ya kisima, wapo panya wawili mmoja mweupe mwingine mweusi ambao wanatafuna kamba. Wakati unakuja ambapo kamba hiyo itakatika. Panya hao wamedhamiria kweli hawako tayari kuondoka. Hii ndiyo hali tuliyonayo. Kamba inawakilisha maisha yetu. Panya mweupe anawakilisha mchana na panya mweusi anawakilisha usiku. Wakati wote nyakati za mchana na usiku ‘zinatafuna’ maisha yetu na wakati wowote ‘tutadondoka’ na kufa. Wakati huu ambao tuko hai, ndiyo tu fursa ya pekee ambayo tumepewa. Hivyo basi, lazima tuzindukane na kuwa waangalifu sana na maisha haya. 2. Kuitambua Nafsi Yake Mtu Mwenyewe: Baada ya kuwa tumezinduka, tunapaswa kujaribu kuona ni nyenzo, fursa na mambo gani ya kuchagua yanayopatikana mbele yetu. Sasa kwa vile tumezinduka, tunataka kufanya kitu. Ni kama mtu ambaye hana kazi au biashara ya kufanya na kwa hiyo hana chanzo cha mapato. Kila mtu anamwambia awajibike kwa kufanya kitu chochote. Anakubali kwamba anapaswa kujishughulisha lakini hajui afanye nini. Mtu huyu hawezi kuanza kufanya kitu chochote bila kuwa na kianzio. Kwanza kabisa mtu huyu anatakiwa kugundua aina gani ya uwezo na ujuzi alionao. Anatakiwa kujua anao wigo wa upana gani wa kuchagua la kufanya. Mathalani, anapaswa ajaribu kujifunza kuhusu hali ya soko la biashara. Anapaswa ajue nani wamefan43

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 43

7/10/2013 3:33:32 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ikiwa ili awachukue hao kama kigezo. Anapaswa pia kuwatambua watu ambao wamefilisika ili aweze kujifunza kutokana na hali zao asije na yeye akafilisika. Huku ndiyo ‘elimu ya nafsi’ (ma`rifat al-nafs) na inachukuliwa kuwa ni “elimu yenye manufaa sana.” Kwa nini mara nyingi sisi huwa na mazoea ya kujisahau wenyewe na badala yake tunajua mambo mengine? Mathalani, wapo watu ambao wanaweza kutumia muda wote wa maisha yao wakichunguza aina mbalimbali za wadudu adimu lakini hawako tayari kutumia hata saa moja wakae mahali peke yao wajaribu kugundua Mwenyezi Mungu ameweka nini ndani mwao. Waislamu masufi wanasema kwamba zipo dunia mbili: dunia ya nje ambayo inajumuisha uzuri wa kimaumbile ya binadamu, wanyama, mimea na viumbe visivyo na uhai Waislamu masufi kwamba zipo dunia mbili: duniaya ya ndani vilivyoumbwa nawanasema Mwenyezi Mungu na pia dunia nje ambayo inajumuisha uzuri wa kimaumbile ya binadamu, ambayo imo ndani mwetu. Na wanasema kwamba dunia hii wanyama, mimea na viumbe visivyo na uhai vilivyoumbwa na iliyopo ndani mwetu ndio dunia kuu zaidi. Kile ambacho Mwenyezi Mungu na pia dunia ya ndani ambayo imo ndani mwetu. Mwenyezi Mungu ameweka ndani ndani mwetu ni ndio kikubwa Na wanasema kwamba dunia hii iliyopo mwetu dunia zaidi kuliko ile dunia yote ya kimaumbile yetu. Ndiyo kuu zaidi. Kile ambacho Mwenyezi Munguiliyoko amewekanje ndani mwetu ni kikubwa zaidi kuliko ile hadith-e dunia yotequdsi ya kimaumbile iliyoko nje maana tunasoma katika nzuri sana: yetu. Ndiyo maana tunasoma katika hadith-e qudsi nzuri sana:

‫ب َع ْب ِدي‬ ُ ‫س َعنِي قَ ْل‬ َ ‫سعنِي‬ َ َ‫لَ ْم ي‬ ِ ‫ضي َو َو‬ ِ ‫س َمائِي و ال أَ ْر‬ ‫ا ْل ُمؤْ ِم ِن‬ “Wala si mbingu Yangu ama ardhi(dunia) (dunia) Yangu viweze “Wala si mbingu Yangu ama ardhi Yangu viweze kunizingira Mimi, ni moyo wa yule yule mtu anayeniamini kunizingira Mimi, ni moyo tutuwa mtu anayeniamini ndiyo unaoweza kunizingira Mimi.”12 Mimi.”12 ndiyo unaoweza kunizingira 12

Kutokana na kwenye hadithi hii, tunaweza kuelewa kwamba moyo wetu lazima uwe mkubwa kuzidi nyota zote na sayari zote, kuliko maumbe yote haya tunayoyaona.

Bihar al-Anwar, Juz. 55, uk. 39.

44

Hivyo basi, tunahitaji kujijua sisi wen yewe ipasavyo. Mara nyingi huwa tunakadiria kwa upungufu uwezo tulionao kwa ajili ya ukamilifu. Kuna uwezekano wa ukamilifu usio na ukomo mbele 09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 44 7/10/2013 yetu. Hata wale watu ambao ni watakatifu sana bado wanaweza

3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Kutokana na hadithi hii, tunaweza kuelewa kwamba moyo wetu lazima uwe mkubwa kuzidi nyota zote na sayari zote, kuliko maumbe yote haya tunayoyaona. Hivyo basi, tunahitaji kujijua sisi wenyewe ipasavyo. Mara nyingi huwa tunakadiria kwa upungufu uwezo tulionao kwa ajili ya ukamilifu. Kuna uwezekano wa ukamilifu usio na ukomo mbele yetu. Hata wale watu ambao ni watakatifu sana bado wanaweza kuendelea. Kila wakati huwepo fursa ya kwenda mbele zaidi kwa sababu umbali baina ya Mwenyezi Mungu na binadamu hauna kikomo kwa hiyo kila wakati upo uwezekano wa kwenda juu zaidi. Ndiyo maana huwa tunaomba baada ya tashahhud, “Ee, Mwenyezi Mungu tunakuomba ukubali shifaa (maombezi) ya Mtukufu Mtume juu yetu na pia unyanyue daraja lake.� Hii ina maana kwamba Mtume anaweza kwenda juu zaidi. Wengi wetu huridhishwa kwa urahisi sana na mafanikio yetu. Tunahitaji kudhamiria zaidi na kuwa na matarajio makubwa. Kama tunatosheka na vitu vidogo, basi tutapoteza na inawezekana hata yale madogo tushindwe kuyapata. Inasemekana hapo zamani palikuwepo na mwanachuoni (`alim) wa kidini ambaye mwanawe alikuwa mwanafunzi wa masomo ya kidini. Baba yake alimuuliza mwanae kwamba siku za usoni alitaka awe nani. Mwanae alijibu kwamba alitaka awe kama yeye (baba yake). Baba yake alijibu kwamba yeye alimsikitikia sana mwanae kwa sababu yeye mwenyewe alitaka kuwa kama Imam Ja`far Sadiq, ambaye alikuwa kigezo chake, na bado hali ile aliyokuwa nayo wakati huo ndicho alichopata. Alim huyo akamwambia mwanae kwamba, kama lengo lake ni kuwa kama yeye baba yake basi hatapata chochote. Hivyo basi, wakati wote tuwe na 45

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 45

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

shauku kubwa na kwa kweli Mwenyezi Mungu ametuumba na uwezekano huo ndani yetu. Kwa hiyo, tunahitaji kujijua sisi wenyewe, tunapaswa kuamini juu ya uwezo uliyopo ndani mwetu na tuvitambue vitu vyenye manufaa kwetu au vyenye madhara kwetu. 3. Kuchunga Nafsi Yake Mtu Mwenyewe: Baada ya kuzinduka, na utambuzi wa nafsi, tunahitaji kutunza nafsi. Haitoshi kuishia katika kujua vitu tu; elimu inapaswa kututumikia kwa kuiweka kwenye vitendo. Mathalani, kama unajua kwamba uvutaji sigara unaua lakini wewe unakuwa hujali afya yako na unaendelea kuvuta sigara, hakuna manufaa katika elimu hiyo. Kwa kweli, inakufanya wewe uwajibike zaidi, na kuhusika zaidi kwa sababu unajua. Bila shaka, hii haimaanishi kwamba tuepuke kujifunza. Kusema kwamba hatukujua si udhuru unaotosha; lazima tujifunze na tuutumie ujuzi huo kivitendo. Kwa hiyo tunahitaji kuchunga nafsi: Qur`ani inasema:

‫ض َّل إِ َذا‬ َ ْ‫ِين آ َم ُنوا َع َل ْي ُك ْم أَ ْنفُ َس ُك ْم ۖ َال َيضُرُّ ُك ْم َمن‬ َ ‫َيا أَ ُّي َھا الَّذ‬ ‫ون‬ َ ُ‫ﷲ َمرْ ِج ُع ُك ْم َجمِي ًعا َف ُي َن ِّب ُئ ُك ْم ِب َما ُك ْن ُت ْم َتعْ َمل‬ ِ َّ ‫اھْ َتدَ ْي ُت ْم ۚ إِ َلى‬ “Enyi mlioamini kilicho lazima juu yenu ni nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotoka ikiwa mmeongoka. Marejeo yenu wote ni kwa Mwenyezi Mungu, basi atawaambieni yale mliyokuwa mkiyatenda.” [5:105]

Kujichunga mwenyewe maana yake ni kushiriki kivitendo katika kutekeleza wajibu wa kijamii, kwani Uislamu ni dini 46

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 46

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

inayotutaka tujihusishe na maisha ya kijamii: wote tukiwa na moyo wa kuzindukana na ufahamu na kujua kile kinachoweza kutunufaisha au kutudhuru. Hata hivyo, kipo kitu ambacho huwatokea watu mara kwa mara katika hali hii. Wanapozinduka na kuwa na hisia kwenye mambo ya kiroho, halafu kwa bahati mbaya badala ya kujihusisha na ucha-Mungu wao, badala ya kujishughulisha zaidi na matatizo yao, huanza kuwahukumu watu wengine. Mathalani: huanza kufikiri kwamba mtu huyu hafai, yule ni mzembe, na mwingine wala si muumini wa kweli. Hii ni hatari sana. Kwanza kabisa, muumini wa kweli angeshughulikia matatizo yake mwenyewe. Tunafahamu kutokana na hadithi kwamba ni vema zaidi kwetu kama tutajishughulisha na matatizo na maradhi yetu badala ya kuwafikiria na kuwahukumu watu wengine. Kwa mfano, Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amenukuliwa akisema: “Amebarikiwa yule ambaye anajishughulisha sana kufikiria mapungufu yake mwenyewe hivyo kwamba hana muda wa kufikiria mapungufu ya wengine.�13

Kwa hiyo lazima tuanze na kujihakiki na kujitathimini sisi wenyewe kabla ya kuangalia mambo ya watu wengine. Wakati mwingine sisi wenyewe tunaweza kuwa na tatizo kubwa sana kwenye nafsi zetu lakini hatulitambui lakini bado tunaona tatizo la kiasi kama hicho linapokuwa kwa mtu mwingine. Mathalani, tunaweza kuwa tumekula kitu kama kitunguu saumu na hatutambui kwamba midomo yetu inanuka na bado tukikutana na mtu ambaye mdomo wake unanuka kwa namna hiyo hiyo, tunakuwa wepesi sana kufikiria au kusema kitu kuhusu hilo 13

Kwa mfano; tazama Bihar al-Anwar, Juz. ya 1. uk. 205. 47

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 47

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Ipo simulizi moja iliyoandikwa na Rumi kwenye ‘Mathnawi’ kwamba watu wanne walikuwa na ahadi ya kuonana na mfalme mara tu baada ya swala ya adhuhuri. Walikuwa na wasiwasi sana kwani hawakutaka kupoteza fursa hii ya kukutana na mfalme na hawakutaka kuchelewa. Kwa hiyo waliamua kuswali harakaharaka halafu waende kukutana na mfalme. Mara walipowasili msikitini walianza kuswali. Hata hivyo, wakati wakiwa katika swala, muadhini alifika msikitini na kupanda kwenye mnara. Sasa walianza kuwa na wasiwasi na walianza kushangaa endapo walianza kuswali mapema kabla ya muda au muadhini siku hiyo alichelewa kuadhini. Kwa hiyo, wakati wanaendelea na swala mmoja wao alimuuliza muadhini kama muda wa swala ulikuwa umefika au la. Yule wa pili alimuuliza wa kwanza kwa nini alizungumza wakati wapo kwenye swala kwa sababu hata kama muda wa swala umewadia au hapana lakini sasa ameharibu swala yake kwa sababu alizungumza wakati wa swala. Mtu wa tatu akasema kwamba mtu wa pili naye pia amezungumza wakati wa swala kwa kumuuliza mtu wa kwanza kwa nini alizungumza. Hata hivyo, mtu wa nne alidhani kwamba yeye “ni mjanja sana”. Alisema: ’Namshukuru Mwenyezi Mungu kwani mimi sikuongea!’ Hivyo, kwenye kisa hiki tunaona kwamba watu wanne walishiriki katika tatizo lilelile lakini kila mmojawao aliliona tatizo kwa mwenzake tu yeye hakujiona kwamba katenda kosa. Kwa hakika walikuwa wakirudia kosa lile lile ambalo walishutumiana wao wenyewe. Hivyo, ni bora sana kujishughulisha kuhusu sisi wenyewe badala ya kushughulika na watu wengine. Wakati mwingine watu hufikiria kwamba hii maana yake ni kwamba wao wasijali yale yanayotokea 48

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 48

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

pembezoni mwao, ndani ya jumuiya au jamii yao. Hivi sivyo. Lakini kama tunataka kuwa na manufaa kwa jamii yetu lazima kwanza tuanze kujisimamia sisi wenyewe ndipo tutakapoweza kuwasaidia wengine. Kwa mfano, tunaona pale yanapotolewa maelekezo ndani ya ndege kuhusu matumizi ya kuvaa kichuja hewa (mask) cha dharura, wale wanaotoa maelekezo wakati wote husisitiza kuanza na sisi wenyewe kwanza halafu ndipo tuwasaidie wengine. Vinginevyo, wakati tunapojaribu kuwasaidia wengine kwanza na vichuja oksijeni vyao, sisi wenyewe tunaweza kuanguka. Hivyo, lazima tujiangalie. Lakini tutajiangalia wenyewe vipi? Hivi tujichunge kwa kusali na kusoma Qur`ani tu? Hivi tuihudumie jamii kwa kufanya kazi za kijumuiya tu basi? 3. a. Kupata Imani na Itikadi zinazofaa: Kitu cha kwanza kabisa tunachohitaji kufanya ni kupata imani zinazofaa na uelewa wa dunia unaofaa. Kama unataka kuwa mfanya biashara mzuri lazima ulijue soko na watu walioko kwenye biashara kama hiyo. Unahitaji kujua hali halisi ya wakati uliopo, uwezekano wa siku za usoni na mambo yanayofanya kazi katika biashara hiyo makhsusi. Kama tunataka kufuzu hapa duniani lazima tujue ni Nani Aliye na udhibiti hapa. Kama tunataka kupata ruhusa ya kufanya biashara lazima tujue mahali inapopatikana ruhusa hiyo. Kwa hali hiyo hiyo, kama tunataka kuanza ‘biashara’ ya kiroho lazima tujue mahali inapopatikana ruhusa hiyo. Tunapaswa tujue sheria na kanuni zipi zinazotumika na ambazo zinapaswa kuzingatiwa. Tunapaswa tujue ni mahitaji 49

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 49

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

gani yanayotolewa na mikopo na misaada ya kifedha ya aina gani tunayoweza kupewa. Mshairi mashuhuri wa ki-Irani aitwaye Sa`di aliyeandika kitabu kiitwacho Gulstan na Bustan, anasimulia kisa kizuri sana. Anasema kwamba wakati fulani mtu alikwenda kufanya biashara zake katika nchi nyingine. Alitambua kwamba katika nchi ile kengele ambayo ilikuwa ikining`inizwa kwenye bafu ya ummah ilikuwa rahisi sana kuinunua. Kwa mfano kama kengele hiyo ingeuzwa kwa $ 100 huko kwao basi katika nchi ile ingeuzwa kwa $1. Kwa hiyo aliuza mali ya dukani kwake na kwa fedha yote aliyokuwa nayo alinunua takriban kengele 1000. Halafu mtu huyu alirudi kwao ambako alitegemea kupata faida ya $ 99 kutokana na mauzo ya kila kengele moja. Akasafirisha kengele zote hadi kwenye mji wa kwao. Hata hivyo tatizo ni kwamba palikuwepo na nyumba mbili au tatu za mabafu ya ummah katika mji wao kwa hiyo hakuna mtu aliyetaka kununua kengele hata alipoteremsha bei mpaka kufika nusu yake lakini hakuna aliyenunua. Kwa hiyo alipoteza mtaji wake wote kwa sababu hakufanya utafiti na kutambua ni mali za aina gani zingenunulika nchini mwake. Watu wengi wapo kama hivi na huwekeza kwenye vitu hapa duniani ambavyo havitakuwa na thamani huko Akhera. Tunawekeza maisha yetu, ambayo ni ‘mtaji’ mkubwa na wenye thamani sana ambao tumepewa, kwenye vitu ambavyo havina thamani huko Akhera, tutaambiwa kwamba havikuwa na faida kwa hiyo tumepoteza ‘mtaji huu.’ Kwa hiyo tunahitaji kuwa na imani na kujua njia ambayo maisha yetu hapa duniani yanaweza kutupatia furaha huko Akhera. Lazima tuwe na imani sahihi na hasa zaidi tunatakiwa kuwa waangalifu sana katika kuelewa uhusiano baina ya maisha 50

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 50

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

yetu hapa duniani na maisha yetu huko Akhera. Takriban theluthi moja ya Qur`ani Tukufu inazungumzia Akhera. Kuna msisitizo mkubwa sana juu yake wa kutufundisha sisi kwamba maisha ya Akhera ndio kitu ambacho hasa ni lazima tujiandae nacho kweli kweli. Mfano mwingine wenye manufaa unaweza kuonekana kwenye hadithi mbalimbali. Upo mfano kwenye kisa cha mtu aliyekuwa anafanya ibada mchana na usiku: siku moja malaika alipita hapo akifikiria kwamba, kwa bidii kama hii, mtu huyu lazima atakuwa na hadhi ya juu sana. Malaika alipokwenda karibu naye, alitambua kwamba mtu yule hakuwa na uelewa sahihi wa Mwenyezi Mungu, kwani alisema “Natamani ungekuwa na punda ili nimlishe huko shambani kwangu kwani ninayo majani mengi sana hapa.� Mtu huyu alimuona Mwenyezi Mungu kama binadamu, ambaye anamiliki punda. Imani ya aina hii haina malipo, na kwa hiyo aqidah ni jambo la kwanza kabisa linalotakiwa kupatikana. Lazima tujitahidi kupata uelewa uliosahihi wa Mwenyezi Mungu Muumba, nafasi Yake hapa duniani, kuamini Upekee Wake (tawhiid), Utume na Siku ya Kiyama. Kwa hiyo, kwanza lazima tuwe na itikadi sahihi, lakini sio aina ya itikadi tunayojifunza na kukariri tu kama kasuku. Lazima iwe ni itikadi ambayo tumeizamisha nafsini mwetu hivyo tukisema Mwenyezi Mungu ni Mmoja tu, basi iwe mwili wetu wote na nafsi yetu yote vimetamka kwamba sisi ni waabudu Mungu Mmoja tu.14 14

Ni muhimu mtu kuwa mwema, mwenye huruma na muangalifu lakini hayo hayatoshi kumpa nafasi Peponi: ni lazima pia tuwe na imani. Kama watu ni wema katika kushughulika na wenzao, lakini hawana imani, watu hao hawana nafasi ya kwenda Peponi: pengine inawezekana wasitupwe Jahannam, au adhabu yao itapunguzwa, lakini hawana njia ya kuipata Pepo. Kumwamini Mwenyezi Mungu, kama ni Mmoja na Muumba Pekee ni itikadi muhimu na msingi. 51

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 51

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

3.b. Kutekeleza vitendo vya ibada na kujizuia na dhambi na uovu: Tunapaswa kujaribu kutekeleza wajibu wetu na kuzingatia masharti yote ya dini yetu. Hata kama tuna imani inayofaa na kutekeleza wajibu wetu wote, lakini hatuachi kutenda dhambi, hatutafuzu. Kama mtu hunawa mikono yake mara kumi kwa siku lakini anaendelea kugusa vitu vichafu na vilivyonajisika, atachafuka tena. Haina maana kusema kwamba amenawa mara kumi kwa siku. Swala za kila siku ni kama josho la kiroho ambalo hututakasa lakini kama tukirudia kufanya mambo maovu yaleyale tena basi ni kwamba tunajichafua tena. Upo mfano mzuri sana wa mtu ambaye ana begi la kubebea vitu anavyonunua ili kupeleka nyumbani. Lakini kuna tundu kubwa chini ya begi hilo kwa hiyo chochote anachoweka humo hudondoka kupitia tundu hilo. Anashangaa na kupigwa na butwaa kwamba inawezekanaje kwamba amejaza begi hilo na vitu mara kumi zaidi ya ujazo wake lakini bado linabakia halina kitu. Anashangaa vitu hivi vinakwenda wapi. Kwa namna hiyo hiyo, kutegemea na umri wetu, tumekuwa tukimuabudu Mwenyezi Mungu kwa miaka 10, 20, 30, au 40. Lakini matokeo ya ibada hizi yako wapi? Kwa nini bado tunaendelea na tabia zetu zile zile za kutenda dhambi? Kwa nini bado tuko vile vile baada ya Ramadhani baada ya mwezi wa Ramdhani kama tulivyokuwa kabla yake? Ni kwa sababu tunafanya matendo mema lakini kwa nyongeza tunaendelea kutenda mambo machafu. Upo mfano mwingine unaofaa uliosimuliwa na Rumi. Alikuwepo mkulima ambaye alikuwa na tabia ya kuvuna 52

