ARDHI NI UHAI Newsletter

Page 1

ISSN NO. 0856-9495

TOLEO LA 14

NAFASI YA SHERIA ZA ARDHI KATIKA KULINDA HAKI ZA WANAWAKE Na: Beatha Fabian

AGOSTI - DESEMBA 2015

MSAADA WA KISHERIA UNAIMARISHA ULINZI WA HAKI ZA ARDHI KWA WANAWAKE. Na. Nakamo Tenende

H

Cheti cha hakimiliki ya kimila ni mojawapo ya haki ya kisheria inayotolewa na Sheria ya Ardhi ya Kijiji katika kulinda haki za ardhi kwa wanawake

K

atiba ya Tanzania inampatia kila mtu haki ya kumiliki mali. Haki hiyo pia inalindwa na Sheria ya Ardhi namba.4 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba. 5 za mwaka 1999. Kulingana na Sheria hizi, mtu au watu wanaoweza kuomba haki ya umiliki wa ardhi ni pamoja na mwanamke au mwanaume mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea. Hivyo wanawake wanaweza kupata ardhi kwa njia ya kununua, kupewa zawadi, kugawiwa na serikali au kugawiwa kurithi mila, desturi na taratibu za sheria husika. Wakati mila na desturi za kitanzania zimekuwa zikiwanyima wanawake haki ya kupata, kutumia, kumiliki na kudhibiti ardhi moja kwa moja, sheria zote mbili

zimetatua suala hili. Sheria za ardhi zimeondoa desturi za kibaguzi ambazo ziliathiri haki za wanawake kumiliki ardhi na kutambua usawa wa wanawake na wanaume katika kumiliki ardhi. Wanawake wana haki katika kumiliki ardhi kimila, haki ambayo hapo awali ilikuwa haipo na kama ilikuwepo basi ni katika baadhi ya mila na desturi nzuri japokuwa ni chache. Wanawake wanapaswa watambue kuwa umiliki wa kisheria na wa kimila una hadhi sawa na wa mwanaume na pia kuna utaratibu wa kisheria mara baada ya kupata ardhi ili kuboresha umiliki wake ni hati maalum kulingana na eneo la ardhi au nyumba ilipo (mjini au kijijini)

YALIYOMO

Inaendelea uk. 3 NAFASI YA SHERIA ZA ARDHI KATIKA KULINDA HAKI ZA WANAWAKE

1-3

HATIMILIKI YA KIMILA NA ULINZI WA HAKI ZA ARDHI KWA WANAWAKE

6

MSAADA WA KISHERIA UNAIMARISHA ULINZI WA HAKI ZA ARDHI KWA WANAWAKE.

1-4

ATHARI ZA MIGOGORO YA ARDHI KWA WANAWAKE

8

MILA POTOFU ZINA ATHIRI UMILIKI WA ARDHI KWA WANAWAKE

5

NAFASI YA WANAWAKE KATIKA UTATUZI WA MIGOGORO YA ARDHI

10-11

AKIARDHI imekuwa ikifanya tafiti katika wilaya mbalimbali nchini kuanzia ilipoanzishwa mwaka 1994. Baadhi ya tafiti zimebainisha kuwa wananchi wanaoishi katika ngazi za msingi hususan vijijini wakiwemo wanawake, wafugaji, waokota matunda na wachimbaji wadogo wamekosa haki zao katika ardhi kutokana na mtazamo hasi wa jamii juu ya mwanamke kumiliki ardhi, kushamiri kwa mfumo usiozingatia haki na usawa katika upatikanaji, uzalishaji na mgawanyo wa mali na rasilimali. Dosari hii inaanzia katika ngazi ya familia hadi ngazi za juu za kiutawala katika serikali kuu huku zikilindwa na baadhi ya sera na sheria. Wanawake wamekuwa ni wahanga wakubwa katika kukosekana huku kwa usawa na haki. Ndiyo maana, HAKIARDHI kwa kutambua hilo, imekuwa na kawaida ya kutoa ushauri na msaada wa kisheria kwa wananchi vijijini, mpango ambao umewezesha wanawake wengi kupata haki ya kupata, kutumia na kumiliki ardhi na rasilimali nyinginezo katika maeneo yao. Msaada wa kisheria umetolewa katika maeneo mengi ya vijijini na pembezoni mwa miji kwa kuwatumia wanasheria wa Taasisi ya HAKIARDHI pamoja na wangalizi wa Masuala ya ardhi waliojengewa uwezo katika maeneo ambayo Taasisi imekuwa

Baadhi ya tafiti zimebainisha kuwa wananchi wanaoishi katika ngazi za msingi hususan vijijini wakiwemo wanawake, wafugaji, waokota matunda na wachimbaji wadogo wamekosa haki zao katika ardhi Agosti - Desemba 2015

1 Inaendelea uk. 4


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.