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 52

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ngano yake na kuiweka kwenye ghala, akiwa na matumaini ya kujaza kwa ajili ya msimu wa baridi. Lakini, kwa mshangao wake kila alipokwenda ghalani kuweka mavuno mengine ya ngano aligundua kwamba kiwango kilikuwa chini kuliko mwanzo hivyo ghala halikuweza kujaa kamwe. Hivyo, alishangaa, hususan kwa vile wakati wote ghala lilikuwa limefungwa na hakuna mtu aliyekuwa na fursa ya kuingia na kutoa kitu chochote nje. Alikuwa mwangalifu wakati wote wa kufunga mlango. Hivyo aliamua kwamba siku moja usiku atakuja kulala ndani ya ghala ili agundue ni nini kinachotokea humo. Hivyo usiku mmoja kwa hakika akabakia macho ndani ya ghala akiangalia kimya kimya. Baada ya usiku wa manane ndipo alipogundua kwamba panya wakubwa walikuwa wanachukua ngano na kutoka nayo nje ya ghala. Kwa hiyo akatambua kwamba panya hao walikuwa ndio chanzo hasa cha tatizo. Rumi anatuambia kwamba sisi ndivyo tulivyo. Wapo panya ndani ya nyoyo zetu ambao huchukua nuru ya matendo yetu mema. Kama hakuna panya, ipo wapi nuru ya swala zetu za miaka 40, nuru ya miaka 40 ya kufunga saumu, ya kwenda kuhiji na kadhalika? Kwa hiyo tunapaswa kuwa waangalifu sana tusifanye vitendo vya dhambi yoyote . Tusifanye hata dhambi moja. Bila shaka sisi ni binadamu na tunaweza tukafanya makosa, lakini muumini wa kweli, ni yule ambaye kama akifanya kosa, kwanza kabisa husikitika na kuhisi vibaya sana pili hutubu haraka sana na kuamua kutokurudia kosa hilo tena. Kwa hiyo, tukitenda dhambi lazima tutubie haraka iwezekanavyo. Kwa bahati mbaya, miongoni mwa baadhi ya watu wengine ambao hupendelea mambo ya kiroho wapo wale wanaodhani kwamba shari`ah ya kidini inatakiwa mwanzoni tu na baadaye tuhusike na masharti ya safari ya kiroho 53

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 53

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

(tariqah). Wakati mwingine wanasema kwamba hii ni sawa na mtu ambaye amefika kwenye kiini kwa hiyo hahitaji tena ganda. Lakini hili sio wazo sahihi kwa sababu wakati wote tunatakiwa kuzingatia shari`ah. Mtukufu Mtume na Maimam wa nyumba ya Mtume (amani juu yao wote) wakati wote walifuata shari`ah na hakuna mtu anayeweza kudai kuwa yeye ametakasika kuzidi wao. Hakuna tukio ambapo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alitenda dhambi na akadai kwamba ilikuwa sawa yeye kufanya hivyo. Kwa mfano kamwe hakuwahi kusema kwamba tusiseme uongo lakini kwamba yeye aliruhusiwa kufanya hivyo. Au kwamba tusinywe kilevi au kucheza kamari lakini kwake yeye inakubalika. Bahati mbaya, siku hizi tunaona kwamba wapo watu wanaoitwa Waislamu ambao wanawafuata watu wanaojiita mabwana au maimam ambao wao wenyewe hawafuati masharti ya ucha-Mungu na bado wafuasi wao wanawaamini na kudhani kwamba kamwe hawataathiriwa na uovu wao. Hata hivyo kufutana na Madhehebu ya Ahlul Bayt jambo hili liko wazi kabisa.Tunapaswa kufuata shari`ah lakini hii haitoshi. Zipo njia mbili za kuiangalia shari`ah. Njia ya kwanza ni ile inayofuatwa na baadhi ya wafuasi wa Usufi; kwamba shari`ah ni kwa ajili ya yule anayeanza tu halafu baada ya kufika kiwango cha juu zaidi hatuhitaji tena kuzingatia shari`ah. Njia ya pili ni ile ya kusema kwamba shari`ah inatakiwa wakati wote lakini kwa kufuata shari`ah tu wakati wote tutajikuta tuko katika kiwango cha chini. Kama tunataka kufika kwenye kiwango cha juu zaidi, basi zaidi ya shari`ah tunatakiwa kuvuka mpaka wa utekelezaji wa vitendo vya ibada tu ili tuweze kugundua msukumo uliomo humo. Mfano unaoweza kusaidia ni ule 54

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 54

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

wa mtu alioko shule ya msingi. Kama mtu yuko shule ya msingi na anajiona ametosheka, basi elimu yake itabaki hivyo bila kukamilika. Mtu huyu anahitaji aende shule ya sekondari, halafu aende chuo kikuu. Lakini hatuwezi kusema kwamba tutakwenda shule ya sekondari na mara tukifika tunasahau tuliyoyasoma shule kwambakule tutakwenda shule yayote sekondari na mara tukifika kule ya msingi. Au kwamba tunapokwenda chuo kikuu tutasahau tunasahau yote tuliyoyasoma shule ya msingi. Au kwamba chuo kikuuHili tutasahau yale yotekazi. ya sekondari. Hili yaletunapokwenda yote ya sekondari. halitafanya halitafanya kazi.

Inatakiwa tutambue kwamba hakuna kinachoweza kuchukua utekelezaji wajibu nakuchukua kujizuia Inatakiwambadala tutambue wa kwamba hakuna wa kinachoweza mbadala wa utekelezaji wa wajibu na kujizuia kutenda dhambi. kutenda dhambi. Kwenye Nahj al-Balaghah, Imam Ali Kwenye Nahj al-Balaghah, Imam Ali anasema: anasema:

‫ول‬ ‫ال تَ ُكنُ ِم ﱠمن يَ ْر ُجو‬ ِ ‫اآلخ َرةَ بِغ ْي ِر َع َم ِل َويُؤ‬ ِ ِ ُ‫َخ ُر الت ْﱠوبَةَ ِبط‬ ‫األَ َم ِل‬ “Usiwe miongoni mwa watu wenye matumaini ya Akhera “Usiwe miongoni mwa watu wenye matumaini ya bila ya mwenendo mzuri na ambaye huahirisha toba kwa Akhera bila ya mwenendo mzuri na ambaye 15 sababu ya kutumainia maisha marefu.” huahirisha toba kwa sababu ya kutumainia maisha 15

marefu.” Kama tukidumisha mwenendo unaofaa, kidogo kidogo, nuru ya matendo yetu itaongoa nyoyo zetu. Hata kama Kama tukidumisha mwenendo unaofaa, kidogo kidogo, nuru ya ukifanya madogo mazuri, inaweza matendomatendo yetu itaongoa nyoyo zetu. Hata kama ukifanyakujengeka, matendo ilimradi tu mazuri, usifanye dhambi. Mtume Muhammad madogo inaweza kujengeka, ilimradi tu usifanye (s.a.w.w.) dhambi. Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alimwambia Abu Dharr; alimwambia Abu Dharr;

“Ewe Abu Dharr, kwa ucha-Mungu , unahitaji kuomba dua “Ewe Abu Dharr, kwa ucha-Mungu , unahitaji kuombachako. dua kiasi kidogo kama ile chumvi ilioko kwenye chakula kiasi kidogo kama ile chumvi ilioko kwenye chakula chako. Ewe Abu Dharr, mfano wa mtu anayeomba dua bila ya maEwe Abu Dharr, mfano wa mtu anayeomba dua bila ya tendo yu sawa na mtu anayejaribu kutupa mshale bila ya matendo yu sawa na mtu anayejaribu kutupa mshale bila ya upinde.”16 upinde.”16 15 16

Nahj al-Balaghah, Hotuba za hekima Na. 140 (150). 15 al-Anwar, Juz. 74. uk. 85. Bihar Nahj al-Balaghah, Hotuba za hekima Na. 140 (150). 16

Bihar al-Anwar, Juz. 74. uk. 85.

55

55 09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 55

7/10/2013 3:33:33 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Kwa upande mwingine, kama mtu akitenda madhambi, matendo yake mengi mema hayatasaidia. Hatuwezi kufidia madhambi yetu kwa matendo mema. Qur`ani inasema:

َّ ‫إِ َّن َما َي َت َق َّب ُل‬ ‫ِين‬ َ ‫ﷲُ م َِن ْال ُم َّتق‬ “…….Mwenyezi Mungu huwapokelea wenye kumcha tu.” [5:27]

3.c. Kuwa na tabia njema na kuondoa zilizo mbaya: Zaidi ya kuwa na imani inayofaa, kutekeleza wajibu wetu, na kujizuia kufanya dhambi tunahitaji kuangalia sifa za nafsi zetu au nyoyo na tutambue sifa zipi nzuri hatunazo ili tuweze kuzipata na sifa zipi mbaya tulizonazo ili tuziondoe. Kwa kawaida haya ndiyo tunayojifunza katika sayansi ya Akhlaq [maadili] na ni ngumu zaidi kuliko kuwa na imani inayofaa au utekelezaji uliosahihi. Mara nyingi tunakuwa na tabia mbaya ambazo ni ngumu kuzibadili au hata kuzigundua, kwa sababu takriban zimekuwa kama ni sehemu yetu. Katika hali hii tunahitaji kupambana na tunahitaji tiba. Mfano, mtu anaweza kuwa na hofu sana. Mara tu giza linapoingia anaingiwa na woga.Wakati mwingine mtu huyu anaweza kuwa amedhamiria kuondoa hofu yake lakini bado ni vigumu na anahitaji tiba ya aina fulani. Kwa namna fulani hivyo ni kama kansa ambayo inataka matibabu magumu. Kwanza lazima tutambue tabia zetu mbaya na halafu tujaribu kujipa ahadi kwamba hatutafanya lolote kufuatana na tabia hiyo kwa sababu kama tukifanya dhambi kufuatana na tabia mbaya huwa na nguvu zaidi na zaidi. Mathalani 56

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 56

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

tunaweza kuwa na tabia mbaya ambayo hatuwezi kuiondoa haraka, lakini kama hatutafanya kitu kufuatana na tabia hiyo mbaya, tabia hiyo itaanza kupoteza nguvu pole pole. Pia upo ufumbuzi mahususi kwa ajili ya tabia mbaya maalum kutegemea na aina ya tabia. Kwa hiyo, ushauri na ufumbuzi wa jumla ni mhusika kujizuia asifanye lolote kufuatana na tabia hiyo mbaya lakini ni muhimu kutumia ufumbuzi maalum kwa ajili ya tabia na sifa mbaya. Mathalani kama mtu fulani anataka kuacha tabia ya kuvuta sigara zipo mbinu fulani ambazo zinaweza kusaidia kusitisha tabia hiyo lakini haziwezi kufaa kwa tabia nyingine. Wakati mwingine baada ya miongo kadhaa unaweza kujihakikisha kwamba wewe ni mtu mzuri, halafu ukagundua kwamba wewe ni mtu mbaya. Mfano ni mtu ambaye kila mara alikuwa mstari wa mbele wakati wa swala za jamaa, lakini baada ya miaka mingi akatambua kwamba alikuwa anafanya hivyo si kwa ajili ya Allah swt, kwani siku moja alipochelewa kuingia msikitini, ikabidi aswali akiwa kwenye safu ya mwisho, akahisi soni kwamba labda watu wengine wangefikiria kwamba siku hiyo hakuwepo kwenye safu ya mbele. Kwa hiyo akatambua kwamba alikuwa akifanya hivyo si kwa ajili ya Allah swt isipokuwa alikuwa akitafuta kusifiwa na watu wengine kwamba yeye kila siku aliswali akiwa safu ya mbele. Kinyume chake, mtu anaweza kurejelea kwenye tukio kuhusu Ayatollah Shaykh Mohammed Husayn Isfahani Qarawi, mwalimu wa marehemu Ayatollah Khu`i. Siku moja alipokuwa anatembea mtaani katika mji wa Najaf, 57

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 57

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

waliona kwamba alikuwa anatabasamu na akiwa amefurahi, na mtu moja akamuuliza kwa nini alikuwa amefurahi. Ayatollah akajibu kwamba kwa sababu mfuko wake wa mboga umedondoka chini, na alipoinama kuuchuka mfuko huo hakuwa anajali kama watu walikuwa wanamtazama. Hali hii ilimfanya afurahi, kwa sababu alikumbuka tukio jingine lililotokea miaka ya nyuma alipokuwa anasoma kwenye hawza hiyo. Wakati huo alikuwa anamiliki tasbihi ya gharama kubwa kwani alikuwa tajiri, na tasbihi hiyo ilipokatika na shanga zingine kudondoka, hakukusanya zile shanga zilizodondoka kwani hakutaka watu wamuone. Sasa alijihisi ametosheka, kwamba pamoja na kwamba yeye ni mwanachuoni mkubwa, hakuhisi vibaya kwamba watu walikuwa wanamtazama wakati anakusanya mboga zilizodondoka. Katika jambo hilo, alijiona kwamba alikuwa hana hisia za majivuno. Kwenye vitabu kama vile “Mi`raaj al-Sa`aadah” na “Jaami` al-Sa`aadah” tunajifunza kuhusu nguvu mbalimbali za nafsi zetu na tabia njema na mbaya zinazoendana nazo. Pia tunajifunza mbinu za kupata tabia njema na kuondoa tabia mbaya. 3.d. Kuendeleza mchakato wa ujenzi wa nafsi hadi anapokuwa mja wa kweli anayekutana na Mola Wake: Tunapaswa kuendeleza mchakato huu. Ni changamoto ya maisha ambayo haiwezi kupewa ukomo wa muda wa mwezi moja au mwaka moja au miaka kumi ambapo baada yake tutahisi kwamba tumeukamilisha na sisi kujiruhusu kupumzika. Kinyume chake, kwa wakati wote tutakapokuwa hapa duniani, hadi dakika 58

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 58

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ya mwisho ya uhai wetu, lazima tuwe waangalifu. Na tusipoteze fursa yoyote. Hakuna umri wa kustaafu au kuhitimu, kwa sababu vyovyote vile tunavyoweza kupata, kwanza hakuna muamana kwamba tutahifadhi vile tulivyopata na pili hata kama tunaweza kuvidumisha, bado havitaweza kutengeneza masurufu kwa ajili ya safari yetu ya Akhera. Qur`ani inasema, “Na umwabudu Mola Wako mpaka yakufikie mauti.� [15:99]. Kabla hatujakutana Naye, hakuna hali ya kustarehe, kustaafu, kuhitimu au kupumzika. Insha-Allah hadi tutakapokutana Naye ndipo tutakapopumzika. Kwa hiyo, lazima tuendeleze mkakati huu hadi tukutane Naye na aridhike na sisi. Kuna kisa kimoja cha kuvutia ambacho kinaonyesha hii hali yetu. Palikuwepo na kundi la watu ambao walikuwa wapelekwe kwenye shimo la kupenya chini ya ardhi (tunnel) lenye giza. Waliambiwa kwamba pindi watakapokuwa wameingia humo itakuwa giza sana na hawataweza kuona kitu chochote. Waliambiwa kwamba wakiingia humo waende mwisho mmoja hadi mwisho mwingine wa shimo hilo na kwamba kwenye sakafu ya shimo hilo yapo mawe ambayo wanaweza wayachukue na kutoka nayo. Watu hao waliambiwa kwamba kama wakichukua mawe hayo watajuta lakini waliambiwa pia kwamba wasipochukua mawe hayo watajuta! Halafu wakaingizwa kwenye njia hiyo ya shimoni. Baadhi ya watu katika kundi hilo waliona kwamba hapakuwepo na manufaa yoyote kuchukua mawe hayo kwa sababu wangejuta kwa kufanya hivyo. Baadhi yao, kwa sababu ya udadisi tu walifikiria wangeyachukua mawe hayo tu ili waone 59

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 59

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

yalikuwa ni nini, hata kama mwisho wa safari wangejuta. Hivyo baadhi yao waliyakusanya na baadhi hawakukusanya, kisha wakatoka nje ya shimo hilo. Wakiwa nje tena, kwenye mwanga wa jua la mchana, wale waliochukua mawe hayo waligundua kwamba yalikuwa ni vito vya thamani sana. Na wale ambao hawakuchukua mawe hayo waliliona hili na walikasirika sana. Walianza kulalamika, wakihoji kwamba kwa nini waliambiwa kwamba wakikusanya mawe hayo watajuta. Halafu waliambiwa kwamba ingawa wale ambao hawakuchukua mawe wamelijutia hilo, lakini hata wale waliochukua mawe wamejuta pia kwamba wamechukua mawe kidogo na walitamani wangechukua mengi zaidi na kujaza mifuko yao vilevile. Kwa hiyo hivi ndivyo tunavyopaswa kufanya. Tuhakikishe kwamba mikono na mifuko yetu inafurika kwa tabia njema na matendo mema, tunufaike kwayo hapa duniani na tuyachukue na kwenda nayo Akhera. Mukhtasari: Zipo hatua kadhaa ambazo mtu lazima azipitie wakati yupo katika njia ya ujenzi wa nafsi. Kwanza lazima tuzindukane kutoka kwenye usingizi mzito wa kuzembea na tutambue uhalisia wa uhai wetu hapa duniani: ni hapo tu ndipo tutakapojitambua na kuwa waangalifu na vitendo vyetu. Hali hii lazima iambatane na imani na itikadi ya kweli juu ya Mungu Mmoja. Imani haijakamilika bila matendo mema na kwa hiyo lazima tuepuke kufanya matendo yaliyokatazwa. Mwisho kabisa, lazima tuepushe nafsi zetu kutokana na tabia na sifa mbaya. Pamoja na kwamba njia hii ni ngumu kuipita, 60

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 60

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Insha-Allah kwa rehema za Allah swt tutapata tawfiiq ya kukamilisha hatua zote hizi na kupata ukaribu zaidi Naye kwa urahisi.

61

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 61

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

MAELEKEZO YA KIVITENDO JUU YA SAFARI YA KIROHO

T

ayari tumekwishazungumzia baadhi ya kanuni za jumla katika sehemu iliyotangulia [Juz. 10, Na. 4], kama vile kufuata shari`ah na uangalizi wa sifa bainifu na tabia zetu. Hata hivyo, vipo pia vitendo fulani ambavyo vinaweza kutuimarisha, kuongeza dhamira na nidhamu zetu na ambavyo vinaweza kutufanya tuwe na juhudi na ujasiri wa kutosha katika kuendelea na safari ya kiroho. Vitendo hivi vinapaswa kutuweka kwenye njia iliyonyooka. Yapo maelekezo matano ambayo yametangazwa na masufi wote wa Kiislamu ambayo kwa kweli yana mizizi kwenye Qur`ani na Sunnah. 1. Kutozungumza ila ikibidi kuwa lazima. Tunapaswa tujaribu kujizuia tusiongee kupita kiasi. Watu wanaweza kufikiria kwamba hili si jambo la muhimu lakini kwa kweli ni jambo la muhimu sana haswa. Tujaribu kuongea tu kwa kiasi cha lazima tu. Kwa bahati mbaya zipo aina nyingi za dhambi zinazofanywa na watu ambazo zinahusiana na matumizi ya ulimi. Baadhi ya wanachuoni wamehesabu na kupata jumla ya dhambi sabini za aina hiyo. Wakati fulani mtu aliomba ushauri kutoka kwa Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.) Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Chunga ulimi wako!” Mtu huyo aliomba tena ushauri. Mtume akasema:”Chunga ulimi wako!” Kwa mara ya tatu mtu huyo aliomba ushauri. 62

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 62

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Mtume (s.a.w.w.) akasema:�Ahaa, hivi kuna kitu kingine zaidi ya yale ambayo watu huyakusanya kwa kutumia ndimi zao ambacho husababisha wao kuangukia nyuso zao motoni?�17 Sababu moja ambayo inaweza kufanya kauli kuwa kisababishi cha dhambi nyingi sana ni kwa kuwa tunaongea wakati wote. Tunaongea mfululizo kwa sababu ni rahisi kufanya hivyo. Hatuhitaji kufanya juhudi yoyote; wala hatuhitaji vitendeakazi vyovyote, nyenzo, mafunzo au fedha; na kwa sababu hiyo, tuna udhibiti mdogo sana kuhusu kile tunachokisema. Siku hizi, imekuwa rahisi zaidi kuongea baina ya mtu na mtu, kwa kuwa njia nyingi mbadala za mawasiliano zimeenea kila mahali, ambazo zinawawezesha watu katika nchi mbalimbali kuwasiliana, kwa hiyo, kuuacha mwanya mpana zaidi wa kutenda dhambi. Katika Uislamu wa mwanzoni, baadhi ya watu walikuwa na desturi ya kuweka mchanga mdomoni kwa lengo la kufanya iwe vigumu kuongea. Ikawa kila walipofikiria kutaka kuongea iliwalazimu kwanza waondoe mchanga mdomoni. Wakati huo walipofikiria juu ya kufanya hivyo, walifikira juu ya haja hasa ya kuongea na kile ambacho walikuwa wakiseme, na wakatambua kwamba ni bora zaidi kutoongea. Zoezi hili lilipunguza mazungumzo yasio na umuhimu. Mimi hili sio ninaloshauri lifanyike, na nimesimulia hadithi hii tu kwa kusisitiza hija yangu kwamba ni muhimu kudhibiti kauli zetu. Hata kama kile tunachotaka kusema hakikukatazwa (sio haramu) bado tunapaswa tusikiseme isipokuwa iwe muhimu kufanya hivyo. Mazungumuzo yasio muhimu yana madhara kwa mambo yetu ya kiroho. Maneno yetu si tu 17

Bihar al-Anwar, Juz. 74, uk. 161. 63

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 63

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kwamba yanafanya akili zetu zishughulike, bali pia huathiri sana nyoyo zetu. Ni kama vile mtu anapokula chakula kingi chenye sumu. Si tu kwamba mhusika atahisi maumivu tumboni mwake kwa sababu ya mfumo wa kumeng`enya chakula utashindwa kufanya kazi sawasawa, bali pia atakuwa na maradhi na kujihisi mgonjwa. Nyoyo zetu huugua kwa sababu ya kusema maneno mengi yasio muhimu. Kwa mtazamo wa kiroho, kila tendo analofanya binadamu au kila neno analotamka binadamu, humsababishia ama nuru au giza. Mazungumzo au kauli isiyo muhimu, husababisha madhara na hufanya nyoyo zetu kuwa nyeusi.18 Tunatakiwa kuwa makini kuhusu jambo hili kwani lina umuhimu wake. Kama tunaweza kusema kitu kwa sentenso tano badala ya kumi, basi na tufanye hivyo. Kama tulitaka kusema kitu 18

aadhi ya watu wanaweza kushangaa kwa nini hawahisi giza kwenye nyoyo zao B wakati wanapoongea sana au hata wanapoongea madhambi kama kusengenya [ghaybah]. Jibu ni kwamba, hisia za watu hutofautiana sana. Kipo kisa kwenye Mathnawi ya Rumi kinachoonyesha mfano wa suala hili. Rumi anasema kwamba mtu mmoja alimpeleka farasi wake kwenye soko la manukato. Farasi huyo akachafua soko. Wauza manukato wakakasirika kwani kabla ya hapo soko lilikuwa likinukia harufu nzuri ya manukato katika kila kona. Kwa hyo, wakataka soko lisafishwe, lakini hakuna mtu ambaye aliweza kuvumilia kuisogelea ile harufu mbaya. Wauza manukato wakaamua kumkodisha mtu aliyezoea harufu mbaya kufanya kazi hiyo na wakampata kijana mmoja ambaye kazi yake ilikuwa kuwaosha na kuwasafisha farasi. Wakamleta sokoni, lakini mara tu kijana huyo aliponusa harufu nzuri ya manukato, akazirai kwani alishindwa kuvumilia harufu ya manukato.Hii ni kwa sababu uvumilivu wake kwa harufu nzuri ya manukato ulikuwa umebadilishwa. Kwa namna hiyo hiyo, wapo watu ambao wamezoea uchafu: wa kimwili au wa kiroho. Si tu kwamba watu hawa wamezoea uchafu, wamekuwa na mzio (allergic) wa usafi. Kwa hiyo kama hatuwezi kuhisi kuwa kitu fulani ni kibaya au hatuhisi kwamba nyoyo zetu zimekuwa na giza, si kwamba kwa sababu vitu vizuri havina athari, bali ni kwa sababu nyoyo zetu zimekuwa na ganzi. Hali hii ni sawa na mtu ambaye ana mafua, na hawezi kuhisi muonjo wa chakula kama ilivyo kawaida. Zaidi ya hayo, wakati mwingine chakula kizuri kwake mtu huyu kinakuwa na ladha chungu: hii si kwa sababu chakula ni kichungu, lakini ni kwa sababu hisi zake za kuonja zimeharibika. 64

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 64

7/10/2013 3:33:34 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

halafu tukatambua kwamba si cha muhimu kukisema basi ni vema zaidi kunyamaza. Watu wanaweza kusema kwamba wanatakiwa kukaa pamoja na wazazi wao, familia au marafiki zao, na kwamba lazima wawe wakunjufu, wachangamfu. Katika mazingira kama haya tunapaswa bila shaka kuongea lakini lazima tuwe waangalifu juu ya kile tunachokisema kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Tunaweza kumwambia Mwenyezi Mungu kwamba tunaongea ili kuwafurahisha familia au marafiki zetu. Kuufurahisha moyo wa muumini ni kitendo cha ibada.Hata hivyo ipo tofauti kubwa sana kati ya mtu anayesema kitu kwa ajili ya kuwafurahisha wengine na mtu anayesema kwa lengo la kuwadhihaki wengine au anayetaka kujifurahisha tu mwenyewe au kujionyesha kwa kusema sana. Hivyo, lazima tutahadhari kuhusu maneno yetu. Kuna hadithi ya kuvutia sana kutoka kwa Mtukufu Mtume ambayo inaashiria kwamba aliwaambia kundi la sahaba wake: “Kama isingekuwa kwa sababu ya kuongea sana na kwa sababu ya hizo fikira mbaya zinazoingia nyoyoni mwenu, mngeweza kuona kile ninachokiona na kusikia kile ninachokisikia�19

Hii inaonyesha kwamba, ama tunasema sana au tunafikiri sana kuhusu vitu visivyo na manufaa, na kwa hiyo hatuwezi kufanya maendeleo yoyote. Mambo yote mawili yanawezekana, kutozungumza kuwa rahisi na kuwa kugumu pia. Inaweza kuwa rahisi kwa sababu hakuna cha kujifunza, hakuna cha kununua sisi na hakuna mahali maalum panapohitajika kwa lengo la kutekeleza ushauri huu. Hatuhitajiki kufanya lolote. Bali 19

I menukuliwa kutoka kwenye chanzo cha Sunni - Al-Mizan fi Tafsir al-Qur`ani, Juz. 5, uk. 315. 65

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 65

7/10/2013 3:33:34 PM


Hii inaonyesha kwamba, ama tunasema sana au tunafikiri sana UJENZI NA UTAKASO WAhiyo NAFSI kuhusu vitu visivyo na manufaa, na kwa hatuwezi kufanya Hii inaonyesha kwamba, ama tunasema sana tunafikiri sana maendeleo yoyote. Mambo yote mawiliau yanawezekana, kuhusu vitu visivyo na manufaa, na kwa hiyo hatuwezi kufanya kutozungumza kuwa rahisi na kuwa kugumu pia. Inaweza kuwa Hii inaonyesha kwamba, ama tunasema sana au yanawezekana, tunafikiri sana maendeleo yoyote. Mambo yote mawili rahisi kwa tu sababu hakunatusiongee cha kujifunza, hakuna cha kununua sisi tunaambiwa kwamba sana. Kwa hiyo inaonekana kuhusu vitu visivyo na manufaa, na kwa hiyopia. hatuwezi kufanya kutozungumza kuwa rahisi na kuwa kugumu Inaweza kuwa na hakuna mahali maalum panapohitajika kwa lengo la kutekeleza kwamba sio sababu vigumu. Lakini kama tukijaribu, tutaona kwa maendeleo yoyote. Mambo yote hakuna mawili yanawezekana, rahisi hakuna cha kujifunza, kununua sisi ushaurikwa huu. Hatuhitajiki kufanya lolote. Bali cha tunaambiwa tu kutozungumza kuwa rahisi na kuwa kugumu pia. Inaweza kuwa hakika kwamba ni vigumu sana. Wakati mwingine tunaweza na hakunatusiongee mahali maalum kwa lengo la kutekeleza kwamba sana. panapohitajika Kwa hiyo inaonekana kwamba sio rahisi kwa sababu hakuna cha kujifunza, hakuna cha kununua sisi ushauri huu. Hatuhitajiki kufanya lolote. Bali tunaambiwa tu kuhisi kama vile tunaweza kupasuka kwa sababu tunataka vigumu. Lakini kama tukijaribu, tutaona kwa hakika kwamba ni na hakunatusiongee mahali maalum panapohitajika kwa lengo la kutekeleza kwamba sana.mwingine Kwa hiyo inaonekana kwamba sio vigumu sana. Wakati tunaweza kuhisi kama vile kusema sana kuhusu kitukufanya fulani.lolote. Lakini kama tukijizoesha ushauri huu. Hatuhitajiki tunaambiwa tu vigumu. Lakini kama tukijaribu, tutaonakusema kwaBali hakika kwamba ni tunaweza kupasuka kwa sababu tunataka sana kuhusu kitu inakuwa rahisi zaidi. kwamba tusiongee sana.mwingine Kwa hiyo inaonekana kwamba sio vigumu sana. Wakati tunaweza kuhisi kama vile fulani. Lakini kama tukijizoesha inakuwa rahisi zaidi. vigumu. kama tutaonakusema kwa hakika ni tunawezaLakini kupasuka kwatukijaribu, sababu tunataka sana kwamba kuhusu kitu Kufuatana na Wakati baadhi ya hadithi, kimyakuhisi ni njia nzuri vigumu sana. mwingine tunaweza kama vilesana fulani. Lakini kama tukijizoesha inakuwa rahisi zaidi. Kufuatana na baadhi ya hadithi, kimya ni njia nzuri sana ya ibada. ya ibada. Mathalani, Imam Alitunataka (a.s.) kusema amenukuliwa akisema tunaweza kupasuka kwa sababu sana kuhusu kitu Mathalani, Imam Ali (a.s.) amenukuliwa akisema fulani. Lakini kama tukijizoesha zaidi.sana ya ibada. Kufuatana na baadhi ya hadithi, inakuwa kimya ni rahisi njia nzuri Mathalani, Imam (a.s.) ‫ا ْلفَ َر‬Ali ‫ظَا ُر‬ya ‫ َو‬amenukuliwa ‫ص ْب ُر َو‬ ‫ا‬njia ‫عبِا َد ِة‬nzuri ‫ أ ْف‬ya ibada. ُ‫ص ْمت‬ ‫ ﱠ‬ni‫ ْل‬akisema َ ‫ال‬kimya َ sana ِ‫ ا ْنت‬hadithi, ِ ‫ض ُل ا ْل‬ ِ baadhi Kufuatana na‫ج‬ Mathalani, Imam ‫ج‬ ‫ا ْل‬Ali ‫(ظَا ُر‬a.s.) ‫ض ُل ا ْل ِعبِا َد ِة ا‬ ُ‫ص ْمت‬ ‫ ْل ﱠ‬akisema َ ‫ص ْب ُر َو ال‬ َ ‫أ ْف‬ ِ‫ َو ا ْنت‬amenukuliwa ِ ‫فَ َر‬ukimya “ٍSubira,“ٍukimya na kungojea (wokovu, msaada) ni Subira, na kungojeafaraja faraja (wokovu, msaada) ni 20 20 ْ َ ْ ْ ْ َ ْ aina nzuri sana za ibada.” aina nzuri sana za ibada.” ‫ج‬ ‫ر‬ ‫ف‬ ‫ل‬ ‫ا‬ ‫ر‬ ‫ا‬ ‫ظ‬ ‫ت‬ ‫ن‬ ‫ا‬ ‫و‬ ‫م‬ ‫ص‬ ‫ال‬ ‫و‬ ‫ر‬ ‫ب‬ ‫ص‬ ‫ل‬ ‫ا‬ ‫ة‬ ‫د‬ ‫ا‬ ‫ب‬ ‫ع‬ ‫ل‬ ‫ا‬ ‫ل‬ ‫ض‬ ‫ف‬ ‫أ‬ ُ‫ت‬ َ ْ ‫ﱠ‬ ُ ُ َ َ َ ِ ِ ِ َ َ ْ ِ ُ ِ ukimya na kungojea faraja (wokovu, msaada) ni “ٍSubira, 20 aina nzuri sana za ibada.” ‫بَادَة‬faraja ‫( آل ِع‬wokovu, msaada) ni “ٍSubira, ukimya na‫كالصمت‬ kungojea 20 aina nzuri sana za ibada.” ‫آل ِعبَادَة كالصمت‬ “Hakuna ibada iliyo bora kuliko ukimya.”21

‫آل ِعبَادَة كالصمت‬

21

“Hakuna ibada iliyo bora kuliko ukimya.” “Hakuna ibada iliyo bora kuliko ukimya.”21 ‫الفكر‬ ‫روضة‬ ‫الصمت‬ “Hakuna ibada iliyo bora‫الصمت‬ kuliko ukimya.”21 ‫الفكر‬ ‫روضة‬ “Ukimya ni bustani ya tafakuri.”22

‫الصمت روضة الفكر‬

20

“Ukimya ni bustani ya tafakuri.”22

Biharul-Anwar, Jz. 68, uk. 97 21 22 22 Ghural al-Hikma wa Durarni al-Kalim, Hadithi namba 10471. “Ukimya tafakuri.” “Ukimya nibustani bustani yaya tafakuri.” 22 20 Ghural al-HikmaJz.wa68, Durar al-Kalim, Hadithi namba 546 Biharul-Anwar, uk. 97 21 Ghural wa Durar al-Kalim, Hadithi namba 10471. Hii ni al-Hikma kwa sababu mtu anapokuwa kimya akili yake 22 20 Ghural al-HikmaJz.wa68, Durar al-Kalim,64 Hadithi namba 546 Biharul-Anwar, uk. 97 21 huanza kufaidi uzuri wa dunia ya kiroho. Lakini kama mtu Ghural al-Hikma wa Durar al-Kalim, Hadithi namba 10471. 22 Ghural al-Hikma wa Durar al-Kalim, Hadithi namba 546 64 atazungumza, akili yake hushughulika zaidi na mambo ya

kidunia ya maumbile.

64

Biharul-Anwar, Jz. 68, uk. 97 Ghural al-Hikma wa Durar al-Kalim, Hadithi namba 10471. 22 Ghural al-Hikma wa Durar al-Kalim, Hadithi namba 546 20 21

66

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 66

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

2. Kutokula zaidi ya kipimo cha lazima. Kwa namna ile ile kama kukaa kimya, kula sehemu ndogo ya chakula nafsi huathirika kwa namna ya uwezo mkubwa, kwani kunairuhusu nafsi kukua. Kinyume chake ni kwamba, tunapokula sana, hata kama chakula chetu ni cha halali, chakula hicho hutufanya tujishughulishe sana na nafsi zetu kupata uvivu. Hatutaweza kuwa na hadhari. Kwa maneno mengine, tunachokula ni kwa ajili ya mwili, lakini saumu ni chakula cha nafsi zetu. Hata hivyo hapa kuna mtanziko kwa sababu mwili na nafsi vyote vinahitaji kulishwa chakula na lazima kila kimoja kitimiziwe haki yake. Nini cha kufanya? Tunapaswa kula kiasi kile kinachohitajika kwa afya zetu na kwa njia hii tunaweza kuwa na uhakika kwamba tumevitendea haki vyote, mwili na nafsi. Kula chakula kingi kupita kiasi hudhuru mwili na nafsi. Saumu ni kitu cha muhimu na manufaa sana kama tutaweza kufunga, lakini hata kama hatutafunga, bado tunaweza kunufaika sana kwa kupunguza kiasi cha chakula chetu tunachokula. Njia moja ya kutekeleza zoezi hili kivitendo imeonyeshwa na Allamah Tabataba`i. Wakati mwingine tunajishughulisha pale na kisha tunasahau ni kiasi gani tulichokula. Marehemu Allamah kwa kukusudia kabisa alikuwa akiweka kwenye sahani yake kile kiasi cha chakula alichotaka kula tu, na baada ya hapo hagusi kitu kingine tena. Zipo hadithi nyingi juu ya ubora wa kufunga saumu au kula kidogo. Mathalani, kwenye ushauri wake maarufu sana kwa al-Unwan al-Basri, Imam Sadiq (a.s.) alisema: 67

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 67

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

“Kuhusu vipande vitatu vya ushauri wa mtu kujinadhimu nafsi: kwanza usile chakula ambacho hana hamu nacho, kwani hili huleta upumbavu na uzuzu. Pili, usile isipokuwa unapokuwa na njaa. Na tatu, na unapokula, ule kile tu ambacho ni halali na uanze kwa kutaja Jina la Allah, na ukumbuke hadithi ya Mtume (s.a.w.w.) “Binadamu kamwe hajawahi kujaza chombo chochote kile kibaya zaidi ya tumbo lake.” Kwa hiyo kama ni lazima kulijaza, basi ruhusu thuluthi moja iwe kwa ajili ya chakula, na thuluthi nyingine iwe kwa ajili ya maji, na thuluthi ya mwisho iwe kwa ajili ya hewa.”23

3. Mtu asilale kupita kiasi Jambo hili ni muhimu hasa ili tusije tukapoteza muda wetu bure na kupoteza fursa adhimu ya kuswali swala za usiku. Mwili ukipata starehe kubwa kupita kiasi, starehe hiyo hugeuka kuwa sumu kwa nafsi. Tunahitaji kiasi sahihi cha chakula na mapumziko ili tuweze kuwa na mwili wenye afya njema kwa sababu mwili lazima uwe na afya njema ili uweze kutuhudumia.24 Lakini chakula kingi zaidi ya kile kiasi cha muhimu, kitakuwa na madhara kwa mwili na nafsi. Mwenyezi Mungu ameuumba mwili kwa namna ambayo kwamba tunapotunza mwili, tunaishia katika kutunza nafsi pia. Hatuhitaji kuuharibu mwili ili tuwe wacha-Mungu. Kama tukila kupita kiasi tunaharibu miili na nafsi zetu. Kama tukilala sana bila kufanya ma23 24

Biharul-Anwar, Jz. 1, uk. 226

Kwa hakika tunaweza kubadili tabia zetu za kula na kupumzika zikawa

ibada baada ya kutia nia nzuri. Kwa mfano, ninaweza kula kwa nia ya kuwa na nguvu ili kumtumikia Allah swt, na kwa hiyo nia yangu ya kula au hata ya kutayarisha chakula hicho ni kitendo cha ibada ambacho kwacho mimi nitalipwa thawabu. 68

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 68

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

zoezi na kufuata mtindo wa maisha ya starehe ya kupita kiasi, hatimaye tutaviharibu vyote viwili; mwili na nafsi. Kwa hiyo, ni muhimu sana kujizuia kulala kupita kiasi. Kwenye Qur`ani Tukufu, Mwenyezi Mungu anawasifu waumini kwa kusema:

ٍ ‫ِين فِي َج َّنا‬ ‫ِين َما آ َتا ُھ ْم َر ُّب ُھ ْم ۚ إِ َّن ُھ ْم‬ ِ ‫ُون آ‬ َ ‫خذ‬ َ ‫إِنَّ ْال ُم َّتق‬ ٍ ‫ت َو ُعي‬ ً ‫ِين َكا ُنوا َقل‬ ‫ُون‬ َ ‫ِيال م َِن اللَّي ِْل َما َيھ َْجع‬ َ ‫َكا ُنوا َق ْب َل ٰ َذل َِك مُحْ سِ ن‬ َ ‫ُون‬ َ ‫ار ُھ ْم َيسْ َت ْغ ِفر‬ ِ ‫َو ِب ْاألسْ َح‬ َ ْ ‫ُوم‬ ِ ‫َوفِي أ ْم َوال ِ​ِھ ْم َح ٌّق لِلسَّائ ِ​ِل َوال َمحْ ر‬ “Kwa hakika wamchao [Mwenyezi Mungu] watakuwa katika Mabustani na chemchem. Wakipokea aliyowapa Mola wao, kwa hakika wao walikuwa wakifanya wema kabla ya haya. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. Na wanaomba msamaha nyakati za kabla ya alfajiri. Na katika mali zao imo haki ya aombaye na ajizuiaye.” [51:15-19]

Baadhi ya watu hawalali kwa muda wa kutosha usiku lakini tatizo lao ni kwamba hawajui muda gani uliosahihi kulala. Kwa hiyo, hulala wakati ambao ndio wakati mzuri sana kwa ibada na huwa macho wakati ambao si murua sana kwa ibada. Mathalani, wakati mwingine mtu huchelewa kulala, yaani huingia kitandani katikati ya usiku, takribani saa 8 au 9 na halafu wakati mzuri kwa ibada na kumkurubia Mwenyezi Mungu kwa tafakuri anakuwa hajiwezi kwani amechoka. Sehemu ya siku ambayo ni ya muhimu sana kwa ibada ni kabla ya mapambazuko na baada ya mapambazuko hadi jua linapochomoza. Yeyote ambaye amefanikiwa katika jambo fulani ni kwa sababu alithamini wakati huu. Allamah 69

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 69

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Tabataba`i anasema kwamba mnamo siku za mwanzo za kuwasili kwake Najaf, mwalimu wake, Marhum Ayatollah Sayyid Ali Qadi alimwambia:�Endapo unaitaka dunia, Swali tahajjud [sala za usiku]; kama unaitaka Akhera [Pepo], tena swali tahajjud.� 4. Kuwa na muda wa faragha wa kutafakari Tunahitaji muda wa kuwa peke yetu, ama wakati wa mchana au ikiwezekana kabisa wakati wa usiku. Ni vema tujiwekee ahadi wenyewe kwamba kwa takribani dakika kumi au robo saa kila siku, tutakaa mahali peke yetu, mathalani kwenye mkeka wa kuswalia au bustanini na kutafakari. Hatua hii inatosha kuanza nayo. Baada ya muda si mrefu mtu utathamini nyakti hizi za faragha, hivyo kwamba utapenda kuitumia siku yako yote kwa namna hii. Hali hii itaelekezea kwenye maisha yako kuwa imara, kwani kuwekeza muda huu kutatengeneza nafasi ya faragha katika moyo wako. Kwa njia hii mtu unaweza kuwa mashughuli katika jamii, na wakati huohuo kuwa na amani ya kina na maono yaliyo wazi juu ya matendo yako, kana kwamba uko peke yako. Haya yanaweza kutokea kama mtu utatumia muda wako fulani ukiwa peke yako kabisa. Mtu utakapoweza kudhibiti nafsi yako, unaweza kuwa mchangamfu, unafanya kazi, na kadhalika, na bado ukadumisha udhibiti wa matendo yako, na kumkumbuka Allah swt. - Lakini tutafikiria kuhusu nini wakati tukiwa katika muda huu wa faragha? Tunapaswa kutafakari kuhusu sifa na kazi za Mwenyezi Mungu. Tufikirie kuhusu mambo ambayo tumeyatenda, 70

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 70

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kuhusu mambo ambayo tulitakiwa tuyafanye lakini hatukuyafanya na kuhusu hali ya nafsi zetu. Tunapaswa tufanye uamuzi endapo tunafanya maendeleo yoyote yale au hapana. Kama tutakuwa tumefanya jambo fulani vizuri basi hatuna budi tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa hilo. Kama tutakuwa tumetenda jambo baya basi tutafute jinsi ya kulirekebisha hilo. Kama hatuna nguvu za kutosha basi tunapaswa tujipangie adhabu juu yetu wenyewe. Baadhi ya watu huuliza wafanye nini ambapo wanajua kwamba jambo fulani ni kosa na hawataki kufanya kosa hilo lakini hata hivyo wanajikuta wamefanya kosa hilo tena na tena. Mathalani, watu wengine husema hawawezi kudhibiti hasira zao na huuliza wafanye nini kuhusu tatizo hili. Husema kwamba hukasirika kwa sababu ya tatizo la kisaikolojia ambalo hawana lakufanya juu ya hilo kwani liko nje ya uwezo wao wa kulidhibiti. Hata hivyo, tunatakiwa kuelewa kwamba Mwenyezi Mungu ametupatia sote uwezo wa kujidhibiti wenyewe, lakini tatizo ni kwamba ni sisi wenyewe hatutaki kuufanyia mazoezi uwezo huo. Ipo simulizi ya kuvutia kuhusu jambo hili. Hapo zamani alikuwepo mtu ambaye alikuwa ndio kwanza ameajiriwa kwenye ofisi. Katika siku yake ya kwanza aliwaambia wafanyakazi wenzake kuwa alitaka kuwaeleza kitu fulani wazi wazi ili siku zijazo wasije wakakasirika au kujihisi wametendewa kosa. Aliwaambia kwamba bahati mbaya yeye ni mtu mwenye hasira na atapokasirika anaweza akawakemea, akawaudhi, au akasema neno baya kwao lakini wasije wakafadhaika au kukasirika kuhusu hilo. Mtu mmoja aliyekuwa anasikiliza alikuwa mjanja sana. Alimshukuru mfanyakazi huyo mgeni kwa kusema kulisema hilo na 71

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 71

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kwamba alikuwa ni vizuri kwamba amelisema jambo hilo. Alisema kwamba mfanyakazi mpya alikuwa mwaminifu kwao, na yeye pia atakuwa mwaminifu kwake. Aliendelea kusema kwamba yeye pia alikuwa mtu mwenye hasira na kwamba kama yeyote angesemea jambo baya, yeye alikuwa na tabia ya kutupa kitu chochote kilichokuwa karibu naye usoni mwa mtu huyo na kwa hiyo alifurahi kwamba mfanyakazi mpya alisema kuhusu hilo. Baada ya maneno haya mfanyakazi mpya hakukasirika kamwe, wakati wote alikuwa mwangalifu na alikuwa akijichunga na alichokisema. Hii inaonyesha kwamba kumbe tunaweza kujidhibiti wenyewe kama kweli tukijaribu kufanya hivyo. Wakati mwingine huwa tunakasirika sana na kuwa washari tunapokuwa nyumbani lakini tunapokuwa mahali pa kazi tunakuwa watulivu sana. Hata kama watu watatuambia mambo mabaya, tunazuia hasira zetu kwa ndani. Hivyo, inawezekana sisi kujidhibiti wenyewe lakini kwa ukweli halisi tunachagua wenyewe kutofanya hivyo. Tufanye nini kuhusu suala hili? Jambo moja ambalo tunaweza kufanya ni kujipangia adhabu sisi wenyewe. Kwa mfano, tunaweza kuamua kwamba kama tukikasirika basi tutafanya jambo fulani ambalo ni gumu kwetu. Na lazima tuitimize ahadi hii ambayo tumeiweka sisi wenyewe. Tunaweza kuahidi kwamba kama tukikasirika na kusema kitu kibaya kwa wake zetu, watoto wetu au wazazi wetu, basi itatubidi tutoe kiasi fulani cha fedha kama sadaka, au tufunge saumu siku inayofuata au tutembee kilomita kumi. Lazima kiwe kitu kigumu. Halafu tutaona kwamba tutaanza kuwa na nguvu kwa sababu nafsi zetu zitakuwa zinafanya mkokotoo wa aina fulani kwamba 72

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 72

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

pamoja na kwamba huwa zinapata kuwa na hasira na kuwa na shari, pia nazo zitapata hasara kwa hiyo adhabu ambayo itakuwa imewekwa baadaye. Hivyo nafsi zetu zitaanza kuwa na nidhamu. Zoezi hili huitwa “musharitah.� Maana ya musharitah ni mtu kujiwekea sharti yeye mwenyewe na kujiwekea adhabu linapovunjwa sharti hilo. Kwa upande mwingine, tunaweza kujipongeza kama tunafanya jambo zuri. Kwa mfano, kama tunapenda peremende sana tunaweza kujiwekea sharti kwamba kama hatukuamka kuswali swala za usiku basi hakuna kula peremende. Kama tukiamka kuswali, basi tutakula peremende. Halafu tutaona kwamba nafsi zetu zitatusaidia kuamka usiku kwa ajili ya sala kwa sababu zinataka peremende. Kwa hiyo, hii ni mbinu ambayo inaweza kutusaidia kuimarisha dhamira yetu. Muda mzuri tu ambao tunaweza kufikiria na kupanga mambo ya aina hii ni ule tunapokuwa na faragha peke yetu. Kama wakati wote tupo na shughuli hatuwezi kufikiria kuhusu mambo kama hayo. Lakini kama tukitumia robo saa au dakika ishirini tukiwa peke yetu basi tunaweza kupata yote haya. Ni vigumu kujua kwa nini watu wanakuwa waoga kubaki peke yao. Mara nyingi tunaweza kuliona hili. Tunajipenda sana lakini kitu kinachotuumiza sana ni kuachwa peke yetu. Kama tukiwekwa chumbani na kufungiwa humo kwa muda wa saa 24 tukiwa peke yetu, hata kama tukiambiwa kwamba tutapewa chakula na vitu vingine vya muhimu lakini tu tutakuwa peke yetu, tutauliza kwa nini tunazuiwa, tunawekwa jela na kuteswa. Lakini kuna ubaya gani kuhusu hili? Hatujafungiwa tukiwa na mnyama wa porini au mhalifu. Tumetakiwa tu kuwa peke yetu. Kwa nini hatutaki kuwa peke yetu? Lazima kuna 73

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 73

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

suala la namna ya maradhi kuhusu tatizo hili. Imam Ali ibn Husayn al-Sajjad anasema: “Endapo watu wote wa mashariki na magharibi wakifariki dunia na nikibaki peke yangu na Qur`ani sitajihisi mpweke.”25

Lakini watu walio wengi ni waoga sana kubaki peke yao hivyo kwamba wakati wote wanajishughulisha. Na kama hakuna mtu karibu yao, watafungulia televisheni au santuri ya mp3 au radio kwa ajili kusababisha kelele ili wasijihisi upweke. Lakini tabia hii ni mbaya sana. Wakati mwingine tunatakiwa tujaribu kuwa peke yetu, tuwe na faragha, tupumzike na kujituliza na tufikirie kuhusu mambo ambayo ni ya muhimu zaidi.

5. Kumkumbuka Mwenyezi Mungu wakati wote. Kumsahau Mwenyezi Mungu ndio chanzo cha matatizo yote ya kiroho na kwa kawaida tiba ya tatizo hili ni kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Kwenye Dua ya Kumayl, tunasoma: “Ee Mungu Wangu! ninaomba kujikurubisha Kwako kwa Utajo Wako…… “Ewe ambaye Jina lako ni tiba na ukumbusho Wako ni ponyo.” Hivyo, kumkumbuka Mwenyezi Mungu huleta utulivu na nuru moyoni: 25

Biharul-Anwar, Jz. 46, uk. 54 74

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 74

7/10/2013 3:33:35 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

‫ﷲ‬ ِ َّ ‫ﷲ ۗ أَ َال ِب ِذ ْك ِر‬ ِ َّ ‫ِين آ َم ُنوا َو َت ْط َمئِنُّ قُلُو ُب ُھ ْم ِبذ ِْك ِر‬ َ ‫الَّذ‬ ُ‫َت ْط َمئِنُّ ْالقُلُوب‬ “Wale walioamini na zikatulia nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu, sikilizeni: kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu, nyoyo hutulia.” [13:28]

Imam Ali (a.s.) anasema: “Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, amefanya utajo Wake kuwa mng`ao unaoangaza ndani ya nyoyo.”26 Hivyo, inakuwa wazi kwa nini msisitizo mkubwa umewekwa kuhusu kumkumbuka ya Mwenyezi Mungu. Qur`ani inasema:

‫ار‬ َ ‫َو ْاذ ُكرْ َر َّب‬ ِ ‫اإل ْب َك‬ ِ ْ ‫ك َك ِثيرً ا َو َسبِّحْ ِب ْال َعشِ يِّ َو‬ َ ‫اإل ْب‬ “…Na mtaje na asuِّ‫ ْال َعشِ ي‬kwa ‫ار‬ ‫ َسبِّحْ ِب‬wingi, ‫ َك ِثيرً ا َو‬na‫َّك‬ ‫و ْاذ ُكرْ َر‬jioni َ ‫ب‬uswali َ ِ ‫ك‬Mola ِ ْ ‫ َو‬wako buhi.”[3:41] ً ‫ِّك َو َت َب َّت ْل إِ َل ْي ِه َت ْبت‬ ‫ِيال‬ َ ‫َو ْاذ ُك ِر اسْ َم َرب‬ ْ ْ َ ‫ار‬ َ ‫َو ْاذ ُكرْ َرب‬ ِ ‫اإل ْبك‬ ِ ‫َّك َك ِثيرً ا َو َسبِّحْ ِبال َعشِ يِّ َو‬ ً ‫َو ْاذ ُك ِر اسْ َم َربِّك و َتب َّت ْل إ َل ْيه َت ْبت‬ ‫ِيال ْال َجھ ِْر م َِن‬ ‫ون‬ َ ‫ض َرُّ َعًا َ َوخ ِ​ِي َف ًة ِ َو ُد‬ َ ‫ك َت‬ َ ِ‫َّك فِي َن ْفس‬ َ ‫َو ْاذ ُكرْ َرب‬ “Na litaje jina ‫ِين‬ la ‫ َِن ْال َغا ِف‬wako ‫ َت ُكنْ م‬na‫و َال‬ujitupe ‫ِب ْال ُغ ُدوِّ َو‬kwa ‫ َق ْو ِل‬kweli.” ‫ْال‬ َ ‫ل‬Mola َ ‫ال‬ َ ‫ ْاآل‬kwake ِ ‫ص‬ ْ ً ُ َ َّ َ ‫ضَمرُّ َرعبًا‬ ‫ِيالھ ِْر م َِن‬ ‫ون َت ْبت ْال َج‬ َ ‫[و َوخ َتِي َب َفت ًة ْل َوإِلُد ْي ِه‬73:8] َ ‫ِّك‬ َ ْ‫كر َتاس‬ َ ‫َو ْاذ ُكرْ َر َّب‬ َِ ‫ك فِي َ َنو ْفاذسِك‬ ‫ِين‬ َ ‫ال َو َال َت ُكنْ م َِن ْال َغا ِفل‬ َ ‫ْال َق ْو ِل ِب ْال ُغ ُدوِّ َو ْاآل‬ Na: ِ ‫ص‬ ‫ون ْال َجھ ِْر م َِن‬ َ ‫ضرُّ عًا َوخِي َف ًة َو ُد‬ َ ‫ك َت‬ َ ِ‫ك فِي َن ْفس‬ َ ‫َو ْاذ ُكرْ َر َّب‬ ‫ِين‬ َ ‫ال َو َال َت ُكنْ م َِن ْال َغا ِفل‬ َ ‫ْال َق ْو ِل ِب ْال ُغ ُدوِّ َو ْاآل‬ ِ ‫ص‬ Na:

26

Nahjul-Balaghah, Semi namba 219.

75

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 75

7/10/2013 3:33:36 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

“Na mkumbuke Mola wako moyoni mwako kwa unyenyekevu na khofu na bila ya kupiga kelele katika usemi, asubuhi na jioni, wala usiwe miongoni mwa walioghafilika” [7:205]

Katika Uislamu, kila kitu kina mipaka yake hata kufunga saumu na hijja. Isipokuwa jambo la kipekee tu ni kumkumbuka Mwenyezi Mungu; jambo ambalo ni zuri sana na linahitajika wakati wote na katika mazingira ya kila aina.27 Ahmad b. Fahd Hilli anasimulia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Jueni kwamba matendo yenu mazuri kabisa karibu na Allah, na yaliyo masafi kabisa na ya daraja la juu kabisa, na kitu kizuri kabisa ambacho jua limemulika mwanga wake ni kumkumbuka Allah, Mwenye Enzi. Kwa kweli Yeye amewataarifuni akisema: “Mimi ni mwenza wa yule anayenikumbuka Mimi.”28 Kumkumbuka Allah swt wakati wote linaweza kuwa zoezi gumu na linaweza kuwa rahisi pia. Zoezi hili sio gumu kwa sababu halitugharimu chochote, hatuhitaji kulipa fedha au kwenda mahali popote maalum au kufanya mazoezi ya viungo. Kwa hiyo linapaswa kuwa rahisi sana, kama yalivyo mazoezi mengine ambayo yametajwa kwenye kurasa za nyuma ambayo hakuna linalotugharimu chochote na kwa hiyo ni mbinu zenye athari ya gharama tunapofikiria yale matokeo yanayoweza yakayazalisha. Hata hivyo, pia ni zoezi gumu sana kwa sababu kila mara nafsi zetu hujaribu kujiendekeza kufanya kile zinachotaka na huwa hazitaki kudhibitiwa kinidhamu. Lakini kama tukiweka kinidhamu nafsi zetu basi mambo yanakuwa rahisi. 27 28

Kwa mfano, tazama al-Kafi, Jz. 2, uk. 498 na 499 Uddat al-Da‘i, uk. 238 76

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 76

7/10/2013 3:33:36 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Kumkumbuka Mwenyezi Mungu ni ponyo. Majina ya Mwenyezi Mungu ni dawa na kama tukinywa dawa hizi kwa lengo la kumkumbuka Mwenyezi Mungu basi tutapona, lakini kama tukikariri mfululizo utajo kama ‘Allahu Akhbar’ tena na tena lakini tusimkumbuke Mwenyezi Mungu basi ni kwamba tunaishughulisha midomo yetu kwa kukariri huku si njia nzuri ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Hata hivyo, kama tukitumia Majina ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kumkumbuka Yeye basi hii ni ponyo. Ni rahisi sana kufanya hivi. Kwa mfano, tunaweza kuwa tunaendesha gari au tunatembea au tunaweza kuwa tunafanya chochote kile na bado tutakuwa tunamkumbuka Mwenyezi Mungu. Qur`ani inazungumza kuhusu watu wasiomsahau Mwenyezi Mungu hata wanapokuwa katika shughuli zao au biashara.Wakati wote wanamkumbuka Mwenyezi Mungu. Tunaweza kuwa tunapika au tunafua nguo, tunafundisha darasani au tunasoma, lakini wakati huohuo lazima tumkumbuke Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo, tunahitaji kumkumbuka Mwenyezi Mungu na dhikiri hizi ni njia ya kutusaidia katika kudumisha umakinikaji wetu na mazingatio. Hizi aina mbali mbali za dhikiri [kama vile; Allahu Akhbar, Alhamdullillah na Subhanallah] ni dawa lakini lazima tutumie dawa hizi kwa usahihi katika kumkumbuka Mwenyezi Mungu, kwa kujaribu kuikaribia ile Sifa ya Mwenyezi Mungu ambayo tunaitaja na halafu tutajihisi kwamba tupo karibu zaidi na Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo hii ni njia ambayo kwayo tunapaswa kuitumia katika kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kama tukionja utamu na uzuri wa kumkumbuka Mwenyezi Mungu kwa kweli basi kamwe hatutapata kitu kingine cha kutufurahisha zaidi ya hicho.Tunahitaji kuviondoa vitu vingine vyote vibaya 77

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 77

7/10/2013 3:33:36 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ndani ya nafsi zetu na hapo ndipo tutakapoanza kufurahia kumkumbuka Mwenyezi Mungu kwa kweli. Kama tukitumia muda fulani wa faragha tukiwa peke yetu basi tunaweza kuanza kujifunza jinsi ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu wakati huo tunapokuwa peke yetu na halafu kupanua zoezi hili katika maisha yetu yote. Mwanzoni tunaweza kuwa tunamkumbuka Mwenyezi Mungu tunapokuwa kwenye mkeka wa swala tu. Lakini polepole tunaweza kujaribu kumkumbuka Mwenyezi Mungu katika kipindi chote cha siku nzima. Na halafu tabia ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu inakuwa ya muda wote.

78

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 78

7/10/2013 3:33:36 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

USHAURI WA KIVITENDO WA KUSHIRIKISHA SIFA HIZI KATIKA MAISHA YAKO

K

ama tulivyoona hapo juu, yapo mambo matano muhimu ambayo tunatakiwa kuyachunga: tusiseme kupita kiasi, tusile kupita kiasi, tusilale kupita kiasi, tuwe na muda wa faragha kwa ajili ya tafakuri na kumkumbuka Allah swt wakati wote. Haya ni mambo matano ambayo ni rahisi sana kuyatekeleza na hayana gharama yoyote. Mambo haya matano ni vitamini zenye nguvu sana kwa ajili ya makuzi na maendeleo yetu ya kiroho. Kama mtu akiyadumisha kwa muda wa wiki kadhaa kwa hakika ataanza kuhisi tofauti na ataona matokeo. Hatua moja ya kivitendo ni kuwa na kijitabu kidogo ambamo mtu utajiwekea malengo yako ya kila siku. Jiwekee maksi kwa kila lengo. Inapohitajika wakati wowote weka maoni. Halafu kwa mpangilio maalum uwe litaleta yale maoni na utathimini maendeleo yako. Fuata utaratibu huu kila siku na ulinganishe matendo yako na malengo yako. Kama matendo yote ni mazuri basi mshukuru Mwenyezi Mungu na uendelee. Kama baadhi ya sehemu ni mbaya, jaribu kuongeza bidii na uboreshe. Kwa wiki chache za mwanzo, usijihatarishe kwa kuchelewesha mpangilio huu kwa sababu yoyote ile. Jaza chati katika mazingira yote. Hili litaleta nidhamu katika maisha yako. Kama ukihisi kama vile unaanza kufanikiwa, utajihisi kudhamiria zaidi. Kama ukihisi zipo sehemu ambazo huwezi kufanya vizuri, hata ukijaribu 79

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 79

7/10/2013 3:33:36 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kufanya hivyo, basi jipangie adhabu mwenyewe .Mathalani, kama nikiona kwamba wiki iliyopita niliendelea kupata hasira, nitapaswa kutafuta jambo ambalo ni gumu kufanya, kama vile kazi za nyumbani; na halafu kuanza adhabu hiyo: mfano unaweza kusema “kama nikipata hasira tena, nitafanya kazi zote za nyumbani kwa siku mbili mfululizo.” Baada ya kufanya adhabu ya aina hii mara kadhaa nitajifunza kufikiri kabla ya kukasirika, na kujizuia mwenyewe. Kwa namna hiyo hiyo toa motisha kidogo kwa matendo mema, unaweza kujipangia mwenyewe namna ya zawadi. Kwa njia hii utaongeza dhamira. Msaada wa Allah swt wakati wote utakuwapo kwa wale wanaojitahidi kwa ajili Yake.

‫ِين‬ َ ‫ﷲ َل َم َع ْالمُحْ سِ ن‬ َ ‫َوالَّذ‬ َ َّ َّ‫ِين َجا َھ ُدوا فِي َنا َل َن ْھ ِد َي َّن ُھ ْم ُس ُب َل َنا ۚ َوإِن‬ “Na wale wanaojitahidi kwa ajili Yetu, lazima tutawaongoza kwenye njia Zetu. Na bila shaka Mwenyezi Mungu yu pamoja na wafanyao mema” [29:69]

‫ت‬ ِ ‫ِين آ َم ُنوا َو َع ِملُوا الصَّال َِحا‬ َ ‫ان َلفِي ُخسْ ٍر إِ َّال الَّذ‬ َ ‫اإل ْن َس‬ ِ ْ َّ‫إِن‬ Pia inasaidia sana kuwa ِّ ‫ُد َح‬karibu ‫ص َلب‬ ‫ ِب ْمال‬marafiki ‫ص ِد ْ َيو َّا‬ ‫واق‬ ‫ِين ْوا َج ِاب َ ْال‬ ‫اص‬ َّ ‫س‬na َ ‫ف َِيو َ َنتا َواَل َن ْھ‬wa َ sana َّ َّ‫ْر ۚ َوإِن‬ ْ ‫ﷲ َل َم َع‬ َّ‫ َو َ َتو َاول‬wenye ِ َ ْ‫ُح‬ ُ ُ ُ ‫ِين‬ ‫ن‬ ‫م‬ ‫ال‬ ‫ا‬ ‫ن‬ ‫ب‬ ‫ھ‬ ‫ن‬ ‫ھ‬ ‫ذ‬ ِ‫س‬ َ َ َ uelekeo kama wa kwako, ambao unaweza kuzungumza nao kuhusu maendeleo yako na matatizo yako. Kwa njia hii, pia mnaweza kushauriana nyinyi .kwa nyinyi. Qur`ani inasema:

‫ت‬ ِ ‫ِين آ َم ُنوا َو َع ِملُوا الصَّال َِحا‬ َ ‫ان َلفِي ُخسْ ٍر إِ َّال الَّذ‬ َ ‫اإل ْن َس‬ ِ ْ َّ‫إِن‬ ‫صب ِْر‬ َّ ‫اص ْوا ِبال‬ َ ‫ص ْوا ِب ْال َح ِّق َو َت َو‬ َ ‫َو َت َوا‬ “Kwa hakika mwanadamu yumo hasarani. Isipokuwa wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri, na wakausiana haki, na wakausiana kusubiri.” [103:2-3]. 80

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 80

7/10/2013 3:33:37 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Mukhtasari: Kwenye makala hii, tumeangalia njia mbalimbali za kivitendo ambazo tunaweza kufanya ujenzi wa nafsi. Kwa kuzungumza kidogo, kula kidogo, kulala kidogo, kujiwekea muda wa faragha, na kumkumbuka Allah swt, hakika tunaweza kuanza kupata ukaribu na Allah swt kwa njia ya kuitakasa nafsi. Mbinu ambazo zimezungumziwa hapo juu, wala si ngumu sana ama zenye gharama kubwa, isipokuwa zinahitaji subira na dhamira.Tunaomba kwamba Allah swt atujaalie na haya ili tuweze kupata malipo ya kweli: kuwa jirani zaidi Naye swt. Mwenyezi Mungu na atusaidie sisi sote!

81

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 81

7/10/2013 3:33:37 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

DHANA ZA MSINGI KATIKA UTAKATIFU WA KIISLAMU: UPENDO, SHUKURANI NA UNYENYEKEVU

U

pendo, Shukurani na Unyenyekevu ni dhana tatu muhimu ama pengine zilizo muhimu zaidi kiroho katika utakatifu wa Kiislamu. Katika makala haya, dhana hizi zitazungumziwa kwa ufupi. Dhana hizi tatu muhimu hazikuchaguliwa kwa sababu ya umuhimu wao kinadharia tu, lakini pia kimsingi ni zenye malipo. Kama tunataka kukua kiroho, tunaweza kufuzu kwa urahisi ikiwa tutakuza sifa hizi katika maisha yetu. UPENDO Kufuatana na hadithi za Kislamu zikiungwa mkono na hoja zenye mantiki, sababu nzima ya kuwa na imani au kutokuwa na imani imejengeka kwenye msingi wa kumpenda Allah swt, na chochote kile chenye uhusiano na Yeye swt. Mathalani, tunasoma kwenye hadithi kwamba wakati fulani Mtume (s.a.w.w.) aliwauliza sahaba wake:”Ni kipi kishiko chenye nguvu kabisa katika Uislamu?” Sahaba walitoa majibu yaliyotofautiana: wengine walisema swala, wengine walisema saumu, na wengine walisema hijja. Baada ya sahaba kutoa majibu haya, wakasema:” Allah na Mtume wake ndio wanaojua zaidi.” Hivyo Mtume akajibu: “Kupenda kwa ajili ya Allah swt na kuchukia kwa ajili ya Allah swt.” 82

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 82

7/10/2013 3:33:37 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Lazima tuulize: kuna tofauti gani baina ya muumini na ambaye si muumini? Haitoshi tu kujua ukweli fulani: Shetani anajua ukweli wote huo kabisa lakini yeye bado anachukuliwa kwamba si mtiifu. Allah anasema katika Qur`ani kwamba wapo watu wanaojua kila kitu lakini si waumini:

ُ ‫َو َج َح ُدوا ِب َھا َواسْ َت ْي َق َن ْت َھا أَ ْنفُ ُس ُھ ْم‬ ۚ ‫ظ ْلمًا َو ُعلُ ًّوا‬ “Na wakaikataa hali ya kuwa nafsi zao zina yakini nayo, [27:14] َّ na‫ا ب‬kujivuna…..” ‫خِر وما ُھم‬kwa ‫م ْاآل‬dhulma ‫ا� وب ْالي ْو‬ ‫اس منْ يقُو ُل آم َّن‬ ‫ِن ال َّن‬.‫وم‬

َ َ Kadhalika, kutamka ukweli hakutoshi ‫ِين‬ kuwa َ ‫ ِبم ُْؤ ِمن‬muumini, ُ ‫فُ ُس ُھ ْم‬ukweli kwani wanafiki ‫اسْ َت ْي َق َن ْت َھا أَ ْن‬kila ‫ ِب َھا َو‬wakati. ‫ َو َج َح ُدوا‬Katika ۚ ‫و ُعلُ ًّوا‬hutamka َ ‫ظ ْلمًا‬ ْ

َ َ ِ

ِ َ ِ َ ِ ِ

َ

َ

َ ِ

kuwaelezea watu kama hao Qur`ani inasema:

‫ا� َو ِب ْال َي ْو ِم ْاآلخ ِ​ِر َو َما ُھ ْم‬ ِ َّ ‫اس َمنْ َيقُو ُل آ َم َّنا ِب‬ ِ ‫َوم َِن ال َّن‬ ‫ِين‬ َ ‫ِبم ُْؤ ِمن‬ “Na miongoni mwa watu,wako wasemao: Tumemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, hali wao si wenye kuamini.” [2:8]

Kupenda ukweli ndio tofauti kuu baina ya muumini na asiye muumini. Upendo huhitaji ujuzi na utayari kutamka. Huu utayari wa kutamka ukweli haujumuishi mazingira ambapo mtu lazima afanye ‘taqiyyah,’ au mtu kuficha imani yake kwa lengo la kuhami maisha yake au maisha ya waumini wengine. Mtu anaweza kushangaa kwa nini Uislamu unalenga katika vyote, kupenda kwa ajili ya Allah swt na kuchukia 83

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 83

7/10/2013 3:33:37 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kwa ajili ya Allah swt. Mtu anaweza kuhoji haja ya kuchukia na kusema kwamba tunapaswa kuwa na mapenzi tu kwenye nyoyo zetu. Hata hivyo, Uislamu ni dini ya mantiki, na inaeleweka kimantiki kwamba tunapokipenda kitu kuna pia ulazima wa kuchukia kile ambacho ni kinyume chake. Tunawezaje kumpenda mwaminifu na tusimchukie asiye mwaminifu? Au tupende ukweli lakini tusichukie batili? Kama unapenda wema, huna jinsi isipokuwa kuuchukia uovu. Kadhalika, kama unampenda Allah swt, moja kwa moja bila kusita utawachukia maadui Zake. Kama mambo yalivyo, muumini hapaswi kujenga chuki binafsi dhidi ya mtu mwingine yeyote. Kama tunamchukia mtu, ni kwa sababu ya sifa zake mbaya. Inawezekana tukampenda mtu kama mja wa Allah swt, lakini hatuwezi kupenda sifa zake mbaya alizonazo. Hii ndio maana halisi ya kimantiki ya kupenda vitu vizuri. Hata kama hizi dhana mbili zikifikiriwa kila moja kivyake, zinakuwa na maana moja kama pande mbili za sarafu moja. Kama tunataka kujiendeleza, tunapaswa kujaribu kuongeza mapenzi yetu kwa Allah swt na wale walio karibu Naye, na kuongeza mapenzi yetu kwenye vitendo vinavyopendwa na Allah swt. Hili linaweza kufanikiwa kwa kupata elimu zaidi na halafu kuifanyia tafakari. Njia mojawapo ya kuvutia na ya kivitendo katika kujiendeleza ni kusoma wasifu wa watu ambao wamempenda sana Allah swt na kuendeleza uhusiano wa karibu sana Naye swt. Simulizi za maisha yao hufichua siri nyingi zilizofichika kuhusu maisha yao, ambazo zinaweza kutusaidia na kututia moyo wa kuelekea zaidi kwenye njia yao ya maisha. Kwa kawaida hii ni nji yenye kutia moyo. 84

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 84

7/10/2013 3:33:37 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Elimu yoyote anayoipata mtu lazima iambatane na mtu kutafakari ili aweze kuitumia elimu hiyo kivitendo. Tafakuri huleta utulivu katika nafsi ya mtu, kwani hisi za mtu huanza kusaidia elimu yake. Kwa mfano, kama ninajua kwamba kusema uwongo ni vibaya, bado ninaweza kuendelea kusema uwongo. Ninahitaji kuchukua dakika chache kila siku za kufikiria kwa nini kusema uwongo ni vibaya, na kutambua, kwa mfano, kwamba uwongo hauleti manufaa yoyote. Kama tukitafakari kuhusu watu tunaowapenda tunaweza kujiuliza: kwa nini tunawapenda watu hawa? Kama mtu akikupa kazi, hutamsahau katika kipindi chote cha uhai wako; kama mtu anakufundisha kitu, utashukuru na utamkumbuka; kama mtu anakusaidia, au anakupa fedha, au kama jirani yako anaonyesha tabasamu kwako, au ni mpole, watu hawa utawapenda. Hatuhitaji sababu kubwa sana kuwapenda watu: ni kujali kidogo tu na upendo vinatosha. Kwa hiyo, kwa nini tusiweze kumpenda Allah swt ambapo kila kitu tulichonacho kinatoka Kwake na hakuna kitu kibaya kinachotoka Kwake? Tunayajua mambo haya, lakini tunahitaji kuyafanyia kutafakuri tu. Kama mapenzi yetu kwa Allah swt yanaongezeka na kuwa makubwa zaidi, basi hatuwezi kumuasi Yeye. Utamuasi vipi na kumkasirisha Yule unayempenda? Kwa hiyo, mapenzi kwa ajili ya Allah swt ni fikra muhimu sana ambayo inaweza kutusaidia kivitendo katika kujiendeleza kiroho, na kuwa karibu Naye swt. SHUKURANI Tabia ya kushukuru inahusiana sana na kupenda kwa ajili ya Allah swt. Kama wewe ni mtu wa kushukuru kwa hakika utampenda Allah swt kwa sababu ya neema Zake zote na 85

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 85

7/10/2013 3:33:37 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kama ukimpenda Allah utamwamini na utamtii Yeye. Hivyo basi, kushukuru ni kiini cha imani. Inawezekana isiwe ni jambo la kubahatisha kwamba katika lugha ya Kiarabu msamiati uliotumika kuonyesha tabia ya kutokushukuru na kutokuamini ni wenye kufanana ama ni ule ule , yaani: kufr. Zifuatazo ni baadhi ya aya za Qur`ani ambamo tofauti imeonyeshwa baina ya kushukuru na kutokushukuru:

ۖ ‫ض ٰى لِ ِع َبا ِد ِه ْال ُك ْف َر‬ َ ْ‫ﷲ َغنِيٌّ َع ْن ُك ْم ۖ َو َال َير‬ َ َّ َّ‫إِنْ َت ْكفُرُوا َفإِن‬ ‫از َرةٌ ِو ْز َر أ ُ ْخ َر ٰى ۗ ُث َّم‬ َ ْ‫َوإِنْ َت ْش ُكرُوا َير‬ ِ ‫ض ُه َل ُك ْم ۗ َو َال َت ِز ُر َو‬ ‫ت‬ ِ ‫ون ۚ إِ َّن ُه َعلِي ٌم ِب َذا‬ َ ُ‫إِ َل ٰى َر ِّب ُك ْم َمرْ ِج ُع ُك ْم َف ُي َن ِّب ُئ ُك ْم ِب َما ُك ْن ُت ْم َتعْ َمل‬ ‫ور‬ ُّ ‫ال‬ ِ ‫ص ُد‬ َّ haja “Mkikufuru, ُ‫ إِنْ َت ْكف‬wala ۖ ‫ ْال ُك ْف َر‬basi ‫لِ ِع َبا ِد ِه‬Mwenyezi ‫ض ٰى‬ ۖ ‫نِيٌّ َع ْن ُك ْم‬hana ‫ﷲ َغ‬ َّ‫رُوا َفإِن‬nanyi, َ ْ‫ َو َال َير‬Mungu َ َ َ ٰ ُ َ ً ْ ْ ُ َ ُ‫ا عِ ن َده‬mkishukuru, haridhii ْ‫ َھذا ِمن‬na ‫ َف َلمَّا َر ْآهُ ُ مُسْ َتق ِّر‬hayo ‫أأ ُشك ُر‬kufru ‫ َي ُ ْب ْل َونِي‬kwa ‫ َفضْ ِل‬wake, ‫قا َل‬kama ِ‫ َرب ِّْي ل‬waja ُ َ َ ٌ َ ٰ ْ‫رُوا َير‬wa ُ ُ ‫م‬ ‫ث‬ ۗ ‫ى‬ ‫ر‬ ‫خ‬ ‫أ‬ ‫ر‬ ‫ز‬ ‫و‬ ‫ة‬ ‫ر‬ ‫از‬ ‫و‬ ‫ر‬ ‫ز‬ ‫ت‬ ‫ال‬ ‫و‬ ۗ ‫م‬ ‫ك‬ ‫ل‬ ‫ه‬ ‫ض‬ ‫شك‬mwingine, ‫َوإِنْ َت‬ َ َ َ َ َ َ ْ َّ atawaridhieni, walaِ mbebaji mzigo ِ ‫ ُر ِ ل َن ْف ه‬hatabeba ْ ُ ُ َّ َ َ َ َ َ َ ْ‫ن‬ ْ‫ن‬ ُ ‫ِّي‬ ‫ب‬ ‫ر‬ ‫إ‬ ‫ف‬ ‫ر‬ ‫ف‬ ‫ك‬ ‫م‬ ‫و‬ ۖ ‫ك‬ ‫ش‬ ‫ي‬ ‫ا‬ ‫م‬ ‫ن‬ ‫إ‬ ‫ف‬ ‫ر‬ ‫ك‬ ‫ش‬ ‫م‬ ‫و‬ ۖ ‫ر‬ ‫ف‬ ‫أَ ْم أَ ْك‬ َّ‫ن‬ ِ ِ‫س‬ ِ َ َ َ َ َ َ َ َ َ kisha ‫ت‬ marejeo ُ ‫ ُك ْم َف ُي َن ِ ِّب ُئ‬basi ْ‫ ُك ْن ُت ْم َتع‬Mola ‫ون ۚ إِ َّن ُه‬ ‫ك ْم ِب َما‬Wenu, ‫ َمرْ ِج ُع‬atakuambieni ‫إِ َل ٰى َر ِّب ُك ْم‬ ِ ‫ َعل ِ​ِي ٌم ِب َذا‬yenu َ niُ‫ َمل‬kwa yale mliyokuwa mkifanya. Bila shaka Yeye ni‫ ٌم‬Mjuzi ‫َغنِيٌّ َك ِري‬wa yali‫ور‬ ُّ ‫ال‬ omo vifuani.” [39:7] ِ ‫ص ُد‬ ‫َف َلمَّا َرآهُ مُسْ َتق ًِّرا عِ ْن َدهُ َقا َل ٰ َھ َذا ِمنْ َفضْ ِل َربِّي لِ َي ْبلُ َونِي أَأَ ْش ُك ُر‬ ‫أَ ْم أَ ْكفُ ُر ۖ َو َمنْ َش َك َر َفإِ َّن َما َي ْش ُك ُر لِ َن ْفسِ ِه ۖ َو َمنْ َك َف َر َفإِنَّ َربِّي‬ ‫َغنِيٌّ َك ِري ٌم‬ “….. Basi alipokiona kimewekwa mbele yake, akasema: Haya ni kwa fadhili za Mola Wangu, ili anijaribu nitashukuru au nitakufuru? Na anayeshukuru, basi anashukuru kwa ajili ya nafsi yake na anayekufuru, hakika Mola Wangu ni Mkwasi, Mkarimu.” [27:40]

86

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 86

7/10/2013 3:33:38 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

‫� ۚ َو َمنْ َي ْش ُكرْ َفإِ َّن َما َي ْش ُك ُر‬ ِ َّ ِ ْ‫ان ْالح ِْك َم َة أَ ِن ا ْش ُكر‬ َ ‫َو َل َق ْد آ َت ْي َنا لُ ْق َم‬ ‫ﷲ َغنِيٌّ َحمِي ٌد‬ َ َّ َّ‫لِ َن ْفسِ ِه ۖ َو َمنْ َك َف َر َفإِن‬ “Na kwa hakika tulimpa Luqmani hekima ya kwamba, َ ‫ ْط َف ٍة‬atakayekushukuru, mshukuru ‫لِي ِه َف َج َع ْل َناهُ َس‬Mungu, ‫اج َن ْب َت‬ ‫ان ِمنْ ُن‬ ‫مِيعًا بَصِ يرً ا‬Mwenyezi َ ‫اإل ْن َس‬ ِ ْ ‫ إِ َّنا َخ َل ْق َنا‬basi ٍ ‫ أ ْم َش‬na kwa hakika atashukuru ُ kwa ajili ya nafsi yake, na َّatakaye ُ‫ إِنا َھدَ ْي َناه‬kusi‫رً ا َوإِمَّا َكفورً ا‬ni ‫ َشا ِك‬Mkwasi, ‫الس َِّبي َل إِ َّما‬Mwenye kufuru, basi Mwenyezi Mungu fiwa.” [31:12]

Aya ya kuvutia sana imo kwenye Sura ya Insaan [76:23], ambapo shukurani kwa Allah swt kwa ajili ya muongozo ْ‫� ۚ َو َمن‬ ‫ َي ْش ُكرْ َفإِ َّن َما َي ْش ُك ُر‬kufanana ‫ ا ْش‬imani ‫ح ِْك َم َة أَ ِن‬na ‫ان ْال‬ ‫َو َل َق ْد آ َت ْي َنا لُ ْق َم‬ Wake inachukuliwa ni ِ َّ ِ ْ‫ ُكر‬na َ kutokushukuru kinyume chake: َّ َّ‫لِ َن ْفسِ ِه ۖ َو َمنْ َك َف َر َفإن‬ ‫ﷲ َغنِيٌّ َحمِي ٌد‬

َ

ِ

َ ْ ‫اج َن ْب َتلِي ِه َف َج َع ْل َناهُ َسمِيعًا بَصِ يرً ا‬ َ ‫اإل ْن َس‬ ِ ْ ‫إِ َّنا َخ َل ْق َنا‬ ٍ ‫ان ِمنْ ُنط َف ٍة أمْ َش‬ ‫إِ َّنا َھدَ ْي َناهُ الس َِّبي َل إِ َّما َشا ِكرً ا َوإِمَّا َكفُورً ا‬ “Kwa hakika tulimuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliochanganyika, tunamjaribu, hivyo tukamfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona. Hakika sisi tumemuongoza njia awe mwenye kushukuru au awe mwenye kukufuru.” [76:2-3]

Kwa hiyo, shukr [kushukuru] ni dhana muhimu sana. Ni jambo la msingi ambalo linahusiana na kiini cha imani. Pia ni jambo la kivitendo ambalo si gumu. Zaidi ya hayo, kama tu wenye kushukuru, tunaweza kupata vitu vingi kama asemavyo Allah swt ndani ya Qur`ani:

87

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 87

7/10/2013 3:33:38 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ْ‫ﷲ َع َل ْي ُك ْم إِ ْذ أَ ْن َجا ُك ْم ِمن‬ ِ َّ ‫ُوس ٰى لِ َق ْو ِم ِه ْاذ ُكرُوا ِنعْ َم َة‬ َ ‫َوإِ ْذ َقا َل م‬ ‫ُون أَ ْب َنا َء ُك ْم‬ ِ ‫آل ِفرْ َع ْو َن َيسُومُو َن ُك ْم سُو َء ْال َع َذا‬ َ ‫ب َو ُي َذ ِّبح‬ ِ ٰ َ ‫ُون ِن َسا َء ُك ْم ۚ َوفِي ذلِ ُك ْم َب َال ٌء ِمنْ َر ِّب ُك ْم عَظِ ي ٌم‬ َ ‫َو َيسْ َتحْ ي‬ ‫َوإِ ْذ َتأ َ َّذ َن َر ُّب ُك ْم َل ِئنْ َش َكرْ ُت ْم َألَ ِزيدَ َّن ُك ْم ۖ َو َل ِئنْ َك َفرْ ُت ْم إِنَّ َع َذ ِابي‬ ‫َل َشدِي ٌد‬ “Na [kumbuka] Musa aliposema kwa watu wake, kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu, alipokuokoeni kwa watu wa Firaun, waliokupeni adhabu mbaya, na wakawachinja watoto wenu wanaume wakawaacha hai watoto wenu wanawake. Na katika hayo ulikuwa mtihani mkubwa unaotoka kwa Mola wenu. Na [kumbukeni] alipotangaza Mola wenu, kama mkishukuru bila shaka nitakuzidishieni, na kama mkikufuru, hakika adhabu yangu ni kali sana.” [14:6-7]

Fikiria mwalimu mwenye mwanafunzi aliye na shukurani. Mwanafunzi huyo anamkubali mwalimu na anatambua kwamba mwalimu anafanya kazi nzuri ya kumsaidia yeye. Zaidi ya hayo, mwanafunzi ametamka kwamba anashukuru sana, na kisiha anatekeleza kwa vitendo yale ambayo amefundishwa na mwalimu wake. Mwalimu naye atapenda kumfundisha mwanafunzi huyu yote yale anayoyajua, kwani mwalimu hata hisi kwamba ujuzi wake unapotea bure. Huu ni mfano wa mja mwenye kushukuru ambaye ndani ya moyo wake anakubali, kwa ulimi wake anatamka, na kwa mwili wake, anatenda. Allah swt atamjaalia mtu kama huyu zaidi na zaidi na Yeye hana mipaka. Jinsi anavyotoa zaidi, ndivyo utakavyopokea zaidi. Katika Dua ya Iftitaah tunasoma: 88

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 88

7/10/2013 3:33:38 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

“Ewe ambaye wingi wa utoaji haumuongezi Yeye, ukiachilia mbali ukarimu na wema!” Mtu anaweza kushangaa kwamba inawezekanaje ukarimu wa Allah swt kuongezeka kwa kutoa zaidi. Pale Allah swt anapokupa wewe kitu na ukamshukuru na ukaweza kudumisha hali hiyo, uwezo wako wa kupokea huongezeka. Ukarimu wa Mwenyezi Mungu hauna mipaka isipokuwa uwezo wetu ndio wenye mipaka. Jinsi Allah swt anavyozidi kutoa, ndivyo na uwezo wetu wa kupokea unavyozidi kuongezeka, na ndivyo ukarimu Wake unavyozidi kuongezeka katika neema Zake zisizo na ukomo. Nadharia ya kushukuru imechunguzwa na wanachuoni wengi wa Kislamu ambao wameifanyia utofautishaji mwingi baina ya aina mbalimbali za shukurani. Kwa mujibu wa Khajeh Abdullah Ansari kwenye kitabu chake ‘Manaazil alSaairiin’ [Vituo vya Wasafiri], zipo aina tatu kuu za shukurani: 1. Shukurani kutoka moyoni: ni kutambua kwamba kitu fulani ni zawadi kutoka kwa Allah swt. 2. Shukurani kwa maneno: ni kutamka kwamba unashukuru juu ya neema za Mwenyezi Mungu. 3. Kushukuru kivitendo: ni kufanya jambo kwa mikono, miguu, macho na kadhalika, kama vitendo vya ibada. Huku ni kushukuru kivitendo. Aina ya kwanza ya kushukuru ni muhimu zaidi, kwani ndio inayoleta zile aina zingine mbili. Pia anasema kwamba shukurani ina mambo matatu makuu: • Mtu kutambua kwamba kitu fulani ni zawadi: kwa mfano, mtu anaweza kujua kila kitu kuhusu afya, 89

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 89

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

lakini kujua kwamba afya ni zawadi kutoka kwa Allah swt ni kujua jambo jingine la nyongeza. • Kukiri kwamba hii ni zawadi kutoka kwa Allah swt: hii ina maana ya kukubali kwamba kile kitu ambacho mtu amepewa ni zawadi, na kwamba yeye ni mpokeaji. Wakati mwingine mtu huweza kutambua kwamba kitu fulani ni zawadi lakini akakataa kukubali kwa sababu tu ya jeuri. Mtu anaweza kufikiri kwamba kitu hicho amekichuma, au kwamba anaweza kuishi bila kuwa nacho. • Kumtukuza Allah swt kwa kumjaalia zawadi hiyo. Mwisho, Khajeh Abdullah Ansari amechunguza dhana hii ya shukurani na kudai kwamba; mtu kuwa mwenye shukurani kuna ngazi tatu: 1. Baadhi ya ngazi hushirikisha watu wa kawaida: huelewa kwamba zawadi zingine hutoka kwa Allah swt ambazo hushukuru tunapozipata, na hujaribu kufurahia na humtukuza Yeye swt. 2. Kuhusu ngazi za juu zaidi, watu sio tu hushukuru kwa yale wanayoyachukulia kwamba ni zawadi kutoka kwa Allah swt, bali kwa lolote lile linalowatokea. Hata kitu kibaya kikimtokea muumini, huelewa kwamba hakikusababishwa na chuki ya Allah swt dhidi yake, kwa hiyo muumini hushukuru kwa hilo. 3. Wapo waja wa Allah swt ambao hujihusisha sana na kuwepo kwa Allah swt: hawa huwa hawahisi raha au maumivu kimwili kwani hawana muda wowote wa kufikiria kama wapo katika hali ya raha au maumivu. Hii ni nguvu 90

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 90

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ya upendo. Vivyo hivyo, mathalani, kama unatazama sinema ya kuvutia sana, unaweza ukasahau kuwa una njaa. Au kama tupo na watu tunaowapenda sana, bila shaka tunaweza kusahau hata muda na kutaka kukutana na mtu huyo kusifike mwisho. Watu wanaompenda Allah swt katika kiwango hicho hutekwa kabisa na Uumbaji Wake swt wa Msingi. Khajeh Abdullah Ansari anaiita hiyo ni shukurani ya wanachuoni. Upendo na shukurani ni dhana mbili zinazoingiliana ambazo zinaweza kutusaidia kivitendo katika safari yetu ya kuendeleza nafsi. Imam Khomeini (r.a.) kwenye kitabu chake Forty Hadiths – Hadithi Arobaini, ameonyesha kwamba kuonekana kwa athari za upendo na shukurani huonekana wazi moyoni, kwenye ulimi, na hata kwenye vitendo na miondoko ya kimwili. Kuhusu moyo, mtu hujawa na unyenyekevu, heshima iliyochanganyikana na hofu, na upendo. Kuhusu ulimi, athari zake ni miongoni mwa kumsifu na kumtukuza Allah swt pekee. Kuhusu mwili, athari zake ni utiifu na kuutumia mwili kwa ajili ya Allah swt. Tumuombe Allah swt azidishe mapenzi yetu Kwake kwa kuongeza uelewa wetu kuhusu Yeye, na atupe moyo wa kuwa wenye kushukuru katika kila hali. UNYENYEKEVU Nadharia nyingine kuu na muhimu ya mambo ya kiroho ya Kislamu ni unyenyekevu wa hali ya juu kabisa au mapungufu ya kiroho. Maana yake ni kuimarisha uelewa wetu wa kumhitaji Allah swt na tupate hisia ya kumtegemea Yeye kikamilifu. Maana yake ni kwamba hata kusema, “Allah swt 91

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 91

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

amekuwa mwema sana kwangu” au kwamba “Allah swt amekuwa mkarimu sana kwangu” haitoshi. Sisi binadamu ni nani bila ya ihsani na rehema ya Allah swt? Sisi binadamu wala si lolote! Sio kwamba Allah swt amekuwa mkarimu kwa kitu ambacho hakimtegemei Yeye. Sisi binadamu si lolote zaidi ya kile alichokiumba Yeye. Vitu vyote vizuri hutoka Kwake; katika mpangilio mzuri sana sisi ni wapokeaji tu, viumbe tegemezi kwa Allah swt na tusio na uhuru kutokana na Yeye kwa hali yoyote ile. Mtu anaweza kulinganisha hili na unyenyekevu: lakini hili ni muhimu zaidi, na zito zaidi, na katika kiwango cha juu zaidi. Wakati mwingine watu hujaribu sana kuwa wanyenyekevu. Mathalani, kama wakijihisi kuwa muhimu sana kwa sababu wamefanikiwa basi hujaribu kujidhibiti ili wasije wakawa na kiburi; hayo ni mapambano. Lakini kama mtu akiwa na mapungufu ya kiroho, huyu hana haja ya mapambano, kwani mtu atakuwa anahisi kwamba hana kitu chochote cha kwake mwenyewe binafsi cha kuweza kujivunia isipokuwa zawadi kutoka kwa Allah swt. Tafakari kuhusu ukomo wetu ya uhitaji na utegemezi wetu kwa Allah swt haiachi mwanya wowote kwa ajili ya namna yoyote ya kujisifu au kujipenda. Chochote kile tulichonacho au tunachoweza kukipata kipo katika umiliki wa Allah swt. Sisi hupewa vitu kama amana kwa kipindi kifupi na tutakuja kuulizwa mnamo Siku ya Hukumu kuhusu jinsi tulivyotumia vitu hivyo. Kwa kweli, sisi wenyewe ni wa Mwenyezi Mungu katika uhai wetu wenyewe hasa. Mwandishi Rene Guenon [1973] ameandika: Mwanadamu tegemezi anaweza kuelezewa kama ni kiumbe asiyejitosheleza mwenyewe, asiye na kiini cha uhai ndani mwake mwenyewe; kwa hiyo ina maana kwamba mwa92

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 92

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

nadamu kama huyo si chochote kwa yeye mwenyewe binafsi na hamiliki chochote katika vile vinavyokwenda kumtengeneza yeye. Hii ndio hali ya mwanadamu kwa kiasi ambacho yeye ni mtu, kama ilivyo hali kwa viumbe wote wanaoonekana, katika hali yoyote watakayokuwa kwayo, kwa ukubwa wa namna yoyote itakavyokuwa tofauti kati ya viwango vya uhai wa kilimwengu, wakati wote si chochote kuhusiana na Kanuni. Viumbe hawa, binadamu au wengineo kwa hiyo, kwa hali yoyote vilivyo, viko katika hali ya uhuru kamili kulingana na Kanuni: “mbali na hicho hakuna chochote, hakuna chochote kabisa ambacho kinaishi.” Ni ufahamu wa utegemezi huu ambao unafanya kile ambacho hadithi mbalimbali zinakiita “mapungufu ya kiroho.” “Wakati huohuo, kwa kiumbe ambaye amepata ufahamu huu, kama matokeo ya mara moja, anakuwa na utengano kuhusiana na vitu vingine vyote vinavyoonekana, kwani kiumbe huyu anajua kuanzia hapo na kuendelea kwamba vitu hivi, kama vile alivyo yeye mwenyewe, si lolote, na kwamba havina umuhimu wa aina yoyote vikilinganishwa na hali ya Uhalisia kamili.” 29 Imam Husayn (a.s.) anamuomba Allah: “Nitaleta nini ninapotaka kuja Kwako?...Je, ninaweza kuja tu na masikio yangu, macho yangu, ulimi wangu, mikono yangu na miguu yangu tu? Hivi hili sio ukweli kwamba vyote hivi ni neema Zako ambazo umenipatia mimi?”30 Mahali pengine Imam Husayn (a.s.) anasema: 29 30

Rene Guenon, 1973. “Du’a al-Arafah” katika Mafatih al-Jinaan 93

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 93

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

“Ee Mola Wangu! Mimi ni masikini katika utajiri wangu hivi kwa nini nisiwe fukara katika umasikini wangu?” 31 Chochote nilichonacho ni ishara ya uhitaji wangu, ishara ya utegemezi wangu. Ni vipi kuhusu kile ambacho sinacho? Tuchukulie kwamba mtu amekopa fedha kutoka benki kiasi cha dola milioni moja na mtu mwingine akakopa dola laki moja. Ni yupi kati ya hawa watu wawili ni tajiri kumzidi mwingine, na yupi ambaye si tajiri? Inaonekana wazi kwamba yule ambaye amechukua fedha nyingi zaidi ndiye mwenye deni kubwa zaidi na mwenye kuwajibika zaidi na lazima awe na wasiwasi zaidi. Chochote kile anachotupatia Allah swt hutufanya sisi kuwa wenye kudaiwa zaidi. Vipo vitu vingi vingi sana ambavyo hatunavyo, na hata vile tulivyo navyo si mali yetu, sasa ni vipi sisi tuweze kujivuna na kujihisi hatuhitaji chochote. Imam Husayn (a.s.) anasema: “Kulingana na elimu yangu, mimi ni mjinga. Kwa vipi nisiweze kuwa mjinga zaidi sana kuhusiana na vile nisivyojua?” 32

Yale tunayojua ni yenye ukomo sana na yaliyozungukwa na maswali mengi. Jinsi tunavyozidi kujua, ndivyo tunavyozidi kukutana na maswali mengi. Ndiyo maana wale wenye kujua zaidi huwa waangalifu sana na wenye hadhari katika madai yao na hujitenga mbali na kiburi. Pia, baada ya kupita muda, kwa urahisi sana tunaweza tukapoteza kile tunachokijua. Wapo watu ambao hawawezi kukumbuka hata majina yao au majina ya ndugu zao wakaribu sana. Imam Husayn (a.s.) pia anasema: “Ee Allah! Kwa hakika mabadiliko ya mambo Yako na kasi 31 32

Biharul-Anwaar, Jz. 95, uk. 225 “Du’a al-Arafah” katika Mafatih al-Jinaan 94

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 94

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ya maendeleo ya maamrisho Yako huzuia wale waja Wako ambao wanakujua Wewe kuwa wenye kujiamini wanapokabiliwa na fadhila Zako ama kujihisi kukata tamaa wanapokabiliwa na majanga.” 33

Kila kitu hubadilika haraka sana katika dunia hii. Wakati mwingine hufurahi na wakati mwingine huwa wenye huzuni. Wakati mwingine watu hutuheshimu na wakati mwingine hakuna anayetuheshimu. Wakati mwingine watoto wetu hututendea wema na wakati mwingine sivyo. Yapo mambo mengi sana mazuri na mabaya. Sababu yake hili ni nini? Tunahitaji kujifunza kwamba hatuwezi kukiamini kitu kingine chochote isipokuwa Allah swt. Hakuna anayejua nini kitatokea, na kwa hiyo hatupaswi kukiamini kitu chochote. Kama semi za Imam Husayn (a.s.) hapo juu zinavyotufundisha, hatupaswi kukiamini kitu chochote au mtu yeyote isipokuwa Allah swt na wakati huo huo tusikate tamaa. Tusipoteze matumaini au tujihisi hatuna msaada pale ambapo mambo mabaya yanapotutokea. Ufunguo upo mikononi mwa Allah swt na anaweza kubadili hali zetu kuwa nzuri wakati wowote. Baada ya kusema yote haya Imam Husayn (a.s.) anasema: “Ninakuomba Wewe kwa ufakiri wangu na uhitaji wangu Kwako. Na ninawezaje kukuomba Wewe nikiwa na kitu kisichoweza kukufikia Wewe? Au ninawezaje kutamka malalamiko yangu Kwako ambapo hayakufichika Kwako? Ee Mungu Wangu! Inawezekanaje nisiwe masikini ambapo Wewe umeniweka mimi miongoni mwa masikini? Na nitawezaje kuwa masikini ambapo Wewe umenitajirisha kwa ukarimu Wako.”34 33 34

“Du’a al-Arafah” katika Mafatih al-Jinaan “Du’a al-Arafah” katika Mafatih al-Jinaan 95

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 95

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Hii inaonyesha kwamba njia (wasilah) ambayo anaitumia Imam kufika karibu zaidi kwa Allah swt ni ule utegemezi wake kwa Allah swt na uelewa wake mkubwa kwamba yeye ni fukara na si chochote mbele ya Allah swt. Hivyo, njia yenye thamani ambayo Imam Husayn (a.s.) ameiona na anataka kuitumia ni ‘ufukara.’ Kwa mujibu wa Qur`ani, sisi sote ni wahitaji. Qur`ani inasema:

َّ ‫ﷲ ۖ َو‬ ‫ﷲُ ھ َُو ْال َغنِيُّ ْال َحمِي ُد‬ ِ َّ ‫َيا أَ ُّي َھا ال َّناسُ أَ ْن ُت ُم ْالفُ َق َرا ُء إِ َلى‬ “Enyi watu! Nyinyi ndiyo wenye haja kwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ndiye Mkwasi, Mwenye kusifiwa.”[35:15]

Sisi sote ni wahitaji na ni Allah swt tu ndiye tajiri na kwa hiyo Yeye si muhitaji. Watu wengi hawaelewi jambo hili. Imam Husayn (a.s.) anasema kwamba yeye anaelewa na anakiri kuhusu jambo hili na anataka kulitumia kama njia ya kumkaribia zaidi Allah swt. Halafu Imam (a.s.) anaeleza kwamba anapotaka kumkaribia Allah swt anapokuwa na ufukara wake kunakuwa na tatizo, kwa vile ufukara hauwezi kumkaribia Allah swt. Hapa upo msisitizo kwamba ufukara upo upande moja tu; ufukara hauwezi kumkaribia Allah swt. Hii inaweza kumaanisha pia kwamba mja anayekwenda kwa Allah swt akiwa masikini, atakutana na Allah swt akiwa tayaru ni tajiri. Ili uwe tajiri ni lazima uende na umasikini wako, lakini watu wanaojihisi kuwa ni masikini sana ndiyo ambao ni matajiri sana mbele ya Allah swt. Yeyote yule aliye mnyenyekevu sana, Allah swt atamnyanyua juu zaidi kuzidi yeyote. Kama tunavyokuta kwenye hadithi, “Yeyote anayejitahidi kuwa mnyenyekevu kwa ajili ya Allah swt, Allah 96

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 96

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

swt atamnyanyua.”35 Kwenye Hadith tukufu (Hadith Qudsi) tunakuta kwamba Allah swt alimwambia Nabii Musa (a.s.) kwamba sababu ya kumfanya yeye (Musa) kuwa Mtume kwa kwamba aliangalia kwenye nyoyo za watu wote na akakuta kwamba Musa alikuwa ndiye mnyenyekevu zaidi kuliko wote. Kwa mujibu wa hadithi ijulikanayo sana, mtu anayeepukana na kiburi na akachagua kuwa mnyenyekevu mble ya Allah swt na kumtumikia kwa uaminifu mtu huyo huwa si mtumwa wa wengine tena, au wa matamanio yake. Mtu huyu atapata aina fulani ya uheshimiwa: “Utumwa kwa Allah swt ni jambo ambalo kiini chake ni uheshimiwa.”36 Kwenye hadithi nyingine tunasoma: “Mja wangu nitii Mimi. [Ukifanya hivyo] nitakufanya wewe kuwa mfano Wangu. Mimi ni hai na kamwe sifi kwa hiyo nitakufanya wewe kuwa hai na kamwe hautakufa. Mimi ni Mkwasi na kamwe siwi masikini kwa hiyo nitakufanya wewe kuwa tajiri na kamwe hutakuwa masikini. Chochote nikitakacho kinakuwa, kwa hiyo nitakufanya uwe kwa namna ambayo kwamba chochote utakachokitaka utakipata.”37

Tukichunguza kuhusu maisha yake, tunaweza kuona mfano kamili wa unyenyekevu kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Sifa iliyosababisha Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kuteuliwa kuwa ‘Mwisho wa Mitume’ na akapewa ujumbe wa mwisho wa Allah swt ipo zaidi kwenye ukweli kwamba alikuwa adithi hii inasimuliwa kutoka kwa Isa (Yesu) ndani ya Bihar al-Anwaar, Jz. H 14, uk. 307, kwa Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Jz. 16, uk. 265, Jz. 72, 120, kwa Imam as-Sadiq (a.s.), Jz. 72, uk. 121 na kutoka kwa Imam al-Kadhiim, Jz. 75, uk. 312. 36 Mizaan al-Hikmah, Jz. 6, uk.13 namba 11317. 37 Al-Jawaahir al-Saniyyah fi al-Ahaadith al-Qudsiyyah cha Hurr ‘Amili, uk. 284 35

97

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 97

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

mtumwa halisi wa Allah swt na alikuwa mtu mnyenyekevu sana mbele ya Allah swt na waja Wake. Waislamu hushahidilia (katika vikao vya at-tashahud – at-tahiyyatu) mara tisa kila siku katika sala zao kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alikuwa mtumwa wa Allah swt na Mjumbe Wake. Maana yake ni kwamba miongoni mwa sifa zake zote zipo sifa mbili ambazo ni za pekee: kwanza, aliweza kuwa mtumwa wa Allah swt na pili, alitunukiwa kwa kuteuliwa kuwa Mtume wa Allah swt. Mtume alikuwa mnyenyekevu sana hivyo kwamba kamwe hakujisifu; kamwe hakujiona yeye ni bora kuliko wengine. Kamwe hakujitenga mbali na watu na kila wakati aliishi maisha ya kawaida kabisa. Alidumisha tabia ile ile wakati alipokuwa peke yake na bila mamlaka na wakati alipotawala Rasi ya Bara Arabu na Waislamu walimfuata yeye kwa dhati ya nyoyo kabisa. Aliishi maisha ya kawaida kabisa na kila wakati alikuwa na watu, hususani masikini. Alikuwa hana jumba la kifalme wala walinzi. Alipoketi na sahaba zake, haikuwa rahisi kwa mtu kumtofautisha na watu wengine waliokuwa pale kwa kuangalia mavazi au kiti alichokalia. Kilichomtofautisha na wengine ni maneno yake na hali yake ya kiroho. Muda mfupi kabla ya kufariki, akiwa ndani ya Msikiti, Mtume alitangaza: “Yeyote miongoni mwenu anayehisi kuna wakati sikumtendea haki, aje mbele na atende haki. Kwa hakika kutenda haki hapa duniani kwa maoni yangu ni vema zaidi kuliko kuhesabiwa huko Akhera mbele ya malaika na Mitume.” Watu waliokuwepo Msikitini walitokwa machozi, kwani walikumbushwa yale yote Mtume aliyojitolea kuwafanyia na kuwahangaikia kote ili 98

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 98

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

awaongoze. Walijua kwamba Mtume hakutoa kipaumbele kwenye haja zake binafsi na kamwe hakundelea starehe na manufaa yake yeye na kuwaacha wengine. Kwa hiyo, watu waliokuwepo Msikitini walijibu kwa shukurani kubwa kwa heshima ya kina, nzito. Lakini mtu mmoja miongoni mwao, Sawadah bin Qays, alisimama na kusema:”Baba yangu na mama yangu wawe kafara yako! Ewe Mjumbe wa Allah swt! Wakati ulipokuwa unarudi kutoka Taif, nilikuja kukukaribisha ulipokuwa umepanda ngamia wako. Ulinyanyua fimbo yako kwa lengo la kumuongoza ngamia wako, lakini fimbo yako ilinigonga tumboni. Sielewi kama ulinipiga kwa makusudi au la.” Mtume akajibu: “Ninaomba hifadhi kwa Allah swt kutokana na mimi kufanya hivyo kwa kukusudia.” Mtume alimwambia Bilal aende nyumbani kwa Fatimah na alete fimbo hiyo. Baada ya kuletwa fimbo hiyo, Mtume alimwambia Sawadah alipize kwa kumpiga Mtume kwa fimbo hiyo. Sawadah akasema fimbo ilimpiga kwenye ngozi ya tumbo lake. Kwa hiyo Mtume alinyanyua shati lake ili Sawadah aweze kumpiga kwenye ngozi ya tumbo lake. Wakati huohuo Sawadah akauliza: “Ewe Mjumbe wa Allah swt! Utaniruhusu nibusu tumbo lako?” Mtume akamruhusu. Sawadah akabusu tumbo la Mtume na akaomba kwamba kwa sababu ya kitendo chake hiki, Allah swt amwepusha asiingie motoni mnamo Siku ya Hukumu. Mtume akasema: “Ewe Sawadah! Je, utanisamehe au bado unataka kulipiza kisasi?” Sawadah akajibu: “Nimekusamehe.” Halafu Mtume akaomba: “Ee Allah! Msamehe Sawadah bin Qays kama alivyomsamehe Mtume Wako, Muhammad!”38 38

Mustadrak Wasaa’il al-Shi’ah, Jz. 18, uk.287 na 288. 99

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 99

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Hivyo basi, sifa muhimu kiroho katika Uislamu ni kuwa wanyenyekevu na kwamba sisi si lolote mbele ya Allah swt. Hii isiwe kama dai ambalo tunaweza kulitamka bila imani ya kweli, lakini tamko hili litokane na ufahamu wa ndani kabisa wa kwamba sisi si lolote. Wakati fulani mtu alimuona Imam Sajjad (a.s.) ndani ya Masjid al-Haram, kando ya Ka`bah kwenye Hijr ya Isma`il. Akasema: “Nilikwenda Hijr Isma`il na nikamuona Ali ibn Husayn (a.s.) anaswali: Kisha akaenda sajida. Nikajisemea mwenyewe: huyu ni mtu mchamungu kutoka kwenye familia ya wachamungu, kwa hiyo ngoja nisikilize wakati anaomba akiwa kwenye sijida. Halafu akamnukuu Imam (a.s.) akisema: “Mola wangu, mtumwa wako mdogo na dhaifu amekuja mlangoni pako, mateka Wako amekuja mlangoni pako, yule ambaye ni masikini amekuja mlangoni pako, yule ambaye hukuomba Wewe amekuja mlangoni pako.”39

Kwenye Qur`ani, Allah swt anawaonya waumini kwamba kama wakiiacha dini Yake, baada ya muda mfupi atawaleta watu ambao miongoni mwa sifa zao ni wanyenyekevu wao mbele ya waumini:

َّ ‫ف َيأْتِي‬ َ ‫ِين آ َم ُنوا َمنْ َيرْ َت َّد ِم ْن ُك ْم َعنْ دِي ِن ِه َف َس ْو‬ َ ‫َيا أَ ُّي َھا الَّذ‬ ُ‫ﷲ‬ ‫ين‬ َ ‫ِين أَعِ َّز ٍة َع َلى ْال َكاف ِ​ِر‬ َ ‫ِب َق ْو ٍم ُي ِح ُّب ُھ ْم َو ُي ِحبُّو َن ُه أَ ِذلَّ ٍة َع َلى ْالم ُْؤ ِمن‬ ‫ك َفضْ ُل‬ َ ُ‫ﷲ َو َال َي َخاف‬ ِ َّ ‫يل‬ َ ‫ي َُجا ِھ ُد‬ َ ِ‫ون َل ْو َم َة َالئ ٍِم ۚ ٰ َذل‬ ِ ‫ون فِي َس ِب‬ َّ ‫ﷲ ُي ْؤتِي ِه َمنْ َي َشا ُء ۚ َو‬ ‫ﷲُ َواسِ ٌع َعلِي ٌم‬ ِ َّ “Enyi mlioamini atakayeiacha miongoni mwenu dini yake basi hivi karibuni Mwenyezi Mungu ataleta watu (ambao) 39

Biharul-Anwaar, Jz. 96, uk. 197 100

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 100

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

atawapenda, nao watampenda wanyeneyekevu kwa Waislamu, wenye nguvu juu ya makafiri. Watapigania dini ya Mwenyezi Mungu, wala hawataogopa lawama ya anayewalaumu. Hiyo ndiyo fadhila ya Mwenyezi Mungu, humpa amtakaye, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa, Mwenye kujua.� [5:54]

Kwenye fasihi ya Kislamu, hususan ile ya washairi wa Kiajemi, msisitizo mkubwa umewekwa kwenye mapungufu ya kiroho. Mathalani, kwenye shairi lake refu katika `Mathnawi,` yake mshairi Rumi ameonyesha umuhimu wa hisia hizi za kujihisi si lolote na unyenyekevu na hatari mbaya ya majivuno na kiburi. Rumi anajadili kwamba yeyote yule ambaye watu watajipendekeza kwake na kusujudu mbele yake kwa hakika wanamlisha sumu. Kama mhusika sio imara kiroho anaweza kudanganyika na kuwa na kiburi na akajiharibu na kupoteza unyenyekevu wake. Watu wanapomdanganya mwerevu atatambua kwamba hayo yanaweza kuleta madhara. Mshairi Rumi anaendelea kuwasifu wale ambao ni wanyenyekevu kinyume na wale ambao wenye kiburi. Mfano wa mtu ambaye hajasimamisha unyenyekevu ndani mwake ni sawa na mtu ambaye anakunywa mvinyo wenye sumu. Mwanzoni atajisikia vizuri na kufurahi, lakini baada ya dakika chache atazirai. Mfano mwingine ambao Rumi anatoa ni wa mapambano baina ya wafalme wawili. Inapotokea mfalme mmoja anashinda vita na akawa ndiye mshindi, basi ama atamfunga jela mfalme aliyeshindwa au atamuua, lakini kamwe hatawaadhibu ombaomba au mafukara wa nchi iliyoshindwa. Kwa kweli anaweza hata kuwasaidia na kuwaendeleza. Rumi anasema kwamba watu wa namna 101

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 101

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ya hawa ni dhaifu na hawana malengo ya kuwa wafalme kwa hiyo wao si tishio kwa mfalme mpya. Mfano mwingine ni msafara uliotoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine. Wezi watakapokuja kuiba kwenye msafara huo, wale ambao hawana fedha watasalimika. Au mbwa mwitu wanaposhambulia hushambulia chochote kinachokuja mbele yao. Wanaweza kushambuliana wao kwa wao na ndiyo maana wanapotaka kulala hukaa katika mduara ili kwamba wanaweza kuonana kwa uangalifu mkubwa. Lakini Rumi anasema kama yupo mbwa mwitu aliyekufa, hawatamshambulia. Tunajua kwamba Nabii Khidr (a.s.) alitoboa tundu chini ya mtumbwi kwa sababu alikuwepo mtawala dhalimu katika nchi hiyo aliyekuwa na tabia ya kunyang`anya kila mtumbwi au meli iliyokuwa inapita hapo. Hivyo, njia pekee ya kusalimisha jahazi hilo ilikuwa kulifanya lisifae kwa matumizi. Kama mlima au kilima kina madini mengi ya thamani, watu watachimba na kutoa nje udongo wote na madini. Lakini kilima cha kawaida au mlima wa kawaida ambao hauna kitu chochote cha thamani ndani yake utabaki kama ulivyo. Mtu ambaye anatembea ni kwamba amesimama kwa miguu yake na shingo yake imenyooka. Kwa hiyo maadui wanaweza kukata shingo yake kwa upanga, lakini hakuna mtu ambaye atakata kichwa cha kivuli cha mtu, kwani kivuli ni “dhaifu� sana hivyo kwamba hakuna mtu anayeweza kufikiria kuwa kinaweza kuwa tishio kwa vyovyote vile. Mfano mwingine ni kwamba, ngazi itaanguka, halafu anatokea mtu anataka kupanda kwenda juu zaidi kwa kutumia ngazi hiyo, huyu ni mpumbavu. Wakati ngazi hiyo itakapoporomoka atavunjika mifupa yake vibaya sana.

102

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 102

7/10/2013 3:33:39 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Baada ya kutaja mifano hii, hatimaye Rumi anasema kwamba yote hayo aliyosema ni kama matawi ambayo mizizi yake au misingi imekwenda chini kina kirefu zaidi. Kimsingi ni kwamba mtu anapokuwa na kiburi ni kwamba tayari anajishirikisha na Allah swt. Hii ni shirk. Rumi anaendelea kusema kwamba kwa kuwa bado hujafa na tena ukapata uhai kutoka kwa Allah swt, huwi na maisha ya kiroho. Bila ya kifo cha aina hiyo, msimamo wowote utakaochukua utakuwa ni shirk. Lakini kama ukifa na ukawa huna roho, yaani kama unahuishwa kupitia Allah unaweza kunyanyuka na kwenda juu zaidi. Katika hali kama hiyo, chochote utakachomiliki ni kwa ajili ya Allah swt na kitatumika kwa ajili ya Allah swt. Hii ndiyo Tawhiid ya kweli imani juu ya Mungu Mmoja. Imependekezwa kwamba ufakara maana yake ni kukosa kumiliki kitu na wakati huohuo kuwa na tamaa ya kukipata. Matahalani, mtu anayejihisi kwamba ndani ya nafsi yake anao upungufu fulani wa ukamilifu wa kibinadamu na kwa kweli anatamani kufanya marekebisho ya mapungufu haya, huyu ni fukara (faqir). Zaidi ya hayo, imependekezwa pia kwamba, kwenye Usufi “kutamani upendo kunatokana na faqr [ufukara wa kiroho].”40 Nadhani kuna matatizo fulani katika kuuelewa ufukara. Kwanza, ufukara ni zaidi kabisa ya kutokumiliki halafu ukawa unatamani kumiliki. Nadhani ufukara ni utambuzi wa uhitaji wetu hasa na utegemezi wetu juu ya Allah swt na madhali tuko hivi tulivyo uhitaji wetu huu hauwezi kuondosheka. Pili, ufahamu huu wa fukara ni zawadi ya kiroho na ni faida ambayo inatakiwa kudumishwa daima milele. Ufukara si kituo cha mpito kuelekea kwenye 40

Nurbakhsh Javad, Spiritual Poverty in Sufisim – Ufakiri wa kiroho katika Usufii, kilichotafsiriwa na Lenard Lewisohn 103

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 103

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

utajiri au neema. bali ufukara wenyewe ni ukwasi mkubwa sana na ustawi ambavyo binadamu wanaweza kuwa nayo kamwe. Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amenukuliwa akisema: “Hadhi yangu inatokana na ufukara wa kiroho. Nimepewa hadhi kubwa zaidi ya mitume wengine wote kwa sababu ya kupewa neema ya ufukara wa kiroho.�41

Hitimisho: Katika makala haya, tumezungumzia dhana ya upendo kuwa ni kishiko chenye nguvu zaidi katika Uislamu, na kama kipengele bainishi cha uhakika cha muumini wa kweli. Ujuzi ukichanganywa pamoja na tafakari na neema ya Allah swt, vinaweza kuongeza upendo wetu. Pili, tulizungumzia nadharia ya shukurani kwamba ni sawa na imani, kama ilivyofundishwa kwenye Qur`ani. Tukielewa daraja mbalmbali za shukurani inaweza kutusaidia kutambua na kuwa wenye kushukuru katika hali zote. Kwenye makala haya pia tulizungumzia unyenyekevu na ufukara wa kiroho, ambamo humo ndimo mtu anaweza kupata ucha-Mungu, mambo ya kiroho na kumwondolea mtu wasiwasi na matatizo. Nadharia hii haimaanishi kwamba binadamu hawana thamani, wala haishushi thamani ya binadamu; bali zaidi yenyewe inakubali na kutambua thamani ya binadamu: kwa kumtumikia Allah swt, aliye Mkamilifu Sana na Aliyetakasika sana tunaweza kuwa karibu zaidi na ukamilifu. 41

Biharul-Anwaar, Jz. 69, uk. 32 na 55. 104

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 104

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Tumuombe Allah swt atusaidie katika kutambua ni kiasi gani sisi tunamhitajia Yeye, kiasi gani ametukirimu, namna iliyo bora zaidi hasa ya kumwomba Yeye kwa dhati na jinsi ya kumfurahisha Allah swt ili na Yeye aturidhie na tuweze kuongoka na kuwa wasafi. Huu ni uwezo na ridhaa ya Allah swt, ambayo haina mipaka. Allah swt anao uwezo wote na sababu zote za kuwa mpole kwetu, na kama kuna vipingamizi vyovyote, vinatokana tu na sisi wenyewe. “Ewe Allah, nijaalie ukwasi wa umasikini, kwani humo kwenye ukarimu mkubwa kama huo ndimo ulimo uwezo na utukufu wangu.� [Hafidh wa Shiraz]

105

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 105

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

MATOKEO YA SAFARI YA KIROHO

N

i wazi kwamba lengo la mwisho la safari ya kiroho ni kufika karibu zaidi na Allah swt kwa kadiri iwezekanavyo. Hata hivyo, dhana ya ukaribu (qurb) na Mwenyezi Mungu inaweza kuonekana kwa wengine kama nadharia, hususani kwa wale ambao hawakupata mafunzo ya falsafa. Makala hii inajaribu kuonyesha mwanga kuhusu dhana ya ukaribu na Allah swt kwa kufafanua yale yanayowatokea wale waliomo kwenye safari hii ya kiroho kuelekea Kwake. Fikira zote zilizotajwa humu zimechukuliwa kutoka kwenye Qur`ani na Sunnah kwa hiyo inatumainiwa kwamba zitakubaliwa na Waislamu wote kutoka madhehebu mbalimbali ya Kiislamu. Tafakuri kuhusu matokeo haya inaweza kumpa moyo kila mtu kuanza safari hii na kama tayari wamekwishaanza safari hii, waweze kuendelea kufuata njia hii yenye mng`aro. Pia safari hii inaweza kuwa kama mtihani kwa wasafiri kuwawezesha kutathimini na kutambua ni kiasi gani cha maendeleo wamekwishafanya. Insha-Allah kwenye toleo lijalo tutachunguza dhana ya ukaribu na Mwenyezi Mungu kama somo la peke yake na kueleza inamaanisha nini kuwa karibu (qurb) na ni nani watu hao ambao wapo karibu [muqarrabin] zaidi na Mwenyezi Mungu. Matokeo ya Safari ya Kiroho. 1. Msaada kamili: Mojawapo ya matokeo ya kuishi maisha ya ucha-Mungu na kuwa na moyo safi na wa kiuchamungu ni kwamba tutapewa msaada kamili na Allah swt. 106

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 106

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Atatusikiliza, atatukirimu kile tunachotaka, Naye atakuwa masikio yetu, macho yetu na mikono yetu. Kwenye Hadithi mashuhuri sana ya ki-Mungu [hadith-i qudis] ya qurb-i nawaafil, tunasoma: “Hapana mja Wangu yeyote anayeweza kutafuta kunikaribia Mimi kwa kile ambacho ni chenye kupendwa zaidi na Mimi kuliko yale mambo ambayo nimeyafanya kuwa wajibu kwake. Halafu, kwa kutekeleza yale matendo yaliyokokotezwa [nawaafil] anaendeelea wakati wote kupata ukaribu na Mimi, hivyo kwamba Nimpende. Nitakapompenda, nitakuwa sikio lake, ambalo kwalo atasikia, macho yake amabayo kwayo ataona, na mkono wake atakaokamatia. Endapo ataniita, Mimi nitaitika wito wake, na kama akiniomba, Nitampa.”42

2. Elimu iliyo Kamili: Zipo hadithi nyingi zinazoonyesha kwamba matokeo mamojawapo ya kupata ukaribu wa kiroho kwa Mwenyezi Mungu ni kujaliwa ujuzi mkubwa wa uhalisia wa ulimwengu, pamoja na miujiza mingi ambayo kamwe haiwezi kujulikana kwa mbinu za kawaida za kujifunza na kufundisha. Akizungumzia mada ya mja ambaye amepata ukaribu na Mwenyezi Mungu, Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.) anamsimulia Allah swt anavyosema: “Nitampenda yeye pale atakaponipenda Mimi na nitamfanya apendwe na viumbe Vyangu, na nitafumbua macho yake ya ndani ili aweze kuona utukufu na ufahari Wangu, na sitamficha [elimu ya] wateule wa viumbe Wangu. Kwa hiyo, kwenye giza la usiku na mwanga wa mchana, nitamwambia siri, ili kwamba mazugumzo yake na viumbe na swahiba zake 42

Al-Kaafi, Jz. 2, uk. 352 na 353. 107

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 107

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

yatakatishwa. Nitamfanya asikie maneno Yangu na maneno ya malaika Wangu na nitamdhihirishia yeye siri ambayo nimewaficha viumbe Wangu.”43 3. Utii wa kipekee kwa Mwenyezi Mungu: Kutengwa na kila kitu kingine chochote zaidi ya Mwenyezi Mungu [tabattul au inqitaa’] maana yake ni kuwa huru kutokana na kutegemea kitu chochote isipokuwa Mwenyezi Mungu, na kuona kila kitu kama ishara Yake na kama udhihirisho wa uwezo na neema Zake. Waja wa kweli wa Mwenyezi Mungu huishi miongoni mwa jamii wakiwa wazingativu kwa Mwenyezi Mungu kwa ukamilifu na wanamkumbuka Yeye wakati wote. Qur`ani inasifu kundi la watu, “Watu ambao haiwasahaulishi biashara au kuuza katika kumkumbuka Mwenyezi Mungu, kusimamisha sala, na kutoa sadaka” (24:37). Kwenye du’a ya mnong`ono ijulikanayo sana ya mwezi wa Sha`ban (al-Munajat al-Shabaniyyah), Imam Ali (a.s.) na watu wengine wa nyumba ya Mtume walimuomba Mwenyezi Mungu, kwa kusema: “Mungu Wangu! Nitenganishe na vitu vyote isipokuwa Wewe, ongoa nyoyo zetu kwa nuru ya kukutazama Wewe, hadi uoni wetu wa nyoyo zetu upenye mapazia ya nuru na kufika kwenye Chanzo cha Utukufu na uziweke nafsi zetu zining`inie kwenye fahari ya utakatifu Wako.”44

Kwenye dua hii, Imam (a.s.) anamuomba Allah swt amwezeshe kuhusiana na Yeye tu na kutenganishwa na kila kitu ambacho hutuzuia sisi tusiwe Naye swt. Kwa bahati mbaya, vimo vitendo vingi ambavyo vinaweza kutuzuia utii wetu kwa Mwenyezi Mungu ambavyo vingekuwa 43 44

Bihaar al-Anwaar, Jz. 77, uk. 28 na 29 Mafaatih al-Jinaan. 108

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 108

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kwa vyema au viovu kwa dhahiri. Bila shaka, matendo mabaya na dhambi huweza kutuweka mbali na kumkumbuka Allah swt, bali matendo mema pia yanaweza kuchafuliwa, kwa mfano na kiburi na majivuno. Kwa hiyo, hatutakiwi kuruhusu kitu chochote kiwe kipingamizi au pazia baina yetu na Allah swt, ambaye ndiye Chanzo cha Nuru na Utukufu, ama iwe dhambi zetu na kuambatana kwetu na maisha ya kidunia au matendo yetu mema na tabia zetu njema. Endapo hatutakuwa waangalifu, hata hayo matendo mema na sifa njema vinaweza kushughulisha akili na nyoyo zetu, na kupotosha mazingatio yetu kwa Mwenyezi Mungu. Inavutia kwamba Imam Ali (a.s.) anaomba “kupenya mapazia ya nuru.” Kwa mujibu wa Ayatullah Khomenei “mapazia ya nuru” inarejelea yale mapazia ambayo yamo ndani ya nuru na yenyewe ni nuru, lakini hutuzuia sisi tusiione ile nuru kuu ambayo ni Mwenyezi Mungu. Ndio sababu elimu, ambayo ni kitu kinachopewa umuhimu mkubwa sana katika Uislam na kila mtu anatakiwa kuitafuta, inaweza kuwa ndio “pazia kuu zaidi” (al-hijab al-akbar) Ni sawa na mtu mwenye miwani ya kusomea, lakini badala ya kutumia miwani hiyo kusomea, anakuwa ameishikilia mkononi mwake, akifurahia kuiangalia, au kucheza nayo. Bila shaka, elimu inayopatikana baada ya utakaso wa nafsi ya mtu ni tofauti. Kulingana na hadithi nyingi, elimu ya aina hii ni nuru ambayo Mwenyezi Mungu anaielekeza ndani ya moyo wa mja ambaye Yeye amemridhia (al-`ilm-u nur-un yaqdhif-uhu `lla fi qalb-i man yashaa). Hadithi ifuatayo, ambayo imesimuliwa kwenye wasifu wa Allamah Sayyid Mohammad Husayn Tabataba`i , inahusiana na jambo hili. Ilitokea wakati fulani Allamah alipewa maelekezo ya zoezi maalum na mwalimu wake wa kiroho, 109

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 109

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Ayatollah Sayyid Ali Qadi Tabataba`i, na alishauriwa kwamba “wakati unapofanya zoezi hili maalum unaweza kuanza kuona malaika, lakini wewe endelea na zoezi na usiache.” Wakati fulani Allamah alipokuwa kwenye ibada yake alimuona malaika anakuja mbele yake. Haraka alikumbuka maelekezo ya mwalimu wake na aliendelea na ibada. Halafu malaika huyo alimzunguka na kana kwamba alitaka kuanza mazungumzo na Allamah, lakini yeye hakumpatiliza, malaika aliondoka akiwa na masikitiko. Allamah alisema kwamba hatasahau masikitiko ya malaika huyo, lakini hii ndio njia ambayo mja wa kweli hujifunga kwa Mola Wake. Tusiruhusu kitu chochote kiingilie kati ya ibada yetu tuliyolenga. 4. Kuingia kwenye uwanja wa nuru. Hadithi zilizotajwa hapo juu na zingine nyingi zinahusu ukweli kwamba mojawapo ya matokeo ya safari ya kiroho ni kuondosha giza na kuingia kwenye uwanja wa nuru. Uwanja wa nuru ni ukweli ambao umetajwa kwenye Qur`ani na hadithi:

ُّ ‫ِين آ َم ُنوا ي ُْخر ُج ُھ ْم م َِن‬ َّ ‫ور‬ ِ ‫الظلُ َما‬ َ ‫ﷲُ َولِيُّ الَّذ‬ ِ ‫ت إِ َلى ال ُّن‬ ِ ُّ ‫ ُھ ْم م َِن‬wa َّ “Mwenyezi huwatoa ُ‫الظل‬ ُ ‫ِين آ َم‬ ‫ور‬ ‫ت إِ َلى ال ُّن‬ ‫ ِر ُج‬wale ‫نوا ي ُْخ‬walioamini, ِ ni‫ َما‬mtawala َ ‫ﷲُ َولِيُّ الَّذ‬ ِ Mungu [2:257] gizani na huwaingiza katika mwangaza.” َّ ‫ َي ْھدِي ِب ِه ﷲُ َم ِن ا َّت َب َع ِرضْ َوا َن ُه ُس ُب َل الس َ​َّال ِم َوي ُْخ ِر ُج ُھ ْم م َِن‬. ُّ ‫ت َّ إ َلى ال ُّنور بإ ْذنه وي ْھدِيھم إ َل ٰى راطٍ مُسْ َتقِيم‬ ِ ‫الظلُب َمها‬ ‫ﷲُ ِ َم ِن ا َّت َب َع ِ ِ ِر ِضْ ِ َ ِوا َ​َن َُه ُس ُب ِ َل ْ ِالس َ​َّال ِمصِ َو َي ُْخ ِر ُج ُھ ْم ٍم َِن‬ ِ ِ ‫َي ْھدِي‬ ُّ ‫ِيھ ْم إِ َل ٰى صِ َراطٍ مُسْ َتق ٍِيم‬ ِ ‫الظلُ َما‬ ِ ‫ور ِبإِ ْذ ِن ِه َو َي ْھد‬ ِ ‫ت إِ َلى ال ُّن‬ “Mwenyezi Mungu huwaongoza kwacho wenye kufuata radhi yake katika njia za amani na huwatoa katika giza kuwapeleka kwenya nuru kwa amri yake, na huwaongoza katika njia iliyonyooka.”[5:16] 110

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 110

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

Nuru pia imeombwa kwenye maombi mengi, kama ilivyo kwenye du’a ambayo husomwa baada ya Ziyarah ya Aal-i Yasin: “Ee Allah! Kwa hakika ninakuomba umrehemu Muhammad (s.a.w.w.), mtume wa rehema Yako na neno la nuru Yako. Na unijaze moyo wangu nuru ya uhakika. Na kifua changu kwa nuru ya imani. Na ujaze kufikiri kwangu na nuru ya nia. Na dhamir yangu na nuru ya elimu. Na nguvu zangu nuru ya utendaji. Na ulimi wangu nuru ya ukweli. Na dini yangu nuru ya uelewa kutoka Kwako. Na uoni wangu nuru ya mng’aro. Na kusikia kwangu nuru ya hikma. Na upendo wangu nuru ya urafiki kwa Muhammad (s.a.w.w.) na watu wa nyumba yake (a.s.). Hadi hapo nitakapokutana na Wewe, ambapo hakika nitakuwa nimetekeleza ahadi Yako na mkataba Wako. Kwa hiyo, utanikirimu neema Zako, Ee Bwana! Ee Uliyetukuka.”45 Kwenye uwanja wa nuru kila kitu kiko wazi na uhalisia wa kweli wa kila kitu unajulikana. Mojawapo ya changamoto kuu tunayokabiliana nayo ni kukielewa kila kitu kama vile kilivyo hasa, na kukitendea kila kitu inavyofaa. 45

Mafaatih al-Jinaan. 111

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 111

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

5. Mapenzi mazito juu ya Mwenyezi Mungu: Njia mojawapo madhubuti sana ya kuimarisha uhusiano wetu na Allah swt ni kupitia mapenzi juu Yake. Mara mmoja anapoonja mapenzi haya, hakuna kitu kingine mbadala. Maimam (a.s.) walikuwa na mapenzi makubwa sana kwa Allah swt. Imam Ali ibn Husayn (a.s.) anasema: “Hakuna kitu kitakacho kata kiu yangu inayochoma isipokuwa kufika Kwako, kitakacho zima nguvu ya shauku yangu isipokuwa kukutana na Wewe, kitakachoangusha ari ya tamaa yangu isipokuwa kutazama uso Wako, kutengeneza mahali pa makazi yangu bila kuwa karibu na Wewe.” 46

Irfan sio yule ambaye anampenda Mwenyezi Mungu tu; bali ni yule anayempenda Mwenyezi Mungu peke yake, kwa sababu kupenda kwake au kuchukia kwake katika jambo lolote lile ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu. Huridhia na kutamani kile tu ambacho Mpendwa wake huridhia na kutamani. Mja huyu hana ridhaa au tamaa nyingine zaidi ya ile Yake swt. Mapenzi ya mja huyu irfan kwa Mwenyezi Mungu huenea kwa kila kingine chochote kile.47 Imam Sadiq (a.s.) anasema: “Moyo safi ni ule unaokutana na Mola ukiwa huru kutokana na mwingine yeyote.” 48

6. Kumshuhudia Mwenyezi Mungu katika kila kitu: Mja irfaan wa kweli ni yule anayemshuhudia Mwenyezi Mungu katika kila kitu. Allah swt hujidhihirisha kwetu katika The Psalms of Islam (Sahifah al-Sajjadiyyah), uk. 251 na252 Kwamaelezo ya kina juu ya mapenzi tazama kitabu; Love ni Christianity and Islam (Kiswahili - Upendo katika Ukristo na Uislam) 2005, toleo la 2, cha Mahnaz Heydarpoor. 48 Al-Kaafi, Jz. 2, uk. 16 46 47

112

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 112

7/10/2013 3:33:40 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

namna mbalimbali wakati wote, na kama nyoyo zetu ni safi, tunaweza kumuona Allah swt kwenye kila kitu. Kwenye Dua ya ‘Arafah, Imam Husayn (a.s.) anasema: “Ee Mungu Wangu! Kupitia ishara Zako za aina mbalimbali [katika ulimwengu wa uhai] na mabadiliko katika hali na mazingira, nimetambua kwamba lengo ni kufanya Wewe ujulikane kwangu katika kila kitu, ili kwamba nisije nikakosa kukujali katika jambo lolote.” 49

Imam Ali (a.s.) anasema: “Sikuona chochote isipokuwa kwamba nilimuona Mwenyezi Mungu kabla yake, pamoja nacho na baada yake.” 50

Ni wazi kwamba uoni unaozungumziwa hapa, kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mtukufu, umetukuzwa kwa kiwango kikubwa kuzidi upeo wa jicho la kawaida. Mwenyezi Mungu hawezi kuonekana kwa jicho la kawaida, si hapa ulimwenguni wala Akhera. Kwa kawaida kuwa na mishughuliko sana kuna maana kwamba tunamsahau Allah swt na kuzama kwenye kazi zetu. Hata hivyo, kuhusu Imam Ali (a.s.), kwake ilimaanisha kwamba alimkumbuka Allah swt wakati wote: kabla, wakati wenyewe na baada ya kila kitu; kwa kuwa Allah swt ni Muumba, Muhifadhi, na ndiye ambaye atabaki baada ya vitu vyote. Mja ambaye amefika kiwango cha juu katika safari yake ya kiroho atamuona Mwenyezi Mungu ndani ya kila kitu. Mathalani, hata kama mtu anatuambia jambo baya au adui yetu anatuambia neno, bado tunaweza kupata ujumbe mzuri 49 50

Mafaatih al-Jinaan. Sadr al-Din al-Shirazii, al-Asfaar, Jz. 1, uk. 117, Jz. 4, uk. 479 na Jz. 5, uk. 27 113

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 113

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ndani ya kile ambacho tunaweza tu kukifasiri na kukielewa. Watu wengine wanaweza kusikiliza ujumbe huohuo lakini wasiweze kupata ujumbe wowote kutoka humo. Hata hivyo, tunaweza kuelewa ujumbe kutoka kwa Allah swt hata kama ni katika maneno ya adui yetu. 7. Amani ya ndani: Wakati wowote mtu anapokuwa karibu na Allah swt, kwake vitu vingine vyote huonekana vyepesi na vidogo. Hujihisi kwamba yu chini ya ulinzi wa Allah swt, na hakuna kinachoweza kumdhuru. Huelewa kwamba hapatwi na maumivu yoyote au tatizo isipokuwa hayo ni kwa faida yake, na kwamba atalipwa thawabu na Mwenyezi Mungu “zisizo na kipimo” [39:10]. Wapo watu wengi duniani ambao wana maisha ya starehe, lakini wanakosa amani na utulivu, hivyo kwamba wengine miongoni mwao huamua kunywa vilevi au kubwia madawa ya kulevya kwa lengo la kupunguza maumivu yao ya kiroho na kujibaini. Hata hivyo, hakuna kitu kingine kinachoweza kuwaridhisha binadamu isipokuwa kumkaribia Mwenyezi Mungu. Qur`ani inasema:

ُ‫ﷲ َت ْط َمئِنُّ ْالقُلُوب‬ ِ َّ ‫أَ َال ِب ِذ ْك ِر‬ “….Ehe! Kwa kumdhukuru Mwenyezi Mungu nyoyo zinatua.”[13:28].

Watu wanaomzingatia Mwenyezi Mungu hawawezi kusumbuliwa na kitu chochote kwa sababu moja, kwamba hawaogopi kupoteza chochote. Kila kitu kinakuwa rahisi 114

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 114

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

kwao, kwa kuwa wameukubali ukuu wa Allah swt, kwa maoni yao hakuna kingine tena chenye umuhimu. Mathalani, kama upo kwenye ufukwe wa bahari, huwezi kuifikiria glasi ndogo ya maji. Akiwaelezea wacha-Mungu Imam Ali (a.s.) anasema: “Ukuu wa Muumbaji umetua ndani ya nyoyo zao na kwa hiyo, kitu kingine chochote kwao kinaonekana kidogo.�51

Hitimisho: Matokeo ya safari ya kiroho ni mengi sana kuweza kupatiwa maelezo ya kutosha katika makala hii fupi. Safari huwa zawadia wale wanaosafiri kwenye njia yake kwa utii wa kipekee, kuingia kwenye uwanja wa nuru, kumpenda sana Allah swt, kuweza kumshuhudia Allah swt ndani ya kila kitu, na kuwa na amani ya ndani. Mara tunapochukua hatua moja kuelekea kwa Allah swt, atatulipa neema zenye thamani zisizohesabika, ambazo zitatufanya sisi tuweze kusonga mbele zaidi kwa urahisi mno.

51

Nahjul-Balaghah, hotuba ya 191 115

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 115

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

ORODHA YA VITABU VILIVYO CHAPISHWA NA AL-ITRAH FOUNDATION 1. Qur’an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka Thelathini 2.

Uharamisho wa Riba

3.

Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Kwanza

4.

Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Pili

5.

Hekaya za Bahlul

6.

Muhanga wa Imamu Husein (A.S.)

7.

Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (A.S.)

8.

Hijab vazi Bora

9.

Ukweli wa Shia Ithnaashari

10.

Madhambi Makuu

11.

Mbingu imenikirimu

12. Abdallah Ibn Saba 13. Khadijatul Kubra 14. Utumwa 15. Umakini katika Swala 16. Misingi ya Maarifa 116

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 116

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

17. Kanuni za Ndoa na maadili ya Familia 18. Bilal wa Afrika 19. Abudharr 20. Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu 21.

Salman Farsi

22. Ammar Yasir 23. Qur’an na Hadithi 24. Elimu ya Nafsi 25. Yajue Madhehebu ya Shia 26. Ukusanyaji na Uhifadhi wa Qur’an Tukufu 27. Al-Wahda 28. Ponyo kutoka katika Qur’an. 29. Uislamu mfumo kamili wa maisha ya kijamii 30. Mashukio ya Akhera 31.

Al Amali

32. Dua Indal Ahlul Bayt 33. Udhuu kwa mujibu wa Kitabu na Sunna. 34. Haki za wanawake katika Uislamu 35. Mwenyeezi Mungu na sifa zake 36. Kumswalia Mtume (s) 37. Nafasi za Ahlul Bayt (a.s) 38. Adhana. 117

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 117

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

39

Upendo katika Ukristo na Uislamu

40. Tiba ya Maradhi ya Kimaadili 41.

Maana ya laana na kutukana katika Qur’ani Tukufu

42. Kupaka juu ya khofu 43. Kukusanya swala mbili 44. Bismillah ni sehemu ya Qur’ani na husomwa kwa Jahara 45. Kuwaongoza vijana wa kizazi kipya 46. Kusujudu juu ya udongo 47. Kusherehekea Maulidi Ya Mtume (s) 48. Tarawehe 49. Malumbano baina ya Sunni na Shia 50. Kupunguza Swala safarini 51.

Kufungua safarini

52. Umaasumu wa Manabii 53. Qur’an inatoa changamoto 54. as-Salaatu Khayrun Mina -’n Nawm 55. Uadilifu wa Masahaba 56. Dua e Kumayl 57. Sauti Ya Uadilifu wa Binadamu 58. Umaasumu wa Mitume - Faida Zake Na Lengo Lake 59. Umaasumu wa Mitume - Majibu Ya Aya Zenye Utata 60. Umaasumu wa Mitume - Umaasumu wa Mitume Muhammad (s)

118

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 118

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

61.

Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Kwanza

62. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Pili 63. Kuzuru Makaburi 64. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Kwanza 65. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Pili 66. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tatu 67. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Nne 68. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tano 69. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Sita 70. Tujifunze Misingi Ya Dini 71.

Sala ni Nguzo ya Dini

72. Mikesha Ya Peshawar 73. Malezi Ya Mtoto Katika Uislamu 74. Ubora wa Imam ‘Ali Juu ya Maswahaba Na Ushia ndio njia iliyonyooka 75. Hukumu za Kifikihi zinazowahusu Wanawake 76. Liqaa-u-llaah 77. Muhammad (s) Mtume wa Allah 78. Amani na Jihadi Katika Uislamu 79. Uislamu Ulienea Vipi? 80. Uadilifu, Amani na Mtume Muhammad (s) 81.

Mitala na Ndoa za Mtume Muhammad (s)

119

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 119

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

82. Urejeo (al-Raja’a ) 83. Mazingira 84. Utokezo (al - Badau) 85. Hukumu ya kujenga juu ya makaburi 86. Swala ya maiti na kumlilia maiti 87. Uislamu na Uwingi wa Dini 88. Mtoto mwema 89. Adabu za Sokoni 90. Johari za hekima kwa vijana 91.

Maalimul Madrasatain Sehemu ya Kwanza

92. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Pili 93. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Tatu 94. Tawasali 95. Imam Mahdi katika Usunni na Ushia 96. Hukumu za Mgonjwa 97. Sadaka yenye kuendelea 98. Msahafu wa Imam Ali 99. Ngano ya kwamba Qur’ani imebadilishwa 100. Idil Ghadiri 101. Kusoma sura zenye Sijda ya wajibu 102 Hukumu zinazomuhusu mkuu wa kazi na Mfanyakazi 103. Huduma ya Afya katika Uislamu 120

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 120

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

104. Sunan an-Nabii 105. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Kwanza) 106. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Pili) 107. Shahiid Mfiadini 108. Kusalia Nabii (s.a.w) 109. Ujumbe -Sehemu ya Kwanza 110. Ujumbe - Sehemu ya Pili 111. Ujumbe - Sehemu ya Tatu 112. Ujumbe - Sehemu ya Nne 113. Mariamu, Yesu na Ukristo kwa mtazamo wa Kiislamu 114. Hadithi ya Thaqalain 115. Maarifa ya Kiislamu 116. Ukweli uliopotea sehemu ya Kwanza 117. Ukweli uliopotea sehemu ya Pili 118. Ukweli uliopotea sehemu ya Tatu 119. Ukweli uliopotea sehmu ya Nne 120. Ukweli uliopotea sehmu ya Tano 121. Johari zenye hekima kwa vijana 122. Safari ya kuifuata Nuru 123. Fatima al-Zahra 124. Myahudi wa Kimataifa 125. Kuanzia ndoa hadi kuwa Wazazi 121

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 121

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

126. Visa vya kweli sehemu ya Kwanza 127. Visa vya kweli sehemu ya Pili 128. Muhadhara wa Maulamaa 129. Mwanadamu na Mustakabali wake 130. Imam Ali (‘a) Ndugu wa Mtume Muhammad (s) (Sehemu ya Kwanza) 131. Imam Ali (‘a) Ndugu wa Mtume Muhammad (s) (Sehemu ya Pili) 132. Khairul Bariyyah 133. Uislamu na mafunzo ya kimalezi 134. Vijana ni Hazina ya Uislamu. 135. Yafaayo kijamii 136. Tabaruku 137. Taqiyya 138. Vikao vya furaha 139. Shia asema haya Sunni asema haya Wewe wasemaje? 140. Visa vya wachamungu 141. Falsafa ya Dini 142. Azadari-Kuhuzunika na Kuomboleza 143. Sunna katika Kitabu Fiqhi al-Sunnah 144. Mtazamo Mpya - Wanawake katika Uislamu 145. Kuonekana kwa Allah 146. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Kwanza) 122

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 122

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

147. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Pili) 148. Ndugu na Jirani 149. Ushia ndani ya Usunni 150. Maswali na Majibu 151. Mafunzo ya hukmu za ibada 152. Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 1 153 Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 2 154. Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 3 155. Abu Huraira 156. Vipengee kadhaa katika Swala ya Jamaa na Msikiti. 157. Mazingatio kutoka katika Qur’an - Sehemu ya Kwanza 158. Mazingatio kutoka kaitka Qur’an - Sehemu ya Pili 159. Mazingatio kutoka katika Uislamu - Sehemu ya kwanza 160. Mazingatio kutoka katika Uislamu - Sehemu ya Pili 161. Qur’ani Tukufu – Pamoja na Tarjuma ya Kiswahili 162. Falsafa ya Mageuzi ya Imam Husein (a.s) 163. Amali za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani 164. Elimu ya Tiba za Kiislamu - Matibabu ya Maimamu 165. Uislamu Safi 166. Majlisi za Imam Husein Majumbani 167. Mshumaa. 168. Uislam wa Shia 123

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 123

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

169. Amali za Makka 170. Amali za Madina 171. Asili ya Madhehebu katika Uislamu 172. Sira ya Imam Ali kuhusu Waasi 173. Ukweli uliofichika katika neno la Allah 174. Uislamu na Mifumo ya Uchumi 175. Umoja wa Kiislamu na Furaha 176. Mas’ala ya Kifiqhi 177. Jifunze kusoma Qur’ani 178. As-Sahifatul Kamilah as-Sajjadiyyah 179. Hayya ‘Alaa Khayri’l-’Amal Katika Adhana 180. Ukweli kuhusu Funga ya Siku ya Ashura 181. Dua za Miezi Mitatu Mitukufu (Rajabu, Shaabani na Ramadhani) 182. Uadilifu katika Uislamu 183. Mahdi katika Sunna 184. Jihadi ya Imam Hussein (‘as) 185. Kazi na Bidii ni njia ya maendeleo 186. Abu Talib – Jabali Imara la Imani 187. Ujenzi na Utakaso wa Nafsi 188. Vijana na Matarajio ya Baadaye 189. Usalafi – Historia yake, maana yake na lengo lake

124

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 124

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

190. Ushia – Hoja na Majibu 191. Mateso ya Dhuria wa Mtume (saww) 192. Maombolezo – Msiba wa Bwana wa Mashahidi (a.s.) 193. Shahidi kwa Ajili ya Ubinadamu 194. Takwa 195. Amirul Muuminina (‘as) na Makhalifa 196. Uongozi na Utawala katika Mwenendo wa Imam ‘Ali (‘a) 197. Kuelewa Rehma ya Mwenyezi Mungu 198. Utawala na Uendeshaji katika Sera ya Imam Ali (a.s.) 199. Mtazamo kuhusu msuguano wa kimadhehebu

200. Upotoshaji Dhahiri katika Turathi ya Kiislamu 201. Nchi na Uraia – Haki na wajibu kwa Taifa 202. Mtazamo wa Ibn Taymiyyah kwa Imam Ali (a.s.) 203. Uongozi wa kidini – Maelekezo na utekelezaji wa Kijamii

125

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 125

7/10/2013 3:33:41 PM


UJENZI NA UTAKASO WA NAFSI

KOPI NNE ZIFUATAZO ZIMETAFSIRIWA KWA LUGHA KINYARWANDA 1.

Amateka Na Aba’Khalifa

2.

Nyuma yaho naje kuyoboka

3.

Amavu n’amavuko by’ubushiya

4.

Shiya na Hadithi

126

09_UJENZI NA UTAKASO_10_July_2013.indd 126

7/10/2013 3:33:41 PM


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.